Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 3/15 kur. 128-134
  • ‘Kujipendekeza Wenyewe kwa Kila Dhamiri ya Kibinadamu Machoni pa Mungu’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Kujipendekeza Wenyewe kwa Kila Dhamiri ya Kibinadamu Machoni pa Mungu’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UHITAJI WA UJUZI NA ROHO YA MUNGU
  • DHAMIRI DHAIFU NA ZENYE NGUVU
  • “HAITUPASI KUJIPENDEZA WENYEWE”
  • DHAMIRI ZILIZOTIWA UNAJISI
  • KUACHA DHAMIRI ZA WENGINE ZIAMUE
  • Kufaidika na Dhamiri Yako Uliyopewa na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Kuendelea Kuwa na Dhamiri Njema
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Je! Wewe Unaongozwa na Dhamiri Nyepesi ya Kikristo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Dhamiri
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 3/15 kur. 128-134

‘Kujipendekeza Wenyewe kwa Kila Dhamiri ya Kibinadamu Machoni pa Mungu’

1. Kwa sababu gani uwezo wa dhamiri peke yake si uongozi wa hakika?

HAITOSHI kwa mtu kuwa na uwezo wa dhamiri. Peke yake si uongozi wa hakika katika maisha. Ni kwa sababu ni sehemu ya sisi, iliyofungamana sana na mioyo yetu na inavutwa kwa kutendeana kwa moyo na akili. Basi kulingana na ambavyo sisi wenyewe tulivyo, mambo tuliyo nayo katika moyo na akili zetu, sauti ya “mshuhudiaji” huyu haitasikika waziwazi, ama ushahidi wake utakuwa mzuri, wenye kutegemewa na wa kweli ama wenye makosa, wenye kupoteza, hata kuwa wa uongo kabisa.

2. Ni mifano gani inayoonyesha namna dhamiri inavyoweza kutoa ushuhuda wa makosa?

2 Kwa mfano, Kristo Yesu aliwaonya wanafunzi wake kwamba “saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada.” (Yohana 16:2) Sauli wa Tarso alikuwa mmoja wa hawa. Katika bidii yake kwa kile ambacho kwa dhamiri yake aliamini kuwa ni haki, Sauli ‘alifanya matendo mengi ya kupingamana na jina la Yesu,’ akiwatesa wanafunzi, na ‘wakati ilipowapasa wauawe, alitoa idhini yake.’ (Matendo 26:9, 10; linganisha Wagalatia 1:13, 14) Lakini wakati uliofuata, alipokuwa mwenyewe akiteswa kama Mkristo mtume Paulo, aliweza kusema hivi kortini: “Mimi kwa dhamiri safi kabisa nimeishi mbele za Mungu hata leo hivi.” (Matendo 23:1) Ijapokuwa dhamiri yake ilikuwa imekuwa “safi” wakati alipokuwa akiupinga Ukristo, ushahidi wa dhamiri hiyo ulikuwa umekuwa wenye makosa, wenye uongo kabisa na ulikuwa umemwongoza katika kupigana na Mungu. Lilikuwa kosa gani?

UHITAJI WA UJUZI NA ROHO YA MUNGU

3. Kwa sababu gani ujuzi wa Biblia ni wa lazima ili dhamiri itoe ushuhuda mzuri?

3 “Nalitenda hivyo kwa ujinga, na kwa kutokuwa na imani,” Paulo anajibu. (1 Tim. 1:13) Ikiwa dhamiri yetu itatusaidia katika njia ya uzima wa milele, ni lazima tujifunze kwa bidii Neno la Mungu, Maandiko Matakatifu. Kwa sababu gani? Kwa sababu kwa ujuzi wa Biblia na kwa kuutumia katika maisha zetu tunaweza kumjua Yehova Mungu, kuujua utu wake, njia na makusudi yake. Pasipo kumjua Yeye waziwazi haiwezekani kuonyesha sifa na kanuni zake, na sauti ya dhamiri yetu haitasikika waziwazi.

4. (a) Ni msaada gani mwingine unaohitajiwa? (b) Onyesha hili. (c) Tunajifunza nini kwa maandiko yaliyotajwa mwishoni mwa fungu hili?

4 Tena ni lazima tutafute sikuzote roho ya Yehova Mungu, kuiomba bila kukoma. Mtume alisema juu ya dhamiri yake kama ‘ikishuhudia pamoja na yeye katika roho takatifu,’ na ni kwa roho ya Mungu inayotenda juu ya akili na mioyo yetu iliyotiwa nuru na kuzoezwa kwa Maandiko kwamba tunaweza kuwa na hakika ya ushahidi wa kweli kutoka kwa mshuhudiaji aliye ndani yetu. (Rum. 9:1, NW) Tunaweza kufananisha hili na mtoto ambaye amelelewa na baba mwenye upendo, aliyetia kwa uangalifu kanuni fulani katika mwana wake, si kwa maneno tu, bali vile vile na kwa mfano. Basi, ikiwa pindi fulani mtoto anapokuwa mbali na baba yake, mtu fulani anajaribu kumwingiza mtoto katika tendo lililo tofauti na kanuni za baba yake. Labda tendo lenyewe linaloshauriwa halikutajwa hata kidogo na baba ya mtoto. Mtu anayemshawishi mtoto afanye tendo hilo huenda hata akasema hivi, “Je! kuna wakati ambapo baba yako amekuambia waziwazi usitende hili?” Huenda jibu likawa hivi, “Hapana, hajaniambia.” Hata hivyo labda mtoto atakataa shauri hilo, akisema, “Ijapokuwa baba yangu hajalitaja, mimi najua sana kwamba hangetaka nifanye​—mimi najua yeye asingependa!” Hata bila amri ya waziwazi, mtoto anajua jambo la kufanya. Kwa sababu gani? Kwa sababu anayo roho ya baba yake, yeye anajua maoni ya baba yake yalivyo juu ya jambo hilo. Katika njia izo hizo sisi tunaweza kujua maoni ya Yehova kwa msaada na Neno lake na ule wa Mwana wake na kwa roho takatifu.​—Linganisha 1 Wakorintho 2:16; tena mfano wa “roho” ya Paulo juu ya kuongoza kundi katika Korintho, kama ilivyoandikwa katika 1 Wakorintho 5:3-5.

5, 6. (a) Kwa sababu gani Wakristo wanaoongozwa na roho ya Mungu hawako “chini ya sheria”? (b) Basi, ni nini kinachotiwa katika ‘sheria inayoandikwa katika mioyo ya Wakristo’?

5 Juu ya mtu anayeongozwa na roho ya Mungu, mtume anasema hivi: “Ikiwa mnaongozwa na roho ya, ninyi hamko chini ya sheria . . . tunda la roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, fadhili, wema, imani, upole, kujiweza. Juu ya mambo haya hakuna sheria.” (Gal. 5:18, 22, 23, NW) Hawako “chini ya sheria” namna gani?

6 Kristo Yesu alionyesha kwamba Torati nzima iliyopewa kwa Israeli ilikuwa juu ya amri mbili za msingi: Kumpenda Mungu kwa moyo wote, akili, nafsi na nguvu, na kumpenda jirani kama mtu anavyojipenda. (Mt. 22:36-40) Tena mtume Paulo anasema kwamba sheria juu ya uzinzi, uuaji, wivi, kutamani “na ikiwapo amri nyingine yo yote, inajumlishwa katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Pendo halimfanyii jirani neno baya; basi pendo ndilo utimilifu wa sheria.” (Rum. 13:9, 10) Je! sisi tunaongozwa na upendo huo wa Mungu na wa jirani na tunao ujuzi wa kweli wa Neno la Mungu na imani yenye nguvu? Basi hata bila taratibu yenye sheria nyingi mno, kanuni na makatazo, tunaweza kuendelea kuwa katika njia ya haki, kwa sababu ‘tumeandikiwa sheria ya Mungu katika mioyo yetu.’ (Ebr. 10:16) “Sheria” maana yake ni ‘kanuni ya mwenendo.’ Yote ambayo tunajua juu ya Mungu, kwa kujifunza na kwa matendo yake pamoja na sisi, yanakuwa ni kanuni yetu ya mwenendo au “sheria.” Hii inapokuwa hivyo, basi dhamiri yetu inatoa ushuhuda mzuri, wenye kutegemeka ili kutuongoza sisi.

DHAMIRI DHAIFU NA ZENYE NGUVU

7, 8. Ni katika njia gani dhamiri ya Wakristo fulani wa Korintho ilikuwa ‘dhaifu,’ na ilikuwa sababu gani ya msingi?

7 Lakini hata kwa Wakristo waliobatizwa, hivi sivyo ilivyo sikuzote. Wengine wanazo dhamiri ‘zenye nguvu,’ wengine wanazo ‘dhaifu,’ kama inavyoonwa katika barua ya kwanza ya Paulo kwa kundi katika Korintho. Katika mji huo, nyama iliyokuwa imetolewa sadaka kwa sanamu na Wakorintho wapagani iliuzwa kwa kawaida katika masoko ya mji ya nyama. Dhamiri ya Wakristo wengine haingewaruhusu wale nyama hiyo bila kujiona hatia. Je! ushahidi huu wa dhamiri yao ulikuwa wa kweli? Ikiwa sivyo, kwa sababu gani?

8 Wakristo hao walikosa ujuzi wa kweli na ufahamu wa kanuni za haki. Paulo alieleza kwamba sanamu za kipagani zilikuwa “si kitu” kwa kuwa “hakuna Mungu ila mmoja,” Muumba. Kwa hiyo nyama isingeweza kweli kuwa ya sanamu kwa kuwa haikuwa hai na bila nguvu ya kupokea au kuwa na nyama hiyo. Nyama iliendelea kuwa chini ya uenyeji wa Yeye ambaye kwa haki ndiye ‘mwenye dunia na vyote vilivyomo,’ Yehova Mungu.​—1 Kor. 8:1-6; linganisha 10:25, 26.

9. (a) Ni sababu gani nyingine ziwezazo kufanyiza dhamiri dhaifu? (b) Kwa sababu gani kula nyama iliyotolewa sadaka kwa sanamu ‘kunatia unajisi’ dhamiri za hao?

9 Lakini jambo fulani jingine lilikuwa linazifanya dhamiri zao kutoa ushahidi usio wa kweli. Akiisha kusema, “Bali ujuzi huu haumo ndani ya watu wote,” Paulo anaongeza, “ila wengine kwa kuizoelea ile sanamu hata sasa hula kana kwamba ni kitu kilichotolewa sadaka kwa sanamu; na dhamiri zao, kwa kuwa dhaifu, hunajisika.” (1 Kor. 8:7) Hii inaonyesha kwamba maisha yetu ya zamani, mazingira, desturi, imani na maoni ya watu ambao kati yao tulikulia​—yote haya yanaweza kugeuza ushahidi wa dhamiri yetu. Wakorintho wengi walikuwa wamezoea ibada ya sanamu mbele ya kuwa Wakristo. Kwa wazi kwa kulazimishwa na mazoea bado walifahamu kwamba ibada ilishirikiana na ile nyama iliyokuwa imetolewa sadaka katika ibada ya sanamu. Hivyo, kwao kuila kungekuwa, kama Paulo alivyosema, ‘kuitia dhamiri yao unajisi.’ Wakati mwingine, ujuzi ungaliweza kuwa na matokeo yenye afya, yenye kuelimisha juu ya dhamiri yao, ‘kutengeneza upya’ maoni yao, kuwasaidia washinde kuchukia kwao kwa zamani kusiko na sababu nzuri, kuogopa, imani zenye makosa na maoni yenye makosa.​—2 Kor. 13:11.

“HAITUPASI KUJIPENDEZA WENYEWE”

10. Wale walio na dhamiri zenye nguvu wangewezaje ‘kuzijenga’ dhamiri za wengine walio katika njia yenye kosa?

10 Lakini sasa wale Wakristo ambao dhamiri zao hazikuwa dhaifu, waliokuwa na ujuzi wa kanuni za kweli na maoni yasiyo na makosa juu ya jambo hilo imewapasa wafanye nini? Je! imewapasa waone mashaka ya wale walio na dhamiri dhaifu kuwa madogo? Je! imewapasa waendelee mbele na kufanya lo lote ambalo dhamiri zao ziliruhusu bila kujali dhamiri dhaifu za wengine, wakidhania kwamba uhodari wao wenyewe katika shauri hilo ungezitia nguvu dhamiri dhaifu za wengine? Paulo anasema kwamba upendo umepaswa utuambie, kwa maana “ujuzi huleta majivuno, bali upendo hujenga” wale wanaouonyesha. (1 Kor. 8:1) Imewapasa waangalie kusije kutumia kwa “uwezo” wao au haki yao (ya kula nyama hiyo ambayo sasa haikamatani na ibada) ‘kukawakwaza wale walio dhaifu.’ Ndiyo, ikiwa wangekula nyama iliyojulikana kuwa imetolewa sadaka kungaliweza kuwa na matokeo ya ‘kujenga’ dhamiri ya walio dhaifu, kuwajenga, si katika njia yenye afya, bali katika njia ambayo dhamiri yao ingegeukia kwenye upande mwingine. Upande gani? Ule wa kula nyama katika sherehe ya kidini yenye kukamatana na ibada ya sanamu, au hata kuila bila kujali kufahamu kwamba inakamatana na ibada. Jambo hili lilikuwa limelaumiwa na baraza inayoongoza ya kundi la Kikristo, kwa uongozi wa roho takatifu.​—1 Kor. 8:9, 10; Matendo 15:28, 29.

11. Kwa sababu gani mtu asiyetenda kulingana na imani “amehukumiwa”?

11 Hata ikiwa dhamiri ya mtu ni yenye kujizuia mno, kusiwe na mtu wa kuilemeza dhamiri hiyo au kujaribu kumshawishi mtu ili atende kwa kupingana nayo. Kama mazungumzo yanayolingana ya mtume katika barua yake kwa Warumi yanavyoonyesha, ikiwa mtu angekula nyama hali akiwa na mashaka juu ya kama inafaa kufanya hivyo, “amehukumiwa . . . kwa maana hakula kwa imani.” Mkristo anayetenda kulingana na imani anayo dhamiri safi; lakini ikiwa anatenda bila imani kwamba anachofanya ni kitu kinachofaa, hapo dhamiri yake si safi, kwa maana, ajapoona kwamba tendo hilo ni tofauti na mapenzi ya Mungu, hata hivyo analifanya.​—Rum. 14:5, 14, 23.

12. Basi kwa sababu gani imani ni ya lazima kwetu ili kuwa na dhamiri itakayotoa uongozi unaofaa?

12 Imani yenye nguvu inafanya dhamiri kuwa nzuri, inayosema kwa uhodari, bila makosa, bila kushindwa kutoa ushuhuda unaohitajiwa katika nyakati za hatari. Imani haitoi uhakika tu; inafanyiza uaminifu kwa kweli na haki. Mkristo ambaye amejenga imani yenye nguvu kwa ujuzi na kwa kuutumia kwa unyofu wa moyo, kwa kuthamini kwa kweli na tumaini, atakuwa mwaminifu. Ingawa huenda dhamiri yake ikamruhusu kutenda mambo ambayo wale walio na imani dhaifu wakaona hayafai kufanywa, wakati uo huo yeye hatajipatia udhuru wa kufanya.​—Gal. 5:13.

13. Kwa sababu gani ni jambo la maana sana kwetu kuonyesha upendo katika kuzifikiria dhamiri za wengine na kuongoza mwenendo wetu kwa huo?

13 Lakini sikuzote upendo unapaswa uongoze. Kanuni hii yenye kuongoza inatiliwa mkazo na Paulo wakati anaposema: “Basi imetupasa sisi tulio na nguvu kuuchukua udhaifu wao wasio na nguvu, wala haitupasi kujipendeza wenyewe. Kila mtu miongoni mwetu na ampendeze jirani yake, apate wema, akajengwe.” (Rum. 15:1, 2) Akionyesha namna lilivyo shauri zito kwa mtu aliye na imani yenye nguvu kushindwa kuwafikiria wale ambao ni dhaifu katika mambo ya dhamiri, Paulo anaonya hivi: “Na ndugu yako akiingia huzuni kwa sababu ya chakula, umeacha kwenda katika upendo. Kwa chakula chako usimharibu mtu yule ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.” “Mkiwatenda dhambi ndugu zenu na kuitia jeraha dhamiri iliyo dhaifu, mnamtenda dhambi Kristo.” (Rum. 14:15; 1 Kor. 8:11, 12) Yanayosemwa juu ya kula na kunywa yanaweza kusemwa juu ya mambo yanayopasa mavazi, tafrija, kazi na sehemu nyingine zote za maisha ya kibinadamu,​—Rum. 14:21.

14. Kunapaswaje kuweko usawa katika maoni ya wale ambao dhamiri zao ni zenye kujizuia sana na dhamiri za wale ambao si wenye kujizuia sana? Ni kanuni gani ambazo jamii zote mbili zimepaswa zikumbukwe sikuzote?

14 Kama vile ilivyo kosa kwa mtu aliye na imani yenye nguvu kuwadharau wale ambao ni wenye mashaka mno au kujaribu kuwatwika dhamiri yake juu ya dhamiri zao, ndivyo ilivyo kosa tena kwa mwenye mashaka kuwahukumu au kuwalaumu wale wanaotumia uhuru wa Kikristo. “Sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu,” Paulo anasema, halafu “kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu.” “Kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?” (Rum. 14:3-12; 1 Kor. 10:29, 30) Hata hivyo, ajaposadiki ana ‘haki’ au “uwezo” fulani juu ya msingi wa Neno la Mungu, Mkristo anayeongozwa na upendo ‘hatatafuta mambo yake mwenyewe,’ akishikilia haki zake na kujipendeza mwenyewe kwa kuwadhuru wengine, bali atafuata mfano wa Kristo, ambaye “hakujipendeza mwenyewe” katika njia ya choyo, isiyo ya kufikiria wengine.​—1 Kor. 8:9; 13:4, 5; Rum. 15:3.

DHAMIRI ZILIZOTIWA UNAJISI

15, 16. Ni tofauti gani kati ya dhamiri dhaifu na ile yenye kutiwa unajisi? Onyesha hili kutoka kwa Maandiko?

15 Ni jambo moja kuwa na dhamiri iliyo dhaifu kwa sababu ya kukosa ujuzi. Ni jambo jingine kuwa na dhamiri iliyotiwa unajisi kwa sababu ya kukataa kweli au kufuata mwendo ulio tofauti na dhamiri yako.

16 Paulo alitaka Wakristo katika Rumi na Korintho wenye mashaka mno, wale wenye kuonyesha ‘imani dhaifu’ wafikiriwe. Lakini alimwagiza Tito ‘awakemee kwa ukali’ watu katika Krete ambao hawakuwa “wazima katika imani.” Kwa sababu gani? Kwa sababu wao hawakuwa wenye mashaka mno kwa sababu ya kukosa ujuzi tu. Hawa walikuwa watu waliokuwa wakijisimamisha wenyewe kama waalimu wa maoni yao, wakipinganisha uamuzi ulioongozwa na roho wa baraza inayoongoza juu ya tohara. Akili zao na dhamiri zao vyote vilitiwa unajisi. Kazi zao zilionyesha haya.​—Rum. 14:1; Tito 1:9-15.

17. (a) Ni matokeo gani mazito yawezayo kutokea kwa sababu ya kushindwa kuwa na dhamiri safi kwa Mungu? (b) Waefeso 4:20 linatoaje msaada mwingine kwa kuonyesha kwetu ‘mfano na sura’ ya Yehova?

17 Kufuata mwendo wa kukusudia wa kosa kunaweza kuiongoza dhamiri ya mtu itiwe alama au ichomwe “kana kwamba kwa chuma cha kupigia chapa.” (1 Tim. 4:2, NW) Wengine wa namna hiyo katika siku za Paulo walikuwa “wameisukumia mbali” imani na dhamiri njema na “wakaangamia kwa habari ya Imani” yao, wakiwa wenye kuwakufuru watumishi waaminifu wa Mungu na kweli Yake. (1 Tim. 1:19, 20) Mkristo angeweza kurudia hali ya kuwa kama watu wa ulimwengu, “ambao akili zao zimetiwa giza, nao wamefarikishwa na uzima wa Mungu.” “Wakiisha kufa ganzi” kwa sababu ya ujinga wao na ugumu wa mioyo yao, dhamiri yao inawapa udhuru wa kufanya namna zote za mwenendo mpotovu, uchafu na kutamani. Lakini, kama Paulo anavyoongeza, “sivyo mlivyojifunza Kristo.” (Efe. 4:17-20) Mwana wa Mungu alitupa Kiolezo na Mfano ambao kwa huo dhamiri zetu zinaweza kuzoezwa ili kutoa ushuhuda mzuri.

KUACHA DHAMIRI ZA WENGINE ZIAMUE

18-20. (a) Simulia njia fulani kati ya zile ambazo katika hizo Paulo aliacha dhamiri za wale ambao alitumikia ziamue. (b) Kulingana na ambavyo aliwaandikia Wathesalonike na Wakorintho, je! yeye aliridhika na imani tu ya kwamba ‘Mungu anajua moyo wangu uko sawa katika mambo niyafanyayo’?

18 Kwa hakika imetupasa tutake kuepuka kuzitia dhamiri zetu unajisi, kwa kujidhuru wenyewe na wengine. Kama mtume Paulo imetupasa tuweze kusema hivi: “Ushuhuda wa dhamiri yetu, ya kwamba kwa utakatifu na weupe wa moyo utokao kwa Mungu; si kwa hekima ya mwili, bali kwa neema ya Mungu; tulienenda katika dunia, na hasa kwenu ninyi.”​—2 Kor. 1:12.

19 Angalia tena nyingine kati ya njia ambazo Paulo alitumia katika kuziacha dhamiri za wale ambao alitumikia ziamue. Yeye hakutafuta ukubwa, sifa wala uwezo juu yao. Hakuna wale kati ya mitume waliofanya bidii zaidi kuliko yeye, hata hivyo yeye hakujigawia mwenyewe mapendeleo ya pekee au kutafuta kilicho bora katika raha za kimwili kama “haki yake.” Hata aliacha kuzitumia haki zake katika njia nyingi,​—1 Kor. 9:3-18; 15:10.

20 Maoni yake hayakuwa hivi, ‘Mimi ni mtume kwa Mataifa niliyewekwa na Mwana wa Mungu mwenyewe basi mimi sijali anavyofikiri mtu ye yote. Mimi najua niko sawa; basi acha wengine wakubali bila kuuliza.’ Akiwa na mamlaka, yeye hakuwa mtawala mwenye mamlaka peke yake. Kuliko kuonyesha ushawishi wenye nguvu, yeye aliziacha dhamiri za watu ziamue katika upendo. Anawakumbusha wale waliomo katika Thesalonike kwamba yeye na wenzi wake walikuwa ‘waanana kama mama mlezi,’ katika kuwapa kwa huruma “si habari njema za Mungu tu, bali pia nafsi zetu wenyewe, kwa sababu ninyi mkawa wapendwa kwetu.” Yeye na wenzi wake walifanya bidii kwa nia katika kazi ya kimwili mchana na usiku ili wasiwatwike wengine mzigo wa gharama. Wathesalonike, anasema, kwa njia hiyo wakawa “mashahidi, na Mungu pia, namna tulivyoonekana kuwa waaminifu na wenye haki na wasio na lawama.” (1 The. 2:5-10, NW) Alipokuwa hakika kwamba moyo wake ulionekana wazi kwa Mungu, Paulo aliwaambia wale waliomo Korintho, “Natumaini ya kuwa tumedhihirishwa katika dhamiri zenu pia.”​—2 Kor. 5:10-12.

21, 22. (a) Je! inatosha kujipendekeza wenyewe kwa Mungu na dhamiri za ndugu zetu? (b) Kwa sababu gani ni jambo la maana sana kuacha dhamiri za wale ambao tunapelekea habari njema za Ufalme ziamue?

21 Katika barua ii hii kwa Wakorintho, Paulo anasema kwamba yeye na wenzi wake walikuwa wameyakana “mambo ya kisiri-siri ya kuaibishwa, tusitembee kwa ujanja, wala kulichanganya neno la Mungu, bali kwa kuifanya kweli ionekane wazi tunajipendekeza wenyewe kwa kila dhamiri ya kibinadamu machoni pa Mungu.” Pamoja na dhamiri safi kwa Mungu na kwa ndugu zetu, kama Wakristo imetupasa sisi vile vile tutafute kuwa na dhamiri safi kwa “kila dhamiri ya kibinadamu,” kutia na wale waliomo katika ulimwengu wa wanadamu. (2 Kor. 4:2, NW) Je! sisi tunafanya hivi?

22 Haitupasi tuwe na shaka hata kidogo kwamba maendeleo na matokeo mazuri ya kuhubiri kwa habari njema za ufalme wa Mungu yanategemea sana ‘kujipendekeza wenyewe kwa kila dhamiri ya kibinadamu’ kwa kuwa na dhamiri njema wenyewe, kwa kundi na kila mtu vile vile. Haitoshi kuhubiri na kufundisha kweli za Biblia kwa wengine. Pamoja na hili​—kwa kweli, kama sehemu ya kazi yetu ya kuhubiri na kufundisha​—inatupasa tuache dhamiri zao ziamue. Hawawezi kuiona mioyo yetu kama Mungu anavyoweza, lakini tunaweza kujitahidi kufunua yaliyomo katika mioyo yetu​—unyofu wetu wa moyo, uaminifu wetu, usafi wetu wa nia, upendo wetu usio wa choyo. Walakini, je! tunaweza kufanya hivi ikiwa sisi wenyewe tunashindwa kufuata yale ambayo tunahubiri?

23. Jambo gani limepaswa lituongoze tusitafute hata kidogo kuwakosesha wale ambao tunahubiria na kufundisha?

23 Tunapendezwa na hali njema ya milele ya wale walio karibu na sisi kwa kadiri gani, si jamaa na ndugu zetu za kiroho tu, bali vile vile jirani zetu, watu tunaoishi mji mmoja nao na watu wa nchi moja na sisi? Paulo aliandika hivi: “Mimi ninasema kweli katika Kristo; mimi sisemi uongo, kwa kuwa dhamiri yangu inashuhudia pamoja na mimi katika roho takatifu, kwamba nina sikitiko kubwa na umivu lisilo na mwisho katika moyo wangu . . . kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kulingana na mwili, ambao, kama hao, ni Waisraeli.” (Rum. 9:1-4, NW) Alionyesha kupendezwa kwake kwa kujitahidi kuwa na mwenendo ambao ungependeza dhamiri yao, kwa kutotaka hata kidogo kuwa mwenye kuchukiza isivyo lazima kwa dhamiri ya Kiyahudi. (Linganisha Warumi 10:1; 1 Wakorintho 9:20.) Tamaa yetu ni nyingi kwa kadiri gani kusaidia wale ambao ni wa taifa letu wapate uzima? Tuna nia ya kufika kwa kadiri gani kuepuka kuwa wenye ‘kuwakosesha wengine’?​—1 Kor. 10:32, 33.

24. Wengi kati ya watumishi wa Mungu katika nyakati za kisasa wamefanya nini ili kujipendekeza wenyewe kwa kila dhamiri ya kibinadamu machoni pa Mungu? (b) Ni maulizo gani yanayotukia kwa kuangaliwa wakati ujao?

24 Kupendezwa katika kuwa na dhamiri njema mbele za Mungu na wanadamu wote kumefanya wengi wa watumishi wa Mungu katika nyakati za kisasa wafanye mageuzi makubwa katika maisha zao​—katika mwenendo wao wa kila siku na usemi, maoni yao na namna wanavyowatendea wengine, kazi yao ya kimwili na mazoea ya biashara. Wao ‘wanajizoeza ili wawe na dhamiri isiyo na hatia mbele za Mungu na mbele ya watu sikuzote.’ (Matendo 24:16) Je! wewe unafanya hivi? Ni nini kati ya mambo yanayotokeza maulizo ya dhamiri kwa watumishi wa Mungu leo? Wakati kuacha dhamiri za wengine kunapotaka mageuzi fulani, je! wanahitaji sheria fulani ya wazi-wazi au amri au agizo ili kuwafanya wageuke? Haya ndiyo maulizo ambayo tunaachia toleo lifuatalo la Mnara wa Mlinzi lijibu.

​—Kutoka The Watchtower, Sept. 15, 1972.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki