Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 4/1 kur. 154-162
  • Dhamiri Yako na Kazi Yako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Dhamiri Yako na Kazi Yako
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MICHEZO YA BAHATI
  • MATUMIZI NA UFANYIZAJI WA VILEO VYENYE HATARI
  • KUTUMIA KANUNI ZA BIBLIA KWA UGUMU
  • ACHA DHAMIRI YAKO ISEME
  • ‘ENENDA KWA ADABU MBELE YA WALE WA NJE’
  • UHITAJI WA IMANI
  • KUWA NA KIASI NA USAWA
  • ‘Kujipendekeza Wenyewe kwa Kila Dhamiri ya Kibinadamu Machoni pa Mungu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Je! Wewe Unaongozwa na Dhamiri Nyepesi ya Kikristo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Kufaidika na Dhamiri Yako Uliyopewa na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Kuendelea Kuwa na Dhamiri Njema
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 4/1 kur. 154-162

Dhamiri Yako na Kazi Yako

1. Kwa sababu gani kazi ya Mkristo ni sehemu ya lazima kwa kutumia dhamiri yake?

KARIBU saa zetu zote za kila siku zinatumiwa kwa kazi. Kwa hakika imempasa Mkristo atake kuwa na dhamiri safi juu ya kazi ambayo anafanya, ‘akifanya mambo yote kwa utukufu wa Mungu.’ (1 Kor. 10:31) Je! kazi yako inakuruhusu ufanye hivyo?

2, 3. (a) Ni kazi gani ambayo kwa waziwazi ni mbaya, na je! Mkristo mwenye kuingia kazi hiyo anaweza kuepuka daraka? (b) Namna fulani za kazi ambazo peke yazo si mbaya zaweza namna gani, hata hivyo, kutokeza maulizo ya dhamiri?

2 Kwa wazi, kazi yo yote ambayo kwa wazi na zaidi inataka mtu atende matendo ambayo kwa wazi yanalaumiwa na Neno la Mungu au hayapatani na kanuni zake ni mbaya. Mkristo hawezi kuweka daraka la kosa juu ya tajiri wake. Lakini namna gani ikiwa kazi peke yake haipingani na Neno la Mungu lakini ni sehemu ya tendo ambalo makusudi yake hayapatani na Neno la Mungu? Hapo itakuwaje?

3 Kama mfano ulio mwepesi, kufanya kazi ya kuendesha motokaa peke yake ni kazi inayofaa. Lakini mtu anayejidai kuwa Mkristo angewezaje kutumikia kama mwendeshaji wa motokaa ya genge la wanyang’anyi wa benki? Au Mkristo angewezaje kujishirikisha na nyumba ya umalaya kwa kutumika kama mlinzi au mjakazi? Lakini, kwa upande mwingine, namna gani ikiwa ungekuwa na watu ambao unapelekea maziwa au magazeti; je! kupeleka kwako maziwa au magazeti kwenye nyumba ya umalaya kungekufanya uwe sehemu ya umalaya?

4. (a) Ikiwa mtu au biashara ni yenye kufanya mabaya, je! utumishi wote unaotolewa kwa mtu au biashara hiyo unamfanya kwa lazima mwenye kutoa utumishi kuwa mwenye kusaidia makosa hayo? (b) Ni mfano gani ambao Mungu mwenyewe anatupa sisi juu ya utoaji wa utumishi fulani kwa wakosaji bila kuwa mshiriki wa matendo yao?

4 Kwa wazi kuna tofauti kati ya kuwa msaidizi wa matendo mabaya na kuwa mtu anayetoa tu utumishi kama ule ambao watu wote wanatolewa kwa kawaida, bila kumbagua huyu au huyu. Tunao mfano wa Mungu mwenyewe juu ya kutoa utumishi kwa mahitaji ya kipekee bila kufikiria haki ya watu au kukosa kwao haki. Kama Yesu alivyoeleza wanafunzi wake, Yehova Mungu “huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.” (Mt. 5:45) Paulo, vile vile, anasema kwamba Mungu Muumba “ndiye anayewapa wote [bila kubagua] uzima na pumzi na vitu vyote.” (Matendo 17:25) Kwa kuwa Mungu anaruhusu mvua iangukie hata juu ya mashamba ya waovu, je! hili linamfanya yeye ashiriki hatia ya kosa lao? Kwa mfano, wakati Mungu alipowavika wenye dhambi Adamu na Hawa mavazi, je! kwa kufanya hivyo alifanya mwenyewe kulaumika juu ya kuachilia au kuwaunga mkono katika kosa lao? Bali, tendo lake lilikuwa la fadhili zisizostahili tu.​—Mwa. 3:21.

5, 6. (a) Ni katika njia gani Wakristo waliweza kufanya utumishi katika watu wa nyumbani mwa Kaisari na bado wakawa na dhamiri njema? (b) Hali zinazofanana zinawezaje kuwako katika nyakati za kisasa?

5 Katika barua yake kwa Wakristo katika Filipi, Paulo anapeleka salamu kutoka kwa ndugu zao za Kikristo “walio wa nyumbani mwa Kaisari.” (Flp. 4:22) Kwa wazi hawa walikuwa watumishi wa nyumbani katika makao ya kifalme, kwamba walikuwa watumwa au watu huru maandishi hayaonyeshi. Labda walitoa utumishi wa kibinadamu humo, kama vile kupika, kufagia na kazi inayofanana, kwa ajili ya jamaa na washiriki wa kifalme. Kama tulivyokwisha kuona, serikali za kibinadamu zinafanya kazi fulani ambazo ni za halali machoni pa Mungu, ijapokuwa vile vile zina hatia ya mazoea mengine yenye kulaumika. (Rum. 13:1-5) Bila kujali kazi yo yote ambayo Wakristo hawa wa nyumbani mwa Kaisari walifanya, kwa wazi hawakuifanya bila kujiona kwamba walikuwa washiriki katika siasa, dini au shughuli na mipango ya kijeshi ya Nero.

6 Ndivyo na katika nyakati za kisasa. Kuna matendo mengi ambayo tunaweza kuwatendea wengine yanayotolewa kwao kama wanadamu wenzetu tu, bila kufikiria sana haki yao au kutokuwa na haki. Kama katika mfano wetu mwepesi, kumwuzia malaya maziwa kulingana na akili kusingemfanya mtu atazamwe kama anakubaliana na umalaya wake, sivyo? Wala kuajiriwa kwa mtu kazi na mwanasiasa ili amfundishe kupiga muziki kulingana na akili kusingemwonyesha mtu huyo kuwa anaunga mkono matendo ya siasa ya tajiri wake.

7, 8. Neno la Mungu linaonyeshaje akili na maoni yanayofaa, na hili limepaswa lituongoze sisi namna gani katika kutumia kwetu kwa kanuni za Biblia katika mambo ya dhamiri?

7 Ijapokuwa ni mwenye kushikamana sana na haki, Yehova Mungu vile vile ni mwenye kutumia akili. (Yak. 3:17) Yeye ni mwenye kutumia njia inayofaa katika kukadiria kwake kwa mambo na katika matakwa yake kwa wale ambao wangempendeza yeye. Hii inaonekana katika maneno ya mtume Paulo yaliyoongozwa na roho ya Mungu katika 1 Wakorintho 5:9, 10. Akiisha kuwakumbusha Wakristo katika Korintho maagizo yake ya kwanza ‘wasichangamane na wazinzi,’ ndipo Paulo aliposema hivi, “sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang’anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia.” Ijapokuwa Wakristo wanataka kuepuka ‘mashirika mabaya yanayoharibu mazoea mazuri,’ hawawezi kuwa kama watu wanaokaa hali ya kujitenga na wengine, wakijitenga wenyewe katika mapango, jangwani au visiwani. Kwa sababu gani sivyo? Agizo lao la kutumikia kama “nuru ya ulimwengu” linawataka wawe ‘katika ulimwengu wangawa si sehemu ya ulimwengu.’ (1 Kor. 15:33, NW; Mt. 5:14-16; Yohana 15:19; 17:15-18) Kuwataka watimize agizo lao na wakati ule ule wajitenge kabisa ingekuwa kutaka mambo yaliyo tofauti kwao. Mungu hafanyi hivi. Wala sisi haitupasi tuwe wasio na akili katika kutumia kwetu kwa kanuni za Neno la Mungu, kujaribu kuitumia kila kanuni kupita kadiri na halafu kusisitiza kwamba ndugu zetu wote wafanye hivyo.​—Flp. 4:5.

8 Kwa kukumbuka mambo haya, na tuangalie namna fulani za utendaji tupate kuona kama hizi zinalaumiwa na Biblia kama zisizo za Kikristo kabisa au ndiyo mambo ambayo ni juu ya kila dhamiri kuamua ambalo inampasa Mkristo afanye, au dhamiri itajitia katika shauri hilo kwa kadiri gani.

MICHEZO YA BAHATI

9, 10. Je! Biblia inatoa amri ya waziwazi juu ya kucheza kamari, na kwa sababu gani huenda upinzani ukatokea juu ya kukuita namna ya “unyang’anyi”?

9 Kucheza kamari (gambling) hakutajwi waziwazi katika Biblia. Basi, Mkristo ataonaje juu yake?

10 Huenda wengine wakashirikisha mchezo huu na unyang’anyi, unaotajwa katika 1 Wakorintho 6:10. Walakini, huenda kukawa na upinzani wa kwamba “kunyang’ anya” kunakuwa na maana ya msingi ya kutumia nguvu, maogofyo au mkazo mwingine (kama vile kwa kutumia vibaya kwa mamlaka ya serikali) ili kupata kitu fulani kutoka kwa mtu asiyetaka. Ijapokuwa watu wanaopoteza fedha katika kucheza kamari hawapendezwi kuipoteza, kwa desturi wanacheza kamari kwa kutaka na kwa kujua sana kwamba wanapata hasara ya kupoteza fedha. Hivyo, basi, ikiwa kucheza kamari si unyang’anyi, Mkristo angekataa kukubali mchezo huu juu ya msingi gani?

11, 12. (a) Ni kanuni gani za Maandiko zinazotoa msingi kwa sauti ya dhamiri kusema juu ya kucheza kamari? (b) Matokeo ambayo kwa historia kucheza kamari kumefanyiza kwa watu yanaonyesha nini?

11 Kuna zaidi ya sababu moja ya Maandiko kwa kufanya hivyo. Kwa hakika kucheza kamari kunastahili kupangwa katika namna ya “tamaa,” na tamaa na kutamani vinapangwa pamoja na ibada ya sanamu katika Neno la Mungu. (1 Kor. 6:9, 10; Kol. 3:5) Mchezo wa kamari unapingana sana na agizo la msingi la Maandiko la kwamba imetupasa tumpende jirani yetu kama tunavyojipenda wenyewe, na ya kwamba inampasa mtu afanye kazi ya uaminifu, yenye kuleta matokeo ili ajipatie mapato. Ni matokeo gani yanayotokana na mchezo wa kamari? Historia yake inaonyesha kwamba unasababisha sana uvunjaji wa sheria katika namna moja au namna nyingine. Na kwa sababu gani? Kwa sababu si wenye upendo. Unachochea choyo na kufanyiza kukosa kuwafikiria wengine. Mcheza kamari anataka fedha za wengine bila yeye naye kuwapa utumishi wo wote wa kweli. Ijapokuwa huenda wengine wakaupanga mchezo wa kamari pamoja na tafrija au mchezo wa kujifurahisha, ushahidi unaonyesha kwamba mara nyingi sana unafanyiza matata, mashaka, kuudhika na hata hasira ya uuaji.

12 Mwanamke mmoja aliyekuwa akifanya kazi katika nyumba mnamofanyiwa michezo ya kamari alisema hivi: “Kucheza kamari kunawashupaza wote wanaoshirikiana nako. Baada ya mwaka mmoja hivi wa kufanya kazi katika nyumba ya kamari, mgawa karata hapendezwi tena na mambo yanayofanywa na wanaume na wanawake, wengi. kati yao ni wenye wazimu, wakipoteza fedha katika kamari ambazo zapaswa zitumiwe katika kujipatia wenyewe na jamaa zao riziki. Mojawapo la mambo ya ulimwengu ambayo ni yenye kuhuzunisha sana na ya kikale zaidi kuliko yote​—uharibifu wa maisha zisizo na hesabu za kibinadamu kwa sababu ya tamaa ya mwanadamu ya fedha pasipo jasho na kurushwa kwa akili zake na mungu mke wa uongo, Mama Bahati​—sasa haumsikitishi [mgawa karata].”

13. Jambo gani linaonyesha kwamba kuunganisha kwa Maandiko tamaa na kutamani pamoja na ibada ya sanamu ni sawasawa na kucheza kamari?

13 Ndiyo, mchezo wa kamari unafanyiza vile vile ushirikina, wacheza kamari kama jamii wakiwa kati ya watu ambao ni wenye ushirikina kuliko wote. Fedha inakuwa sanamu na Mama Bahati mungu mke. Katika Isaya 65:11 Neno la Mungu linasema juu ya wale wanaomwacha Yeye na “kuandika meza kwa ajili ya [mungu] Bahati, na kuijazia [mungu] Ajali vyombo vya divai iliyochanganyika.”

14. Kutofautisha na mwendo wa kutamani wa mcheza kamari, ni onyo gani linalofanywa kwa Wakristo?

14 Kwa hakika yote haya yanatofautiana kabisa na onyo la mtume kwa Wakristo katika Thesalonike “mjitahidi kutulia . . . na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe . . . ili mwenende kwa adabu mbele yao walio nje, wala msiwe na haja ya kitu cho chote.” (1 The. 4:11, 12) Ndiyo, zingali ziko kanuni za ustahifu katika ulimwengu wa wanadamu juu ya kufanya kazi ya uaminifu, yenye matokeo, na Mkristo atataka ‘ajipendekeze mwenyewe kwa kila dhamiri ya kibinadamu’ katika shauri hili kama katika mambo mengine yote.​—2 Kor. 4:2.

MATUMIZI NA UFANYIZAJI WA VILEO VYENYE HATARI

15-17. (a) Ni mazoea gani yanayohusu matumizi ya tambuu yako katika maeneo fulani ya dunia? (b) Ni matokeo gani yanayofanyizwa na haya juu ya mtumiaji, na mamlaka katika nchi fulani zimeonaje mazoea haya?

15 Jambo jingine lenye kusikitisha katika sehemu nyingi za dunia ni matumizi na ufanyizaji wa vitu vinavyotokeza mazoea yenye hatari. Kwa mfano, katika India, Philippines na maeneo ya Malaysia mazoea ya kale na yenye kupendwa na watu wengi ni kutafuna tambuu, ambayo vile vile inajulikana kama popoo, mbegu ya mpopoo au mtambuu. Vipande vya tambuu vinakunjwa katika jani linalopakwa chokaa na kutafunwa. Tambuu inafanya utembe au mate ya mtu kuwa mekundu sana na kuchafua meno, kwa kawaida kuyafanya yaoze. Watu wengi ambao wamezoea kutafuna tambuu wanakuwa vibogoyo au bila meno mapema wakiwa na umri wa miaka 25. Kulingana na Encyclopedia Americana (1956, Vol. 20, ukur. 573), kutafuna tambuu kunafanyiza “matokeo yanayofanana na ya kutafuna tumbako.” Kwa kweli, katika India mara nyingine tumbako inatiwa katika tambuu, mchanganyiko unaojulikana kama pan au uraibu.

16 Bombay Evening News la Aprili 4, 1972, linatuambia kwamba Extra Pharmacopia, kitabu cha Pharmaceutical Society ya Uingereza, kinapanga tambuu katika namna ya “dawa zenye kulevya.” Kwa hiyo korti ya Kihindi iliamuru kwamba tambuu isingeweza kupangwa katika namna ya “chakula.”

17 Kwa wazi, watu wengi ambao wametumia tumbako na tambuu wanasema kwamba, kati ya hivi viwili, wameona mazoea ya kutafuna tambuu ni magumu zaidi kuvunja. Wakati wa utawala wa Kijapani juu ya Taiwan, jitihada ilifanywa ili kuondoa kabisa mazoea haya lakini haikuwa na matokeo. Madaktari wengi wa Kitaiwani wanasadiki kuna uhusiano kati ya mazoea haya na donda baya sana la kinywani na usoni linalowapata watu wengi katika Taiwan.

18. Ni mazoea gani yanayofanana yaliyoko katika nchi za Latin-America, na matokeo yake ni nini?

18 Katika nchi fulani za Latin-America kuna mazoea yanayofanana kidogo na hayo, yale ya kutafuna majani ya mmea unaoitwa coca pamoja na chokaa. Kwa kuwa majani yana kileo, tabia hii inaleta mazoea mabaya. Ijapokuwa inazuia watumiaji wasione ukali wa njaa au kuchoka, mwisho inaharibu sana afya yao na vile vile akili zao kama dawa nyingine zenye vileo.

19. Ushuhuda wa kisasa unaonyesha nini juu ya matumizi ya tumbako katika kuvuta na tambuu?

19 Matumizi ya tambuu na majani mengine hayaenei ulimwenguni pote. Kwa upande mwingine, matumizi ya tumbako karibu yanaenea ulimwenguni pote. Nayo vile vile, ni yenye kuleta mazoea mabaya. Ushuhuda unaoonyesha nguvu ya mazoea yake mabaya unaweza kuonwa kwa vile kufanyizwa kwa tumbako kungali kunafikia karibu uzito wa bilioni tatu na nusu kila mwaka​—ijapokuwa maonyo ya utabibu juu ya uharibifu ambao inaleta kwa afya ya kibinadamu. Kwa mfano, katika United States sigareti kama bilioni 576 na sigara milioni 7 zinatengenezwa kila mwaka. Hata hivyo halmashauri iliyowekwa na Surgeon General ya United States iligundua kwamba hatari ya ugonjwa wa mapafuni ilikuwa kubwa zaidi mara 10 katika watu ambao si wavutaji sana wa tumbako, na kubwa zaidi mara 20 katika watu ambao ni wavutaji sana, kuliko watu wasiovuta. Dr. Charles Cameron wa American Cancer Society alisema hivi: “Ugonjwa wa mapafuni unaongezeka kwa haraka zaidi sikuzote kuliko ugonjwa wo wote usioambukia katika historia ya utabibu.” Vile vile kuvuta tumbako kuliripotiwa kama kukisaidia kuleta ugonjwa wa moyo, mkamba na uvimbe wa mapafuni kwa sababu ya moyo kutofanya kazi sawasawa. Kwa sababu hiyo, serikali mbalimbali zimetunga sheria za kukataza kuwatangazia watu wote juu ya sigareti.

KUTUMIA KANUNI ZA BIBLIA KWA UGUMU

20. Kwa kuwa hakuna moja ya mazoea haya yanayotajwa katika Biblia, je! hii inayaondoa katika kuwa maulizo ya dhamiri ya Kikristo?

20 Tena, Biblia haitaji juu ya kutafuna tambuu au uraibu, kutumia ugolo au kuvuta tumbako. Watu wengine wamesema hivi: “Usiponionyesha jambo fulani katika Biblia juu ya matumizi ya tumbako [au vitu vingine vinavyofanana], mimi nitaendelea kuitumia.” Lakini je! si sawasawa na mtu kusema kwamba, kwa kuwa Biblia haikatazi waziwazi kutupa takataka katika uwanja wa nyumba ya jirani yako, si vibaya kufanya hivyo?

21, 22. Ni kanuni gani za Biblia zinazotiwa ndani wazi-wazi, na ni maulizo gani ambayo inampasa Mkristo ajiulize mwenyewe kwa dhamiri juu ya kushiriki katika mazoea hayo?

21 Kwa hakika Biblia inatupatia sisi kanuni za kutuongoza katika jambo hili. Mtume mwenye kuongozwa na roho ya Mungu aliandika katika 2 Wakorintho 7:1 hivi: “Wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo [za kukubaliwa na Mungu kama watoto na watumishi wake waliokubaliwa], na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu.”

22 “Utakatifu” unamaanisha hali ya kuwa safi, yenye kutakata, isiyo na madoa na kutolewa kwa matumizi matakatifu. Je! matumizi ya tambuu na matokeo yake machafu kinywani na katika meno ya mtumiaji, au uchafu unaojulikana kuwa unaletwa na tumbako kwa mwili wa mtumiaji, yanaweza kupatana na shauri hili la Maandiko? Amri iliyo kubwa kuliko amri zote ni ‘kumpenda Mungu kwa moyo wetu wote, nafsi, akili na nguvu.’ Je! unaweza kusema unamtumikia Mungu kwa ‘nguvu zako zote’ na huku unatumia vitu ambavyo hata serikali za kitaifa zinalaumu sana kuwa vinaharibu sana afya ya mtu? Au, ikiwa mtu anakuwa mwenye kuzoea kutafuna tambuu, je! anaweza kusema anamtumikia Yehova kwa ‘akili zake zote’? Kwa kweli, je! kutumia vitu hivyo siyo kutenda ‘tofauti na asili,’ kuutumikisha mwili vibaya kwa namna ambavyo haukukusudiwa ufanywe?​—Marko 12:29, 30; Rum. 1:26.

ACHA DHAMIRI YAKO ISEME

23, 24. (a) Je! ni matumizi ya kipekee ya vileo vyenye hatari tu ndiyo yanayoamsha maulizo ya dhamiri ya Kikristo? (b) Je! uhakika wa kwamba mazao haya ya mimea yanatokana na kuumba kwa Mungu unaondoa kupinga kote juu ya kufanyizwa na kugawanywa kwayo kwa kibiashara leo? Onyesha mfano.

23 Namna gani, basi mtu anayelima, anayetengeneza au kuuza vitu hivyo kama njia yake ya kupatia riziki? Kwa hakika hili ni shauri la dhamiri. Ni kanuni gani ambazo zimepaswa zituongoze sisi?

24 Labda watu wengine watabisha kwamba vitu hivi vyote ni sehemu ya uumbaji wa Mungu uliofanywa hapa duniani, na kwa hiyo hakuna sababu ya kumkataza mtu ye yote kulima vitu hivyo. Kweli, vitu hivi ni kuumba kwa Mungu, lakini vitu ambavyo havina makosa katika vyenyewe huenda vikatumiwa vibaya. Uyoga ni sehemu ya mimea iliyoumbwa na Mungu lakini ni mchache tu unaoliwa. Ikiwa tunakosea na kula mmoja wa namna yenye sumu hii inaweza kutuua. Yehova alitoa madini na mabati, vile vile, lakini wakati watu wanapogeuza chuma kikawa silaha zenye kuangamiza kwa matumizi ya vita vya kisiasa, je! haya ndiyo matumizi ya mipango ya Mungu?

25, 26. (a) Je! ni mwuzaji wa vileo vyenye hatari peke yake ndiye mwenye daraka kwa uharibifu ambao vinafanya kwa wanadamu? (b) Ni maulizo gani ambayo Mkristo ataangalia kwa dhamiri katika neno hili?

25 Ebu fikiria shauri la zile dawa za hatari zenye kulevya kama afyuni au kasumba na heroin. Watu wanaozoea kutumia dawa hizi hawazichumi katika ardhi tu. Kuna hatua zinazotumiwa. Ni lazima kulima na kupanda mimea yenyewe inayotoa dawa hizo, maji yake yakamuliwe na kutengenezwa vizuri mpaka yawe unga wa afyuni. Ili kupata dawa zenye kutia usingizi na kuzuia mtu asisikie maumivu zinaoitwa morphine au heroin, ni lazima tena kuchemsha zaidi mpaka kuwa maji ya mvuke. Halafu kuna uuzaji wa dawa hizi zenye kulevya sokoni. Basi daraka kwa dhara kubwa na uvunjaji wa sheria vilivyomo katika kuzoea dawa za kulevya linaanza na kuishia wapi?

26 Ijapokuwa labda tumbako na tambuu vina matokeo ya polepole zaidi ya kuharibu kuliko dawa zenye hatari, labda ulizo lile lile litaulizwa juu ya kufanyizwa na kuuzwa. Huenda mazao haya ya mimea yakawa na matumizi ya halali​—sumu iliyomo katika tumbako, kwa mfano, inatumiwa kama chanzo cha dawa ya kuua madudu​—hata hivyo uhakika ni wa kwamba matumizi ya halali ni ya kadiri ndogo sana yakilinganishwa na matumizi ya jumla. Hatuwezi kusahau kwamba ya pili kwa amri kubwa kuliko zote ni ya kwamba tumpende jirani yetu kama tunavyojipenda wenyewe. Ikiwa kwa kutaka na kwa kujua sisi tunasaidia kuharibu afya yake kwa sababu ya faida, je! tunaonyesha upendo huu?​—Mt. 22:39.

27, 28. Je! matumizi ya vinywaji fulani vya kawaida yanaweza kwa akili kupangwa katika namna ya vileo vyenye kudhuru vilivyoelezwa, hivyo kufanyiza msingi wa kukataliwa kule kule kwa kufanyizwa na kuuzwa kwavyo? Ikiwa sivyo, pana tofauti gani?

27 Labda wengine watapinga kwamba hata vitu kama chai, kahawa na, zaidi, vinywaji vyenye kileo kama pombe, vile vile vinalaumiwa kuwa vyenye kuharibu afya. Lakini, kwa habari ya vinywaji vyenye kileo Biblia inaruhusu waziwazi kuvitumia kwa kiasi. (Kum. 14:26; Yohana 2:1-10; Mit. 23:29-31; 1 Tim. 3:3, 8; 5:23) Lakini ruhusa hiyo haiwezi kupatikana juu ya tumbako na tambuu, au bangi, afyuni na mazao mengine.

28 Kwa habari ya vinywaji kama chai na kahawa, ingefaa kuulizwa hivi: Kwa karne zote ambazo vimetumiwa, ni ushahidi gani wa wazi ambao umetolewa kuonyesha ni vyenye hatari, au ni wapi ambapo serikali imetoa maonyo ya afya juu ya vinywaji hivyo? Kweli, kwa mtu mwenye kusumbuliwa na afya, kama vile vidonda vya tumboni, cho chote cha vinywaji hivi kingeweza kuwa chenye hatari na, kwa hiyo, imempasa aviepuke. Kwa mtu mwenye ugonjwa wa sukari sukari ni yenye hatari; lakini si yenye hatari kwa watu wengine. Kwa mtu mnene mno hata mkate na viazi au mchele waweza kuwa wa hatari. (Linganisha Mithali 25:27.) Basi, imetupasa tuwe wenye akili katika kufikiria kwetu kwa mambo. Je! tunataka tuzuie sauti ya dhamiri kwa kujaribu kutoa sababu za kukanusha mambo ya hakika juu ya vitu ambavyo vimeonyeshwa kwa msingi kuwa vyenye kuharibu na vyenye hatari?

‘ENENDA KWA ADABU MBELE YA WALE WA NJE’

29. Kupatana na Wagalatia 6:7, ni maulizo gani mazito ambayo imempasa mtu aulize juu ya kazi ambayo, katika matokeo yake ya mwisho, inaleta dhara kwa wanadamu?

29 Haya ni mambo machache ambayo huenda katika hayo yakatokea maulizo ya dhamiri juu ya kazi ya mtu. Katika mambo hayo yote, walakini, inafaa Mkristo ajue kwamba ‘apandacho mtu ndicho anachovuna’​—katika zaidi ya njia moja. (Gal. 6:7) Namna gani ikiwa kazi ya mtu ni ile ambayo, kuliko kufaidi, inafanyiza hatari au dhara kwa wengine? Ijapokuwa hailaumiwi waziwazi katika Biblia, je! kazi hiyo haitakuwa na matokeo mabaya, labda hata yenye kuharibu tabia katika moyo na akili za mfanya kazi? Na je! tena haielekei itakuwa na matokeo yenye kudhoofisha juu ya dhamiri yake, labda ikimruhusu kujipa mwenyewe sababu kwa kushiriki katika mazoea ambayo kwa wazi yanalaumiwa katika Neno la Mungu?​—1 The. 4:12.

30. Dhamiri za wale walio nje ya kundi la Kikristo zinapaswa vile vile zifikiriweje juu ya kazi hiyo?

30 Halafu, tena, kuna shauri la kujipendekeza wenyewe kwa dhamiri za wengine kwa habari ya unyofu. Si zamani sana matengenezo fulani makubwa ya kidini katika United States yalilaumiwa kwa sababu, yalipokuwa yakijidai kutetea amani, yalikuwa yakisaidia sana mipango ya vita. Ikiwa Mkristo anapinga desturi fulani isiyopatana na kanuni za Biblia, lakini anajipatia riziki yake kwa kazi ambayo inahusiana na kuendelezwa na kufanyizwa kwa desturi hiyo, je! atakuwa akijipendekeza mwenyewe kwa dhamiri za wengine? Je! watamwamini kuwa mnyofu katika kutetea kwake kanuni nyingine za Neno la Mungu na ahadi yake ya taratibu mpya ya haki?

31, 32. (a) Ni maulizo gani ambayo huenda yakatokea juu ya mwanamume Mkristo aliyeajiriwa kazi hivyo juu ya kufaa kwa vyeo vya daraka la kundi? (b) Je! kuwa ‘bila shtaka’ kuna maana ya kwamba inampasa mwangalizi au mtumishi wa huduma apendeze kila jambo au imani ambazo mtu kwa dhamiri yake anaona ni kosa?

31 Namna gani Mkristo ‘anayefikia cheo cha mwangalizi’ au anatamani kutumikia kama mtumishi wa huduma katika kundi? Ikiwa ameajiriwa kazi inayofanyiza vitu ambavyo ni vyenye hatari kwa wanadamu, je! mtu huyo angeweza kuonwa kama ‘asiye na shtaka’ au kama akiwa na “ushuhuda mzuri kutoka kwa watu walio nje”?​—1 Tim. 3:1, 7-10; Tito 1:6, NW.

32 Matakwa haya kwa waangalizi wa Kikristo na watumishi wa huduma hayashughuliki na mashtaka yasiyo na msingi au yasiyo ya haki. Katika nchi zinazotawaliwa na Kanisa la Kikatoliki, kwa mfano, huenda talaka ikaonyeshwa sikuzote kama kosa, hata ikiwa ziko sababu za Maandiko za uzinzi. Kulaumiwa kwa sababu ya kutalikiwa kulingana na Maandiko kusingemfanya mtu awe asiyestahili kutumikia kama mwangalizi au mtumishi wa huduma, kwa maana lawama hiyo haina msingi.

33, 34. Je! kuenea kwa kazi fulani katika eneo fulani au kwa vile inakubaliwa na watu wote katika eneo hilo kunaondoa kwa lazima kupinga kwa dhamiri juu yake?

33 Labda mtu atasema, ‘Kweli, kazi ambayo mimi nafanya haimtendei jirani yangu mema. Lakini ninakoishi wingi wa watu wanafanya kazi ya namna hii. Biashara au mazao haya ndio uchumi mkubwa katika eneo hili.’ Je! hili lingegeuza mambo kwa kadiri dhamiri ya mtu inavyohusika?

34 Ikiwa kucheza kamari, kwa mfano, ndiyo kazi kubwa katika mji au nchi fulani, labda watu wa huko hawangejali sana ikiwa mtu angeajiriwa kazi na kampani ya kucheza kamari, hata ijapokuwa mtu huyo angejidai kuwa mfuasi mnyofu wa Yesu Kristo. Lakini je! hiyo inalifanya liwe jema machoni pa Mungu? Tena, namna gani juu ya matokeo juu ya dhamiri na moyo wa mtu mwenyewe? Je! dhamiri yake ingemruhusu amkaribie Baba yake kwa “ujasiri” kama akiwa hana lo lote la kuleta kukosa kibali cha Mungu? 1 Yohana,3:19-22 anasema: “Katika hili tutafahamu ya kwamba tu wa kweli, nasi tutaituliza mioyo yetu mbele zake, ikiwa mioyo yetu inatuhukumu; kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu naye anajua yote. Wapenzi, mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu; na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake.” Bila shaka “ujasiri” huu ni jambo la kuthamini sana na kuonwa bora sana, ndiyo, kutunzwa kwa vyo vyote.

UHITAJI WA IMANI

35. Jaribu la imani huenda likatokeaje kwa sababu ya kufuata kwetu dhamiri juu ya kazi yetu?

35 Kweli, kushindania kuwa na dhamiri safi mbele za Mungu na kujipendekeza wenyewe kwa dhamiri za wengine huenda kukataka mageuzi fulani makubwa katika maisha zetu. Huenda ikawa vigumu kuona kazi ambayo haipingani na dhamiri zetu. Hii inaweka jaribu juu ya imani yetu katika uwezo wa Mungu kutusaidia kwa kuitikia jitahada zetu za uaminifu kutaka kumpendeza. Biblia inaunganisha sana imani na shauri la dhamiri kwa sababu nzuri. (1 Tim. 1:5, 18, 19; 3:8, 9; Ebr. 10:22) Je! kweli tunaamini si kwamba Yehova Mungu yuko tu bali vile vile kwamba “huwapa thawabu wale wamtafutao”?​—Ebr. 11:6.

36, 37. Ikiwa kuona kazi nyingine ambayo haipingani na dhamiri ya Kikristo kunaonekana karibu kusikowezekana, tunaweza kupata faraja na uhakikisho kutoka kwa mifano gani ya kisasa na ya kale?

36 Katika dunia yote kuna wanaume na wanawake kwa maelfu wanaoweza kutoa ushuhuda juu ya nguvu, uwezo na nia ya Mungu ya kusaidia wale wanaojitahidi kushika dhamiri njema mbele zake. Huenda mtu akadhani kwamba kuacha kazi yake aliyo nayo sasa kwa sababu za dhamiri kungemwacha katika hali isiyo na tumaini kabisa. Lakini ebu fikiria ambayo wengine wamefanya. Wafikirie wanawake waliokuwa wakiishi katika hali ya kinyumba kwa wanaume waliooa na wakawa wamewazalia watoto mbele ya kujifunza kweli ya Neno la Mungu. Kukataa kuendelea kuishi katika hali hiyo ya kinyumba kulikuwa na maana ya kupoteza msaada wote unaoonekana, hata nyumba walimokuwa wakiishi. Hata hivyo mamia ya wanawake walichukua hatua hiyo katika imani, na Yehova Mungu aliwaangalia.

37 Wafikirie tena watumwa wengi katika Milki ya Kirumi walioukubali Ukristo. Walikuwa mali ya watu waliokuwa mabwana zao, wakiwategemea kwa riziki yote. Hata hivyo iliwapasa wazitumie dhamiri zao za Kikristo na ikiwa mabwana zao wangewaamuru watende matendo kwa kuvunja kanuni za Kikristo ingewapasa wakatae, wakimkubali Mungu na Mwana wake kama mabwana wao wakubwa zaidi. Hili, vile vile, lingetaka imani kubwa sana.​—1 Pet. 2:18-20; Efe. 6:5-8; Kol. 3:22-25.

38. Ijapokuwa hawakuacha namna yao ya kisasa ya kazi, wanaume wengi wa Kikristo wamefanya mageuzi gani makubwa ili wawe na dhamiri safi?

38 Halafu, tena, kuna maelfu ya wanaume ambao, ijapokuwa hawakugeuza namna ya kazi yao, imewapasa wageuze njia zao za biashara au imewapasa wajiuzulu kwa sababu kampani ambazo walikuwa wakifanyia kazi zilisisitiza kwamba wawe wakitumia mazoea ya udanganyifu katika biashara ya halali. Mara nyingi namna nyingi za kazi za kipekee, kama vile kutengeneza radio, motokaa, saa, na kazi zinazofanana, zinatia udanganyifu, kutoza wanunuzi bei kubwa mno au kuwatoza kwa sehemu ambazo hazikuwekwa hata kidogo au kwa kazi ambayo haikufanywa hata kidogo. Hii ni namna ya wivi. Watu wengine wanaofanya kazi ya uchuuzi, wakati hawajawa Wakristo wa kweli, walikuwa wakifanya mambo ya udanganyifu ili kupata wanunuzi. Huu ni uongo na udanganyifu. Wakristo ‘wamekataa mambo ya aibu yaliyositirika’ na hawaenendi “kwa hila” ama katika kundi ama nje yake. (2 Kor. 4:2) Wanatii onyo hili: “Basi uvueni uongo, mkaseme kweli kila mtu na jirani yake; . . . Mwibaji asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akitenda kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe, apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji.” Dhamiri zao zinawaongoza waziache njia zao mbaya ili ‘wasiihuzunishe roho takatifu ya Mungu.’​—Efe. 4:25-30.

KUWA NA KIASI NA USAWA

39-41. (a) Kama katika mambo yote mengine, ni maoni ya nani ambayo inatupasa tushike wakati wa kutumia dhamiri yetu juu ya kazi? (b) Wakati kazi ya mtu inapoamsha maulizo ya dhamiri, ni uamuzi gani ambao wazee katika kundi wanaweza kufanya? Wanaongozwa na dhamiri ya nani?

39 Tena, na ifahamike kwamba Yehova Mungu ni mwenye uhakika katika matakwa yake yote. Yeye anatupatia kanuni zinazotoa uongozi mzuri, wa waziwazi; hata hivyo yeye hafanyi mambo yawe yenye kupita kiasi, kwa kiasi cha kwamba ingetupasa “kutoka katika dunia” ili tuwe na dhamiri safi.​—1 Kor. 5:10.

40 Kwa mfano, mfikirie mtu ambaye labda anafanya kazi katika shamba ambalo karibu kazi yake peke yake ni kulima mazao ambayo ni yenye kudhuru kwa matumizi ya kibinadamu. Huenda kazi yake ikahusiana kabisa na ufanyizaji au ugawaji wa vitu hivi. Huenda dhamiri yake ikamwongoza au isimwongoze kuacha kazi hiyo. Ijapokuwa dhamiri yake haimwongozi kuacha, ikiwa yeye ni wa kundi la Kikristo dhamiri za wazee wa kundi hilo labda hazitawaruhusu wampendekeze kama anastahili kuwa mzee au mtumishi wa huduma katika kundi.

41 Kwa upande mwingine, huenda mtu anafanya kazi katika shamba lakini anafanya kazi ambayo kwa wazi haihusiani na ufanyizaji wa mazao hayo, labda anafanya kazi ya kipekee kwa jamaa ya mwenye shamba, akifanya kazi ya kusafisha nyumba au inayofanana na hiyo. Huenda akaona kwamba kazi yake haihusiani na utendaji unaofanyiza mazao yenye kudhuru. Kwamba wazee wa kundi ambalo mtu huyo anashirikiana nalo wangempendekeza kama mzee au mtumishi wa huduma ama sivyo ingetegemea juu ya dhamiri zao. Wangefikiria matokeo ambayo pendekezo hilo lingekuwa nayo juu ya kundi lote na juu ya watu ambao ndani yao kundi hilo linapatikana.

42. (a) Tunapojitahidi kuwa na dhamiri safi, ni utendaji gani wa ubatili ambao tutaepuka, na tutafanya nini kuwa lengu letu? (b) Katika mambo ya kuamua jema na baya, tutakuwa na usawa gani?

42 Hivyo, basi, kama mtume, sisi sote yatupasa tuwe ‘tukijizoeza ili tuwe na dhamiri isiyo na hatia mbele za Mungu na mbele ya watu sikuzote.’ (Matendo 24:16) Wakati uo huo imetupasa tufahamu ubatili wa kubishia sehemu ndogo ndogo zote au matumizi yanayowezekana ya kanuni yo yote ya Maandiko au kujaribu kuweka kanuni za mambo yanayopaswa kufanywa na mambo yasiyopaswa kufanywa na kwa njia hiyo kutunga taratibu ya sheria na kanuni juu ya jambo linaloruhusiwa na lisiloruhusiwa. Katika kumwagiza Timotheo juu ya huduma yake katika Efeso, Paulo aliandika hivi: “Kwa kweli lengo la amri hii ni upendo kwa moyo safi na kwa dhamiri njema na kwa imani bila unafiki. Kwa kupotoka katika mambo haya watu fulani wamegeukia katika usemi wa upuzi, wakitaka kuwa waalimu wa sheria, lakini bila kufahamu wala mambo ambayo wanasema wala mambo ambayo juu yake wanathibitisha kwa nguvu.” (1 Tim. 1:3-7, NW; linganisha 6:3-5.) Wakati uamuzi unapopaswa uwe juu ya dhamiri ya kila mtu, sisi hatutajaribu kuweka dhamiri yetu juu ya wengine, wala kuwadharau wengine kama waangalifu mno kwa mambo madogo madogo wala kuwalaumu na kuwahukumu wale ambao dhamiri zao si zenye kujizuia kama dhamiri zetu katika mambo ya kuamua kati ya mabaya na mema.​—Rum. 14:3, 10.

43. Tunapojitahidi kutenda sikuzote kwa dhamiri njema, ikiwa tunafanya makosa, tunaweza kufanya nini ili tusiwe na dhamiri mbaya?

43 Tutafanya makosa, tutafanya mambo ambayo mwisho tunakuja kusikitikia​—kwa sababu sisi si wakamilifu. Lakini hatutapata maumivu kwa sababu ya dhamiri yenye hatia ikiwa tunakuwa wepesi wa kuungama kosa letu kwa Mungu na kuliacha, tukitafuta msamaha wa Yehova kupitia kwa Mwana wake. Soma yaliyompata Mfalme Daudi mwenyewe katika jambo hili kama ilivyoandikwa katika Zaburi 32:1-6. Furahia kujua kwamba dhabihu ya ukombozi ya Mwana wa Mungu inaweza kufanya upatanisho wa dhambi zetu na kuzitakasa dhamiri zetu, kutupa uhakikisho wenye kufariji kwamba Mungu hatuhesabii sisi makosa hayo. Kwa hiyo tunaweza kuendelea kumtumikia yeye kwa dhamiri njema na kwa furaha, uradhi, amani yote ya akili na tumaini la uzima wa milele linaloletwa na hili.

​—Kutoka The Watchtower, Oct. 1, 1972.

[Picha katika ukurasa wa 156]

Kucheza kamari​—shina lake ni tamaa, kunaleta uvunjaji wa sheria na kufanyiza ushirikina. Je! Mkristo angeweza kushirikiana na mazoea hayo?

[Picha katika ukurasa wa 158]

Je! ni jambo linalopatana kusema juu ya upendo wa jirani lakini kulima tumbako inayoweza kuharibu afya ya jirani yako?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki