Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 4/1 kur. 9-150
  • Je! Kwa Kweli Uharibifu wa Moto Unakaribia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Kwa Kweli Uharibifu wa Moto Unakaribia?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • DUNIA NA UHAI JUU YAKE KUBAKI
  • UHARIBIFU WA MOTO WAONYESHWA KATIKA UNABII, WAFANANISHWA
  • “MOTO” KUTOKA MBINGUNI
  • ONYO LA MAPEMA
  • EPUKA KUWA ‘MWOMBOLEZAJI’
  • Gari La Yehova La Kimbingu Liko Katika Mwendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • “Nikaanza Kuona Maono ya Mungu”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Sikiliza—Mlinzi wa Yehova Anena!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Kitabu Cha Biblia Namba 28—Ezekieli
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 4/1 kur. 9-150

Je! Kwa Kweli Uharibifu wa Moto Unakaribia?

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1. Ni maoni gani ya kawaida juu ya hali ijayo ya dunia?

MAISHA yetu yote tumesikia kwamba ‘siku moja dunia itachomwa kwa moto.’ Dini nyingine zinaamini jambo hili litafanywa na Mungu. Wanasayansi wengine wanasema kwamba jambo hili litatukia wakati jua litakapovimba likiwa katika maumivu makuu ya kifo, matokeo yake yakiwa ni kugharikisha dunia yote na kuiunguza.

2-6. Ni sababu gani inayoweza kutolewa, kutokana na maoni ya kisayansi, kwamba dunia na uhai ulio juu yake ilifanywa kuwako milele?

2 Je! yo yote ya tafsiri hizi ni ya kweli?

3 Mwanasayansi wa Kiingereza, H. W. Chatfield, katika kitabu chake A Scientist in Search of God, anatoa ushuhuda mwingi kwamba akili kuu ya Muumba mkuu ilifikiria namna ya kufanya dunia na uhai juu yake, na kutoa mapema matumizi ya vitu vyote vinavyotakiwa ili kuishi, zaidi kwa wanadamu. Halafu, katika sura ya mwisho, anaonyesha sababu jambo hili linatoa ushuhuda kwamba kupendezwa kwa Mungu katika mwanadamu kungeendelea vile vile:

4 “Kuumba kunakozaana sikuzote kwa kadiri kubwa hakulingani na Mkusudiaji ambaye kupendezwa kwake kulipunguzwa na muda tu wa utendaji wenyewe, na ambaye nyuma ya hapo hakupendezwa hata kidogo na viumbe ambavyo kwa njia fulani viliumbwa kwa mfano wake.”

5 Pahali pake, yeye aliyepanga namna ya kumfanya mwanadamu na akamuumba katika mfano wake mwenyewe hangemwacha kama vile baba mwenye upendo asiyoweza kuwaacha watoto wake mwenyewe kwa ghafula. Chatfield anaendelea kusema:

6 “Ujuzi wa matendo ya uumbaji unaonyeshwa na uhakika wa kisayansi kuwa ulichukua miaka mingi sana kulingana na inavyodhaniwa na mwanadamu, na inaelekea kuwa jambo lisilo la busara kwamba nyuma ya kupendezwa huko kwingi matokeo ya viumbe vyenye uhai yatupiliwe mbali kabisa na mjenzi wake.”

7. Ni jambo gani jingine Mungu amefanya linaloonyesha utunzaji wake mkuu na kumfikiria mwanadamu?

7 Basi, Muumba ambaye angefanya vitu katika njia nzuri kama hiyo na kwa uangalifu kama huo na kutumia wakati mwingi vile vile kwa busara angeweza kuarifiana na kuumba kwake, mwanadamu. Hii ingekuwa kweli zaidi kwa sababu ya uhakika wa kwamba alimpa mwanadamu daraka la kutunza uumbaji wake wa kidunia. (Mwa. 1:26-28) Biblia ina kuarifiana huko, maagizo ya Mungu na kusudi. Je! inategemeza maoni ya kwamba dunia na uhai ulio juu yake vitaendelea sikuzote?

DUNIA NA UHAI JUU YAKE KUBAKI

8. Mungu alionyeshaje utunzaji wake kwa uhai duniani wakati wa gharika ya siku za Nuhu?

8 Mungu alionyesha alipendezwa na kukusudia dunia iwepo sikuzote imejazwa na wanyama na wanadamu alipohifadhi namna ya wanadamu na za wanyama katika gharika ya dunia nzima ya siku za Nuhu. Sababu gani Mungu afanye hivyo ikiwa hakujali, au ikiwa alikusudia kuviondosha vitu hivi vyote siku moja?​—Mwa. 7:1-3; 8:1, 17.

9. Ni katika njia gani kubwa kupita zote Mungu alifunua utunzaji wake wa uhai duniani?

9 Vile vile, Mungu alikuwa mwangalifu watu wake Waisraeli waweke maandishi ya nasaba, zaidi ya ukoo ambao kupitia kwake Masihi angekuja. Sababu gani maandishi yawekwe ikiwa ukoo huo usingekumbukwa? Na sababu gani Masihi, Mwana wa Mungu, alikuja duniani? Ili uhai uhifadhiwe na uzima mkamilifu uliopotezwa na Adamu kwa jamaa yake kwa uasi urudishwe. Kwa hiyo, kwa kutoa ukombozi kwa wanadamu wanaokufa, Kristo anakuwa “Adamu wa mwisho” na “Baba wa milele.” Hivyo Mungu alionyesha kwa njia kubwa sana utunzaji wake kwa wanadamu.​—1 Kor. 15:45; Isa. 9:6.

10. Maneno ya mtunga Zaburi aliyeongozwa na roho ya Mungu yanaonyeshaje kwamba Mungu anakusudia kuendeleza uhai duniani milele?

10 Zaidi ya hayo, mtunga Zaburi aliyeongozwa na roho ya Mungu anaimba juu yake: “Uliiweka nchi juu ya misingi yake, isitikisike milele.” Halafu, nyuma ya kueleza ajabu ya kazi za Mungu za uumbaji, zaidi utoaji wake kwa wanyama, mwandikaji huyu kwa kutoa unabii anaongeza: “Utukufu wa Yehova utadumu milele. Yehova atafurahia kazi zake.” (Zab. 104:5, 31, NW) Je! Muumba angefurahiaje kazi hizi kama angeziteketeza?

UHARIBIFU WA MOTO WAONYESHWA KATIKA UNABII, WAFANANISHWA

11-13. (a) Tunawezaje kujua Biblia inachomaanisha inaposema juu ya Mungu kama akitumia moto wa kuangamiza juu ya dunia? (b) Mfano unaoangaliwa unaonyeshaje kwamba dai peke yake, au ushirika tu na wale wanaomtumikia Mungu, hautahakikisha usalama? (c) Yehova alimwonyeshaje Ezekieli kwamba angeleta hukumu kwa Yerusalemu?

11 Basi je! Biblia ina maana gani inapomsema Mungu kama akitumia moto wa uharibifu juu ya dunia? Ebu na tuone mfano katika Biblia ambao kwa wazi unatuonyesha maana yake na vile vile jambo litakalotukia karibuni sana, unaotupa sisi nafasi ya kuokoka uharibifu wa moto.

12 Jambo la kushangaza, katika kisa tutakachozungumza, moto ulikuja juu ya watu waliodai kuwa taifa la Mungu. Hii inafunua kwamba kudai tu kumtumikia Mungu, au hata ushirika na wale ambao kwa kweli wanamtumikia yeye hakuhakikishi usalama.

13 Kisa chenyewe kilikuwa njozi iliyopewa nabii Ezekieli akiwa Babeli katika mwaka wa 612 B.C.E., pamoja na utimizo wake miaka mitano nyumaye. Gari la vita la ukubwa wa kustaajabisha lilionekana na Ezekieli, juu yake pakiwa na mfano uliomwakilisha Yehova Mungu kama mwendeshaji wa gari hilo la kimbinguni. Ezekieli alikuwa amekwisha kueleza gari aliloona katika sehemu ya kwanza ya habari yake (sura ya kwanza), akieleza urefu wa kwenda juu wa magurudumu yake na wa viumbe vyenye uhai vilivyoambatana nalo. Nyumaye, gari la vita, lililoonwa na Ezekieli kama likiwa Yerusalemu, lilisimama nje ya lango la kaskazini lililoongoza mpaka kwenye behewa la ndani la hekalu. Utukufu wa Yehova ulikwisha toka juu ya gari na kukaa juu ya kizingiti cha Patakatifu Zaidi Sana pa hekalu.​—Eze. 8:3, 4; 9:3.

14. Yehova alionyeshaje kwamba angewaachilia wengine katika hukumu yenye maangamizi ambayo angeleta juu ya Yerusalemu?

14 Kwa sababu ya uasi wa Yerusalemu kwake na mazoea yake machafu na ya kuchukiza sana sana, Yehova hapo mapema kwa njia ya mfano alimwonyesha Ezekieli kwamba angewaangamiza waovu humo. Lakini kwanza alimwamuru mtu wa mfano, ‘mtu aliyevaa bafta,’ aende akipita katika mji wote na kuwatia alama watu wenye mioyo yenye haki ili wahifadhiwe. Pamoja na mtu huyu Ezekieli vile vile aliwaona watu wengine sita wenye ‘vitu vya kufisha’ mikononi mwao.​—Eze. 9:2-7.

“MOTO” KUTOKA MBINGUNI

15-17. “Mtu yule aliyekuwa amevaa bafta” alipomaliza kazi yake ya kutia alama, aliamriwa kufanya nini, na ni nini kilichoonyeshwa na uhakika wa kwamba utukufu wa Yehova ulijaza hekalu amri ilipotolewa?

15 Ezekieli anaendelea kutuambia lililotukia nyuma ya hapo:

16 “Ndipo nikaangalia, na tazama, katika anga lililokuwa juu ya vichwa vya makerubi, kulionekana juu yao kana kwamba ni yakuti samawi, kuonekana kama mfano wa kiti cha enzi. Naye akamwambia mtu yule aliyevaa bafta, akasema, Ingia kati ya magurudumu yazungukayo, yaani, chini ya kerubi, ukaijaze mikono yako yote miwili makaa ya moto, toka katikati ya makerubi, ukayamwage juu ya mji. Akaingia ndani mbele ya macho yangu.”​—Eze. 10:1, 2.

17 Kitu ambacho kingechoma mji wa Yerusalemu kingetoka katikati ya magurudumu ya gari. Utukufu wa Yehova ukijaa hekaluni, ilikuwa wazi kwamba alikuwapo kuhakikisha kwamba hukumu yake imetekelezwa.​—Eze. 10:3-5.

18-20. (a) Je! ni moto wa kibinadamu ungeteketeza Yerusalemu, au nini? (b) Matumizi ya moto katika njozi yanamaanisha nini?

18 Ezekieli ndipo anaendelea kusimulia matendo ya mtu aliyevaa bafta:

19 “Ikawa, hapo alipomwagiza huyo mtu aliyevaa bafta, akisema, Twaa moto kutoka katikati ya magurudumu yazungukayo katikati ya hao makerubi, akaingia, akasimama karibu na gurudumu moja. Na kerubi yule akanyosha mkono wake toka katikati ya makerubi, kwa moto ule uliokuwa katikati ya makerubi, akatwaa baadhi ya moto ule, akautia katika mikono ya mtu yule aliyevaa bafta; naye akautwaa, akatoka. Kukaonekana katika makerubi mfano wa mkono wa mwanadamu chini ya mabawa yao.”​—Eze. 10:6-8.

20 Haukuwa moto wa kufanywa kwa mikono ya mwanadamu ulioteketeza Yerusalemu hivyo katika njozi. Ulikuwa moto wa mwujiza kutoka kwa tengenezo la kimbinguni la Mungu likifananishwa na gari. Hii maana yake ni nini? Hii: kwamba uharibifu wa Yerusalemu KAMA kwa moto ungekuwa wonyesho wa hasira ya Yehova na ghadhabu juu ya mji huo. Katika kitabu chake cha Maombolezo nabii Yeremia anafananisha hasira ya Yehova (ambayo kwayo Yerusalemu uliharibiwa) na moto, ingawa upanga, njaa na ugonjwa wa kipuku, na vile vile moto, vilitumiwa.​—Omb. 2:2-4; 4:11.

ONYO LA MAPEMA

21. Utimizo wa kisasa wa kutawanya makaa kunakofanywa na “mtu yule aliyevaa bafta” ni nini?

21 Kwa kumtumia mtu aliyevaa bafta Yehova alikuwa akijulisha mapema kumwagwa kwa hasira yake yenye moto ambayo ingeharibu Yerusalemu. Vivyo hivyo mfano wa kisasa wa mtu aliyevaa bafta, yaani, ndugu za Yesu Kristo, waliotiwa mafuta na kuzaliwa kwa roho ya Mungu, wanatawanya ujumbe wa moto kutoka kwa Neno la Mungu katika Kristendomu yote. Hii ni kumjulisha mapema kwamba hasira ya moto ya Yehova itamwagwa juu yake katika “dhiki kubwa” inayokuja.​—Mt. 24:21.

22. Je! mashahidi wa Kikristo wa Yehova waliotiwa mafuta watashiriki sehemu yo yote katika uharibifu wa Kristendomu?

22 Njozi hii iliyopewa Ezekieli inaonyesha kwamba mashahidi wa Kikristo wa Yehova waliotiwa mafuta kwa kweli hawatamwasha moto Kristendomu, wala hawatashiriki katika kumwangamiza. Si mtu aliyevaa bafta aliyefanya kazi ya kuangamiza. Ilikuwa ni wale “watu sita” wenye vitu vya kufisha. (Eze. 9:2, 4, 5) Vivyo hivyo, mashahidi wa Yehova leo wanatangaza tu “siku ya kisasi cha Mungu wetu” kwa Kristendomu. Hawatekelezi kisasi.​—Isa. 61:1, 2; Rum. 12:19.

23, 24. (a) Mashahidi wa Yehova walitoa wapi ujumbe wa moto? (b) Kristendomu ataangamizwa namna gani?

23 Mashahidi wa Yehova walichukua ujumbe huu wa moto kwa Yehova kupitia kwa tengenezo lake la kimbinguni, “gari” lake la kimbinguni. Mmoja wa makerubi wa kimbinguni wa gari hilo la kimbinguni aliyaweka “makaa ya moto, toka katikati ya makerubi” katika mikono yao wakayatupe juu ya mji wa Kristendomu kama onyo.

24 Lakini, tengenezo la kimbinguni lisiloonekana la Yehova chini ya Yesu Kristo aliyetukuzwa litashiriki katika kuharibu Kristendomu. Chini ya uongozi wa kimbinguni mawakili wa kisiasa wa kidunia vile vile watatumiwa kufikiliza uharibifu mkubwa juu ya Kristendomu kama Wababeli walivyofanya kwa Yerusalemu mnafiki katika mwaka wa 607 B.C.E.

EPUKA KUWA ‘MWOMBOLEZAJI’

25. Kitabu cha Ufunuo kinategemezaje njozi ya Ezekieli kwa habari ya kuangamizwa kwa Kristendomu kama kwa moto?

25 Kwa hiyo uharibifu wa moto kwa Kristendomu unakaribia. Matengenezo yake ya kidini yataharibiwa. Mtume Yohana alisikia maneno ya unabii kutoka mbinguni yakisema juu ya Babeli Mkuu, milki ya ulimwengu ya dini ya uongo, ambamo dini za Kristendomu ndizo sehemu kubwa: “Kwa sababu hiyo mapigo yake yatakuja katika siku moja, mauti, na huzuni, na njaa, naye atateketezwa kabisa kwa moto. Kwa maana [Yehova] Mungu aliyemhukumu ni mwenye nguvu.”​—Ufu. 18:8.

26, 27. Sababu gani ni hatari kuwa kati ya waombolezaji wa kuanguka kwa Kristendomu au sehemu yo yote ya Babeli Mkuu?

26 Kufa kwa Babeli Mkuu, ingawa kunapatana kabisa na haki, kutakuwa na waombolezaji. Juu yao, sauti ya kimalaika ya kimbinguni inasema: “Na hao wafalme wa nchi, waliozini naye na kufanya anasa pamoja naye, watalia na kumwombolezea; wauonapo moshi wa kuungua kwake; wakisimama mbali kwa hofu ya maumivu yake, wakisema, Ole, ole, mji ule ulio mkuu, Babeli, mji ule ulio na nguvu! kwa kuwa katika saa moja hukumu yako imekuja.”​—Ufu. 18:9, 10.

27 Maandiko yanaendelea kutuambia kwamba waombolezaji wa Babeli Mkuu na vile vile wengine wote wanaokana Utawala wa Enzi Yote wa Mungu na kuchafua uumbaji wake watamfuata Babeli Mkuu katika uharibifu. Ni hatari, basi, kuendelea kushikilia kwa huruma tengenezo hilo kubwa la dini ya uongo.​—Ufu. 11:18; 19:19-21.

28. “Moto” utakaoletwa na Yehova utakuwaje kwa faida ya wanadamu, na ni lazima tufanye nini ikiwa tunapenda uzima?

28 Kwa hivyo, ingawa uharibifu wa moto unakuja, ni uharibifu utakaotakasa dunia na wale ambao kwa uchoyo hawawaheshimu wanadamu wenzao wanaotaka kuishi kulingana na kanuni za haki wakizifuata. (2 Pet. 3:12, 13) Wale wanaopendezwa na mambo yao wenyewe na si na Mungu au uumbaji wake wa ajabu ni lazima wafutiliwe mbali kana kwamba kwa moto. (Mal. 4:1) Hasira ya Mungu ni kali zaidi kwa Kristendomu, kwa kuwa amekuwa msingiziaji aliye mkubwa zaidi wa jina lake. (Ufu. 18:5-7) Ikiwa unapenda uzima na unafurahia uumbaji wa Mungu, mwache Kristendomu na dini nyingine za uongo SASA. Epuka uharibifu wa moto unaokuja kwa wafuasi wake na ‘waombolezaji.’

​—Kutoka Kitabu “The Nations Shall Know that I Am Jehovah”​—How?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki