Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 9/15 kur. 429-431
  • Mungu Anaheshimu Mpango wa Jamaa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Anaheshimu Mpango wa Jamaa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • WATOTO WACHANGA SI WATU WASIO NA DHAMBI
  • WAZAZI WANA WAJIBU KWA WATOTO WAO
  • MATOKEO YENYE MFIKO WA MBALI YA MAZOEZI YA WAZAZI
  • Wazazi—Wasaidieni Watoto Wenu Wampende Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Watoto Ni “Urithi Kutoka kwa Yehova”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2026
  • Kutumia Neno la Mungu Katika Jamaa Zetu Wenyewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Watoto Wetu Ni Urithi Wenye Thamani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 9/15 kur. 429-431

Mungu Anaheshimu Mpango wa Jamaa

MTOTO anapozaliwa, marafiki na watu wa udugu wanakusanyika karibu na maneno yanasikiwa, kama haya: ‘Anafanana na baba yake!’ au, ‘Anafanana kabisa na mama yake!’ Nyakati nyingine kule kufanana na mzazi yule mwingine si kwa wazi sana katika umbo la kimwili lakini kunaonekana nyumaye katika tabia za mtoto mwenyewe. Kwa kweli, ilivyo kwetu leo ndivyo ilivyokuwa kwa mwanadamu wa kwanza Adamu, ambaye, Biblia inaeleza, “akazaa mwana kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi.”​—Mwa. 5:3.

Katika mambo ya uzazi na haki za uzazi Yehova Mungu amekuwa imara sana. Aliwapa wazazi pendeleo na uwezo wa kuwazaa watoto kwa sura yao wenyewe na mfano wao. Ndiyo, na zaidi ya hayo, anawaruhusu kuwalea watoto wao kwa njia wanayotaka. Na ijapokuwa wazazi wengine wamewaacha watoto wao na hata wengine kuwalea kama wapinzani wa Mungu, hajawanyang’anya watoto wao na kuwapa watu wengine wawatunze.

Bila shaka hii ni haki na uvumilivu mwingi kwa upande wa Mungu. Hakuna anayeweza kulalamika kwa haki kwamba Mungu alimkataza kuwazoeza watoto wake kama alivyotaka. Na hakuna mtu aliyeshindwa kuwafundisha watoto wake kanuni za Mungu anaweza kulalamika kwa haki juu ya masumbufu yanayoletwa na mwenendo mbaya wa watoto wake. Wazazi wasiojali hawawezi kuepuka kanuni ya kwamba “mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.”​—Mit. 29:15.

WATOTO WACHANGA SI WATU WASIO NA DHAMBI

Watoto wote wa wanadamu, ingawa wanarithi tabia fulani za kupendeza kutoka kwa wazazi wao, vile vile wanarithi zisizopendeza. Na, bila kumtenga ye yote kando, wote wamezaliwa wenye dhambi kama matokeo ya kupoteza hali ya baba yao wa zamani na Mungu kwa kutokutii. Biblia inatuambia: “Kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi.”​—Rum. 5:12.

Kwa kufanya dhambi, ‘kukosa shabaha’ ya kanuni ya Mungu ya ukamilifu kwake, kupungukiwa na utukufu wa Mungu, ambao alipaswa aonyeshe, Adamu alishindwa kuwapitishia watoto wake ukamilifu. Kwa hiyo taifa lote la kibinadamu lilipatwa. “Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.”​—Rum. 3:23.

Shukrani kwa fadhili isiyostahili ya Mungu, dhabihu ya ukombozi ya Kristo inaweza kuondoa dhambi ambayo mtu alizaliwa nayo. Mtu mwenyewe, kweli, ni lazima awe mwenye umri wa kuweza kuukubali mpango wa Mungu yeye mwenyewe. Lakini namna gani juu ya watoto wasio na umri wa kutosha kuweza kuonyesha imani hiyo? Wao si watu wasio na dhambi. Mtunga Zaburi Daudi alisema: “Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; mama yangu alinichukua mimba hatiani.” (Zab. 51:5) Kwa hiyo, Mungu anawatendeaje? Anawatendea hawa watoto kupitia kwa mpango wa jamaa. Sababu gani? Na kanuni hii inafanya kazi namna gani?

Yehova ana imani katika mpango wa jamaa na ameifanya jamaa kuwa umoja wenye msingi wa jamii ya kidunia. Mahali, maana na utendaji wa jamaa vinatoka kwake. Yeye ndiye Baba “ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.” (Efe. 3:15) Anaipa jamaa heshima na cheo. Baba katika jamaa ndiye kichwa, mama ndiye msaidizi, na wote wawili pamoja wana daraka walilopewa na Mungu la kuwaongoza watoto.

WAZAZI WANA WAJIBU KWA WATOTO WAO

Watoto wachanga sana ambao hawajafikia umri wa kuchukua madaraka kwa jumla wanafanana na wazazi wao kupitia kwa urithi, pamoja na, hata, mazoezi na mazingira wanayopewa na wazazi. Kwa hiyo, Mungu anawapasisha wazazi daraka mpaka mtoto atakapofikia umri wa kujitegemea mwenyewe kwa maamuzi yake na matendo yake mwenyewe. Kwa hiyo wanayofanya wazazi juu ya kukamatana kwao na Mungu yanaipata jamaa yote. Kama vile sheria ya wanadamu inavyotaka sababu ya matendo ya watoto wao wadogo, ndivyo na Mungu. Kama mtoto amefanya uhalifu, akiharibu mali, baba anaweza kuwatazamia polisi wabishe hodi kwake na kumfanyia mashtaka na kumtaka alipe vitu vilivyoharibiwa. Sababu gani, basi, haimpasi Mungu vile vile kutaka sababu kutoka kwa wazazi ya matendo ya watoto wao wachanga?

MATOKEO YENYE MFIKO WA MBALI YA MAZOEZI YA WAZAZI

Matendo ya haki au mabaya ya wazazi au mazoezi mema au mabaya wanayotoa yanaweza kuonekana katika watoto wa watoto wao, na hata katika vilembwe vyao. Kwa mfano, kizazi kinachoshughulika na mambo ya ulimwengu kinapotia fujo katika vita kinavipasisha kwa kadiri kubwa vizazi vitakavyofuata, kama yalivyokuwa matokeo ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu na ya Pili.

Kwa kuwa Mungu anawapa wazazi haki ya kuwalea watoto wao bila kuwazuia anaweza kusimulia matokeo kwa wazazi wanaofuata sheria zake na wale ambao hawafanyi hivyo. Alimwambia Musa: “Mimi, [Yehova], Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.” (Kut. 20:5, 6) Hakuna shaka juu yake: Watoto wanaolelewa vibaya wataelekea kuzoea mabaya na kupata adhabu inayostahili matendo yao.

Ibrahimu alikuwa mfano wa kichwa cha jamaa ambaye alishika njia ya Mungu na kuwafundisha watoto wake utii kwa Mungu. Hii iliendelea kuwa baraka ya muda mrefu kwa wazao wake.​—Mwa. 18:19; Kum. 4:37.

Lakini, wazao wa Ibrahimu walipogeukia ibada ya sanamu na mambo mengine maovu walichukuliwa utumwani na mataifa maadui. Kwa kweli, tangu uhamisho katika Babeli mpaka kwenye uharibifu wa Yerusalemu katika mwaka wa 70 C.E. Wayahudi mara nyingi walikuwa chini ya utawala wa mamlaka za ulimwengu, kwanza Babeli, halafu Uajemi, Ugiriki na Rumi. Wazao kwa muda wa vizazi vingi waliumia kwa sababu ya dhambi ya babu zao.

Kanuni hii vile vile ilihakikishwa katika mataifa ya kipagani. Wakati wa ujenzi wa Mnara wa Babeli, watu waliokuwa wametoka katika ibada ya Mungu wa Nuhu, Yehova, waligawanyika katika vikundi vyenye lugha mbalimbali, na mataifa yalikua kutoka kwao. Wazao wao nyumaye walijikuta ‘wamefarakana na jamii ya Israeli, wageni wasio wa maagano ya ahadi ile na walikuwa hawana tumaini, hawana Mungu duniani.’ (Efe. 2:12) Ni wale tu wamegeuka kutoka kwenye mwendo mbaya wa babu zao, wakiacha upagani, wamekuja kumjua Mungu kwa kuchukua ibada yake.

Mfano wa jambo hili, wa hukumu ya watoto wachanga pamoja na wazazi wao waovu, ni ule wa Wakanaani. Kwa sababu ya historia yao ya uovu mwingi sana watoto wao wachanga waliuawa pamoja nao, kwa amri ya Mungu, Waisraeli walipokaa katika nchi ile.​—Kum. 7:1, 2.

Haya yote yanaonyesha kwamba Mungu anawahesabia watoto wachanga wa jamaa fulani sifa njema au kosa, kwa kutegemea hali ya wazazi wenyewe. Je! kuna jambo jingine linalotakiwa kutoka kwa wazazi, kuliko kuwa tu waabudu wa Mungu wa kweli Yehova? Na kuna jambo lo lote linalotakiwa kutoka kwa watoto? Vile vile, namna gani juu ya jamaa ambapo ni mzazi mmoja tu aliye mwabudu wa Yehova na mwanafunzi wa Yesu Kristo? Maulizo haya yatazungumzwa katika makala ifuatayo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki