Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • es26 uku. 77-87
  • Mwezi wa 8

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mwezi wa 8
  • Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
  • Vichwa Vidogo
  • Siku ya Posho, 1 Mwezi wa 8
  • Siku ya Yenga, 2 Mwezi wa 8
  • Siku ya Kwanza, 3 Mwezi wa 8
  • Siku ya Pili, 4 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tatu, 5 Mwezi wa 8
  • Siku ya Ine, 6 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tano, 7 Mwezi wa 8
  • Siku ya Posho, 8 Mwezi wa 8
  • Siku ya Yenga, 9 Mwezi wa 8
  • Siku ya Kwanza, 10 Mwezi wa 8
  • Siku ya Pili, 11 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tatu, 12 Mwezi wa 8
  • Siku ya Ine, 13 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tano, 14 Mwezi wa 8
  • Siku ya Posho, 15 Mwezi wa 8
  • Siku ya Yenga, 16 Mwezi wa 8
  • Siku ya Kwanza, 17 Mwezi wa 8
  • Siku ya Pili, 18 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tatu, 19 Mwezi wa 8
  • Siku ya Ine, 20 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tano, 21 Mwezi wa 8
  • Siku ya Posho, 22 Mwezi wa 8
  • Siku ya Yenga, 23 Mwezi wa 8
  • Siku ya Kwanza, 24 Mwezi wa 8
  • Siku ya Pili, 25 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tatu, 26 Mwezi wa 8
  • Siku ya Ine, 27 Mwezi wa 8
  • Siku ya Tano, 28 Mwezi wa 8
  • Siku ya Posho, 29 Mwezi wa 8
  • Siku ya Yenga, 30 Mwezi wa 8
  • Siku ya Kwanza, 31 Mwezi wa 8
Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
es26 uku. 77-87

Mwezi wa 8

Siku ya Posho, 1 Mwezi wa 8

Kutakuwa taabu kubwa yenye haijatokea tangu mwanzo wa ulimwengu mupaka sasa.—Mt. 24:21.

Tunasali ili watu wengi kadiri inawezekana, wasikilize onyo yenye tunawatolea na wajiunge na siye mu ibada safi. Lakini itakuwa namna gani juu ya wale wenye hawasikie onyo yenye tunawatolea leo? Inaweza kuwa mapenzi ya Yehova kuokoa watu wenye watabadilika na kuamua kuwa upande wake wakati wataona uharibifu wa Babiloni Mukubwa. Kama ni vile, ni jambo ya haraka sana tuendelee kuonya watu. Pengine watakumbuka mambo yenye tuko nawaambia leo. (Linganisha na Eze. 33:33.) Pengine watakumbuka onyo yenye tuliwatolea, na ile itawachochea wajiunge na siye mu ibada safi mbele ikuwe nyuma kufanya vile. Kama ule mulinzi wa gereza katika Filipi mwenye alibadilika kisha tu “tetemeko kubwa la inchi” kutokea, pengine wamoja kati ya watu wenye hawasikilize habari njema leo, watabadilika kisha kuona uharibifu wa Babiloni Mukubwa, wenye utashangaza sana watu.—Mdo. 16:​25-34. w24.05 16-17 fu. 9-10

Siku ya Yenga, 2 Mwezi wa 8

Kristo ndiye mwisho wa Sheria.—Ro. 10:4.

Mambo yenye mutume Paulo aliandikia Wakristo Waebrania inaweza kutufundisha mambo mingi ya maana. Wakristo fulani Waebrania hawakuendelea kukomaa kiroho; walikuwa ‘wamerudia nyuma na kuwa tena na lazima ya maziwa, hapana ya chakula kigumu [cha kiroho].’ (Ebr. 5:12) Walishindwa kujipatanisha na kweli za mupya, zenye zilikuwa zinafunuliwa kupitia kutaniko. (Mez. 4:18) Kwa mufano, Wakristo fulani Wayahudi walikuwa wangali wanatetea Sheria ya Musa hata kama kulikuwa kumepita miaka 30 hivi tangu ile sheria iondolewe kwa musingi wa zabihu ya Kristo. (Tit. 1:10) Mutu yeyote mwenye amesoma barua yenye kuongozwa na roho ya Mungu yenye Paulo aliandikia Waebrania, anaweza kukubali kama ile kitabu iko na chakula kigumu cha kiroho. Mambo yenye kuwa mu ile kitabu njo yenye wale Wakristo walikuwa nayo lazima ili waamini kama mupango wa ibada ya Kikristo ni wa hali ya juu zaidi, na ili wakuwe na uhodari wa kuendelea kuhubiri.—Ebr. 10:​19-23. w24.04 6 fu. 15

Siku ya Kwanza, 3 Mwezi wa 8

Kutakuwa ufufuo wa wenye haki na wenye hawako wenye haki.—Mdo. 24:15.

Tangu Adamu na Eva wajiunge na Shetani na wamuasi Yehova Mungu, mamiliare ya wanadamu wamekufa. Bale batu yote biko nangoya nini wakati wenye kuya? Kati ya wanafunzi waaminifu wa Yesu, hesabu kidogo ya watu, ni kusema watu 144000 watafufuliwa ili kuenda mbinguni na watapewa uzima wenye hauwezi kufa. (Ufu. 14:1) Na hesabu kubwa ya wanaume na wanamuke waaminifu wenye walimupenda Yehova watafufuliwa kati ya “wenye haki,” na wataishi milele ku dunia kama wanaendelea kuwa waaminifu wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo na wakati wa jaribu ya mwisho. (Da. 12:13; Ebr. 12:1) Pia mu kipindi ya Miaka Elfu, “wenye hawako wenye haki,” ni kusema wale wenye hawakumutumikia Yehova ao hata wale wenye “walizoea kutenda mambo maovu,” watapewa nafasi ya kubadilisha tabia yao na kuwa waaminifu. (Yoh. 5:29; Lu. 23:​42, 43) Lakini wanadamu fulani walikuwa waovu sana, kwa hiyo Yehova ameamua kama hatawafufua.—Lu. 12:​4, 5. w24.05 2 fu. 3; 5 fu. 15; 6 fu. 17

Siku ya Pili, 4 Mwezi wa 8

Wananiheshimia kwa midomo yao, lakini moyo wao uko mbali sana na mimi.—Isa. 29:13.

Mutu mwenye anapenda Yehova amukubali anapaswa “kusema kweli katika moyo wake.” (

. 15:2) Kusema kweli katika moyo haiko tu kuepuka kudanganya. Yehova anapenda tukuwe wanyoofu mu mambo yote. (Ebr. 13:18) Ile ni jambo ya maana juu “Yehova anachukia mutu mudanganyifu, lakini anafanya urafiki wa karibu pamoja na watu wanyoofu.” (Mez. 3:32) Wale wenye ‘kusema kweli katika moyo wao’ hawajifanye kuwa watiifu wakati wako pamoya na watu wengi na kuvunja sheria ya Mungu wakati wako peke yao. Wanaepuka kutenda kwa udanganyifu. Mutu mudanganyifu anaweza kuwaza kama sheria fulani za Yehova hazifae. (Yak. 1:​5-8) Anaweza kukosa kumutii Yehova mu mambo yenye anaona kuwa ya kidogo kidogo. Kisha kama anaona kuwa matendo yake hailete matokeo ya mubaya, anaweza kuvunja sheria zingine za Mungu, na ile inafanya ibada yake ikuwe ya kinafiki. (Muh. 8:11) Lakini, tunapenda kuwa wanyoofu mu mambo yote. w24.06 10 fu. 7-8

Siku ya Tatu, 5 Mwezi wa 8

Musimame imara, mukiwa mumejifunga kwenye kiuno mukaba wa ile kweli.—Efe. 6:14.

Watu wa Yehova wanapenda kweli yenye kuwa mu Neno ya Mungu. Imani yetu inategemea ile kweli. (Ro. 10:17) Tumefikia kuamini kama Yehova ameweka kutaniko ya Kikristo kuwa “nguzo na tegemezo la ile kweli.” (1 Ti. 3:15) Jambo yenye inamufurahishaka sana Shetani ni kutuchochea tusiamini tena Biblia ao muongozo wenye Yehova anatupatia kupitia tengenezo yake. (Efe. 4:14) Hivi karibuni, Shetani ataeneza uongo mukubwa ili kudanganya mataifa juu imupinge Yehova. (Ufu. 16:​13, 14) Tunaweza pia kutazamia kama Shetani atafanya yake yote ili kupotosha watu wa Yehova. (Ufu. 12:9) Kwa hiyo, ni jambo ya maana sana tujizoeze kuona tofauti kati ya kweli na uongo, na kisha tutii ile kweli. (Ro. 6:17; 1 Pe. 1:22) Kufanya vile kutaokoa uzima wetu wakati wa taabu kubwa! w24.07 8 fu. 1-3

Siku ya Ine, 6 Mwezi wa 8

Amri hii yenye ninakuamuru leo haiko nguvu sana kwako, wala haiko kwenye hauwezi kufika.—Kum. 30:11.

Wakati Yehova alifanya Waisraeli kuwa taifa, alifanya agano pamoya nao, ni kusema alifanya makubaliano pamoya nao. Kama wangeendelea kutii sheria zake, angewalinda na kuwabariki. Lakini, kama wangeacha kumutii, kwa mufano kwa kuchagua kuabudu miungu ingine, Yehova angeacha kuwabariki na wangeteseka. Lakini hata mu ile hali, kuko jambo yenye wangefanya juu Mungu awakubali tena. ‘Wangerudia kwa Yehova Mungu wao na kusikiliza sauti yake.’ (Kum. 30:​1-3, 17-20) Mu maneno ingine, walipaswa kutubu. Kama wangefanya vile, Yehova angewakaribia na kuwabariki tena. Waisraeli walimuasi Yehova tena na tena. Ile iliwaletea mateso. Lakini Yehova hakuachilia batu yake. Alituma manabii tena na tena babashaurie juu batubu na bamurudilie.— 2 Fa. 17:​13, 14. w24.08 9 fu. 4-5

Siku ya Tano, 7 Mwezi wa 8

Mateso makubwa yakatokea juu ya kutaniko lenye lilikuwa Yerusalemu.—Mdo. 8:1.

Kisha kifo ya Yesu, Wakristo Waebrania wenye walikuwa naishi mu Yerusalemu na Yudea walipitia mu kipindi ya nguvu sana. Wakati kidogo kisha kutaniko ya Kikristo kuanzishwa, Wakristo waliteswa sana. Na miaka 20 kisha pale, Wakristo walipambana na hali ya umaskini na njala. (Mdo. 11:​27-30) Lakini mu mwaka wa 61 hivi K.K.Y., Wakristo waliingia mu kipindi yenye ilionekana kuwa ya amani kama tunailinganisha na mambo yenye ingetokea kisha. Ni mu ile kipindi njo walipata barua yenye iliongozwa na roho yenye mutume Paulo aliwaandikia. Ile barua ilifika kwa wakati wenye kufaa kabisa! Barua kwa Waebrania ilifika kwa wakati wenye kufaa kabisa kwa sababu amani yenye walikuwa nayo haingeendelea. Paulo alitolea Wakristo mashauri yenye ingewasaidia kuvumilia majaribu yenye walikuwa karibu kupata. w24.09 8 fu. 1-2

Siku ya Posho, 8 Mwezi wa 8

Wamekuwa chanzo cha faraja nyingi kwangu.—Kol. 4:11.

Wakati wa magumu, ndugu na dada zetu wanaweza kuwa “chanzo cha faraja nyingi.” (Kol. 4:11) Yehova anatumia bandugu na badada juu ya kutuonyesha kama anatupenda. Banatufariji kwa kutusikiliza na kujiweka pa nafasi yetu, ao kwa kupitisha wakati pamoya na siye. Banaweza kutupatia andiko ya Biblia yenye kutia moyo ao kusali pamoya na siye. (Ro. 15:4) Wakati fulani, banaweza kutukumbusha namna ya Yehova ya kuona mambo na ile inaweza kutusaidia tuendelee kuvumilia. Wakristo wenzetu wanaweza pia kutupatia mambo yenye tuko nayo lazima, sawa vile kututayarishia chakula wakati tuko mu magumu. Juu bengine batusaidie, inaweza kuwa muzuri tubaombe musaada. (Mez. 17:17) Pengine habajue namna tuko najisikia na mambo yenye tuko nayo lazima. (Mez. 14:10) Kwa hiyo, unaweza kuzungumuza na barafiki bazuri na kubaambia namna uko najisikia. Ubaambie mambo yenye banaweza kufanya juu ya kukusaidia. Unaweza kuzungumuza na muzee moya ao bawili benye unazoea. Badada fulani bameona kama kuzungumuza na dada mwenye kukomaa kiroho kunasaidiaka. w24.10 10 fu. 15-16

Siku ya Yenga, 9 Mwezi wa 8

Kila mutu mwenye anakubali Mwana na kumuamini akuwe na uzima wa milele.—Yoh. 6:40.

Batu mingi banakuwaka baangalifu juu ya chakula yenye batakula na banafanyaka mazoezi kwa ukawaida juu baendelee kuwa na afya ya muzuri. Lakini, banajua kama haiko ile njo itafanya basizeeke na kufa. Pengine banawaza kama haiwezekane kuishi milele. Lakini, Yesu alisema kama inawezekana wanadamu wapate “uzima wa milele,” sawa vile Yohana 3:16 na 5:24 inasema. Siku moya, Yesu alifanya muujiza kwa kutolea batu mingi mikate na samaki. Ile ilikuwa jambo ya kushangaza. Lakini jambo yenye alisema kisha pale, ilikuwa ya kushangaza tena zaidi. Bale batu balimufuata Kapernaumu, karibu na bahari ya Galilaya, na kule alibaambia kama inawezekana batu bafufuliwe na kuishi milele. (Yoh. 6:​39, 40) Maneno ya Yesu inaonyesha kama batu mingi benye bamekufa banaweza kufufuliwa na kama weye na batu benye unapenda munaweza kuishi milele. w24.12 8 fu. 1-2

Siku ya Kwanza, 10 Mwezi wa 8

Ninyi bwana, . . . muwapatie heshima kama chombo kizaifu zaidi, ni kusema, mwanamuke.—1 Pe. 3:7.

Ripoti fulani ya hivi karibuni ya OMS inaonyesha kama bwana wengi wanapiga bibi zao, wanawatukana, na kuwatendea mubaya mu njia zingine za mingi. Bwana anaweza kuwa anatendeaka bibi yake muzuri wakati wako mbele ya watu, lakini anamutendea mubaya wakati wako ku nyumba. Nini inaweza kufanya bwana atendee bibi yake mubaya? Pengine mu familia yenye bwana alikomalia, baba yake alikuwa na jeuri na ile inaweza kufanya awaze kama ni jambo ya kawaida kutendea bibi mubaya. Ao kwenye anaishi watu wanawaza kama “mwanaume wa kweli” anapaswa kutumia nguvu juu ya kuonyesha bibi yake kama yeye njo shefu. Ao pengine hakufundishwa kujizuia, hata kuzuia kasirani yake. Na juu wanaume fulani wanazoea kuangalia pornografia, ile inafanya wakuwe na mawazo ya mubaya, wanawaza kama wanamuke wako tu pale juu ya kuwatimizia tamaa yao ya ngono. Zaidi ya ile, ripoti zinaonyesha kama tangu ugonjwa wa Korona, ile matatizo imeongezeka. Lakini ile mambo yote haipatie bwana sheria ya kutendea bibi yake mubaya. w25.01 8 fu. 2-3

Siku ya Pili, 11 Mwezi wa 8

Kwa kuwa Kristo aliteseka katika mwili, ninyi pia mujipatie nguvu kwa muelekeo uleule wa akili.—1 Pe. 4:1.

“Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote.” (Lu. 10:27) Yesu alionyesha kama ile njo amri ya maana zaidi ya mu Sheria ya Musa. Tunapaswa kumupenda Yehova kwa moyo wetu, ni kusema namna tunajisikia na tamaa zetu zinapaswa kuonyesha kama tunamupenda. Pia tunapaswa kumupenda Yehova kwa nafsi yetu yote na nguvu yetu. Lakini, tunapaswa pia kumupenda Yehova kwa akili yetu, ni kusema namna yetu ya kufikiri inapaswa kuonyesha kama tunamupenda. Kusema kweli, hatuwezi kuelewa kabisa-kabisa namna yote ya kufikiri ya Yehova. Lakini tunaweza kuelewa zaidi namna yake ya kufikiri kwa kujifunza “akili ya Kristo,” juu Yesu aliiga kwa ukamili namna ya kufikiri ya Baba yake.—1 Ko. 2:16. w25.03 8 fu. 1

Siku ya Tatu, 12 Mwezi wa 8

Kupitia yeye tunaachiliwa huru kwa njia ya bei ya ukombozi kupitia damu ya huyo, ndiyo, musamaha wa makosa yetu, kulingana na utajiri wa fazili zake zenye hazistahiliwe.—Efe. 1:7.

Juu alikuwa mwanaume mukamilifu, Yesu alikuwa sawasawa na mutu wa kwanza, Adamu, mbele Adamu afanye zambi. (1 Ko. 15:45) Kwa hiyo wakati Yesu alikufa, aliweza kufunika zambi yenye Adamu alifanya, ni kusema kulipia jambo yenye Adamu alipoteza. (Ro. 5:19) Yesu akakuwa “Adamu wa mwisho.” Haiko lazima mutu mwingine mukamilifu akuye kulipa jambo yenye Adamu alipoteza. Yesu alikufa “mara moja kwa wakati wote.” (Ebr. 7:27; 10:12) Sasa, kuko tofauti gani kati ya mupango wa kufunika zambi na bei ya ukombozi? Mupango wa kufunika zambi ni hatua yenye Mungu alikamata ili kurudisha uhusiano muzuri kati yake na wanadamu. Bei ya ukombozi ni bei yenye ililipwa ili iwezekane kufunika zambi za wanadamu. Ile bei inafananishwa na damu yenye Yesu alimwanga kwa ajili yetu.—Ebr. 9:14. w25.02 4-5 fu. 12-13

Siku ya Ine, 13 Mwezi wa 8

Mungu ni muaminifu, na hatawaacha ninyi mujaribiwe kupita vile munaweza kuvumilia, lakini pamoja na jaribu hilo atafanya pia njia ya kutokea ili muweze kulivumilia.—1 Ko. 10:13.

Kuona Yehova kuwa Mungu mwenye kuishi kutatusaidia tukuwe na mawazo yenye kufaa juu ya magumu yetu. Namna gani? Tutaona magumu yetu kuwa nafasi ya kujibia mashitaka yenye Shetani anamushitaki Yehova. Shetani anasema kama wakati tuko na magumu tutamuacha Yehova. (Yob. 1:​10, 11; Mez. 27:11) Lakini wakati tunabakia waaminifu, hata wakati wa magumu, tunaonyesha kama tunamupenda Yehova na kama Ibilisi ni muongo. Kwa sasa uko napambana na upinzani kutoka kwa serikali, uko unapambana na magumu ya kupata makuta, watu hawakubali wakati unawahubiria, ao uko napambana na magumu ingine? Kama ni vile, ukumbuke kama hali yako inakupatia nafasi ya kufurahisha moyo wa Yehova. Kumbuka pia kama hatakuacha ujaribiwe kupita vile unaweza kuvumilia. Atakupatia nguvu ya kuvumilia. w24.06 22 fu. 9

Siku ya Tano, 14 Mwezi wa 8

Kila mutu anajaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe.—Yak. 1:14.

Unawaza inaweza kuwa mwepesi kwako kuangukia mu jaribu gani? Ni hatari sana kujidanganya na kusema kama hatuna uzaifu fulani ao kusema kama tuko na nguvu sana na hatuwezi kuangukia mu zambi. (1 Yo. 1:8) Paulo alisema kama hata wale wenye kuwa na “sifa za kustahili kiroho” wanaweza kuangukia mu jaribu kama hawaendelee kuwa waangalifu. (Gal. 6:1) Hatupaswe kujidanganya, na tunapaswa kukubali uzaifu wenye tuko nao(2 Ko. 13:5) Wakati unatambua jaribu yenye inaweza kuwa mwepesi kwako kuangukia ndani, unapaswa kufanya nini? Unapaswa kutumika sana ili uweze kushinda ile jaribu. Kwa mufano, zamani milango njo ilikuwa sehemu ya kuta ya muji yenye ilikuwa mwepesi kushambulia. Kwa hiyo, milango njo ililindwa sana. Vilevile, tunapaswa kuwa waangalifu sana mu mambo yenye tunajua kuwa tuko wazaifu.—1 Ko. 9:27. w24.07 15 fu. 5-7

Siku ya Posho, 15 Mwezi wa 8

Mukiendelea kuzaa matunda katika kila kazi njema na kuongezeka katika ujuzi wenye hauna makosa wa Mungu.—Kol. 1:10.

Kazi njema yenye kuzungumuziwa mu andiko ya leo, inatia ndani, inatia ndani kuhubiri habari njema. Kwa hiyo wakati tunasoma Neno ya Mungu na kutafakari juu ya mambo yenye tunajifunza, tunamutumainia Yehova zaidi na tunaona kama ni jambo ya maana sana kuhubiri habari njema ya Ufalme. Ili Neno ya Mungu ituletee faida kabisa, hatupaswe kuenda mbio-mbio wakati tuko nasoma, wakati tuko najifunza, na kutafakari juu ya mambo yenye tumesoma. Enda polepole. Kama unasoma andiko yenye hauelewe muzuri, usiipite tu. Tumia kitabu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova ao vyombo vyetu vingine vya kutafuta habari ili upate mafasirio zaidi juu ya ile andiko. Kama unaenda polepole wakati uko najifunza, utaamini kabisa kama mambo yenye Neno ya Mungu inasema ni ya kweli. (1 Te. 5:21) Kadiri unaamini zaidi mambo yenye uko najifunza, ni vile utafurahia kuielezea wengine. w24.04 15 fu. 4-5

Siku ya Yenga, 16 Mwezi wa 8

Niliwaandikia ninyi: ili kujua kama mungetoa jambo lenye kuhakikisha kwamba muko watiifu katika mambo yote.—2 Ko. 2:9.

Daudi alisema hivi juu ya Yehova: “Uko mwema na uko tayari kusamehe.” (Zb. 86:5) Mika aliandika hivi: “Ni Mungu gani mwenye kuwa kama wewe, mwenye kusamehe makosa na mwenye haangalie makosa?” (Mik. 7:18) Na Isaya alisema: “Mutu muovu aache njia yake na mutu mubaya mawazo yake; na amurudilie Yehova, mwenye atamuonyesha rehema, kwa Mungu wetu, kwa maana atasamehe kwa njia kubwa.” (Isa. 55:7) Ili kumuiga Yehova, kutaniko ya Korinto iliambiwa ikaribishe mu kutaniko ule mwanaume mwenye alitubu na kumuhakikishia kama wanamupenda. Kutaniko ilifuata muongozo wa Paulo. Kwa kufanya vile ndugu na dada walionyesha kama walikuwa “watiifu katika mambo yote.” Kusema kweli, kulipita tu miezi tangu ule mwanaume aondolewe mu kutaniko, lakini nizamu ilimuongoza kwenye toba. Kwa hiyo hakukukuwa sababu ya kukawia kumurudisha mu kutaniko. w24.08 17-18 fu. 12-13

Siku ya Kwanza, 17 Mwezi wa 8

Mumoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.—Mt. 24:40.

Tunaishi mu kipindi ya wakati yenye itakuwa na mabadiliko mingi! Hivi karibuni Yesu atahukumu kila mutu. Wakati Yesu alikuwa nazungumuzia kipindi ya wakati yenye kuongoza ku hukumu, alipatia wanafunzi wake “alama” ya unabii ya kuwasaidia kutambua kuwapo kwake na “umalizio wa mupangilio wa mambo.” (Mt. 24:3) Ule unabii unapatikana mu Matayo sura ya 24 na 25, mu Marko sura ya 13, na mu Luka sura ya 21. Yesu alitupatia onyo ya maana sana kwa kutumia mifano tatu. Mufano wa kwanza ni wa kondoo na mbuzi, wa pili ni wa mabikira wenye busara na mabikira wapumbavu, na wa tatu ni mufano wa talanta. Kila mufano unatusaidia kuelewa kama kila mutu atahukumiwa kufuatana na matendo yake. w24.09 20 fu. 1-2

Siku ya Pili, 18 Mwezi wa 8

Mambo yote yenye munafanya, yafanywe kwa upendo.—1 Ko. 16:14.

Yesu ni mufano muzuri sana. Upendo njo ulimuchochea kutumikia bengine. Alipenda Baba yake na alipenda batu. Upendo ulimuchochea kutumika kwa bidii na kufanya kazi za hali ya chini juu ya kusaidia bengine. (Mt. 20:28; Yoh. 13:​5, 14, 15) Ndugu, ikiwa unapenda kuwa mutumishi wa huduma juu unamupenda Yehova na unapenda batu, Yehova atakubariki na atakusaidia ufikie muradi wako, sawa vile muradi wa kuwa mutumishi wa huduma. (1 Pe. 5:5) Mu hii dunia, batu mingi banapendaka batu ya kujitafutia sifa. Lakini mambo haiko vile mu tengenezo ya Yehova. Ndugu mwenye anachochewa na upendo sawa Yesu, hajitafutie mamlaka, cheo, ao kutafuta kuonekana. Kama ndugu mwenye iko najitafutia sifa anapewa madaraka mu kutaniko, inawezekana hatakubali kufanya kazi za hali ya chini zenye inaomba kufanya juu ya kuhangaikia kondoo wa Yehova, wenye Yehova anapenda sana. Anaweza kuona kama zile kazi zinamushushia heshima.—Yoh. 10:12. w24.11 15 fu. 6-7

Siku ya Tatu, 19 Mwezi wa 8

Roho takatifu imewaweka ninyi kuwa waangalizi.—Mdo. 20:28.

Mu dunia yote tuko na lazima ya ndugu wengi zaidi wa kutumikia kama “zawadi katika wanadamu.” (Efe. 4:8) Kama uko ndugu mwenye kubatizwa, “uko na uwezo wa kusaidia”? (Mez. 3:27) Uko tayari kutimiza mambo yenye inaombwa ili kuwa mutumishi wa huduma? Unaweza kutimiza mambo yenye inaombwa ili ufikie kuwa muzee, juu usaidie kutimiza mahitaji ya ndugu zako? Unaweza kubadilisha mambo fulani mu maisha yako juu ufikie kujaza fomu ya kuenda ku Masomo ya Waeneza-injili wa Ufalme? Ku ile masomo utajifunza mambo mingi yenye itakusaidia juu Yesu aweze kukutumikisha zaidi. Ikiwa unaona kama haustahili, sali kwa Yehova. Umuombe akusaidie na roho yake takatifu juu utimize muzuri mugao wowote wenye unapewa. (Lu. 11:13) Juu Yesu ametutolea ndugu wenye kuwa “zawadi katika wanadamu,” ile inaonyesha kama iko natuongoza mu hizi siku za mwisho. (Mt. 28:20) Kwa kweli, tuko wenye shukrani juu Mufalme wetu ni mwenye upendo, ni mukarimu, na anatutolea wanaume wenye kustahili juu watimize mahitaji yetu. w24.10 23 fu. 16-17

Siku ya Ine, 20 Mwezi wa 8

Mambo ya zamani hayatakumbukwa.—Isa. 65:17.

Tuseme nini kuhusu mambo yote yenye imeletea watu wa Mungu maumivu na mahangaiko? Ku mwisho ile mambo yote “itasahauliwa [na] itafichwa ili macho [ya Mungu] yasiione.” (Isa. 65:16) Yehova atatosha magumu yetu yote, na kisha wakati hatutakumbuka tena maumivu yote yenye ile magumu ilituletea. Hata leo akili yetu inatulia wakati tuko ku mikutano ya Kikristo kwenye tunaweza kutia pembeni mahangaiko yenye huu ulimwengu wa Shetani unatuletea. Tunasaidia mu paradiso yetu ya kiroho mukuwe utulivu wakati tunaonyesha sifa za tunda la roho sawa vile upendo, furaha, amani, fazili, na upole. (Gal. 5:​22, 23) Ni baraka sana kuwa mu tengenezo ya Mungu! Wale wenye wanabakia mu paradiso ya kiroho wataona utimizo kamili wa ahadi ya Mungu ya “mbingu mupya na dunia mupya.” w24.04 22 fu. 9-10

Siku ya Tano, 21 Mwezi wa 8

Ni mutego kwa mutu kutangaza haraka-haraka, “Ni kitakatifu!” Na kisha tu wakati fulani anachunguza kile aliwekea naziri.—Mez. 20:25.

Wakati wa urafiki wa kimapenzi ni wakati wenye kufurahisha, lakini pia ni hatua ya maana yenye inaweza kuongoza ku ndoa. Siku ya ndoa, ndugu na dada wenye kuwa mu uhusiano wa kimapenzi wanafanya naziri mbele ya Yehova kama watapendana na kuheshimiana muda wote wa maisha yao. Mbele ya kufanya naziri yoyote, tunapaswa kufikiria naziri yetu kwa uzito. Ni vile pia kuhusu naziri ya ndoa. Urafiki wa kimapenzi unasaidia ndugu na dada wajuane muzuri, na wakamate uamuzi wa muzuri. Ule uamuzi unaweza kuwa kuoana na wakati fulani unaweza kuwa kuvunja urafiki. Kama ndugu na dada wanavunja urafiki wao wa kimapenzi, ile haimaanishe kama wamekosea. Lakini inaonyesha kama ule urafiki ulitimiza kusudi yake, uliwasaidia kujua ikiwa wanaweza kuoana ao hapana. Juu ya nini ni jambo ya maana tukuwe na mawazo yenye kufaa juu ya urafiki wa kimapenzi? Wakati ndugu ao dada mwenye hayafunga ndoa iko na mawazo yenye kufaa, hatafanya urafiki wa kimapenzi na mutu mwenye hana nia ya kuoana naye. w24.05 26-27 fu. 3-4

Siku ya Posho, 22 Mwezi wa 8

Usisikilie haya. . . ushahidi juu ya Bwana wetu.—2 Ti. 1:8.

Wakati fulani vijana Wakristo wanaweza kuogopa kutetea imani yao. Wanaweza kukosa mambo ya kusema wakati wanajifunza mageuzi ku masomo. Juu ya nini? Juu mwalimu anaweza kuonyesha kama fundisho ya mageuzi ni ya kweli kabisa. Kama uko muzazi, namna gani unaweza kusaidia mutoto wako atetee imani yake bila kuogopa? Umuhakikishie kama hapaswe kusikia haya juu anaamini kama kuko Muumbaji. Juu ya nini? Kusema kweli, wanasayansi wengi wanaamini pia kama uzima haukujitokeza tu wenyewe. Wametambua kama vitu vyenye uzima vilifanywa kwa njia ya ajabu sana, na wameelewa kama kuko mutu fulani mwenye akili mwenye alivifanya. Kwa hiyo, hawakubaliane na fundisho la mageuzi. Juu mutoto wako akuwe hakika kabisa kama kuko Muumbaji, anaweza kufikiria mambo yenye ilisaidia ndugu na dada wengine waamini kama uzima uliumbwa. w24.12 18 fu. 14-15

Siku ya Yenga, 23 Mwezi wa 8

Akakuwa na furaha kubwa kupitia roho takatifu.—Lu. 10:21.

Yesu aliendelea kuwa na mawazo ya muzuri juu ya kazi ya kuhubiri. Ile ilimusaidia aendelee kuhubiri kwa bidii. Kwa mufano, ku mwisho-mwisho wa mwaka wa 30, Yesu aliona kama batu mingi balikuwa tayari kusikiliza mafundisho yake, na alibalinganisha na shamba yenye ilikuwa tayari kwa ajili ya mavuno. (Yoh. 4:35) Mwaka moya kisha pale, aliambia banafunzi yake hivi: “Mavuno ni mengi.” (Mt. 9:​37, 38) Kisha alifikia kusema tena hivi: “Mavuno ni mengi . . . mumuombe Bwana wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno yake.” (Lu. 10:2) Yesu aliendelea kuwa na tumaini kama batu bangekubali habari njema, na alifurahi wakati balifanya vile. Yesu aliambia banafunzi yake baendelee kuwa na mawazo ya muzuri juu ya habari yenye balikuwa natangazia batu. Ile ingefanya baendelee kuhubiri kwa bidii. w25.03 18-19 fu. 15-16

Siku ya Kwanza, 24 Mwezi wa 8

Mungu wangu ni mwamba wangu wenye ninakimbilia.—Zb. 94:22.

Yehova ni kimbilio yetu. Sawa vile mwamba kubwa unaweza kuwa fasi kwenye mutu anaweza kujificha wakati wa mvua kubwa yenye upepo, Yehova anatulinda wakati tunakutana na hali za nguvu mu maisha. Anatulinda na anatuhakikishia kama magumu yenye tuko nayo haitaendelea kututesa milele. Na zaidi ya ile, anatupatia hii ahadi: Atatosha mambo yote yenye inatuletea mahangaiko na mateso. (Eze. 34:​25, 26) Njia moya ya kumufanya Yehova kuwa Kimbilio yetu ni kusali kwake. Wakati tunasali, Yehova anatupatia “amani ya Mungu” yenye inalinda moyo na akili yetu. (Flp. 4:​6, 7) Kila siku Yehova iko pale kwa ajili yetu. Tunaweza kumutegemea kwa sababu yeye ni “Mwamba wa milele.” (Isa. 26:​3, 4) Sikuzote atakuwa pale ili kutimiza ahadi zake, kusikiliza sala zetu, na kututegemeza. Tunaweza pia kumutegemea Yehova kwa sababu ni mushikamanifu kwa wale wenye kumutumikia. (2 Sa. 22:26) Hatasahau hata siku moya mambo yenye tunafanya, na kila wakati atakuwa tayari kutubariki.—Ebr. 6:10; 11:6. w24.06 27 fu. 4-6

Siku ya Pili, 25 Mwezi wa 8

Linda moyo wako kuliko vitu vyote vyenye unalinda, kwa maana ni mule munatoka chemchemi za uzima.—Mez. 4:23.

Mambo ya kujifurahisha yenye haifae, marafiki wabaya, na kupenda sana vitu vya kimwili, kunaweza kugawanya moyo wetu. Kama tunatambua kama jambo fulani inaanza kupunguza upendo wetu kwa Yehova, tutende bila kukawia na tuepuke kabisa ile jambo. (Mt. 5:​29, 30) Hatupaswe kuacha moyo wetu ugawanyike. Tunaweza kujidanganya kwa kuwaza kama ikiwa tunaongeza bidii yetu mu mambo ya kiroho, mambo ya mubaya haitakuwa na matokeo juu yetu. Ili kuelewa, fikiria hii mufano: Wazia kuko baridi sana na upepo. Wakati unafika ku nyumba, unakonga moto. Lakini, ile moto itakusaidia kabisa kama unaacha mulango wazi? Hapana. Hewa ya baridi itaingia tena na kujaa mu nyumba yote. Somo ni nini? Haitoshe tu kula chakula ya kiroho yenye inafanya tubakie karibu na Yehova. Tunapaswa pia kufungia mulango mambo ya mubaya. Ile itafanya “hewa” ya mubaya ya huu ulimwengu, ni kusema tabia zenye hazimufurahishe Mungu zisiingie mu moyo wetu na kuugawanya.—Efe. 2:2. w24.07 21 fu. 6-7

Siku ya Tatu, 26 Mwezi wa 8

Muendelee kupenda maadui wenu na kusali kwa ajili ya wale wenye kuwatesa ninyi.—Mt. 5:44.

Ni nguvu kuelewa maumivu yenye Yesu alisikiaka wakati alitendewa mambo ya kuumiza sana. Lakini, hakushindwa na uovu wenye alitendewa. Kuliko kuomba Yehova apatie malipizi wale maaskari wenye walimupigilia misumari ku muti, alisali hivi: “Baba, uwasamehe, kwa maana hawajue jambo lenye wanafanya.” (Lu. 23:34) Wakati tunasali kwa ajili ya batu benye kututendea mubaya, ile inapunguza maumivu yetu na kasirani yetu na hata inabadilisha namna yetu ya kuona batu benye kutukosea. Mbele mwisho wa huu ulimwengu ufike, inawezekana tutatendewa bila haki. Lakini, hata kutokee nini, tusiache kusali hata siku moya kwa Yehova juu atusaidie. Pia tuige namna Yesu alitenda wakati balimutendea mubaya, na tuendelee kutumikisha kanuni za Biblia. Kama tunafanya vile, tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatubariki.—1 Pe. 3:​8, 9. w24.11 6 fu. 16; 7 fu. 17, 19

Siku ya Ine, 27 Mwezi wa 8

Hauko Mungu mwenye anafurahia uovu; hakuna mutu yeyote mubaya mwenye anaweza kukaa pamoja na wewe.—Zb. 5:4.

Yehova haiko Mungu mwenye anaachiliaka tu mambo. Anachukia zambi. (Zb. 5:​4-6) Anatuomba tuheshimie kanuni zake za haki zenye anatutolea mu Neno yake. Ni kweli Yehova hatazamie tukuwe wakamilifu juu anajua kama hatukamilike. (Zb. 130:​3, 4) Lakini Yehova hakubali ‘watu wenye hawamuogope, wenye wanatumia fazili zake zenye hazistahiliwe kama kisingizio cha kuwa na mwenendo mupotovu wa bila haya.’ (Yud. 4) Na hata, Biblia inazungumuzia “uharibifu wa watu wenye hawamuogope Mungu” ku vita ya Mungu ya Armagedoni. (2 Pe. 3:7; Ufu. 16:16) Lakini, Yehova hapendi mutu yeyote aharibiwe. Biblia inaonyesha wazi kama Yehova “anataka wote wafikie kutubu.” (2 Pe. 3:9) Wazee Wakristo wanamuiga Yehova wakati wanajikaza kusaidia wakosaji kwa uvumilivu wabadilishe matendo yao na wakuwe tena na urafiki muzuri pamoya na Yehova. w24.08 26 fu. 1-2

Siku ya Tano, 28 Mwezi wa 8

Unafungua mukono wako na kutimiza tamaa ya kila kitu chenye uzima.—Zb. 145:16.

Sawa vile Yehova, na siye tunaweza kupatia watu vitu juu tunawapenda. Kwa mufano, unajua ndugu ao dada fulani mwenye iko na lazima ya chakula ao manguo? Yehova anaweza kukutumikisha juu amupatie ule mutu vitu vyenye iko navyo lazima. Watu wa Yehova wanajulikana kuwa watu wakarimu, zaidi sana wakati wa misiba. Kwa mufano mu kipindi ya Korona ndugu na dada walitolea wengine chakula, manguo, na vitu vingine vya lazima. Pia wengi walitoa michango juu ya kutegemeza kazi ya ulimwenguni pote. Ile michango ilifanya iwezekane kusaidia ndugu na dada wa mu dunia yote mu ile kipindi ya nguvu. Wale ndugu na dada wakarimu walifuata shauri yenye kuwa mu Waebrania 13:16 yenye inasema: “Musisahau kutenda mema na kushiriki pamoja na wengine vile vyenye muko navyo, kwa maana Mungu anapendezwa na zabihu za namna hiyo.” w24.09 27 fu. 6-7

Siku ya Posho, 29 Mwezi wa 8

Muhakikishe mambo ya maana zaidi.—Flp. 1:10.

Fikiria hii hali. Uko natafuta kazi ya kukusaidia kutimiza mahitaji ya familia yako. Unapata kazi mbili. Unatafuta kujua habari zote; kwa mufano ni kazi ya namna gani, programu ya kazi itakuwa namna gani, itakuwa nakamata wakati ngapi juu ya kufika ku kazi, na mambo ingine. Zile kazi zote mbili hazipingane na kanuni za Biblia. Pengine unafurahia zaidi kazi moya kati ya zile kazi mbili juu ni kazi yenye unapendaka ao juu watakuwa nakulipa makuta mingi. Lakini kuko mambo ingine ya kufikiria mbele ya kukamata uamuzi. Kwa mufano, mu zile kazi mbili kuko yenye itakuzuia kukusanyika? Kuko yenye itakukula wakati mingi mupaka ukose wakati wa kupitisha pamoya na familia yako na kuitimizia mahitaji ya kiroho? Kujiuliza maulizo ya vile kutakusaidia utie “mambo ya maana zaidi,” ni kusema ibada na mahitaji ya familia yako, pa nafasi ya kwanza kuliko vitu vya kimwili. Kisha unaweza sasa kukamata uamuzi wenye Yehova atabariki. w25.01 17-18 fu. 11-13

Siku ya Yenga, 30 Mwezi wa 8

Yehova iko karibu na wale wenye kuvunjika moyo.—Zb. 34:18.

Hata kama batu fulani balikutendea mubaya, ukuwe hakika kama Yehova anakupenda na anakuona kuwa wa maana. Kama unajisikia kuwa mwenye “kupondwa roho,” kumbuka kama Yehova aliona mambo ya muzuri mu moyo wako na alikualika kwake. (Yoh. 6:44) Kila siku, Yehova iko tayari kukusaidia juu uko wa maana kwake. Wakati tunachunguza mufano wa Yesu, tunaelewa namna Yehova anatuona. Mu utumishi wake ku dunia, Yesu alihangaikia bale benye balikuwa naonewa, na alibatendea muzuri. (Mt. 9:​9-12) Wakati mwanamuke mwenye alikuwa na ugonjwa mubaya sana aligusa nguo yake juu apone, Yesu alimufariji na alimupongeza juu ya imani yake. (Mk. 5:​25-34) Yesu anaiga kwa ukamili sifa za Baba yake. (Yoh. 14:9) Kwa hiyo, unaweza kuwa hakika kama Yehova anakuona kuwa wa maana na anaona sifa zako za muzuri, anaona imani yako, na namna unamupenda. w24.10 7 fu. 4-5

Siku ya Kwanza, 31 Mwezi wa 8

Kusanya machozi yangu katika chupa yako ya ngozi.—Zb. 56:8.

Daudi alipata magumu mingi sana mu maisha yake yenye ilifanya alie. Batu balimuchukia na hata batu benye alitumainia balimusaliti. (1 Sa. 19:​10, 11; 2 Sa. 15:​10-14, 30) Wakati fulani, aliandika hivi: “Nimechoka kwa sababu ya kilio changu cha maumivu; usiku wote ninalowanisha kitanda changu kwa machozi.” (Zb. 6:6) Hata kama Daudi alipata magumu mingi, alikuwa hakika kama Yehova alimupenda. Aliandika hivi: “Yehova atasikia sauti ya kilio changu.” (Zb. 6:8) Maneno ya andiko ya leo inaonyesha wazi namna Yehova anatupenda na kutuhangaikia sana. Daudi alisikia sawa vile Yehova iko anakusanya machozi yake mu chupa ao kuiandika mu kitabu. Daudi alikuwa hakika kama Yehova aliona na alikumbuka maumivu yake. Alikuwa hakika kama Baba yake wa mbinguni mwenye upendo alijua magumu yenye alipita ndani, lakini pia alijua maumivu yenye ile magumu ilimuletea. w24.12 22 fu. 11-12

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine