Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • es26 uku. 67-77
  • Mwezi wa 7

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mwezi wa 7
  • Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
  • Vichwa Vidogo
  • Siku ya Tatu, 1 Mwezi wa 7
  • Siku ya Ine, 2 Mwezi wa 7
  • Siku ya Tano, 3 Mwezi wa 7
  • Siku ya Posho, 4 Mwezi wa 7
  • Siku ya Yenga, 5 Mwezi wa 7
  • Siku ya Kwanza, 6 Mwezi wa 7
  • Siku ya Pili, 7 Mwezi wa 7
  • Siku ya Tatu, 8 Mwezi wa 7
  • Siku ya Ine, 9 Mwezi wa 7
  • Siku ya Tano, 10 Mwezi wa 7
  • Siku ya Posho, 11 Mwezi wa 7
  • Siku ya Yenga, 12 Mwezi wa 7
  • Siku ya Kwanza, 13 Mwezi wa 7
  • Siku ya Pili, 14 Mwezi wa 7
  • Siku ya Tatu, 15 Mwezi wa 7
  • Siku ya Ine, 16 Mwezi wa 7
  • Siku ya Tano, 17 Mwezi wa 7
  • Siku ya Posho, 18 Mwezi wa 7
  • Siku ya Yenga, 19 Mwezi wa 7
  • Siku ya Kwanza, 20 Mwezi wa 7
  • Siku ya Pili, 21 Mwezi wa 7
  • Siku ya Tatu, 22 Mwezi wa 7
  • Siku ya Ine, 23 Mwezi wa 7
  • Siku ya Tano, 24 Mwezi wa 7
  • Siku ya Posho, 25 Mwezi wa 7
  • Siku ya Yenga, 26 Mwezi wa 7
  • Siku ya Kwanza, 27 Mwezi wa 7
  • Siku ya Pili, 28 Mwezi wa 7
  • Siku ya Tatu, 29 Mwezi wa 7
  • Siku ya Ine, 30 Mwezi wa 7
  • Siku ya Tano, 31 Mwezi wa 7
Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
es26 uku. 67-77

Mwezi wa 7

Siku ya Tatu, 1 Mwezi wa 7

Sijamuona mutu yeyote mwenye haki akiwa ameachwa.—Zb. 37:25.

Batumishi fulani ya Yehova banateseka kwa sababu ya uzee, magonjwa, ao ulemavu. Ile inaweza kufanya bajisikie kuwa Yehova habaone kuwa ba maana. Banaweza kujiuliza hivi: ‘Yehova anaweza tena kunitumikisha?’ Muandikaji wa Zaburi 71 alikuwa pia na ile mahangaiko. Alisali hivi: “Usiniache wakati nguvu zangu zinaisha.” (Zb. 71:​9, 18) Lakini aliendelea kuwa hakika kama, ikiwa anamutumikia Yehova kwa uaminifu, Yehova atamuongoza na kumutegemeza. Sawa vile ule muandikaji wa zaburi alifikia kuelewa, Yehova anafurahia wale wenye wanafanya yao yote juu ya kuendelea kumutumikia hata kama hali yao inawatilia mipaka fulani. (Zb. 37:​23-25) Ndugu na dada wenye kuzeeka, mujione vile Yehova anawaona. Anaweza kuwasaidia kuwa nguvu kiroho hata kama hamuna tena nguvu mingi kimwili. (Zb. 92:​12-15) Kuliko kukazia akili mambo yenye hauwezi kufanya, kazia akili mambo yenye unaweza kufanya. w24.10 28 fu. 14-16

Siku ya Ine, 2 Mwezi wa 7

Kuhusu kula chakula chenye kilitolewa kwa sanamu, tunajua kwamba sanamu haiko kitu katika ulimwengu.—1 Ko. 8:4.

Mara mingi Wakristo wenye wangali watoto kiroho hawajuake wafanye nini wakati wanakutana na hali zenye zinaomba kufikiria kanuni za Biblia na kuzitumikisha. Kama mu Biblia hamuna sheria yenye inahusu hali yao, wamoja wanaweza kuona kama wako huru kufanya jambo yoyote yenye wanapenda. Wengine wanaweza kuomba sheria iwekwe kwenye haiko lazima kufanya vile. Kwa mufano, inawezekana Wakristo katika Korinto waliomba mutume Paulo awapatie sheria kuhusu kula ao kutokula chakula yenye ilitolewa kwa sanamu. Kuliko kuwaambia mambo ya kufanya, Paulo aliwaambia kama kila mumoja wao alikuwa na “haki ya kuchagua” kwa kutegemea mambo yenye zamiri yake inamuruhusu kufanya. Alitumia kanuni zenye zingesaidia kila mutu aendelee kuwa na zamiri safi na wakati uleule asikwaze wengine. (1 Ko. 8:​7-9) Kwa kufanya vile, Paulo alikuwa nasaidia Wakorinto wakomae kiroho ili waweze kutumia nguvu zao za utambuzi kuliko kutegemea watu wengine ao kutafuta tu sheria. w24.04 5 fu. 14

Siku ya Tano, 3 Mwezi wa 7

Mimi, Yehova, ninachunguza moyo . . . ili kumupatia kila mumoja kulingana na njia zake.—Yer. 17:10.

Mu siku za Yona, watu wa Ninawi walikuwa na nafasi ya kutubu. Zaidi ya ile, kumbuka mambo yenye Yesu alisema kuhusu “ufufuo wa hukumu.” Alisema kama kati ya wenye watafufuliwa kutakuwa “wale wenye walizoea kutenda mambo maovu.” (Yoh. 5:29) Inaonekana kama kunaweza kuwa tumaini fulani kwa ajili ya watu wa Sodoma na Gomora pia. Inawezekana hata wamoja kati yao wafufuliwe. Kama ni vile, tutakuwa na nafasi ya kuwafundisha juu ya Yehova na Yesu Kristo. Sikuzote Yehova ‘anachunguza moyo, anachunguza mawazo ya ndani kabisa.’ Hata kuhusu ufufuo, ni vile atafanya; ‘atamupatia kila mumoja kulingana na njia zake.’ Yehova atapatia watu malipizi wakati ni lazima kufanya vile, lakini ataonyesha rehema wakati inawezekana kufanya vile. Kwa hiyo, hatupaswe kuwaza kama mutu fulani hana tumaini ya ufufuo ikiwa Biblia haiseme vile waziwazi! w24.05 5-6 fu. 15-16

Siku ya Posho, 4 Mwezi wa 7

Usiogope. Nitakusaidia.—Isa. 41:13.

Wakati watumishi wa Mungu wa zamani walikuwa na mugao wa nguvu, Neno ya Mungu iliwatia nguvu. Kwa mufano, fikiria nabii Yeremia. Alisita wakati Mungu alimupatia mugao wa kuhubiri. Yeremia alisema hivi: “Sijue namna ya kusema, kwa maana niko kijana mudogo tu.” (Yer. 1:6) Ni nini ilimusaidia akuwe na uhodari wa kuhubiri? Neno la Mungu njo lilimutia nguvu. Alisema hivi: “Lilikuwa kama moto wenye kuwaka wenye kufungiwa katika mifupa yangu, na nikachoka kulizuia.” (Yer. 20:​8, 9) Hata kama watu wa mu eneo yenye Yeremia alihubiri hawakupendezwa na ujumbe wake, ujumbe wenye alikuwa nahubiri ulimupatia nguvu yenye alikuwa nayo lazima ili kutimiza mugao wake. Ujumbe wenye kuwa mu Neno ya Mungu unatia Wakriso nguvu. Mutume Paulo alisema kama kuwa na ujuzi wenye hauna makosa kungechochea wale ndugu “watembee kwa namna yenye kumustahili Yehova” wakati walikuwa naendelea “kuzaa matunda katika kila kazi njema.”—Kol. 1:​9, 10. w24.04 14-15 fu. 2-4

Siku ya Yenga, 5 Mwezi wa 7

Sadoki kuhani . . . akamutia Sulemani mafuta.—1 Fa. 1:39.

Sadoki alibakia mushikamanifu kwa Yehova hata kama Kuhani Mukubwa Abiatari alikamata uamuzi mubaya wa kuunga mukono Adoniya mwana wa Daudi, mwenye alikuwa napanga kuiba ufalme. Daudi alikuwa hakika kama Sadoki alikuwa mushikamanifu. Wakati mupango wa Adoniya ulijulikana, Daudi alimuomba Sadoki, Natani, na Benaya wamuweke Sulemani kuwa mufalme. (1 Fa. 1:​32-34) Inawezekana kabisa kama kuwa pamoya na waabudu wa Yehova washikamanifu, sawa vile Natani na wengine wenye walimuunga mukono Mufalme Daudi, kulimutia nguvu Sadoki na kulimutia moyo. Wakati Sulemani alikuwa sasa mufalme, ‘aliweka Sadoki kuwa kuhani pa nafasi ya Abiatari.’ (1 Fa. 2:35) Namna gani tunaweza kuiga Sadoki? Kama mutu fulani mwenye tunapenda anaamua kumuacha Yehova, tuonyeshe wazi kama siye tutabakia washikamanifu kwa Yehova. (Yos. 24:15) Yehova atakupatia nguvu na uhodari wenye uko nao lazima. Umutegemee kwa kuendelea kusali kwake na kubakia karibu na waabudu wenzako wenye kuwa washikamanifu. Yehova anafurahia sana ushikamanifu wako, na atakubariki.—2 Sa. 22:26. w24.07 6-7 fu. 16-17

Siku ya Kwanza, 6 Mwezi wa 7

Tusiache kufanya mema.—Gal. 6:9.

Zaburi 15:​2, inaonyesha kama rafiki ya Mungu ni “ule mwenye anatembea bila kosa, mwenye anazoea kufanya mambo yenye kuwa sawa.” Maneno “anatembea” na “anazoea kufanya” inaonyesha kama tunapaswa kuendelea kufanya jambo fulani. Lakini inawezekana kabisa ‘kutembea bila kosa’? Ndiyo. Ni kweli kwamba hakuna mwanadamu mukamilifu. Lakini Yehova anaweza kuona kuwa ‘tunatembea bila kosa’ ikiwa tunafanya yetu yote ili kumutii. Wakati tunajitoa kwa Mungu na kubatizwa, ni sawa vile tunaanza safari pamoya na Mungu. Kumbuka kama zamani, kuwa mu taifa ya Israeli hakukufanya mara moya mutu astahili kuwa mugeni wa Yehova. Waisraeli fulani walikuwa namuitia Yehova, lakini hapana “katika kweli na haki.” (Isa. 48:1) Waisraeli waaminifu walipaswa kujifunza kuhusu mambo yenye Yehova anaomba na kuifuata. Leo pia, juu Mungu atukubali, haitoshe tu kubatizwa na kupitisha wakati pamoya na Wakristo mu kutaniko. Tunapaswa ‘kuzoea kufanya mambo yenye kuwa sawa.’ w24.06 9 fu. 4; 10 fu. 6

Siku ya Pili, 7 Mwezi wa 7

Mukuwe waigaji wa Mungu.—Efe. 5:1.

Ni mu njia gani fulani Yehova anaonyesha ukarimu? Tuzungumuzie mifano fulani. Yehova anatupatia vitu vya kimwili. Ni kweli kwamba hatukuwake sikuzote na vitu vya bei sana. Lakini Yehova anahakikisha kila siku kama tuko na vitu vyenye tuko navyo lazima. Kwa mufano, anahakikisha kama tuko na chakula, manguo, na fasi ya kuishi. (Zb. 4:8; Mt. 6:​31-33; 1 Ti. 6:​6-8) Yehova anatupatia vitu vya kimwili juu tu analazimika kufanya vile? Hapana. Ona maneno ya Yesu yenye kuwa mu Matayo 6:​25, 26. Wakati Yesu alizungumuzia ndege, alisema hivi: “Hawapande mbegu ao kuvuna ao kukusanya katika madepo.” Kisha Yesu alisema hivi: “Baba yenu wa mbinguni anawalisha.” Na kisha akauliza hivi: “Je, ninyi hamuko wa maana kuliko wao?” Yesu alipenda kufundisha nini? Juu Yehova anahangaikia wanyama, tuko hakika kama atatupatia vitu vyenye tuko nayo lazima. Sawa baba, Yehova anahangaikia familia yake kwa upendo.—Zb. 145:16; Mt. 6:32. w24.09 26-27 fu. 4-6

Siku ya Tatu, 8 Mwezi wa 7

Wanaume wenye kutumikia muzuri wanajipatia wenyewe sifa ya muzuri na uhuru mwingi wa kusema katika imani.—1 Ti. 3:13.

Mutumishi wa huduma ni ndugu mwenye kubatizwa mwenye anawekwa na roho takatifu juu ya kusaidia wazee kufanya mambo mbalimbali mu kutaniko. Watumishi huduma ni wanaume wa kiroho. Wanamupenda Yehova na wanatii kanuni zake. Wanapenda sana ndugu na dada zao. (Mt. 22:​37-39) Namna gani ndugu mwenye kubatizwa anaweza kujikaza juu afikie kuwa mutumishi wa huduma? Biblia inaonyesha mambo yenye ndugu wenye kubatizwa wanapaswa kutimiza juu wawekwe kuwa watumishi wa huduma. (1 Ti. 3:​8-10, 12) Unaweza kujikaza juu ufikie ile pendeleo kwa kujifunza juu ya ile mambo na kujikaza sana kuitimiza. Lakini kwanza ni muzuri ufikirie nia yenye inakuchochea kujikaza kufikia ile pendeleo. w24.11 15 fu. 4-5

Siku ya Ine, 9 Mwezi wa 7

Hamukulikubali kama neno la wanadamu, lakini mulilikubali kama vile liko kwa kweli, kama neno la Mungu.—1 Te. 2:13.

Watu wengi wanasema kama wamesoma Biblia mara mingi. Lakini, wanaamini kabisa mambo yenye Biblia inasema? Wanatumikisha mambo yenye wanasoma na kufanya mabadiliko mu maisha yao? Jambo ya kuhuzunisha ni kama, mara mingi jibu ni hapana. Wako tofauti kabisa na watu wa Yehova! Tunajikaza kuonyesha kama Neno ya Mungu iko nafanya kazi mu maisha yetu. Haikuwake mwepesi sikuzote kusoma na kutumikisha mambo yenye tunasoma mu Neno ya Mungu. Inaweza kuwa nguvu kupata wakati wa kusoma. Ao pengine tunaweza kuanza kusoma mbiombio bila kufikiria mambo yenye tuko nasoma. Ao tena, tunaweza kuona kama tuko na mambo mingi ya kufanyia kazi. Ikuwe unapambana na hali gani, ujue kama unaweza kuishinda. Utaishinda kwa musaada wa Yehova. Tuazimie basi kuwa watendaji wa Neno. Bila shaka, kadiri tunajikaza kusoma Neno ya Mungu na kuitumikisha mu maisha yetu, ni vile tutakuwa na furaha.—Yak. 1:25. w24.09 7 fu. 15-16

Siku ya Tano, 10 Mwezi wa 7

Muendelee kuomba, na mutapewa.—Lu. 11:9.

Kupitia roho yake takatifu, Yehova anatufariji wakati jambo fulani ya mubaya inatufikia. Kama uko mu magumu ya nguvu sana, unaweza kumumwangia Yehova moyo wako katika sala, unaweza kusali saa yoyote na sala zako zinaweza kuwa na urefu wenye unapenda. (Zb. 86:3; 88:1) Umuombe Yehova roho yake takatifu tena na tena. Yehova hawezi kuzarau mambo yenye unamuomba.Umepata magumu ya nguvu yenye imekumaliza nguvu? Roho takatifu inaweza kukupatia nguvu ya kuendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu. (Efe. 3:16) Namna gani unaweza kutenda kulingana na sala yako ya kuomba roho takatifu? Fanya mambo mbalimbali yenye itasaidia roho takatifu ya Mungu ifanye kazi mu maisha yako. Mambo sawa vile kukusanyika na kuhubiri. Jaza mu akili yako mawazo ya Yehova kwa kusoma Neno yake kila siku. (Flp. 4:​8, 9) Wakati uko nasoma, tafuta habari za watu wa Mungu wenye walipambana na magumu na ufikiri sana juu ya namna Yehova aliwasaidia kuvumilia. w24.10 9 fu. 12-14

Siku ya Posho, 11 Mwezi wa 7

Mungu alipenda ulimwengu sana.—Yoh. 3:16.

Kama Yehova na Mwana wake, tunapenda watu. (Mez. 8:31) Tunasikilia huruma wale wenye wako “bila Mungu” na wenye “hawana tumaini.” (Efe. 2:12) Wako nahangaika sana kwa sababu ya magumu ya maisha, lakini tuko na jambo yenye wako nayo lazima kabisa, ni kusema habari njema ya Ufalme wa Mungu. Upendo na huruma inatusaidia kufanya yote yenye tunaweza ili kuwatangazia habari njema. Ile habari ya maana sana inaweza kuwapatia tumaini, kuwasaidia wakuwe na maisha ya muzuri leo kadiri inawezekana, na kuwapatia tumaini ya kuwa na “uzima wa kwelikweli,” ni kusema uzima wa milele mu ulimwengu mupya wa Mungu. (1 Ti. 6:19)Kupenda watu kunatuchochea pia tuwaonye kuhusu mwisho wa huu ulimwengu wenye unakaribia. (Eze. 33:​7, 8) Tunapenda wajue mambo yenye itatokea wakati wa taabu kubwa: Dini ya uongo itaharibiwa na mupangilio wote wa mambo wa Shetani utaharibiwa ku Armagedoni.—Ufu. 16:​14, 16; 17:​16, 17; 19:​11, 19, 20. w24.05 16 fu. 8-9

Siku ya Yenga, 12 Mwezi wa 7

Musijilipizie kisasi, lakini muachie kasirani kali nafasi; kwa maana imeandikwa: “‘Kisasi ni changu; mimi nitalipa,’ ni vile Yehova anasema.”—Ro. 12:19.

Wakati mutume Paulo aliambia Wakristo “muachie kasirani kali nafasi,” alikuwa nazungumuzia kasirani ya nani? Kama tunachunguza maandiko yenye kufuata tunaona kama alikuwa nazungumuzia kasirani ya Yehova. Tunaachia kasirani ya Yehova nafasi wakati tunamuacha atende kwa haki kwa wakati wenye anaona kuwa unafaa, na mu njia yenye anaona kuwa inafaa. Kisha ndugu mwenye kuitwa John kutendewa mubaya, alisema hivi: “Nilipaswa kujikaza sana juu nisitende jambo ya mubaya, haikukuwa mwepesi kufanya vile. Waroma 12:19 ilinisaidia nimungoye Yehova atende.” Tunapata faida wakati tunangoya Yehova ashugulikie mambo. Kama tunafanya vile, tutaepuka kubeba muzigo na mahangaiko ya kujaribu kushugulikia mambo siye wenyewe. Yehova iko tayari kutusaidia. Ni sawa vile anasema hivi: ‘Acha ile ukosefu wa haki mu mikono yangu; nitashugulikia mambo.’ Yehova anasema “mimi nitalipa.” Kama tunaamini ile ahadi, tunaweza kuacha mambo mu mikono yake na kuwa hakika kama ataishugulikia mu njia ya muzuri zaidi. w24.11 6 fu. 14-15

Siku ya Kwanza, 13 Mwezi wa 7

Utupatie kila siku mukate wetu kulingana na mahitaji yetu ya kila siku.—Lu. 11:3.

Hatupaswe kutia vitu vya kimwili fasi ya kwanza mu maisha yetu. Mutume Paulo alionyesha ile jambo wakati aliandikia Wakristo wenye waliishi karibu na mwisho wa mupangilio wa mambo wa Wayahudi. Alizungumuzia mufano mubaya wa Waisraeli wakati walikuwa mu jangwa, na mambo yenye ilitokea karibu na Mulima Sinai. Alionya Wakristo ‘wasitamani mambo ya mubaya, kama vile [Waisraeli] waliyatamani.’ (1 Ko. 10:​6, 7, 11) Yehova alikuwa ametolea Waisraeli mana kwa muujiza, lakini juu walikuwa na pupa ya chakula, walifikia kuona ule muujiza kuwa “mambo ya mubaya.” (Hes. 11:​4-6, 31-34) Na wakati waliabudu kitoto dume cha ngombe cha zahabu, walionyesha kama walihangaikia sana kula, kunywa, na kujifurahisha kuliko kumutii Mungu. (Kut. 32:​4-6) Paulo alitumia mufano wa wale Waisraeli juu ya kuonya Wakristo wenye walikuwa naishi karibu na wakati wenye Yerusalemu na hekalu yake ingeharibiwa mu mwaka wa 70 K.K.Y. Leo tunaishi karibu na mwisho wa huu ulimwengu, kwa hiyo ni muzuri tukamate kwa uzito mashauri ya Paulo. w24.12 6 fu. 13

Siku ya Pili, 14 Mwezi wa 7

Ufurahi pamoja na bibi wa ujana wako.—Mez. 5:18.

Yehova ni “Mungu mwenye furaha,” na anapenda na siye tukuwe na furaha. (1 Ti. 1:11) Ametupatia zawadi za mingi juu tufurahie maisha. (Yak. 1:17) Ndoa iko kati ya zile zawadi. Wakati mwanamuke na mwanaume wanaoana, wanafanya naziri kama watapendana na kuheshimiana. Kama bibi na bwana wanaendelea kupendana sana, watakuwa na furaha ya kweli. Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba, mu dunia ya leo bibi na bwana wengi wanasahau naziri yenye walifanya siku yenye walioana. Ile inafanya wasikuwe na furaha. Yehova anapenda bwana atendee bibi yake namna gani? Yehova anaomba bwana waonyeshe bibi zao heshima. Bwana mwenye anaheshimia bibi yake anamutendea kwa upole na kwa upendo.—1 Pe. 3:7. w25.01 8 fu. 1-2; 9 fu. 4-5

Siku ya Tatu, 15 Mwezi wa 7

Yehovaa ni musaidizi wangu; sitaogopa.—Ebr. 13:6.

Ni wazi kama barua ya mutume Paulo kwa Waebrania ilisaidia Wakristo kujitayarisha juu ya mateso yenye walikutana nayo. Paulo alitia moyo ndugu zake wajue na waelewe muzuri zaidi maandiko. Kufanya vile kungewasaidia kutambua na kuepuka mafundisho yenye ingeharibu imani yao. Aliwatia moyo watie nguvu imani yao juu waweze kufuata bila kukawia muongozo wa Yesu na wa ndugu wenye kuongoza katika kutaniko. Alisaidia Wakristo wakuwe na uvumilivu zaidi kwa kuwa na mawazo yenye kufaa juu ya majaribu na waone majaribu kuwa nafasi ya kuzoezwa na Baba yao mwenye upendo. Na siye tunapaswa kutumikisha hii mashauri yenye kuwa mu Biblia. Tukifanya vile tutaweza kuvumilia kwa uaminifu mupaka mwisho.—Ebr. 3:14. w24.09 12-13 fu. 17, 19

Siku ya Ine, 16 Mwezi wa 7

Tumetakaswa kupitia toleo la mwili wa Yesu Kristo mara moja kwa wakati wote.—Ebr. 10:10.

Kulingana na Biblia, bei ya ukombozi ni bei yenye inalipwa ili kufunika zambi na kufanya upatanisho. Kwa Yehova, bei ya ukombozi inafanya iwezekane kurudisha jambo yenye ilipotea. Namna gani? Kumbuka kama, Adamu na Eva walipoteza uzima mukamilifu na tumaini ya kuishi milele. Kwa hiyo, bei ya ukombozi ingekuwa bei yenye kuwa sawasawa na jambo yenye ilipotea. (1 Ti. 2:6) Ingeweza tu kulipwa na mwanaume mwenye kukomaa (1) mwenye alikuwa mukamilifu; (2) mwenye angeweza kuishi milele ku dunia; na (3) mwenye alikuwa tayari kutoa uzima wake kwa ajili yetu. Ona sababu tatu zenye zilifanya Yesu aweze kulipa bei ya ukombozi. (1) Alikuwa mukamilifu, “hakufanya zambi.” (1 Pe. 2:22) (2) Angeweza kuishi milele ku dunia. (3) Alikuwa tayari kufa na kutoa uzima wake kwa ajili yetu.— Ebr. 10:9. w25.02 4 fu. 11-12

Siku ya Tano, 17 Mwezi wa 7

Yeye anatoa roho yake kwa wingi.—Yoh. 3:34.

Yehova anakupenda na anapenda ukuwe mu familia yake. Hata ukuwe mu hali gani yenye inaweza kukuzuia usibatizwe, usisaabu ile jambo. Yesu aliambia hivi kikundi ya banafunzi yake mu karne ya kwanza: “Kama muko na imani yenye ukubwa wa mbegu ya haradali, mutaambia mulima huu, ‘toka hapa uende pale,’ na utatoka, na hakuna jambo lenye litawashinda.” (Mt. 17:20) Benye balikuwa pale wakati Yesu alisema ile maneno balikuwa balishapitisha na Yesu miaka kidogo tu, kwa hiyo imani yao ilikuwa ingali nakomala. Lakini Yesu alibahakikishia kama ikiwa banajikaza kuwa na imani yenye nguvu, Yehova atabasaidia kushinda mambo yenye iko nabazuia kubatizwa, hata kama ile mambo iko sawa milima. Yehova atakusaidia na weye kufanya vile! Kama unatambua mambo yenye iko nakuzuia kubatizwa, kamata hatua ya kuachana na ile mambo bila kukawia. Ujitoe kwa Yehova na kubatizwa. Ule njo uamuzi wa maana sana wenye unaweza kukamata mu maisha! w25.03 6-7 fu. 18-20

Siku ya Posho, 18 Mwezi wa 7

Yehova iko upande wangu; sitaogopa.—Zb. 118:6.

Tutaweza kupambana na magumu yetu ikiwa tunakumbuka kama Mungu mwenye kuishi iko tayari kutusaidia. Kukumbuka mambo yenye Yehova alifanya zamani kunaweza kutusaidia tukuwe hakika kama atatusaidia. (Isa. 37:​17, 33-37) Pia soma habari zenye kuwa ku jw.org zenye kuonyesha namna Yehova ametegemeza ndugu na dada zetu leo. Zaidi ya ile, kumbuka namna Yehova alikusaidia mu maisha yako. Pengine mu maisha yako hamuna jambo ya ajabu. Ile isikuhangaishe. Juu ya nini? Juu, kusema kweli, Yehova amekufanyia mambo mingi. Amekualika ili ukuwe rafiki yake. (Yoh. 6:44) Hauone kama inaweza kuwa muzuri umuombe akusaidie kukumbuka wakati mbalimbali wenye alijibia sala zako? Alikusaidia wakati ulikuwa na lazima kabisa ya musaada wake? Alikutegemeza mu hali fulani ya nguvu? Kufikiria ile mambo kutakusaidia ukuwe hakika zaidi kama Yehova ataendelea kukusaidia. w24.06 21 fu. 8

Siku ya Yenga, 19 Mwezi wa 7

Kifo kilienea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.—Ro. 5:12.

Tumeazimia kuepuka kufanya jambo yoyote yenye itatutenganisha na Yehova. Lakini hatukamilike na ni mwepesi kwetu kuangukia mu jaribu. (Ro. 7:​21-23) Bila kutazamia, tunaweza kujikuta mu hali yenye inaweza kutuongoza kufanya jambo fulani ya mubaya. Ili kubakia washikamanifu kwa Yehova na Mwana wake, tunapaswa kufuata shauri ya Yesu ya kuendelea kuwa waangalifu ili tusiangukie mu jaribu ya kufanya zambi. Siye wote tunajaribiwa kufanya zambi. Lakini kila mumoja wetu iko na uzaifu wake. Inaweza kuwa uzaifu wa kuangukia mu zambi nzito, kuangukia mu mwenendo fulani muchafu, ao kuwa na mawazo ya ulimwengu. Kwa mufano, pengine mutu fulani iko napiganisha jaribu ya kuangukia mu uasherati. Pengine mwingine iko na muelekeo wa kuwa na matendo machafu, sawa vile kugusa-gusa viungo vya uzazi ili kutimiza tamaa ya ngono ao kuangalia pornografia. Pengine mwingine uzaifu wenye iko napiganisha ni kuogopa wanadamu, kutegemea mawazo yake mwenyewe, kukasirika haraka, ao jambo ingine. w24.07 14 fu. 3; 15 fu. 5.

Siku ya Kwanza, 20 Mwezi wa 7

Munapaswa kumusamehe kwa fazili na kumufariji, ili asilemewe na huzuni yenye kupita kiasi.—2 Ko. 2:7.

Wazia namna mambo ingekuwa kama wazee wangekatala kurudisha mu kutaniko ule mwanaume mwenye alitubu, ao kama kisha kumurudisha kutaniko ingekatala kumuonyesha upendo. Ule mwanaume angelemewa na “huzuni yenye kupita kiasi.” Angeona kama hatamutumikiaka Yehova tena. Na hata angeacha kujikaza kurudisha uhusiano wake pamoya na Yehova. Jambo ya mubaya zaidi ni: kama ndugu na dada mu kutaniko wangekatala kusamehe ule mutenda-zambi mwenye alitubu, urafiki wao pamoya na Yehova ungekuwa mu hatari. Juu ya nini? Juu kwa kufanya vile, hawangekuwa naiga Yehova mwenye anakuwaka tayari kusamehe watenda-zambi wenye kutubu, lakini wangekuwa naiga Shetani mwenye hakuwake na huruma na mwenye ni mukali. Wangekuwa sasa vyombo vyenye Shetani anatumikisha juu ya kuharibu hali ya kiroho ya ule mwanaume.—2 Ko. 2:​10, 11; Efe. 4:27. w24.08 17 fu. 7, 10-11

Siku ya Pili, 21 Mwezi wa 7

Wakati alipanda juu . . . , alitoa zawadi katika wanadamu.—Efe. 4:8.

Yesu alipatia kutaniko “zawadi katika wanadamu” wenye wanatumika mu njia ingine. Chini ya muongozo wake, wazee katika Yerusalemu walituma Paulo na Barnaba na wengine wakuwe waangalizi wenye kusafiri. (Mdo. 11:22) Juu ya nini? Sababu ni ileile yenye inafanya watumishi wa huduma na wazee wawekwe: Ili kujenga kutaniko. (Mdo. 15:​40, 41) Waangalizi wa muzunguko hawabakiake tu fasi moya. Waangalizi fulani wanafanya safari za murefu juu ya kutembelea makutaniko. Kila juma mwangalizi wa muzunguko anatoaka hotuba mbalimbali, anafanyaka ziara za uchungaji, anaongozaka mukutano wa mapainia, mukutano wa wazee, na mikutano kwa ajili ya mahubiri. Zaidi ya ile, anatayarishaka hotuba mbalimbali na anapangaka mikusanyiko ya mizunguko na ya eneo. Anafundishaka masomo ya mapainia, anapangaka mukutano wa pekee pamoya na mapainia wa mu muzunguko wake, na anafanyaka mambo ingine. Pia wakati fulani tawi inamuombaka ashugulikie mambo fulani ya haraka. w24.10 21 fu. 12-13

Siku ya Tatu, 22 Mwezi wa 7

Nitasamehe kosa lao, na sitakumbuka tena zambi yao.—Yer. 31:34.

Yehova njo alisema maneno ya mu andiko ya leo yenye Yeremia aliandika. Wakati mutume Paulo alikuwa nazungumuzia ile maneno alitumia maneno yenye kufanana na ile. Alisema hivi: “Sitakumbuka tena zambi zao.” (Ebr. 8:12) Lakini ile inamaanisha nini kabisa? Mu Biblia neno kukumbuka haimaanishake tu kufikiria jambo fulani yenye ilishapita. Lakini inaweza pia kumaanisha kutenda mu njia fulani. Mutenda-zambi mwenye alitundikwa ku muti pembeni ya Yesu alimuomba hivi: “Yesu, unikumbuke wakati utaingia katika Ufalme wako.” (Lu. 23:​42, 43) Ule mutenda-zambi hakukuwa tu naambia Yesu asimusahau, lakini alikuwa namuambia afanye jambo fulani kwa ajili yake. Jibu ya Yesu ilionyesha kama Yesu atafanya jambo fulani, atamufufua. Kwa hiyo, wakati Yehova anasema kama hatakumbuka zambi zetu anamaanisha kama hatatuhukumu wakati wenye kuya kwa sababu ya zambi yenye alishasamehe. w25.02 10-11 fu. 14-15

Siku ya Ine, 23 Mwezi wa 7

Kumujua Mwenye Kuwa Mutakatifu Zaidi ni uelewaji.—Mez. 9:10.

Kujua muzuri sifa za Yehova, kusudi yake na mambo yenye anapenda ao kuchukia, njo uelewaji wa kweli. Ujiulize hivi: ‘Kulingana na mambo yenye ninajua juu ya Yehova, ni uamuzi gani njo ninaweza kukamata wenye utamufurahisha?’ (Efe. 5:17) Juu ya kumufurahisha Yehova, wakati fulani tunalazimika kukamata maamuzi yenye wengine hawafurahie. Kwa mufano, wazazi fulani wenye kuwa na nia ya muzuri wanaweza kukaza mutoto wao aolewe na mwanaume mwenye kuwa na makuta mingi ao mwenye ataleta mali ya mingi hata kama ule mwanaume hana hali ya muzuri ya kiroho. Ni kweli wanapenda mutoto wao asikose kitu kimwili; lakini nani njo atasaidia mutoto wao aendelee muzuri kiroho? Yehova iko na mawazo gani juu ya ile jambo? Matayo 6:33 inaonyesha mawazo ya Yehova. Mu ile andiko, Yesu anashauria Wakristo waendelee “kutafuta kwanza Ufalme.” Ni kweli kama tunapaswa kuheshimia wazazi wetu na watu wa mu eneo yetu, lakini jambo ya maana zaidi kwetu ni kumufurahisha Yehova. w25.01 17 fu. 9-10

Siku ya Tano, 24 Mwezi wa 7

Bwana alisimama karibu yangu na kunitia nguvu.—2 Ti. 4:17.

Leo tuko lazima na musaada wa Yehova juu tuendelee kuhubiri kwa bidii wakati tunapata upinzani. (Ufu. 12:17) Juu ya nini unapaswa kuwa hakika kama Yehova atakutegemeza? Fikiria sala yenye Yesu alitoa yenye kuwa mu Yohana sura ya 17. Yesu alimuomba Yehova alinde mitume wake, na Yehova alijibia ile sala. Kitabu ya Matendo iko na habari ya namna Yehova alisaidia mitume wahubiri kwa bidii hata wakati waliteswa. Mu ile sala, Yesu alimuomba pia Yehova alinde bote benye batakubali mahubiri ya mitume. Ni kusema akulinde na weye. Yehova anaendelea kujibia ile sala ya Yesu; atakusaidia sawa vile alisaidia mitume. (Yoh. 17:​11, 15, 20) Kadiri mwisho unakaribia, inawezekana itakuwa nguvu kwetu kuhubiri habari njema kwa bidii. Lakini tukuwe hakika kama Yehova atatutegemeza.—Lu. 21:​12-15. w25.03 18 fu. 13-14

Siku ya Posho, 25 Mwezi wa 7

Watumishi wangu watapiga vigelegele vya shangwe.—Isa. 65:14.

Watu wa Mungu ‘wanapiga vigelegele vya shangwe’ juu moyo wao unajaa shukrani. Kweli zenye kujenga, ahadi zenye kufariji zenye kuwa mu Neno ya Mungu, na tumaini yetu yenye nguvu yenye kutegemea zabihu ya ukombozi ya Yesu Kristo, vinafanya tukuwe na “hali ya muzuri ya moyo.” Kuzungumuzia ile mambo kunafanya tukuwe na furaha ya kweli! (Zb. 34:8; 133:​1-3) Upendo na umoja kati ya watu wa Yehova ni mambo mbili ya maana sana yenye kuwa mu paradiso ya kiroho. ‘Kifungo cha umoja’ chenye kuwa kati yetu kinatusaidia kuwazia namna maisha itakuwa mu dunia mupya, wakati watumishi wa Yehova watakuwa na umoja na upendo mwingi sana kupita leo. (Kol. 3:14) Mutu yeyote mwenye anapenda kuwa na furaha ya kweli na kuwa mwenye kutosheka, anapaswa kuingia mu paradiso yetu ya kiroho. Hata watu wa mu hii dunia wakuwe na mawazo gani juu ya watumishi wa Yehova, watu wa Yehova wamejifanyia jina ya muzuri pamoja na Yehova na pamoja na wote wenye kumuabudu.—Isa. 65:15. w24.04 21 fu. 7-8

Siku ya Yenga, 26 Mwezi wa 7

Muendelee. . . kujengana.—1 Te. 5:11.

Namna gani tunaweza kutegemeza Wakristo wenye wanapenda kufunga ndoa? Njia moya ya kufanya vile ni kuwa waangalifu juu ya mambo yenye tunasema. (Efe. 4:29) Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Nafanyaka mizaha yenye inaweza kuumiza wenye wanapenda kufunga ndoa? Wakati ninaona ndugu mwenye hayaoa na dada mwenye hayaolewa wako nazungumuza, nawazaka kama wanapendana?’ (1 Ti. 5:13) Hatupaswe kufanya ndugu ao dada ajisikie kuwa anakosa jambo fulani juu tu hayaoa ao kuolewa. Inaweza kuwa muzuri kama tunatafuta nafasi ya kupongeza ndugu na dada wenye hawayafunga ndoa! Sasa tutafanya nini kama tunawaza kama inaweza kuwa muzuri ndugu na dada fulani waoane? Biblia inatuambia tufikirie mawazo ya wengine. (Ro. 15:2) Wakristo wengi wenye hawayafunga ndoa hawapendake wengine wawapendekeze kwa ndugu ao dada fulani mwenye anaweza kuwa bibi ao bwana yao, na tunapaswa kuheshimia uamuzi wao. (2 Te. 3:11) Wengine wanaweza kufurahi kama tunawasaidia, lakini hatupaswe kufanya vile kama hawatuombe tuwasaidie.—Mez. 3:27. w24.05 24-25 fu. 14-15

Siku ya Kwanza, 27 Mwezi wa 7

Mwamba wao haiko kama Mwamba wetu.—Kum. 32:31.

Mu hii dunia, magumu yenye haitazamiwe inaweza kuvuruga ao hata kubadilisha kabisa maisha yetu. Lakini tunafurahi juu tunajua kama Yehova iko pale juu ya kutusaidia! Wakati anatutegemeza, ile inatusaidia tukuwe hakika kama “ni mwenye kuishi.” (Zb. 18:46) Lakini, kisha tu kusema ile maneno, Daudi alimuita Mungu kuwa “Mwamba wangu.” Juu ya nini Daudi alimufananisha Yehova, na mwamba, kitu yenye haina uzima? Biblia inatumia neno “mwamba” ili kutusaidia kuelewa sifa zenye Yehova iko nazo. Mara mingi ile neno inatumiwa mu maandiko yenye watumishi wa Yehova wanamusifu kwa sababu ya sifa za ajabu zenye iko nazo. Mu andiko ya Kumbukumbu la Torati 32:4 njo Yehova anaitwa kwa mara ya kwanza “Mwamba.” Mu sala yenye Hana alitoa, alisema kama “hakuna mwamba kama Mungu wetu.” (1 Sa. 2:2) Habakuki alimuita Yehova “Mwamba wangu.” (Hab. 1:12) Muandikaji wa Zaburi 73 alimuita Mungu “mwamba wa moyo wangu.” (Zb. 73: 26) Na hata Yehova mwenyewe alijiita kuwa mwamba.—Isa. 44:8. w24.06 26 fu. 1, 3

Siku ya Pili, 28 Mwezi wa 7

Yehoshafati . . . alitafuta Yehova kwa moyo wake wote.—2 Ny. 22:9.

Wafalme wa Israeli wenye walimufurahisha Yehova walimuabudu kwa moyo wote. Biblia inasema hivi juu ya Yosia: “Hakuna mufalme mwenye alikuwa kama yeye, mwenye alimurudilia Yehova kwa moyo wake wote.” (2 Fa. 23:25) Halafu Sulemani, mwenye ku mwisho wa maisha yake alifanya mambo ya mubaya? Biblia inasema hivi juu yake: “Moyo wake haukukuwa kamili.” (1 Fa. 11:4) Na kuhusu Abiyamu, mufalme mwingine mubaya, Biblia inasema hivi: “Moyo wake haukukuwa kamili kumuelekea Yehova.” (1 Fa. 15:3) Mara mingi Biblia inatumia neno “moyo” ili kuzungumuzia mutu wa ndani, ni kusema tamaa, mawazo, muelekeo, mutazamo, uwezo, nia, na miradi ya mutu. Sasa, kumutumikia Yehova kwa moyo wote maana yake nini? Mutu mwenye anamutumikia Mungu kwa moyo wote hamuabudu juu tu anajua kama ile njo jambo yenye anapaswa kufanya. Lakini anamutumikia kwa sababu anamupenda na anapenda kujitoa kabisa kwake mu maisha yake yote. w24.07 21 fu. 4-5

Siku ya Tatu, 29 Mwezi wa 7

Ufutilie mbali makosa yangu yote.—Zb. 51:9.

Yehova anatumia maneno ya mufano ili kuonyesha namna anafuta zambi zetu. Anasema hivi: “Nitafuta makosa yako kama kwa wingu na zambi zako kama kwa wingu nzito.” (Isa. 44:22) Wakati Yehova anasamehe ni sawa vile anatumia wingu nzito ili kufunika makosa yetu juu isionekane hata kidogo. Tunajifunza nini? Wakati Yehova anasamehe zambi zetu, hatupaswe kuendelea kujihukumu mu maisha yetu yote juu ya zile zambi. Kupitia damu ya Yesu Kristo, zambi zetu zinasamehewa kabisa-kabisa. Ni sawa vile hatuyafanyaka zambi hata siku moya. Wakati tunatubu ni vile njo Yehova anatusamehe. Musamaha wa Yehova unaturuhusu pia tukukuwe tena na urafiki wa muzuri pamoya naye. Ile inatusaidia tusiendelee kujihukumu. w25.02 10 fu. 11-14

Siku ya Ine, 30 Mwezi wa 7

Mungu kwa fazili zake anajaribu kukuongoza kwenye toba.—Ro. 2:4.

Yehova anaomba wazee walinde kutaniko juu iendelee kuwa safi. (1 Ko. 5:7) Lakini wazee wanafanya pia yao yote juu ya kusaidia mukosaji atubu wakati inawezekana. Njo maana wakati wazee wako nasaidia mukosaji wanatumainia kama atabadilika. Juu ya nini? Juu wanapenda kumuiga Yehova mwenye “upendo mwingi sana na mwenye rehema.” (Yak. 5:11) Ona namna mutume Yohana alionyesha kama anamuiga Yehova. Aliandika hivi: “Watoto wangu wadogo, ninawaandikia ninyi mambo haya ili musifanye zambi. Lakini, kama mutu yeyote anafanya zambi, tuko na musaidizi kwa Baba, Yesu Kristo, mwenye haki.” (1 Yo. 2:1) Jambo ya kuhuzunisha ni kama, wakati fulani Mukristo anaweza kukatala kutubu. Na kama ni vile anapaswa kuondolewa mu kutaniko. w24.08 25 fu. 19-20

Siku ya Tano, 31 Mwezi wa 7

Musimame imara katika imani.—1 Ko. 16:13.

Pengine umeanza kujilinganisha na bengine. Uepuke kufanya vile. Juu ya nini? Juu Yehova hatulinganishake na bengine. (Gal. 6:4) Kwa mufano, Maria alimutolea Yesu zawadi ya mafuta yenye marashi ya bei sana. (Yoh. 12:​3-5) Lakini mujane maskini alitoa ku hekalu feza mbili za kidogo zenye zilikuwa na samani ya kidogo sana. (Lu. 21:​1-4) Lakini, Yesu aliona kama wale wanamuke wote wawili walionyesha imani. Yehova Baba yake anafurahia kila kitu yenye unafanya juu umejitoa kwake na unamupenda, hata kama weye unaona ni ya kidogo sana. Wakati fulani siye wote tunakuwaka na mashaka. Lakini, Biblia Neno ya Mungu yenye kutegemeka na yenye haiseme uongo inaweza kutusaidia kupiganisha ile mashaka juu isituvunje moyo. Kwa kweli, Yehova anakujua weye kipekee. Anaona mambo yote yenye ulijiima juu ya kumutumikia na anaahidi kukubariki. Anaona batumishi yake bote baaminifu kuwa ba maana, anabapenda, na kubahangaikia. w24.10 25 fu. 3; 29 fu. 17-18

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine