Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • es26 uku. 108-118
  • Mwezi wa 11

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mwezi wa 11
  • Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
  • Vichwa Vidogo
  • Siku ya Yenga, 1 Mwezi wa 11
  • Siku ya Kwanza, 2 Mwezi wa 11
  • Siku ya Pili, 3 Mwezi wa 11
  • Siku ya Tatu, 4 Mwezi wa 11
  • Siku ya Ine, 5 Mwezi wa 11
  • Siku ya Tano, 6 Mwezi wa 11
  • Siku ya Posho, 7 Mwezi wa 11
  • Siku ya Yenga, 8 Mwezi wa 11
  • Siku ya Kwanza, 9 Mwezi wa 11
  • Siku ya Pili, 10 Mwezi wa 11
  • Siku ya Tatu, 11 Mwezi wa 11
  • Siku ya Ine, 12 Mwezi wa 11
  • Siku ya Tano, 13 Mwezi wa 11
  • Siku ya Posho, 14 Mwezi wa 11
  • Siku ya Yenga, 15 Mwezi wa 11
  • Siku ya Kwanza, 16 Mwezi wa 11
  • Siku ya Pili, 17 Mwezi wa 11
  • Siku ya Tatu, 18 Mwezi wa 11
  • Siku ya Ine, 19 Mwezi wa 11
  • Siku ya Tano, 20 Mwezi wa 11
  • Siku ya Posho, 21 Mwezi wa 11
  • Siku ya Yenga, 22 Mwezi wa 11
  • Siku ya Kwanza, 23 Mwezi wa 11
  • Siku ya Pili, 24 Mwezi wa 11
  • Siku ya Tatu, 25 Mwezi wa 11
  • Siku ya Ine, 26 Mwezi wa 11
  • Siku ya Tano, 27 Mwezi wa 11
  • Siku ya Posho, 28 Mwezi wa 11
  • Siku ya Yenga, 29 Mwezi wa 11
  • Siku ya Kwanza, 30 Mwezi wa 11
Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
es26 uku. 108-118

Mwezi wa 11

Siku ya Yenga, 1 Mwezi wa 11

Sitaendelea kuwa na kinyongo milele.—Yer. 3:12.

Kama Yehova, wazee wanajikaza kuonyesha huruma wale wenye wameondolewa mu kutaniko. Kwa mufano, Yehova hakungoya watu wake wenye walimuacha, Waisraeli wa zamani, njo wakamate hatua ya kwanza ya kumurudilia. Alikamata hatua ya kuwasaidia hata kama hakuna alama yoyote yenye ilionyesha kama walipenda kutubu. Yehova alionyesha kupitia nabii Hosea namna ni mwenye huruma. Aliambia nabii Hosea aende kukamata bibi yake mwenye alikuwa angali anafanya zambi. (Hos. 3:1; Mal. 3:7) Kama Yehova, wazee Wakristo wanapenda kabisa mukosaji amurudilie Yehova, na hawafanye mambo yenye itafanya ikuwe nguvu kwake kurudia. Mu mufano wa Yesu wa mwana mupotevu baba ‘alimukimbilia [mwana wake], akamukumbatia kwa upole wote na kumubusu.’ (Lu. 15:20) Ona kama baba hakungoya mutoto wake akuye kumulomba huruma. Lakini sawa baba mwenye upendo, alikamata hatua ya kwanza. w24.08 28 fu. 7-8

Siku ya Kwanza, 2 Mwezi wa 11

Kama mutu yeyote kati yenu anakosa hekima, aendelee kumuomba Mungu, kwa maana yeye anapatia wote kwa ukarimu na bila kutafuta-tafuta makosa.— Yak. 1:5; maelezo ya chini.

Sawa vile maneno ya andiko ya leo inaonyesha, Yehova haiko muchoyo. Anapatia wengine kwa ukarimu hekima yake. Ona kama wakati Yehova anapatia wengine hekima yake, anafanya vile “bila kulaumu,” ao “bila kutafuta-tafuta makosa.” Hapendi tujisikie mubaya juu tuko na lazima ya muongozo wake. Na hata, anatutia moyo tutafute muongozo wake. (Mez. 2:​1-6) Halafu siye, tunaweza kumuiga Yehova kwa kupatia wengine hekima yenye tuko nayo? (Zb. 32:8) Watu wa Yehova wako na nafasi za mingi za kufundisha wengine mambo yenye wamejifunza. Mara mingi tunazoezaka wapya mu mahubiri. Wazee wanazoezaka kwa uvumilivu watumishi wa huduma na ndugu mu kutaniko wenye kubatizwa watimize muzuri migao yao mu kutaniko. Na ndugu na dada wenye kuwa na ufundi mu kazi ya kujenga na kutunza majengo wanasaidia kuzoeza wengine juu waweze kuhangaikia majengo ya tengenezo ya Yehova. w24.09 28-29 fu. 11-12

Siku ya Pili, 3 Mwezi wa 11

Mulikuwa wapendwa sana kwetu.—1 Te. 2:8.

Ndugu, juu ufikie kuwa muzee unapaswa “kuwa bila lawama.” Maana yake bengine mu kutaniko banapaswa kukujua kuwa mutu muzuri juu ya tabia yako ya muzuri. (1 Ti. 3:2) Zaidi ya ile, kunapaswa kuwaushuhuda muzuri kutoka kwa watu wa injejuu yako. Batu benye habiko Mashahidi banaweza kusema mubaya juu ya imani yako, lakini habapaswe kuwa na sababu yoyote ya kusema kama hauko munyoofu ao hauna mwenendo muzuri. (Da. 6:​4, 5) Ujiulize hivi: ‘Inje na ndani ya kutaniko ninajulikana kuwa mutu muzuri?’ Kama uko “mwenye kupenda wema,” unaona sifa za muzuri za bengine na unabapongeza juu ya zile sifa. (Tit. 1:8) Unafurahia pia kufanyia bengine mambo ya muzuri hata kama haulazimike kufanya vile. Juu ya nini ni jambo ya maana sana wazee wakuwe na ile sifa? Juu ile itafanya bafurahie kupitisha wakati mingi mu kazi ya uchungaji na mu migao yao ingine. (1 Pe. 5:​1-3) Furaha yenye banapata wakati banatumikia bengine ni ya mingi kupita mambo yenye banajiima.—Mdo. 20:35. w24.11 20 fu. 3; 21 fu. 4-5

Siku ya Tatu, 4 Mwezi wa 11

Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.—Mdo. 20:35.

Watumishi wa huduma wanafanya kazi ya maana sana mu makutaniko. Mutume Paulo alifurahia sana wale wanaume waaminifu. Kwa mufano wakati aliandikia Wafilipi, alisalimia watumishi wa huduma na wazee. (Flp. 1:1) Bandugu mingi benye kubatizwa, ikuwe vijana ao wazee, banafurahia sana kuwa watumishi wa huduma. Kwa mufano, ndugu Devan aliwekwa kuwa mutumishi wa huduma wakati alikuwa na miaka 18. Lakini ndugu Luis aliwekwa kuwa mutumishi wa huduma wakati alikuwa na miaka zaidi ya 50. Maneno yake inaonyesha namna watumishi wa huduma wengi wanajisikiaka. Alisema hivi: “Ninaona kama ni pendeleo kubwa kuwa mutumishi wa huduma, zaidi sana wakati ninafikiria upendo wenye kutaniko imenionyesha!” Kama uko ndugu mwenye kubatizwa na hauyakuwa mutumishi wa huduma, unaweza kujikaza kufikia ule muradi? w24.11 14 fu. 1-3

Siku ya Ine, 5 Mwezi wa 11

Ninakuomba, Ee Yehova, kumbuka . . . namna . . . nimetenda mambo ya muzuri mbele ya macho yako.—2 Fa. 20:3.

Wakati alikuwa na miaka 39, Mufalme Hezekia wa Yuda alifikia kujua kama iko na magonjwa yenye haitapona. Nabii Isaya alimuambia Mufalme Hezekia ujumbe wa Yehova wenye ulionyesha kama atakufa juu ya ile magonjwa. (2 Fa. 20:1) Ilionekana sawa vile hakuna tena tumaini. Wakati Hezekia alisikia ile habari, alihuzunika na alilia sana. Alimulilia Yehova sana katika sala juu amusaidie. Wakati Yehova alisikia sala ya Hezekia, na wakati aliona machozi yake, Yehova alimusikilia huruma na alimuambia hivi: “Nimesikia sala yako. Nimeona machozi yako. Angalia, ninakuponyesha.” Kupitia Isaya, Yehova alimuahidi Hezekia kama atarefusha maisha yake na ataokoa Yerusalemu kutoka mu mikono ya Waashuru. (2 Fa. 20:​4-6) Uko na magonjwa yenye inaonekana kama haitapona? Sali kwa Yehova. Atakusikiliza hata kama uko nalia wakati uko nasali. Biblia inatuhakikishia kama “Baba wa rehema nyingi na Mungu wa faraja yote” atatufariji mu magumu yetu yote.—2 Ko. 1:​3, 4. w24.12 24 fu. 15-17

Siku ya Tano, 6 Mwezi wa 11

Niko na tumaini kwa Mungu, tumaini lenye watu hawa pia wanangojea, kwamba kutakuwa ufufuo wa wenye haki na wenye hawako wenye haki.—Mdo. 24:15.

Tutafurahi sana kukaribisha wenye watafufuliwa! Wazia pia furaha yenye utakuwa nayo wakati utajifunza mambo mingi juu ya Yehova kwa kuchunguza vitu mingi vyenye aliumba. (Zb. 104:24; Isa. 11:9) Na zaidi ya yote itafurahisha sana kumutumikia Yehova bila kufanya zambi hata kidogo! Unaweza kuitika kupoteza zile baraka zote juu tu ya “kufurahia zambi kwa muda”? (Ebr. 11:25) Hapana! Tuko tayari kujiima jambo yoyote leo, juu tu tupate zile baraka. Kumbuka kama hatutachunga dunia Paradiso milele! Kuko siku tutaishi ndani. Ile mambo yote haingewezekana kama Yehova hangetupenda sana na kututolea Mwana wake kuwa zawadi! w25.01 29 fu. 12

Siku ya Posho, 7 Mwezi wa 11

Je, mukono wa Yehova ni mufupi sana?—Hes. 11:23.

Kitabu ya Waebrania inazungumuzia batu mingi benye balionyesha imani. Kwa mufano, Musa alionyesha imani ya ajabu. (Ebr. 3:​2-5; 11:​23-25) Musa hakukosea kumutumainia Yehova, juu kwa muujiza Yehova alitolea batu yake chakula na maji mu ile jangwa ya kukauka. (Kut. 15:​22-25; Zb. 78:​23-25) Hata kama Musa alikuwa na imani ya nguvu, mwaka moya hivi kisha Yehova kuokoa Waisraeli kwa muujiza kutoka Misri, Musa alijiuliza ikiwa Yehova ataweza kutolea batu yake nyama. Waisraeli walikuwa wengi sana mu jangwa, na Musa alijiuliza namna gani Yehova ataweza kutolea bale batu yote nyama. Kwa hiyo Yehova alimuuliza Musa hivi: “Je, mukono wa Yehova ni mufupi sana?” (Hes. 11:​21-23) Ni sawa vile Yehova alikuwa namuuliza Musa, ‘Unawaza ninaweza kushidwa kufanya kitu yenye ninasema?’ w25.03 26 fu. 1-2

Siku ya Yenga, 8 Mwezi wa 11

[Mungu] hakujizuia kupatia ulimwengu wa zamani azabu.—2 Pe. 2:5.

Habari kuhusu garika ilifananisha jambo fulani yenye itatokea mu wakati wenye kuya? Hapana. Juu ya nini? Juu Biblia haiseme vile. Yesu alilinganisha “siku za Noa” na wakati wa kuwapo kwake, lakini hakusema kama kila tukio yenye ilitokea mu siku za Noa ilifananisha jambo fulani yenye itatokea mu wakati wenye kuya; hakusema kama kufunga mulango wa safina kulikuwa na maana fulani ya kiunabii. (Mt. 24:​37-39) Noa alifanya nini wakati alisikia onyo yenye Yehova alimupatia? Alionyesha kama alikuwa na imani kwa kujenga safina. (Ebr. 11:7; 1 Pe. 3:20) Vilevile, wale wenye wanasikia habari njema kuhusu Ufalme wa Mungu wanapaswa kutenda kulingana na mambo yenye wanasikia. (Mdo. 3:​17-20) Petro alimuita Noa kuwa “muhubiri wa haki.” Leo tuko nafanya kazi ya kuhubiria watu mu dunia yote, na tunajikaza kuifanya kwa bidii. Lakini, hata tujikaze namna gani, hatuwezi kutangazia kila mutu ku dunia habari njema mbele mwisho ufike. w24.05 9-10 fu. 3-5

Siku ya Kwanza, 9 Mwezi wa 11

Anaheshimia wale wenye kumuogopa Yehova.—Zb. 15:4.

Tunapaswa kutafuta njia za kuheshimia marafiki wa Yehova na kuwatendea mambo ya muzuri. (Ro. 12:10) Tunafanya vile namna gani? Njia moya inapatikana mu Zaburi 15:4 yenye kuonyesha kama mugeni mu hema ya Yehova “havunje ahadi yake, hata wakati inamuletea matatizo.” Kukosa kutimiza ahadi zetu kunaweza kuumiza wengine. (Mt. 5:37) Kwa mufano, Yehova anatazamia wageni wake waheshimie naziri ya ndoa. Pia anafurahi wakati wazazi wanajikaza kutimiza ahadi zenye wanafanyia watoto wao. Upendo wetu kwa Mungu na kwa jirani utatuchochea tufanye yetu yote ili kutimiza ahadi zetu. Njia ingine ya kuonyesha kama tunaheshimia marafiki wa Yehova ni kuwa wakarimu na wakaribishaji-wageni. (Ro. 12:13) Wakati tunapitisha wakati pamoya na ndugu na dada ili kujifurahisha, ile inatia nguvu urafiki wetu pamoya nao na pamoya na Yehova. Zaidi ya ile, wakati tunakaribisha wengine, tunamuiga Yehova. w24.06 12 fu. 15-16

Siku ya Pili, 10 Mwezi wa 11

Mwanadamu mwenye anaweza kufa ni nini ili umuweke katika akili?—Zb. 8:4.

Yehova anafunua kweli yake kwa watu wanyenyekevu. (Mt. 11:25) Kwa unyenyekevu tulikubali kusaidiwa kujifunza kweli. (Mdo. 8:​30, 31) Lakini, tunapaswa kuwa waangalifu juu tusikuwe na majivuno. Majivuno inaweza kufanya tuwaze kama maoni yetu ni yenye hekima, sawa tu vile kanuni za Biblia na muongozo wenye tengenezo ya Yehova unatutolea ni vyenye hekima. Juu tuendelee kuwa wanyenyekevu, tunapaswa kukumbuka kama tuko wa hali ya chini sana kama tunalinganishwa na ukubwa wa Yehova. (Zb. 8:​3, 4) Tunaweza pia kumuomba Yehova atusaidie tukomalishe sifa ya unyenyekevu, na tukuwe tayari kufundishwa. Kuliko kutia mawazo yetu pa nafasi ya kwanza, Yehova atatusaidia tutie pa nafasi ya kwanza mawazo yake yenye anatutolea kupitia Neno yake na tengenezo yake. Mu usomaji wako wa Biblia, tafuta mambo yenye inaonyesha kama Yehova anapenda unyenyekevu na anachukia majivuno na kiburi. Na ujikaze sana ili uendelee kuwa munyenyekevu hata kama unapewa mapendeleo yenye inaweza kufanya uonekane sana. w24.07 10 fu. 8-9

Siku ya Tatu, 11 Mwezi wa 11

Mudogo atakuwa elfu (1000) Na mutu wa hali ya chini atakuwa taifa lenye nguvu. Mimi mwenyewe, Yehova, nitaharakisha jambo hilo kwa wakati wake.—Isa. 60:22.

Hata leo, Yehova anaendelea kupanga muzuri watu wake. Tangu 1919, Yesu anatumia kikundi kidogo cha wanaume watiwa-mafuta ili kupanga kazi ya kuhubiri na kutolea wanafunzi wake chakula ya kiroho. (Lu. 12:42) Bila shaka, Yehova iko nabariki kazi yao. (Isa. 65:​13, 14) Kama hatukukuwa napangwa muzuri, hatungeweza kufanya kazi yenye Yesu alitupatia. (Mt. 28:​19, 20) Kwa mufano, wazia mambo ingekuwa namna gani kama hatungepewa maeneo ya kuhubiri; kila mutu angehubiri kwenye anapenda. Maeneo fulani ingehubiriwa tena na tena na wahubiri tofauti-tofauti, na maeneo ingine ingebakia bila kuhubiriwa. Na weye unaona faida zingine zenye tunapata juu tunapangwa muzuri? Yesu alipanga muzuri wafuasi wake wakati alikuwa ku dunia na anaendelea kufanya vile leo. w24.04 8-9 fu. 2-4

Siku ya Ine, 12 Mwezi wa 11

Ukibadilika na kutenda mambo ya muzuri, je, hautakubaliwa? Lakini kama haubadilike na kutenda mambo ya muzuri, zambi inashutama kwenye mulango, na inatamani sana kukutawala.—Mwa. 4:7.

Kaini njo alikuwa mutoto mwanaume wa kwanza wa Adamu na Eva. Aliriti muelekeo wa kufanya zambi kutoka kwa wazazi wake. Pia Biblia inasema hivi juu yake: “Matendo yake mwenyewe yalikuwa maovu.” (1 Yo. 3:12) Pengine njo maana Yehova “hakumukubali Kaini na toleo lake” wakati alitoa zabihu. Kuliko kubadilika, “Kaini akakasirika sana na kuhuzunika.” Yehova alifanya nini? Alizungumuza na Kaini. (Mwa. 4:​3-7) Yehova alizungumuza na Kaini kwa upole na alimuambia kama atamubariki akibadilika. Pia alimuonya kama kasirani yake itamuongoza ku zambi. Jambo ya kuhuzunisha ni kama Kaini hakusikiliza Yehova. Hakuacha Yehova amusaidie juu afikie kutubu. Kisha Kaini kutenda vile, Yehova aliacha kusaidia watenda-zambi juu wafikie kutubu? Hapana! w24.08 10 fu. 8

Siku ya Tano, 13 Mwezi wa 11

Unapaswa kuchagua uzima ili uendelee kuishi.—Kum. 30:19.

Waisraeli wangeweza kuwa na maisha ya muzuri mu siku zenye kuya. Yehova angewabariki na wangeishi wakati murefu mu inchi yenye aliwaahidi. Ilikuwa inchi ya muzuri sana na ilitoa chakula mingi! Musa aliwaambia hivi juu ya ile inchi: “Miji mikubwa na yenye kupendeza yenye haukujenga, nyumba zenye kujaa vitu vya muzuri vya namna mbalimbali vyenye haukufanya kazi ili kuvipata, matangi yenye haukuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni yenye haukupanda.” (Kum. 6:​10, 11) Musa alipatia pia Waisraeli onyo. Juu waendelee kuishi mu ile inchi ya muzuri sana, walipaswa kutii amri za Yehova. Musa aliwashauria ‘wachague uzima’ kwa kumusikiliza Yehova na kwa “kushikamana naye.” (Kum. 30:20) Lakini, Waisraeli hawakumutii Yehova. Kwa hiyo kisha wakati, Yehova aliruhusu Waashuru na kisha Wababiloni wapate ushindi juu yao na kuwapeleka mu uhamisho.—2 Fa. 17:​6-8, 13, 14; 2 Ny. 36:​15-17, 20. w24.11 9 fu. 5-6

Siku ya Posho, 14 Mwezi wa 11

Hakuna mutu mwenye anaweza kuja kwangu isipokuwa Baba mwenye alinituma amuvute.—Yoh. 6:44.

Batu mingi benye kujiita Bakristo banawaza kama ikiwa tu banamuamini Yesu na kumuona kuwa Bwana na mwokozi wao, bataokolewa. (Yoh. 6:29) Lakini ile haitoshe juu ku mwanzo batu mingi mu Galilaya balimuamini Yesu, lakini kisha wakati baliacha kumufuata. Juu ya nini? Batu mingi benye Yesu alikulisha balikuwa namufuata juu tu alikuwa nabapatia mambo yenye balipenda. Balifurahia namna Yesu aliponyesha batu kwa muujiza, chakula ya bure, na mafundisho yenye ilipatana na mawazo yao. Lakini, Yesu alionyesha kama wanafunzi wake wa kweli wanapaswa kufanya mambo mingi zaidi. Yesu hakukuya ku dunia juu tu ya kutimiza tamaa za batu. Batu balipaswa kukubali mwaliko wake wakati alisema ‘mukuye kwangu.’ Bangefanya vile kwa kukubali na kutii mambo yote yenye alifundisha.—Yoh. 5:40. w24.12 12 fu. 12-13

Siku ya Yenga, 15 Mwezi wa 11

Bwana, muendelee kupenda bibi zenu, kama vile Kristo pia alipenda kutaniko.—Efe. 5:25.

Ni nini inaweza kusaidia bwana aache kumutendea bibi yake mubaya na kumushushia heshima? Anapaswa kujikaza kumuiga Yesu. Namna alitendea wanafunzi wake ni mufano wenye unaweza kusaidia bwana ajue namna ya kutendea bibi yake. Tuone mambo yenye bwana anaweza kujifunza kupitia namna Yesu alitendea mitume wake na namna alizungumuza nao. Yesu alitendea mitume wake kwa upole na heshima. Hakuwatendea kwa ukali. Hakutumia nguvu yake juu ya kuwaogopesha. Lakini, aliwatumikia kwa unyenyekevu. (Yoh. 13:​12-17) Aliambia wanafunzi wake hivi: “Mujifunze kupitia mimi, kwa maana mimi ni mwenye tabia ya upole na munyenyekevu katika moyo, na mutapata pumuziko kwa ajili yenu.” (Mt. 11:​28-30) Yesu alikuwa na tabia ya upole. Mutu mupole haiko muzaifu, lakini ni mutu mwenye iko na nguvu ya kujizuia. Wakati wanamuchokoza, anabakia mwenye kutulia. w25.01 10 fu. 10-11

Siku ya Kwanza, 16 Mwezi wa 11

Tia kila jambo lenye unafanya katika mukono wa Yehova.—Mez. 16:3.

Vile mwisho uko nakaribia tunaweza kutazamia kama magumu ya kupata makuta itaendelea kuongezeka. Muvurugo mu mambo ya politike, vita, misiba ya asili, ao magonjwa ya mupya ya kuambukiza inaweza kufanya tukuwe na lazima ya makuta zaidi ao tupoteze kazi, vitu, ao nyumba. Ni nini inaweza kutusaidia kukamata maamuzi yenye inaonyesha kama tanaamini kuwa mukono wa Yehova hauko mufupi? Jambo ya kwanza na ya maana sana ya kufanya ni kumuambia Yehova mahangaiko yako. Muombe akupatie hekima yenye uko nayo lazima juu ya kukamata maamuzi ya muzuri, na akusaidie utulie juu uepuke “kuhangaika sana” juu ya hali yako. (Lu. 12:​29-31) Umulilie akusaidie utosheke na mambo ya lazima. (1 Ti. 6:​7, 8) Tafuta habari mu vichapo vyetu juu ujue mambo ya kufanya wakati uko na magumu ya kupata makuta. Habari za ku jw.org zenye kuzungumuzia magumu ya kupata makuta zimesaidia watu wengi. w25.03 28-29 fu. 10-11

Siku ya Pili, 17 Mwezi wa 11

Mungu amenionyesha kwamba sipaswe kuita mutu yeyote kuwa muchafu ao haiko safi.—Mdo. 10:28.

Wakati ulifika juu Batu ya Mataifa bajiunge pia na batu ya Mungu. Mutume Petro alipewa mugao wa kuhubiria Kornelio, mwenye alikuwa kati ya Batu ya Mataifa ba kwanza-kwanza benye balifikia kuwa Bakristo. Wayahudi hawakukuwa najiunga na Batu ya Mataifa, njo maana iliomba Petro atayarishwe mbele ya kutimiza mugao wake. Wakati Petro alielewa mapenzi ya Mungu juu ya ile jambo, alibadilisha mawazo yake. Kwa hiyo wakati Mungu alimutuma, alienda “bila kupinga.” (Mdo. 10:​28, 29) Alihubiria Kornelio na batu ya nyumba yake, na bote bakabatizwa. (Mdo. 10:​21-23, 34, 35, 44-48) Kisha miaka, Petro alitia moyo Wakristo wenzake ‘wakuwe na umoja wa akili.’ (1 Pe. 3:​8, maelezo ya chini) Juu tuko batu ya Yehova, tunaweza kuwa na namna moya ya kufikiri kama tunaiga namna ya Yehova ya kufikiri yenye kuonyeshwa mu Neno yake. w25.03 9-10 fu. 7-8

Siku ya Tatu, 18 Mwezi wa 11

Musipotoshwe na mafundisho mbalimbali na yenye kuwa mageni.—Ebr. 13:9.

Muelekeo na namna ya kuona mambo ya watu wa mu hii dunia iko naendelea kuwa mbali sana na namna ya Yehova ya kuona mambo. (Mez. 17:15) Njo maana tunapaswa kutia nguvu uwezo wetu wa kutambua na wa kuepuka mawazo ya wapinzani wetu; ile mawazo inaweza kutuvunja moyo ao hata kutupoteza. Paulo alishauria Wakristo Waebrania waendelee kukomala kiroho. Ni muzuri na siye tufuate ile shauri. Kukomala kiroho inatia ndani kujua kweli muzuri zaidi na kuona mambo vile Yehova anaiona. Maendeleo ya kiroho inaendelea hata kisha mutu kujitoa kwa Yehova na kubatizwa. Ikuwe tumefanya miaka ngapi mu kweli, siye wote tunapaswa kuendelea kusoma na kujifunza Neno ya Mungu. (Zb. 1:2) Kuwa na programu ya muzuri ya funzo ya kipekee kutatusaidia tutie nguvu imani yetu, sifa yenye Paulo alikazia mu barua yake kwa Waebrania.—Ebr. 11:​1, 6. w24.09 10 fu. 7-8

Siku ya Ine, 19 Mwezi wa 11

Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.—Yak. 4:8.

Ikiwa tunamuona Yehova kuwa mutu wa kweli kabisa, itakuwa mwepesi zaidi kwetu kuendelea kuwa waaminifu kwake. Ni ile njo ilimusaidia Yosefu. Alikatala kabisa kufanya uasherati. Mungu alikuwa mutu wa kweli kabisa kwake na hakupenda kumuhuzunisha. (Mwa. 39:9) Juu Yehova akuwe mutu wa kweli kabisa kwetu, tunapaswa kuwa na wakati wa kusali na kujifunza Neno yake. Ile itafanya urafiki wetu pamoja naye ukuwe nguvu. Kama tunakuwa na urafiki wa karibu pamoya na Yehova sawa vile Yosefu, tutaepuka kufanya jambo yoyote yenye itamuhuzunisha. Kusahau kama Yehova ni Mungu mwenye kuishi kunaweza kufanya ikuwe mwepesi kumuacha. Fikiria mambo yenye ilifikia Waisraeli wakati walikuwa mu jangwa. Walijua kama Yehova iko, lakini walianza kuwa na mashaka kama Yehova anaweza kuwapatia mambo yenye wako nayo lazima. (Kut. 17:​2, 7) Kisha, walimuasi Mungu. Kwa kweli hatupendi kufuata mufano wao wa kukosa kutii, na mufano wao ni onyo kwetu.—Ebr. 3:12. w24.06 24 fu. 14-15

Siku ya Tano, 20 Mwezi wa 11

Macho ya Yehova yako juu ya wenye haki, na masikio yake yanasikiliza kilio chao cha kuomba musaada.—Zb. 34:15.

Tuko ku mwisho-mwisho wa siku za mwisho, kwa hiyo tunaweza kutazamia kama mambo ya kuleta machozi itaongezeka. Yehova anaona machozi yetu na ile inamufanya ahuzunike. Anatupenda na hasahau machozi yetu. Kwa hiyo, wakati tuko mu hali za nguvu, tukuwe tayari kumufungulia Yehova moyo wetu mu sala. Tusijitenge hata siku moya na ndugu na dada zetu wenye wanatupenda. Na maneno yenye kutuliza yenye kuwa mu Biblia iendelee kutufariji. Tunaweza kuwa hakika kama tukiendelea kuvumilia kwa uaminifu, Yehova atatubariki. Atatupanguza machozi yetu yote yenye tunalia kwa sababu ya huzuni, kusalitiwa, na kukosa tumaini. Ile ni kati ya baraka zenye ametuahidi. (Ufu. 21:4) Ku mwisho, machozi yetu yote itakuwa tu ya furaha. w24.12 20 fu. 3; 25 fu. 19

Siku ya Posho, 21 Mwezi wa 11

“Muko mashahidi wangu,” ni vile Yehova anasema.—Isa. 43:12.

Yehova ametuweka kuwa Mashahidi wake, na anatuahidi kama atatusaidia tukuwe hodari. (Isa. 43:​10, 11) Anafanya vile mu njia mbalimbali. Tuzungumuzie tu njia ine. Kwanza, Yesu iko pamoya na siye wakati wote wenye tuko nahubiri habari njema. (Mt. 28:​18-20) Pili, Yehova ameweka malaika ili watusaidie. (Ufu. 14:6) Tatu, Yehova ametupatia musaidizi, ni kusema roho takatifu ili itukumbushe mambo yenye tumejifunza. (Yoh. 14:​25, 26) Ine, Yehova ametupatia ndugu na dada wa kutusindikiza mu mahubiri. Kwa musaada wa Yehova na wa ndugu na dada zetu wenye upendo, tuko na mambo yote ya lazima ili tutimize muzuri mugao wetu. Lakini kama unavunjikaka moyo wakati unapata tu watu kidogo mu mahubiri ya nyumba kwa nyumba, ujiulize hivi: ‘Watu wa mu eneo yangu, wako wapi hii saa?’ (Mdo. 16:13) ‘Wako ku kazi ao wako mu soko?’ Kama ni vile, hauone kama unaweza kupata watu wengi zaidi ukifanya mahubiri ya mu barabara? w24.04 17 fu. 10-11

Siku ya Yenga, 22 Mwezi wa 11

Kama mutu hajue namna ya kusimamia nyumba yake mwenyewe, atatunza namna gani kutaniko la Mungu?—1 Ti. 3:5.

Kama uko bwana na unapenda kuwa muzee, familia yako pia inapaswa kuwa mufano muzuri. Kwa hiyo unapaswa “kusimamia muzuri nyumba [yako] mwenyewe.” Unapaswa kujulikana kuwa kichwa ya familia mwenye upendo na mwenye kuhangaikia familia yake. Ile inamaanisha usaidie familia yako imuabudu Yehova muzuri. Kama uko baba unapaswa kuhakikisha kama “watoto [wako wenye wangali wadogo ni] watiifu na wenye kuchukua mambo kwa uzito.” (1 Ti. 3:4) Unapaswa kuwafundisha na kuwazoeza kwa upendo. Kusema kweli, sawa batoto bote nabo batapenda kucheka na kucheza. Lakini juu unabazoeza muzuri, batakuwa batiifu, batakuwa na adabu na tabia ya muzuri. Pia, unapaswa kujikaza kusaidia batoto yako bakuwe na uhusiano wa muzuri pamoya na Yehova, batumikishe kanuni za Biblia mu maisha yao, na bafanye maendeleo juu bafikie kubatizwa. w24.11 22 fu. 10-11

Siku ya Kwanza, 23 Mwezi wa 11

Hakuna mwenye iko na upendo mukubwa kuliko huu, kwamba mutu atoe uzima wake kwa ajili ya marafiki wake.—Yoh. 15:13.

Kadiri tunafanya mambo mingi mu kazi ya Yehova, ni vile tunaona namna anatutegemeza na ile inafanya tumutumainie zaidi. (1 Ko. 3:9) Lakini kumbuka kama Yehova hatalinganisha mambo yenye unafanya na mambo yenye watu wengine wanafanya; Yehova anaona mambo yenye kuwa mu moyo wako. Anafurahi wakati unaonyesha shukrani kutoka ku moyo kwa ajili ya zawadi yake ya muzuri sana, bei ya ukombozi. (1 Sa. 16:7; Mk. 12:​41-44) Ni kupitia tu bei ya ukombozi njo tunasamehewa zambi zetu, tuko marafiki wa Yehova, na tuko na tumaini ya kuishi milele. Tuendelee basi kuonyesha kila siku shukrani juu ya upendo wa Yehova, wenye ulimuchochea atutolee zile baraka zote. (1 Yo. 4:19) Tuendelee pia kumuonyesha shukrani Yesu, mwenye alitupenda sana mupaka akatoa uzima wake wa kibinadamu kwa ajili yetu! w25.01 31 fu. 16-18

Siku ya Pili, 24 Mwezi wa 11

Nilisumbuka muchana wote.—Zb. 73:14.

Fikiria namna muandikaji wa Zaburi 73 alijisikia. Aliona bengine banaonekana kuwa na afya ya muzuri na mali mingi, na banaonekana kuwa habana mahangaiko mu maisha. (Zb. 73:​3-5, 12) Wakati alibaangalia na kuona namna maisha yao ilionekana kuwa ya muzuri, aliona kama bidii yake ya kumutumikia Yehova ilikuwa ya bure. Ile mawazo yenye kuvunja moyo ‘ilimusumbua muchana wote.’ (Zb. 73:​13, 14) Alifanya nini juu ya kupiganisha ile mawazo? Muandikaji wa zaburi alienda ku hekalu ya Yehova. (Zb. 73:​16-18) Kule aliweza kufikiri muzuri. Alitambua kuwa hata kama bengine balionekana kuwa na maisha ya muzuri, habakukuwa na tumaini ya wakati wenye kuya. Kujua vile kulimusaidia kuwa na amani ya akili juu alijua kama kutia mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza, ilikuwa uamuzi wa muzuri zaidi. Ile ilifanya aazimie tena zaidi kuendelea kumutumikia Yehova.—Zb. 73:​23-28. w24.10 26-27 fu. 11-12

Siku ya Tatu, 25 Mwezi wa 11

Wajue kwamba wewe, mwenye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote.—Zb. 83:18.

Yehova ametuita ili tukuwe “mashahidi.” (Isa. 43:​10-12) Miaka fulani yenye imepita, barua fulani yenye ilitoka ku Baraza Yenye Kuongoza ilisema hivi: “Pendeleo kubwa zaidi yenye kila mumoja wetu iko nayo, ni kuitwa Shahidi wa Yehova.” Juu ya nini? Fikiria hii mufano: Kama unapenda mutu fulani akuwe shahidi wako ku tribinali, utachagua mutu mwenye unajua na mwenye unatumainia, mwenye namna yake ya kuwa itafanya wengine watumainie ushahidi wenye atatoa. Juu Yehova ametuchagua kuwa Mashahidi wake, ile inaonyesha kama anatujua muzuri na kama anatumainia kuwa tutaambia wengine kama yeye njo Mungu wa kweli. Tunaona kuwa ni pendeleo kubwa sana kuwa Mashahidi wake, njo maana tunatumia kila nafasi yenye tunapata ili kuambia wengine kuhusu jina yake na kuwasaidia waelewe kama mambo mingi yenye imesemwa juu yake ni ya uongo. Wakati tunafanya vile, tunaonyesha kama tunaishi kulingana na jina yetu yenye tunajivunia sana, Mashahidi wa Yehova!—Ro. 10:​13-15. w24.05 18 fu. 13

Siku ya Ine, 26 Mwezi wa 11

Akaponyesha wote wenye walikuwa wagonjwa.—Mt. 8:16.

Kutumikia bengine kulimuletea Yesu furaha. Siku moya zaidi ya kufundisha batu, Yesu alihangaikia pia mahitaji yao ya kimwili. Kwa muujiza alibatolea chakula. Na aliipatia banafunzi yake juu babagabulie. (Mk. 6:41) Kwa kufanya vile, Yesu alifundisha banafunzi yake namna ya kutumikia bengine. Alionyesha pia kama kazi zenye tunafanyia bengine ni za maana. Wazia furaha yenye mitume walikuwa nayo ya kutumika pamoya na Yesu juu ya kugabulia batu ile chakula yenye ilitolewa kwa muujiza mupaka “wote wakakula na kushiba”! (Mk. 6:42) Haiko ile mara moya tu njo Yesu alihangaikia kwanza mahitaji ya bengine kisha yake ikafuata nyuma. Alitumia maisha yake yote juu ya kutumikia bengine. (Mt. 4:23) Kufundisha bengine na kuhangaikia mahitaji yao kwa unyenyekevu kulimuletea furaha sana. w24.11 16 fu. 10-11

Siku ya Tano, 27 Mwezi wa 11

Katika siku za mwisho kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia.—2 Ti. 3:1.

Vile mambo inaendelea kuwa mubaya sana mu “siku za mwisho,” ni wazi kwamba tutakuwa na nafasi mingi za kusaidiana. Tunaweza pia kuonyesha ndugu zetu upendo na kuwategemeza. Njia moya ya kufanya vile ni kufanya ndugu na dada wajisikie kuwa wanakaribishwa muzuri wakati wanafika ku Jumba ya Ufalme. Kwa hiyo, wakati ndugu na dada wanafika ku mikutano, tunajikaza kufanya yote yenye tunaweza ili wajisikie kuwa wanapendwa, wanatiwa moyo, na wako salama. Wazee wanaweza kuwa kimbilio kwa wale wenye wanapambana na magumu mbalimbali. Wakati wa misiba na wakati wa matatizo ya afya yenye inaomba kutenda kwa haraka, wazee wanakamata mipango ya kusaidia. Wanatoa pia musaada wa kiroho. Ndugu na dada watajisikia huru kukaribia muzee ikiwa ule muzee anajulikana kuwa mutu mupole, mwenye anajitia pa nafasi ya wengine, na mwenye iko tayari kusikiliza. Zile sifa zinafanya wengine wajisikie kuwa wanahangaikiwa. Kwa hiyo inakuwa mwepesi kwao kutumikisha muongozo wenye kutegemea Biblia wenye muzee anaweza kuwatolea.—1 Te. 2:​7, 8, 11. w24.06 29 fu. 12-13

Siku ya Posho, 28 Mwezi wa 11

Hakujizuia kutoa hata Mwana wake mwenyewe.—Ro. 8:32.

Juu Yehova ni Mweza-Yote, tusiwaze kama yeye hasikiake huzuni. Tuliumbwa kwa mufano ya Mungu na tunasikiaka huzuni, ni wazi kwamba Yehova naye anasikiaka huzuni. Biblia inasema kama Yehova naye ‘anahuzunikaka.’ (Zb. 78:​40, 41) Bila shaka Yehova alijisikia mubaya sana kupita Abrahamu wakati aliona watu wako natesa na kuua mutoto wake! Bei ya ukombozi inatufundisha kama hakuna mutu mwenye anatupenda sana kupita Yehova. Hata marafiki ao watu wa familia wa karibu sana hawatupendi kupita vile Yehova anatupenda. (Ro. 8:​32, 38, 39) Yehova anatupenda kupita hata vile tunajipenda. Unapenda kuishi milele? Yehova anapenda hata zaidi uishi milele. Unapenda zambi zako zisamehewe? Yehova anapenda hata zaidi kusamehe zambi zako. Anakuomba jambo moya tu: Ukubali zawadi ya bei ya ukombozi kwa kuonyesha imani na kwa kumutii. Bila shaka, bei ya ukombozi inaonyesha kabisa kama Yehova anatupenda.—Muh. 3:11. w25.01 22 fu. 8-9

Siku ya Yenga, 29 Mwezi wa 11

Muendelee kuhakikisha ni nini yenye kukubaliwa kwa Bwana.—Efe. 5:10.

Siye bote tunakamataka maamuzi yenye inategemea namna tunajisikia, mambo yenye tunaona, ao mambo yenye tunasikia. Lakini wakati fulani macho na masikio yetu inaweza kutudanganya. Hata kama haitudanganye, kama tunakamata maamuzi kwa kutegemea tu mambo yenye tunaona, tunaweza kuanza kutia pembeni mashauri ya Mungu. (Muh. 11:9; Mt. 24:​37-39) Lakini kama tunatembea kwa imani, inawezekana kabisa tukamate maamuzi yenye “kukubaliwa kwa Bwana.” Kufuata mashauri ya Mungu kutatusaidia tukuwe na amani ya moyo na kutatuletea furaha ya kweli. (Zb. 16:​8, 9; Isa. 48:​17, 18) Na kama tunaendelea kutembea kwa imani, tutapata uzima wa milele wakati wenye kuya. ( 2 Ko 4:18) Sasa, tutajua namna gani kama tuko natembea kwa imani ao kwa kuona? Juu tujue, ni muzuri tujiulize hii maulizo: Maamuzi yangu inategemea nini? Inategemea mambo yenye ninaona, ao inategemea mashauri ya Yehova? w25.03 20-21 fu. 3-4

Siku ya Kwanza, 30 Mwezi wa 11

Mukuwe wenye kufanya amani kati yenu.—1 Te. 5:13.

Kila mumoja wetu iko na daraka ya maana ya kusaidia wengine wapende kuingia mu paradiso ya kiroho. Ili kutimiza ile daraka tunapaswa kumuiga Yehova. Yehova hakaze watu waingie mu tengenezo yake. Lakini, kwa upole ‘anavuta’ watu kwake. (Yoh. 6:44; Yer. 31:3) Watu wenye mioyo mizuri wenye wamejifunza kuhusu sifa za muzuri za Yehova na kuhusu utu wake wenye kupendeza, wanachochewa kumukaribia. Namna gani, kupitia sifa zetu za muzuri na mwenendo wetu muzuri, tunaweza kusaidia watu wapende kuingia mu paradiso ya kiroho? Njia moya ya kufanya vile ni kutendea waamini wenzetu kwa wema na kwa upendo. Tunapenda wapya wenye wanafika ku mikutano yetu wajisikie sawa wale watu wenye hawakukuwa waamini, wenye inawezekana walihuzuria mikutano mu Korinto ya zamani. Walisema hivi: “Kwa kweli Mungu iko katikati yenu.” (1 Ko. 14:​24, 25; Zek. 8:23) Kwa hiyo, tunapaswa kuendelea kufuata hii shauri yenye kuwa mu andiko yetu ya leo. w24.04 23-24 fu. 16-17

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine