Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • es26 uku. 88-97
  • Mwezi wa 9

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mwezi wa 9
  • Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
  • Vichwa Vidogo
  • Siku ya Pili, 1 Mwezi wa 9
  • Siku ya Tatu, 2 Mwezi wa 9
  • Siku ya Ine, 3 Mwezi wa 9
  • Siku ya Tano, 4 Mwezi wa 9
  • Siku ya Posho, 5 Mwezi wa 9
  • Siku ya Yenga, 6 Mwezi wa 9
  • Siku ya Kwanza, 7 Mwezi wa 9
  • Siku ya Pili, 8 Mwezi wa 9
  • Siku ya Tatu, 9 Mwezi wa 9
  • Siku ya Ine, 10 Mwezi wa 9
  • Siku ya Tano, 11 Mwezi wa 9
  • Siku ya Posho, 12 Mwezi wa 9
  • Siku ya Yenga, 13 Mwezi wa 9
  • Siku ya Kwanza, 14 Mwezi wa 9
  • Siku ya Pili, 15 Mwezi wa 9
  • Siku ya Tatu, 16 Mwezi wa 9
  • Siku ya Ine, 17 Mwezi wa 9
  • Siku ya Tano, 18 Mwezi wa 9
  • Siku ya Posho, 19 Mwezi wa 9
  • Siku ya Yenga, 20 Mwezi wa 9
  • Siku ya Kwanza, 21 Mwezi wa 9
  • Siku ya Pili, 22 Mwezi wa 9
  • Siku ya Tatu, 23 Mwezi wa 9
  • Siku ya Ine, 24 Mwezi wa 9
  • Siku ya Tano, 25 Mwezi wa 9
  • Siku ya Posho, 26 Mwezi wa 9
  • Siku ya Yenga, 27 Mwezi wa 9
  • Siku ya Kwanza, 28 Mwezi wa 9
  • Siku ya Pili, 29 Mwezi wa 9
  • Siku ya Tatu, 30 Mwezi wa 9
Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
es26 uku. 88-97

Mwezi wa 9

Siku ya Pili, 1 Mwezi wa 9

Muendelee kujijaribu ili kuona kama muko katika imani.—2 Ko. 13:5.

Tunapaswa kujikaza kufikia kuwa watu wakomavu kiroho, lakini pia tunapaswa kuendelea kuwa wakomavu. Ili kufanya vile hatupaswe kujitumainia kupita kiasi. (1 Ko. 10:12) Tunapaswa ‘kuendelea kujijaribu’ ili kuhakikisha kama tunaendelea kufanya maendeleo. Mu barua yake kwa Wakolosai, mutume Paulo anakazia tena kama ni jambo ya maana kuendelea kuwa wakomavu kiroho. Hata kama Wakolosai walikuwa watu wazima kiroho, Paulo aliwaambia wakuwe waangalifu ili wasidanganywe na mawazo ya ulimwengu. (Kol. 2:​6-10) Epafra pia, mwenye inaonekana alijua muzuri Wakristo wa ile kutaniko, alisali siku zote ili ‘mwishowe wasimame wakiwa kamili,’ ni kusema wenye kukomaa kiroho. (Kol. 4:12) Ile inatufundisha nini? Paulo na Epafra walielewa kama ili tuendelee kuwa wakomavu kiroho, tuko na lazima ya musaada wa Mungu na tunapaswa kujikaza sana. Walipenda Wakolosai waendelee kuwa wakomavu ao watu wazima kiroho, hata wapambane na magumu gani. w24.04 6-7 fu. 16-17

Siku ya Tatu, 2 Mwezi wa 9

Yehova iko pamoja na sisi. Musiwaogope.—Hes. 14:9.

Wakati tunamuogopa Yehova mu njia yenye kufaa, tunamupenda sana na hatupendi hata siku moya kufanya jambo fulani yenye inaweza kumuhuzunisha. Ili Yehova atukubali, tunapaswa kujifunza tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa, kati ya mambo ya kweli na mambo ya uongo. (Mez. 2:​3-6; Ebr. 5:14) Kama tunaanza kuogopa wanadamu kuliko Mungu, pole kwa pole tutaanza kuacha kweli. Fikiria mufano wa wakubwa 12 wenye walienda kupeleleza inchi yenye Yehova alikuwa ameahidi kama atapatia Waisraeli. Woga wenye wale wapelelezi kumi walikuwa nao kwa Wakanaani, ulikuwa nguvu sana kupita upendo wao kwa Yehova. Waliambia hivi Waisraeli wenzao: “Hatuwezi kupanda ili kupigana na watu hao, kwa sababu wako na nguvu kutupita.” (Hes. 13:​27-31) Ku macho ya wanadamu, ni kweli kama Wakanaani walikuwa nguvu zaidi. Lakini kusema kama Waisraeli hawangeweza kushinda maadui wao, ilikuwa kumutia Yehova pembeni. w24.07 9 fu. 5-6

Siku ya Ine, 3 Mwezi wa 9

Je, Muamuzi wa dunia yote hatatenda jambo lenye kuwa sawa?—Mwa. 18:25.

Unawaza tuko na sababu ya muzuri ya kutumainia hukumu zote za Yehova, hata zikuwe za namna gani? Ndiyo! Sawa vile Abrahamu alielewa, Yehova “Muamuzi wa dunia yote” ni mukamilifu, ni mwenye hekima mingi sana, na ni mwenye rehema. Amezoeza Mwana wake na amemupatia daraka ya kuhukumu wengine. (Yoh. 5:22) Yehova na Mwana wake wanaweza kusoma mambo yenye kuwa mu moyo wa kila mwanadamu. (Mt. 9:4) Sikuzote, wanafanya “jambo lenye kuwa sawa”! Tuazimie basi kumutumainia Yehova na kuwa hakika kama maamuzi yake inakuwaka ya muzuri sikuzote. Tunajua kama hakuna hata mumoja kati yetu mwenye anastahili kuhukumu wengine, lakini Yehova yeye anastahili! (Isa. 55:​8, 9) Kwa hiyo tunaachia Yehova na Mwana wake kazi ya kuhukumu watu. Tuko hakika kama Yesu anaiga rehema na haki ya Baba yake kwa ukamilifu.—Isa. 11:​3, 4. w24.05 7 fu. 18-19

Siku ya Tano, 4 Mwezi wa 9

Yehova anachukia mutu mudanganyifu, lakini anafanya urafiki wa karibu pamoja na watu wanyoofu.—Mez. 3:32.

Mambo yenye Yesu alisema wakati alikutana na Natanaeli kwa mara ya kwanza inaweza kutufundisha jambo ya maana kuhusu kuwa na moyo wenye hauna udanganyifu. Wakati Filipo alileta rafiki yake Natanaeli ili akutane na Yesu, jambo fulani ya pekee ilitokea. Hata kama ilikuwa mara ya kwanza Yesu aonane na Natanaeli, alisema hivi: “Ona, Mwisraeli wa kweli mwenye hana udanganyifu ndani yake.” (Yoh. 1:47) Yesu aliona unyoofu wa pekee katika Natanaeli. Kama siye wote, Natanaeli pia hakukuwa mukamilifu. Lakini hakukuwa na udanganyifu ndani yake. Yesu alifurahia ile jambo na alimupongeza. Mambo mingi yenye Yehova anatuomba tufanye mu Zaburi 15 ili kumufurahisha inahusu namna tunatendea wengine. Zaburi 15:3 inasema kama mugeni mu hema ya Yehova “hasingizie kwa ulimi wake, hamutendee jirani yake jambo lolote la mubaya, naye hawaharibishie marafiki wake sifa.” Kutumia mubaya ulimi wetu mu ile njia kunaweza kuumiza sana wengine.—Yak. 1:26. w24.06 10 fu. 7, 9; 11 fu. 10

Siku ya Posho, 5 Mwezi wa 9

Bwana, hata pepo wachafu wanatutii wakati tunatumia jina lako.—Lu. 10:17.

Kama unajitayarisha muzuri kwa ajili ya mahubiri, itakuwa mwepesi zaidi kwako kuzungumuza na wengine. Mbele ya kuwatuma mu mahubiri, Yesu alisaidia wanafunzi wake wajitayarishe. (Lu. 10:​1-11) Juu walitumikisha mambo yenye Yesu aliwafundisha, walifurahi sana kwa sababu ya mambo yenye waliweza kutimiza. Tunaweza kujitayarisha namna gani kwa ajili ya mahubiri? Tufikirie namna tunaweza kufasiria kweli muzuri zaidi mu maneno yetu wenyewe. Pia ni jambo ya maana tufikirie mawazo ao maulizo mbili ao tatu yenye watu wa mu eneo yetu wanazoea kuwa nayo, kisha tufikirie mbele ya wakati namna tunaweza kuwajibu. Na wakati tunakaribia watu, tunaweza kujikaza kutulia, kucheka kidogo, na kuzungumuza nao kwa njia ya urafiki. w24.04 16 fu. 6-7

Siku ya Yenga, 6 Mwezi wa 9

Unastahili, Yehova Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote.—Ufu. 4:11.

Sababu ya maana zaidi yenye inatuchochea kuhubiri habari njema ni juu tunamupenda Mungu na jina yake takatifu. Tunaona kuwa, kazi yetu ya kuhubiri ni nafasi ya kumusifu Mungu mwenye tunapenda. Tunakubaliana kama Yehova Mungu anastahili kupokea utukufu, heshima, na nguvu, kutoka kwa waabudu wake washikamanifu. Tunamutolea Yehova utukufu na heshima wakati tunaonyesha wengine ushuhuda wenye kuonyesha kama ‘aliumba vitu vyote’ na kama ni yeye njo alitupatia uzima. Tunamutolea nguvu yetu wakati tunatumia uwezo wetu, wakati wetu, na vitu vyetu ili kutegemeza kazi ya kuhubiri kadiri hali yetu inaruhusu. (Mt. 6:33; Lu. 13:24; Kol. 3:23) Mu maneno ingine, tunapenda kuzungumuza juu ya Mungu mwenye tunapenda. Tunachochewa pia kuambia wengine kuhusu jina yake na maana ya jina yake. w24.05 17 fu. 11

Siku ya Kwanza, 7 Mwezi wa 9

Anakuwa mwenye kuwapatia zawabu wale wenye wanamutafuta kwa bidii.—Ebr. 11:6.

Yehova anapatia zawabu ao anabariki wale wenye kumuabudu. (Ebr. 11:6) Anatupatia amani na anatusaidia tutosheke sasa, na wakati wenye kuya atatupatia uzima wa milele. Tunaweza kumutumainia na kuwa hakika kama anapenda kutupatia zawabu na iko na nguvu ya kufanya vile. Kuwa hakika na ile jambo kunatuchochea tuendelee kumutumikia kwa bidii, sawa vile watumishi wake waaminifu wa zamani walifanya. Ni vile Timoteo alifanya mu karne ya kwanza (Ebr. 6:​10-12) Timoteo alimutumainia Mungu mwenye kuishi. (1 Ti. 4:10) Ile ilimuchochea atumike kwa bidii na ajitoe kabisa. Alifanya vile namna gani? Paulo alimutia moyo akuwe mufundishaji muzuri zaidi mu kutaniko na mu mahubiri. Timoteo alipaswa pia kuwekea waabudu wenzake, vijana na wazee, mufano muzuri. Na wakati fulani aliombwa kufanya mambo yenye haikukuwa mwepesi, sawa vile kutolea Wakristo mashauri mazito lakini yenye upendo. (1 Ti. 4:​11-16; 2 Ti. 4:​1-5) Timoteo angekuwa hakika kuwa Yehova angemupatia zawabu.—Ro. 2: 6, 7. w24.06 22-23 fu. 10-11

Siku ya Pili, 8 Mwezi wa 9

Yehova aliendelea kuonya Israeli na Yuda kupitia manabii wake wote.—2 Fa. 17:13.

Mara kwa mara Yehova alitumia manabii wake juu waonye na kurekebisha batu yake. Kwa mufano, Mungu alisema hivi kupitia nabii Yeremia: “Rudia, Ee Israeli mwenye kuasi . . . Sitakuangalia kwa kasirani, kwa maana mimi ni mushikamanifu . . . Sitaendelea kuwa na kinyongo milele. Isipokuwa tu ukubali hatia yako, kwa maana umemuasi Yehova.” (Yer. 3:​12, 13) Kupitia Yoeli Yehova alisema hivi: “Murudie kwangu kwa mioyo yenu yote.” (Yoe. 2:​12, 13) Alimuomba Isaya aseme hivi: “Mujinawishe, mujisafishe; muondoe matendo yenu maovu mbele ya macho yangu; muache kutenda mabaya.” (Isa. 1:​16-19) Kupitia Ezekieli Yehova aliuliza hivi: “Je, ninafurahia kabisa kifo cha mutu muovu? . . . Je, mimi sifurahie kwamba aache njia zake naye aendelee kuishi? Sifurahie hata kidogo kifo cha mutu yeyote, . . . kwa hiyo mugeuke na kuishi.” (Eze. 18:​23, 32) Yehova anafurahia kuona batu banatubu juu anapenda baishi milele. w24.08 9 fu. 5-6

Siku ya Tatu, 9 Mwezi wa 9

Kila Andiko limeongozwa na roho ya Mungu na liko na faida.—2 Ti. 3:16.

Watu wote wa Yehova wanapata chakula ya kiroho, muongozo, na ulinzi wenye wako nao lazima. Jambo yenye inaonyesha kama Yehova hana ubaguzi ni hii: Anahakikisha kama watu wote mu dunia wanaweza kupata Biblia. Maandiko Matakatifu iliandikwa mu luga tatu za kwanza-kwanza: Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Je, wale wenye wanajua kusoma zile luga wako na urafiki wa karibu pamoya na Yehova kuliko watu wengine? Hapana. (Mt. 11:25) Haiko masomo yenye tulisoma ao uwezo wetu wa kujua luga fulani njo unafanya Yehova atukubali. Haiko wale wenye walisoma sana njo tu Yehova anapatiaka hekima yake. Watu wote wenye kuwa ku dunia wanaweza kupata hekima yake, ikuwe walisoma sana ao hapana. Neno yake Biblia yenye iliongozwa na roho yake takatifu, imetafsiriwa mu maelfu ya luga. Kwa hiyo, watu mu dunia yote wanaweza kupata mafundisho yake na kujifunza mambo yenye wanaweza kufanya juu wakuwe marafiki wake.—2 Ti. 3:​16, 17. w24.06 6-7 fu. 13-15

Siku ya Ine, 10 Mwezi wa 9

Uharibifu wa Yerusalemu] umekaribia.—Lu. 21:20.

Sawa vile Yesu alitabiri, mupangilio wa mambo wa Wayahudi ulikuwa karibu kuharibiwa. Wakristo walipaswa kutumia wakati yenye ilibakia juu ya kujitayarisha kwa kukomalisha sifa sawa vile imani na uvumilivu. (Ebr. 10:25; 12:​1, 2) Hivi karibuni tutapambana na taabu kubwa kupita yenye Wakristo Waebrania walipambana nayo. (Mt. 24:21; Ufu. 16:​14, 16) Tuone mashauri fulani yenye Yehova alitolea wale Wakristo juu inaweza pia kutusaidia. Mutume Paulo alitia moyo waamini wenzake wajifunze Neno ya Mungu kwa undani kabisa. (Ebr. 5:14–6:1) Paulo alitumia Maandiko ya Kiebrania ili kufikiri na ndugu zake juu ya kuwasaidia waelewe kama namna ya kuabudu ya Wakristo ni ya hali ya juu sana kupita namna ya kuabudu ya Wayahudi. Paulo alijua kama, ikiwa wale Wakristo wanakuwa na ujuzi ya mingi na ikiwa wanaelewa muzuri zaidi kweli, wataweza kutambua na kuepuka mafundisho ya bongo juu wasidanganywe. w24.09 8-9 fu. 2-3; 10 fu. 6

Siku ya Tano, 11 Mwezi wa 9

Kwa kweli Bwana alifufuliwa.—Lu. 24:34.

Banafunzi ya Yesu balikuwa na lazima ya kutiwa moyo. Juu ya nini? Bamoya baliacha nyumba, familia, na kazi juu ya kumufuata Yesu wakati wote. (Mt. 19:27) Bengine balitendewa mubaya juu balikuwa banafunzi ya Yesu. (Yoh. 9:22) Balijitoa sana juu balijua kama Yesu alikuwa Masiya mwenye aliahidiwa. (Mt. 16:16) Lakini wakati Yesu aliuawa, tumaini yabo ilipotea na balivunjika moyo. Yesu hakuona huzuni ya banafunzi yake kuwa alama ya kuonyesha kama habakukuwa nguvu kiroho. Lakini alielewa kama balitenda vile juu balimupoteza. Kwa hiyo, siku ya kwanza tu kisha kufufuka, Yesu alianza kutia moyo barafiki yake. Kwa mufano, alimutokea Maria Magdalene wakati alikuwa nalia ku kaburi. (Yoh. 20:​11, 16) Alitokea pia banafunzi bawili benye balikuwa naenda mu kijiji ya Emau. Na alitokea pia mutume Petro. w24.10 13 fu. 5-6

Siku ya Posho, 12 Mwezi wa 9

Sikuzote mukuwe tayari kujitetea mbele ya kila mutu mwenye anawauliza ninyi sababu ya tumaini lenye muko nalo.—1 Pe. 3:15.

Muzazi, tayarisha mutoto wako aweze kufasiria juu ya nini anaamini kama kuko Muumbaji. Kati ya mambo yenye inaweza kusaidia sana ni kuchunguza pamoya na mutoto wako habari zenye kuwa ku jw.org chini ya kichwa “Vijana Huuliza— Uumbaji au Mageuzi?” Muchague mafasirio yenye mutoto wako anaona inaweza kusaidia wengine waamini kama kuko Muumbaji. Umutie moyo atumikishe mafasirio yenye kuwa mwepesi kuelewa na yenye kuwa wazi ikiwa kuko mutu mwenye iko tayari kumusikiliza. Kwa mufano, mwanafunzi fulani anaweza kusema hivi: “Miye ninaaminiaka tu mambo yenye ninaona, lakini siyamuonaka Mungu.” Kijana Mukristo anaweza kujibia hivi: “Wazia uko natembea mu pori mbali sana na batu kisha unakuta kisima yenye inajengewa muzuri. Utawaza nini? Kunapaswa kuwa mutu wa akili mwenye alijenga ile kisima. Sasa, tuseme nini juu ya ulimwengu?” w24.12 18 fu. 16

Siku ya Yenga, 13 Mwezi wa 9

Je, haiko wazee ndio wenye kuwa na hekima, Na je, uelewaji haukuje kwa sababu ya kuishi siku nyingi?—Yob. 12:12.

Siye bote tuko na lazima ya muongozo juu ya kukamata maamuzi ya maana mu maisha yetu. Wazee na Wakristo wengine wenye kukomala kiroho wanaweza kutupatia ule muongozo. Kama wako na miaka mingi kutupita, tusiwaze mara moya kama mashauri yao ni ya zamani na haina tena faida leo. Yehova anapenda tujifunze mambo fulani kutoka kwa batu benye kukomala. Bameishi miaka mingi, kwa hiyo biko na uzoefu, uelewaji, na hekima.Zamani, Yehova alitumia batu baaminifu benye kuzeeka juu ya kutia moyo batu yake na kubaongoza. Kwa mufano alitumia Musa, Daudi, na mutume Yohana. Bale banaume baliishi mu vipindi tofauti na hali zao zilikuwa tofauti kabisa. Wakati balikaribia kufa, balipatia vijana mashauri yenye hekima. Kila mumoya wao alikazia kama ni jambo ya maana kumutii Mungu. Ikuwe tuko vijana ao wazee, tunaweza kujifunza mambo mingi kupitia ile mashauri.—Ro. 15:4; 2 Ti. 3:16. w24.11 8 fu. 1-2

Siku ya Kwanza, 14 Mwezi wa 9

Kama hamukule mwili wa Mwana wa binadamu na kunywa damu yake, hamuna uzima ndani yenu wenyewe.—Yoh. 6:53.

Mu siku za Noa, Mungu alikataza banadamu kula damu. (Mwa. 9:​3, 4) Yehova alirudilia ile jambo mu Sheria yenye alipatia Waisraeli. Mutu yeyote mwenye angekula damu alipaswa “kuuawa.” (Law. 7:​27, maelezo ya chini) Yesu aliheshimia ile Sheria. (Mt. 5:​17-19) Kwa hiyo haingewezekana atie moyo Wayahudi wakule mwili wake na wakunywe damu yenye kuwa mu mishipa yake. Yesu alikuwa natumia maneno ya mufano, sawa vile alifanya mbele ya pale, wakati aliambia hivi mwanamuke Musamaria: ‘Maji yenye nitamupatia . . . itatoa uzima wa milele’ (Yoh. 4:​7, 14) Yesu hakukuwa namaanisha kama ule mwanamuke Musamaria angepata uzima wa milele kwa kunywa tu maji fulani. Vilevile, hakukuwa naambia bale batu mingi katika Kapernaumu kama bangeishi milele kama tu banakula mwili wake na kunywa damu yake sawa vile banakulaka chakula. w24.12 9 fu. 4-6

Siku ya Pili, 15 Mwezi wa 9

Mutoe miili yenu ikuwe zabihu yenye uzima, takatifu, na yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mutakatifu pamoja na nguvu zenu za kufikiri.—Ro. 12:1.

Bwana Wakristo wanapaswa kuwa waangalifu juu wasikuwe na mawazo yenye haifae kuhusu wanamuke. Juu ya nini? Sababu moya ni kwamba mambo yenye mutu anawaza njo yenye anafanyaka. Mutume Paulo alionya hivi Wakristo watiwa-mafuta wa Roma: “Muache kufinyangwa na mupangilio huu wa mambo.” (Ro. 12:​1, 2) Wakati Paulo aliandikia kutaniko ya Roma, inaonekana kulikuwa kulishapita wakati fulani tangu ile kutaniko ianzishwe. Lakini, maneno ya Paulo inaonyesha kama watu fulani mu ile kutaniko walikuwa wangali wanachochewa na desturi na mawazo ya ulimwengu. Njo maana aliwashauria wabadilishe mawazo na tabia yao. Ile mashauri inahusu pia bwana Wakristo leo. Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba, bwana fulani Wakristo wamechochewa na mawazo ya ulimwengu na hata wametendea mubaya bibi zao. w25.01 9 fu. 4

Siku ya Tatu, 16 Mwezi wa 9

Muchunge kundi la Mungu lenye liko chini ya uongozi wenu, mukiwa waangalizi.—1 Pe. 5:2.

Leo wazee wako na mambo mingi ya kufanya. Ni waeneza-injili. (2 Ti. 4:5) Wanafanya kazi ya kuhubiri kwa bidii, wanapanga eneo ya kuhubiri ya kutaniko, na wanatuzoeza kuhubiri na kufundisha muzuri. Wanatumikaka kama waamuzi wenye huruma na wenye hawana upendeleo. Wakati Mukristo anafanya zambi nzito, wazee wanajikaza kumusaidia juu arudishe tena uhusiano wake pamoya na Yehova. Hata vile, ni waangalifu juu waendelee kulinda usafi wa kutaniko. (1 Ko. 5:​12, 13; Gal. 6:1) Lakini, wazee wanajulikana zaidi sana kuwa wachungaji. (1 Pe. 5:​1-3) Wanatoa hotuba zenye kutegemea Maandiko zenye kutayarishwa muzuri, wanajikaza kujua kila mutu mu kutaniko, na wanafanya ziara za uchungaji. Zaidi ya migao yao ingine, wazee fulani wanasaidia mu kazi ya kujenga na kutunza Majumba ya Ufalme, kupanga mikusanyiko, kutumika mu Halmashauri za Uhusiano na Hopitali na mu Vikundi vya Kutembelea Wagonjwa. Wazee wanatumika kwa bidii kwa ajili yetu! w24.10 20 fu. 9

Siku ya Ine, 17 Mwezi wa 9

Kama vile katika Adamu wote wanakufa, vilevile pia katika Kristo wote watafanywa kuwa wazima.—1 Ko. 15:22.

Mu Biblia, neno “kukombolewa” maana yake kuachiliwa wakati bei ya ukombozi inalipwa. Mutume Petro alifasiria hivi: “Munajua kama haiko kwa vitu vyenye vinaweza kuharibika, kwa feza ao zahabu, ndiyo muliwekwa huru [neno kwa neno, “mulikombolewa”] kutoka kwenye njia yenu ya maisha yenye haina maana, yenye mulipokea kutoka kwa mababu zenu. Lakini ilikuwa kwa damu yenye samani, kama ile ya mwana-kondoo mwenye hana kasoro na mwenye hana doa, ile ya Kristo.” (1 Pe. 1:​18, 19; maelezo ya chini) Kwa sababu ya bei ya ukombozi, tunaweza kuachiliwa huru kutokana na zambi na kifo yenye kutuletea mateso. (Ro. 5:21) Kwa hiyo, tuko wenye shukrani sana kwa Yehova na Yesu juu wametukomboa kupitia damu ao uzima wa Yesu. w25.02 5 fu. 15-16

Siku ya Tano, 18 Mwezi wa 9

Mwenye furaha ni mutu mwenye kuwa muangalifu sikuzote.—Mez. 28:14.

Namna gani tunaweza kujilinda? Tuchunguze mufano wa kijana mwenye kuzungumuziwa mu Mezali sura ya 7, na tuone mufano wake unaweza kutufundisha nini. Alifanya uasherati na mwanamuke mwasherati. Mustari wa 22 unasema kama ule kijana alifuata ule mwanamuke “mara moja” ao kwa kushitukia. Lakini mistari yenye kutangulia inaonyesha kama mbele ya pale, alikuwa amekamata hatua mbalimbali zenye zilimuongoza pole kwa pole kwenye zambi. Ni nini ilimuongoza kwenye zambi? Kwanza, mangaribi “alipita katika . . . njia yenye kupeleka kwa mwanamuke [mwasherati].” Kisha, akaanza kuenda kwenye nyumba ya ule mwanamuke ilikuwa. (Mez. 7:​8, 9) Na kisha, wakati aliona ule mwanamuke, hakugeuka na kubadilisha njia. Lakini alikubali ule mwanamuke amubusu na alisikiliza wakati alikuwa nazungumuzia zabihu za ushirika zenye alikuwa ametoa. Pengine alizungumuzia ile jambo juu afanye ule kijana awaze kama hakukuwa mutu mubaya. (Mez. 7:​13, 14, 21) Kama ule kijana angeepuka hatari zenye zilimuongoza kwenye zambi, angejilinda ili asiangukie mu jaribu na asifanye zambi. w24.07 16 fu. 8-9; 19 fu. 19

Siku ya Posho, 19 Mwezi wa 9

Munapaswa kumusamehe kwa fazili na kumufariji.—2 Ko. 2:7.

Yehova haruhusu zambi nzito kati ya watu wake. Watu fulani wanaweza kuwaza kama juu Yehova ni Mungu mwenye “rehema,” watenda-zambi wenye hawatubu wanapaswa kuruhusiwa kuendelea kujiunga na waabudu waaminifu. Lakini ile haiko rehema ya Yehova; Yehova iko na rehema lakini haachiliake mambo, hapunguzake uzito wa kanuni zake. (Yud. 4) Kuruhusu watenda-zambi wenye hawatubu wabakie mu kutaniko, haiko kuonyesha rehema juu ile inaweza kutia kutaniko yote mu hatari. (Mez. 13:20; 1 Ko. 15:33) Lakini, tumejifunza kama Yehova hapendi mutu yeyote aharibiwe. Anapenda kuokoa watu kila wakati wenye inawezekana. Anaonyesha rehema watu wenye wanabadilisha moyo wao na wenye wanapenda tena kuwa na urafiki muzuri pamoya naye. (Eze. 33:11; 2 Pe. 3:9) Njo maana, wakati ule mwanaume wa Korinto alitubu na kuacha zambi yake, Yehova alitumia mutume Paulo juu ya kufasiria kutaniko kama ule mwanaume alipaswa kusamehewa na kukaribishwa tena mu kutaniko. w24.08 17 fu. 7; 18-19 fu. 14-15

Siku ya Yenga, 20 Mwezi wa 9

Kwa kadiri mulitendea vile mumoja wa wadogo zaidi kati ya hawa ndugu zangu, mulinitendea mimi.—Mt. 25:40.

Mu mufano wa kondoo na mbuzi, Yesu anazungumuzia hukumu ya watu wenye walipata nafasi ya kutegemeza ndugu zake watiwa-mafuta. (Mt. 25:​31-46) Mu kipindi ya “taabu kubwa,” atatoa hukumu yake mbele tu ya Armagedoni. (Mt. 24:21) Sawa vile tu muchungaji anatenganisha kondoo na mbuzi, Yesu atatenganisha watu wenye walitegemeza kwa uaminifu wafuasi wake watiwa-mafuta na wale wenye hawakufanya vile. Unabii wa Biblia unaonyesha kama Yesu, Muamuzi mwenye Yehova aliweka, atahukumu kwa haki. (Isa. 11:​3, 4) Anachunguza mwenendo, muelekeo, na maneno ya watu, anachunguza pia namna wanatendea ndugu zake watiwa-mafuta. (Mt. 12:​36, 37) Yesu atajua ni nani alitegemeza ndugu zake watiwa-mafuta na kazi yao. Njia moya ya maana sana ya kutegemeza ndugu za Yesu ni kuwasaidia mu kazi ya kuhubiri. w24.09 20-21 fu. 3-4

Siku ya Kwanza, 21 Mwezi wa 9

Muchunguze mambo yote.—1 Te. 5:21.

Tujihakikishie kama mambo yenye tunaamini ni ya kweli kwa kuilinganisha na mambo yenye Biblia inasema. Kwa mufano, fikiria ule kijana mwenye iko najiuliza ikiwa Yehova anamuona kuwa wa maana. Anapaswa tu kuacha ile ulizo vile? Hapana, anapaswa ‘kuchunguza mambo yote’ kwa kutafuta kujua mawazo ya Yehova juu ya ile jambo. Wakati tuko nasoma Neno ya Mungu “tunasikia” Yehova iko nazungumuza na siye. Lakini ili kujua mawazo yake juu ya jambo fulani, kuko jambo ingine yenye tunapaswa kufanya. Tunapaswa kutafuta maandiko yenye kuzungumuzia mambo yenye kutuhangaisha. Tunapaswa kutafuta habari kwa kutumia vyombo vya kutafuta habari vyenye tengenezo ya Yehova inatupatia. (Mez. 2:​3-6) Tunapaswa kusali kwa Yehova atusaidie wakati tuko natafuta habari kusudi tupate mawazo yake juu ya jambo yenye kutuhangaisha. w24.10 25 fu. 4-5

Siku ya Pili, 22 Mwezi wa 9

[Upendo] hautafute faida zake wenyewe.—1 Ko. 13:5.

Yehova hatabariki mutu yeyote mwenye majivuno ao mwenye iko najitafutia sifa (1 Ko. 10:​24, 33; 13:4) Wakati fulani, hata marafiki wa karibu wa Yesu walikuwa na nia ya mubaya wakati walitafuta mapendeleo. Fikiria mambo yenye Yakobo na Yohana, mitume wawili wa Yesu, walifanya; waliomba Yesu awapatie cheo ya juu mu Ufalme wake. Yesu hakuwapongeza juu walijitafutia cheo, lakini aliambia mitume wote 12 hivi: “Kila mutu mwenye anataka kuwa wa kwanza katikati yenu anapaswa kuwa mutumwa wa wote.” (Mk. 10:​35-37, 43, 44) Ndugu wenye wanajikaza kufikia mapendeleo na wako na nia ya muzuri, ni kusema nia ya kutumikia bengine, ni baraka kwa kutaniko.—1 Te. 2:8. w24.11 15-16 fu. 7-8

Siku ya Tatu, 23 Mwezi wa 9

Mambo yanatimizwa kupitia washauri wengi.—Mez. 15:22.

Wakati tuko nakamata maamuzi, upendo utatusaidia kutafuta faida ya ‘wengine’ na kuwa na kiasi. (1 Ko. 10:​23, 24, 32; 1 Ti. 2:​9, 10) Kwa hiyo tutakamata uamuzi wenye unaonyesha kama tunapenda na kuheshimia wengine. Kama unataka kukamata uamuzi kuhusu jambo fulani ya maana sana, fikiria mambo yote yenye inaomba ufanye juu utimize ule uamuzi. Yesu alisema kama tunapaswa “kuhesabia garama.” (Lu. 14:28) Kwa hiyo fikiria wakati, vitu, na nguvu yenye itakuomba juu ya kutimiza uamuzi wako. Wakati fulani, ni muzuri uzungumuze na watu ya familia yako juu ya kujua jambo yenye kila mutu mu familia anapaswa kufanya ili kutegemeza ule uamuzi. Juu ya nini ni muzuri kufanya vile? Ile inaweza kukusaidia kujua ikiwa unapaswa kubadilisha mambo fulani mu uamuzi wenye unataka kukamata ao ikiwa ni muzuri zaidi kukamata uamuzi ingine. Kama unazungumuza na watu wa familia yako na kusikiliza mawazo yao, watakuwa tayari kukutegemeza juu ule uamuzi ukuwe na matokeo ya muzuri. w25.01 18-19 fu. 14-15

Siku ya Ine, 24 Mwezi wa 9

Mufurahi na mukuwe na shangwe.—Isa. 65:18.

Isaya anaonyesha juu ya nini tuko na sababu za ‘kufurahi na kuwa na shangwe’ mu paradiso ya kiroho. Yehova njo mwenye ameumba, ao ameanzisha paradiso ya kiroho. (Isa.65:​18, 19) Kwa hiyo haishangaze kuona kama Yehova iko natutumikisha ili kusaidia watu watoke mu matengenezo yenye kudanganya watu ya mu hii ulimwengu ili waingie mu paradiso yetu ya kiroho yenye kupendeza! Tunafurahia sana baraka zenye tunapata juu tuko katika kweli na ile inatuchochea tuelezee wengine kuhusu zile baraka. (Yer. 31:12) Tuko pia wenye shukrani na tunafurahia sana tumaini yenye tuko nayo kwa sababu tuko mu paradiso ya kiroho. Biblia inaahidi kama ‘tutajenga nyumba na kuishi ndani, na tutapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.’ ‘Hatutafanya kazi ya jasho ya bure’ kwa sababu ‘tutabarikiwa na Yehova.’ Anatuahidi kama tutakuwa na usalama, na tutakuwa na maisha ya muzuri na yenye kusudi. Anajua mahitaji ya kila mutu na ‘atatimiza tamaa ya kila kitu chenye uzima.’—Isa. 65:​20-24; Zb. 145:16. w24.04 22-23 fu. 11-12

Siku ya Tano, 25 Mwezi wa 9

Mwamba wangu wenye nguvu, kimbilio langu, ni Mungu.—Zb. 62:7.

Tunamufanya Yehova kuwa mwamba wetu wakati tunamutegemea kwa moyo wote. Tuko hakika kama tutapata faida wakati tunamutii hata mu hali za nguvu. (Isa. 48:​17, 18) Wakati tunajionea namna anatusaidia, tunamutegemea zaidi. Ile itatusaidia tukuwe tayari kupambana na magumu ya nguvu yenye Yehova tu njo anaweza kutusaidia kupambana nayo. Sawa vile mwamba mukubwa, Yehova ni uleule. Utu wake na kusudi yake havibadilikake. (Mal. 3:6) Wakati wanadamu waliasi mu Edeni, Yehova hakubadilisha kusudi yake kwa ajili ya wanadamu. Kama vile mutume Paulo aliandika, Yehova “hawezi kujikana yeye mwenyewe.” (2 Ti. 2:13) Ile inamaanisha kama hata kutokee nini ao wengine wafanye nini, Yehova hawezi kubadilisha sifa zake, kusudi yake, ao kanuni zake. Juu Yehova hawezi kubadilika, tuko hakika kama anaweza kutuokoa na kutusaidia mu wakati wa magumu.—Zb. 62:​6, 7. w24.06 27-28 fu. 7-8

Siku ya Posho, 26 Mwezi wa 9

Mutu wa siri wa ndani ya moyo . . . [ni] mwenye samani kubwa mbele ya macho ya Mungu.—1 Pe. 3:4

Kama muko mu urafiki wa kimapenzi, ni nini itawasaidia kujua ikiwa mutaoana ao hapana? Mujikaze kujuana muzuri. Mbele uanzishe urafiki wa kimapenzi, inawezekana ulikuwa ulishajua mambo fulani juu ya ule ndugu ao juu ya ule dada. Lakini sasa uko na nafasi ya kujua “mutu wa siri wa ndani ya moyo.” Ile inatia ndani kujua mambo mingi juu ya hali yake ya kiroho, utu wake, na mawazo yake. Kisha wakati fulani, unapaswa kuwa na majibu ya hii maulizo: ‘Huyu mutu atakuwa bwana ao bibi muzuri kwangu?’ (Mez. 31:​26, 27, 30; Efe. 5:33; 1 Ti. 5:8) ‘Ninaweza kumupenda na kumuhangaikia vile inastahili, na yeye anaweza kunipenda na kunihangaikia vile inastahili? Kila mumoja wetu iko tayari kuvumilia uzaifu wa mwingine?’ (Ro. 3:23) Kadiri munaendelea kujuana muzuri, mukumbuke kama jambo yenye inaonyesha kama munastahili kuoana, haiko juu munapatana mu kila jambo, lakini juu kila mumoja iko tayari kujipatanisha na hali ya mwingine. w24.05 27 fu. 5

Siku ya Yenga, 27 Mwezi wa 9

Nimemutendea Yehova zambi.—2 Sa. 12:13.

Mufalme Daudi alifanya makosa makubwa. Lakini wakati nabii Natani alimukaripia kwa sababu ya zambi zake, Daudi alitubu kwa unyenyekevu. (Zb. 51:​3, 4, 17, utangulizi) Mufalme Hezekia naye alimukosea Yehova. (2 Ny. 32:25) Lakini kama Daudi, Hezekia alitubu kwa unyenyekevu. (2 Ny. 32:26) Na ku mwisho, Yehova alimuona kuwa mufalme muaminifu, mwenye “aliendelea kufanya mambo yenye yalikuwa sawa.” (2 Fa. 18:3) Ile inatufundisha nini? Tunapaswa kutubu zambi zetu na kufanya yetu yote ili tusizirudilie. Sasa, tutafanya nini kama wazee wa kutaniko wanatutolea mashauri hata mu mambo yenye inaonekana kuwa ya kidogo? Hatupaswe kuwaza kama Yehova hatukubali tena ao kama wazee hawatupendi. Hata wafalme wazuri wa Israeli walishauriwa na kurekebishwa. (Ebr. 12:6) Wakati tunarekebishwa tunapaswa (1) kukubali mashauri kwa unyenyekevu, (2) kufanya mabadiliko, na (3) kuendelea kumutumikia Yehova kwa moyo wote. Kama tunatubu zambi zetu Yehova atatusamehe.—2 Ko. 7:​9, 11. w24.07 21 fu. 8; 22 fu. 9, 11

Siku ya Kwanza, 28 Mwezi wa 9

Muondoe mutu muovu katikati yenu.—1 Ko. 5:13.

Mukosaji anaondolewa mu kutaniko wakati anakatala kutubu hata kama wazee wamejaribu kumusaidia tena na tena. (2 Fa. 17:​12-15) Matendo yake inaonyesha kama amekatala kufuata kanuni za Yehova. (Kum. 30:​19, 20) Wazee wanafanyia kutaniko tangazo kama ule mutu haiko tena Shahidi wa Yehova. Kusudi ya ile tangazo haiko kumupatisha haya. Lakini inatolewa juu kutaniko ifuate hii mashauri ya Biblia: ‘Muache kushirikiana’ na ule mutu, na “hata musikule chakula pamoja” naye. (1 Ko. 5:​9-11) Kuko sababu ya muzuri yenye ilifanya Yehova atupatie ile muongozo. Mutume Paulo aliandika hivi: “Chachu kidogo inachachisha donge lote.” (1 Ko. 5:6) Kama mukosaji mwenye hatubu anabakia mu kutaniko, ile inaweza kufanya bengine baone kama haiko lazima kufuata kanuni za Yehova mu maisha yao.—Mez. 13:20; 1 Ko. 15:33. w24.08 27 fu. 3-4

Siku ya Pili, 29 Mwezi wa 9

Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia nguvu.—Flp. 4:13.

Hatuna uwezo wa kupatia wengine nguvu, lakini tunaweza kutumikisha nguvu yetu ili kusaidia wengine. Kwa mufano unaweza kusaidia ndugu ao dada wenye kuzeeka ao wenye ni wagonjwa kuhangaikia nyumba ao kuenda kuuza vitu fulani. Ao tunaweza kujitoa juu ya kusaidia kusafisha na kutunza Jumba ya Ufalme. Usisahau kama maneno inakuwaka na nguvu. Unajua mutu mwenye anaweza kufurahi kama unamupongeza? Unajua mutu fulani mwenye iko na lazima ya kutiwa moyo? Kama ni vile onyesha ule mutu kama unamuhangaikia. Unaweza kumuita ku telefone ao kumuandikia ujumbe. Usitafutishe sana maneno ya kusema. Maneno ya mwepesi yenye kutoka mu moyo, inaweza kuwa njo yenye ndugu yako iko nayo lazima juu aendelee kuwa muaminifu na ajisikie muzuri.—Mez. 12:25; Efe. 4:29. w24.09 28 fu. 8-10

Siku ya Tatu, 30 Mwezi wa 9

Kama mwanaume anajikaza ili akuwe mwangalizi, anatamani kazi ya muzuri.—1 Ti. 3:1.

Kama kulishapita wakati fulani tangu uko mutumishi wa huduma, pengine uko mu njia ya kutimiza mambo yenye inaombwa juu ya kuwa muzee. Unaweza kujikaza juu ufikie ile “kazi ya muzuri”? Muzee anafanyaka kazi gani? Anahubiri kwa bidii, anafanya kazi ya uchungaji na ya kufundisha, na anatia nguvu kutaniko kupitia maneno na mufano wake. Njo maana Biblia inaita bale banaume benye kutumika sana kuwa “zawadi katika wanadamu.” (Efe. 4:8) Unaweza kufanya nini juu ustahili kuwa muzee? Mambo yenye mutu anapaswa kutimiza juu afikie kuwa muzee ni tofauti na mambo yenye mutu anapaswa kutimiza juu apate kazi fulani. Mu ulimwengu kama uko na ufundi wenye mukubwa wa kazi iko natafuta unaweza kupata kazi. Lakini kama unapenda kuwa muzee haitoshe tu kuwa na ufundi wa kuhubiri na kufundisha. Unapaswa kutimiza mambo yenye Maandiko inaomba ndugu watimize juu wakuwe wazee. Ile mambo iko mu 1 Timoteo 3:​1-7 na Tito 1:​5-9. w24.11 20 fu. 1-3

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine