Siku ya Ine, 16 Mwezi wa 4
Katika taabu yangu nilimuitia Yehova, . . . na kilio changu cha kumuomba musaada kikafika katika masikio yake.—Zb. 18:6.
Mufalme Daudi alimujua Yehova na alimutegemea. Wakati alikuwa nakimbia maadui wake, kutia ndani Mufalme Sauli, Daudi aliomba Yehova amusaidie. Kisha Mungu kujibia sala yake na kumuokoa, Daudi alisema hivi: “Yehova ni mwenye kuishi.” (Zb. 18:46) Wakati Daudi alisema ile maneno hakukuwa tu anamaanisha kuwa anajua kama Mungu iko. Kitabu fulani kinasema kama Daudi alikuwa naonyesha kuwa iko hakika kama Yehova “ni Mungu mwenye kuishi mwenye anatenda kwa ajili ya watu wake sikuzote.” Kwa kweli Daudi alijionea mu maisha yake namna Yehova ni Mungu mwenye kuishi, na kujua vile kulifanya aazimie kabisa kumutumikia na kumusifu. (Zb. 18:28, 29, 49) Kuwa hakika kama Yehova ni Mungu mwenye kuishi kunaweza kutusaidia tuendelee kumutumikia kwa bidii. Tutakuwa na nguvu ya kuvumilia magumu na tutachochewa kuendelea kumutumikia Mungu kwa nguvu yetu yote. Pia tutaazimia kuendelea kubakia karibu na Yehova. w24.06 20-21 fu. 3-4
Siku ya Tano, 17 Mwezi wa 4
Musiache mutu yeyote awadanganye ninyi kwa njia yoyote.—2 Te. 2:3.
Maneno ya mutume Paulo kwa Watesalonike inaweza kutufundisha nini? Wakati tunasikia habari fulani yenye haipatane na mambo yenye tumejifunza mu Biblia ao wakati tunasikia habari za ajabu-ajabu, tunapaswa kuwa na utambuzi. Wakati wa utawala wa Wasovieti, maadui wetu walipatia ndugu barua yenye ilisemekana kuwa inatoka ku makao makubwa. Ile barua ilitia moyo ndugu fulani wajitenge na tengenezo na wafanyize kikundi yao. Ile barua ilionekana kuwa ya kweli. Lakini ndugu waaminifu hawakudanganywa. Walitambua kama ujumbe wenye ulikuwa mu ile barua haukupatana na mambo yenye walikuwa wamefundishwa. Leo, wakati fulani maadui wetu wanatumia teknolojia ya sasa ili kujaribu kutuvuruga na kutugawanya. Kama ile hali inatokea, “akili [yetu] isivurugwe haraka,” tujilinde kwa kujiuliza ikiwa mambo yenye tunasikia inapatana na kweli zenye tunajua tayari.—2 Te. 2:2; 1 Yo. 4:1. w24.07 12 fu. 14-15
Siku ya Posho, 18 Mwezi wa 4
Kama mutu yeyote anafanya zambi, tuko na musaidizi.—1 Yo. 2:1.
Uamuzi wa maana zaidi wenye mutu anaweza kukamata ni uamuzi wa kujitoa kwa Yehova na kuingia mu familia ya waabudu wake. Yehova anapenda batu yote bafanye vile. Juu ya nini? Anapenda bakuwe barafiki yake na baishi milele. (Kum. 30:19, 20; Gal. 6:7, 8) Lakini, Yehova hakaze mutu kumutumikia. Anaacha kila mutu aamue mambo yenye atafanya. Sasa mambo itakuwa namna gani kama Mukristo mwenye kubatizwa anavunja sheria ya Mungu na kufanya zambi nzito? Kama hatubu, anapaswa kuondolewa mu kutaniko. (1 Ko. 5:13) Hata vile, Yehova anatumainia kabisa kama ule mutenda-zambi atamurudilia. Na ile njo sababu kubwa yenye ilifanya Yehova atoe zabihu ya ukombozi, juu watenda-zambi wenye kutubu waweze kusamehewa. Yehova ni Mungu mwenye upendo sana, anaomba watenda-zambi watubu.—Zek. 1:3; Ro. 2:4; Yak. 4:8. w24.08 14 fu. 1-2