Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 5/1 kur. 207-212
  • Utawala wa Kimungu—Je! Sisi Tunauunga Mkono au Tunaupinga?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Utawala wa Kimungu—Je! Sisi Tunauunga Mkono au Tunaupinga?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NAMNA UTAWALA WA KIMUNGU UNAVYOONYESHWA SASA
  • MAANA YA KUUNGA MKONO UTAWALA WA KIMUNGU
  • Utawala wa Kimungu— Juu ya Wanadamu Mwanzoni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Utawala wa Kimungu—Tumaini la Pekee la Wanadamu Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Kwa Nini Tunahitaji Ufalme wa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2020
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 5/1 kur. 207-212

Utawala wa Kimungu​—Je! Sisi Tunauunga Mkono au Tunaupinga?

1. (a) Kufuata Gharika, utawala wa kibinadamu ulianza kutengenezwaje? (b) Uwezo wa Shetani kwa utawala juu ya wanadamu ulikuwa umefikilizwaje, na tuna ushuhuda gani kuonyesha kuwako kwa mashetani katika historia tangu wakati huo?

MAMBO YOTE ya hakika leo yanaonyesha kwamba wanadamu hawapendelei utawala wa kimungu. Hii ni kwa sababu kwa muda usiopungua karne mbili kufuata Gharika utawala wa kibinadamu ulianza kutengenezwa na viongozi wa kibinadamu katika kupingana na Yehova Mungu. Aliyekuwa mbaya sana katika hili alikuwa Nimrodi, mjenzi wa Babeli na Mnara wa Babeli. (Mwa. 10:8-12; 11:1-9) Kwa kufanya hivi, walikuwa wakileta wingi wa wanadamu, si chini ya utawala wenye kuonea, usiokamilika tu, bali vile vile chini ya utawala wa Kishetani. Uwezo wa Shetani Ibilisi ulitiwa nguvu sasa na wale “wana wa Mungu” wengine waliokuwa wameupinga utawala mkuu wa Mungu na wakawa wamechangamana katika kuoana na binti za wanadamu. Kama Shetani Ibilisi, hawa walikuwa wamejifanya wenyewe mashetani. Watu wa leo wenye kufikiria mambo ya kimwili yenye kuonekana wanaodhihaki kwamba Shetani Ibilisi na mashetani wake ni watu wa kuwazika tu hawawezi kufuta maandishi ya historia yote ya kale. Habari za kale, zilizoandikwa na zilizo katika mahekalu na magofu ya kidini zote zinashuhudia kwamba mataifa ya kale yaliabudu mashetani na waliongozwa nao. Kuna mashetani! Wako!

2, 3. (a) Habari kutoka kwenye chanzo gani chenye kutumainika ndiyo ya maana zaidi kuliko ushuhuda huo wa historia, na kinasemaje juu ya mashetani? (b) Ni shauri gani ambalo Paulo aliwaandikia Waefeso juu ya mashetani?

2 Zaidi ya hayo, Kitabu chenye kweli takatifu, Biblia iliyoongozwa na roho ya Mungu, kinatupa habari juu ya mashetani hawa na kiongozi wao, Shetani Ibilisi. Kitabu hicho kinatuonya juu ya hila, mipango ya ujanja na makusudi yenye werevu, ya watu hao wa kiroho, wakorofi na wasioonekana, ambao si wa damu na mwili. Watu leo, hata wale waliomo katika Kristendomu, hawalioni kwa uzito shauri ambalo mtume wa Kikristo Paulo aliwaandikia Wakristo wote katika barua yake kwa kundi la Efeso, akisema:

3 “Vaeni silaha kamili kutoka kwa Mungu mpate kuweza kusimama imara kushindana na hila za Ibilisi; kwa sababu sisi tuna kushindana mweleka, si juu ya damu na nyama, bali juu ya serikali, juu ya mamlaka, juu ya watawala wa ulimwengu wa giza hili, juu ya majeshi ya roho za uovu katika mahali pa kimbinguni.”​—Efe. 6:11, 12, NW.

4. (a) Maneno hayo yana maana gani juu ya utendaji wa Shetani wa kutengeneza, na hivyo Yesu na Paulo wanamwita Shetani nini? (b) Watawala wa kibinadamu wanaonaje juu ya kupangwa katika jamii hiyo, hata hivyo ni nani aliyewaweka hapo?

4 Je! tunafahamu maana ya hili? Maana yake Shetani Ibilisi analo tengenezo lisiloonekana, lenye kupita uwezo wa kibinadamu. Maana yake ameyatengeneza majeshi ya kiroho yenye uovu katika mahali pa kimbinguni kuwa “serikali,” kuwa “mamlaka,” kuwa “watawala wa ulimwengu wa giza hili.” Uwezo huu usioonekana uliotengenezwa ni wenye nguvu zaidi kuliko na mwungano wa mataifa ya kikomunisti yenye nguvu nyingi za kivita; ni wenye nguvu zaidi kuliko na mwungano wa mataifa ya kidemokrasi yenye utajiri mkubwa pamoja na nguvu zao zote za kivita. Yesu Kristo, ambaye yampasa kujua, alimwita Ibilisi, Shetani, “mtawala wa ulimwengu huu.” Mtume wa Kikristo Paulo alimwita Shetani “mungu wa taratibu hii ya mambo.” (Yohana 12:31; 14:30; 16:11; 2 Kor. 4:4, NW) Labda serikali za kidunia zitataka kutufunga vinywa kwa kusema jambo hili kama kuwadharau wao, lakini sisi tunatumia tu maneno ambayo Yesu Kristo na mtume wake Paulo wanasema katika kurasa za Biblia Takatifu. Wao hawataki waambiwe katika Neno la Mungu kwamba wamo katika jamii hiyo, lakini sio sisi tuliowaweka humo. Lakini, ikiwa wao hawapendelei utawala wa kimungu kupitia kwa Yehova Mungu, wanaweza kujikuta wenyewe wako wapi?

NAMNA UTAWALA WA KIMUNGU UNAVYOONYESHWA SASA

5. (a) Utawala wa kimungu unaonyeshwa kupitia kwa nani leo? (b) Katika siku za Yesu duniani, lilikuwa ulizo gani lililowaandama watu, na ulikuwa ugumu gani ambao iliwapasa wauondoe?

5 Utawala wa kimungu unaonyeshwaje leo, ili tupate kujua kama sisi tunauunga mkono au tunaupinga? Utawala wa kimungu sasa unaongozwa kupitia kwa ufalme wa Mwana wake mwaminifu, Yesu Kristo wa mbinguni. Kama Ayubu wa kale wa nchi ya Usi, Yesu Kristo kama mwanadamu mkamilifu mwenye damu na nyama duniani alivumilia majaribu makubwa zaidi kupita yote katika mikono ya Shetani Ibilisi na wajumbe wake wa kibinadamu duniani. Kwa hiyo alionyesha ukamilifu wake usiovunjika kabisa kwa Yehova Mungu kama Mtawala wa Kimungu. Ayubu hakufia mikononi mwa Shetani Ibilisi. Lakini Yesu Kristo alikufa kifo cha ukatili mikononi mwa kundi la Shetani duniani. Hii ilitukia nje ya kuta za Yerusalemu. Wakaaji wa Yerusalemu na wa majimbo ya Kirumi ya Kiyahudi na Galilaya walitiwa ndani. Kwa watu hawa wenye kufuata sana dini ulizo lililowaandama wakati huo lilikuwa, Utawala wa kimungu kupitia kwa Masihi wa Yehova Mungu. Ugumu mkubwa ambao watu hao waliokuwa wakimtafuta Masihi wa Yehova walipaswa kuuondoa ulikuwa huu: Je! Yesu mzao wa Mfalme Daudi ndiye Masihi aliyeahidiwa kwa muda mrefu au siye?

6. (a) Yale ambayo Yesu alisema na kufanya yalilingana namna gani na ambayo watu walimtazamia Masihi wa kweli kufanya? (b) Watu walitazamia nani kwa kuwaondolea ugumu wao wa Kimasihi, na walimpeleka Yesu kwa gavana mpagani kwa shtaka gani?

6 Tangu wakati wa kubatizwa kwake na Yohana Mbatizaji katika Mto Yordani mpaka kufa kwake miaka mitatu na nusu iliyofuata, watu waliopokea tumaini la Kimasihi hawakumtazamia Masihi au Kristo wakati wo wote kusema na kufanya mambo ambayo Yesu alisema na miujiza ambayo alifanya. Wao walitazamia kwamba Masihi angewakomboa kutoka katika utawala wa Mataifa au watu wasio Wayahudi tu na kuifanya nchi yao kuwa yenye kufanikiwa na taifa lao kuwa taifa kubwa duniani ambalo mataifa yasiyo ya Kiyahudi wangeendea makundi makundi. Ule ugumu haukuwa wa kiserikali tu bali vile vile ulikuwa zaidi wa kidini. Watu waliwatumaini viongozi wao wa kidini kuwaongoza katika kuondoa ugumu huu. Viongozi hawa walikatia wingi wa watu mashauri. Walimwona Yesu kuwa mwenye kumkufuru Mungu, Kristo wa uongo. Hata hivyo, ili wasizuiwe katika kumwua, walimpeleka Yesu kwa gavana wa Kirumi, Pontio Pilato. Kwa shtaka gani? Kwa shtaka la kuwa mfitini wa serikali, mwenye kujidai kuwa mfalme, si mfalme wa Milki ya Kirumi, bali mfalme wao, Mfalme wa taifa la Kiyahudi. Hivyo wakasingizia kuwa wakifanya urafiki na Milki ya Kirumi, kulinda faida zake, ingawa ni za kipagani.

7. (a) Watu waliokuwa mbele ya Pontio Pilato walisingizia kuwa rafiki za nani, kwa aibu ya Pilato? (b) Kwa kufanya hivyo, watu walikuwa wakichukua maoni gani juu ya utawala wa kimungu, kulingana na Yakobo 4:4?

7 Wakati Gavana Pilato aliposema mwenyewe kwa kutaka kumwacha Yesu huru kama asiyestahili kufa, watu walioongozwa na makuhani wao wakuu walijifananisha kama wakiwa rafiki za Tiberio Kaisari lakini Gavana Pilato hakuwa rafiki yake. Habari ya Biblia inatuambia hivi: “Pilato akatafuta kumfungua; lakini Wayahudi wakapiga makelele wakisema, Ukimfungua huyu, wewe si rafiki yake Kaisari; kila mtu ajifanyaye kuwa mfalme humfitini Kaisari.” Ndivyo ulizo lilivyofanywa kuwa la kisiasa, na watu hao walikuwa wakisema na kutenda kwa kupendelea kuwa rafiki​—za Mungu au za Kaisari mpagani? Za Mtawala wa kimungu au mtawala wa kibinadamu? Wasingeweza kuwa rafiki za Mungu na za Kaisari wakati mmoja, hata ikiwa walidai kwamba Yesu alikuwa Masihi au Kristo wa uongo. Yatupasa tufuate kanuni iliyoongozwa na roho ya Mungu, kama ilivyoandikwa katika Yerusalemu miaka fulani iliyofuata: “Je! ninyi hamjui kwamba urafiki wa ulimwengu maana yake ni uadui wa Mungu? Kwa hiyo, ye yote anayetaka kuwa rafiki ya ulimwengu anajifanya mwenyewe adui ya Mungu.” (Yak. 4:4, H. J. Schonfield, 1955) Basi, katika kujaribu kufanya urafiki na Kaisari mpagani juu ya ulizo hili la Masihi au Kristo, je! watu hao wa kidini walikuwa wakijionyesha wenyewe kuwa rafiki za utawala wa kimungu?

8. Watu wenyewe walijionyesha namna gani wakipendelea utawala wa kipagani wa kibinadamu kuliko utawala wa kimungu?

8 Mwisho watu walimaliza lile ulizo, wakati walipopiga makelele ili Yesu apigiliwe misumari, naye Pilato akapinga, akisema: “Je! nimsulibishe mfalme wenu!” Hapa walimkataa Yesu kama mfalme wa Kimasihi, kwa maana, kulingana na habari, “wakuu wa makuhani wakamjibu, Sisi hatuna mfalme ila Kaisari.” (Yohana 19:12-15) Hakuna mtu awezaye kukana kwamba hapa hawakuchagua utawala wa kibinadamu wa kipagani. Kwa lazima hii iliwaweka katika kuupinga utawala wa kimungu.

9. (a) Ili kuonyesha ushuhuda kwamba Yesu alikuwa Masihi, Mungu alifanya nini siku ya tatu? (b) Sasa, kwa wakati unaofaa, ni nani anayetolewa kwa ulimwengu wote kama Mfalme wa Kimasihi, na Utawala wake ni wa namna gani?

9 Mambo ya hakika yote yaliyoandikwa yanaonyesha kwamba Yesu alitimiza unabii wa Biblia juu ya Masihi au Kristo aliyeahidiwa. Ndiyo sababu Mungu Mwenye Nguvu Zote alimfufua kutoka kwa wafu siku ya tatu na akamtukuza katika mkono Wake mwenyewe wa kuume mbinguni. Sasa yeye ni Masihi au Kristo wa kimbinguni. (Matendo 1:1 mpaka 2:36; 13:26-39; 1 Pet. 3:18-22) Na sasa, karne kumi na tisa nyuma, kama vile Gavana Pilato alivyomtoa Masihi kwa wenye kuadhimisha Sikukuu ya Kupitwa katika Yerusalemu katika mwaka wa 33 C.E., vivyo leo Mungu Aliye Juu Zaidi Yehova anamtoa Masihi au Kristo wake kwa ulimwengu mzima wa wanadamu. Huu ndio wakati wa kufanya hivi. Muda mrefu unaotajwa kama “majira ya Mataifa” au “nyakati zilizowekwa za mataifa” ulimalizika katika mwaka wa 1914 wa karne yetu ya ishirini, mwaka ulioonyeshwa kwa kutokea kwa ghafula kwa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza. (Luka 21:24; Dan. 4:16, 23, 25) Ufalme wa nyumba ya kifalme ya Mfalme Daudi uliopinduliwa na majeshi ya kipagani ya Babeli katika mwaka wa 607 B.C.E. sasa umesimamishwa tena, si duniani kama utawala wa kibinadamu, bali mbinguni mikononi mwa mwa Masihi wa kweli, Kristo wa Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote Yehova.

10. (a) Tangu mwaka wa 1914 C.E., tunasikia kwa imani maneno gani yakivuma kutoka mbinguni juu ya ufalme wa ulimwengu? (b) Kwa vita vya ulimwengu na kwa uanachama katika Umoja wa Mataifa Kristendomu amejionyeshaje mwenyewe kuwa anapendelea utawala wa kibinadamu?

10 Kwa imani masikio yetu yanaweza kusikia, tangu mwaka wa 1914 C.E., sauti mbinguni zikisema sana maneno yaliyoandikwa katika kitabu cha mwisho cha Biblia hivi: “Ufalme wa ulimwengu ukawa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atatawala kama mfalme milele na milele.” (Ufu. 11:15, NW) Huo “ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake” haumaanishi Kristendomu​—hata kidogo! Unamaanisha serikali ya kifalme ya kimbinguni ya Masihi au Kristo ambaye ametiwa mafuta na Bwana Mungu Yehova amwakilishaye Yeye katika kuwatawala watu wote wa dunia. Kulingana na jina lake la kidini, ingempasa Kristendomu aunge mkono ufalme huo wa Mungu wa Kimasihi, lakini je! anafanya hivyo? Majira ya Mataifa yalipomalizika katika mwaka wa 1914, je! Kristendomu aliupigania ufalme wa Kimasihi wa mbinguni au alipigania utawala wa ulimwengu kupitia kwa utawala wa kibinadamu? Ebu utazame Ushirika wa Mataifa na Umoja wa Mataifa wa sasa, matengenezo yote mawili ambayo Kristendomu alianzisha na kutia nguvu na kuendeleza leo. Je! matengenezo hayo yanatetea utawala wa kimungu kupitia kwa ufalme wa Kimasihi wa mbingu au yanatetea utawala wa kibinadamu? Zaidi ya nusu ya wanachama wa Umoja wa Mataifa ambao hawajidai kuwa mataifa ya Kikristo wanasemaje katika kujibu? Wanasema hivi: ‘Hapana! Umoja wa Mataifa hautetei utawala wa kimungu kwa njia ya ufalme wa Kimasihi wa mbinguni! Unatetea utawala wa kibinadamu wa dunia yote. Sisi wanadamu tutaitawala kwa namna zetu za serikali za kujichagulia wenyewe.’ Kwa akili, basi, kwa kuwa yeye yuko upande wa Umoja wa Mataifa, Kristendomu anaunga mkono utawala wa kibinadamu (si wa kimungu.)

MAANA YA KUUNGA MKONO UTAWALA WA KIMUNGU

11. Kwa habari ya mwendo wake tangu mwisho wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza katika mwaka wa 1918, kwa sababu gani Kristendomu hana msamaha juu ya kutojua, na hivyo je! watu wamtazamie kwa uongozi unaofaa juu ya kuchagua utawala?

11 Kristendomu ameonekana mwongo kwa jina lake, na hana msamaha. Tangu mwaka ule wa maana sana wa 1914, na zaidi tangu mwisho wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza katika mwaka wa 1918, ufalme wa Kimasihi wa Mungu kama serikali iliyosimamishwa katika mbingu umekuwa ukihubiriwa. Huu umekuwa utimizo wa maneno ya Yesu Kristo juu ya ishara ambayo kwa hiyo “mwisho wa taratibu ya mambo” ungejulikana, yaani: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo mwisho utakuja.” (Mt. 24:14, NW) Kwamba Kristendomu anajua kwamba hizo “habari njema” zinahubiriwa inaonyeshwa kwa kupinga kwake, hata kuwatesa na kuwazuia wahubiri wa “habari njema” hizo. Kwa hiyo, kuchagua kwa Kristendomu utawala wa kibinadamu pamoja na serikali za dunia zisizo za Kikristo hakukufanywa kwa kutokujua na bila kuwa na Biblia Takatifu. Kwa sababu hii, wanadamu hawawezi kumtazamia Kristendomu kwa usalama kuwaongoza katika kufanya uchaguzi mzuri, kuliko Wayahudi wasivyoweza kuwatazamia makuhani na waalimu wao karne kumi na tisa zilizopita.

12. Ni ulizo gani ambalo ni la maana sana leo, na kwa sababu gani uchaguzi ni wa haraka sana kwetu kufanya?

12 Ulizo la maana sana leo si Ukomunisti au demokrasi yenye utajiri mkubwa​—ni utawala gani utakaotawala? maana zote hizi mbili ni namna tu za utawala wa kibinadamu. Bali, ni hili: Utawala wa kibinadamu kupitia kwa wanadamu wasiokamilika, wenye dhambi, wenye kufa na wasiopatana na Yehova Mungu, au utawala wa kimungu kupitia kwa ufalme wa Kimasihi wa Yesu aliyefufuka, Mwana-Kondoo wa Mungu aliyefia wanadamu wote kama dhabihu? Leo uchaguzi unatakiwa kufanywa kwa haraka zaidi kuliko ilivyokuwa miaka mia kumi na tisa iliyopita wakati Yesu Kristo alipotolewa na Gavana Pilato kwa makutano ya wenye kuadhimisha Sikukuu ya Kupitwa katika Yerusalemu. Leo sisi tuko karibu sana na kumalizika kwa kipindi cha “mwisho wa taratibu ya mambo.” Karibu utawala wa kibinadamu kupitia kwa wanadamu wasiokamilika, wenye dhambi, wenye kufa utaondolewa kabisa kutoka katika uso wa dunia katika “dhiki” ya wanadamu iliyo kubwa kuliko zote iliyotabiriwa katika unabii wa Biblia.

13. Kwa sababu gani haimtendei mtu wema kuendelea kuupinga utawala wa kimungu, na ni nini kinachofanya shauri hili liwe zito sana kwa wapinzani?

13 Haitutendei mema, na haitatokeza matokeo mazuri, ikiwa sisi tunaupinga utawala wa kimungu. Utawala wa kimungu kupitia kwa Mwongozi Mwenye Nguvu Zote wa “mpango” mkubwa ajabu ambao dunia yetu ni sehemu ndogo sana utakuja hata iweje na kuchukua dunia nzima. Kinachofanya shauri hili liwe zito sana ni kwamba wale ambao wanaendelea kuupinga utawala wa kimungu, wataharibiwa kama adui katika dhiki ambayo kwa hiyo taratibu hii ya mambo itakwisha.​—Mt. 24:21, 22; Dan. 2:44.

14. (a) Kuchagua utawala wa kibinadamu vile vile kunamaanisha kuchagua utawala gani mwingine, na ni jambo gani litakaloupata utawala huu wa pili? (b) Kuchagua utawala wa kimungu wa milele hakuna maana ya nini juu ya maoni yetu juu ya serikali zilizopo za kibinadamu na vyama?

14 Tusisahau jambo hili baya sana: Kuchagua utawala wa kibinadamu kwa wakati uo huo kunamaanisha kuchagua utawala wa Kishetani, kuendelea kwa utawala wa wanadamu kupitia kwa “mungu wa taratibu hii ya mambo.” Wakati taratibu hii ya kibinadamu ya mambo itakapoharibiwa, Yehova Mungu kupitia kwa Masihi wake atazuia Shetani na jeshi lake la mashetani wasiendeleze utawala wao usioonekana juu ya wanadamu duniani. (Ufu. 20:1-3) Basi, je! tutachagua kitu ambacho kwa kitambo kidogo tu kitaharibiwa? Lo! ni hekima zaidi kama nini katika wakati huu wenye maana sana kuchagua kitu kitakachokuwa cha milele​—utawala wa kimungu! Kuunga mkono utawala wa kimungu sasa wakati “dhiki kubwa” haijaja hakumaanishi kwamba tutakuwa wapinduzi wenye jeuri na kujaribu kuzipindua serikali zilizopo za kisiasa na vyama vingine vya kibinadamu kwa nguvu. Hapana, kwa maana Yehova Mungu anawakataza sana mashahidi wake wa Kikristo duniani kufanya hivyo. (Rum. 12:17 mpaka 13:7) Kuliko kuchagua kuinua mkono wenye jeuri juu ya serikali za kibinadamu ambazo Mungu ameruhusu ziweko mpaka sasa, wataendelea kwa upole kupata mateso makali mikononi mwa watawala wa kibinadamu wa kisiasa.

15. (a) Kwa kuvumilia mateso hayo yasiyo ya haki bila kuona uchungu, watashika nini, kama Ayubu na Yesu walivyoshika? (b) Wanatafuta nini kwanza, na inawapasa wahubiri nini, kwa muda gani?

15 Kwa kuvumilia mateso hayo yasiyo ya haki bila kumwonea uchungu Mungu Mwenye Nguvu Zote anayeyaruhusu, wanashika ukamilifu wao kwa Yeye, kama vile Ayubu mvumilivu na Bwana Yesu Kristo walivyofanya, wakijifurahisha sikuzote dhamiri safi kwa Mungu na kwa wanadamu. (Matendo 23:1; 1 Pet. 2:19, 20) Ili kuonyesha maoni yao na uchaguzi ambao wamefanya, wanatafuta kwanza ufalme wa Baba yao wa kimbinguni na haki Yake kuliko kujishughulisha na siasa za kibinadamu na kushiriki ndani yake. Mtawala wa Kimungu amewapa “habari njema za ufalme” wazihubiri kila mahali. Hivi ndivyo wanavyofanya kwa utii mpaka Mungu mwenyewe kupitia kwa Yesu Masihi atakapoisimamisha kabisa serikali hiyo ya kimungu, pasipo kupingwa na kutawala juu ya dunia yote.​—Mt. 6:33; 24:14.

16, 17. (a) Yehova Mungu atawafanyia nini wale wanaochukua mwendo huo wa uaminifu? (b) Kuchunguza sasa kwa Yehova mioyo yote ya kibinadamu kutaamua nini, na wale wanaochagua uzima katika taratibu Yake ya Kimasihi wataitikia maneno gani ya Daudi?

16 Wale wanaochukua mwendo huu ndio hao Mwenye Enzi Yote ya Ulimwengu Wote Bwana Yehova ataokoa katika “dhiki kubwa” inayokaribia na kuingia katika taratibu Yake mpya ya haki yenye dunia ya Paradiso. Sasa anapoichunguza mioyo ya kibinadamu, anatutazamia sisi tuonyeshe kwa neno la mdomo na kwa tendo lisilo la unafiki uchaguzi ambao tumefanya juu ya utawala. Je! sisi tunauunga mkono utawala wa kimungu juu ya dunia yote na vile vile mbinguni, au tunaupinga? Mtawala wa Kimungu anawachagua kwa uzima katika taratibu yake mpya ya Kimasihi wale wanaoitikia maneno ya Mfalme Daudi aliyeongozwa na roho ya Mungu, aliyeketi katika “kiti cha enzi cha [Yehova]” katika Yerusalemu:

17 “Yehova mwenyewe ameweka imara kiti chake cha enzi katika mbingu zenyewe; na juu ya kila kitu ufalme wake mwenyewe umetawala. Mtukuzeni Yehova, Enyi malaika zake, mlio hodari katika nguvu, wenye kutimiza neno lake, kwa kusikiliza sauti ya neno lake. Mtukuzeni Yehova, enyi majeshi yake yote, ninyi wahudumu wake, mnaofanya mapenzi yake. Mtukuzeni Yehova, enyi kazi zake zote, katika mahali pote pa utawala wake. Mtukuze Yehova, Ee nafsi yangu.”​—Zab. 103:19-22, NW.

18. Kwa msaada wa maneno hayo ya mtunga Zaburi, sisi tunajibuje ulizo juu ya utawala?

18 Utawala wa kimungu wa Yehova Mungu kupitia kwa Yesu Kristo​—Je! sisi tunauunga mkono au tunaupinga? Pamoja na malaika wote wa Yehova, hodari katika nguvu, pamoja na majeshi yake yote ya kimbinguni, pamoja na wahudumu wake wote, sisi tunajibu kwa nguvu, Sisi tunauunga mkono Utawala wa Kimungu sasa na milele na milele.​—Kutoka The Watchtower, Nov. 1, 1972.

[Picha katika ukurasa wa 209]

Wayahudi walipomkataa Yesu kama mfalme wao kwa kupendelea Kaisari, walichagua utawala wa kibinadamu. Leo Yehova anamtoa Masihi wake kwa wanadamu wote; wewe utafanya uchaguzi gani?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki