Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 4/1 kur. 150-153
  • Kushughulika na Maulizo ya Dhamiri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kushughulika na Maulizo ya Dhamiri
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAAMUZI MAGUMU YA DHAMIRI
  • ‘Kujipendekeza Wenyewe kwa Kila Dhamiri ya Kibinadamu Machoni pa Mungu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Kuendelea Kuwa na Dhamiri Njema
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Kufaidika na Dhamiri Yako Uliyopewa na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Je, Dhamiri Yako Imezoezwa Vizuri?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 4/1 kur. 150-153

Kushughulika na Maulizo ya Dhamiri

“Sijui sababu ya kujishitaki nafsi yangu, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni [Yehova].”​—1 Kor. 4:4.

1. Ni jambo gani ambalo bado ni la kweli juu ya uwezo wa kupambanua mema na mabaya wa watu wote?

IJAPOKUWA wingi wa ufisadi, udanganyifu na uvunjaji wa sheria leo, si watu wote katika ulimwengu wa wanadamu “wamepungukiwa uwezo wa kupambanua mema na mabaya.” (Efe. 4:19, NW) Kama katika siku za Paulo, kuna wengine leo ambao, ijapokuwa hawana ujuzi ulio sawa wa Neno la Mungu, wangali wana ustahifu fulani, masalio fulani ya uwezo huo wa ndani wa kupambanua mema na mabaya ambao tunauita dhamiri.

2, 3. Maneno ya Paulo katika Warumi 2:12-16 yanasaidiaje kufahamu jambo hili, na yanatusaidia tufahamu nini juu ya sheria za kibinadamu na mwenendo wa ustahifu upande wa watu wengi?

2 Kwa habari ya mataifa yasiyo ya Kiisraeli, wale ambao hawakuwa chini ya agano la Torati wakati wo wote Paulo alisema hivi: “Kwa maana watu wa Mataifa wasio na sheria wafanyapo kwa tabia zao yaliyo ndani ya torati, hao wasio na sheria [yaani, taratibu ya sheria kutoka kwa Mungu] wamekuwa sheria kwa nafsi zao wenyewe.” Katika njia gani? Kwa vile “waionyesha kazi ya torati iliyoandikwa mioyoni mwao, dhamiri yao ikiwashuhudia, na mawazo yao, yenyewe kwa yenyewe, yakiwashitaki au kuwatetea.” (Rum. 2:12-16) Hivyo “sheria” hii ambayo wamekuwa “kwa nafsi zao wenyewe” siyo sheria ambayo wao wenyewe wanajifanyia wenyewe bila kujali ambavyo wengine wanafikiria.

3 Tabia hii ya mema na mabaya, iliyorithiwa kutoka kwa mwana wa kibinadamu wa kwanza wa Mungu, inatenda kama “sheria” au kanuni ya mwenendo katika watu wa mataifa yote, sasa kama zamani. Hii ndiyo sababu sheria za kitaifa au za kikabila za karibu watu wote zimeonyesha bila kupunguka chache za kanuni za haki za Mungu, ijapokuwa watu hawa walikuwa bila Biblia kama uongozi wao. Inaeleza sababu gani watu fulani, wajapokuwa si watumishi wa kweli wa Yehova Mungu au hata wanaojidai kuwa Wakristo, kwa desturi wanaweza kuishi kwa ustahifu, mara nyingi wakionyesha kushikamana na kanuni fulani nzuri. Wakati uo huo inaeleza sababu gani Mungu angeweza kwa haki kuweka si watu wake wa agano wa Israeli peke yao bali na ulimwengu mzima wa wanadamu “uwe chini ya hukumu,” na sababu gani, katika kuonyesha kunakokuja kwa hukumu yake, anaweza kwa haki ‘kumlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.’​—Rum. 2:6; 3:9, 19.

4, 5. (a) Mkristo anawezaje kuwatahayarisha wale wanaoutukana mwenendo wake? (b) Toa mifano.

4 Kwa sababu ya kuwa tofauti na ulimwengu wa wanadamu uliojitenga na Mungu, Mkristo atapingwa. (Yohana 15:18-20) Lakini hili halimwachilii asitende ili aache uwezo wo wote wa ustahifu, haki au adili ambazo huenda zingali zinabaki katika watu wa ulimwengu ziamue. Huenda watu wakatafsiri vibaya kusudi la kujitenga kwetu, wakituita ‘wenye kumchukia kila mtu,’ ‘wenye kuchukia watu,’ na kutulaumu juu ya kuwa wasio na huruma, washupavu, wasio na rehema. Mtume Petro anaonyesha kwamba tunaweza na imetupasa tutende ili washtaki wetu wasiwe na jambo la kulaumu. “Mwe na dhamiri njema,” anaonya, “ili katika neno lile mnalosingiziwa, watahayarishwe wale wautukanao mwenendo wenu mwema katika Kristo. Maana ni afadhali kuteswa kwa kutenda mema, ikiwa ndiyo mapenzi ya Mungu, kuliko kwa kutenda mabaya.”​—1 Pet. 3:16, 17.

5 Katika nyakati za kisasa kuna mifano mingi inayoonyesha namna fadhili za Kikristo, hali ya kusaidia au ukarimu kwa watu waliomo katika ulimwengu zimegeuza kabisa maoni yao juu ya watangazaji wa Ufalme wa Yehova na kazi na ujumbe wao. Hata wanapoteswa isivyo haki na kutiwa vifungoni na kambi za mateso, kazi yao nzuri ya uaminifu na njia yenye staha imewafanya watumishi wa Yehova wapate kuheshimiwa na wakuu wa serikali, nao wamewekwa katika vyeo vya kutumainiwa na vyenye madaraka, kama ilivyokuwa kwa habari ya Yusufu katika Misri ya kale.​—Mwa. 39:21-23.

6. Dhamiri inahusuje uhusiano wa Mkristo na serikali za kilimwengu?

6 Yehova Mungu ameziruhusu serikali za kibinadamu zitende kazi duniani na anaziruhusu zitumikie kama “mtumishi” wake hata kwa kuadhibu uvunjaji wa sheria na makosa mengi. Kwa kadiri Mungu anavyoziruhusu serikali hizi ziweko, haimpasi Mkristo azipinge, haimpasi atende isivyotaka sheria. Yeye hawezi kutazamia ulinzi wa Mungu ikiwa anafanya matendo mabaya na kuteswa na wakuu wa serikali kwa sababu hiyo. Lakini kuna sababu iliyo kubwa zaidi kuliko kuogopa adhabu ya serikali ambayo imepaswa ituongoze sisi tuwe wenye kutii sheria. Warumi 13:5, NW, linatuambia hivi: “Kwa hiyo kuna sababu ya lazima kwenu ninyi watu kutii, si kwa sababu ya hasira kuu tu [inayoonyeshwa katika adhabu ya serikali juu ya kuvunja sheria] bali pia kwa sababu ya dhamiri yenu.” Adhabu kuwa nyepesi au kali silo jambo linaloongoza maoni ya Mkristo. Dhamiri yake inamwongoza katika kutenda yaliyo haki, kwa maana anajua ya kwamba, kama serikali za “Kaisari” duniani zitachukua hatua ama zisichukue, “ni lazima sisi sote tuonyeshwe mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo.”​—2 Kor. 5:10, NW.

7. Katika ‘kuziacha dhamiri za wengine ziamue,’ je! tunaweza kwa usalama kuziacha dhamiri zao zituwekee kanuni yetu wenyewe?

7 Bila shaka, hatuwezi hata kidogo kuziacha dhamiri za wengine ambazo hazikuelimishwa au zenye kutiwa unajisi na mbaya ziweke kanuni kwa dhamiri zetu wenyewe. Ni lazima dhamiri yetu iongozwe na Neno la Mungu na roho yake na huenda nyakati nyingine ikashuhudia tofauti kabisa na yale ambayo wakuu fulani wa serikali wanataka kwetu. Halafu inatupasa kwa dhamiri tuitikie kama walivyoitikia mitume: “Inatupasa kumtii Mungu kama mtawala kuliko wanadamu.”​—Matendo 5:29-32, NW.

8. Toa mifano ya amri za msingi, makatazo za kanuni zinazopatikana katika Neno la Mungu ambazo zimepaswa zifanyize dhamiri ya Kikristo. (a) Kwa vile Mkristo hayuko bila sheria za Maandiko na kanuni, kwa sababu gani maulizo ya dhamiri bado yanatokea? (b) Ni nini kwa kawaida inachoamua ukubwa wa sehemu ambayo kila dhamiri lapaswa ifanye katika kuamua juu ya wema au ubaya wa jambo?

8 Biblia inasema waziwazi sana, kwa mfano, katika kuonyesha uhitaji wa Wakristo wa kweli kujiondoa wenyewe katika ushirika wote wa “Babeli Mkuu,” milki ya ulimwengu ya dini ya uongo. (Ufu. 18:2-5; 2 Kor. 6:4-18) Inaonyesha kwamba inawapasa Wakristo wasiwe “wa ulimwengu,” hivyo wasishiriki katika siasa zake au kushindania kufanikiwa kwa miradi yake inayopinga Ufalme. (Yohana 17:14; 18:36; Yak. 4:4) Biblia inaonyesha waziwazi utakatifu wa damu, wa uhai wa kibinadamu na vile vile kanuni kwa watu wa Mungu ‘kufua panga zao kuwa majembe na kutokujifunza vita tena,’ kwa kuwa vita yao “si juu ya damu na nyama” bali juu ya nguvu za mashetani. (Mwa. 9:4-6; Isa. 2:2-4; Efe. 6:11, 12) Vile vile Neno la Mungu liko wazi sana katika kulaumu ufisadi katika namna zake zote (uasherati, uzinzi na tendo la kulalana wanaume kwa wanaume na wanawake kwa wanawake), na vile vile mwenendo mwingine mbaya kama ulevi, udanganyifu na wivi.​—1 Kor. 6:9, 10; Yohana 8:44; Efe. 4:28.

MAAMUZI MAGUMU YA DHAMIRI

9. (a) Kwa vile Mkristo hayuko bila sheria za Maandiko na kanunui, kwa sababu gani maulizo ya dhamiri bado yanatokea? (b) Ni nini kwa kawaida kinachoamua ukubwa wa sehemu ambayo kila dhamiri inapaswa ifanye katika kuamua juu ya wema au ubaya wa jambo?

9 Ndivyo yalivyo matendo na mazoea mengi sana ambayo kwa wazi yanakubaliwa au yanalaumiwa katika Biblia. Mengine mengi sana yanapatana kwa wazi, au yanavunja kanuni zilizomo. Hata hivyo, hasa katika jamii ya watu ya kisasa yenye mambo magumu ambayo imetokea katika sehemu nyingi za dunia, zinabaki hali zinazotaka uamuzi wa kipekee, ukiwa juu ya dhamiri ya mtu mwenyewe anayepaswa. Mambo mengi sana katika maisha ni shauri la kadiri. Tofauti kati ya pigo la upole na ngumi ni shauri la kadiri ya nguvu. Tofauti kati ya heshima ya vivi hivi​—kama, kwa mfano, kumheshimu mtawala au kuheshimu mfano wa kitaifa​—na ibada ya heshima vile vile ni shauri la kadiri. Kukiwako kufanya kupita kadiri hakuna shaka kubwa. Ni wakati shauri linapokuwa kati ya uamuzi wa jambo ambalo kwa wazi ni jema na ambalo kwa wazi ni kosa, ndipo maulizo yanapotokea. Kwa kadiri shauri linavyokuwa karibu zaidi na uamuzi wa kati ya jambo jema na jambo baya, ndivyo dhamiri ya mtu inavyokuwa na sehemu kubwa zaidi ya kufanya. Tukikutana na hali hizo, imetupasa tufanye nini?

10, 11. (a) Wakati maulizo hayo ya dhamiri yanapotokea Mungu anatutazamia nini? (b) Wakati tunapokutana na jambo hilo la kipekee juu ya dhamiri, je! tutazamie amri fulani itolewe kutuambia jambo la kufanya, na ni nani ambaye amepaswa awe na daraka kwa maamuzi yetu? (c) Maamuzi hayo yanafunua nini juu yetu kwa Mungu?

10 Yehova Mungu anatutazamia kutumia uwezo wetu wa akili, ujuzi wetu, ufahamu na uamuzi wetu, na kufanya kwa dhamiri jambo ambalo imani yetu inatuelekeza kufanya. Mungu hatuweki chini ya dhamiri ya binadamu fulani mwingine katika mambo hayo. Inatupasa kila mmoja tujifanyie uamuzi wetu wenyewe kupatana na dhamiri​—dhamiri yenye kufanyizwa kwa mfano wa Neno la Mungu. Tena inatupasa tukubali matokeo ya dhamiri zetu wenyewe, si kumtazamia mtu mwingine kutufanyia uamuzi na kutuchukulia daraka hilo.

11 Kwa hiyo lingekuwa kosa katika mambo hayo kujaribu kuchukua kutoka kwa mtu mwingine, kutoka kwa baraza ya wazee au kutoka kwa baraza inayoongoza ya kundi la Kikristo, kanuni au sheria fulani zenye kuonyesha mambo ya kufanya na mambo ambayo hayaruhusiwi kufanywa. Hakuna binadamu aliye na haki ya kuongeza lo lote kwa Neno la Mungu mahali ambapo halisemi mambo ya kufanya na yasiyoruhusiwa kufanywa. Katika hekima yake Mungu anaturuhusu tuonyeshe namna tulivyo katika “utu wa moyoni usioonekana,” na huenda maamuzi ambayo tunafanya katika mambo hayo ya kipekee yakafunua hili. Kweli, mara nyingine huenda tukakosa bila kuwa na nia mbaya, na Mungu anayeijua mioyo, aweza kufahamu hili.

12. Je! uhakika peke yake wa kwamba hatujui kosa lo lote ni uhakikisho wa haki yetu? Kwa sababu gani?

12 Lakini bila kujali maamuzi yetu yo yote, na ijapokuwa haya yafanywe kwa dhamiri safi, inatupasa sikuzote tufahamu ya kwamba, mwisho, Mungu Ndiye atakayefunua uhaki au ukosefu wa mwendo wetu na hilo katika wakati na njia yake mwenyewe. Akifahamu hili, mtume Paulo aliandika hivi: “Maana sijui sababu ya kujishitaki nafsi yangu, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni [Yehova]. Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulikisha yaliyositirika ya giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu.”​—1 Kor. 4:3-5.

13. (a) Warumi 14:4, 10-12 linaonyesha nini juu ya maoni mazuri kuchukua juu ya mtu anayefanya maamuzi hayo ya kipekee ya dhamiri? (b) Walakini, ni wapi ambapo dhamiri za wale walio katika vyeo vyenye madaraka katika kundi zinapoonekana vile vile kwa habari ya watu hao?

13 Yanapotukia mambo ya kuamua kati ya jema na baya, haitupasi tujiweke wenyewe kama mahakimu wa kila mtu ambaye ni lazima ajifanyie mwenyewe uamuzi wake wa dhamiri. Wala sisi wenyewe haitupasi tujione kuwa na hatia ya kwamba tunakosea kwa kumkubali mtu huyo kama angali mtumishi anayekubaliwa wa Mungu ikiwa uamuzi wake kati ya jambo jema na jambo baya hauko sawasawa na ambavyo uamuzi wetu ungalikuwa. Mungu ndiye Hakimu wake. (Rum. 14:4, 10-12) Kwa upande mwingine, wale wenye vyeo vyenye madaraka katika kundi la Kikristo yawapasa vile vile wazitumie dhamiri zao wenyewe katika uangalizi wao wa kundi. Ijapokuwa huenda wakaona kwamba uamuzi wao ungalikuwa tofauti na ule wa ndugu mwingine katika shauri fulani, huenda kupinga kwa dhamiri zao kukawa kwa upole sana, kwa vile Maandiko kwa wazi yanamwachia kila mtu shauri ajifanyie uamuzi wake mwenyewe. Mtu akitoa ushahidi wa kuonyesha kuwa ametenda kwa dhamiri safi, dhamiri zao zaweza kuwaruhusu wamgawie daraka au kumpendekeza yeye kwa cheo fulani cha madaraka. Hata hivyo, huenda ikawa kwamba dhamiri zao zitasema kwa nguvu ya kutosha katika shauri hilo hata hawawezi kumpendekeza katika njia hii kwa sababu ya dhamiri. Tena, Mungu ndiye Hakimu wao na wao wasilaumiwe.

14. Sasa kunatokea maulizo gani kwa mazungumzo?

14 Mara nyingi maulizo haya ya kuamua kati ya jambo jema na jambo baya yanatokea katika upande wa kazi. Je! kazi ambayo unafanya inakuruhusu kuwa na dhamiri safi mbele za Mungu? Je! inakuruhusu ‘ujipendekeze mwenyewe kwa kila dhamiri ya kibinadamu’ kama mfuasi wa kweli wa Yesu Kristo? Haya ndiyo maulizo ya maana sana ambayo tutazungumza katika makala inayofuata.

[Picha katika ukurasa wa 152]

Je! imekupasa uiandikie Sosaiti kwa agizo juu ya shauri hili? Ikiwa uamuzi wa kipekee, wa dhamiri yako, unatakiwa, ni juu yako kufanya uamuzi huo. Tenda ili uwe na dhamiri safi mbele za Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki