Mwezi wa 12
Siku ya Pili, 1 Mwezi wa 12
Akafungua akili zao waziwazi ili waelewe maana ya Maandiko.—Lu. 24:45.
Banafunzi ya Yesu balikubali Neno ya Mungu na balifanya yote juu ya kuitumikisha mu maisha yao. (Yoh. 17:6) Lakini balivurugika juu Yesu alikufa ku muti wa mateso sawa vile mutenda-zambi. Yesu alielewa kama balikuwa na mashaka, hapana juu balikuwa batu babaya, lakini juu habakuelewa mambo muzuri. (Lu. 9:44, 45; Yoh. 20:9) Kwa hiyo, alibafundisha kutumia Maandiko ili kuelewa mambo. Ona namna alifanya vile wakati alitokea banafunzi bawili mu njia ya kuenda Emau. Yesu hakuambia palepale bale banaume kama yeye ni nani. Lakini, alibauliza maulizo. Juu ya nini? Pengine alipenda baeleze mambo yenye ilikuwa mu akili na mu moyo wao. Na ni vile balifanya. Balimuambia kama balitazamia kuwa Yesu atakomboa Waisraeli kutoka mu mikono ya Waroma. (Lu. 24:18-27), Yesu alitumia Maandiko juu ya kubasaidia kuelewa mambo yenye ilitokea. Kisha, mangaribi ya ile siku Yesu alifasiria banafunzi bengine zile kweli.—Lu. 24:33-48. w24.10 14 fu. 9-10
Siku ya Tatu, 2 Mwezi wa 12
Sifanye jambo lolote kwa uamuzi wangu mwenyewe; lakini kama vile Baba alinifundisha, ni vile ninasema mambo haya.—Yoh. 8:28.
Yesu alijifunza kutoka kwa Baba yake wa mbinguni mambo ya kufanya na mambo ya kusema. Kwa kufuata mufano wa Yesu, tengenezo ya Yehova inatosha mu Neno ya Mungu mafundisho kuhusu mwenendo na muongozo wenye inatutolea. (2 Ti. 3:16, 17) Mara kwa mara tunakumbushwa kama tunapaswa kusoma Biblia na kutumikisha mambo yenye tunajifunza. Tunapata faida kubwa wakati tunajifunza Biblia kwa kutumia vichapo vyenye vinategemea Biblia. Kwa mufano ile inatusaidia tuweze kulinganisha mafundisho ya Biblia na muongozo wenye tengenezo inatutolea. Wakati tunaona kama ule muongozo unategemea Biblia, tunatumainia zaidi tengenezo ya Yehova. (Ro. 12:2) Yesu alihubiri “habari njema ya Ufalme wa Mungu.” (Lu. 4:43, 44) Pia, Yesu aliamuru wanafunzi wake wahubiri kuhusu Ufalme. (Lu. 9:1, 2; 10:8, 9) Leo, wote wenye kuwa mu tengenezo ya Yehova wanahubiri ujumbe wa Ufalme hata wakuwe wanaishi wapi. w24.04 9 fu. 5-7
Siku ya Ine, 3 Mwezi wa 12
Tutafanya mambo yote yenye umetuamuru, na tutaenda kila mahali kwenye utatutuma.—Yos. 1:16.
Endelea kutumainia muongozo wa kiteokrasi. Mu Israeli ya zamani, Yehova alitumia Musa na Yoshua ili kupatia watu wake maagizo. (Yos. 1:17) Waisraeli walibarikiwa wakati waliona wale wanaume kuwa wajumbe wa Yehova Mungu. Kisha miaka mingi, wakati kutaniko ya Kikristo ilianzishwa, mitume 12 njo walikuwa natoa muongozo. (Mdo. 8:14, 15) Kisha wazee wengine katika Yerusalemu waliongezwa mu ile kikundi. Wakati Wakristo walifuata muongozo wenye wale wanaume waaminifu walitoa, ‘makutaniko yaliendelea kuwa nguvu katika imani na hesabu ya waamini iliendelea kuongezeka siku kwa siku.’ (Mdo. 16:4, 5) Siye pia tunabarikiwa wakati tunafuata muongozo wa kiteokrasi wenye tengenezo ya Yehova inatutolea. w24.07 10 fu. 10
Siku ya Tano, 4 Mwezi wa 12
Nimemupata Daudi mwana wa Yese, mutu mwenye kufurahisha moyo wangu.—Mdo. 13:22.
Yehova alimupenda sana Mufalme Daudi. Na hata alimuona kuwa ‘mutu mwenye kufurahisha moyo wake.’ Lakini Daudi alifikia kufanya zambi nzito. Alifanya uzinifu na aliua. Kulingana na Sheria ya Musa, Daudi alipaswa kufa. (Law. 20:10; Hes. 35:31) Lakini Yehova alikamata hatua ya kumusaidia. Yehova alituma nabii Natani amutembelee Daudi, hata mbele Daudi aonyeshe alama yoyote ya toba. Natani alitumia mufano wenye ulikuwa na kusudi ya kugusa moyo wa Daudi. Daudi aliguswa sana na akatubu. (2 Sa. 12:1-14) Aliandika zaburi yenye ilionyesha namna alihuzunika sana juu ya makosa yake na namna alitubu. (Zb. 51, utangulizi) Ile zaburi imefariji watenda-zambi wengi na imewachochea kutubu. Hauone kama inafurahisha sana kuona namna Yehova, Mungu mwenye upendo, alimusaidia mutumishi wake juu afikie kutubu? w24.08 10 fu. 9
Siku ya Posho, 5 Mwezi wa 12
Mujihakikishie ninyi wenyewe mapenzi ya Mungu yenye kuwa mema na yenye kukubalika na makamilifu.—Ro. 12:2.
Batu mingi banakubali kama kuwa muzazi haiko kazi ya mwepesi. Kama uko muzazi na mutoto wako angali mudogo, tunakupongeza sana juu uko najikaza sana kumusaidia akuwe na imani ya nguvu. (Kum. 6:6, 7) Wakati mutoto wako anaendelea kukomala, anaweza kuanza kuuliza maulizo ya maana kuhusu mambo yenye tunaamini na kuhusu kanuni za Biblia za mwenendo. Ku mwanzo, maulizo ya mutoto wako inaweza kukufanya ukuwe na wasiwasi. Unaweza hata kuwaza kama mutoto wako iko nauliza ile maulizo juu hana imani. Lakini, wakati mutoto iko nakomala, iko na lazima ya kuuliza maulizo juu akuwe hakika na mambo yenye anaamini. (1 Ko. 13:11) Kwa hiyo usiogope. Wakati mutoto wako anauliza maulizo kuhusu mambo yenye tunaamini, uone ile kuwa nafasi ya kumusaidia akomalishe uwezo wake wa kufikiri. w24.12 14 fu. 1-2
Siku ya Yenga, 6 Mwezi wa 12
Sisi ni . . . namna ya watu wenye wako na imani ili kulinda uzima wetu.—Ebr. 10:39.
Wakristo Waebrania walikuwa na lazima ya imani ya nguvu juu ingewasaidia waokoe uzima wao wakati mateso makubwa ingetokea Yudea. (Ebr. 10:37, 38) Yesu aliambia wafuasi wake mbele ya wakati kama, wakati wataona maaskari wanazunguka Yerusalemu, wanapaswa kukimbilia ku milima. Ile shauri ya Yesu ilihusu Wakristo wote, ikuwe waliishi mu muji wa Yerusalemu ao mu maeneo ya pembeni-pembeni. (Lu. 21:20-24) Ile wakati, mu kipindi ya vita watu walizoea kukimbilia mu muji wenye kuzungukwa na ukuta sawa vile Yerusalemu. Iliomba imani ya nguvu ili kukimbilia mu eneo ya milima, juu kufanya vile ilionekana kama ni kukosa akili. Wakristo Waebrania walipaswa pia kutumainia watu wenye Yesu alikuwa anatumikisha ili kuongoza kutaniko. Inawezekana wenye walikuwa naongoza walipatia kutaniko maagizo yenye ingewasaidia wajue namna ya kukimbia na wakati wa kukimbia.—Ebr. 13:17. w24.09 10 fu. 9-10
Siku ya Kwanza, 7 Mwezi wa 12
Alitoa zawadi katika wanadamu.—Efe. 4:8.
Wakati alikuwa ku dunia Yesu alihangaikia kazi yenye Baba yake alimupatia. (Yoh. 17:4) Yesu hakukuwa na hii mawazo: ‘Kama unapenda kitu ifanyiwe muzuri, uifanye weye peke.’ Yesu alizoeza bengine. Alipatia banafunzi yake daraka ya kuhangaikia kondoo wa Mungu na ya kuongoza kazi ya kuhubiri na kufundisha. Yesu alipatia banafunzi yake mashauri yenye ilikuwa wazi lakini yenye upendo. Banafunzi yake fulani balikuwa na muelekeo wa kuwa na mashaka, kwa hiyo alibashauria. (Lu. 24:25-27; Yoh. 20:27) Alibaambia kama ni jambo ya maana sana kutia pa nafasi ya kwanza kazi ya uchungaji kuliko kazi ya kimwili. (Yoh. 21:15) Alibaambia kama haiko jambo ya maana kuhangaikia mapendeleo yenye bengine banaweza kupata. (Yoh. 21:20-22) Na alibasaidia kubadilisha mawazo fulani yenye balikuwa nayo juu ya Ufalme na akabasaidia kukazia akili kazi ya kuhubiri habari njema.—Mdo.1:6-8. w24.10 15-16 fu. 13-14
Siku ya Pili, 8 Mwezi wa 12
Wenye haki watariti dunia, na wataishi milele juu yake.—Zb. 37:29.
Kutii kunaleta uzima. Kama Waisraeli wenye walikuwa karibu kuingia mu inchi ya ahadi, tuko karibu kuingia mu ulimwengu mupya wenye Mungu ameahidi, dunia yote itageuzwa kuwa paradiso. (Isa. 35:1; Lu. 23:43) Shetani na pepo wake wachafu hawatakuwa tena. (Ufu. 20:2, 3) Hakutakuwa dini za uongo za kufanya watu wasimukaribie Yehova. (Ufu. 17:16) Hakutakuwa serikali za wanadamu zenye kutesa batu. (Ufu. 19:19, 20) Mu paradiso hamutakuwa waasi. (Zb. 37:10, 11) Fasi yote batu batatii sheria zenye haki za Yehova, na ile itafanya kukuwe umoja na amani. Kwa hiyo, batu batapendana na kutumainiana. (Isa. 11:9) Ile ni tumaini ya ajabu sana! Zaidi ya ile, kama tunamutii Yehova, tutaendelea kuishi mu paradiso, hapana tu mamia ya miaka, lakini milele. Yoh. 3:16. w24.11 9 fu. 7
Siku ya Tatu, 9 Mwezi wa 12
Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote.—Mt. 24:14.
Unabii wenye uko mu andiko ya siku ya leo uko natimia kabisa-kabisa wakati wetu. Ujumbe wa Ufalme uko nahubiriwa mu luga zaidi ya 1000, na kupitia site yetu jw.org, watu wengi mu dunia wanaweza kusikia ule ujumbe. Lakini, Yesu aliambia pia wanafunzi wake kama ‘hawatamaliza kuzunguka miji,’ ao kuhubiria watu wote mbele akuje. (Mt. 10:23; 25:31-33) Mambo yenye Yesu alisema inaonekana pia leo. Mamilioni ya watu wanaishi mu maeneo yenye kazi ya kuhubiri imetiliwa vizuizi. Zaidi ya ile, kila dakika mamia ya watoto wanazaliwa. Tunafanya yetu yote ili kutangazia habari njema “kila taifa na kabila na luga na watu.” (Ufu. 14:6) Lakini hata tufanye nini hatutaweza kutangazia kila mutu habari njema mbele mwisho ufike. w24.05 10 fu. 6-7
Siku ya Ine, 10 Mwezi wa 12
Hawako wawili tena, lakini mwili mumoja.—Mt. 19:6.
Yesu alitumia maneno yake juu ya kufariji na kutia moyo wengine. Hakuzungumuza na wafuasi wake kwa ukali. (Lu. 8:47, 48) Yesu ni mufano muzuri sana kwa bwana Wakristo! Yesu alisema kama bwana wanapaswa kubakia washikamanifu kwa bibi zao. Alirudilia maneno ya Baba yake, mwenye alisema kama mwanaume anapaswa ‘kushikamana na bibi yake.’ (Mt. 19:4-6) Maneno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa ‘kushikamana na’ yenye inatumiwa mu hii andiko, inamaanisha neno kwa neno “kubanisha vitu mbili kwa kutumia kolo.” Kwa hiyo, uhusiano kati ya bibi na bwana unapaswa kuwa nguvu sana sawa vile wamebananishwa na kolo. Wakiwaachanisha, wote wawili watalumia. Bwana mwenye anajikaza kuwa na uhusiano wa vile na bibi yake ataepuka kuangalia aina yoyote ya pornografia. Bila kukawia, atageuza macho yake juu “yasiangalie mambo yenye hayana mafaa yoyote.” (Zb. 119:37) Ni sawa vile anafanya agano na macho yake juu asiangalie kwa njia ya kutamani mwanamuke yeyote mwenye haiko bibi yake.—Yob. 31:1. w25.01 10 fu. 12-13
Siku ya Tano, 11 Mwezi wa 12
Mungu wetu . . . atasamehe kwa njia kubwa.—Isa. 55:7.
Ni nguvu kuelewa mutu anamaanisha nini wakati anakuambia kama anakusamehe. Namna Yehova anatusamehe siye wanadamu wenye hawakamilike iko tofauti sana na namna siye tunasemehe wengine. Musamaha wa Yehova ni wa pekee. Muandikaji fulani wa zaburi alisema hivi juu ya Yehova: “Wewe unatoa musamaha wa kweli, ili wakuogope sana.” (Zb. 130:4) Kwa kweli, musamaha wa Yehova ni “musamaha wa kweli.” Yeye njo anatuonyesha musamaha wa kweli nini kabisa. Ili kuzungumuzia musamaha wa Yehova, wakati fulani waandikaji wa Biblia walitumia neno fulani ya Kiebrania yenye kumaanisha musamaha yenye haiwezi kutumiwa juu ya musamaha wenye wanadamu wanaonyesha. Wakati Yehova anasamehe mutu, ni kusema zambi za ule mutu haziko tena. Na urafiki wenye Yehova alikuwa nao pamoya na ule mutu unarudia tena. Wakati Yehova anasamehe anafanya vile kabisa-kabisa na iko tayari kufanya vile tena na tena. w25.02 8 fu. 1-3
Siku ya Posho, 12 Mwezi wa 12
Alituamuru tuhubirie watu na kutoa ushahidi kamili.—Mdo. 10:42.
Kama watu wanakataa ujumbe wetu, ile haimaanishe kama hatukutimiza muzuri mugao wetu wa kuhubiri. Juu ya nini? Juu tumefanya mambo yenye Yehova na Mwana wake wanatuomba kufanya, ni kusema tumetoa ushahidi. Hata wakati hatupate mutu wa kuzungumuza naye mu mahubiri ao wakati watu wanakataa ujumbe wetu, tunaweza kuwa na furaha kwa sababu tunajua kama tuko namufurahisha Baba yetu wa mbinguni. (Mez. 27:11) Tunaweza pia kufurahi wakati muhubiri mwingine anapata mutu mwenye kupendezwa mu eneo. Munara wa Mulinzi umefananisha kazi yetu ya kuhubiri na kazi ya kutafuta mutoto mwenye amepotea. Watu wengi wanasaidia kutafuta, wanatafuta mu kila eneo. Wakati mutoto anapatikana, kila mutu anafurahi, hapana ule tu mwenye alimupata. Vilevile, kazi ya kufanya wanafunzi haiko kazi ya mutu mumoja, ni kazi yenye tunafanya siye wote pamoya. Siye wote tunapaswa kutumika pamoya ili kuhubiria eneo yote, na siye wote tunafurahi wakati mutu anaanza kukusanyika. w24.04 18 fu. 13-14
Siku ya Yenga, 13 Mwezi wa 12
Wote wenye walikuwa na muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele wakakuwa waamini.—Mdo. 13:48.
Tunangoya kwa hamu sana mambo yenye itatokea karibuni. Kwa musaada wa Yehova tunatumaini kama watu wengi zaidi watakubali kweli mbele taabu kubwa ianze. Pia tunafurahi kujua kama hata wakati wa taabu kubwa inawezekana watu fulani wataachana na ulimwengu wa Shetani na kujiunga na siye ili kumusifu Yehova! Lakini mbele ile wakati ifike, kwa sasa tuko na kazi ya kufanya. Tuko na pendeleo ya kutangaza ujumbe wenye hautatangaziwa tena, ni kusema kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu mu dunia yote. Wakati uleule, tunapaswa kuendelea kuonya watu. Watu wanapaswa kujua kama mwisho wa huu ulimwengu mubaya, uko nakaribia sana. Kupenda habari njema, kupenda watu, na zaidi ya yote kumupenda Yehova na jina yake. Ile mambo ituchochee basi kuendelea kuhubiri kwa bidii na kuona kama hii kazi ni ya haraka sana. Tufanye vile mupaka wakati Yehova atasema, “Basi, muache sasa!” w24.05 19 fu. 14-16
Siku ya Kwanza, 14 Mwezi wa 12
Muvae unyenyekevu wamoja kuelekea wengine, kwa sababu Mungu anawapinga wenye majivuno, lakini anawapatia wanyenyekevu fazili zenye hazistahiliwe.—1 Pe. 5:5.
Usiku mbele Yesu auawe, alifundisha Petro na mitume wengine somo ya maana sana juu ya unyenyekevu. Alifanya jambo yenye kwa kawaida mutumishi njo anafanyaka. Ile ilishangaza sana mitume wake. Yesu alitosha nguo yake ya inje, akajifunga mu kiuno nguo ya kupanguzia, akatia mayi mu beseni, na akaanza kunawisha mitume migulu. (Yoh. 13:4, 5) Inawezekana ilikamata wakati juu ya kunawisha migulu ya mitume wote 12, kutia ndani Yuda mwenye alifikia kumusaliti. Lakini kwa unyenyekevu Yesu alifanya ile kazi. Kisha Yesu akaambia mitume hivi: “Je, munaelewa jambo lenye nimewafanyia? Ninyi munaniita, ‘Mwalimu,’ na, ‘Bwana,’ na munasema kweli, kwa maana ni vile niko. Kwa hiyo, kama mimi mwenye ni Bwana na Mwalimu, niliwanawisha ninyi miguu, ninyi pia munapaswa kunawishana miguu.”—Yoh. 13:12-14. w25.03 10 fu. 9-11
Siku ya Pili, 15 Mwezi wa 12
Unaniongoza kupitia shauri lako, na kisha utaniongoza kwenye utukufu.—Zb. 73:24.
Ulimwengu unafanya ikuwe nguvu kwetu kubakia karibu na Yehova. Watu wengi wanasema kama Mungu haiko. Mara mingi wale wenye hawafuate mambo yenye Mungu anaomba wanaonekana kuwa na maisha ya muzuri. Kuona ile kunaweza kujaribu imani yetu. Ni kweli kwamba hatutasema kama Mungu haiko, lakini tunaweza kuanza kujiuliza ikiwa Mungu atatusaidia. Muandikaji wa Zaburi 73 alijiuliza pia vile. Aliona watu wenye hawakukuwa natii sheria za Mungu lakini walikuwa nafurahia maisha, na ile ilifanya aanze kujiuliza ikiwa kumutumikia Mungu kuko na faida. (Zb. 73:11-13) Ni nini ilisaidia ule muandikaji wa Zaburi abadilishe mawazo yake? Alitafakari juu ya mambo yenye itafikia wale wenye wanamusahau Yehova. (Zb. 73:18, 19, 27) Pia alifikiria faida za kumutumikia Mungu. Siye pia tunaweza kufikiria baraka zenye Yehova ametupatia. w24.06 25 fu. 16-17
Siku ya Tatu, 16 Mwezi wa 12
Njia yenu ya maisha ikuwe bila upendo wa feza.—Ebr. 13:5.
Zamani, watu fulani walikuwa naonea ndugu zao maskini, walikuwa nawakopesha na kuwaomba faida. Pia, waamuzi fulani walikuwa wanakubali rushwa na kisha walikuwa nahukumu bila haki watu wenye hawakukuwa na kosa. Yehova anachukia matendo ya vile. (Eze. 22:12) Ni muzuri tuchunguze namna yetu ya kuona makuta. Ujiulize hivi: ‘Mara mingi ninajikutaka niko nafikiria makuta na vitu vyenye ninaweza kuuza? Kama wananikopesha makuta, ninachelewaka kulipa, na kuwaza kama mutu mwenye alinikopesha hana lazima ya ile makuta? Kuwa na makuta kunanifanya nijisikie kuwa mutu wa maana na kunanifanya nikuwe muchoyo? Ninahukumu ndugu na dada zangu kuwa wanapenda vitu vya kimwili juu tu wako na makuta? Ninafanyaka urafiki na matajiri na kuepuka maskini?’ Tunaweza kulinda urafiki wetu pamoya na Mungu kwa kuendelea kuepuka kupenda makuta. Kama tunafanya vile, Yehova hatatuacha hata siku moya! w24.06 12-13 fu. 17-18
Siku ya Ine, 17 Mwezi wa 12
Ninakataa kutembea kwenye njia yoyote ya uovu, ili nishike neno lako.—Zb. 119:101.
Juu tujilinde ili tusiangukie mu jaribu, tunapaswa kukomalisha tamaa ya kufanya mambo ya muzuri. Kama tunajifunza ‘kuchukia mambo ya mubaya, na kupenda mambo ya muzuri,’ tutatia nguvu azimio yetu ya kufanya mambo yenye kuwa sawa. (Amo. 5:15) Tamaa ya kufanya mambo ya muzuri itatusaidia pia kukamata maamuzi ya muzuri wakati tunajikuta mu hali yenye inatujaribu. Tunapaswa kuwa na mambo mengi ya kiroho ya kufanya. Wakati tuko ku mikutano ao mu mahubiri, tunakomalisha tamaa ya kumufurahisha Yehova. (Mt. 28:19, 20; Ebr. 10:24, 25) Wakati tunasoma na kujifunza Neno ya Mungu na kutafakari sana juu ya mambo yenye tunajifunza, tunapenda sana kufanya mambo ya muzuri na tunachukia zaidi mambo ya mubaya. (Yos. 1:8; Zb. 1:2, 3; 119:97) Kumbuka kama Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: ‘Musali bila kuacha, ili musiingie katika jaribu.’ (Mt. 26:41) Kwa kufanya vile, tunamupatia nafasi ya kutusaidia na ya kutia nguvu azimio yetu ya kumufurahisha.—Yak. 4:8. w24.07 17 fu. 14-16
Siku ya Tano, 18 Mwezi wa 12
Nitakupatia ufahamu na kukufundisha katika njia yenye unapaswa kufuata. Nitakupatia shauri jicho langu likikuangalia.—Zb. 32:8.
Ni muzuri wale wenye wanazoeza wengine waige namna ya Yehova ya kupatia wengine hekima. Kumbuka kama Yehova anatoa hekima yake kwa ukarimu. Na siye tunaonyesha wengine mambo yote yenye tunajua. Hatufiche mambo fulani yenye tunajua juu ya kuogopa kama ule mwenye tuko nazoeza atakamata fasi yetu. Ao hatusemake: ‘Hakuna mwenye alinifundishaka, naye ajifunze ye peke.’ Ile mawazo ya vile haipaswe kuwa kati ya watu wa Yehova. Kwa furaha tunatoa mambo yenye tunajua lakini pia ‘tunapenda kuwapatia uzima wetu wenyewe’ wale wenye tuko nazoeza. (1 Te. 2:8) Tunatumaini kama, “nao watastahili kabisa kufundisha wengine.” (2 Ti. 2:1, 2) Kama kila mumoya wetu anapatia wengine hekima yenye iko nayo, siye wote tutaendelea kuwa na furaha zaidi. w24.09 29 fu. 12-13
Siku ya Posho, 19 Mwezi wa 12
Kila mumoja wetu ni kiungo cha mwingine.—Ro. 12:5.
Kama unawaza kama hauna uwezo fulani wa pekee, usivunjike moyo. Bila shaka uko na sifa zenye zinaweza kusaidia kutaniko. Kusali na kusoma mambo yenye Paulo alisema mu 1 Wakorinto 12:12-30, kunaweza kukusaidia. Maneno ya Paulo inaonyesha wazi kama kila mutumishi wa Yehova ni wa lazima mu kutaniko, ni kusema na weye uko wa lazima. Fanya yote yenye unaweza juu ya kumutumikia Yehova na kutumikia ndugu na dada zako. Ukuwe hakika kama wazee watafikiria hali yako na watakupatia mugao wenye uko na uwezo wa kutimiza. (Ro. 12:4-8) Wakristo wote wanapaswa kumukaribia Yehova, kutoa kwa furaha, na kuishi maisha yenye kumufurahisha Mungu. w24.11 17 fu. 12-13
Siku ya Yenga, 20 Mwezi wa 12
Akaanza kusali kwa Yehova na kulia bila kujizuia.—1 Sa. 1:10.
Hana alipata magumu ya mingi yenye ilimufanya alie kwa huzuni. Bwana yake alikuwa na bibi mwingine mwenye kuitwa Penina, na ule bibi alikuwa anamutendea Hana mubaya. Zaidi ya ile magumu, Hana hakukuwa nazala, lakini Penina alikuwa na batoto mingi. (1 Sa. 1:1, 2) Penina alikuwa anamuzarau Hana kila wakati juu hakukuwa anazala. Hana alihuzunika sana mupaka “alikuwa analia na hakukuwa anakula. . . . Alikuwa na uchungu mwingi sana” mu moyo wake. (1 Sa. 1:6, 7, 10) Nini njo ilimufariji Hana? Jambo moya yenye ilimusaidia ni kuenda kuabudu Yehova ku tabenakulo. Kule, alimulilia Yehova hivi: “[Ona] mateso ya mutumishi wako na kunikumbuka.” (1 Sa. 1:11) Yehova aliona huzuni yake, alisikia kilio yake, na kisha alimubariki kwa kumupatia mutoto.—1 Sa. 1:19, 20; 2:21. w24.12 21 fu. 5-7
Siku ya Kwanza, 21 Mwezi wa 12
Wana wa binadamu ndio nilipenda zaidi sana.—Mez. 8:31.
Bei ya ukombozi inatufundisha kama Yesu anahangaikia sana watu, zaidi sana wanafunzi wake. (Yoh. 13:1) Kwa mufano, Yesu alijua kama angepata magumu mingi mu utumishi wake ku dunia na angekufa kifo ya maumivu. Lakini alitimiza utumishi wake ku dunia, haiko juu alilazimika kufanya vile, lakini juu alipenda watu. Alihubiri, alifundisha, na kusaidia wengine kwa moyo wake wote. Hata siku ya kifo yake, Yesu alikamata wakati wa kusafisha migulu ya mitume wake, kuwafundisha mambo mingi, na kuwafariji. (Yoh. 13:12-15) Kisha, wakati alikuwa ku muti wa mateso, Yesu alikamata wakati fulani juu ya kupatia tumaini mutenda-maovu mwenye alikuwa pembeni yake. Alikamata pia mipango juu kukuwe mutu wa kuhangaikia mama yake. (Lu. 23:42, 43; Yoh. 19:26, 27) Yesu alikuwa na upendo mingi sana, ule upendo ulionekana kupitia kifo yake lakini pia kupitia maisha yake yote ku dunia. w25.01 23 fu. 11
Siku ya Pili, 22 Mwezi wa 12
Alibeba azabu kwa ajili ya amani yetu, na kwa sababu ya vidonda vyake tuliponyeshwa.—Isa. 53:5.
Biblia inatumia neno ya mufano ili kutusaidia kuelewa uhuru wenye tunakuwa nao wakati Yehova anatusamehe. Juu tuko watenda-zambi na tuko na muelekeo wa kufanya zambi tuko “watumwa wa zambi.” Lakini kupitia musamaha wa Yehova tuko sawa vile watumwa wenye ‘wamewekwa huru kutoka katika zambi.’ (Ro. 6:17, 18; Ufu. 1:5) Kwa kweli, wakati Yehova anatusamehe tunasikia furaha sana, sawa watu wenye wamewekwa huru kutoka katika utumwa. Tumeponyeshwa kwa njia ya mufano kupitia zabihu ya ukombozi yenye Yehova alitoa kupitia Mwana wake.(1 Pe. 2:24) Wakati tunafanya zambi tunaharibu urafiki wetu pamoya na Yehova, lakini kwa sababu ya zabihu ya ukombozi, Yehova anaweza kutusamehe na tunaweza tena kuwa na urafiki muzuri pamoya naye. Sawa tu vile mutu mweye ameponyeshwa ugonjwa mubaya sana anasikiaka furaha sana, siye pia tunafurahi sana kwa sababu tumeponyeshwa kupitia musamaha wa Yehova na anatukubali tena. w25.02 11 fu. 16, 17
Siku ya Tatu, 23 Mwezi wa 12
Kama munaendelea kufanya mambo hayo, hamutashindwa hata kidogo.—2 Pe. 1:10.
Mu mufano wa talanta, Yesu anazungumuzia watumwa wawili wenye walikuwa waaminifu kwa bwana wao na mumoya mwenye hakukuwa muaminifu. (Mt. 25:14-30) Wale watumwa wawili waaminifu wanafananisha Wakristo watiwa-mafuta waaminifu. Bwana wao Yesu anawaalika ‘waingie katika furaha ya bwana wao.’ Wanapokea zawabu yao ya mbinguni, ni kusema ufufuo wa kwanza. (Mt. 25:21, 23; Ufu. 20:5b) Lakini mufano mubaya wa mutumwa muvivu ni onyo kwa Wakristo watiwa-mafuta. Namna gani? Wanapaswa kutumika kwa bidii. Sawa mu mufano wa mabikira, mu mufano wa talanta Yesu hakukuwa anatabiri kama watiwa-mafuta watakuwa wavivu. Lakini alikuwa anafasiria mambo yenye inaweza kutokea ikiwa wanaacha kutumika kwa bidii. Wakifanya vile watashindwa “kufanya mwito na kuchaguliwa [kwao] kukuwe hakika,” na hawataruhusiwa kuingia mu Ufalme wa mbinguni. w24.09 22 fu. 10; 23 fu. 12-13
Siku ya Ine, 24 Mwezi wa 12
Muhakikishe mambo ya maana zaidi.—Flp. 1:10.
Siye bote tunapendaka kuwa na kazi yenye itatusaidia kutimiza mahitaji yetu na ya batu ya familia yetu. (Muh. 7:12; 1 Ti. 5:8) Wakati tuko naamua ikiwa tutakubali kazi fulani ao hapana. Ni jambo ya kawaida kufikiria tutakuwa napata makuta ngapi. Lakini kama ile tu njo jambo yenye tunafikiria mbele ya kukamata uamuzi, ile itaonyesha kama tuko natembea kwa kuona. Kama tunatembea kwa imani, tutafikiria pia matokeo yenye kazi itakuwa nayo juu ya uhusiano wetu pamoya na Yehova. Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Hii kazi itaniomba nifanye mambo yenye Yehova anachukia?’ (Mez. 6:16-19) ‘Itanizuia kufanya mambo fulani ya kiroho, na pengine kufanya nikuwe mbali na familia yangu kwa wakati murefu?’ Kusema kweli haikuwake mwepesi kupata kazi. Lakini kama unajibia ndiyo hata ku ulizo moya kati ya ile maulizo, ni jambo ya hekima usikubali ile kazi. Juu tunatembea kwa imani, tunakamata maamuzi yenye inaonyesha kama tuko hakika kama Yehova atatupatia mambo yenye tuko nayo lazima.—Mt. 6:33; Ebr. 13:5. w25.03 21 fu. 5-6
Siku ya Tano, 25 Mwezi wa 12
Mukuwe wenye fazili ninyi kwa ninyi, wenye huruma nyingi, na musameheane kwa kupenda.—Efe. 4:32.
Sikuzote tunapaswa kujikaza kuona ndugu na dada zetu Wakristo sawa vile Yehova anawaona. Tunafanya vile kwa kukazia akili sifa zao za muzuri hapana uzaifu wao, wenye utafikia kuisha kabisa. Tunaweza kumaliza kwa njia ya upendo matatizo ya kukosa kuelewana. Ile itafanya watu wenye wanapenda kutendewa kwa upendo, wapende kuingia mu paradiso ya kiroho. Tuazimie basi kuwa wenye shukrani milele kwa sababu ya paradiso ya kiroho yenye Yehova ametupatia. Kila mutu mwenye hapendi kukosa kitu, mwenye anapenda kutosheka, kutulia, na kuwa salama, anapaswa kuingia mu paradiso ya kiroho na anapaswa kubakia ndani milele! Lakini, ukuwe muangalifu juu Shetani iko nafanya yake yote ili kutudanganya na kutufanya tutoke mu paradiso ya kiroho. (1 Pe. 5:8; Ufu. 12:9) Tusimuruhusu afanye vile. Kwa nguvu yetu yote, tuendelee basi kulinda uzuri, usafi, na amani ya paradiso yetu ya kiroho. w24.04 24-25 fu. 18-19
Siku ya Posho, 26 Mwezi wa 12
Tafuta kwanza Ufalme.—Mt. 6:33.
Wazazi, munaweza kusaidia watoto wenu wamutumikie Yehova kwa bidii. Mufundishe watoto wenu kupitia maneno na matendo kama mambo ya kiroho sawa vile kujifunza Biblia, kuhuzuria mikutano, na kuhubiri, njo mambo ya maana zaidi kupita mambo ingine yote. Kama hamufanye vile, watoto wenu wanaweza kumutumikia Yehova juu tu nyie wazazi wao muko Mashahidi wa Yehova, haiko juu wao wenyewe wanamupenda kabisa. Matokeo itakuwa nini? Hawatatia ibada ya kweli pa nafasi ya kwanza ao hata wanaweza kuacha kabisa kumutumikia Yehova. Kama mutu ameacha kumutumikia Yehova, ni kusema hakuna tena tumaini? Hapana, kuko tumaini juu anaweza kutubu na kurudilia tena ibada safi. Lakini juu afanye vile, anapaswa kujishusha na kukubali musaada wa wazee wa kutaniko. (Yak. 5:14) Mambo yote yenye mutu anaweza kujikaza kufanya juu ya kumurudilia Yehova, haiko kitu tukiilinganisha na furaha ya kuwa tena rafiki yake! w24.07 24-25 fu. 18-19
Siku ya Yenga, 27 Mwezi wa 12
Mukimbie uasherati!—1 Ko. 6:18.
Munaweza kufanya nini ili urafiki wenu umuletee Yehova sifa? Kadiri urafiki wenu utaendelea kukomaa, ni vile kila mumoja wenu atavutiwa zaidi na mwenzake. Nini njo inaweza kuwasaidia muendelee kuwa na mwenendo safi? Muepuke mazungumuzo machafu, kupitisha wakati nyie wawili tu, na kunywa sana. (Efe. 5:3) Ile mambo inaweza kuamusha tamaa zenu za ngono na kufanya ikuwe nguvu kwenu kutii kanuni za Yehova. Hamuone kama itakuwa muzuri mukuwe nazungumuzia mipaka yenye munapaswa kukamata ili uhusiano wenu umuletee Yehova sifa? (Mez. 22:3) Kadiri upendo wenu unaendelea kukomaa, haiko mubaya kuonyesha upendo mu njia fulani zenye kufaa. Lakini kama tamaa yako ya ngono inakuwa nguvu sana, itakuwa nguvu sana kwako kukamata uamuzi muzuri. (Wim. 1:2; 2:6) Pia wakati muko naonyeshana upendo, inaweza kuwa mwepesi kukosa kujizuia na kufanya jambo fulani yenye haitamufurahisha Yehova. (Mez. 6:27) Kwa hiyo, ku mwanzo wa uhusiano wenu, muzungumuzie mipaka yenye mutaheshimia yenye kupatana na kanuni za Biblia.— 1 Te. 4:3-7. w24.05 29 fu. 10-11
Siku ya Kwanza, 28 Mwezi wa 12
Muache tu neno lenu ‘Ndiyo’ limaanishe ndiyo, na ‘Hapana’ yenu imaanishe hapana.—Mt. 5:37.
Tunapenda wengine watutumainie, zaidi sana wakati wanapambana na magumu. (Mez. 17:17) Tunaweza kufanya nini juu tukuwe watu wenye wengine wanaweza kutegemea? Tujikaze kila siku kuonyesha sifa za Kikristo. Kwa mufano tujikaze kutimiza ahadi zetu na kufanya yetu yote ili kuheshimia wakati. Wazee wenye kutegemeka ni baraka kwa kutaniko. Namna gani? Wakati wazee wanapatikana wakati wowote wenye wahubiri wako nao lazima, wahubiri wanajisikia kuwa wenye kutulia. Wanajisikia pia kuwa wanahangaikiwa muzuri wakati wanajua kama wazee wako tayari kuwasaidia. Wanatumainia wazee wakati wanaona kama mashauri yao inategemea Biblia na vichapo vya mutumwa muaminifu na mwenye busara kuliko kutegemea mawazo yao wenyewe. Ndugu na dada wanatumainia zaidi sana muzee mwenye anajua kuchunga siri na mwenye anatimiza mambo yenye anaahidi. w24.06 30 fu. 14-15
Siku ya Pili, 29 Mwezi wa 12
Utawapatia amani ya kudumu,kwa sababu wanakutegemea wewe.—Isa. 26:3.
Hatuwezi kutazamia kama Yehova atatosha magumu yetu yote kwa sasa, lakini tunaweza kuwa hakika kama atatutegemeza. (Zb. 41:3) Kupitia roho yake takatifu, Yehova anatupatia nguvu, hekima, na amani ya moyo ili tuweze kuvumilia. (Mez. 18:14; Flp. 4:13) Pia anatutegemeza kupitia tumaini yenye kuwa mu Biblia yenye inaonyesha kama magonjwa yote itaisha. (Isa. 33:24) Mu Biblia muko maneno yenye Yehova aliandikisha, yenye inaweza kutufariji wakati tuko napambana na hali za nguvu. (Ro. 15:4) Wakati dada moya wa mu Afrika ya Mangaribi alipata habari kama iko na ugonjwa wa cancer, alilia mara mingi. Anasema hivi: “Andiko moya yenye ilinifariji sana ni Isaya 26:3. . . . Ile andiko ilinihakikishia kama Yehova anaweza kutupatia amani ya moyo yenye itatusaidia kuamua namna tutatenda wakati tunapata magumu.” Kuko andiko yenye inakutulizaka wakati uko mu hali ya nguvu, pengine mu hali yenye unaona kama hakuna jambo ya kufanya? w24.12 24 fu. 17-18
Siku ya Tatu, 30 Mwezi wa 12
Wakati alikuwa angali mbali, baba yake akamuona na akamusikilia huruma, akamukimbilia, akamukumbatia kwa upole wote na kumubusu.—Lu. 15:20.
Wazee wanajikaza kuonyesha roho ya kusamehe kwa wale wenye wamepotea. Wanapenda wale kondoo wenye wamepotea “warudie ku nyumba.” (Lu. 15:22-24, 32) Wakati mutenda-zambi anarudia, mbinguni kunakuwaka furaha na ku dunia pia! (Lu. 15:7) Tunaona kama Yehova hakubali wakosaji wenye wanakatala kutubu. Lakini anaendelea kujaribu kuwasaidia. Anapenda wamurudilie. Hosea 14:4 inaonyesha namna Yehova anajisikia juu ya wakosaji wenye wanatubu: “Nitaponyesha ukosefu wao wa uaminifu. Nitawapenda kwa kupenda kwangu mwenyewe, kwa sababu kasirani yangu imegeuka.” Kujua mawazo ya Yehova juu ya wakosaji, kunachochea wazee watafute alama yoyote yenye inaonyesha kama mutu anaanza kutubu. Na kunachochea pia wale wenye walimuacha Yehova wamurudilie bila kukawia. w24.08 28 fu. 8-9
Siku ya Ine, 31 Mwezi wa 12
Mujionyeshe kuwa wenye shukrani.—Kol. 3:15.
Kusema kweli, watu fulani hawataonyesha shukrani. Tunaweza kutumikisha nguvu yetu, wakati yetu, ao hata vitu vyetu juu ya kusaidia mutu, lakini ule mutu haonyeshe kama anafurahia mambo yenye tulimufanyia. Kama hali ya vile inafika, namna gani tunaweza kuepuka kukasirika na kupoteza furaha yetu? Kumbuka kama furaha yetu ya kutoa haitegemee namna watu watatenda wakati tunawapatia kitu fulani. (Mdo. 20:35) Tunaweza kuamua kuendelea kuwa na furaha hata kama wengine hawaonyeshe shukrani. Namna gani? Kumbuka kama ni Yehova njo tuko naiga. Anapatia watu vitu vizuri ikuwe wataonyesha shukrani ao hapana. (Mt. 5:43-48) Yehova anaahidi kama ikiwa na siye tunapatia wengine “bila kutumaini kurudishiwa kitu chochote, zawabu [yetu] itakuwa kubwa.” (Lu. 6:35) “Kitu chochote” kinaweza kuwa kuonyeshwa shukrani. Ikuwe wengine wanaonyesha shukrani ao hapana, Yehova atatulipa juu ya mambo ya muzuri yenye tuko nafanya, juu ‘tunatoa kwa furaha.’—Mez. 19:17; 2 Ko. 9:7. w24.09 29 fu. 14-16