Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • es26 uku. 57-67
  • Mwezi wa 6

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mwezi wa 6
  • Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
  • Vichwa Vidogo
  • Siku ya Kwanza, 1 Mwezi wa 6
  • Siku ya Pili, 2 Mwezi wa 6
  • Siku ya Tatu, 3 Mwezi wa 6
  • Siku ya Ine, 4 Mwezi wa 6
  • Siku ya Tano, 5 Mwezi wa 6
  • Siku ya Posho, 6 Mwezi wa 6
  • Siku ya Yenga, 7 Mwezi wa 6
  • Siku ya Kwanza, 8 Mwezi wa 6
  • Siku ya Pili, 9 Mwezi wa 6
  • Siku ya Tatu, 10 Mwezi wa 6
  • Siku ya Ine, 11 Mwezi wa 6
  • Siku ya Tano, 12 Mwezi wa 6
  • Siku ya Posho, 13 Mwezi wa 6
  • Siku ya Yenga, 14 Mwezi wa 6
  • Siku ya Kwanza, 15 Mwezi wa 6
  • Siku ya Pili, 16 Mwezi wa 6
  • Siku ya Tatu, 17 Mwezi wa 6
  • Siku ya Ine, 18 Mwezi wa 6
  • Siku ya Tano, 19 Mwezi wa 6
  • Siku ya Posho, 20 Mwezi wa 6
  • Siku ya Yenga, 21 Mwezi wa 6
  • Siku ya Kwanza, 22 Mwezi wa 6
  • Siku ya Pili, 23 Mwezi wa 6
  • Siku ya Tatu, 24 Mwezi wa 6
  • Siku ya Ine, 25 Mwezi wa 6
  • Siku ya Tano, 26 Mwezi wa 6
  • Siku ya Posho, 27 Mwezi wa 6
  • Siku ya Yenga, 28 Mwezi wa 6
  • Siku ya Kwanza, 29 Mwezi wa 6
  • Siku ya Pili, 30 Mwezi wa 6
Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
es26 uku. 57-67

Mwezi wa 6

Siku ya Kwanza, 1 Mwezi wa 6

Kwa maana wewe, Ee Yehova, uko mwema na uko tayari kusamehe.—Zb. 86:5.

Hata leo, bei ya ukombozi yenye Yesu alitoa iko natuletea faida. Kwa mufano, kupitia bei ya ukombozi, Yehova anasamehe zambi zetu. Halazimike kutusamehe, lakini anapenda kufanya vile. (Zb. 103:​3, 10-13) Watu fulani wanaweza kuona kama hawastahili musamaha wa Yehova. Kusema kweli, siye wote hatustahili musamaha wake. Mutume Paulo alielewa kama ‘hastahili kuitwa mutume.’ Hata vile, alisema hivi: “Kwa fazili zenye hazistahiliwe za Mungu mimi niko kile niko.” (1 Ko. 15:​9, 10) Wakati tunatubu zambi zetu, Yehova anatusamehe. Juu ya nini? Haiko juu tunastahili musamaha wake, lakini juu anatupenda. Kama uko nahangaika juu unawaza kama haustahili, kumbuka kama Yehova alitoa bei ya ukombozi kwa ajili ya watenda-zambi wenye kutubu, hapana kwa ajili ya watu wenye hawana zambi—Lu. 5:32; 1 Ti. 1:15. w25.01 27 fu. 3-4

Siku ya Pili, 2 Mwezi wa 6

Mutu mwenye fazili anajiletea faida, lakini mutu mwenye hana huruma anajiletea shida.—Mez. 11:17.

Hatuna uwezo juu ya mambo yenye watu wengine wanasema na kufanya. Lakini tunaweza kuamua namna tutatenda. Na mara mingi namna ya muzuri ya kutenda ni kusamehe. Juu ya nini? Juu tunamupenda Yehova na juu anapenda tusamehe. Kama tunabakia wenye kukasirika na hatupendi kusamehe, tunaweza kutenda bila kufikiri na pengine ile inaweza kutuletea magumu ya kimwili. (Mez. 14:​17, 29, 30) Wakati tunaacha kukasirika, tunalinda moyo wetu usiendelee kuumia. Na tunajipatia nafasi ya kuendelea kufurahia maisha. Jambo moya ya kufanya ni kujipatia wakati wa kupona. Kisha kupata matunzo, mutu mwenye aliumia sana iko na lazima ya wakati ili apone. Vilevile tunaweza kuwa na lazima ya wakati ili kupona maumivu ya mu moyo mbele tukuwe tayari kusamehe kwa moyo wote mutu mwenye alituumiza. (Muh. 3:3; 1 Pe. 1:22) Usali, omba Yehova akusaidie juu uweze kusamehe. w25.02 15-16 fu. 8-11

Siku ya Tatu, 3 Mwezi wa 6

Chakula kigumu ni cha watu wakomavu.—Ebr. 5:14.

Mafundisho ya musingi inatia ndani fundisho kuhusu kutubu, imani, ubatizo, na ufufuo. (Ebr. 6:​1, 2) Ile mafundisho ni musingi wa Ukristo. Njo maana mutume Petro aliizungumuzia wakati alikuwa nahubiria watu wengi siku ya Pentekoste. (Mdo. 2:​32-35, 38) Ili tukuwe wanafunzi wa Kristo, tunapaswa kukubali ile mafundisho ya musingi. Kwa mufano, mutume Paulo alionya kama mutu yeyote mwenye anakataa fundisho ya ufufuo, anakana imani yote ya Ukristo. (1 Ko. 15:​12-14) Lakini, hatupaswe tu kuishia ku kweli za musingi za Biblia. Tofauti na mafundisho ya musingi, chakula kigumu kinatia ndani kanuni za Yehova, hapana tu sheria zake. Zile kanuni zinatusaidia kuelewa mawazo ya Yehova. Juu tufaidike na ile chakula ya kiroho, tunapaswa kujifunza, kutafakari, na kutumikisha kwa uangalifu mambo yenye tunajifunza mu Neno ya Mungu. Wakati tunafanya vile, tunajizoeza kukamata maamuzi yenye inamufurahisha Yehova. w24.04 5 fu. 12-13

Siku ya Ine, 4 Mwezi wa 6

Watu wa Ninawi watasimama katika hukumu.—Mt. 12:41.

Mungu alimukumbusha Yona kama watu wa Ninawi “hawajue hata kufanya tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa.” (Yon. 1:​1, 2; 3:10; 4:​9-11) Miaka mingi kisha pale, Yesu alitumia mufano wa watu wa Ninawi ili kufundisha watu juu ya haki na rehema ya Yehova. Watu wa Ninawi “watasimama” katika “hukumu” gani? Yesu alifundisha kama kutakuwa “ufufuo wa hukumu.” (Yoh. 5:29) Yesu alikuwa nazungumuzia miaka 1000 ya utawala wake, wakati “wenye haki na wenye hawako wenye haki” watafufuliwa. (Mdo. 24:15) Kwa wale wenye hawako wenye haki, ule ufufuo utakuwa “ufufuo wa hukumu,” ni kusema, Yehova na Yesu wataangalia na kuchunguza mwenendo wao ili kuona ikiwa wako natumikisha mambo yenye wako nafundishwa. Ikiwa Muninawi mwenye alifufuliwa anakataa kujiunga na ibada safi, hukumu yake itakuwa uharibifu. (Isa. 65:20) Lakini wote wenye watachagua kumuabudu Yehova kwa uaminifu, hukumu yao itakuwa ya muzuri, ni kusema watakuwa na tumaini ya kuishi milele!—Da. 12:2. w24.05 5 fu. 13-14

Siku ya Tano, 5 Mwezi wa 6

Mwana wa binadamu alikuja kutafuta na kuokoa wale wenye walipotea.—Lu. 19:10.

Yesu alionyesha kwa ukamili rehema ya Baba yake. (Yoh. 14:9) Kupitia maneno na matendo yake, alionyesha kama Baba yake mwenye huruma na rehema anapenda watu na anapenda kusaidia kila mutu apiganishe zambi. Yesu alisaidia watenda-zambi wenye walipenda kubadilika na kumufuata. (Lu. 5:​27, 28) Yesu alijua mambo yenye ingemufikia. Zaidi ya mara moya, aliambia wanafunzi wake kama atasalitiwa na kuuawa ku muti. (Mt. 17:22; 20:​18, 19) Alijua kama zabihu yake ingetosha zambi ya ulimwengu. Yesu alifundisha pia kama kisha kutoa uzima wake, ‘atavuta kwake watu wa namna zote.’ (Yoh. 12:32) Kama wanadamu wenye zambi wangemukubali Yesu kuwa Bwana wao na kutii amri zake, wangemufurahisha Yehova. Ile ingefanya ku mwisho ‘wawekwe huru kutoka katika zambi.’ (Ro. 6:​14, 18, 22; Yoh. 8:32) Kwa hiyo, kwa kupenda na kwa uhodari Yesu alikubali kufa kifo ya maumivu sana.—Yoh. 10:​17, 18. w24.08 5 fu. 11-12

Siku ya Posho, 6 Mwezi wa 6

Katika mataifa yote, lazima habari njema ihubiriwe kwanza.—Mk. 13:10.

Kumbuka namna ulijisikia wakati ulijifunza kwa mara ya kwanza kweli za Biblia. Ulijifunza kama Baba yako wa mbinguni anakupenda, anapenda ukuwe mu familia ya waabudu wake, anaahidi kumaliza maumivu na mateso, na kama anakupatia tumaini ya kuonana tena na wapendwa wako wenye wamekufa; na ulijifunza mambo ingine ya mingi. (Mk. 10:​29, 30; Yoh. 5:​28, 29; Ro. 8:​38, 39; Ufu. 21:​3, 4) Ile mafundisho ya Biblia ilikufurahisha sana. (Lu. 24:32) Ulipenda sana mambo yenye ulikuwa najifunza, na ulipenda kabisa kuielezea wengine! (Linganisha na Yeremia 20:9) Wakati tunapenda sana kweli za Biblia na zinatia mizizi mu moyo wetu, hatuwezi kujizuia kuzielezea wengine. (Lu. 6:45) Tunajisikia sawa wanafunzi wa Yesu wa karne ya kwanza wenye walisema: “Hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yenye tumeona na kusikia.” (Mdo. 4:20) Tunapenda sana kweli ya Biblia, njo maana tunapenda kuielezea watu wengi kadiri inawezekana. w24.05 15 fu. 5; 16 fu. 7

Siku ya Yenga, 7 Mwezi wa 6

Mumutumikie Yehova kwa furaha.—Zb. 100:2.

Siye watu wa Yehova, tunahubiria wengine kwa sababu tunamupenda Baba yetu wa mbinguni na tunapenda kusaidia majirani wetu wafikie kumujua. Lakini ni nguvu kwa wengine kufurahia kazi ya kuhubiri. Juu ya nini? Wahubiri fulani ni watu wa haya na hawajitumainie. Wengine hawajisikie huru kuenda ku nyumba za watu bila kualikwa. Wengine wanaogopa kama watu watawakasirikia. Pengine wengine walifundishwa kuepuka mambo yenye inaweza kukasirisha watu. Inakuwaka nguvu kwa wale ndugu na dada kuhubiria watu wenye hawajue. Ni nguvu kwako kufurahia kazi ya kuhubiri kwa sababu ya mambo kama ile? Kama ni vile, usivunjike moyo. Kukosa kujitumainia kunaonyesha kama uko munyenyekevu na haupendi watu wakukazie uangalifu. Kunaonyesha pia kama unapenda kuepuka mabishano. Tena hakuna mwenye anapendaka wengine wamukasirikie, zaidi sana wakati iko najikaza kuwafanyia mambo ya muzuri. Baba yako wa mbinguni anajua ile matatizo yote yenye uko napambana nayo na anapenda kukupatia musaada wenye uko nao lazima.—Isa. 41:13. w24.04 14 fu. 1-2

Siku ya Kwanza, 8 Mwezi wa 6

Wenye kiasi wako na hekima.—Mez. 11:2.

Wakati uko nasoma Biblia, kuliko kujaribu kutumikisha mara moya mambo yote yenye umesoma, jaribu kwanza kutumikisha jambo moya ao mbili. Unaweza kufanya hivi: Kwanza fanya liste ya mambo yote yenye unapaswa kufanyia kazi. Kisha chagula jambo moya ao mbili yenye utatumikia kwanza; na mambo ingine yote yenye inabakia, utaendelea kuitumikia polepole. Utaanza na ya wapi? Unaweza kuanza kutumikia muradi wenye ni mwepesi kwako kufikia. Ao unaweza kuamua kutumikia jambo yenye unaona kama ni lazima kabisa ufanyie maendeleo. Wakati unaamua jambo yenye utatumikia kwanza, ufanye utafiti mu vichapo vyetu. Sali juu ya muradi wako, umuombe Yehova akupatie “hamu na pia nguvu za kutenda.” (Flp. 2:13) Kisha, utumikishe mambo yenye umejifunza. Kisha kufanyia kazi muradi wako wa kwanza, utakuwa na hamu sana ya kutumikia muradi ingine. Kwa kweli, wakati unafanya maendeleo mu jambo fulani yenye kuhusu maisha yako ya Kikristo ao unajikaza kukomalisha sifa fulani ya Kikristo, utaona kama inakuwa mwepesi zaidi kufanya maendeleo mu mambo ingine. w24.09 6 fu. 13-14

Siku ya Pili, 9 Mwezi wa 6

Katika kila njia mulijionyesha kuwa safi juu ya jambo hili.—2 Ko. 7:11.

Unaweza kujisikia mubaya juu ya matendo yako ya zamani yenye iliumiza bengine. Nini njo inaweza kukusaidia? Fanya yote yenye unaweza juu ya kutengeneza mambo, uombe musamaha na uonyeshe kupitia matendo yako kama unahuzunika. Umuombe Yehova asaidie bale benye matendo yako iliumiza. Yehova anaweza kukusaidia weye na benye uliumiza juu nyie bote muweze kuvumilia na kuwa tena na amani. Makosa yako ya zamani ikufundishe na uache Yehova akutumikishe mu njia yoyote yenye anataka. Fikiria mufano wa nabii Yona. Kuliko kuenda Ninawi vile Mungu alimuambia, Yona alikimbia na kuenda fasi ingine. Yehova alimurekebisha, na Yona alijifunza kupitia makosa yake. (Yon. 1:​1-4, 15-17; 2:​7-10) Lakini Yehova hakuacha kumutumikisha nabii wake Yona. Alimupatia nafasi ingine ya kuenda Ninawi, na Yona alitii bila kukawia. Hakuacha huzuni juu ya makosa yake ya zamani imuzuie kuitika ile mugao yenye Yehova alimupatia.—Yon. 3:​1-3. w24.10 8-9 fu. 10-11

Siku ya Tatu, 10 Mwezi wa 6

Kwa hiyo, mutubu na mugeuke ili zambi zenu zipate kufutwa, ili vipindi vya kutuliza vikuje kutoka kwa Yehova mwenyewe.—Mdo. 3:19.

Yehova hatie tu alama ya kuonyesha kama hahesabie tena madeni ao zambi zetu; anazivuta kabisa. Wakati mutu hahesabie tena deni anaweza kutia hii alama X. Hata kama mutu anatia ile alama, hesabu ya deni inaweza kuendelea kuonekana. Lakini kufuta kitu ni tofauti. Ili kuelewa muzuri ile maneno tukumbuke kama ilikuwa mwepesi kufuta maandishi ya zamani. Mutu angeweza tu kubeba nguo yenye kuwa na mayi na kupanguza maandishi. Kwa hiyo wakati deni ilifutwa ilipotea kabisa-kabisa. Haingewezekana tena kuona mambo yenye ilikuwa imeandikwa, ni sawa vile deni haikukuwaka hata siku moya. Inatia moyo sana kujua kama Yehova hatie tu alama ya kuonyesha kama hahesabie tena zambi yetu, lakini anaifuta kabisa-kabisa!—Zb. 51:9. w25.02 10 fu. 11

Siku ya Ine, 11 Mwezi wa 6

Usikasirike na kuanza kutenda uovu.—Zb. 37:8.

Wakati bengine banatuwazia mubaya ao kututendea mubaya, tunapaswa kuwa hakika kama Yehova anajua kweli yote. Kuwa hakika na ile jambo kunaweza kutusaidia juu tunajua kama ku mwisho Yehova atashugulikia mambo. Kama tunaacha mambo mu mikono ya Yehova hatutaendelea kukasirika ao kuwa na chuki mu moyo wetu. Kujisikia vile kunaweza kufanya tutende jambo fulani ya mubaya, tupoteze furaha yetu, na kunaweza kuharibu uhusiano wetu pamoya na Yehova. Kusema kweli, hatuwezi kuiga mufano wa Yesu kwa ukamili. Wakati fulani, tunaweza kufanya ao kusema jambo yenye tutahuzunikia kisha. (Yak. 3:2) Matendo fulani ya ukosefu wa haki inaweza kufanya tuendelee kuwa na maumivu ya kimwili ao ya mu moyo yenye kuwa nguvu kuvumilia. Kama na weye uko mu ile hali, ukuwe hakika kama Yehova anajua maumivu yako. Yesu pia alitendewa bila haki, kwa hiyo anaweza kuelewa namna uko najisikia. (Ebr. 4:​15, 16) Tunafurahi sana juu Yehova anatupatia mashauri yenye inaweza kutusaidia kujua mambo ya kufanya wakati banatutendea bila haki. w24.11 6 fu. 12-13

Siku ya Tano, 12 Mwezi wa 6

Hii ndiyo kazi ya Mungu, kwamba ninyi muamini ule mwenye huyo alimutuma.—Yoh. 6:29.

Juu mutu apate “uzima wa milele” anapaswa kuamini Yesu. (Yoh. 3:​16-18, 36; 17:3) Wayahudi wengi hawakukubali mafundisho ya Yesu kuhusu “kazi ya Mungu” ya mupya. Walimuuliza hivi Yesu: “Unafanya alama gani, ili tuione na tukuamini? Ni kazi gani yenye unafanya?” (Yoh. 6:30) Walisema kama mu siku za Musa mababu zao walipokea mana, yenye ilikuwa sawa mukate. (Neh. 9:15; Zb. 78:​24, 25) Ni wazi kama, walikuwa tu wangali nafikiria mukate ya kukula. Na wakati Yesu alizungumuzia “mukate wa kweli kutoka mbinguni” yenye, tofauti na mana, inaleta uzima wa milele, hawakumuuliza anapenda kumaanisha nini. (Yoh. 6:32) Walihangaikia sana mahitaji yao ya kimwili mupaka wakazarau mafundisho ya maana yenye Yesu alipenda kuwafundisha. w24.12 5-6 fu. 10-11

Siku ya Posho, 13 Mwezi wa 6

Ule mwenye alijenga vitu vyote ni Mungu.—Ebr. 3:4.

Wakati wa kujifunza sayansi ku masomo, pengine mutoto wako atajifunza kama vitu mingi mu ulimwengu vinafuataka sheria ao mupangilio fulani. Kwa mufano, miti mingi inafuataka mupangilio fulani wakati iko nakomala. Kunakuwaka shina, kisha ile shina inatokeza matawi yenye inaifanana, kisha matawi nayo inatokeza matawi ingine ya kidogo-kidogo yenye inaifanana. Kuko vitu vingine vyenye kuwa mu ulimwengu vyenye vinafuataka pia ile mupangilio. Lakini, nani njo alifanya sheria zenye zinafanya vitu mbalimbali vifuate mupangilio fulani? Nani njo aliumba ile mupangilio? Kama mutoto wako anazoea kufikiria mambo ya ajabu yenye iko mu ulimwengu, inawezekana ile itamusaidia aamini kabisa kama Mungu njo aliumba vitu vyote. Wakati fulani, unaweza kuuliza mutoto wako hivi: “kama Mungu njo alituumba, hauone kama ni yeye njo anapaswa kujua muzuri zaidi kanuni zenye tunapaswa kufuata mu maisha juu tukuwe na furaha?” Kisha unaweza kumuambia kama zile kanuni zenye zinaweza kutusaidia mu maisha zinapatikana mu Biblia. w24.12 16 fu. 8.

Siku ya Yenga, 14 Mwezi wa 6

Kuko uasherati katikati yenu, tena uasherati wenye haujatokea hata kati ya watu wa mataifa—wa mwanaume mumoja mwenye anaishi na bibi ya baba yake.—1 Ko. 5:1.

Kwa muongozo wa roho ya Mungu, mutume Paulo aliandika barua, na mu ile barua alionyesha kama mutenda-zambi mwenye hakutubu, alipaswa kuondolewa mu kutaniko.(1 Ko. 5:13) Wakristo waaminifu walipaswa kumutendea namna gani? Paulo aliwaambia hivi: “Muache kushirikiana” pamoya naye. Maana yake nini? Paulo alifasiria kama ile ilimaanisha kama hawakupaswa ‘hata kula chakula pamoja na mutu wa namna hiyo.’ (1 Ko. 5:11) Kwa kawaida, saa ya kula njo batu banaongeaka, na ile inaweza kufanya baanze kupitisha wakati pamoya. Mambo iko wazi, Paulo alimaanisha kama kutaniko haikupaswa kupitisha wakati na ule mwanaume. Ile ingelinda kutaniko juu tabia yake isiambukie bengine. (1 Ko. 5:​5-7) Zaidi ya ile, kuepuka kuwa karibu na ule mwanaume kungemusaidia aelewe kama alifanya mambo yenye ilimuumiza sana Yehova, kisha angehuzunika, na ile ingemuchochea atubu. w24.08 15 fu. 4-5

Siku ya Kwanza, 15 Mwezi wa 6

Mungu alipenda ulimwengu sana na hivyo akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee.—Yoh. 3:16.

Ili Waisraeli wakuwe na uhusiano muzuri pamoya naye, Yehova aliweka mupango wenye ungetumiwa kwa wakati fulani, wenye ungefanya zambi zao zisamehewe. Mara moya ku mwaka, mu Israeli ya zamani, kulikuwa siku ya kufunika zambi. Ile siku, kuhani mukubwa angetoa zabihu za wanyama kwa ajili ya watu. Ni kweli kama, zabihu za wanyama hazingefunika kabisa-kabisa zambi za mutu yeyote juu wanyama ni wa hali ya chini kupita wanadamu. Lakini wakati Waisraeli wenye kutubu walikuwa natoa zabihu zenye Yehova aliwaomba, Yehova alikuwa tayari kusamehe zambi zao. (Ebr. 10:​1-4) Ule mupango uliwakumbusha kama walikuwa watenda-zambi. Lakini Yehova alikuwa alishafikiria mupango wenye ungefanya zambi zisamehewe lote. Alifanya mupango ili Mwana wake mupendwa ‘atolewe mara moja kwa wakati wote ili kubeba zambi za watu wengi.’ (Ebr. 9:28) Yesu alitoa “uzima wake kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi.”— Mt. 20:28. w25.02 4 fu. 9-10

Siku ya Pili, 16 Mwezi wa 6

Muendelee kukesha na kusali bila kuacha, ili musiingie katika jaribu.—Mt. 26:41.

“Roho inataka lakini mwili ni muzaifu.” (Mt. 26:41b) Kupitia ile maneno, Yesu alionyesha kama alielewa hali yetu ya kutokamilika. Lakini maneno yake iko pia na onyo fulani: Tuepuke kujitumainia sana. Uleule usiku, wanafunzi walisema kwa uhakika kama wataendelea kushikamana na mwalimu wao. (Mt. 26:35) Walikuwa na nia ya muzuri. Lakini hawakutambua kama ingekuwa mwepesi kwao kukosa nguvu wakati wa jaribu. Njo maana Yesu aliwaonya na maneno yenye kuwa mu andiko ya leo. Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba wanafunzi hawakuendelea kukesha. Wakati Yesu alikamatwa, je, walishikamana naye ao waliangukia mu jaribu na kukimbia? Juu hawakukuwa waangalifu, wanafunzi walifanya jambo yenye walisema kama hawatafanyaka: Walimuacha Yesu.—Mt. 26:56. w24.07 14 fu. 1-2

Siku ya Tatu, 17 Mwezi wa 6

Tulipatanishwa na Mungu kupitia kifo cha Mwana wake.—Ro. 5:10.

Adamu na Eva walipoteza uhusiano muzuri pamoya na Baba yao, Yehova. Ku mwanzo, walikuwa mu familia ya Mungu. (Lu. 3:38) Lakini wakati walikosa kumutii Yehova, walifukuzwa mu ile familia mbele wakuwe na watoto. (Mwa. 3:​23, 24; 4:1) Juu tuko watoto wao, tuko na lazima ya kupatanishwa na Yehova. (Ro. 5:​10, 11) Mu maneno ingine, tuko na lazima ya kuwa na uhusiano wa muzuri pamoya na Yehova. Kulingana na kitabu fulani, neno ya Kigiriki yenye inatumiwa hapa ili kuzungumuzia “kupatanisha” inaweza kumaanisha “kufanya adui kuwa rafiki.” Inagusa moyo kujua kama Yehova njo alikamata hatua ya kwanza juu ya kufanya ile iwezekane. Alifanya vile namna gani? Alifanya vile kupitia mupango wa kufunika zambi, wenye aliweka ili akuwe tena na uhusiano muzuri pamoya na wanadamu wenye zambi. Juu ile iwezekane inaomba kubadilisha kitu moya na kitu ingine yenye kuwa na samani ileile. Kwa kufanya vile, kitu ingine inaweza kukamata nafasi ya kitu yenye ilipotea ao yenye iliharibiwa. w25.02 3-4 fu. 7-8

Siku ya Ine, 18 Mwezi wa 6

Huzuni kwa njia yenye kupatana na mapenzi ya Mungu kunatokeza toba yenye kuongoza kwenye wokovu.—2 Ko. 7:10.

Mutume Paulo alisema kama “kemeo lenye linatolewa na wenye kuwa wengi linatosha kwa mutu wa namna hiyo.” (2 Ko. 2:​5-8) Mu maneno ingine, ni kusema nizamu ilitimiza kusudi yake juu ya ule mwanaume mwenye alikuwa amefanya ngono na bibi ya baba yake. (Ebr. 12:11) Kwa hiyo, Paulo aliambia kutaniko hivi: “Munapaswa kumusamehe kwa fazili na kumufariji” ule ndugu mwenye alikuwa amekosea, na “mumuhakikishie upendo wenu.” Ona kama Paulo hakuomba tu kutaniko imukubali tena kati ya watu wa Mungu, lakini ilipaswa kufanya mambo mingi zaidi. Paulo alipenda ndugu na dada wahakikishie ule mwanaume mwenye alitubu, kupitia maneno na matendo yao, kama wamemusamehe kabisa na wanamupenda. Kwa kufanya vile, wangeonyesha wazi kama wanamukaribisha tena mu kutaniko. w24.08 15 fu. 4; 16-17 fu. 6-8

Siku ya Tano, 19 Mwezi wa 6

Mulifunuliwa mbele ya watu wote kwa lawama na pia taabu.—Ebr. 10:33.

Mutume Paulo alijua muzuri mambo yenye mutu anapaswa kufanya juu aweze kuvumilia. Alikumbusha Wakristo kama ili kuvumilia magumu hawapaswe kujitegemea, lakini wanapaswa kumutegemea Yehova. Paulo alisema hivi kwa uhodari: “Yehova ni musaidizi wangu; sitaogopa.” (Ebr. 13:6) Kwa sasa ndugu na dada zetu fulani wako navumilia upinzani. Njia moya ya kuwategemeza ni kusali kwa ajili yao, na kama inawezekana, kuwasaidia kwa kuwapatia mambo yenye wako nayo lazima.Lakini Biblia inasema waziwazi kama “wale wote wenye wanapenda kuishi maisha ya ushikamanifu kwa Mungu katika umoja na Kristo Yesu watateswa pia.” (2 Ti. 3:12) Kwa hiyo siye wote tunapaswa kujitayarisha juu ya magumu yenye iko nakuya. Tuendelee kumutumainia sana Yehova, na tukuwe hakika kama atatusaidia tuvumilie magumu yote yenye tunaweza kukutana nayo. Kwa wakati wenye kufaa, Yehova atamaliza magumu ya waabudu wake wote waaminifu.—2 Te. 1:​7, 8. w24.09 12-13 fu. 17-18

Siku ya Posho, 20 Mwezi wa 6

Wakorinto wengi wenye walisikia wakaanza kuamini na kubatizwa.—Mdo. 18:8.

Nini ilisaidia Wakorinto wabatizwe? (2 Ko. 10:​4, 5) Neno ya Mungu na roho yake yenye nguvu ilibasaidia kufanya mabadiliko makubwa mu maisha yabo. (Ebr. 4:12) Batu ya Korinto benye balikubali habari njema juu ya Kristo baliweza kuacha tabia za mubaya, sawa vile kulewa, kuiba, na tabia ya wanaume kulala na wanaume ao wanamuke kulala na wanamuke. (1 Ko. 6:​9-11) Hata kama batu fulani ba Korinto balizoea sana kufanya mambo ya mubaya, habakusema kama habataweza hata siku moya kuwa Bakristo. Balifanya nguvu yote juu ya kuingia mu barabara ya mwembamba yenye inaongoza ku uzima wa milele. (Mt. 7:​13, 14) Ni nguvu kwako kuachana na tabia fulani ya mubaya juu ustahili kubatizwa? Endelea kujikaza! Umulilie Yehova akupatie roho yake juu ikusaidie kupiganisha tamaa ya kufanya jambo ya mubaya. w25.03 6 fu. 15-17

Siku ya Yenga, 21 Mwezi wa 6

Kama mutu yeyote kati yenu anakosa hekima, aendelee kumuomba Mungu.—Yak. 1:5.

Yehova anaahidi kutupatia hekima yenye itatusaidia kujua ikiwa uamuzi wenye tunakamata unamufurahisha ao hapana. Anatupatia hekima “kwa ukarimu na bila kulaumu.” Kisha kumuomba Yehova muongozo wake, ukuwe muangalifu juu utambue jibu yake. Kwa mufano: Tuseme uko nasafiri, kisha unapotea. Unaweza kuuliza njia mutu wa ile eneo. Lakini, utauliza tu kisha unaenda bila kungoya jibu? Hapana. Utasikiliza kwa uangalifu muongozo wenye ule mutu anakupatia. Vilevile, kisha kumuomba Yehova hekima, tafuta kujua jibu yake kwa kutafuta sheria na kanuni za Biblia zenye zinahusu hali yako. Kwa mufano, mbele ya kuamua kama utaenda ku fete fulani, unaweza kuchunguza mambo yenye Biblia inasema juu ya karamu za kupita kiasi, marafiki wabaya. Unaweza pia kuchunguza juu ya nini ni jambo ya lazima utie faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza kuliko mambo yenye unapenda.—Mt. 6:33; Ro. 13:13; 1 Ko. 15:33. w25.01 16 fu. 6-7

Siku ya Kwanza, 22 Mwezi wa 6

Angalia! Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mutakuwa na njaa.—Isa. 65:13.

Unabii wa Isaya unaonyesha tofauti kubwa yenye kuwa kati ya wale wenye wako mu paradiso ya kiroho na wale wenye kuwa inje ya paradiso ya kiroho. Yehova anatolea watumishi wake chakula mingi ya kiroho. Tuko na roho yake takatifu, Neno yake Biblia, na chakula ingine mingi ya kiroho, ili ‘kula, . . . kunywa, . . . [na] kushangilia.’ (Linganisha na Ufu. 22:17.) Lakini wale wenye kuwa inje ya paradiso ya kiroho ‘wako na njaa . . . , wako na kiu . . . , [na] wanapata haya.’ Mahitaji yao ya kiroho haitimizwe. (Amo. 8:11) Yehova anatolea watu wake kwa ukarimu mambo yenye wako nayo lazima, kutia ndani chakula ya kiroho. (Yoe. 2:​21-24) Anafanya vile kupitia Biblia, vichapo vyetu vyenye kutegemea Biblia, site yetu ya Enternete, na pia mikutano na mikusanyiko yetu. Kama tunatumia ile chakula ya kiroho kila siku, tutakuwa na afya ya muzuri na hatutakosa kitu. w24.04 21 fu. 5-6

Siku ya Pili, 23 Mwezi wa 6

Maneno yenu yakuwe yenye kupendeza sikuzote.—Kol. 4:6.

Kama unapenda kuanzisha urafiki wa kimapenzi pamoya na mutu fulani, unaweza kufanya mipango ili kuzungumuza na ule mutu fasi kwenye kuwa watu wengi ao ku telefone. Sema waziwazi nia yako. (1 Ko. 14:9) Kama ni lazima, patia ule mutu wakati wa kufikiri mbele akujibie. (Mez. 15:28) Kama mutu hapendi kuanzisha urafiki wa kimapenzi uheshimie uamuzi wake. Sasa utafanya nini kama mutu anakuambia kuwa anapendezwa na weye? Inawezekana iliomba ule mutu ajikaze sana juu azungumuze na weye. Kwa hiyo, umujibie kwa upole na kwa heshimaKama uko na lazima ya wakati ya kuwaza juu ya kuamua ikiwa utaanza urafiki wa kimapenzi ao hapana, umuambie. Lakini usikawie sana mbele ya kumujibia. (Mez. 13:12) Kama haupendi kuanzisha urafiki wa kimapenzi, umuambie kwa upole na waziwazi. Lakini, kama na weye unapenda kuanzisha urafiki wa kimapenzi na ule mutu, umuambie waziwazi namna unajisikia na mambo yenye unatazamia kwake. Mambo yenye kila mutu anatazamia kwa mwenzake inaweza kuwa tofauti. w24.05 23-24 fu. 12-13

Siku ya Tatu, 24 Mwezi wa 6

Nakuja kupigana na wewe katika jina la Yehova wa majeshi.—1 Sa. 17:45.

Inawezekana wakati alikuwa angali kijana, Daudi alitembelea maaskari wa Israeli wenye walikuwa wameenda kupigana. Alitambua kama maaskari walikuwa naogopa sana kwa sababu ya mwanaume Mufilisti murefu na mwenye nguvu sana mwenye aliitwa Goliati. Ule mwanaume alikuwa amekuya ‘kuchokoza kikundi cha wapiganaji cha Israeli.’ (1 Sa. 17:​10, 11) Maaskari waliogopa kwa sababu walikuwa nakazia akili ukubwa wa ule mwanaume na maneno yake. (1 Sa. 17:​24, 25) Lakini Daudi yeye alikazia akili jambo tofauti. Aliona kama ule mwanaume alikuwa nachokoza, haiko tu maaskari wa Israeli, lakini “kikundi cha wapiganaji cha Mungu mwenye kuishi.” (1 Sa. 17:26) Daudi alikazia akili Yehova. Alikuwa hakika kama Mungu mwenye alimusaidia wakati alikuwa muchunguji angemusaidia pia mu ile hali. Yehova alimusaidia. Daudi alipigana na Goliati na alipata ushindi!—1 Sa. 17:​45-51. w24.06 21 fu. 7

Siku ya Ine, 25 Mwezi wa 6

Usiogope, kwa maana niko pamoja na wewe. Usihangaike, kwa maana niko Mungu wako. Nitakutia nguvu, ndiyo, nitakusaidia, nitakushika kwelikweli kwa mukono wangu wa kuume wa haki.—Isa. 41:10.

Fikiria namna maisha yetu ingekuwa kama hatungekuwa namutumikia Yehova. Kufanya vile kunaweza kutusaidia tuendelee kuwa waaminifu, na tuseme maneno sawa hii ya muandikaji wa zaburi: “Lakini mimi, kumukaribia Mungu ni jambo la muzuri kwangu.” (Zb. 73:28) Inawezekana tupambane na magumu yote yenye tunaweza kupata mu hizi siku za mwisho juu ‘tunamutumikia Mungu wa kweli mwenye kuishi.’ (1 Te. 1:9) Mungu wetu ni mutu wa kweli kabisa mwenye iko tayari kusaidia watu wake sikuzote. Alisaidia watumishi wake zamani, na iko natusaidia leo. Hivi karibuni ku dunia kutatokea taabu kubwa yenye haiyatokeaka. Lakini hatutakuwa peke yetu. Basi, siye wote tukuwe hodari na kusema: “Yehova ni musaidizi wangu; sitaogopa.”—Ebr. 13: 5, 6. w24.06 25 fu. 17-18

Siku ya Tano, 26 Mwezi wa 6

Mutaona . . . tofauti kati ya mutu mwenye haki na mutu muovu.—Mal. 3:18.

Biblia inazungumuzia zaidi ya wanaume 40 wenye walikuwa wafalme wa Israeli. Wafalme wazuri walifanya mambo fulani ya mubaya. Fikiria mufalme muzuri Daudi. Yehova alisema hivi juu yake: “Mutumishi wangu . . . alinifuata kwa moyo wake wote, akifanya tu mambo yenye yalikuwa sawa mbele ya macho yangu.” (1 Fa. 14:8) Lakini Daudi alifanya uzinifu na bibi ya mwanaume mwingine, na akafanya mipango juu bwana yake auawe mu vita. (2 Sa. 11:​4, 14, 15) Kuko pia wafalme wengi wabaya wenye walifanya mambo fulani ya muzuri. Fikiria Mufalme Rehoboamu. Biblia inasema kama “alifanya mambo ya mubaya.” (2 Ny. 12:14) Lakini alitii amri ya Yehova ya kuruhusu makabila kumi itoke mu ufalme wake na ikuwe na mufalme mwingine. Alisaidia pia kulinda watu wake kwa kutia nguvu miji. (1 Fa. 12:​21-24; 2 Ny. 11:​5-12) Ni nini njo ilifanya Yehova aamue ikiwa Mufalme fulani alikuwa muaminifu? Bila shaka aliangalia hali yake ya moyo, ikiwa alitubu, na ikiwa alimuabudu mu njia yenye kufaa. w24.07 20 fu. 1-3

Siku ya Posho, 27 Mwezi wa 6

Muendelee kuwalea katika nizamu na maonyo ya Yehova.—Efe. 6:4.

Tuseme nini juu ya Wakristo wenye kubatizwa wenye kuwa chini ya miaka 18 wenye wamefanya kosa nzito? Baraza ya wazee itatuma wazee wawili wakutane na ule Mukristo na bazazi yake. Wale wazee watauliza bazazi mambo yenye balishafanya juu ya kusaidia mutoto wao abadilike na atubu. Kama ule mutoto iko najikaza kubadilika na bazazi yake biko namusaidia, wale wazee wawili wanaweza kuamua kama haiko lazima ule mutoto pamoya na bazazi yake bakutane na halmashauri ya wazee. Kwa kweli, ni bazazi njo Yehova alipatia daraka ya kurekebisha batoto yao kwa upendo. (Kum. 6:​6, 7; Mez. 6:20; 22:6; Efe. 6:​2-4) Kisha pale wazee wataendelea kuzungumuza na bazazi juu ya kuhakikisha kama mutoto wao iko napata musaada wenye iko nao lazima. Lakini mambo itakuwa namna gani kama mutoto anakatala kutubu na anaendelea kufanya zambi? Mu ile hali, halmashauri ya wazee ni kusema wazee watatu watakutana naye pamoya na bazazi yake. w24.08 24 fu. 18

Siku ya Yenga, 28 Mwezi wa 6

Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.—Mdo. 20:35.

Siye wenyewe tumejionea kama tunajisikiaka muzuri wakati tunapewa zawadi. Lakini tunasikiaka furaha zaidi wakati siye njo tunapatia wengine zawadi. Juu Yehova alituumba vile, tunaweza kuongeza furaha yetu. Tunaweza kufanya vile kwa kutafuta nafasi zingine za kupatia watu. Hauone kama tuliumbwa mu njia ya ajabu? (Zb. 139:14) Maandiko inatuhakikishia kama kutoa kunaleta furaha. Kwa hiyo, haishangaze kuona kama Biblia inamuita Yehova kuwa “Mungu mwenye furaha.” (1 Ti. 1:11) Yeye njo wa kwanza kupatia wengine na hakuna mutu mwenye anatoaka sana kumupita. Mutume Paulo alisema kama ni kwa sababu yake njo “tuko na uzima na tunatembea na tuko.” (Mdo. 17:28) Na hata “kila zawadi ya muzuri na kila zawadi kamilifu” inatoka kwa Yehova. (Yak. 1:17) Kila mumoya wetu anaweza kupenda kuwa na furaha zaidi yenye inatokana na kutoa. Tunaweza kupata ile furaha kwa kuiga ukarimu wa Yehova.—Efe. 5:1. w24.09 26 fu. 1-4

Siku ya Kwanza, 29 Mwezi wa 6

Kwa kadiri tumefanya maendeleo, tuendelee kutembea kwa utaratibu katika mwendo uleule.—Flp. 3:16.

Kisha kuchunguza mambo yenye mutu anapaswa kufanya juu akuwe muzee, watumishi wa huduma fulani wanaweza kuwaza kama hawatafikiaka kuwa wazee. Lakini ukumbuke kama Yehova na tengenezo yake hawatazamie kama utatimiza zile sifa kwa ukamilifu. (1 Pe. 2:21) Na ni roho takatifu ya Yehova yenye nguvu njo itakusaidia kutimiza ile mambo. (Flp. 2:13) Kuko sifa fulani yenye ungependa kufanyia maendeleo? Sali kwa Yehova juu ya ile jambo. Tafuta habari, na uombe muzee fulani akupatie mashauri yenye inaweza kukusaidia. Endelea kujikaza! Umuombe Yehova akuzoeze juu umutumikie zaidi na utumikie zaidi kutaniko. (Isa. 64:8) Yehova abariki mambo yote yenye uko najikaza kufanya juu ufikie kuwa muzee. w24.11 25 fu. 17-18

Siku ya Pili, 30 Mwezi wa 6

Mungu hana ukosefu wa haki ili asahau kazi yenu na upendo wenye mulionyesha kwa ajili ya jina lake kwa kutumikia na kuendelea kutumikia watakatifu.—Ebr. 6:10.

Ni kweli kwamba Yehova anafurahia uaminifu wetu, lakini hakuna hata mumoya wetu mwenye anaweza kuwaza kama anastahili rehema ya Yehova hata kama alishafanya miaka mingi mu utumishi wake. Alitupatia bei ya ukombozi kwa bure, hapana juu ya kutulipa kwa ajili ya kazi fulani yenye tumefanya. Ikiwa tunawaza kama tunastahili rehema ya Yehova ao tunastahili kutendewa mu njia fulani ya pekee, ni sawa vile tunasema Yesu alikufa tu bure. (Linganisha na Wagalatia 2:21.) Mutume Paulo alijua kama, hata afanye nini hatastahili rehema ya Yehova. Sasa, juu ya nini alifanya mambo mingi mu utumishi wa Yehova? Haiko juu ya kuonyesha kama anastahili, lakini juu ya kuonyesha kama iko mwenye shukrani kwa sababu ya fazili zenye hazistahiliwe za Yehova. (Efe. 3:7) Kama Paulo, tunaendelea kumutumikia Yehova kwa bidii, haiko juu tustahili rehema yake, lakini juu ya kumuonyesha shukrani kwa sababu ya rehema yake. w25.01 27 fu. 5-6

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine