Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 10/15 kur. 465-475
  • Utawala wa Kimungu—Tumaini la Pekee la Wanadamu Wote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Utawala wa Kimungu—Tumaini la Pekee la Wanadamu Wote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KITU AMBACHO IMETUPASA TUTUMAINIE
  • YEYE AMBAYE CHINI YA MIGUU YAKE KUPONDWA KUNATUKIA
  • KUWEKWA HURU!
  • KRISTENDOMU, MFANO WA UCHAGUZI MBAYA
  • Utawala wa Kimungu—Je! Sisi Tunauunga Mkono au Tunaupinga?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Utawala wa Kimungu— Juu ya Wanadamu Mwanzoni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Kungoja Sana Katika Tumaini Karibu Kumalizike
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Adui wa Uzima wa Milele
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 10/15 kur. 465-475

Utawala wa Kimungu​—Tumaini la Pekee la Wanadamu Wote

“Irudieni ngome, enyi wafungwa wa tumaini.”​—Zek. 9:12.

1. Ni nini kinachopaswa kusemwa juu ya ambacho utawala wa kibinadamu umewapa wanadamu wote mpaka hapo tulipo, na namna gani juu ya kuweka tumaini kwa wakati ujao juu ya matokeo ya fundisho la mageuzi?

JE! “UTAWALA wa kimungu” unaweza kuwapa wanadamu wote nini ambacho taifa la kibinadamu halikupewa na utawala wa kibinadamu? Kile ambacho utawala wa kibinadamu umewapa wanadamu wote mpaka sasa bila shaka hakikuwa “cha kimungu,” kama tunavyokiita kitu kilicho “bora sana sana” mara nyingi. Ukiamuliwa kulingana na namna mambo yanavyoendelea katika ulimwengu huu, utawala wa kibinadamu hauahidi kutupa sisi cho chote kilicho bora kuliko ambacho umekwisha tupa kufikia hapo. Na hiyo hairidhishi nafsi kamwe. Kwa kweli inakatisha tamaa sana. Katika karne zote na maelfu ya miaka iliyopita, wanadamu wameonyesha kwamba wanachoweza kutupa sisi kwa habari ya utawala wa kiserikali ni utawala wa kibinadamu tu. Kwa kuwa wanadamu si wakamilifu, umekuwa utawala wa kibinadamu usiokamilika. Fundisho linaloshikiliwa sana la mageuzi ya mwanadamu halitupi sababu zo zote za kutumaini kwamba wanadamu watageuka wawe miungu wakati wa kizazi chetu wala mamia ya mamilioni ya miaka itakayokuja, kwa “mabadili” ya ghafula ya namna ya kushangaza na yenye kufaidi. Tumaini la msaada kwa taabu iliyopo ya ulimwengu haliwezi kuwekwa katika utawala wa kibinadamu.

2. (a) Tumaini limeelezwa kuwa nini, na tumaini la wanadamu wote lingekuwa la namna gani? (b) Umoja wa Mataifa unafaaje kama tumaini la ulimwengu, na namna gani kama ungeondolewa?

2 Ulimwengu wote wa wanadamu umeachwa kabisa pasipo tumaini. Tumaini limeelezwa kuwa “taraja la kitu fulani kinachotamaniwa,” au, “tamaa pamoja na taraja la kuridhishwa kwake.” Tumaini linaweza vile vile kumaanisha “mtu au kitu ambacho katika hicho mataraja yanawekwa.” Sisi sote tunayo matumaini madogo ya kipekee na mambo tunayoogopa, lakini je! isingekuwa ajabu kama lingekuwako tumaini ambalo wanadamu wote wangeshiriki, bila kujali kabila, rangi, taifa wala cheo? Ingekuwa ajabu kweli kweli, kwa kuwa lisingekuwa jambo la kichoyo, la kitaifa, la kikabila, bali lingeziridhisha tamaa za kawaida na mahitaji ya wanadamu wote. Umoja wa Mataifa kama tengenezo la amani na usalama wa ulimwengu, nyuma ya karibu miaka 30 ya utendaji, umeshindwa kuwa au kutoa tumaini la namna hiyo. Kuongezwa kwa mataifa zaidi kama washirika wake hakutakufanikisha kushindwa kwake. Ulimwenguni kote, Umoja wa Mataifa umekuwa ndicho kitu kikubwa zaidi ambacho wanadamu wameweza kutoa kwa mahitaji ya haraka ya kibinadamu. Watu wengi wanashangaa, Ikiwa Umoja wa Mataifa ungeondolewa kwa lazima kama Ushirika wa Mataifa uliotangulia, wanadamu wangetoa kitu gani kingine?

3. Watu wengi ambao matumaini yao kwa wanadamu yameharibiwa wana tamaa gani kubwa?

3 Hapana shaka juu yake: wanadamu hawajui la kufanya! Hesabu ya watu wenye busara wanaokubali kwa unyofu kwamba utawala wa kibinadamu umeshindwa inaongezeka. Matumaini yao kwa mwanadamu yameharibiwa. La kusikitisha zaidi juu yake ni kwamba hawana tumaini zaidi la kujifariji wenyewe na kuwafariji wengine. Wanachofanya sasa ni kutamani sana tu kitu fulani, kutamani kitu fulani wasichokijua katika akili zao, bila maoni yo yote juu ya njia ya kukipata au ni wapi kitu hiki chenye kuridhisha moyo kitakakotoka au kinakoweza kutazamiwa.

4. Hali za ulimwengu zimeyapasaje matumaini ya watu wengine wenye taraja, na kwa hiyo wao si kama mabaharia gani?

4 Lakini, ingawa hali zenye kukatisha tamaa za ulimwengu zinazozidi kuwa mbaya zimeyamaliza matumaini ya watu wasiohesabika, hali izi hizi zilitia nguvu mpya matumaini ya wengine. Wao si kama mabaharia wanaoshuka ndani ya bahari katika meli na wanaopatwa na tufani kali, ambao juu yao mwandikaji wa mashairi alisema: “Wayumba-yumba, wapepesuka kama mlevi, akili zao zote zawapotea.”​—Zab. 107:23-27.

5. (a) Ni shauri gani la mtunga Zaburi wanalofuata watu hawa wa kipekee? (b) Ni nini kisicho utawala wa kibinadamu cha kutazamia, tofauti na mafundisho gani?

5 Ni akina nani watu hawa wa kipekee, ambao matumaini yao yanazidi kuwa maangavu zaidi na zaidi kwa kadiri ambavyo taabu ya ulimwengu inavyozidi kuwa mbaya? Je! ni nini walicho nacho wasicho nacho watu wengine? Hawa ndio wanaofuata shauri lenye busara la mwandikaji wa mashairi wa kale aliyesema: “Msiwatumainie wakuu, wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake. Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, siku hiyo mawazo yake yapotea.” (Zab. 146:3, 4) Mwandikaji wa kale alitushauri tusiyaweke matumaini yetu katika utawala wa kibinadamu, na kwa hiyo wale wanaofuata shauri hili leo wanatazama kingine kuliko utawala wa kibinadamu. Lakini ni pengine wapi pa kutazama? Wanaolitegemeza fundisho la mageuzi ya mwanadamu na wanaofuata fundisho la kifilosofia la mambo ya kimwili wanasema kwamba hakuna cho chote cha kutazamia ila mambo ya kimwili kama wanadamu. Hiyo ndiyo sababu wanajipata bila tumaini na mwishowe watakatishwa tamaa. Si kwamba mafundisho yao hayaridhishi tu bali hayasadikishi vile vile, kwa maana si yenye busara na yanapingana na kweli za historia. Lakini kwa kweli kuna kitu kingine kuliko utawala wa kibinadamu cha kutazamia. Hicho ni nini? Utawala wa kimungu! Watu wenye tumaini leo wanautazamia huu!

KITU AMBACHO IMETUPASA TUTUMAINIE

6. Mwandikaji wa kale anatuelekeza kwenye nini katika Zaburi 146:5-10?

6 Mtungaji wa mashairi wa kale anatuelekeza kwenye hiki. Akisema kutokana na maono yake mwenyewe, yeye anaendelea kusema: “Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, na tumaini lake ni kwa [Yehova], Mungu wake. Aliyezifanya mbingu na nchi, bahari na vitu vyote vilivyomo. Huishika kweli milele, huwafanyia hukumu walioonewa, huwapa wenye njaa chakula; [Yehova] hufungua waliofungwa; [Yehova] huwafumbua macho waliopofuka; [Yehova] huwainua walioinama; [Yehova] huwapenda wenye haki; [Yehova] huwahifadhi wageni; huwategemeza yatima na mjane; bali njia ya wasio haki huipotosha. [Yehova] atamiliki milele.”​—Zab. 146:5-10.

7. Ni akina nani, basi, wanaomhitaji mtawala wa kimungu huyu, na jina lake ni la kutokeza namna gani?

7 Kwa sababu ya utawala wa kibinadamu na makosa yake na hali ya kutoweza, je! wewe u mmoja wa “walioonewa,” au wa “wenye njaa”? Je! wewe u mmoja wa “waliofungwa,” au wa “waliopofuka,” au wa “walioinama”? Je! wewe u ‘mgeni,’ au “yatima,” au “mjane”? Basi Mfalme huyu anayetajwa na mwandikaji wa mashairi wa kale ndiye Yeye wa kutazamia. Utawala wake ni utawala wa kimungu, kwa kuwa yeye kama Mtawala ndiye Mungu. Yeye si Mungu asiye na jina ambaye kujulikana kwake kumesahaulika kati ya mamia yote ya mamilioni ya miungu inayoabudiwa katika India na sehemu nyingine iliyobaki ya dunia inayokaliwa na watu. Yeye ni Mungu asiyepewa jina lake na wanadamu, bali ni Mungu aliyejipa mwenyewe jina, jina ambalo mungu ye yote mwingine haitwi mbinguni wala duniani. Mwandikaji wa mashairi aliyeongozwa na roho ya Mungu analitaja jina la kimungu mara saba, nalo ni Yehova.

8. (a) Mtu atakuwa mwenye furaha akiweka tumaini lake kwa nani, na Warumi 15:13 inamwita nani Yeye? (b) Ili watu wa namna zote wawe na tumaini hili lililohakikishwa kwa njia ya kimungu, Yeye aliandikisha nini?

8 Watu waliojulishwa makosa na wenye maoni mabaya yasiyo na msingi, huenda wakajaribu kukuvunja moyo usishughulike hata kidogo na Mungu huyu, Yehova. Lakini unayo furaha inayokungoja, hata katika nyakati hizi za kuhuzunisha, ukimtumainia Yeye. Mwandikaji wa mashairi wa kale alisema: “Heri ambaye . . . tumaini lake ni kwa [Yehova], Mungu wake.” (Zab. 146:5) Karne kumi na tisa zilizopita mwanamume ambaye alimtumainia Yehova alimwita “Mungu wa tumaini.” (Rum. 15:13) Yeye ndiye Wa Pekee anayeweza kutupa sisi tumaini ambalo wanadamu wote wanaweza kulishiriki, kwa maana Yeye ndiye Muumba wa taifa la kibinadamu. Tumaini la wanadamu wote limo katika Yeye peke yake. Utawala wa kimungu anaotoa ndilo tumaini la wanadamu wote. Ili watu wa makabila yote, mataifa na lugha wawe na tumaini hili lililohakikishwa kwa njia ya kimungu Yeye aliandikisha Kitabu kilichoongozwa na roho yake, Biblia Takatifu. Kwa Kitabu hiki kizuri sana, kilichoandikwa juu ya jina la Mungu, unaweza kujifunza yote juu ya tumaini hili la hakika.

9. (a) Kwa sababu ya kuuona uhitaji wa wanadamu wa tumaini, Mungu aliwapa tumaini la namna gani? (b) Ni sala gani iliyotolewa, katika Warumi 15:13, kwa wanaoshiriki tumaini hili?

9 Huko kale Yehova Mungu aliona kwamba wanadamu walihitaji tumaini, na akawawekea moja. Tumaini hili analotupa Yeye lina uwezo wa kututegemeza katika nyakati zilizo ngumu zaidi na kutuokoa mpaka tumaini lenyewe litakapotimizwa kwa furaha. Hiyo ndiyo sababu, miaka 1900 iliyopita, washirika wa tumaini hili waliandikiwa hivi: “Kwa maana tuliokolewa kwa taraja; lakini kitu kilichotarajiwa kikionekana, hakuna taraja tena. Kwa maana ni nani anayekitarajia kile akionacho? Bali tukikitarajia kitu tusichokiona, twakingojea kwa saburi.” (Rum. 8:24, 25) Tumaini hili lililotolewa kwa njia ya kimungu linatujaza furaha na kutufanya watulivu kati ya msukosuko wa ulimwengu, hivyo kwamba tumaini letu linaenea na kujionyesha kwa wengine wakiwa katika hali yao ya kukatisha tamaa. Hiyo ndiyo sababu sala ilitolewa kwa ajili ya washirika katika tumaini hili: “Basi Mungu wa tumaini na awajaze ninyi furaha yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana kuwa na tumaini, katika nguvu za [roho takatifu].”​—Rum. 15:13.

10. Mungu atamponda nani karibuni chini ya miguu ya washirika wa tumaini hili, na matokeo yatakuwa nini kwa mbingu na dunia?

10 Inatupasa tulikaribishe tumaini hili kati ya ulimwengu unaojitoa zaidi na zaidi kwa maovu, chini ya maongozi yasiyoonekana ya “mungu wa taratibu hii ya mambo” asiyeonekana, Shetani Ibilisi. Lakini ukombozi kutoka kwa uovu huu unaoongezeka unakaribia sana, ndiyo, sasa u karibu. Hiyo ndiyo sababu mwandikaji aliyeongozwa na roho ya Mungu alipokuwa akisema kwa washirika hao wa tumaini la kimungu mnamo karne ya kwanza ya Wakati wetu wa Kawaida aliwaandikia hivi: “Nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya. Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi.” (Rum. 16:19, 20) Neno la kale la Kiebrania Shetani lina maana ya “Mpinzani; Adui,” na hapa linaelekeza kwa Mpinzani Mkubwa wa Mungu, Mpinzani aliyeuanza upinzani kwa Mungu na anayeviongoza viumbe vingine vyote katika kumpinga Mungu na makusudi yake mema mbinguni na duniani. Mungu ni mwenye uwezo zaidi kumpita huyu Shetani. Kwa hiyo Mungu atamponda huyu Shetani, lakini ni chini ya miguu ya washirika hawa wa tumaini kwamba Shetani atalala amepondwa. Usemi huu unamfananisha Shetani na kitu kinachoweza kupondwa chini ya miguu​—si nge, bali nyoka. Ni amani ya namna gani ya ulimwengu wote itakayoletwa na kupondwa huku kwa Shetani!

11. Kwa kusema hivyo juu ya kumponda Shetani, mwandikaji aliyeongozwa na roho ya Mungu alikuwa akitaja nini katika Mwanzo, na kwa kweli Mungu alikuwa akisema kwa nani hapo?

11 Twawezaje, hata hivyo, kuwa na uhakika kwamba kupondwa huku ni kwa Shetani kana kwamba alikuwa nyoka? Kwa sababu hapa mwandikaji wa barua hiyo kwa wenye tumaini katika Rumi, Italia, alitoa usemi wake wa mfano katika kitabu cha kwanza cha Maandiko Matakatifu, au katika Mwanzo. Katika barua yake yote anataja mara nyingi kitabu cha Mwanzo. (Rum. 4:3, 9, 11, 17, 18, 22; 9:7, 9, 12) Na hapa mwandikaji alikuwa akitaja Mwanzo 3:14, 15, ambapo Mungu anaelekea kusema kwa nyoka akiwa udongoni lakini kwa kweli anasema kwa Mpinzani Mkuu aliyemtumia nyoka huyo. Hapo twasoma hivi: “[Yehova] Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako; nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.” Zaidi ya miaka elfu nne nyumaye mwandikaji aliyeongozwa na roho ya Mungu, mtume wa Kikristo Paulo, anasema juu ya mwali huo wa kwanza wa tumaini.

12. (a) Ni muda mrefu namna gani tangu hukumu hiyo ilipotangazwa kwa Shetani? (b) Kwa sababu gani sisi sote tunakufa na dunia inaharibiwa?

12 Sisi leo tu zaidi ya karne kumi na tisa karibu na utimizo wa ahadi hiyo yenye kutia tumaini ya Yehova Mungu ya kumponda Nyoka mwenyewe, Shetani Ibilisi, chini ya miguu ya Uzao ambao kisigino chake kilipondwa mpaka kufa na vile vile chini ya miguu ya wafuasi waaminifu wa Yeye huyo aliyepondwa. Hii inamaanisha kwamba miaka elfu sita karibu imalizike sasa tangu Mungu alipotangaza kwa njia ya mfano hukumu ya uharibifu juu ya Mpinzani wa kwanza, Shetani, kwa kuwapindua mwanamume wa kwanza na mwanamke wa kwanza, ambao sisi sote tumetoka kwao, wampinge Yehova Mungu. Kuungana katika upinzani huo wa Kishetani kulileta kifo kwa jamaa yote ya kibinadamu. Vile vile kulimaanisha kufukuzwa kwa wazazi wetu wa kwanza wa kibinadamu katika Paradiso ya Furaha, Bustani ya Edeni, na kufungiwa kwetu sote nje ya makao hayo ya Paradiso ambamo wazazi wetu wa kwanza wa kibinadamu walikuwa wameumbwa katika ukamilifu. (Mwa. 2:7 mpaka 3:24) Ni ajabu kwamba leo, ijapokuwa majaribio yote katika sayansi ya dawa, sisi sote tunakufa na kwamba, ijapokuwa njia zetu zilizoendelezwa za ukulima, dunia inachafuka sana na kuharibika kwa kadiri ya kutofaa kwetu kuishi ndani yake kama makao yetu?

YEYE AMBAYE CHINI YA MIGUU YAKE KUPONDWA KUNATUKIA

13. Ni nani peke yake aliyezaliwa katika dunia hii aliyeokoka laana ya kifo kutoka kwa Adamu na Hawa, na hili lilitukiaje?

13 Hakuna hata mmoja kati yetu ambaye ameweza kuepuka kutorithi matokeo ya kifo katika miili yetu. Hii ni kwa kuwa sisi sote tulitoka kwa wazazi wetu wenye kumpinga Mungu waliojiondoa katika utawala wa kimungu katika makao ya Paradiso ya kidunia na kujiweka chini ya utawala wa Mpinzani Mkubwa wa Mungu, Shetani Ibilisi. (Rum. 5:12) Ni mtu mmoja tu aliyezaliwa katika dunia hii aliyeepuka kurithi laana ya kifo kutoka kwa mwanamume wa kwanza na mwanamke wa kwanza, Adamu na Hawa wenye dhambi, na huyo alikuwa mtu aliyeitwa Yesu Kristo. Jambo hili lisilowezekana kwa njia ya kibinadamu lilitukiaje? Ni kwa sababu Yesu hakuwa na baba wa kibinadamu au mpaji wa uzima. Kiini katika mwili wa mama yake wa kibinadamu Mariamu hakikuzalishwa na mume wa kibinadamu. Ni Mwenyezi Mungu mbinguni aliyetia uhai katika kiini cha Mariamu na kukifanya kiwe kiumbe kikamilifu cha kibinadamu. Haukuwa uhai mpya ambao Mwenyezi aliutia katika kiini hicho cha kibinadamu. Bali, aliihamisha nguvu ya uhai ya Mwana wake wa kimbinguni aliyejulikana kama Neno na kuitia katika kiini cha bikira na kukifanya kianze kukua.

14. (a) Ni nani aliyemjulisha Mariamu juu ya kuzaliwa kwa mwujiza ambako kungetukia? (b) Ni ushuhuda gani uliopo kuonyesha kwamba Yesu alizaliwa bila dhambi?

14 Kupitia kwa malaika wake Gabrieli yeye alimjulisha kwanza Mariamu Myahudi juu ya tendo hili la mwujiza na akamwambia kwamba angemwita mtoto wake, ambaye angekuwa mwanamume, Yesu. (Luka 1:26-38) Hivyo mwanamume ambaye nyumaye alioa Mariamu hakuwa baba mwenyewe wa mwana wake Yesu. (Mt. 1:18-25) Hivyo, kama Maandiko Matakatifu yanavyotujulisha, Yesu alizaliwa “asiyekuwa na waa lo lote, aliyetengwa na wakosaji.” (Ebr. 7:26) Yeye aliweza kusema hivi kwa wakinzani wake wa Kiyahudi alipokuwa mtu mzima: “Ni nani miongoni mwenu anishuhudiaye ya kuwa nina dhambi?”​—Yohana 8:46.

15. (a) Kwa sababu gani Shetani alimfanya Yesu shabaha kubwa ya shambulio lake? (b) Yesu hakushindwa na woga wa nini, na kwa hiyo alikufa kifo cha namna gani?

15 Mpinzani Mkuu, Shetani Ibilisi, alimfanya Yesu Kristo huyu shabaha yake ya mashambulio. Kwa sababu gani? Kwa maana alijua kwamba Mwana wa Mungu huyu alikuwa ndiye Wakili Mkuu wa Mungu wa kukiponda kichwa cha nyoka au wa ‘kumseta Shetani chini ya miguu.’ Sawa na ilivyotabiriwa katika Mwanzo 3:15, Shetani alikuwa na uadui na Uzao Ulioahidiwa, Yesu Kristo, na akajitayarisha kumponda “kisigino.” Lakini aliona kwamba hangeweza kumwogopesha Yesu kwa vitisho vya kifo, kifo chenye jeuri ili ajitiishe katika utumwa wa Shetani. Yesu hakushindwa na “hofu ya mauti” mikononi mwa mawakili wa kidunia wa Shetani bali aliuzidisha uadui wake kwa Shetani Nyoka na mawakili zake au “uzao.” Yesu alimwogopa Yehova Mungu peke yake. Kwa hiyo hakujipatanisha na Shetani Nyoka na hakuepa kifo chenye jeuri kwa woga mikononi mwa “uzao” wa Nyoka Mkubwa. Shetani hangeweza kumfanya Yesu arudi nyuma hata kutoka kwa kifo kama mhalifu mbaya juu ya mti wa kufishia. Mashtaka yaliyomfanya Yesu auawe yalikuwa ya uongo. Alikufa mwenye dhamiri safi katika kifo cha dhabihu kwa ajili ya viumbe vyenye nyama na damu vilivyokuwa utumwani mwa Shetani Ibilisi.

16. Kwa kuleta kifo cha Yesu kwa mashtaka ya uongo, Shetani alikuwa akijishinda mwenyewe namna gani, kulingana na Waebrania 2:14, 15?

16 Kwa kumfisha Yesu kwa mashtaka ya uongo, Shetani Nyoka Mkubwa alikuwa akijishinda mwenyewe tu. Alikuwa akitoa sababu iliyo kubwa kupita zote ya kuharibiwa kwake mwenyewe tu, kufutiliwa mbali asionekane tena. Hili ndilo jambo linaloonyeshwa katika maneno yaliyoongozwa na roho ya Mungu yaliyoandikwa juu ya Yesu kama mtu mwenye nyama na damu: “Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi, awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa.”​—Ebr. 2:14, 15.

17. (a) Ni kwa njia gani Mungu hakujiacha mwenyewe azuiwe na mauti asimtumie mshuhudiaji wake mkuu? (b) Kwa hiyo Yesu alifanywaje mwenye nguvu zaidi sana kuliko Nyoka Mkubwa, Shetani?

17 Kwa unyofu “kwa njia ya mauti” yake Yesu Kristo alionyesha kwamba alikuwa na uadui na Shetani Nyoka Mkubwa pasipo kujipatanisha naye mpaka kifo chenyewe. Vile vile aliushuhudia utawala wa kimungu wa Baba yake wa kimbinguni Yehova Mungu kama Yeye ambaye chini yake viumbe vyote mbinguni na duniani, kutoka kilicho juu zaidi hata kilicho chini zaidi, vimepaswa vijitiishe kabisa. Je! Mwenyezi, Mungu Aliye Juu Zaidi angemwacha mshuhudiaji wake mkuu vifungoni vya mauti na hivyo mwenyewe aache kumtumia zaidi mwaminifu huyo? Sivyo kulingana na ambayo Yehova alikwisha tabiri alipokuwa akisema kwa nyoka katika Bustani ya Edeni. Alikuwa ametabiri kwamba kutiwa jeraha kwa Uzao wa “mwanamke” kungekuwa jeraha la kisigino tu, si kama kuchubuliwa ama kupondwa kichwani. Kwa hiyo Mungu Mwenyezi aliliponya jeraha kwa kumwinua Yesu kutoka kwa wafu siku ya tatu, Nisani 16, ya mwaka wa 33 C.E. Mungu alikubali kwamba Mwana wake Yesu Kristo alikuwa ameutoa ubinadamu wake mkamilifu dhabihu kama toleo la dhambi kwa ajili ya wanadamu wote, na kwa hiyo Mungu hakumfufua uzimani tena kama mwanadamu mkamilifu mwenye damu na nyama. Bali, Mungu alimrudisha kwenye makao ya kimbinguni ambako uhai wake mbele ya kuwa mwanadamu ulikuwa umehamishwa kutiwa katika tumbo la uzazi la bikira Myahudi. Mungu alifanya hivi kwa kumfufua Mwana wake Yesu Kristo kama kiumbe cha kiroho kitukufu, akiwa amevalishwa hali ya kutokufa na “tabia ya Uungu.” (1 Pet. 3:18; 1 Kor. 15:42-54; 2 Pet. 1:4) Namna hii ya ufufuo ilimfanya Yesu Kristo mwenye nguvu zaidi sana kumpita Nyoka Mkubwa Shetani na ikamweka katika cheo cha uwezo ambapo anaweza ‘kumharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi.’​—Ebr. 2:14.

KUWEKWA HURU!

18. (a) Kulingana na Waebrania 2:15, inawapasa wanadamu wote watazamie nini kutokana na kupona kwa jeraha la kisigino la Uzao Ulioahidiwa? (b) Ingawa wanawaweka huru watu wao waliofungwa, watawala wa kibinadamu wameshindwa kuwafungua wanadamu katika utumwa wa nani?

18 Inawapasa wanadamu wote watazamie nini kutokana na kupona huku kwa jeraha ambalo Nyoka Mkubwa Shetani Ibilisi alitia katika “kisigino” cha Uzao Ulioahidiwa wa Mungu? Ni jambo ambalo wanadamu wote wametamani kwa maelfu ya miaka? Ndiyo: Kuwekwa huru! Ndiyo, uhuru kutoka utumwani kwa wanadamu wote! Kusudi lililotajwa la Uzao Ulioahidiwa katika kuonja mauti kama mtu mwenye damu na nyama lilikuwa, si kumwondoa Ibilisi aliyewatisha wanadamu na kifo kama wasingekuwa watumwa wake tu, bali vile vile “awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa.” (Ebr. 2:15) Watawala wa kisiasa wengine wa kidunia waliwafungua wingi wa watumwa wa mataifa yao waliuokuwa mikononi mwa wanadamu waliowaweka utumwani, lakini hakuna mmoja wao ameweza kuwaweka huru watu wao wenyewe wala wanadamu wote kutoka kwa utumwa mzito wa wanadamu mikononi mwa Nyoka Mkubwa Shetani Ibilisi. Hili si jambo la kudhihaki, tukiwa na maoni ya kwamba hakuna kitu kama Ibilisi bali kwamba Ibilisi ni hadithi tu. Ibilisi huyu mwenye umri wa miaka elfu sita ni mwerevu vya kutosha kuweza kuwapumbaza watu wenye hekima ya kilimwengu wa leo wafikiri kwamba yeye hayuko!

19. Kwa sababu gani wanadamu wote hawakuwekwa huru kufikia hapo, lakini ni nini kinachoonyesha kwamba hili sasa linakaribia?

19 Inaelekea watu wengi leo watasema: ‘Ikiwa Ibilisi yuko na ikiwa Yesu Kristo alikufa karne kumi na tisa zilizopita atuweke huru kutoka utumwani mwa Ibilisi huyo, kwa sababu gani mpaka sasa wanadamu wote hawajapata kuwekwa huru? Kwa sababu gani wanadamu wote leo wanaona hawajapata uhuru, bali, twajiona tumo utumwani mwa taratibu ya mambo inayokuwa mbaya zaidi na zaidi mwaka kwa mwaka?’ Sababu yake, kama Biblia Takatifu inavyoonyesha, ni kwamba wakati haujafika bado wa Uzao Ulioahidiwa wa Mungu ‘kuponda kichwa cha Nyoka,’ au, ‘kumharibu’ Shetani Ibilisi. Lakini, wakati huo unaotamanika u karibu sana sasa. Kama, huko nyuma katika karne ya kwanza, mtume Paulo aliwaandikia Wakristo wenzake katika Rumi, “Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi,” lazima hili liwe linakaribia sana leo, karne kumi na tisa nyumaye. (Rum. 16:20) Si kumalizika kwa kipindi kirefu tu kunakohakikisha hili, bali “dhiki ya mataifa” inayoendelea duniani tangu mwaka wa 1914 C.E. vile vile inafanya hivyo. (Luka 21:25) Ndiyo sababu taraja la wenye tumaini walilopewa na Mungu linakuwa kubwa zaidi na zaidi.

20. (a) Ili wasadikishwe, ulipaswa wakati uruhusiwe wa kuhakikisha nini? (b) Kwa sababu ya mwisho unaokaribia wa wakati ulioruhusiwa, ni uchaguzi gani unaompasa kila mtu kufanya?

20 Mbele ya mabilioni ya watu ambao wangali wakiutumainia utawala wa kibinadamu kusadikishwa, lazima waruhusiwe kabisa wakati wa kuonyesha kwamba utawala wa kibinadamu ndio ufumbuzi (kama wanavyodai), kwamba wenyewe waweza kupata njia ya kutokea na kuwa mkombozi wa wanadamu wote. Kuruhusiwa huku kwa wakati kungali hakujamalizika kabisa. Kwa sababu ya mwisho huo unaokaribia, huu ndio wakati wa watu kujifanyia uchaguzi wa wanaoutaka, utawala wa kibinadamu peke yake, au Mkombozi wa Mungu aliyewekwa. Mwishoni mwa wakati ulioruhusiwa kila mmoja atalipwa kulingana na uchaguzi wake. Ndipo Mtawala wa Kimungu atakapowaweka huru wale walioweka tumaini lao kwa Mkombozi wa kimbinguni peke yao ambaye Mungu ametoa. Mbele ya wakati huo Uzao Ulioahidiwa, Yesu Kristo, hautaleta uhuru uliotumainiwa kwa kipindi kirefu.

21, 22. (a) Yesu alijua nini kama mwanadamu juu ya wakati wa Ufalme, na kwa sababu gani akabatizwa mwenye umri wa miaka 30? (b) Shetani alitaka kumjaribu Yesu afuate maisha ya namna gani, na lilikuwa jaribu gani la mwisho alilotoa?

21 Katika karne ya kwanza ya Wakati wetu wa Kawaida, wakati Yesu Kristo aliposhiriki damu na nyama duniani kama mwanadamu mkamilifu, alijua kwamba huo haukuwa wakati wa kuwekwa huru kwa wanadamu wote kupitia kwa serikali yake mwenyewe. Alikuwa mwenye umri wa miaka 30 alipoamua kuchukua mwendo wa kujitoa mwenyewe dhabihu kulingana na mapenzi ya Mungu, na alifananisha kujitoa kwake kwa dhabihu kwa kubatizwa katika Mto Yordani. (Ebr. 10:1-5; Mt. 3:13-17) Nyuma ya ubatizo huo alikwenda yeye peke yake katika jangwa la Uyahudi kufunga na kurudia kujifunza jambo hili kwa siku 40. Mwishoni mwa wakati huo alikuwa amejitahidi kabisa kuutimiza mwendo uliowekwa wa kimungu wa dhabihu, hata kifo chenyewe. Siku ya 40 na ya mwisho ya kufunga jangwani alikuja kujua kwamba hakuwa peke yake. Mtu fulani alimjia, mtu fulani wa kumjaribu ajiepushe na mwendo wa kujitoa mwenyewe dhabihu. Mjaribu huyo alikuwa Shetani Ibilisi. Alitaka kumjaribu Yesu afuate maisha ya mapendezi ya kichoyo na utukufu na uwezo kama mtu mwenye damu na nyama. Jaribu la tatu na la mwisho ndilo lililofikia upeo. Hii ndiyo habari ya jaribu hili lenye nguvu kama ilivyoandikwa na mwanafunzi wa Yesu Kristo mwenyewe, yaani, Mathayo (4:1-9):

22 “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.”

23. Yesu alitofautianaje na watawala wa kibinadamu wa kisasa kwa habari ya maoni yao juu ya uwezo wa Shetani, na ni dai gani la Shetani ambalo Yesu hakukana?

23 Yesu hakulitupilia mbali jambo hili na kusema: ‘Ibilisi hayuko. Hivyo basi anawezaje kunipa mimi “milki zote za ulimwengu, na fahari yake” nikifanya tendo dogo tu la ibada kwake? Nawezaje kweli kuabudu kisichokuwako?’ Yesu hakuwa kama watawala wa kitaifa wa kibinadamu wa leo wanaoyapinga maoni na hata kulichukia fundisho la kwamba “milki zote za ulimwengu” zimo mikononi mwa Mjaribu, Shetani Ibilisi. Yeye hakukana kuwako kwa Ibilisi na kwamba Ibilisi ndiye anayeziongoza “milki zote za ulimwengu” bila kuonekana. Yeye hakukana kwamba Ibilisi hakusema kwa haki juu ya “milki zote za ulimwengu” alipomwambia hivi: “Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo. Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako.” (Luka 4:5-7) Hapa jaribu lenyewe lilikuwa likifanywa kwa Yesu na mtu kweli kweli aliyetaja mambo ya hakika. Lo! namna uchaguzi wa Yesu ulivyokuwa wa maana kwa wanadamu waliotumikishwa!

24. (a) Ibilisi alikuwa akimtolea Yesu utawala wa namna gani? (b) Hapa ulizo lilikuwa nini, na ni uchaguzi gani ungalifanywa hapa?

24 Hapa Nyoka Mkubwa, Shetani Ibilisi, hakuwa akijaribu kuuponda Uzao Ulioahidiwa wa Mungu katika kisigino. Alikuwa akimpa Yesu kitu ambacho kwa wazi kingemwepusha na kifo chenye jeuri chenye kuletwa na ‘aliye na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi.’ Yeye alikuwa akimtolea Yesu utawala wa ulimwengu kama mwanadamu, utawala juu ya “milki zote za ulimwengu,” utawala wa kibinadamu juu ya dunia yote. Ndiyo, lakini “utawala wa kibinadamu” kama mwabudu Ibilisi na chini ya uongozi wa Ibilisi, mtu wa kiroho mwenye uwezo zaidi ya mwanadamu. Uchaguzi mkubwa hapa ulikuwa kati ya utawala. Ulizo lilikuwa, Utawala! Utawala wa kibinadamu au utawala wa kimungu? Utawala wa kibinadamu kama zawadi kutoka kwa Ibilisi na kwa kumnyenyekea Ibilisi, au utawala mikononi mwa Mungu na kwa kumnyenyekea Yeye? Kama Yesu angejichagulia utawala wa kibinadamu kama mwanasiasa wa kilimwengu, hiyo ingeacha tumaini gani kwa wanadamu waliotumikishwa?

KRISTENDOMU, MFANO WA UCHAGUZI MBAYA

25. (a) Ni wapi leo tulipo na mfano wa ambalo lingalifuata kama Yesu angalilikubali toleo la Ibilisi? (b) Je! Yesu na mitume wake ndio waliomwanzisha Kristendomu, au taifa la Kiyahudi ndilo mwanzo wake?

25 Hatukuachwa tuwazie wenyewe! Tunao mfano wa kweli wa kihistoria wa ambacho kingetukia. Wapi? Umu humu ndani ya Kristendomu. Namna gani? Basi, Kristendomu anajidai kuwa makao ambamo Ukristo unazoewa duniani. Mataifa mengi na serikali zao wanajidai kuwa Wakristo. Kristendomu hakuanzishwa na Yesu Kristo na mitume wake kumi na wawili. Taifa la Yesu mwenyewe la kidunia, taifa la Kiyahudi, halikumwanzisha Kristendomu. Taifa la Kiyahudi kama jamii ya kisiasa lilikwisha mwaka wa 70 C.E., likiupigania Uyahudi na uhuru wake wa kisiasa kutoka kwa Rumi mkuu huko Yerusalemu, si Yesu Masihi kama Mfalme. Miaka mitatu nyuma ya kuuharibu Yerusalemu, majeshi ya Kirumi yaliiteka ngome ya mwisho ya Kiyahudi, ngome ya Masada, mwaka wa 73 C.E. Mpaka leo hii, Wayahudi wa asili wa Kiorthodokis si sehemu ya Kristendomu ulimwenguni pote, ijapokuwa wanashirikiana na Kristendomu.

26. Kristendomu alianzishwa lini, na namna gani, na akiwa na Wakristo wa kujidai wa namna gani?

26 Kristendomu alitokezwa karibu karne tatu nyuma ya jaribu la Yesu Kristo katika jangwa la Uyahudi. Hii ilikuwa katika siku za Mfalme wa Kirumi Konstantino Mkuu, aliyebatizwa kama mtaalamu wa Ukristo mbele tu ya kifo chake mwaka wa 337 C.E. Lakini alikuwa amedai kugeuzwa kwenye Ukristo miaka mingi mbele ya hapa, mwaka wa 312 C.E. Wakati huo kilichoitwa Ukristo kilikwisha ondoka mbali sana na mafundisho ya Yesu Kristo na mitume wake hivyo kwamba walioitwa Wakristo walishika silaha za kijeshi wampiganie mkuu huyu wa kipagani na mwanasiasa Konstantino. Mbali na hayo, walikuwako maaskofu makanisani ya siku hizo waliokuwa wakifundisha fundisho la kipagani la Utatu, utatu wa Mungu wenye “Mungu Baba na Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu.” Maaskofu walikuwa wakibishana vikali juu ya kama Mungu alikuwa yule Mungu mmoja, Yehova, wa Maandiko ya Kiebrania, au anayeitwa “Mungu katika nafsi tatu,” “nafsi” zote zikiwa zenye uwezo sawasawa na zote zikiwa za milele. Konstantino alijaribu kuyamaliza mabishano.

27. (a) Konstantino alijaribu kuanza dini ya namna gani, na aliwatolea maaskofu wa makanisa nini? (b) Ni nani aliyekuwa akitoa toleo hili kwa maaskofu, Kristo au Shetani?

27 Kama Askofu Mkuu, wasadikisha maaskofu wote wa makanisa. Alijaribu kuanzisha mchanganyiko wa dini mbalimbali, kuunganisha upagani na Ukristo. Akitenda kama Askofu Mkuu na hivyo kama kiongozi wa kidini wa Milki ya Kirumi, aliwatolea maaskofu vyeo vya uwezo, ukuu na utajiri katika serikali ya Kirumi kama maafisa wa dini ya Taifa la Kirumi. Sasa hili lilikuwa toleo la utawala wa kibinadamu kwa kuungana na serikali ya kisiasa likifanywa kwa wanaoitwa maaskofu wa Kikristo. Je! tufikiri kwamba Yesu mbinguni hapa alikuwa akiwatolea “maaskofu” hao utawala wa kibinadamu kukamatana na “milki zote za ulimwengu” alizokuwa amezikataa Yeye? Au, alikuwa ni Mjaribu, Shetani Ibilisi, ambaye bado alikuwa akijidai kwamba falme hizo zilitolewa kwake? Si vigumu kulifikia jibu linalofaa: alikuwa ni Shetani Ibilisi kupitia kwa Askofu Mkuu duniani aliyekuwa akiwajaribu maaskofu sawa na vile alivyofanyiwa Yesu Kristo. Lakini je! maaskofu, kutia na “askofu wa Rumi,” walifuata mfano wa Yesu?

28. (a) Je! maaskofu hao waliufuata mfano wa Kristo, na kwa hiyo matokeo yalikuwa nini? (b) “Askofu wa Rumi” alijipa cheo gani, na ni nini kilichotokea kwa umoja wa Kristendomu?

28 Historia ya kilimwengu na ya kidini inajibu Hapana! Maaskofu wengi walishindwa na jaribu na wakauchukua utumishi wa kifalme kama jamii ya mapadre ya dini ya Taifa la Kirumi, Kanisa la Taifa la Kirumi. Hivyo Kristendomu alizaliwa na akakua. Mwaka wa 378 C.E. askofu wa Rumi aliendelea sana hata kwa kadiri ya kuchagua cheo na madaraka ya Askofu Mkuu, yaliyokuwa yameondoshwa na Mfalme wa Kirumi Gratian. Katika karne zote zilizofuata Kristendomu aligawanyika, akapigana vita vingi vya kidini, vita vitakatifu na mateso kati ya wanaoitwa Wakristo. Makanisa ya Kitaifa mbali mbali yalianzishwa. Kristendomu amekuwa tengenezo lenye nguvu zaidi na lenye watu wengi zaidi duniani. Amekuwa tamasha kwa wapagani wote, ulimwengu usio wa Wakristo, sasa wenye zaidi ya theluthi mbili za idadi ya watu duniani. Lakini amekuwa mfano wa nini? Wa Ukristo wa kweli? Au wa kinachoitwa utawala wa kimungu ukizoewa kupitia kwa jamii ya kidini ya mapadre inayoshirikiana na wafalme wa kibinadamu wanaojidai kuwa na “haki ya kimungu ya wafalme”?

29. Kwa sababu gani twauliza juu ya Ukristo wa vile vita vya ulimwengu viwili na matengenezo ya ulimwengu ya amani na matayarisho ya vita nyingine ya ulimwengu?

29 Je! Vita ya Kwanza ya Ulimwengu ilikuwa ya Kikristo kwa kuwa ilianza kati ya mataifa ya kisiasa mawili ya Ulaya yaliyojidai kuwa ya Kikristo? Je! Ushirika wa Mataifa ulikuwa wa Kikristo kwa sababu ya kutegemezwa na Kanisa la Uingereza na kwa sababu viongozi wa dini wa Kiamerika waliuita “wonyesho wa kisiasa wa Ufalme wa Mungu duniani”? Je! Vita ya Pili ya Ulimwengu ilikuwa ya Kikristo kwa kuwa ilianza wakati linaloitwa Taifa la Kikristo lilipoingia katika eneo la Taifa jingine la “Kikristo”? Je! Umoja wa Mataifa ni tengenezo la Kikristo la amani na usalama wa ulimwengu kwa kuwa karibu nusu ya mataifa washirika 132 wanadai kuwa Wakristo? Je! matayarisho ya taratibu ya Vita ya Tatu ya Ulimwengu yenye makombora ya atomiki ni ya Kikristo kwa sababu Kristendomu anajiona mwenye wajibu wa kujikinga mwenyewe na silaha hizo ili aokoke?

30. (a) Ni hali gani mbaya zinazoonyesha alivyo Kristendomu leo, na je! hizi ndio wonyesho wa Ukristo? (b) Mambo haya yanaonyesha nini juu ya uchaguzi wa utawala wa ulimwengu uliotolewa kwa Yesu na Mjaribu?

30 Zitazame hali zilizomo katika Kristendomu leo nyuma ya karne kumi na sita za kuwako kwake. Uharibifu wa tabia za adili uliomo ndani yake, uhalifu unaoongezeka, dhuluma za kijamii na za kitaifa, maonezi, magumu ya fedha, umaskini na njaa, kutoheshimiwa kwa mamlaka inayostahili, kutawala vibaya, kutamani sana anasa za kichoyo, kukosa upendo kwa jirani, ambayo maana yake ni kutompenda Mungu​—je! mambo haya ndio wonyesho wa Ukristo? Hata! Hayo ndio ukuzi wa kuanzishwa kwa Kristendomu katika karne ya nne C.E. Na kwa kuwa Kristendomu alitokezwa na kushindwa kwa maaskofu wa makanisa na majaribu yaliyowekwa mbele yao na Milki ya Kirumi ya kipagani, kwa wazi na kwa kusikitisha yanaonyesha ambacho kingalitokea kama Yesu Kristo mwenyewe angalikubali hongo lililotolewa kwake la utawala wa kibinadamu wa “milki zote za ulimwengu.” Lakini je! Yesu Kristo alilikubali toleo lenye kujaribu la Shetani Ibilisi? Je! yeye ndiye wa kulaumiwa kwa sababu ya dhiki ya ulimwengu leo?

31. Yesu alilionaje toleo la Mjaribu?

31 Maandishi ya Biblia yanasema: “Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie [Yehova] Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia.”​—Mt. 4:10, 11; Marko 1:12, 13.

32. (a) Yesu aliukubali utawala gani, kama inavyoonyeshwa na ujumbe uliohubiriwa? (b) Kwa habari hii, Yesu alimngoja Yehova Mungu afanye nini?

32 Yesu aliukataa kabisa utawala wa kibinadamu mikononi mwa Shetani Ibilisi. Yeye aliukubali utawala wa kimungu, ule wa Yehova Mungu. Ndiyo sababu alizunguka-zunguka katika nchi ya taifa la Israeli akitangaza: “Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.” Nyuma ya ubatizo wake katika Mto Yordani alikuwa ametiwa mafuta na roho ya Mungu auhubiri ujumbe huo. Aliwatuma mitume wake kumi na wawili wakauhubiri ujumbe uo huo wa tumaini kwa wanadamu wote. (Mt. 4:13-17; Luka 4:16-21; 9:1-6; Mt. 10:1-7) Yesu Kristo alimngoja Mungu auonyeshe utawala wake wa kimungu kwa kuusimamisha ufalme wa kimbinguni mikononi mwa Uzao Ulioahidiwa utakaomponda Nyoka Mkubwa kichwani na hivyo kumharibu ili wanadamu wote wapate kuwekwa huru. Yesu alikufa mwaminifu kwa utawala wa kimungu, akimkubali si mwingine ila Yehova Mungu kama Mtawala Aliye Mkuu Zaidi, Mwenye Enzi wa Ulimwengu Wote.

[Picha katika ukurasa wa 466]

Ujumbe huu wenye kutia tumaini uliomo katika makala hii umetolewa kama hotuba kubwa kwa hudhurio la jumla ya wasikilizaji 1,300,000 mpaka sasa katika sehemu nyingi za dunia

[Picha katika ukurasa wa 467]

Umoja wa Mataifa, kama tengenezo la amani na usalama, umeshindwa kutoa tumaini ambalo wanadamu wote wanaweza kulishiriki

[Picha katika ukurasa wa 468]

Tumaini la pekee la wanadamu wote​—kutia na yatima, wajane, wenye njaa, vipofu na watu walioonewa​—li katika serikali ya Mungu

[Picture katika ukurasa wa 472]

Shetani Ibilisi alimtolea Yesu falme zote za ulimwengu. Ulizo lilikuwa: Utawala wa kibinadamu au utawala wa kimungu?

[Picha katika ukurasa wa 473]

Yesu aliukataa utawala wa kibinadamu

[Picha katika ukurasa wa 473]

Konstantino alipowatolea maaskofu vyeo vya uwezo na ukuu katika Nicaea, kama maafisa wa dini ya Taifa la Kirumi, ni nani kwa kweli aliyekuwa akitoa toleo hilo​—Yesu Kristo au Shetani Ibilisi?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki