Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 4/1 kur. 162-165
  • Ambayo Namna Unavyovaa Inaeleza Juu Yako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ambayo Namna Unavyovaa Inaeleza Juu Yako
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • AMBAYO NAMNA UNAVYOVAA INAFUNUA
  • SURA YAKO INAWEZA KUKUKAMATANISHA NA WENGINE
  • KINACHOPASWA KUAMUA MITINDO YA NYWELE
  • NAMNA GANI JUU YA MARASHI?
  • KUFUATA UONGOZI MWEMA
  • Mavazi na Sura Yako Huonyesha Ulivyo WEWE
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Kuwa Nadhifu
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kwa Nini Mavazi na Mwonekano Wetu Ni Muhimu?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Je, Mtindo Wako wa Mavazi Unamtukuza Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 4/1 kur. 162-165

Ambayo Namna Unavyovaa Inaeleza Juu Yako

Mambo ya hakika ambayo vijana wanataka kujua

“WANADAMU huitazama sura ya nje, bali [Yehova] huutazama moyo.” (1 Sam. 16:7) Kwa kuwa Mungu anautazama moyo wetu, je! ni kitu namna sura yetu ya nje inavyoonekana?

Ndiyo, ni kitu. Kwa sababu, kama vile ilivyo kweli kwamba Yehova anauona moyo, ndivyo ilivyo kweli kwamba ‘mwanadamu huitazama sura ya nje.’ Mara ya kwanza watu wanaongozwa na yale ambayo sura ya mtu inaonyesha.

Na, kwa kweli, namna unavyovaa inaweza vile vile kuonyesha jambo fulani juu ya yaliyo moyoni mwako. Namna gani?

AMBAYO NAMNA UNAVYOVAA INAFUNUA

Ulipokuwa mchanga sana, wazazi wako walikuchagulia mavazi yako. (Linganisha 1 Samweli 2:18, 19.) Huenda ikawa walikuchanulia nywele kwa njia fulani vile vile. Lakini ulipoendelea kukua inaelekea walikuruhusu useme zaidi juu ya kuchagua mavazi, vile vile mtindo wako wa nywele. Kadiri chaguo lako lilivyoonekana, ndivyo namna ulivyovaa ilionyesha ulivyo ndani, utu wako mwenyewe. Kwa hiyo, basi, mavazi yako yanaeleza nini juu yako wewe?

Je! yanakuonyesha wewe kuwa mtu mwenye majivuno na kiburi, mwenye kushikilia sana sana mitindo na kutaka kuvaa kuwapita wengine? (Linganisha Isaya 3:16-23.) Au pahali pake yanaonyesha kwamba una nia ya kutojali juu ya namna unavyoonekana, ukivaa mavazi ovyo ovyo, bila kujali matokeo yake kwa wengine?

Au​—katikati ya kadiri hizo mbili zisizofaa​—je! njia yako ya kuvaa inakuonyesha kuwa mtu wa kadiri na mwenye kuwafikiria wengine, wakati ule ule ukionyesha yanayokupendeza na chaguo la busara katika mavazi yako na mambo mengine yanayokamatana na sura yako? Kwa kweli, moyo wako unakusukuma kufanya nini katika haya yote?

Vijana wengine huenda wakalalamika kwamba kama wasipojipatanisha na mitindo wataonekana tofauti sana na wengine, wataonekana wenye mitindo ya kale. Lakini kila mara kuna kadiri unayoweza kushikilia, si kushikilia mitindo ya kale kupita kadiri wala kushikilia ya kisasa kupita kadiri. Ngoja na ufikiri, vile vile. Ni nani anayefaidika kutokana na kuwa kwako mtu wa kufikiria sana mitindo? Zaidi, mitindo inawekwa au kutiwa moyo na ulimwengu wa biashara. Wanapendezwa na jambo moja kubwa: kukusanya fedha. Unapoingia katika mikono yao kwa kweli hujifaidi mwenyewe kwa njia yo yote ya kweli au ya milele.

Kwa upande mwingine, haitupasi kuwa wachafu kwa sura. Kweli, watu wengi wana fedha kidogo. Hawana uhuru wa kutaka vitu vingi kwa kuwa hawana fedha. Lakini hata hivyo, mtu akiweka mavazi yake kuwa safi, hii inaonyesha kwamba anajiheshimu mwenyewe na ana adabu. Inaonyesha hana hatia ya nia ya kutojali. Kwa jumla hii inamletea heshima zaidi kutoka kwa wengine.

Sheria nzuri ya kufuata katika mambo yote ya maisha inapatikana katika Biblia katika Warumi 15:2: “Kila mtu miongoni mwetu na ampendeze jirani yake, apate wema, akajengwe.” Watu wengine wanatutazama zaidi kuliko tunavyojitazama wenyewe. Kwa kuwa ndivyo, je! haitupasi tujaribu kuwapa kitu watakachoona kinapendeza kutazama? Si kitu ambacho kinawafanya wajisikie kuwa hafifu kwa sababu ya sura yao wenyewe, lakini kitu kinachoonyesha tunawajali wao na maoni yao.

SURA YAKO INAWEZA KUKUKAMATANISHA NA WENGINE

Namna unavyovaa inakueleza kwa njia nyingine. Inaweza kuonyesha kuwa wewe u mmoja wa kundi fulani. Hii ilikuwa hivyo hata maelfu ya miaka iliyopita, wakati ambao Biblia ilikuwa inaandikwa.

Kwa mfano, katika kitabu cha Wafalme wa Pili tunasoma juu ya wajumbe wakirudi kwa Mfalme Ahazia na kusimulia juu ya mtu aliyewapa ujumbe fulani. Mfalme aliuliza: “Alikuwa mtu wa namna gani?” Walipoeleza mavazi yake, mfalme alisema mara moja: “Ndiye yule Eliya.” Alijuaje? Kwa sababu Eliya alivaa vazi la kumtofautisha kama nabii.​—2 Fal. 1:2, 7, 8; linganisha 2 Wafalme 2:13, 14; Mt. 3:4.

Kujulikana kama nabii lilikuwa jambo la heshima. Lakini vazi la mtu vile vile lingeweza kumkamatanisha mtu na jambo lisiloheshimiwa. Ili kutimiza kusudi fulani, mkwe wa Yuda Tamari alivua mavazi ya kumtambulisha kama mjane na akavaa kitambaa kichwani na kifuniko na kuketi kando ya njia. Yuda alipopita pale, maandishi yanasema kwamba “alipomwona alimdhania kuwa ni kahaba, maana amejifunika uso [na kifuniko cha uso].” Vazi lake lilimpa sura ya malaya.​—Mwa. 38:13-15.

Leo, kama kule nyuma, namna tunavyovaa inaweza kutushirikisha na makundi fulani ya watu, ingawa inawezekana tusizoee wanayozoea au kuamini wanayoamini. Watu wanadhani kuwa tunakubaliana na kundi la watu linalovaa namna hiyo. Je! tunaweza kuwalaumu?

Namna ya kuvaa haiwatambulishi tu mapolisi, wazima moto, au wauguzi; vile vile inawatambulisha watu ambao kazi yao ni ya aibu. Leo malaya hawavai sana shali au vifuniko vya kichwa kama walivyofanya katika Kanaani karibu miaka elfu tatu iliyopita. Lakini, mavazi yao ya kufunua uchi, ya aibu leo yanaeleza wazi hata zaidi kazi wanayozoea. Kati ya wanaume, wale wanaopendelea uasi au matendo ya kisiasa ya upinduzi wana mitindo yao ya kuwatambulisha; ndivyo na wanaume au wanawake wanaolalana wenyewe kwa wenyewe.

Je! tunataka kushirikishwa na wo wote wa hawa? Na kama tukivaa kama wao na kupatwa na magumu kama matokeo yake​—kama wakati wa kutafuta kazi au kufurahia mapendeleo fulani katika kundi la Kikristo​—je! ni nani wa kulaumiwa?

KINACHOPASWA KUAMUA MITINDO YA NYWELE

Hatuwezi kugeuza sana umbo la uso wetu au ukubwa wa masikio yetu au urefu wa shingo yetu. Lakini nywele zinaweza kupangwa sana na kutunzwa. Zinaweza kufanya mengi kwa sura ya kuvuta.

Kupamba nywele kuna historia ya kale sana. Katika kame nyingi, mitindo ya nywele imetofautiana katika nchi mbali-mbali na katika vipindi mbalimbali. Nyakati nyingine majivuno ya mwanadamu yametokeza mitindo ya nywele iliyopita kadiri. Nyuma katika karne ya kwanza mitume Paulo na Petro waliona lilikuwa jambo la maana kuwaonya wanawake wa Kikristo wasipite kadiri au kuiona mitindo ya nywele kama jambo la maana kupita kadiri. (1 Tim. 2:9; 1 Pet. 3:3) Leo, lakini, vijana wa kiume wengi, kwa nywele zao ndefu sana na nywele za mashavuni, wanavuta fikira zaidi.

Je! wanaume katika nyakati za Biblia kwa jumla hawakuwa na nywele ndefu zaidi kuliko ilivyo desturi katika nchi nyingi leo? Bila shaka walikuwa na nyingi. Lakini jambo jingine ni la hakika vile vile. Lipi? Kwamba nywele za wanaume bado zilikuwa fupi zaidi kwa kufaa kuliko zile za wanawake. Hiyo ndiyo sababu mtume Paulo angeweza kuliandikia kundi la Korintho, Ugiriki, na kusema: “Je! hayo maumbile yenyewe hayawafundishi ya kwamba mwanamume akiwa na nywele ndefu ni aibu kwake? Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni fahari kwake.” (1 Kor. 11:14, 15) “Maumbile” yanatufundishaje jambo hili?

Usemi wa Paulo haumaanishi kwamba wanaume hawawezi kukuza nywele ndefu kama za mwanamke, kwa kuwa wanaweza, na leo hesabu fulani inafanya hivyo. Akieleza juu ya matumizi ya Paulo ya neno “maumbile” hapa, mwanafunzi wa Biblia Albert Barnes alisema: “Neno hilo . . . linamaanisha kwa wazi adabu ambayo wanaume wote wanayo . . . Ni vile asili ya usawa wa wanaume inavyotaka. . . . Neno hilo . . . linaelekeza kwenye maoni ya ndani sana juu ya mambo yanayofaa na ya haki.”​—Notes on the First Epistle of Paul to the Corinthians, kur. 225, 226, tazama vile vile Aid to Bible Understanding, ukur. 1207.

Kwa hiyo watu wakati huo walijua kwamba lilikuwa jambo la “maumbile”​—linalofaa​—kwa wanaume kunyoa nywele zao kufikia urefu wa kadiri, fupi zaidi kupita zile za wanawake. Sisi, leo, tunapaswa kujua lililo la “maumbile” vile vile. Mwanamume angeweza kuacha makucha yake ya vidole yakue kwa urefu fulani​—lakini ni jambo la “maumbile” kwake ayakate, kwa kuwa hii inamrahisishia kuokota vitu na kufanya kazi. Mtu angeweza kwenda bila kunawa mikono yake au kuosha mwili kwa mwaka mzima wakati fulani​—lakini jambo linalolingana na “maumbile” (vile vile la busara na la kuleta afya njema) ni kuoga mara kwa mara. Hata wanyama wanafanya hivyo.

Kwa hiyo, kwa sababu tu jambo linawezekana, hiyo hailifanyi kuwa linalolingana na maumbile, kulingana na maelezo ya Biblia. Kwa mwanamume au kijana wa kiume kuziacha nywele hivyo kwamba anaonekana kama kijana wa kike lingali ni jambo ‘lisilo la asili.’ Ni jambo linalolingana na kizazi (na nchi) ambapo tendo la wanaume kuwalala wenzao na wanawake vile vile linaongezeka. Na Biblia inaonyesha kwamba kulalana kwa mwanamume na mwanamume na mwanamke na mwanamke vile vile ni jambo ‘lisilo la asili,’ lisilofaa na la kuchukiza mbele za Mungu.​—Rum. 1:26, 27.

Je! hii inatuwekea mipaka kuliko kadiri? Hapana, kwa kuwa sawasawa na mavazi, ndivyo zilivyo njia mbalimbali za kupanga mitindo ya nywele kwa njia ya kupendeza na kuvuta bila kuwa na adabu mbaya au kwenda kinyume cha maumbile. Kunaweza kuwa na namna nyingi za kufurahisha pasipo kupita mipaka ya yaliyo haki machoni pa Mungu.

NAMNA GANI JUU YA MARASHI?

Je! vile vile marashi yanakatazwa kama mambo yasiyolingana na maumbile? Biblia haisemi hivyo. Kama vile watu wanavyotumia mavazi si kwa sababu tu ya kufunika mwili lakini vile vile wapate sura nzuri, na kama vile Waebrania wa kale mara nyingi walivyotumia manukato ili kuifanya miili yao ipendeze zaidi, ndivyo kwa wazi marashi fulani, zaidi marhamu, yalivyotumiwa kati ya wanawake wa Kiebrania kuzuia ukavu wa ngozi na kuendeleza sura yao.

Ni nini, basi, kinachopaswa kuwa kiongozi kwa vijana wa kike leo wanaotaka kufanya yanayoleta ukubali wa Mungu? Wana lazima ya kufuata shauri jema kufanya mambo yote “pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi [au, wenye afya],” wakiacha mapambo ya maana yawe “utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.”​—1 Tim. 2:9, 10; 1 Pet. 3:3, 4.

Kweli, ni vizuri kwa vijana wa kike kujua kwamba marashi yanaweza kudhuru zaidi kuliko kuleta mema. Yanaweza kuharibu sura nzuri au kuifanya mbaya iwe mbaya zaidi. Mbali na hayo, marashi mara kwa mara yanaficha nguvu ya uchanga ambayo kwa kweli ni yenye uzuri zaidi kupita matokeo ya kuiga yanayoletwa na marashi.

Matumizi yanayopita kadiri ya marashi ya vijana wa kike kwa kawaida yanavuta fikira kwenye mambo hafifu. Lililo baya zaidi, yanaweza kuzuia uzuri wo wote wa utu (ambao kwa kweli unavuta zaidi na kuendelea kwa muda mrefu zaidi) usionekane. Matumizi yanayopita kadiri ya marashi yanaweza kuharibu utu wako mbele ya wengine na, nyumaye, yanaweza hata kuelekea kugeuza utu wako kuwa mfano ovyo ovyo ambao kwa sababu hiyo unaonyesha.​—Linganisha 2 Wafalme 9:30.

KUFUATA UONGOZI MWEMA

Katika Neno la Mungu hakuna sheria za wazi juu ya mambo haya, lakini, pahali pake, uongozi mwema unatolewa. Vijana wanapaswa wajaribu kupata maoni yaliyosawazishwa ya ulimwengu, na Biblia itawasaidia kufanya hivyo.

Wazazi wako wana haki ya asili kuweka uongozi zaidi. Kama nyumba unamoishi ingepakwa rangi ovyo ovyo kwa kuchanganya rangi vyo vyote, watu wangeshangaa kama kichwa cha nyumba (au mkewe) kina akili yo yote. Au, kama nyumba ingeachiliwa na kuwa chafuchafu, hawangemheshimu sana mwenye nyumba. Unawawakilisha wazazi wako hata zaidi ya inavyofanya nyumba. Unachukua jina lao na, kama vile yale unayofanya na kusema yanavyoonyesha mafundisho wanayokupa na namna walivyo, ndivyo na sura yako inavyoonekana. La maana zaidi, ikiwa unadai kuwa mmoja wa watumishi wa Mungu vile vile unamwakilisha. Je! sura yako inalingana na dai lako?

Fikiria maneno ya Yesu: “Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda.” (Yohana 13:17) Je! unaweza kufahamu mwenyewe maana ya yale Biblia inashauri? Au wewe u namna ya mtu anayemngoja mwingine kila mara amwambie analopaswa kufanya? Unaweza kuonyesha una ufahamu wa kweli na nguvu za utu kwa kutumia shauri la Biblia katika maisha yako. Ndipo utapata furaha ya kujua kwamba unapendeza machoni pa Mungu, Mwanawe, na wote wanaowapenda na kuwatumikia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki