Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • es26 uku. 98-108
  • Mwezi wa 10

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mwezi wa 10
  • Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
  • Vichwa Vidogo
  • Siku ya Ine, 1 Mwezi wa 10
  • Siku ya Tano, 2 Mwezi wa 10
  • Siku ya Posho, 3 Mwezi wa 10
  • Siku ya Yenga, 4 Mwezi wa 10
  • Siku ya Kwanza, 5 Mwezi wa 10
  • Siku ya Pili, 6 Mwezi wa 10
  • Siku ya Tatu, 7 Mwezi wa 10
  • Siku ya Ine, 8 Mwezi wa 10
  • Siku ya Tano, 9 Mwezi wa 10
  • Siku ya Posho, 10 Mwezi wa 10
  • Siku ya Yenga, 11 Mwezi wa 10
  • Siku ya Kwanza, 12 Mwezi wa 10
  • Siku ya Pili, 13 Mwezi wa 10
  • Siku ya Tatu, 14 Mwezi wa 10
  • Siku ya Ine, 15 Mwezi wa 10
  • Siku ya Tano, 16 Mwezi wa 10
  • Siku ya Posho, 17 Mwezi wa 10
  • Siku ya Yenga, 18 Mwezi wa 10
  • Siku ya Kwanza, 19 Mwezi wa 10
  • Siku ya Pili, 20 Mwezi wa 10
  • Siku ya Tatu, 21 Mwezi wa 10
  • Siku ya Ine, 22 Mwezi wa 10
  • Siku ya Tano, 23 Mwezi wa 10
  • Siku ya Posho, 24 Mwezi wa 10
  • Siku ya Yenga, 25 Mwezi wa 10
  • Siku ya Kwanza, 26 Mwezi wa 10
  • Siku ya Pili, 27 Mwezi wa 10
  • Siku ya Tatu, 28 Mwezi wa 10
  • Siku ya Ine, 29 Mwezi wa 10
  • Siku ya Tano, 30 Mwezi wa 10
  • Siku ya Posho, 31 Mwezi wa 10
Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
es26 uku. 98-108

Mwezi wa 10

Siku ya Ine, 1 Mwezi wa 10

Nitaendelea kumungojea Yehova.—Mik. 7:7.

Mara mingi tunapataka muongozo juu tuweze kumutumikia Yehova muzuri. Ile muongozo inatoka kwa wazee, waangalizi wa muzunguko, biro ya tawi, ao Baraza Yenye Kuongoza. Lakini tutafanya nini kama hatuelewe juu ya nini tunapewa muongozo fulani? Pengine tunaweza kuanza kuona tu matokeo ya mubaya yenye ule muongozo unaweza kuwa nao. Na hata, tunaweza kuanza kukazia akili uzaifu wa ndugu wenye wanatupatia muongozo. Wakati tunatembea kwa imani, tuko hakika kama ni Yehova njo anaongoza tengenezo yake, na anajua hali yetu. Kwa hiyo tunatii bila kukawia na tunafanya vile kwa kupenda. (Ebr. 13:17) Tunajua kama wakati tunatii tunasaidia kutaniko iendelee kuwa na umoja. (Efe. 4:​2, 3) Na tunajua kuwa hata kama bandugu benye kutuongoza habakamilike, Yehova atatubariki juu tuko natii. (1 Sa. 15:22) Na kama kuko mambo yenye inaomba kabisa kurekebisha, kwa wakati wenye kufaa Yehova atatengeneza mambo. w25.03 24 fu. 13-14

Siku ya Tano, 2 Mwezi wa 10

Mungu . . . [ni] Mufunuaji wa siri.—Da. 2:28.

Tunaishi mu kipindi ya ajabu sana! Kila siku, tuko najionea namna unabii wa Biblia uko natimia. Kwa mufano, tuko naona namna “mufalme wa kaskazini” na “mufalme wa kusini” wako napigania utawala wa ulimwengu. (Da. 11:​40, maelezo ya chini) Tuko naona namna habari njema iko nahubiriwa sana vile haiyahubiriwaka, na mamilioni ya watu wako nakubali kweli. (Isa. 60:22; Mt. 24:14) Na tuko napata chakula mingi ya kiroho “kwa wakati wenye kufaa.” (Mt. 24:​45-47) Yehova anaendelea kutusaidia kuelewa muzuri zaidi matukio makubwa yenye kuwa mbele yetu. (Mez. 4:18) Tunaweza kuwa hakika kama, mbele taabu kubwa ianze, tutajua mambo yote yenye tuko nayo lazima ili tuendelee kuvumilia kwa uaminifu na tuendelee kuwa na umoja mu ile kipindi ya nguvu sana. Lakini, tunapaswa kukubali kama kuko mambo fulani yenye hatujue kuhusu mambo yenye itatokea hivi karibuni. w24.05 8 fu. 1-2

Siku ya Posho, 3 Mwezi wa 10

Hasingizie kwa ulimi wake.—Zb. 15:3.

Muandikaji wa Zaburi anazungumuzia kusingizia. Kusingizia maana yake nini? Ni maneno ya uongo yenye inaweza kuharibu sifa ya mutu. Zaburi 15:3 inatukumbusha kama wageni wa Yehova hawatendee majirani wao mambo ya mubaya na hawaharibishie marafiki wao sifa. (Zb. 15:1) Tunaweza kuharibishia wengine sifa namna gani? Bila kukusudia, tunaweza kuharibishia mutu sifa kwa kueneza habari zenye haziko za kweli juu yake. Kwa mufano: (1) dada anaacha upainia, (2) bibi na bwana hawatumikie tena ku beteli, ao (3) ndugu haiko tena mutumishi wa huduma ao muzee. Hauone kama haiko muzuri kuwazia-wazia sababu zenye zilifanya hali za wale watu zibadilike na kujaribu kuzielezea wengine? Pengine kuko sababu zenye zilifanya ile mabadiliko itokee zenye siye hatujue. Zaidi ya ile, mugeni mu hema ya Yehova “hamutendee jirani yake jambo lolote la mubaya, naye hawaharibishie marafiki wake sifa.” w24.06 11 fu. 11-13

Siku ya Yenga, 4 Mwezi wa 10

Ninamuweka Yehova mbele yangu kila wakati. Kwa sababu iko kwenye mukono wangu wa kuume, sitatikiswa hata kidogo.—Zb. 16:8.

Juu tumuogope Yehova zaidi, tunapaswa kufanya yetu yote ili kumufurahisha mu kila uamuzi wenye tunakamata. Wakati uko nasoma habari za Biblia, ujiulize hivi: ‘Kama ningekuwa pale, ningekamata uamuzi gani?’ Kwa mufano, wazia uko pale wakati wale wapelelezi kumi Waisraeli wanaleta habari ya kuvunja moyo kisha kupeleleza inchi yenye Yehova alikuwa ameahidi kama atapatia Waisraeli. Utaamini habari yao na kuanza kuogopa wanadamu, ao hautaogopa juu unamupenda Yehova na unapenda kumufurahisha? Kizazi yote ya Waisraeli ilishindwa kutambua kweli yenye Yoshua na Kalebu walisema. Matokeo ilikuwa nini? Walipoteza pendeleo ya kuingia mu inchi ya ahadi.—Hes. 14:​10, 22, 23. w24.07 10 fu. 7

Siku ya Kwanza, 5 Mwezi wa 10

Yehova ndiye anachunguza mioyo.—Mez. 17:3.

Gomeri, bibi ya nabii Hosea aliacha Hosea na kuenda kwa banaume bengine. Gomeri angeweza kubadilika na kutubu? Yehova mwenye anasomaka moyo aliambia hivi Hosea: “Uende tena, umupende ule mwanamuke mwenye anapendwa na mwanaume mwingine na mwenye anafanya uzinifu, kama vile Yehova anapenda watu wa Israeli wakati wanageuka kuelekea miungu mingine.” (Ho. 3:1; Mez. 16:2) Tunaona kama bibi ya Hosea alikuwa angali anafanya zambi nzito. Lakini Yehova alimuambia Hosea akamate hatua ya kuenda kumutafuta, amusamehe, na amufanye tena kuwa bibi yake. Vilevile, Yehova hakuachilia batu yake benye balikuwa habayabadilika. Hata kama balikuwa bangali nafanya zambi nzito, Yehova aliendelea kubapenda. Na aliendelea kukamata hatua juu ya kubasaidia batubu na babadilishe njia zao. Ile mufano inaonyesha kama Yehova, mwenye “anachunguza mioyo,” atakamata hatua ya kusaidia mutu mwenye angali anafanya zambi nzito juu ya kujaribu kumusaidia atubu. w24.08 10 fu. 7

Siku ya Pili, 6 Mwezi wa 10

Sheria iko na kivuli cha mambo ya muzuri yenye yatakuja.—Ebr. 10:1.

Wayahudi wenye walifikia kuwa Wakristo wa kwanza-kwanza walipata magumu ya nguvu. Zamani Wayahudi walikuwa taifa yenye Yehova alichagua. Yerusalemu njo iliwakilisha Ufalme wa Mungu ku dunia, na hekalu njo ilikuwa fasi ya maana sana kwenye ibada safi ilifanyika. Wayahudi wote waaminifu walifuata Sheria ya Musa na sheria zingine zenye wakubwa wa dini waliwapatia. Zile sheria njo ziliongoza maisha yao yote: Mambo sawa vile kutahiriwa, chakula yenye walipaswa kula, na hata namna yao ya kutendea Watu wa Mataifa. Lakini kisha kifo ya Yesu, Yehova hakukubali tena zabihu zenye Wayahudi walitoa ku hekalu. Ile ilikuwa tatizo kwa Wakristo Wayahudi juu walizoea kufuata Sheria. (Ebr. 10:​1, 4, 10) Ilikuwa nguvu kujipatanisha na ile mabadiliko hata kwa Wakristo wenye kukomala kiroho, sawa vile mutume Petro. (Mdo. 10:​9-14; Gal. 2:​11-14) Wakubwa wa dini ya Wayahudi walianza kutesa Wakristo Wayahudi juu ya mambo ya mupya yenye waliamini. w24.09 9 fu. 4

Siku ya Tatu, 7 Mwezi wa 10

Mukumbuke wale wenye wanaongoza kati yenu, wenye wamewafundisha neno la Mungu.—Ebr. 13:7.

Wakati Yehova anapatia watu wake mugao, anatazamia watimize mu namna yenye kupangwa muzuri. (1 Ko. 14:33) Kwa mufano, Yehova anapenda habari njema ihubiriwe mu dunia yote yenye kuikaliwa na watu. (Mt. 24:14) ameweka Yesu asimamie ile kazi. Yesu amehakikisha kwamba ile kazi inafanywa mu njia yenye kupangwa muzuri. Mu karne ya kwanza, wakati makutaniko ilikuwa naanzishwa mu maeneo mbalimbali, wazee waliwekwa ili watolee ndugu muongozo na ili wasimamie kazi. (Mdo. 14:23) Mu Yerusalemu, baraza yenye kuongoza yenye ilifanyizwa na mitume na wanaume wazee, ilikamata maamuzi fulani yenye makutaniko yote ilipaswa kufuata. (Mdo. 15:2; 16:4) Juu makutaniko ilitii maagizo yenye ilipewa, ‘iliendelea kuwa nguvu katika imani na hesabu ya waamini iliendelea kuongezeka.’—Mdo. 16:5. w24.04 8 fu. 1

Siku ya Ine, 8 Mwezi wa 10

Maria Magdalene akakuja na kuletea wanafunzi habari: “Nimemuona Bwana!”—Yoh. 20:18.

Asubui ya Nisani 16, kikundi ya banamuke baaminifu inaenda ku kaburi ya Yesu. (Lu. 24:​1, 10) Acha tuzungumuzie mufano wa mwanamuke moya kati yao, Maria Magdalene. Wakati alifika ku kaburi, mwili wa Yesu haukukuwa ndani. Alikimbia na kuenda kumujulisha Petro na Yohana. Kisha, wakati Petro na Yohana walikimbia kuenda ku kaburi, alikuwa nabafuata. Kisha kuhakikisha kama mwili wa Yesu haukukuwa mu kaburi, Petro na Yohana balirudia. Lakini Maria hakurudia. Alibakia pale ku kaburi na iko nalia. Hata kama Maria hakujua, Yesu alikuwa namuona. Yesu aliona machozi ya ule mwanamuke muaminifu na ile ilimugusa sana. Kwa hiyo, alimutokea Maria na alimufanyia kitu fulani ya mwepesi yenye ilimutia moyo sana. Alizungumuza naye na alimupatia mugao wa lazima sana. Mugao ya kuenda kuambia ndugu zake kama Yesu amefufuliwa.—Yoh. 20:​17, 18. w24.10 13 fu. 7

Siku ya Tano, 9 Mwezi wa 10

Nitafanya alama na miujiza mingi katika inchi ya Misri.—Kut. 7:3.

Musa alikuwa nabii, muamuzi, kiongozi, na muandikaji. Aliongoza Waisraeli kutoka mu utumwa Misri na alijionea miujiza mingi ya Yehova. Yehova alimutumikisha juu ya kuandika vitabu tano vya kwanza vya Biblia, Zaburi 90, na inawezekana Zaburi 91. Pia inawezekana ni Musa njo aliandika kitabu ya Yobu Wakati kidogo mbele akufe, wakati alikuwa na miaka 120, Musa aliita Waisraeli wote juu ya kuwakumbusha mambo yenye walikuwa wameona. Walijionea, wakati balikuwa vijana namna Yehova alifanya miujiza mingi na namna alihukumu Wamisri. (Kut. 7:4) Walitembea ku inchi kavu wakati mayi ya Bahari Nyekundu iliachanishwa, na waliona namna maaskari wa Farao waliharibiwa. (Kut. 14:​29-31) Wakati walikuwa mu jangwa, waliona vile Yehova aliwalinda na kuwahangaikia. (Kum. 8:​3, 4) Waisraeli walikuwa sasa karibu kuingia mu inchi ya ahadi na Musa alitumia ile nafasi ya mwisho juu ya kuwatia moyo. w24.11 8-9 fu. 3-4

Siku ya Posho, 10 Mwezi wa 10

Kama mutu yeyote anakula mukate huu ataishi milele. . . Mukate wenye nitatoa ni mwili wangu kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.—Yoh. 6:51.

Mambo yenye Yesu aliambia mitume wake wakati wa Chakula cha Mangaribi cha Bwana ilihusu batu kidogo. Lakini maneno yenye alisema katika Galilaya ilihusu batu mingi zaidi. Wakati Yesu alikuwa Galilaya mu mwaka wa 32, alikuwa nazungumuza na Wayahudi wenye walikuwa wanamutafuta juu awapatie mukate. Lakini, Yesu alizungumuza nao juu ya jambo fulani ya maana zaidi kupita chakula. Alizungumuzia mupango wenye ungewasaidia kupata uzima wa milele. Yesu alisema pia kama wale wenye walikuwa wamekufa wangefufuliwa siku ya mwisho na kuishi milele. Yesu hakukuwa nazungumuzia batu kidogo, sawa vile alifanya wakati wa Chakula cha Mangaribi cha Bwana. Lakini, mu Galilaya Yesu alikuwa nazungumuzia baraka yenye batu yote bangeweza kupata. w24.12 11 fu. 10-11

Siku ya Yenga, 11 Mwezi wa 10

Bwana, muendelee kupenda bibi zenu.—Kol. 3:19.

Yehova anachukia kila mutu mwenye jeuri. (Zb. 11:5) Anachukia sana wakati bwana anapiga bibi yake. (Mal. 2:16) Kama bwana hatendee bibi yake muzuri, ile inaweza kuwa na matokeo ya mubaya juu ya uhusiano wake pamoya na Yehova. Yehova anaweza hata kukatala kusikiliza sala zake. (1 Pe. 3:7) Bwana fulani wanatendea bibi zao mubaya kwa kuwaambia maneno makali na yenye kuumiza. Lakini Yehova anachukia “hasira, kasirani kali, kufoka, [na] matukano.” (Efe. 4:​31, 32) Bwana mwenye anazungumuza na bibi yake kwa ukali, anaharibisha ndoa yake lakini pia urafiki wake pamoya na Mungu. (Yak. 1:26) Ni vile pia kuhusu bwana mwenye anaangalia pornografia. Naye pia anaharibisha urafiki wake pamoya na Yehova, na anashushia bibi yake heshima. Yehova anapenda bwana aendelee kuwa mushikamanifu kwa bibi yake, hapana tu mu matendo lakini pia mu mawazo. Yesu alisema kama mwanaume mwenye anaangalia mwanamuke kwa kumutamani, tayari amefanya naye uzinifu “katika moyo wake.”—Mt. 5:​28, 29. w25.01 9 fu. 6-8

Siku ya Kwanza, 12 Mwezi wa 10

Mutu anatangazwa kuwa mwenye haki . . . kupitia tu imani katika Yesu Kristo.—Gal. 2:16.

Kutangazwa kuwa wenye haki maana yake Yehova hatuombe tulipie zambi zenye tunafanya. Kwa kufanya vile, Yehova havunje kanuni zake za haki. Haiko juu tunastahili njo anatutangaza kuwa wenye haki; na ile haimaanishe kama anakubali zambi zetu. Lakini juu tuko na imani katika mupango wa kufunika zambi na bei ya ukombozi, ile inafanya Yehova aweze kutusamehe zambi zetu. (Ro. 3:24) Ile inaletea kila mumoya wetu faida gani? Wale wenye wamechaguliwa ili kutawala pamoya na Yesu mbinguni, tayari wametangazwa kuwa wenye haki na wamekuwa watoto wa Mungu. (Tit. 3:7; 1 Yo.3:1) Zambi zao zimesamehewa. Ni sawa vile hawayafanyaka zambi, na kwa hiyo wanastahili kuwa katika Ufalme. (Ro. 8:​1, 2, 30) Wengine wenye wametangazwa kuwa wenye haki wataishi milele ku dunia. Yehova amesamehe zambi zao na wamekuwa marafiki wake.—Yak. 2:​21-23. w25.02 5 fu. 17-18

Siku ya Pili, 13 Mwezi wa 10

Unawaza mawazo ya wanadamu, lakini haiko mawazo ya Mungu.—Mt. 16:23.

Wakati fulani, namna ya kufikiri ya mutume Petro haikupatana na namna ya kufikiri ya Yehova. Yesu aliambia mitume wake kama ataenda Yerusalemu, na kule viongozi wa dini watamukamata, atateswa, na kisha atauawa. (Mt. 16:21) Pengine ilikuwa nguvu kwa Petro kukubali kama Yehova ataruhusu Yesu, tumaini ya Israeli na Masiya mwenye aliahidiwa, auawe. (Mt. 16:16) Kwa hiyo Petro alimubeba Yesu pembeni na akamuambia hivi: “Jitendee kwa fazili, Bwana; mambo hayo hayatakupata hata kidogo.” (Mt. 16:22) Petro hakukuwa na mawazo sawa ya Yehova juu ya ile jambo, njo maana mawazo yake haikupatana na mawazo ya Yesu. Pengine Petro alikuwa na nia ya muzuri, lakini Yesu alikatala shauri yake. Ile inatufundisha jambo ya maana. Mapenzi ya Yehova haikukuwa Yesu akwepe mateso. Mu ile hali, Petro alijifunza somo ya maana sana kuhusu namna ya kupatanisha mawazo yake na mawazo ya Yehova. w25.03 9 fu. 5-6

Siku ya Tatu, 14 Mwezi wa 10

Yehova iko karibu na wale wenye kuvunjika moyo; anaokoa wale wenye kupondwa roho.—Zb. 34:18.

Uko najisikia mubaya juu mutu fulani alikuvunja moyo ao mutu fulani mwenye ulikuwa natumainia alikusaliti? Hata mutu akutendee namna gani, Baba yako wa mbinguni yeye anakupenda tu. Wakati banatusaliti, tunaweza kufarijiwa na maneno yenye kutia moyo yenye Daudi alisema mu andiko ya siku ya leo. Kitabu fulani inasema kama benye “kupondwa roho” banaweza kuwa “benye habatumainie kama kuko jambo yoyote ya muzuri yenye itabafikia.” Yehova anasaidia namna gani bale benye banajisikia vile kwa sababu bamevunjwa moyo? Sawa vile muzazi mwenye upendo anabebaka mutoto wake na kumufariji wakati mutoto iko nalia, Yehova “iko karibu na” siye wakati mutu fulani anatusaliti ao anatuacha. Yehova anasikia maumivu yenye tuko nasikia na anatusaidia bila kukawia. Iko tayari kutufariji wakati tuko na maumivu mu moyo na wakati tunajiona kuwa wa bure. Na anatuahidi mambo mingi ya muzuri yenye inatusaidia tuvumilie magumu yetu ya leo.—Isa. 65:17. w24.12 23 fu. 13-14

Siku ya Ine, 15 Mwezi wa 10

Mutapokea kutoka kwa Yehova . . . zawabu.—Kol. 3:24.

Leo, wazee wanaweza kuwa hakika kama Yehova anaona na anafurahia kazi yao ya muzuri. Zaidi ya kufanya kazi ya uchungaji, kufundisha, na kuhubiri, wazee wengi wanategemeza kazi ya ujenzi na ya kutoa misaada. Wengine wanatumika mu Vikundi vya Kutembelea Wagonjwa, ao mu Halmashauri za Uhusiano na Hopitale. Wazee wenye wanajitolea ili kusaidia mu zile kazi wanaona kutaniko kuwa ya Yehova. Wanatimiza migao yao kwa moyo wote na wako hakika kama Mungu atawapatia zawabu kwa sababu ya mambo yote yenye wanafanya. (Kol. 3:​23, 24) Siye wote hatuwezi kuwa wazee, lakini siye wote tunaweza kumutolea Yehova jambo fulani. Yehova anafurahi wakati tunafanya yetu yote ili kumutumikia. Anaona michango yenye tunatoa kwa ajili ya kazi ya mu dunia yote, hata kama ni ya kidogo sana. Na anafurahi wakati tunaamua kusamehe wengine. Ukuwe hakika kama Yehova anaiona kuwa ya maana. Ile inafanya akupende na atakupatia zawabu.—Lu. 21: 1-4. w24.06 23 fu. 12-13

Siku ya Tano, 16 Mwezi wa 10

Musiruhusu moyo wenu ugeuke na kufuata njia zake. Musipotee njia na kufuata njia zake.—Mez. 7:25.

Mufano wenye Sulemani alitoa unaonyesha jambo yenye inaweza kufikia muabudu yeyote wa Yehova. Anaweza kuangukia mu zambi nzito na kuwaza kama mambo ilitokea mara moja ao kwa kushitukia. Ao anaweza kusema, “nilishituka tu nilishafanya zambi.” Lakini, kama anafikiri juu ya mambo yenye ilitokea, anaweza kutambua kama alichukua hatua fulani za mubaya zenye zilimuongoza kwenye zambi. Pengine alikuwa na marafiki wabaya, alianza kujifurahisha na mambo yenye haifae, alikuwa naenda fasi zenye kuwa hatari, ao kuingia mu site zenye kuwa hatari. Pia, pengine alikuwa ameacha kusali, kusoma Biblia, kuenda ku mikutano, na kuhubiri. Sawa ule kijana mwenye kuzungumuziwa mu Mezali, inawezekana hakuangukia mu zambi kwa kushitukia tu. Tunajifunza nini? Hatupaswe tu kuepuka zambi, tunapaswa pia kuepuka mambo yote yenye inaweza kutuongoza kwenye zambi. Kisha tu kuzungumuzia ile habari, Sulemani anakazia pia ile wazo.—Mt. 5:​29, 30. w24.07 16 fu. 10-11

Siku ya Posho, 17 Mwezi wa 10

Tuko na hazina hii katika vyombo vya udongo.— 2 Ko. 4:7.

Ile hazina ni nini? Ni kazi ya kuhubiri ujumbe wa Ufalme wenye unaweza kuokoa uzima. (2 Ko. 4:1) Vyombo vya udongo ni nini? Vinafananisha watumishi wa Mungu, wenye wanahubiria wengine habari njema. Mu wakati wa Paulo, wafanyabiashara walizoea kuweka mu mitungi ya udongo vitu vya maana sawa vile chakula, divai, na makuta. Vilevile, Yehova ametupatia ujumbe wa maana, ni kusema habari njema. Kwa musaada wa Yehova, tunaweza kuwa na nguvu yenye tuko nayo lazima ili kutangazia wengine ule ujumbe kwa uaminifu. Wakati fulani, tunaweza kuogopa watu. Namna gani tunaweza kupambana na ile hali? Fikiria sala yenye mitume walitoa wakati wapinzani waliwaamuru waache kuhubiri. Kuliko kuogopa, walimuomba Yehova awasaidie waendelee kusema kwa uhodari. Bila kukawia Yehova alijibia sala yao. (Mdo. 4:​18, 29, 31) Kama wakati fulani unaogopa watu, umuombe Yehova akusaidie ili upendo wako kwa watu ukuwe nguvu zaidi kuliko woga wako. w24.04 16 fu. 8-9

Siku ya Yenga, 18 Mwezi wa 10

Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe.—Mt. 6:9.

Upendo wetu kwa Yehova unatuchochea tutakase jina yake. Tunapenda kuchangia kutakasa jina ya Mungu, kwa kuambia wengine kama mambo yenye Shetani anasema juu ya Mungu ni ya uongo kabisa. (Mwa. 3:​1-5; Yob. 2:4; Yoh. 8:44) Mu mahubiri tuko tayari kutetea Mungu wetu na kuambia wenye wanapenda kutusikiliza mambo ya kweli kumuhusu. Tunapenda watu wote wajue kama sifa yake kubwa zaidi ni upendo, kama namna yake ya kutawala njo ya muzuri zaidi na yenye haki, na kama karibuni Ufalme wake utamaliza mateso yote na kuletea wanadamu wote amani na furaha. (Zb. 37:​10, 11, 29; 1 Yo. 4:8) Wakati tunamutetea Yehova mu mahubiri tunatakasa jina yake. Tunafurahi pia juu tuko natimiza daraka yetu ya kuwa Mashahidi wake. w24.05 18 fu. 12

Siku ya Kwanza, 19 Mwezi wa 10

Wakati unatayarisha karamu, ualike maskini, viwete, vilema, na vipofu; na utakuwa mwenye furaha, kwa sababu hawana kitu cha kukulipa. Kwa maana utalipwa katika ufufuo wa wenye haki.—Lu. 14:​13, 14.

Ndugu, unaonyesha kama uko “mukaribishaji-wageni” wakati unafanyia bengine mambo ya muzuri, hata benye habiko barafiki yako ya karibu. (1 Pe. 4:9) Kitabu fulani inasema hivi juu ya mwanaume mwenye ni mukaribishaji-wageni: “Mulango wa nyumba yake na wa moyo wake unapaswa kuwa wazi kwa ajili ya batu benye hajue.” Ujiulize hivi: ‘Najulikana kuwa mutu mwenye anakaribishaka bageni?’ (Ebr. 13:​2, 16) Mwanaume mwenye ni mukaribishaji-wageni anachangia kidogo yenye iko nayo pamoya na bengine. Kwa mufano anaalika Wakristo wenye hawana bitu mingi na Wakristo wenye kutumika kwa bidii, sawa vile waangalizi wa muzunguko na wasemaji wageni.—Mwa. 18:​2-8; Mez. 3:27; Mdo. 16:15; Ro. 12:13. w24.11 21 fu. 6

Siku ya Pili, 20 Mwezi wa 10

Wale mabikira wenye walikuwa tayari wakaingia pamoja naye kwenye karamu ya ndoa.—Mt. 25:10.

Mu mufano wa mabikira, Yesu anazungumuzia mabikira kumi wenye walienda kukutana na bwana-arusi. (Mt. 25:​1-4) Wote walitumaini kama watamusindikiza bwana-arusi ku karamu yake ya ndoa. Yesu alisema kama mabikira tano wa kwanza walikuwa “wenye busara” na wengine tano walikuwa “wapumbavu.” Mabikira wenye busara walijitayarisha muzuri kumuchunga bwana-arusi hata kama anakuya nyuma sana katika usiku. Njo maana walileta tala za mafuta juu ziwaangazie usiku. Walileta hata mafuta ingine pembeni yenye ingewasaidia kama bwana-arusi anakawia. Kwa hiyo walijitayarisha muzuri juu tala zao zisizimike. (Mt. 25:​6-10) Wakati bwana-arusi alifika, wale mabikira wenye busara waliingia pamoya naye mu karamu ya ndoa. Vilevile, Wakristo watiwa-mafuta wenye wataendelea kuwa tayari na kubakia macho na waaminifu mupaka wakati Kristo atafika, watastahili kuingia pamoya na Bwana-arusi, ni kusema Yesu Kristo, mu Ufalme wa mbinguni.—Ufu. 7:​1-3. w24.09 21 fu. 6

Siku ya Tatu, 21 Mwezi wa 10

Nikaona. . . kundi kubwa la watu . . . kutoka mataifa yote.—Ufu. 7:9.

Wakati tunafikiria mambo yote yenye iko natimizwa mu dunia leo, ile inatuchochea tuhubiri kwa bidii. Kila mwaka, mamilioni ya batu benye kupendezwa banafika ku Ukumbusho na banaanza kujifunza Biblia. Maelfu ya batu banabatizwa na banajiunga na siye mu kazi ya kuhubiri. Hatujue ni batu bengine ngapi batatusikiliza, lakini tunajua kama Yehova iko nakusanya kundi kubwa ya batu benye bataokoka taabu kubwa yenye iko nakuya. (Ufu. 7:​9, 14) Bwana wa mavuno angali anaona kama kungali batu benye batakubali habari njema, ile inapaswa kutuchochea tuendelee kuhubiri kwa bidii. (Luke 10:2) Tangu zamani banafunzi ya Yesu banajulikana kuwa bahubiri benye bidii. Wakati watu waliona mitume wa Yesu wanahubiri kwa bidii na bila kuogopa, “wakaanza kutambua kwamba walikuwa pamoja na Yesu.” (Mdo. 4:13) Leo wakati batu banatuona mu mahubiri, banaweza kutambua kama na siye tunafuata mufano wa Yesu wa kuhubiri kwa bidii. w25.03 18 fu. 15; 19 fu. 17-18

Siku ya Ine, 22 Mwezi wa 10

Ee Yehova, mwanadamu ni nini ili umutambue?—Zb. 144:3.

Biblia inaonyesha kama Yehova anaona batu benye bengine banaona kuwa ba hali ya chini. Kwa mufano, Yehova alimutuma nabii Samweli ku nyumba ya Yese juu atie mafuta mutoto wake umoya mwenye angefikia kuwa mufalme wa Israeli. Yese alikuwa na batoto banaume munane, lakini aliita batoto saba bakutane na Samweli. Hakuita Daudi mwenye alikuwa mudogo zaidi. Lakini ni Daudi njo Yehova alichagua. (1Sa.16:​6, 7, 10-12) Yehova aliona moyo wa Daudi, aliona kama alikuwa kijana mwanaume mwenye alihangaikia mambo ya kiroho. Fikiria mambo yenye Yehova amefanya juu ya kuonyesha kama anakujua. Anakupatia mashauri yenye inapatana kabisa na hali yako. (Zb. 32:8) Anaweza kufanya vile namna gani kama hakujue muzuri? (Zb. 139:1) Wakati unatumikisha mashauri ya Yehova na kuona namna inakusaidia, utakuwa hakika kama Yehova anakuhangaikia. (1 Ny. 28:9; Mdo. 17:​26, 27) Yehova anaona mambo yote yenye uko nafanya juu ya kumutii na kumutumikia. Yehova anaona sifa za muzuri zenye uko nazo na anapenda kuwa rafiki yako.—Yer. 17:10. w24.10 25-26 fu. 7-9

Siku ya Tano, 23 Mwezi wa 10

Akawasikilia huruma, kwa sababu walikuwa kama kondoo wenye hawana muchungaji.—Mk. 6:34.

Bila shaka unamupenda Yehova na unapenda kutumikia bengine. Unaweza kufanya nini juu upende zaidi kutumikia bengine? Fikiria furaha yenye utapata wakati unatumikia ndugu na dada zako. Yesu alisema hivi: “Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.” (Mdo. 20:35) Yesu alitumikisha ile maneno mu maisha yake. Kutumikia bengine kulimuletea furaha. Fikiria mufano wenye kuwa mu Marko 6:​31-34. Ile siku Yesu na mitume wake walichoka sana. Walikuwa naenda fasi kwenye wangekuwa peke yao na kupumuzika. Lakini batu mingi balifika kule mbele yabo na balipenda Yesu abafundishe. Yesu angeweza kusema hapana juu yeye na mitume wake “hawakupata hata wakati wa kula chakula.” Ao Yesu angewafundisha tu jambo moya ao mbili. Lakini juu alikuwa na upendo, ‘alianza kuwafundisha.’ mupaka “saa ilikuwa imepita.”—Mk. 6:35. w24.11 16 fu. 9-10

Siku ya Posho, 24 Mwezi wa 10

Kazi yenu itapewa zawabu.—2 Ny. 15:7.

Muzazi, tia mutoto wako moyo atafute nafasi za kuzungumuza na wengine juu ya mafundisho ya Biblia. (Ro. 10:10) Unaweza kumusaidia aone kama kufundisha batu Biblia iko sawa vile kujifunza chombo fulani ya muziki. Ku mwanzo, mutu mwenye iko najifunza anaanzaka kwanza na nyimbo za teketeke. Kisha wakati, itakuwa mwepesi zaidi kwake kutumikisha ile chombo ya kupiga muziki. Vilevile, ku mwanzo kijana Mukristo anaweza kuanza mazungumuzo mu njia ya mwepesi. Kwa mufano, anaweza kuuliza hivi mwanafunzi mwenzake: “Unajua kama batu banaiga vitu vyenye kuwa mu ulimwengu juu ya kutengeneza vitu mbalimbali vya mupya? Acha nikuonyeshe video moya ya muzuri.” Kisha kuonyesha video yenye kuwa ku sehemu Kitu Hiki Kilijifanya Chenyewe?, kijana Mukristo anaweza kusema hivi: “Kama wanasayansi wanapewa sifa juu vitu vyenye wametengeneza kwa kuiga vitu vyenye tayari viko mu ulimwengu, unawaza nani njo anastahili sifa juu ya vitu vya mu ulimwengu vyenye waliiga?” Ile namna ya mwepesi ya kuanzisha mazungumuzo inaweza kufanya kijana mwenzake apendezwe na apende kujua mambo mingi zaidi. w24.12 19 fu. 17-18

Siku ya Yenga, 25 Mwezi wa 10

Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi.—Ro. 5:12.

Ili kutukomboa kutoka mu zambi na kifo, Yehova alifanya mipango juu Yesu atoe zabihu ya ukombozi. Namna gani zabihu ya mutu moya mukamilifu ingeweza kukomboa mamilioni ya watu? Mutume Paulo alifasiria hivi: “Kama vile kupitia kukosa kutii kwa ule mutu mumoja [Adamu] wengi walifanywa kuwa watenda-zambi, vilevile pia kupitia kutii kwa mutu mumoja [Yesu] wengi watafanywa kuwa wenye haki.” (Ro. 5:19; 1 Ti. 2:6) Mu maneno ingine, ni kupitia mwanadamu moya mukamilifu mwenye hakutii njo tulifikia kuwa watumwa wa zambi na kifo. Njo maana, kupitia mwanadamu moya mukamilifu mwenye kutii tunaweza kukombolewa. Yehova hangeacha tu watoto wa Adamu wenye wanamutii waishi milele? Mwanadamu mwenye hakamilike anaweza kuona kama ile njo ingekuwa namna ya muzuri ya kumaliza ile mambo. Lakini kuwaza vile ni kusahau kama haki ya Yehova ni kamilifu. Juu Yehova ni mwenye haki, hangefanya sawa vile Adamu hakufanya zambi wakati alikatala kutii. w25.01 21 fu. 3-4

Siku ya Kwanza, 26 Mwezi wa 10

Tunatembea kwa imani, hapana kwa kuona.—2 Ko. 5:7.

Wakati fulani, mutume Paulo alijua kama balikuwa kumuua. Lakini alifurahi wakati alifikiria namna alitumia maisha yake. Njo maana alisema hivi: “Nimekimbia mbio mupaka mwisho, nimeshika imani.” (2 Ti. 4:​6-8) Paulo alikamata maamuzi ya hekima mu utumishi wake kwa Yehova. Na alikuwa hakika kama Yehova alimufurahia. Na siye tunapenda kukamata maamuzi ya muzuri na kukubaliwa na Yehova. Tunaweza kufanya vile namna gani? Paulo alisema hivi juu yake na juu ya Wakristo wengine waaminifu: “Tunatembea kwa imani, hapana kwa kuona.” Mu Biblia neno ‘kutembea,’ inatumiwa wakati fulani juu ya kuzungumuzia namna mutu anatumia maisha yake. Wakati mutu anatembea kwa imani, anakamata maamuzi yenye inaonyesha kama anamutegemea Yehova. Matendo yake inaonyesha kama iko hakika kama Mungu atamubariki, na kama kufuata mashauri ya Yehova yenye kuwa mu Neno yake, kutamuletea faida.—Zb. 119:66; Ebr. 11:6. w25.03 20 fu. 1-2

Siku ya Pili, 27 Mwezi wa 10

Mugeuzwe kwa kufanya upya akili yenu.—Ro. 12:2.

Kwa musaada wa roho ya Mungu, watu wengi wenye zamani walikuwa na tabia za kinyama, wamefanya mabadiliko makubwa mu maisha yao. (Isa. 65:25) Wameachana na tabia zao za mubaya. (Efe. 4:​22-24) Kusema kweli, tungali wanadamu wenye hawakamilike, wakati fulani tunafanya makosa. Lakini, Yehova ameunganisha “watu wa namna zote” wenye wanamupenda na wanapendana. Ile inafanya tukuwe na amani na umoja. (Tit. 2:11) Ule ni muujiza wenye Mungu Mweza-Yote tu njo anaweza kufanya! Maneno yake haiwezi kukosa kutimia. (Isa. 55:​10, 11) Leo, paradiso ya kiroho iko kabisa. Yehova amefanya familia ya pekee sana ya watu wenye kumuabudu. Kati ya watu wake, tunaweza kupata amani na kujisikia kuwa salama kadiri inawezekana mu huu ulimwengu wenye muvurugo. (Zb. 72:7) Njo maana, tunapenda kusaidia watu wengi kadiri inawezekana waingie mu familia yetu ya ndugu na dada. Tunaweza kufanya vile kwa kutia kazi ya kufanya wanafunzi pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu.—Mt. 28:​19, 20. w24.04 23 fu. 13, 15

Siku ya Tatu, 28 Mwezi wa 10

Sisi tuko na akili ya Kristo.—1 Ko. 2:16.

Yesu alimupenda Yehova kwa akili yake yote. Alijua mambo yenye Mungu alipenda afanye na aliazimia kuishi kulingana nayo, hata kama kufanya vile kungemuletea mateso. Juu Yesu alikazia akili kufanya mapenzi ya Baba yake, hakuacha jambo yoyote imuzuie kuifanya. Petro na mitume wengine walikuwa na pendeleo ya kupitisha wakati pamoya na Yesu na kujifunza namna yake ya kufikiri. Wakati Petro aliandika barua yake ya kwanza yenye iliongozwa na roho ya Mungu, alitia moyo Wakristo wajipatie nguvu kwa muelekeo uleule wa Kristo. (1 Pe. 4:1) Wakati Petro aliandika “mujipatie nguvu,” alitumia maneno yenye mu luga ya kwanza-kwanza ilitumiwa juu ya kuzungumuzia askari mwenye anavala silaha ili kujitayarisha kwa ajili ya vita. Kwa hiyo, kama Wakristo wanaiga muelekeo wa akili wa Yesu ao namna yake ya kufikiri, watakuwa na silaha yenye nguvu yenye itawasaidia kupiganisha muelekeo wa kufanya zambi na vishawishi vya mu hii dunia yenye kutawaliwa na Shetani.—2 Ko. 10:​3-5; Efe. 6:12. w25.03 8-9 fu. 1-3

Siku ya Ine, 29 Mwezi wa 10

Mawazo ya moyo wa mutu ni kama maji yenye kuenda chini sana, Lakini mutu mwenye utambuzi anayashota.—Mez. 20:5.

Wakati uko nafanya urafiki wa kimapenzi, ni mambo gani ingine yenye unapaswa kujua juu ya mwenzako? Mbele upendo wako kwa ule mutu ukuwe nguvu sana, inaweza kuwa muzuri muzungumuzie mambo fulani ya maana sana sawa vile miradi yake. Unaweza kufanya nini juu ujue mutu muzuri kabisa? Jambo moya ya maana ya kufanya ni kuzungumuza waziwazi na bila kuficha kitu, kuuliza maulizo, na kusikiliza kwa uangalifu. (Yak. 1:19) Ili kufanya vile, inaweza kuwa muzuri kufanya mambo fulani yenye inawapatia nafasi ya kuzungumuza. Sawa vile kula pamoya, kutembea pamoya mahali pa watu wengi, na kuhubiri pamoya. Munaweza pia kujuana muzuri wakati munapitisha wakati pamoya na marafiki na watu wa familia. Zaidi ya ile, panga kufanya mambo yenye inaweza kukusaidia kujua namna mwenzako anatendaka mu hali tofauti-tofauti na wakati iko na watu tofauti-tofauti. w24.05 28 fu. 6-7

Siku ya Tano, 30 Mwezi wa 10

Mukuwe waigaji wa Mungu, kama watoto wapendwa.—Efe. 5:1.

Mu siku zenye ziko nakuya, tutakutana na magumu ya nguvu yenye itaomba tumutegemee Yehova tena zaidi. Habari kuhusu watumishi wa Yehova wenye kuzungumuziwa mu Biblia na kuhusu watumishi wa Yehova leo zitatusaidia kuona namna Yehova ametegemeza watumishi wake. Fikiria sana zile habari. Kufanya vile kutakusaidia ufanye Yehova kuwa Mwamba wako. Pia utakuwa tayari kutia nguvu ndugu na dada zetu. Kwa mufano, Yesu alipatia Simoni jina Kefa (yenye inatafsiriwa “Petro”), yenye inamaanisha “Kipande ya Mwamba.” (Yoh. 1:42) Ile ilionyesha kama Petro angetia nguvu na kutegemeza wengine mu kutaniko. Wazee wa kutaniko wanafananishwa na “kivuli cha mwamba mukubwa.” Ile inaonyesha namna wanalinda kutaniko. (Isa. 32:2) Lakini, kutaniko inapata faida wakati ndugu na dada wote wanajikaza kuiga sifa zenye zinamufanya Yehova kuwa mwamba. w24.06 28 fu. 10-11

Siku ya Posho, 31 Mwezi wa 10

Yehova . . . anataka watu washikamane na yeye tu.—Kum. 4:24.

Wafalme wa Israeli wenye Yehova aliona kuwa waaminifu walimuabudu mu njia yenye anapenda. Wafalme wengi wenye Yehova aliona kuwa wabaya waliacha Sheria yake na wakaanza kuabudu miungu ya uongo. (1 Fa. 21:​25, 26; 2 Ny. 12:1) Sababu gani mambo yenye kuhusu ibada ilikuwa ya maana sana kwa Yehova? Sababu moya ni hii: Wafalme walipaswa kusaidia watu wamuabudu Yehova mu njia ya muzuri. Pia ibada ya uongo inachocheaka watu kufanya zambi zingine nzito na inaletaka matendo ya ukosefu wa haki. (Hos. 4:​1, 2) Zaidi ya ile, wafalme na watu wenye walikuwa chini ya mamlaka yao, walikuwa wamejitoa kwa Yehova. Njo maana Biblia inalinganisha ibada ya uongo na uzinifu. (Yer. 3:​8, 9) Mutu mwenye anafanya uzinifu anakosea sana tena sana bibi ao bwana yake. Ni vile pia wakati mutumishi wa Yehova mwenye kujitoa kwake anajiingiza mu ibada ya uongo, anamukosea Yehova sana tena sana.—Kum. 4:23. w24.07 22-23 fu. 12-15

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine