Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • es26 uku. 17-26
  • Mwezi wa 2

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mwezi wa 2
  • Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
  • Vichwa Vidogo
  • Siku ya Yenga, 1 Mwezi wa 2
  • Siku ya Kwanza, 2 Mwezi wa 2
  • Siku ya Pili, 3 Mwezi wa 2
  • Siku ya Tatu, 4 Mwezi wa 2
  • Siku ya Ine, 5 Mwezi wa 2
  • Siku ya Tano, 6 Mwezi wa 2
  • Siku ya Posho, 7 Mwezi wa 2
  • Siku ya Yenga, 8 Mwezi wa 2
  • Siku ya Kwanza, 9 Mwezi wa 2
  • Siku ya Pili, 10 Mwezi wa 2
  • Siku ya Tatu, 11 Mwezi wa 2
  • Siku ya Ine, 12 Mwezi wa 2
  • Siku ya Tano, 13 Mwezi wa 2
  • Siku ya Posho, 14 Mwezi wa 2
  • Siku ya Yenga, 15 Mwezi wa 2
  • Siku ya Kwanza, 16 Mwezi wa 2
  • Siku ya Pili, 17 Mwezi wa 2
  • Siku ya Tatu, 18 Mwezi wa 2
  • Siku ya Ine, 19 Mwezi wa 2
  • Siku ya Tano, 20 Mwezi wa 2
  • Siku ya Posho, 21 Mwezi wa 2
  • Siku ya Yenga, 22 Mwezi wa 2
  • Siku ya Kwanza, 23 Mwezi wa 2
  • Siku ya Pili, 24 Mwezi wa 2
  • Siku ya Tatu, 25 Mwezi wa 2
  • Siku ya Ine, 26 Mwezi wa 2
  • Siku ya Tano, 27 Mwezi wa 2
  • Siku ya Posho, 28 Mwezi wa 2
Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
es26 uku. 17-26

Mwezi wa 2

Siku ya Yenga, 1 Mwezi wa 2

Ni heshima kwa mutu kujiepusha na mabishano, lakini kila mupumbavu atajiingiza ndani.—Mez. 20:3.

Ndugu wenye kuwa na sifa za Kikristo wanasaidia sana kutaniko. Mwanaume mwenye usawaziko anafuatilia amani. Kama unapenda kujulikana kuwa mutu mwenye usawaziko, sikiliza bengine na ukuwe tayari kukubali mawazo yao. Mu mukutano utakuwa tayari kukubali uamuzi wa batu mingi kama hakuna sheria ao kanuni fulani ya Biblia yenye inavunjwa. Haupaswe kukazia mambo ikuwe tu vile weye unapenda. Unajua kama ni jambo ya lazima kusikiliza mawazo ya bengine. (Mwa. 13:​8, 9; Mez. 15:22) Kuliko kuwa mukali ao kubishana na bengine, ubatendee kwa busara na kwa upole. Juu unapenda amani, unakamata hatua ya kufanya amani hata kama hali iko nguvu. (Yak. 3:​17, 18) Maneno yako yenye upendo inaweza kutuliza bengine, hata bapinzani.—Amu. 8:​1-3; Mez. 25:15; Mt. 5:​23, 24. w24.11 23 fu. 13

Siku ya Kwanza, 2 Mwezi wa 2

Atatuma malaika na kukusanya watu wake wenye kuchaguliwa kutoka pande ine (4) za dunia, kutoka mwisho wa dunia mupaka mwisho wa mbingu.—Mk. 13:27.

Hata kama Yesu alikufa “mara moja kwa wakati wote,” angali anatumika sana kwa ajili yetu. (Ro. 6:10) Namna gani? Anaendelea kutumia wakati na nguvu yake juu tupate baraka zenye bei ya ukombozi inatuletea. Fikiria mambo yenye iko nafanya: Iko natawala mbinguni akiwa Mufalme wetu, Kuhani Mukubwa, na kichwa cha kutaniko. (1 Ko. 15:25; Efe. 5:23; Ebr. 2:17) Anasimamia kazi ya kukusanya watiwa-mafuta na kundi kubwa, na anapaswa kumaliza ile kazi mbele taabu kubwa imalizike. (Mt. 25:32) Anahakikisha pia kama watumishi wake waaminifu wanapata chakula ya kiroho yenye wako nayo lazima mu hizi siku za mwisho. (Mt. 24:45) Na hata mu Utawala wake wa Miaka Elfu ataendelea kututumikia. Kwa kweli, Yehova alitoa Mwana wake haiko tu juu akufe kwa ajili yetu lakini pia juu aendelee kutufanyia mambo ingine ya mingi! w25.01 24 fu. 12

Siku ya Pili, 3 Mwezi wa 2

Ni zawadi ya bure kwamba wanatangazwa kuwa wenye haki kwa fazili zake zenye hazistahiliwe kupitia kuachiliwa huru kwa njia ya bei ya ukombozi yenye Kristo Yesu alilipa.—Ro. 3:24.

Wakati Yehova anasamehe, anasamehe kabisa-kabisa. Ile inafanya tukuwe na uhusiano muzuri pamoya na Baba yetu wa mbinguni. Wakati uleule tunakumbuka kama musamaha wa kweli ni zawadi. Yehova anatusamehe haiko juu tunastahili musamaha wake, lakini musamaha ni zawadi yenye Yehova anapatia wanadamu wenye hawakamilike kwa sababu ya upendo wake na fazili zake zenye hazistahiliwe. Tuko wenye shukrani sana juu Yehova ni Mungu wa “musamaha wa kweli”! (Zb. 130:4; Ro. 4:8) Lakini juu Yehova atusamehe tunapaswa kufanya jambo fulani ya maana. Yesu alisema hivi: “Kama hamusamehe watu makosa yao, Baba yenu pia hatawasamehe ninyi makosa yenu.” (Mt. 6:​14, 15) Kwa hiyo, ni jambo ya maana kuiga musamaha wa Yehova. w25.02 13 fu. 18-19

Siku ya Tatu, 4 Mwezi wa 2

Kutakuwa ufufuo wa wenye haki na wenye hawako wenye haki.—Mdo. 24:15.

Fikiria watu wa Sodoma na Gomora. Loti, mwanaume mwenye haki, aliishi kati yao. Lakini, tunajua ikiwa aliwahubiria wote? Hapana. Ni kweli kwamba walikuwa watu wabaya, lakini walijua kabisa tofauti kati ya mema na mabaya? Kumbuka kama kikundi ya wanaume wa mu ule muji walitafuta kulala kinguvu wageni wa Loti. Biblia inasema kama mu ile kikundi mulikuwa “kuanzia kijana mwanaume mupaka muzee.” (Mwa. 19:4; 2 Pe. 2:7) Tunajua kabisa ikiwa Yehova, Mungu mwenye rehema, alihukumu kila mumoja wao bila tumaini ya ufufuo? Yehova alihakikishia Abrahamu kama mu ule muji hamukukuwa hata wanaume kumi wenye haki. (Mwa. 18:32) Juu hawakukuwa wenye haki, Yehova alikuwa na haki ya kuwaharibu kwa sababu ya matendo yao. Lakini tunaweza kusema kwa uhakika kabisa kama hakuna hata mumoja wao mwenye atafufuliwa kati ya “wenye hawako wenye haki”? Hapana, hatuwezi kusema vile kwa uhakika! w24.05 2 fu. 3; 3 fu. 8

Siku ya Ine, 5 Mwezi wa 2

Muendelee kutafuta kwanza Ufalme na haki yake, na mutaongezewa vitu hivyo vingine vyote.—Mt. 6:33.

Kwa sababu ya magumu ya kupata makuta, Wakristo fulani bamekubali kazi yenye iliobaomba baende mbali na famlia, lakini ku mwisho balielewa kama ile haikukuwa uamuzi wa hekima. Mbele ya kuitika kazi ya mupya, usifikirie tu makuta yenye utapata lakini fikiria pia matokeo yenye ile kazi itakuwa nayo juu ya hali yako ya kiroho. (Lu. 14:28) Ujiulize hivi: ‘Kama ninaenda kutumikia mbali, ile itakuwa na matokeo gani juu ya ndoa yangu? Kwenye nitaenda nitakuwa nakusanyika, kuhubiri, na kupitisha wakati pamoya na ndugu na dada kwa ukawaida?’ Kama uko na batoto ujiulize pia hii ulizo ya maana: ‘Namna gani nitakomalisha batoto yangu “katika nizamu na maonyo ya Yehova” kama siishi nabo fasi moya?’ (Efe. 6:4) Mawazo ya Mungu njo ikuongoze, hapana ya batu ya familia ao barafiki benye habaheshimie kanuni za Biblia. w25.03 29 fu. 12

Siku ya Tano, 6 Mwezi wa 2

Tusikuwe tena watoto.—Efe. 4:14.

Ni mwepesi kwa Mukristo mwenye anabakia mutoto kiroho aamini “udanganyifu” na “ujanja wa watu.” Pia ni mwepesi aamini waasi-imani na habari za uongo zenye kuenezwa, ao habari zenye hazina musingi zenye kutolewa ku vyombo vya habari. Anaweza kuwa na muelekeo wa kusikilia wengine wivu, wa kukosa kuelewana na wengine, kukasirika haraka, ao kuangukia mu jaribu. (1 Ko. 3:3) Maandiko inalinganisha kukomaa kiroho na kukomaa kimwili. (Efe. 4:15) Mutoto mudogo hakuwake na utambuzi, na iko na lazima mutu amuongoze. Kwa mufano, mama anaweza kukamata mukono wa mutoto wake mbele wavuke barabara. Wakati anaanza kukomaa, mama yake anaweza kumuruhusu avuke barabara yeye peke, lakini atamukumbusha aangalie pande zote mbele ya kuvuka. Wakati ule mutoto anakuwa mutu muzima, yeye mwenyewe atajua namna ya kuepuka hatari za mu barabara. Vilevile, wakati Mukristo anakomaa kiroho, anachunguza kanuni za Biblia juu ajue mawazo ya Yehova kuhusu ile jambo na kisha anatenda kulingana na mambo yenye amejifunza. w24.04 3 fu. 5-6

Siku ya Posho, 7 Mwezi wa 2

Ee Yehova, ni nani anaweza kuwa mugeni katika hema yako?—Zb. 15:1.

Kwa wakati fulani, marafiki wa Yehova walikuwa tu wale wenye walikuwa naishi pamoya naye mbinguni. Kisha aliumba wanadamu ku dunia. Nao pia wangekuwa wageni mu hema yake. Kisha wakati, kati ya wanadamu wenye walifikia kuwa wageni wa Yehova kulikuwa Enoko, Noa, Abrahamu, na Yobu. Biblia inasema kama wale waabudu wa kweli walikuwa marafiki wa Mungu, ao walitembea “pamoja na Mungu wa kweli.” (Mwa. 5:24; 6:9; Yob. 29:4; Isa. 41:8) Kwa miaka mingi, Yehova aliendelea kualika marafiki wake ili wakuwe wageni wake. (Eze. 37:​26, 27) Kwa mufano, unabii wa Ezekieli unaonyesha kama Mungu anapenda kabisa waabudu wake washikamanifu wakuwe na urafiki wa karibu pamoya naye. Anaahidi kufanya “agano la amani pamoja nao.” Ule unabii unazungumuzia wakati wenye wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi mbinguni na wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi milele ku dunia, wataunganishwa na kuwa “kundi moja” mu hema yake ya mufano. (Yoh. 10:16) Ule unabii uko natimia mu wakati wetu! w24.06 2 fu. 2; 3 fu. 4, 5

Siku ya Yenga, 8 Mwezi wa 2

Mungu wetu alitufanya tusikuwe na woga.—1 Te. 2:2.

Juu tuko watu wa Yehova, tunaunga mukono Ufalme wa Mungu kwa moyo wote. Lakini mara mingi inaombaka tukuwe hodari juu tuweze kufanya vile. (Mt. 6:33) Kwa mufano, mu huu ulimwengu muovu, inaomba kuwa hodari ili kutumikisha kanuni za Yehova mu maisha yetu, na kuhubiri habari njema. Na juu watu wanaendelea kugawanyika, inaomba uhodari ili kuepuka kujiingiza mu mambo ya politike. (Yoh. 18:36) Watumishi wengi wa Yehova wamepoteza vitu vyao, wametendewa mubaya kimwili, ao hata wamefungwa juu wamekataa kujiingiza mu mambo ya politike ao mu jeshi. Tunapata nguvu na uhodari wakati tunafikiria mifano ya wale wenye kuwa hodari, wenye waliunga mukono Ufalme wa Yehova. Mufalme wetu, Kristo Yesu, alikataa kabisa kujiingiza mu mambo ya politike ya huu ulimwengu wa Shetani. (Mt. 4:​8-11; Yoh. 6:​14, 15) Sikuzote alimutegemea Yehova ili amupatie nguvu. w24.07 3 fu. 4; 4 fu. 7

Siku ya Kwanza, 9 Mwezi wa 2

Akaanza kukamata matunda ya muti huo na kuyakula. Kisha, wakati alikuwa pamoja na bwana yake, akamupatia pia, naye akaanza kuyakula.—Mwa. 3:6.

Yehova aliandikisha ile habari ya kuhuzunisha kwa ajili yetu. Inatusaidia kuelewa juu ya nini anachukia sana zambi. Zambi inatutenganisha na Yehova Baba yetu na inaleta kifo. (Isa. 59:2) Njo maana Shetani, ule kiumbe wa roho muasi mwenye alianzisha hii magumu yote, anapenda sana zambi na anapenda kuchochea batu baifanye. Pengine aliwaza kama wakati Adamu na Eva walifanya zambi alisimamisha kusudi ya Yehova kwa ajili ya wanadamu. Hakuelewa kama Yehova iko na upendo mingi sana. Yehova hakubadilisha kusudi yake kwa ajili ya wazao wa Adamu na Eva. Juu anapenda wanadamu, palepale bila kukawia, aliwatolea tumaini. (Ro. 8:​20, 21) Yehova alijua kama wazao fulani wa Adamu na Eva wangechagua kumupenda na wangetafuta musaada wake juu ya kupiganisha zambi. Na juu Yehova ni Baba yao na Muumbaji wao, angewafungulia njia ya kutoka katika zambi juu wamukaribie. w24.08 3 fu. 3-4

Siku ya Pili, 10 Mwezi wa 2

Muhakikishe mambo ya maana zaidi.—Flp. 1:10.

Watumishi wengi wa Yehova wako na mambo mingi ya kufanya. Wanatumikaka juu ya kutimiza mahitaji yao ya kimwili na mahitaji ya familia zao. (1 Ti. 5:8) Wakristo wengi wanahangaikia watu wa familia yao wenye kuwa wagonjwa ao wenye kuzeeka. Na siye wote tunapaswa kuhangaikia afya yetu, ile pia inakamataka wakati. Zaidi ya ile mambo, tuko na migao mu kutaniko. Na mugao wa maana zaidi wenye tuko nao, ni kufanya kazi ya kuhubiri kwa bidii. Kwetu siye Wakristo, kusoma Biblia ni kati ya “mambo ya maana zaidi.” Kwa hiyo, tunapaswa kuhakikisha kama tunaisoma. Kuhusu mutu mwenye furaha, zaburi ya kwanza inasema hivi: “Anapendezwa na sheria ya Yehova, na anasoma sheria Yake kwa sauti ya chini muchana na usiku.” (Zb. 1:​1, 2) Ile maneno inaonyesha kama inaomba kutia wakati pembeni ili kusoma. Inakuwaka muzuri kusoma Biblia saa gani? Kila mutu iko na saa yenye ni ya muzuri kwake. Lakini inapaswa kuwa saa yenye utaweza kufanya vile kwa ukawaida. w24.09 3 fu. 5-6

Siku ya Tatu, 11 Mwezi wa 2

Kila mutu atabeba muzigo wake mwenyewe.—Gal. 6:5.

Mukristo mukomavu anaweza kuwa na lazima ya musaada wa mutu mwingine? Ndiyo. Wakati fulani Mukristo mukomavu anaweza kuwa na lazima ya kuomba musaada. Lakini iko tofauti na mutu mwenye hakomae kiroho mwenye anaweza kutazamia wengine wamuambie mambo ya kufanya ao wamukamatie uamuzi. Mukristo mukomavu yeye anaweza kufaidika na hekima na uzoefu wa wengine, lakini wakati uleule anatambua kama Yehova anapenda kila mutu ‘abebe muzigo wake mwenyewe.’ Sawa vile watu wazima hawafanane kimwili, Wakristo wakomavu wanaweza kuonyesha mu njia tofauti sifa mbalimbali za Kikristo sawa vile hekima, uhodari, ukarimu, na sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine. Zaidi ya ile, mu hali ileile, Wakristo wawili wenye kukomaa kiroho wanaweza kukamata maamuzi yenye haifanane. Lakini, hata kama ile maamuzi iko tofauti, yote inategemea Biblia. Inakuwaka vile zaidi sana mu mambo yenye kuhusu zamiri. Njo maana Wakristo wakomavu wanaepuka kuhukumu maamuzi ya wengine juu tu iko tofauti na yao. Lakini, wanajikaza kuendeleza umoja.—Ro. 14:10; 1 Ko. 1:10. w24.04 4 fu. 7-8

Siku ya Ine, 12 Mwezi wa 2

Wakati mahangaiko yalinilemea, ulinifariji na kunituliza.—Zb. 94:19.

Unaweza kufanya nini kama unajiona kuwa mutu wa bure? Soma maandiko ya Biblia yenye itakuhakikishia kama Yehova anakuona kuwa wa maana, na ufikiri sana juu ya ile maandiko. Kama ulishindwa kutimiza muradi fulani ao kama unavunjika moyo juu hauwezi kafanya mambo mingi sawa bengine, usijihukumu kupita kiasi. Yehova hatuombake mambo yenye inapita uwezo wetu. (Zb. 103:​13, 14) Kama mutu alikutendea mubaya zamani, usiwaze kama ni kosa yako. Kosa ni ya mutu mwenye alikutendea mubaya! Kumbuka kama kwa Yehova ni ule mwenye alitenda mubaya njo iko na kosa, haiko mwenye balitendea mubaya. (1 Pe. 3:12) Kuwa hakika kama Yehova anaweza kukutumikisha juu ya kusaidia bengine. Amekupatia pendeleo ya kutumika pamoya naye mu kazi ya kuhubiri. (1 Ko. 3:9) Mambo yenye ilikufikia mu maisha zamani inakusaidia kujitia pa nafasi ya bengine na kuelewa muzuri namna bengine banajisikia. Unaweza kubasaidia. w24.10 7-8 fu. 6-7

Siku ya Tano, 13 Mwezi wa 2

Je, Mungu hatahakikisha kuwa haki imefanywa kwa ajili ya wachaguliwa wake wenye wanamulilia muchana na usiku, wakati yeye anaendelea kuwavumilia? Ninawaambia ninyi, atahakikisha kwamba wanatendewa haki haraka.—Lu. 18:​7, 8.

Yehova anahangaikia sana namna tunatendewa. “Yehova anapenda haki.” (Zb. 37:28) Yesu alisema kama Yehova ‘atahakikisha kuwa haki imefanywa . . . haraka,’ kwa wakati wenye kufaa. Na karibuni atamaliza mateso yetu yote na ukosefu wote wa haki. (Zb. 72:​1, 2) Kuko wakati wenye ku dunia kutakuwa tu batu benye haki. Mbele ile wakati ifike, Yehova anatuonyesha namna ya kutenda wakati tunatendewa bila haki. (2 Pe. 3:13) Anatufundisha kuepuka kutenda mu njia yenye haifae wakati banatutendea bila haki. Yehova anatupatia mufano muzuri sana wa Mwana wake wenye unaonyesha namna ya kutenda wakati banatutendea bila haki. Na anatupatia mashauri ya muzuri sana yenye tunaweza kutumikisha. w24.11 2-3 fu. 3-4

Siku ya Posho, 14 Mwezi wa 2

Muwapatie chakula.—Mt. 14:16.

Ombi ya Yesu ya kupatia batu chakula ilionekana kuwa haitawezekana juu kulikuwa banaume karibu 5000, na kuongeza banamuke na batoto pengine kulikuwa batu 15000. (Mt. 14:21) Kisha Andrea akasema hivi: “Hapa kuko kijana mwanaume mwenye iko na mikate tano (5) ya shayiri na samaki wawili wadogo. Lakini vitu hivi ni nini kwa watu hawa wengi?” (Yoh. 6:9) Bamaskini balizoea kula mikate ya shahiri, batu bengine pia balikuwa naikula. Na pengine zile samaki za kidogo zilikuwa zimetiwa chumvi na kukaushwa. Lakini, ile chakula yenye ule kijana alikuwa nayo ilikuwa ya kidogo sana, haingeenea bale batu yote. Juu Yesu alipenda kuonyesha bale batu ukarimu, alibaambia baikale chini mu mayani mu bikundi-bikundi. (Mk. 6:​39, 40; Yoh. 6:​11-13) Biblia inasema kama kisha pale Yesu alitoa shukrani kwa Baba yake kwa ajili ya ile mikate na samaki. Ilifaa kabisa kumushukuru Mungu juu ile chakula ilitoka kwake. Ile inatufundisha kama tunapaswa kufuata mufano wa Yesu kwa kusali mbele ya kula. Kisha Yesu akaambia mitume wake wagabulie batu chakula, na batu yote bakakula na kushiba. w24.12 3 fu. 3-4

Siku ya Yenga, 15 Mwezi wa 2

Mumusifu Yehova Mungu wenu.—1 Ny. 29:20.

Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alitukuza Baba yake kwa kuonyesha kama ni Baba yake njo alimupatia nguvu ya kufanya miujiza. (Mk. 5:​18-20) Yesu alimutukuza Baba yake mu njia ingine. Alimutukuza kupitia namna alitendea wengine, na kupitia mambo yenye alisema juu ya Baba yake. Siku moya, Yesu alikuwa nafundisha mu sinagogi. Kati ya wenye walikuwa namusikiliza, kulikuwa mwanamuke moya mwenye alikuwa na pepo muchafu kwa miaka 18. Ule pepo muchafu alifanya mwili wa ule mwanamuke ukunjame mara mbili na hangeweza kusimama wima. Ile ilikuwa hali ya kuhuzunisha sana! Juu Yesu alimusikilia huruma, alimukaribia na akamuambia hivi kwa upole: “Mwanamuke, umefunguliwa kutoka katika uzaifu wako.” Kisha akamugusa na mara moya akasimama wima na “kuanza kumutukuza Mungu.” Ule mwanamuke alikuwa sasa na afya ya muzuri! (Lu. 13:​10-13) Alikuwa na sababu ya muzuri ya kumupatia Yehova utukufu, na siye tuko na sababu za kufanya vile. w25.01 2-3 fu. 3-4

Siku ya Kwanza, 16 Mwezi wa 2

Utusamehe zambi zetu.—Lu. 11:4.

Inawezekana tupate tena mambo yote yenye Adamu na Eva walipoteza? Kwa uwezo wetu siye wenyewe haiwezekane. (Zb. 49:​7-9) Bila musaada, hatungekuwa na tumaini ya wakati wenye kuya ao ya ufufuo. Sawa vile wanyama hawakuwake na tumaini, wakati tungekufa, na siye maisha yetu ingeishia pale. (Muh. 3:19; 2 Pe. 2:12) Baba yetu mwenye upendo, Yehova, ametupatia zawadi yenye inalipa deni ya zambi yenye tuliriti kutoka kwa Adamu. Yesu alisema hivi juu ya ile: “Mungu alipenda ulimwengu sana na hivyo akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee, ili kila mutu mwenye anamuamini asiharibiwe lakini apate uzima wa milele.” (Yoh. 3:16) Zaidi ya ile, ile zawadi inafanya iwezekane tukuwe na uhusiano muzuri pamoya na Yehova. Ile zawadi ya muzuri sana inafanya “madeni” yetu ao zambi zetu zisamehewe. w25.02 3 fu. 3-6

Siku ya Pili, 17 Mwezi wa 2

Kisha [Sauli] akasimama na kubatizwa.—Mdo. 9:18.

Ni nini ilimusaidia Sauli abatizwe? Wakati Yesu mwenye alikuwa sasa mbinguni alimutokea, Sauli akakuwa kipofu. (Mdo. 9:​3-9) Alifunga kwa siku tatu, na bila shaka aliwaza sana juu ya jambo yenye ilimufikia. Sauli akakuwa hakika kama Yesu alikuwa Masiya na kama banafunzi ba Yesu balikuwa mu dini ya kweli. Mufano wa Sauli unaweza kutufundisha mambo mingi. Kiburi na kuogopa banadamu vingemuzuia kubatizwa. Lakini hakuruhusu ile mambo imuzuie. Alikuwa tayari kuwa Mukristo hata kama alijua kama kuwa Mukristo kutamuletea mateso. (Mdo. 9:​15, 16; 20:​22, 23) Kisha kubatizwa, aliendelea kumutumainia Yehova amusaidie kuvumilia majaribu. (2 Ko. 4:​7-10) Wakati unabatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova, na weye unaweza kupata majaribu ya imani ao magumu; lakini hauko weye peke. Unaweza kuwa hakika kama Yehova na Kristo wataendelea kukutegemeza.—Flp. 4:13. w25.03 4 fu. 8-9

Siku ya Tatu, 18 Mwezi wa 2

Namna ninakimbia haiko bila kusudi.—1 Ko. 9:26.

Kusoma Biblia ni muradi ya muzuri. Lakini, kuko mambo ingine yenye tunapaswa kufanya kama tunapenda usomaji wetu utuletee kabisa faida. Fikiria hii mufano: Mvula ni ya lazima juu mimea iote, lakini kama mvula inanyesha ya mingi sana mu wakati kidogo, mayi inaweza kuwa ya mingi sana, na kama ile inatokea, mvula haitasaidia. Inaomba wakati juu mayi ya mvula iingie mu budongo na kusaidia mimea ikomale. Vilevile tunapaswa kuepuka kusoma Biblia mbiombio, ni kusema kusoma haraka mupaka mambo yenye tulisoma inakosa wakati wa kuingia kabisa mu moyo wetu juu tuweze kuikumbuka na kuitumikisha. (Yak. 1:24) Wakati fulani unasomaka Biblia mbiombio? Kama ni vile, unapaswa kufanya nini? Punguza mwendo. Ujikaze kufikiria mambo yenye uko nasoma ao yenye unatoka tu kusoma. Unaweza kuamua kuongeza wakati yenye unatumia juu ya kujifunza, juu upate wakati wa kufikiri ao kutafakari. w24.09 4 fu. 7-9

Siku ya Ine, 19 Mwezi wa 2

Mutii wale wenye wanaongoza kati yenu.—Ebr. 13:17.

Wakati wazee wanapewa muongozo, wanapaswa kuusoma kwa uangalifu na kisha kujikaza sana kuutumikisha. Wanapewa muongozo kuhusu namna ya kuongoza mikutano na namna ya kusali kwa ajili ya kutaniko, lakini pia namna ya kuhangaikia kondoo wa Kristo. Wakati wazee wanafuata muongozo wa tengenezo, ile inafanya ndugu na dada wenye kuwa chini ya uongozi wao wajisikie kuwa salama na wajisikie kuwa wanapendwa. Wakati wazee wanatutolea muongozo, tunapaswa kuwa tayari kuufuata. Kama tunafanya vile, tutasaidia wale wenye kuongoza wafanye kazi yao muzuri zaidi. Biblia inatutia moyo tutii na tujitiishe kwa wale wenye kuongoza. (Ebr. 13:7) Wakati fulani haikuwake mwepesi kufanya vile. Juu ya nini? Juu wale wanaume hawakamilike. Kama tunakazia akili makosa yao kuliko kukazia akili sifa zao, tutakuwa tuko nafanya wengine wasitumainie tengenezo ya Mungu. w24.04 10 fu. 11-12

Siku ya Tano, 20 Mwezi wa 2

Atatenganisha watu mumoja na mwingine.—Mt. 25:32.

Wote wenye watakufa wakati wa taabu kubwa hawatakuwa na tumaini ya kufufuliwa? Biblia inaonyesha kama wapinzani wenye Yehova na majeshi yake wataharibu ku vita ya Armagedoni, hawatafufuliwa. (2 Te. 1:​6-10) Lakini, tuseme nini juu ya watu wengine, kwa mufano, wale wenye inawezekana watakufa kwa sababu ya magonjwa, uzee, aksida, ao wenye watauawa na wanadamu wenzao? (Muh. 9:11; Zek. 14:13) Wamoja wao wanaweza kuwa kati ya “wenye hawako wenye haki” wenye watafufuliwa mu dunia mupya? (Mdo. 24:15) Hatujue. Lakini tunajua mambo mbalimbali kuhusu matukio ya wakati wenye kuya. Kwa mufano, tunajua kama ku Armagedoni, watu watahukumiwa kulingana na namna walitendea ndugu za Kristo. (Mt. 25:40) Na wale wenye watahukumiwa kuwa kondoo, ni wale wenye waliunga mukono Wakristo watiwa-mafuta na Kristo.—Ufu. 12:17. w24.05 10-11 fu. 9-11

Siku ya Posho, 21 Mwezi wa 2

Yehova ni mwenye kuishi! Mwamba wangu asifiwe! Mungu wa wokovu wangu atukuzwe.—Zb. 18:46.

Biblia inasema kama tunaishi “nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia.” (2 Ti. 3:1) Zaidi ya magumu yenye watu wote wanapata mu hii dunia, watu wa Yehova wanapambana na upinzani na mateso. Ni nini inatusaidia tuendelee kumuabudu Yehova hata kama tunapata magumu? Jambo moya ya maana yenye inatusaidia ni kufikia kumujua Yehova kuwa “Mungu mwenye kuishi.” (Yer. 10:10; 2 Ti. 1:12) Yehova ni mutu wa kweli kabisa mwenye anatutegemeza wakati wa magumu na anatafuta nafasi za kutusaidia. (2 Ny. 16:9; Zb. 23:4) Kumuona kuwa Mungu mwenye kuishi kunaweza kutusaidia kupambana na magumu yetu. w24.06 20 fu. 1-2

Siku ya Yenga, 22 Mwezi wa 2

Njia ya wenye haki iko kama mwangaza wenye kungaa wa asubui wenye kungaa zaidi na zaidi mupaka muchana kamili.—Mez. 4:18.

Tunapaswa kuendelea kutumainia tengenezo ya Yehova. Wakati inaonekana kuwa ni lazima tubadilishe namna yetu ya kuelewa kweli fulani ya Biblia ao namna ya kupanga kazi yetu ya kuhubiri, wale wenye kuongoza wako tayari kufanya mabadiliko. Wanafanya vile juu wanapenda kumufurahisha Yehova, kuliko kufurahisha wanadamu. Pia wanajikaza sana ili maamuzi yao yote itegemee Neno ya Mungu, yenye watu wote wa Yehova wanapaswa kufuata. Mutume Paulo alitoa hii shauri: “Endelea kushika mufano wa maneno yenye faida.” (2 Ti. 1:13) “Mufano wa maneno yenye faida” ni mafundisho ya Kikristo yenye kuwa mu Biblia. (Yoh. 17:17) Ile mafundisho njo musingi wa mambo yote yenye tunaamini. Tengenezo ya Yehova imetufundisha kushikamana na ile maneno. Kama tunaendelea kufanya vile, tutabarikiwa. w24.07 11 fu. 12-13

Siku ya Kwanza, 23 Mwezi wa 2

Yehova . . . ni muvumilivu kuwaelekea ninyi kwa sababu hataki mutu yeyote aharibiwe lakini anataka wote wafikie kutubu.—2 Pe. 3:9.

Juu Mutume Petro mwenyewe alisamehewa, aliweza kufundisha bengine juu ya toba na musamaha. Wakati kidogo kisha sikukuu ya Pentekoste, Petro alitoa hotuba mbele ya Wayahudi wengi wenye hawakukuwa waamini. Aliwaambia kama waliua Masiya. Lakini aliwashauria hivi kwa upendo: “Kwa hiyo, mutubu na mugeuke ili zambi zenu zipate kufutwa, ili vipindi vya kutuliza vikuje kutoka kwa Yehova mwenyewe.” (Mdo. 3:​14, 15, 17, 19) Petro alionyesha kama kutubu kunafanya mutenda-zambi abadilike, aache mawazo na matendo ya mubaya, na afuate njia ya mupya, njia yenye inamufurahisha Mungu. Mutume Petro alionyesha pia kama Yehova angefuta zambi zao, ni kusema angefanya zipotee kabisa. Wakati tunafanya zambi, hata zambi nzito, inatia moyo kujua kama Yehova iko tayari kutusamehe! w24.08 12 fu. 14

Siku ya Pili, 24 Mwezi wa 2

Njia yenu ya maisha ikuwe bila upendo wa feza.—Ebr. 13:5.

Kama tuko na imani ya nguvu, hatutapenda sana vitu vya kimwili, juu tutakuwa hakika kama mwisho unakaribia. Watu “watatupa feza yao katika barabara” juu wataelewa kama “feza yao wala zahabu yao haitaweza kuwaokoa katika siku ya kasirani kali ya Yehova.” (Eze. 7:19) Kuliko kutafuta makuta mingi sana, tunapaswa kukamata maamuzi yenye itatusaidia kuwa na maisha mepesi. Ni kusema tunapaswa kukamata maamuzi yenye itatusaidia kujihangaikia na kuhangaikia batu ya mu familia yetu wakati tunaendelea kumutumikia Yehova. Ile itatusaidia tuepuke madeni yenye haiko ya lazima ao kujilundikia vitu mingi vya kimwili. Tena, itatusaidia tuepuke kupenda sana vitu vya kimwili vyenye tuko navyo. (Mt. 6:​19, 24) Vile mwisho uko unakaribia, tunapaswa kuonyesha wazi ikiwa ni Yehova njo tunatumainia ao ni vitu vyetu vya kimwili. w24.09 11 fu. 13-14

Siku ya Tatu, 25 Mwezi wa 2

Ule mwenye anawaza kama anasimama afanye angalisho asianguke.—1 Ko. 10:12.

Inaweza kuwa mwepesi kushinda kabisa uzaifu fulani. Lakini kuko uzaifu wenye pengine inaomba tuendelee kupiganisha kwa muda murefu zaidi. Fikiria mufano wa mutume Petro. Aliangukia mu mutego wa kuogopa wanadamu wakati alimukana Yesu mara tatu. (Mt. 26:​69-75) Ilionekana kama Petro alishinda uzaifu wake wa kuogopa wanadamu wakati alitoa ushahidi kwa uhodari mbele ya Sanhedrini. (Mdo. 5:​27-29) Lakini, miaka fulani kisha pale, juu ya “kuogopa wale wa kikundi cha wenye kutahiriwa,” kwa wakati fulani aliacha kula na Wakristo wa mataifa. (Gal. 2:​11, 12) Uzaifu wa kuogopa wanadamu wenye Petro alikuwa nao ulirudia. Pengine haukukuwa umeisha kabisa-kabisa. Tunaweza kujikuta mu hali sawa ya Petro. Hata vile, tunaweza kupiganisha uzaifu wenye haupendi kuisha kwa kufuata hii shauri ya Yesu: “Muendelee kukesha”. Hata wakati unajisikia kama uko na nguvu, uendelee kuepuka hali zenye zinaweza kukuingiza mu jaribu. Endelea kutumikisha mambo yenye ilikusaidia kupiganisha uzaifu wako.—2 Pe. 3:14. w24.07 18-19 fu.17-19

Siku ya Ine, 26 Mwezi wa 2

Alitoa zawadi katika wanadamu.—Efe. 4:8.

Hakuna mwanadamu mwenye amekuwa mukarimu sana sawa Yesu. Wakati alikuwa ku dunia alikuwa tayari kutumia nguvu yake ya kufanya miujiza juu ya kusaidia bengine. (Lu. 9:​12-17) Alitutolea zawadi kubwa zaidi wakati alitoa uzima wake kwa ajili yetu. (Yoh. 15:13) Tangu afufuliwe ameendelea kuwa mukarimu. Sawa vile aliahidi, alimuomba Yehova atumwangie roho yake takatifu juu itufundishe na kutufariji. (Yoh. 14:​16, 17, maelezo ya chini; 16:13) Na kupitia mikutano yetu, Yesu anaendelea kutupatia mambo yenye tuko nayo lazima juu ya kufanya wanafunzi mu dunia yote. (Mt. 28:​18-20) Mutume Paulo aliandika kama kisha Yesu kupanda mbinguni, “alitoa zawadi katika wanadamu.” (Efe. 4:​7, 8) Paulo alifasiria kama kisha Yesu kupanda mbinguni, alitoa ile zawadi ili isaidie kutaniko mu njia mbalimbali. (Efe. 1:​22, 23; 4:​11-13) . Kusema kweli bale banaume habakamilike na banafanyaka makosa. (Yak. 3:2) Lakini Bwana wetu, Yesu Kristo, anabatumia juu ya kutusaidia. Bale banaume ni zawadi yenye Yesu ametupatia. w24.10 18 fu. 1-2

Siku ya Tano, 27 Mwezi wa 2

Utambuzi utakuchunga.—Mez. 2:11.

Daudi alimuambia mwana wake Sulemani kama angeendelea kupata matokeo ya muzuri kama tu anaendelea kumutii Yehova Mungu. Jambo ya kuhuzunisha ni kama, ku mwisho-mwisho wa maisha yake, Sulemani alianza kuabudu miungu ingine. Yehova hakumukubali tena, na Sulemani alipoteza hekima ya kuongoza taifa mu njia ya muzuri na ya haki. (1 Fa. 11:​9, 10; 12:4) Tunajifunza nini? Kutii kunaleta matokeo ya muzuri. (Zb. 1:​1-3) Kusema kweli, Yehova hatuahidi kama atatupatia utajiri na utukufu sawa Sulemani. Lakini kama tunatii Mungu wetu, atatupatia hekima yenye itatusaidia kukamata maamuzi ya muzuri. (Mez. 2:​6, 7; Yak. 1:5) Kanuni zake zinaweza kutusaidia kukamata maamuzi ya muzuri mu mambo sawa vile kazi, masomo, mambo ya kujifurahisha, na makuta. Kutumikisha hekima yenye kutoka kwa Yehova kunaweza kutulinda juu tusipate matokeo ya mubaya yenye inaweza kutukosesha uzima wa milele. (Mez. 2:​10, 11) Tutapata marafiki wazuri na tutapata muongozo wenye utatusaidia tukuwe na furaha mu familia. w24.11 10 fu. 11-12

Siku ya Posho, 28 Mwezi wa 2

Muchunguze mambo yote; mushikamane na mambo ya muzuri.—1 Te. 5:21.

Muzazi iko na nafasi za mingi za kuzungumuza pamoya na watoto wao juu ya Biblia na juu ya Mungu. Unaweza kupata zile nafasi wakati munatembelea musée (fasi kwenye banachungiaka vitu vya zamani juu ya kuvionyesha batu). Unaweza kuonyesha mutoto wako habari fulani za zamani ao vitu fulani vya zamani vyenye vitamusaidia akuwe hakika kama mambo yenye Biblia inasema ni ya kweli. Mutoto wako anajua kama jina ya Mungu inapatikana ku jiwe yenye iko na miaka 3000 yenye inajulikana kuwa jiwe ya Moabu? Kopi ya ile jiwe inaonyeshwa mu maonyesho ya “Biblia na Jina la Mungu” yenye kuwa ku Makao Makubwa ya Mashahidi wa Yehova katika Warwick, New York. Jiwe ya Moabu inaonyesha kama Mufalme Mesha wa Moabu aliasi Israeli. Ile inapatana na mambo yenye Biblia inasema. (2 Fa. 3:​4, 5) Wakati mutoto wako anajionea na macho yake mwenyewe mambo yenye inaonyesha kama Biblia inasema kweli, imani yake itakuwa nguvu. w24.12 14 fu. 4; 15 fu. 6

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine