Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 10/1 kur. 435-437
  • Je! Hali Yako na Mungu Yawapasaje Watoto Wako?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Hali Yako na Mungu Yawapasaje Watoto Wako?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Habari Zinazolingana
  • Mtumaini Mungu, Si Ufahamu Wako Mwenyewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Mungu Anaheshimu Mpango wa Jamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 10/1 kur. 435-437

Je! Hali Yako na Mungu Yawapasaje Watoto Wako?

UHAKIKA wa kihistoria unaonyesha kwamba anayofanya mzazi yana matokeo makubwa juu ya watoto wake, yanayoendelea mpaka kwenye vizazi vingi vya siku za usoni. Mwendo wa maisha unaofaa wa wazazi na mfano unaofaa lazima vitaleta matokeo mema kwa watoto wao, zaidi hivyo ikiwa wazazi ni watumishi wa kweli wa Yehova Mungu. Hali yao na Mungu ni uzima kwa watoto, iwapo watawafundisha kwa makini sheria za Mungu na kukazia ndani yao utii kwa mamlaka (uwezo) ya wazazi.

Namna gani juu ya hali, hata hivyo, ambapo mmojawapo wa wazazi ni “mwamini,” Mkristo, lakini yule mwingine si mwamini? Je! umoja huu, au uendeleo huu wa umoja bila kuachana, unamtia mwamini unajisi au uchafu, ukiwafanya watoto kuwa wachafu kama matokeo?

Hapana. Sababu gani sivyo? Kwa sababu ya kanuni za haki za Mungu, ambazo kwa hizo anaendelea kwa uaminifu, na kwa sababu ya fadhili yake yenye upendo kuwaelekea wale wanaomtumikia kwa ibada ya pekee. Anawafariji wale walio katika nyumba zilizogawanyika kwa njia ya kidini, ambapo mmoja ni mwamini na yule mwingine siyo, akisema katika Neno lake: “Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu.”​—1 Kor. 7:14.

Katika lugha za Kiebrania na Kigiriki, ambazo katika hizo Biblia iliandikwa, maneno yaliyotungwa kutoka katika neno la Kiebrania qa·dhashʹ, lililo na maana ya asili “kuwa-angavu, mpya, safi,” na kutoka katika neno la Kigiriki haʹgi·os yanatafsiriwa “-takatifu,” “-liotakaswa” na “-liotengwa.” Matumizi yote ya Kiebrania na Kigiriki yalikuwa na maana ya kidini, ya kiroho na ya kiadili. Cho chote kilichotakaswa, basi, kingekuwa safi, kitakatifu, kilichotengwa kando kwa utumishi wa Mungu.

Hali hii safi mbele za Mungu inakuja kwa mazoea ya imani katika mpango wa Mungu kupitia kwa Mwanawe. Mtu asiyezoea imani hii hajasafishwa kutokana na kutokamilika alikorithi, hali ya kuwa mwenye dhambi. Watu kama hao, wanaotajwa na mtume Paulo kama ‘wasioamini,’ huenda wakawa wanaishi maisha ya uaminifu, ya adili. Lakini hawajajitenga na ulimwengu mchafu. Hawajakubali mpango wa Mungu ili hali yao yenye dhambi iondolewe, bado hawajafunguliwa kutoka katika utumwa wa dhambi kwa kuwa wafuasi wa kweli wa Bwana Yesu Kristo. Watu kama hao, wao wenyewe, si safi mbele za macho ya Mungu.​—2 Kor. 6:17; Yak. 4:4; Yohana 8:34-36.

Angalia kwamba maneno ya mtume, katika 1 Wakorintho 7:14, hayasemi kwamba asiyeamini, kwa kifungo cha ndoa, anafanywa kuwa safi yeye mwenyewe. Yeye, kwa kweli, huenda ikawa ni mtu anayezoea mabaya au mazoea machafu. Kuliko hivyo, Paulo anasema asiyeamini anatakaswa “katika” anayeamini. Kwa hiyo Mungu anahesabu kukamatana huko kwa ndoa au umoja kuwa safi, kama fadhili yenye upendo kwa anayeamini na watoto wachanga.

Hivyo ni juu ya msingi gani Mungu anaweza kuwapendelea watoto wachanga walio katika jamaa zilizogawanyika kwa njia ya kidini? Ndoa ni kawaida iliyoanzishwa na Mungu, na kukamatana kwa ndoa ni mpango unaofaa kwa wanadamu. Kwa hiyo, ndoa yo yote inayofaa ina kibali cha Mungu. Anawahesabu wenzi wa ndoa kama “mwili mmoja.” (Mt. 19:5) Kwa hiyo, wakati ambao mmojawapo wa wenzi ni Mkristo mwaminifu, huyo hatiwi unajisi kwa kuendelea kuishi pamoja na asiyeamini. Ndoa hiyo inakubalika kwa Mungu. Kama isingalikubalika, watoto wangekuwa kama watoto wa haramu. Lakini sasa wanahesabiwa kama watakatifu, safi. Au, ikiwa wenzi wote ni wasioamini, ndoa yenyewe hailaumiwi, lakini watoto wanahesabiwa kama wazazi wao, wasiotakaswa au watakatifu kwa Mungu.

Lakini, watoto wanaohesabiwa na Mungu kama watakatifu juu ya msingi wa ustahili wa wazazi ni watoto wale wasio na umri wa kutosha kuweza kufahamu kabisa yote yanayotakiwa kutoka kwa wale wanaomtumikia Mungu. Hawawezi kufanya uamuzi wenye maana sana wao wenyewe unaotakiwa kutoka kwa wale wanaokuwa wanafunzi waliobatizwa wa Bwana Yesu Kristo. Lakini ni jambo la maana sana kukumbuka kwamba hata watoto kama hao wachanga ni lazima wajue maana ya utii ni nini. Ni lazima wawe watii kwa wazazi wao. Ni lazima wawe watoto ambao si wakaidi au wanaozoea yaliyo mabaya. (Mit. 20:11) Hii ingeweka lazima kwa wazazi, au mzazi anayeamini, awafunze watoto utii, na vile vile awafundishe kweli ya Biblia katika kila nafasi.

Si baba tu anayetakiwa kuwalea watoto “katika adabu na rekebisho la moyoni la Yehova (NW)” bali watoto vile vile wanapewa amri ya moja kwa moja: “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika kila jambo, kwa kuwa hili ni jambo la kupendeza katika Bwana,” na, “Watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki. Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi, Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia.”​—Efe. 6:1-4; Kol. 3:20, NW.

Kwa hivyo, ikiwa mtoto mchanga ni mkaidi na anatenda tofauti ya amri na maombi ya wazazi wake, ikiwa yeye, asipokuwa karibu na wazazi wake, anafanya mambo anayojua ni tofauti na mapenzi yao, au ni mabaya mbele za macho ya Mungu, ikiwa anafuatana na washiriki wanaozoea mabaya, basi bila shaka hawezi kudai yuko chini ya baraka za ustahili wa jamaa. Yeye anafuta ustahili ambao mzazi wake au wazazi wake huenda wakaleta mbele za macho ya Mungu, na ni mchafu, kama wale anaozoea mabaya nao walivyo.​—Zab. 50:16-20.

Je! kuwa na ustahili wa mzazi wa Kikristo au wazazi kuna maana gani kwa mtoto mtiifu? Maana yake ni kwamba ana kibali cha Mungu. Ana ulinzi wa Mungu na msaada, kama mzazi wake wa Kikristo alivyo navyo. Hukumu ya Mungu haimkalii, kama inavyofanya kwa ulimwengu. (2 Pet. 2:9; linganisha Zaburi 37:25, 26.) Wakati Mungu anapotekeleza hukumu juu ya waovu atawaachilia watoto hao kama walio safi, watakatifu, kama vile mzazi anayeamini alivyo mtakatifu.

Kwa upande wa pili, Biblia inatangaza: “Kwa maana, angalieni, siku ile inakuja, inawaka kama tanuru; na watu wote wenye kiburi, nao wote watendao uovu, watakuwa makapi; na siku ile inayokuja itawateketeza, asema [Yehova] wa majeshi; hata haitawaachia shina wala tawi.” (Mal. 4:1) Yerusalemu ulipoharibiwa katika mwaka wa 70 C.E. kwa sababu ya kukosa uaminifu kwa Mungu, watoto waliuawa pamoja na wazazi wao. Wakristo waliokuwa wamesikiza onyo la kinabii la Yesu kutoka nje ya mji uliohukumiwa mbele ya Warumi kuufunga kabisa pasiwe na mahali pa kutokea waliokolewa pamoja na watoto wao.

Vivyo hivyo katika uharibifu wa waovu katika taratibu hii iliyopo ya mambo kanuni itatumika: Wazao (tawi) wasiokuwa na hali yenye haki wao wenyewe watapata hukumu ile ile mbaya itakayowapata wazazi (shina).

Ufahamu wa Yehova Mungu wa watumishi wake waaminifu unafunua wazi upendo wake mkuu na shukrani kwa wale wanaompenda, vile vile kuonyesha uwezo wake wenye hekima wa kufanya “kazi zake zote zishirikiane pamoja kwa faida ya wale wanaompenda Mungu.” (Rum. 8:28, NW) Tena, haki ya Yehova inatukuzwa kwa sababu anafanya haya yote kulingana na kanuni zake zinazotajwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki