Maswali Kutoka kwa Wasomaji
● Je! inapatana na kuendeleza dhamiri ya Kikristo kwa mtu kukubali kazi inayotia kuwa na silaha, kuchukua ama bunduki ama rungu?—U.S.A.
Yehova mwenyewe aliziruhusu serikali za kibinadamu zitumie mamlaka ili kufikiliza sheria, kwa njia ya kutumia silaha iwapo ni lazima. Kwa habari ya mamlaka hiyo ya kiserikali tunasoma hivi: “Kwa maana hauchukui upanga bure; kwa kuwa ni mtumishi wa Mungu, amlipizaye kisasi mtenda mabaya kwa ajili ya ghadhabu.” (Rum. 13:4) Kwa sababu hiyo hakuna katazo la Maandiko liwezalo kutokezwa kupinga kuwako kwa serikali wala kupinga serikali kuwaruhusu watu fulani kuchukua silaha wanapolinda mali na au watu.
Walakini, kwamba Mkristo angechagua kazi, kama ile ya kuwa askari polisi, mlinzi (guard au night watchman) au anayelinda usiku, ikiwa angetakiwa kuchukua bunduki ama silaha nyingine hilo ni jambo ambalo ingempasa aamue mwenyewe. Angetaka afikirie haya: Je! mimi nataka nichukue mzigo wa kufanya maamuzi ya haraka na magumu wakati wa hali ya hatari ikiwa uhai wa kibinadamu uko hatarini? Je! mimi ninayo nia ya kuingia katika hali ambazo zingeweza kunitaka mimi nitumie silaha, labda nikifanya hivyo katika njia ambayo ingeleta hatia ya damu mbele za Yehova?
Tena, shabaha kubwa ya Mkristo ni kuwasaidia wengine wapate maarifa ya kweli. Yeye anataka awafundishe wengine namna ya kuwa “katika amani na watu wote.” (Rum. 12:18) Kulingana na hili, labda atajiuliza mwenyewe hivi, Je! kuchukua kwangu silaha katika kazi yangu kutaonekana kwa wengine kama kupinganisha mafundisho ya Kikristo? Je! kunayo sababu ya kusadiki kwamba litakuwa kwazo? Inampasa Mkristo ajifanyie uamuzi wake mwenyewe ukiwa juu ya msingi wa Neno la Mungu na kujua kwake hali zilizoko. Ikiwa yeye anaona kwamba kufanya kazi hiyo ya kuchukua silaha kungekuwa kwenye madhara katika kuenezwa kwa kweli ya Biblia, lingekuwa jambo la hekima kwa Mkristo kuchagua kazi nyingine. Shauri la maandiko ni ‘kutokuwakwaza wengine.’—Flp. 1:10, NW.
Uamuzi wo wote anaofanya Mkristo, umepaswa upatane na dhamiri yake iliyozoezwa na Maandiko. Lakini si lazima ajione hata kidogo kukazwa na hangaiko kwa sababu ya kukosa riziki. Uhakikisho wa Neno la Mungu ni: “Yehova ni mpenda haki, naye hatawaacha waaminifu wake.” (Zab. 37:28, NW) “Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa.”—Ebr. 13:5.