Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • es26 uku. 7-17
  • Mwezi wa 1

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mwezi wa 1
  • Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
  • Vichwa Vidogo
  • Siku ya Ine, 1 Mwezi wa 1
  • Siku ya Tano, 2 Mwezi wa 1
  • Siku ya Posho, 3 Mwezi wa 1
  • Siku ya Yenga, 4 Mwezi wa 1
  • Siku ya Kwanza, 5 Mwezi wa 1
  • Siku ya Pili, 6 Mwezi wa 1
  • Siku ya Tatu, 7 Mwezi wa 1
  • Siku ya Ine, 8 Mwezi wa 1
  • Siku ya Tano, 9 Mwezi wa 1
  • Siku ya Posho, 10 Mwezi wa 1
  • Siku ya Yenga, 11 Mwezi wa 1
  • Siku ya Kwanza, 12 Mwezi wa 1
  • Siku ya Pili, 13 Mwezi wa 1
  • Siku ya Tatu, 14 Mwezi wa 1
  • Siku ya Ine, 15 Mwezi wa 1
  • Siku ya Tano, 16 Mwezi wa 1
  • Siku ya Posho, 17 Mwezi wa 1
  • Siku ya Yenga, 18 Mwezi wa 1
  • Siku ya Kwanza, 19 Mwezi wa 1
  • Siku ya Pili, 20 Mwezi wa 1
  • Siku ya Tatu, 21 Mwezi wa 1
  • Siku ya Ine, 22 Mwezi wa 1
  • Siku ya Tano, 23 Mwezi wa 1
  • Siku ya Posho, 24 Mwezi wa 1
  • Siku ya Yenga, 25 Mwezi wa 1
  • Siku ya Kwanza, 26 Mwezi wa 1
  • Siku ya Pili, 27 Mwezi wa 1
  • Siku ya Tatu, 28 Mwezi wa 1
  • Siku ya Ine, 29 Mwezi wa 1
  • Siku ya Tano, 30 Mwezi wa 1
  • Siku ya Posho, 31 Mwezi wa 1
Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2026
es26 uku. 7-17

Mwezi wa 1

Siku ya Ine, 1 Mwezi wa 1

Mukuwe watu wazima katika uelewaji wenu.—1 Ko. 14:20.

Wazazi wanakuwaka na furaha sana wakati mutoto wao anazaliwa na afya ya muzuri. Hata kama wazazi wanapendaka mutoto wao mudogo, hawawezi kufurahia abakie mutoto maisha yote. Na wakiona mutoto wao hakomale, ile inaweza kuwaletea wasiwasi sana. Vilevile, Yehova anafurahi wakati tunaanza kutembea, ni kusema wakati tunakamata hatua ya kufuata Yesu. Lakini hapendi tubakie watoto kiroho. (1 Ko. 3:1) Anatuomba tukuwe “watu wazima” kiroho. Mu Biblia, neno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa “mutu muzima” inaweza pia kumaanisha “mukomavu,” “kamili,” ao “mwenye kuenea.” (1 Ko. 2:6) Tunakuwa Wakristo wakomavu, ao watu wazima kiroho, wakati tunaacha kuwa watoto kiroho na tunakuwa wanaume na wanamuke wenye kukomaa kiroho. Lakini, hata kisha kufikia kukomaa kiroho hatupaswe kuacha kufanya maendeleo.—1 Ti. 4:15. w24.04 2 fu. 1, 3

Siku ya Tano, 2 Mwezi wa 1

Hema yangu itakuwa pamoja nao, na mimi nitakuwa Mungu wao.—Eze. 37:27.

Kama mutu anakuuliza Yehova ni nani mu maisha yako, utajibu namna gani? Unaweza kujibu, ‘ni Baba yangu, Mungu wangu, na Rafiki yangu.’ Na kuko majina ingine mingi ya cheo yenye unaweza kumuita. Lakini, unamuona pia Yehova kuwa mutu mwenye anakualika kwake? Mufalme Daudi alionyesha kama uhusiano wenye Yehova iko nao pamoya na waabudu wake washikamanifu uko sawa uhusiano wenye kuwa kati ya mugeni na mutu mwenye alimualika. Daudi aliuliza hivi: “Ee Yehova, ni nani anaweza kuwa mugeni katika hema yako? Ni nani anaweza kukaa katika mulima wako mutakatifu?” (Zb. 15:1) Ile maneno yenye kuongozwa na roho ya Mungu inaonyesha kama tunaweza kuwa wageni wa Yehova, ni kusema marafiki wake. Mbele aanze kuumba, Yehova alikuwa peke yake. Lakini wakati fulani, aliumba Mwana wake muzaliwa wa kwanza. Alimualika mu hema yake ya mufano na ile ilimufurahisha sana. Biblia inasema kama Yehova “alipenda sana” Mwana wake. Mugeni wake wa kwanza, ni kusema Mwana wake, ‘alifurahi [pia] mbele yake wakati wote.’—Mez. 8:30. w24.06 2 fu. 1-3

Siku ya Posho, 3 Mwezi wa 1

Sadoki [alikuwa] kijana mwanaume mwenye nguvu na hodari.—1 Ny. 12:28.

Wazia hii hali: Kikundi ya wanaume zaidi ya 340000 wanakutana ili kumufanya Daudi kuwa mufalme juu ya Israeli yote. Kwa siku tatu, wale wanaume walibakia ku milima yenye kuwa karibu na Hebroni na wako wanazungumuza na kuimba nyimbo za kumusifu Yehova. (1 Ny. 12:39) Ingekuwa nguvu kutambua kijana mwanaume mwenye kuitwa Sadoki mu ile kundi kubwa ya watu. Lakini, Yehova alimuona na alipenda tujue kama alikuwa pale. (1 Ny. 12:​22, 26-28) Sadoki alikuwa kuhani mwenye alitumika sana na Kuhani Mukubwa Abiatari. Sadoki alikuwa pia muonaji mwenye aliweza kutambua mapenzi ya Mungu, na Mungu alimupatia ufahamu wa ajabu. (2 Sa. 15:27) Alikuwa mwanaume hodari. Mu hizi siku za mwisho, Shetani iko nashambulia watu wa Mungu zaidi na zaidi. (1 Pe. 5:8) Wakati tuko nangoya Yehova aharibu Shetani na ulimwengu wake muovu, tunapaswa kuwa hodari. (Zb. 31:24) Kwa kufanya vile, tunaweza kuiga uhodari wa Sadoki. w24.07 2 fu. 1-3

Siku ya Yenga, 4 Mwezi wa 1

Maisha ya Adamu ikakuwa miaka mia kenda makumi tatu (930), kisha akakufa.—Mwa. 5:5

Wakati Yehova aliumba mwanaume na mwanamuke wa kwanza, alipenda bakuwe na furaha. Alibapatia fasi ya muzuri ya kuishi, alibapatia ndoa, na alibapatia kazi ya muzuri sana. Balipaswa kujaza dunia wazao wao na kufanya dunia yote kuwa paradiso sawa bustani ya Edeni. Yehova alibapatia amri moya tu ya mwepesi. Na alibaonya kama bakivunja ile amri kwa kukosa kumutii kimakusudi, zambi yao itabaletea kifo. Tunajua vile mambo ilifikia kuwa. Kiumbe fulani wa roho, mwenye hakupenda Mungu na hakubapenda, alibashawishi bafanye zambi. Adamu na Eva balifanya mambo yenye Shetani, ule kiumbe wa roho alibaambia. Habakumutumainia Yehova, Baba yao mwenye upendo, na bakafanya zambi. Sawa vile tunajua, maneno ya Yehova ilitimia. Kuanzia ile siku, balijionea matokeo ya zambi yao: balianza kuzeeka na ku mwisho bakakufa.—Mwa. 1:​28, 29; 2:​8, 9, 16-18; 3:​1-6, 17-19, 24. w24.08 3 fu. 3

Siku ya Kwanza, 5 Mwezi wa 1

Mukuwe watendaji wa neno, na hapana wasikiaji tu.—Yak. 1:22.

Yehova na Mwana wake wanapenda tukuwe na furaha. Zaburi 119:2 inasema hivi: “Wenye furaha ni wale wenye wanashika vikumbusho vyake, wenye wanamutafuta kwa moyo wao wote.” Yesu alisema pia hivi: “Wenye furaha ni wale wenye wanasikia neno la Mungu na kulishika.” (Lu. 11:28) Siye waabudu wa Yehova tunakuwa na furaha wakati tunasoma Neno ya Mungu kwa ukawaida na kujikaza kutumikisha mambo yenye tunajifunza. (Yak. 1:​22-25) Na ile inamufurahisha Yehova. (Muh. 12:13) Wakati tunatumikisha mambo yenye tunasoma mu Neno ya Mungu yenye kuongozwa na roho yake, tunakuwa na furaha mu familia na tunakuwa na urafiki muzuri pamoya na waabudu wenzetu. Zaidi ya ile, tunaepuka magumu yenye watu wenye hawafuate amri za Yehova wanapata. Kwa kweli, tunakubaliana kabisa na mambo yenye Mufalme Daudi alisema. Kisha kutaya sheria, maagizo, na hukumu za Yehova mu wimbo wake, alimalizia kwa kusema hivi: “Katika kuzishika, kuko zawabu kubwa .”—Zb. 19:​7-11. w24.09 2 fu. 1-3

Siku ya Pili, 6 Mwezi wa 1

Anaponyesha wenye kuvunjika moyo; anafunga vidonda vyao.—Zb. 147:3.

Yehova anaona nini wakati anaangalia batumishi yake ku dunia? Anajua maumivu yetu na furaha yetu. (Zb. 37:18) Wakati anaona namna tuko nafanya yetu yote juu ya kuendelea kumutumikia hata kama tuko na maumivu mu moyo, anafurahi sana! Zaidi ya ile, iko tayari kutusaidia na kutufariji. Zaburi 147:3 inaonyesha kama Yehova ‘anafunga vidonda’ vya wenye kuvunjika moyo. Hii andiko inamuonyesha Yehova kuwa mutu mwenye anahangaikia kwa upendo batu benye kuwa na vidonda vya moyo. Tunapaswa kufanya nini juu tupate musaada wa Yehova? Fikiria hii mufano: Munganga mwenye uzoefu anaweza kutunza muzuri mutu mwenye kuumia na kumusaidia apone. Lakini juu ule mutu apone, anapaswa kufuata kwa uangalifu mambo yenye munganga anamuambia. Yehova anazungumuza kupitia Neno yake na bale benye biko na maumivu ya moyo na anabapatia mashauri yenye upendo. w24.10 6 fu. 1-2

Siku ya Tatu, 7 Mwezi wa 1

Wote wakafutwa juu ya dunia.—Mwa. 7:23.

Zamani, vichapo vyetu vilisema kama wale wenye Yehova alihukumu kuwa hawako wenye haki, hawana tumaini. Tulisema kama watu wa vile hawana tumaini yoyote ya ufufuo. Kuko habari mingi za Biblia zenye zinazungumuzia namna Yehova alihukumu watu wenye hawako wenye haki. Kwa mufano, watu wengi wenye walikufa wakati wa Garika, mataifa saba yenye Yehova aliamuru Waisraeli waharibu mu Inchi ya Ahadi, ao tena maaskari wa Ashuru 185000 wenye malaika wa Yehova aliharibu mu usiku moya. (Kum. 7:​1-3; Isa. 37:​36, 37) Mu ile mifano, je, Biblia inatupatia habari zote zenye tuko nazo lazima ili kusema kama Yehova aliharibu wale watu milele, bila tumaini ya ufufuo? Hapana. Hatujue namna Yehova alihukumu kila mumoja wao; na hatujue ikiwa wale wenye waliuawa walipata nafasi ya kujifunza juu ya Yehova na nafasi ya kutubu. w24.05 3 fu. 5-7

Siku ya Ine, 8 Mwezi wa 1

Endelea kushinda uovu kwa wema.—Ro. 12:21.

Mu mufano fulani Yesu alizungumuzia mujane mwenye aliendelea kuomba muamuzi amutendee kwa haki. Ni wazi kama ile mufano iligusa sana wanafunzi wa Yesu, juu ile wakati watu wa kawaida walikuwa natendewa bila haki. (Lu. 18:​1-5) Ile habari ni ya maana pia kwetu juu siye bote banatutendeaka bila haki wakati fulani. Leo, mu dunia muko ubaguzi, batu banaonewa na kutendewa mubaya. Kwa hiyo, hatushangale wakati banatutendea mubaya. (Muh. 5:8) Lakini, inahuzunisha sana wakati ni ndugu ao dada njo anatutendea mubaya. Na ile inafikaka. Ndugu na dada zetu hawako maadui wetu, hawapendi kututendea mubaya. Hawakamilike tu. Namna Yesu alitenda wakati bapinzani balimutendea bila haki inaweza kutufundisha mambo mingi. Kama tunaweza kuvumilia wakati bapinzani banatutendea bila haki, juu ya nini basi tusivumilie Wakristo wenzetu? w24.11 2 fu. 1-2

Siku ya Tano, 9 Mwezi wa 1

Tutanunua wapi mikate ili watu hawa wakule? —Yoh. 6:5.

Mukate njo chakula yenye batu mingi ba zamani balizoea kula. (Mwa. 14:18; Lu. 4:4) Ilikuwa nakuliwa sana, njo maana wakati fulani Biblia inatumia neno “mukate” juu ya kumaanisha chakula. (Mt. 6:11; Mdo. 20:7) Kati ya miujiza ya Yesu yenye kujulikana sana, kuko miujiza mbili yenye kuhusu mukate. (Mt. 16:​9, 10) Yohana sura ya 6 inazungumuzia muujiza moya kati ya ile miujiza mbili. Kisha mitume wa Yesu kumaliza kuhubiri, Yesu aliingia pamoya nao mu mashua, na wakavuka Bahari ya Galilaya juu wapumuzike. (Mk. 6:​7, 30-32; Lu. 9:10) Kisha wakafika fasi fulani ya kimya karibu na Betsaida. Bila kukawia, maelfu ya batu bakafika pale na kuwazunguka. Yesu hakufanya sawa vile hakubaona. Kwa upendo alikamata wakati wa kubafundisha juu ya Ufalme wa Mungu na akaponyesha bagonjwa. Vile saa ilikuwa napita, mitume walikuwa najiuliza ikiwa bale batu bote batapata wapi chakula. Pengine bamoya kati ya bale batu balikuwa na chakula kidogo, lakini bamingi bangekuwa na lazima ya kuenda mu vijiji juu ya kuuza chakula.—Mt. 14:15. w24.12 2 fu. 1-2

Siku ya Posho, 10 Mwezi wa 1

Zawadi yenye Mungu anatoa ni uzima wa milele kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.—Ro. 6:23.

Wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Eva, walikuwa wakamilifu na waliishi mu paradiso yenye kupendeza. (Mwa. 1:27; 2:​7-9) Walikuwa na tumaini ya kuishi maisha ya muzuri na yenye haina mwisho. Lakini mambo ilibadilika. Walipoteza paradiso, makao yao ya muzuri, na tumaini yao ya kuishi milele. Wangeachia watoto wao uriti gani? Biblia inasema hivi: “Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na ni vile kifo kilienea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.” (Ro. 5:12) Uriti wenye walituachia ni zambi yenye inaleta kifo. Zambi iko sawa deni kubwa, yenye hakuna hata moya kati yetu anaweza kulipa. (Zb. 49:8) Yesu alifananisha zambi na “madeni.” (Mt. 6:12; Lu. 11:4) Wakati tunafanya zambi, iko sawa vile tunakuwa na deni ya Yehova. Tungepaswa kuilipa. Kama ile deni ingebakia bila kulipwa, ni wakati tu tunakufa njo ingepotea.—Ro. 6:7. w25.02 2-3 fu. 2-3

Siku ya Yenga, 11 Mwezi wa 1

Nimewajulisha jina lako.—Yoh. 17:26.

Tunaona kuwa ni pendeleo kuambia wengine kweli kuhusu Ufalme wa Mungu! Haiko kila mutu njo iko na ile pendeleo. Kwa mufano, wakati Yesu alikuwa ku dunia, hakuruhusu roho wachafu watoe ushahidi juu yake. (Lu. 4:41) Leo, juu mutu akubaliwe kuhubiri na watu wa Mungu, anapaswa kutimiza mambo yenye inaombwa. Tunaonyesha kama tunaona pendeleo yetu kuwa ya maana wakati tunatoa ushahidi fasi yoyote na wakati wowote kadiri inawezekana. Kama Yesu, muradi wetu ni kupanda na kutilia maji mbegu za kweli ya Ufalme mu mioyo ya watu. (Mt. 13:​3, 23; 1 Ko. 3:6) Kwa kufuata mufano wa Yesu, tengenezo ya Yehova inajikaza sana ili kusaidia watu wengine wajue jina ya Mungu. Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mupya imesaidia watu kujua jina ya Mungu, juu mu ile tafsiri jina ya Mungu imerudishwa kila fasi kwenye inastahili kuwa. Kwa sasa ile tafsiri ya Biblia inapatikana ya muzima ao kwa sehemu mu luga zaidi ya 270. w24.04 9 fu. 8-9

Siku ya Kwanza, 12 Mwezi wa 1

Bwana yake anasimama na kumusifu.—Mez. 31:28.

Ndugu fulani wenye kuwa mu ndoa yenye furaha wanazoea kufanyia bibi zao kila siku jambo fulani yenye inaonyesha kama wanawapenda. (1 Yo. 3:18) Bwana anaweza kuonyesha bibi yake kama anamupenda kupitia mambo ya kidogo-kidogo sawa vile kumukamata mukono ao kumukumbatia. Anaweza kumutumia ka ujumbe ku telefone na kumuambia kwa mufano “niko nakuwaza” ao kumuuliza “mambo ni sawa?” Wakati fulani, anaweza kumuandikia bibi yake maneno fulani ku karatasi ili kumuonyesha kama anamupenda, ao anaweza kumupatia zawadi. Wakati bwana anafanya hii mambo, anamuonyesha bibi yake heshima na anafanya ndoa yao ikuwe nguvu zaidi. Bwana mwenye anaheshimia bibi yake anamutia moyo na anamuambia juu ya nini ni wa maana kwake. Bwana anaweza kufanya vile kwa kukumbuka kumushukuru bibi yake juu ya mambo yote yenye anafanya ili kumutegemeza. (Kol. 3: 15) Wakati bwana anapongeza bibi yake kwa moyo wote, anamufanya ajisikie muzuri. Bibi anajisikia kuwa salama, kuwa anapendwa, na anaheshimiwa. w25.01 11 fu. 15; 13 fu. 16

Siku ya Pili, 13 Mwezi wa 1

Mimi, Yehova, niko Mungu wako, . . . mwenye anakuongoza katika njia yenye unapaswa kutembea ndani yake.—Isa. 48:17.

Zaburi 15 inaisha na hii maneno: “Mutu yeyote mwenye kufanya mambo hayo hatatikiswa hata kidogo.” Mu ile andiko, muandikaji wa Zaburi anaonyesha sababu yenye inafanya Yehova atuombe kufanya mambo yenye kuwa mu Zaburi 15. Anapenda tukuwe na furaha. Kwa hiyo, kama tunafuata muongozo wake, tutapata baraka na ulinzi. Wale wenye Yehova anakubali kuwa wageni wake, wako na tumaini ya muzuri ya wakati wenye kuya. Wakristo waaminifu watiwa-mafuta wataenda katika “makao mengi” yenye Yesu amewatayarishia mbinguni. (Yoh. 14:2) Wale wenye kuwa na tumaini ya kuishi milele ku dunia wanangoya kwa hamu kutimizwa kwa ahadi zenye kuwa mu Ufunuo 21:3. Kwa kweli, siye wote tunaona kuwa ni pendeleo kubwa sana kualikwa na Yehova ili kuwa marafiki wake, ni kusema kuwa wageni milele mu hema yake!—Zb. 15:​1-5. w24.06 13 fu. 19-20

Siku ya Tatu, 14 Mwezi wa 1

Mumupatie Yehova utukufu wenye jina lake linastahili.—Zb. 96:8.

Utukufu maana yake nini? Mu Biblia, neno “utukufu” inaweza kumaanisha mambo yote ya ajabu yenye inaweza kushangaza mutu. Wakati kidogo kisha taifa ya Israeli kutoka mu utumwa Misri, Yehova alionyesha utukufu wake mu njia ya ajabu sana. Wazia namna mambo ilikuwa: Mamilioni ya Waisraeli wanakutana chini ya Mulima Sinai juu ya kusikiliza mambo yenye Mungu atawaambia. Wingu yenye giza inafunika mulima. Mara moya kunakuwa tetemeko ya inchi. Udongo unatetemeka kwenye wanasimama na kunatokea pia mwangaza wa radi, mungurumo, na sauti kubwa ya baragumu. (Kut. 19:​16-18; 24:17; Zb. 68:8) Wazia namna wale Waisraeli walishangala sana wakati Yehova alionyesha utukufu wake mu ile njia ya ajabu sana. Leo tunamupatia Yehova utukufu kwa kuambia wengine juu ya nguvu zake za ajabu na sifa zake zenye kupendeza. Pia tunamupatia Mungu utukufu wakati tunamusifu kwa sababu ya mambo yenye anatuwezesha kufanya.—Isa. 26:12. w25.01 2 fu. 2-3

Siku ya Ine, 15 Mwezi wa 1

Yehova amenituma.—Hes. 16:28.

Mu safari ya Waisraeli ya kuenda mu inchi ya ahadi, wakati fulani wanaume fulani wenye walikuwa na mamlaka walipinga Musa na daraka yenye Yehova alikuwa amemupatia. Walisema hivi: “Mukusanyiko wote [hapana tu Musa] ni mutakatifu, watu wote, na Yehova iko katikati yao.” (Hes. 16:​1-3) Ni kweli kama Yehova aliona “mukusanyiko wote” kuwa mutakatifu, lakini alikuwa amechagua Musa ili aongoze watu wake. Kwa kusema mubaya juu ya Musa, ni Yehova njo wale waasi walikuwa wanasema mubaya. Hawakufikiria mambo yenye Yehova alipenda, lakini walifikiria mambo yenye wao walipenda; walipenda kuwa na mamlaka zaidi na kujulikana. Mungu aliua wale wenye walianzisha ule uasi, na maelfu ya watu wenye waliwaunga mukono. (Hes. 16:​30-35, 41, 49) Leo tunaweza kuwa hakika kama Yehova hakubali wale wenye hawaheshimie mipango yenye ametia mu tengenezo yake. w24.07 11 fu. 11

Siku ya Tano, 16 Mwezi wa 1

Kwa maana maono haya ni ya wakati wenye uliwekwa.—Hab. 2:3.

Mu kipindi yenye tunaishi, watu mingi hawakubali mambo yenye Biblia inasema kuhusu mwisho wa ulimwengu huu na hata wanatuchekelea juu tunaamini ile mambo. (2 Pe. 3:​3, 4) Hata kama kuko mambo mingi yenye hatujue kuhusu taabu kubwa, tuko na lazima ya imani ya nguvu juu tuamini kama mwisho utafika kwa wakati wenye kufaa, na kama Yehova atatulinda. Tunapaswa kutumainia zaidi njia yenye Yehova anatumikisha leo juu ya kutuongoza, ni kusema “mutumwa muaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45) Inawezekana tutapata maagizo yenye itaokoa uzima wetu wakati taabu kubwa itaanza. Hii njo wakati wa kujifunza kutumainia zaidi muongozo wenye tunapewa kutoka kwa wenye kuongoza mu tengenezo ya Yehova. Tusiwaze kama ni wakati wa taabu kubwa njo tutaweza kutumainia muzuri muongozo wao kama tunashindwa kufanya vile leo. w24.09 11 fu. 11-12

Siku ya Posho, 17 Mwezi wa 1

Mujihakikishie ninyi wenyewe mapenzi ya Mungu yenye kuwa mema na yenye kukubalika na makamilifu.—Ro. 12:2.

Wazazi Wakristo wanajua kama mutoto hazaliwake na imani kwa Mungu. Kisha wakati, anaweza kuanza kujiuliza maulizo sawa vile: ‘Tunajua namna gani kama kuko Mungu? Naweza kuaminia mambo yenye Biblia inasema?’ Biblia yenyewe inatutia moyo tutumie ‘nguvu zetu za kufikiri’ na ‘tuchunguze mambo yote.’ (Ro. 12:1; 1 Te. 5:21) Sasa, namna gani unaweza kusaidia mutoto wako atie nguvu imani yake? Tia mutoto wako moyo ajihakikishie yeye mwenyewe kama mambo yenye anaamini ni ya kweli. Wakati mutoto wako anauliza maulizo, tumia ile nafasi juu ya kumuonyesha namna ya kutafuta majibu kwa kutumia vyombo vyetu vya kutafuta habari. Unaweza kutumia Index des publications de la Société Watch Tower na Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova. Mu sehemu “Biblia,” chini ya kichwa “Iliongozwa na Roho ya Mungu” anaweza kutafuta mambo yenye itamuhakikishia kama Biblia haiko tu kitabu ya muzuri yenye batu baliandika, lakini ni “neno la Mungu.”—1 Te. 2:13. w24.12 14-15 fu. 4-5

Siku ya Yenga, 18 Mwezi wa 1

Mambo hayo uyapatie wanaume waaminifu, wenye nao watastahili kabisa kufundisha wengine.—2 Ti. 2:2.

Wazee wanaweza kumuiga Yesu namna gani? Wanapaswa kuzoeza na kusaidia ndugu, hata wale wenye wangali vijana sana juu wastahili kutumikia madaraka zaidi mu kutaniko. Wazee hawatazamie kama ndugu wenye wanazoeza watakuwa wakamilifu. Wanapaswa kuwatolea mashauri kwa upendo juu wale ndugu vijana wakuwe na uzoefu na waone kama ni jambo ya lazima wakuwe wanyenyekevu, waaminifu, na tayari kutumikia bengine. (1 Ti. 3:1; 1 Pe. 5:5) Yesu alipatia banafunzi yake mugao wa kuhubiri, lakini pia mugao wa kufundisha. Pengine banafunzi baliona kama habastahili ile mugao. Lakini Yesu alikuwa hakika kama batafanya ile kazi na alibaambia vile. Ili kuonyesha kama alibatumainia kabisa, Yesu alibaambia hivi: “Kama vile Baba amenituma, mimi pia ninawatuma ninyi.”—Yoh. 20:21. w24.10 16 fu. 15; 17 fu. 17

Siku ya Kwanza, 19 Mwezi wa 1

Daudi . . . , mutu mwenye kufurahisha moyo wangu.—Mdo. 13:22.

Daudi alikuwa mufalme, mwanamuziki, mutunga-mashahiri, mupiganaji-vita, na nabii. Alipata magumu mingi. Kwa miaka fulani alikuwa mukimbizi; alikuwa nakimbia Mufalme Sauli, mwenye alikuwa namusikilia wivu. Kisha kuwa mufalme, Daudi alikimbia tena juu ya kuokoa uzima wake wakati mwana wake Absalomu alijaribu kumunyanganya ufalme. Hata kama alipata Daudi ile magumu yote na alifanya makosa fulani, aliendelea kuwa mushikamanifu kwa Mungu mupaka mwisho wa maisha yake. Na hata Yehova alimuita kuwa “mutu mwenye kufurahisha moyo [wake].” Bila shaka mashauri ya Daudi inaweza kutusaidia! (1 Fa. 15:5) Kwa mufano, fikiria mashauri yenye Daudi alipatia mwana wake Sulemani, mbele akuwe mufalme. Yehova alichagua kijana Sulemani juu aendeleshe ibada safi na ajenge hekalu yenye ingemuletea sifa. (1 Ny. 22:5) Sulemani angepambana na magumu. Daudi alimuambia nini? Daudi alimuambia mwana wake kama ikiwa anamutii Yehova, atapata matokeo ya muzuri mu maisha.—1 Fa. 2:​2, 3. w24.11 10 fu. 9-11

Siku ya Pili, 20 Mwezi wa 1

Tia njia yako katika mukono wa Yehova; umutegemee yeye, naye atatenda kwa ajili yako.—Zb. 37:5.

Bwana mwenye anapigaka bibi yake ao kumutukana anapaswa kufanya mambo fulani ili atengeneze tena urafiki wake pamoya na Yehova na pamoya na bibi yake. Kwanza, anapaswa kutambua kama iko na tatizo kubwa. Yehova anaonaka mambo yote, anaona mambo yote yenye anasema na kufanya. (Zb. 44:21; Muh. 12:14; Ebr. 4:13) Pili, anapaswa kuacha kutendea bibi yake mubaya na anapaswa kubadilika. (Mez. 28:13) Tatu, anapaswa kumuomba bibi yake na Yehova huruma na kutafuta musamaha wao. (Mdo. 3:19) Anapaswa pia kumuomba Yehova amupatie hamu ya kubadilika na amusaidie kuzuia mawazo, maneno, na matendo yake ya mubaya. (Zb. 51:​10-12; 2 Ko. 10:5; Flp. 2:13) Ine, anapaswa kutenda kulingana na sala zake kwa kujifunza namna ya kuchukia kila aina ya jeuri na maneno makali. (Zb. 97:10) Tano, anapaswa kutafuta bila kukawia musaada wa wazee wa kutaniko. (Yak. 5:​14-16) Sita, anapaswa kukamata mipango juu asiangukie tena mu zile tabia. w25.01 11 fu. 14

Siku ya Tatu, 21 Mwezi wa 1

Sababu gani unakawia? Simama, ubatizwe.—Mdo. 22:16.

Unamupenda Yehova Mungu, mwenye alikupatia mambo yote ya muzuri yenye uko nayo na mwenye alikupatia uzima? Unapenda kumuonyesha kama unamupenda? Namna ya muzuri sana ya kufanya vile ni kujitoa kwake na kubatizwa. Kama unafanya vile, utaingia mu familia ya Yehova. Na Yehova Baba yako na rafiki yako atakuongoza na atakuhangaikia juu sasa unakuwa wake. (Zb. 73:24; Isa. 43:​1, 2) Tena, kujitoa kwa Yehova na kubatizwa kunakupatia tumaini ya kuishi milele. (1 Pe. 3:21) Kuko kitu yenye inakuzuia kubatizwa? Kama ni vile, haiko weye peke. Kuko batu mingi sana benye balipaswa pia kubadilisha mwenendo na namna yabo ya kuwaza juu bastahili kubatizwa. Lakini sasa biko namutumikia Yehova kwa furaha na kwa bidii. w25.03 2 fu. 1-2

Siku ya Ine, 22 Mwezi wa 1

Wewe unatoa musamaha wa kweli.—Zb. 130:4.

Mu Biblia mara mingi zambi inafananishwa na muzigo muzito. Mufalme Daudi alisema hivi juu ya zambi zake: “Makosa yangu yamekuwa mengi sana juu ya kichwa changu; kama muzigo muzito, ni mengi sana siwezi kuyabeba.” (Zb. 38:4) Lakini Yehova anasamehe watenda-zambi wenye kutubu. (Zb. 25:18; 32:5) Neno ya Kiebrania yenye kutafsiriwa “kusamehe,” kwanza inamaanisha “kunyangula” ao “kubeba.” Tunaweza kuwazia kama Yehova iko sawa mwanaume mwenye nguvu mwenye ananyangula kwa njia ya mufano muzigo wa zambi kutoka ku mabega yetu na kuutia mbali sana na siye. Maneno ingine ya mufano inaonyesha namna Yehova anatia zambi zetu mbali sana na siye. Zaburi 103:12 inasema hivi: “Kama vile mahali jua linatokea kuko mbali sana na mahali jua linashukia, ni vile ametia zambi zetu mbali sana na sisi.” Mashariki ni mbali sana tena sana na mangaribi. Hakuna siku mashariki na mangaribi vitakutanaka. Mu maneno ingine Yehova anatia zambi zetu mbali sana na siye kuliko vile tunaweza kuwazia. Ile maneno yenye kuzungumuzia musamaha wa Yehova inagusa moyo sana! w25.02 9 fu. 5-6

Siku ya Tano, 23 Mwezi wa 1

Wakati unatoa zawadi za rehema, usipige tarumbeta mbele yako.—Mt. 6:2.

Kisha Yesu kurudia mbinguni, mutume Petro alifanya muujiza fulani: aliponyesha mwanaume mwenye alikuwa kilema tangu kuzaliwa. (Mdo. 1:​8, 9; 3:​2, 6-8) Bila shaka ile ilifanya batu mingi bamuzunguke. (Mdo. 3:11) Petro hakujisifu hata kama alikomalia mu desturi yenye batu balipenda kusifiwa na kujulikana. Kwa unyenyekevu alionyesha kama ni Yehova na Yesu njo banastahili sifa, alisema hivi: “Kupitia jina lake [Yesu], na kupitia imani yetu katika jina lake, mwanaume huyu mwenye munaona na munamujua, amefanywa akuwe na nguvu.” (Mdo. 3:​12-16) Tunaweza kufuata mufano wa Petro kwa kujikaza kukomalisha sifa ya unyenyekevu. Tunatumikia bengine juu tunamupenda Yehova na tunapenda batu, haiko juu tunapenda batuone. Kama tunafanya yetu yote juu ya kumutumikia Yehova na kutumikia bandugu yetu kwa furaha, ikuwe bengine banaona ao hapana, tunaonyesha kama tuko banyenyekevu.—Mt. 6:​1-4. w25.03 10-11 fu. 11-12

Siku ya Posho, 24 Mwezi wa 1

Kuwa muangalifu juu yako mwenyewe na kuhusu kufundisha kwako.—1 Ti. 4:16.

Tunaweza kuongeza bidii yetu mu kazi ya kuhubiri ikiwa tunakazia akili upendo wetu kwa Yehova na kwa jirani. (Mt. 22:​37-39) Fikiria namna Yehova anafurahi sana wakati anatuona tuko nafanya kazi ya kuhubiri, na namna watu watafurahi wakati wataanza kujifunza Biblia! Fikiria pia namna ujumbe wetu utasaidia watu wenye kuukubali waokolewe. (Yoh. 6:40) Kuko sababu zenye zinafanya usiweze kutoka ku nyumba? Kama ni vile, kazia akili mambo yenye unaweza kufanya juu ya kuonyesha kama unamupenda Yehova na unapenda jirani. Mu kipindi ya Korona, Samuel na Dania hawakuweza kutoka ku nyumba. Hata kama walikuwa na ile magumu, waliendelea kutoa ushahidi kwa ukawaida kupitia telefone, barua, na waliongoza mafunzo ya Biblia kupitia Zoom. Hali ya Samuel na Dania iliwazuia kufanya mambo fulani, lakini walifanya yote yenye waliweza na ile iliwaletea furaha. w24.04 18 fu. 15-16

Siku ya Yenga, 25 Mwezi wa 1

Ni nani anaweza kupata bibi mwenye uwezo? Samani yake inapita sana samani ya marijani.—Mez. 31:10.

Hata kama haiombe mutu afunge ndoa juu akuwe na furaha, Wakristo wengi wenye hawayafunga ndoa, ikuwe ni watu wazima ao vijana, wanatazamia kupata mutu mwenye wanaweza kufunga naye ndoa. Lakini mbele ya kuanzisha urafiki wa kimapenzi unapaswa kuwa na hali ya muzuri ya kiroho, unapaswa kujijua muzuri, na unapaswa kuwa na uwezo wa kutimiza mahitaji ya kimwili ya familia yako. (1 Ko. 7:36) Ni muzuri pia ujue ni bibi ao bwana wa namna gani njo uko natafuta. Kama haufanye vile unaweza kuacha mutu mwenye anaweza kuwa bibi oa bwana muzuri kwako, na kuanzisha urafiki wa kimapenzi na mutu mwenye hakufae. Kwa kweli, mutu mwenye tunapenda akuwe bibi ao bwana yetu anapaswa kuwa Mukristo mwenye kubatizwa. (1 Ko. 7:39) Lakini haiko kila Mukristo mwenye kubatizwa njo anaweza kuwa bibi ao bwana muzuri kwako. Kwa hiyo ujiulize hivi: ‘Niko na miradi gani mu maisha? Na naweza kupenda bibi ao bwana yangu akuwe na sifa gani? Niko mwenye usawaziko wakati ninafikiria namna bibi ao bwana yangu anapaswa kuwa?’ w24.05 20 fu. 1; 21 fu. 3

Siku ya Kwanza, 26 Mwezi wa 1

Mukuwe wenye fazili ninyi kwa ninyi.—Efe. 4:32.

Wakati muko nachumbiana namna gani munaweza kushugulikia matatizo na hali ya kukosa kuelewana? Kutoelewana wakati fulani inaonyesha kama hamustahili kuoana? Hatuwezi kusema vile kwa uhakika, juu wakati fulani bibi na bwana hawaelewanake. Ndoa yenye furaha inafanyizwa na watu wawili wenye wako na uwezo wa kutumika pamoya ili kumaliza matatizo yao ya kukosa kuelewana. Kwa hiyo, namna munashugulikia matatizo leo, inaweza kuonyesha ikiwa mutakuwa na ndoa yenye furaha. Mujiulize hivi: ‘Tunaweza kuzungumuzia mambo kwa utulivu na kwa heshima? Kila mumoja wetu anakuwaka tayari kukubali makosa yake na kujikaza kubadilika? Inakuwaka mwepesi kwetu kuacha kushikilia mawazo yetu, kuomba musamaha, na kusamehe?’ (Efe. 4:31) Lakini, kama mara kwa mara hamuelewane ao munazoea kubishana wakati muko mu urafiki wa kimapenzi, inawezekana mambo haitabadilika wakati mutaoana. Ikiwa unatambua kama ule ndugu ao ule dada hatakuwa bibi ao bwana muzuri kwako, kuvunja urafiki wa kimapenzi njo inaweza kuwa uamuzi muzuri zaidi kwenu. w24.05 29 fu. 12

Siku ya Pili, 27 Mwezi wa 1

Yehova, Mwamba wangu, asifiwe, yeye mwenye kuzoeza mikono yangu kwa ajili ya pigano.—Zb. 144:1.

Tunaweza kuwa mufano muzuri kwa wengine kama tunashikamana na mambo ya muzuri na kama tunakamata maamuzi yenye inategemea kabisa kanuni za Biblia. Kadiri tunaendelea kuwa na imani ya nguvu na kuendelea kuwa na ujuzi wa kweli, ni vile tunakuwa imara zaidi katika kweli. Hatuko watu wenye kusitasita, wenye kuyumbayumba, ao wenye kudanganywa haraka na mafundisho ya uongo na mawazo ya ulimwengu. (Efe. 4:14; Yak. 1:​6-8) Tuko pia tayari kusaidia wale wenye wanapambana na majaribu. (1 Te. 3:​2, 3) Wazee wanapaswa kuwa na kiasi, na akili ya muzuri, wenye utaratibu, na wenye usawaziko. Wazee wanasaidia wengine wasiyumbeyumbe kwa ‘kushikamana kabisa na neno la uaminifu.’ (Tit. 1:9; 1 Ti. 3:​1-3) Kupitia mufano wao na kazi yao ya uchungaji, wazee wanasaidia wahubiri wakuwe wanakusanyika na kuhubiri kwa ukawaida, na wakuwe wanafanya funzo yao ya kipekee. Wakati ndugu na dada wanapambana na mambo yenye inawaletea mahangaiko, wazee wanaweza kuwasaidia waendelee kukazia akili ahadi za Yehova. w24.06 31 fu. 16-18

Siku ya Tatu, 28 Mwezi wa 1

Mutubu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia.—Mt. 4:17.

Mu mahubiri yake, Yesu alifundisha wasikilizaji wake kama Baba yake ni mwenye kusamehe sana. Fikiria mufano wa mwana mupotevu. Kwa wakati fulani, ule mwana aliamua kufanya mambo ya mubaya mu maisha yake. Lakini “alirudiwa na fahamu” na akaamua kurudia kwao. Baba yake alitenda namna gani? Yesu alisema kama wakati ule mwana “alikuwa angali mbali, baba yake akamuona na . . . , akamukimbilia, akamukumbatia kwa upole wote na kumubusu.” Ule mwana alipenda kuomba baba yake amuruhusu kuwa mutumishi mu nyumba yake, lakini baba yake alimuita “huyu mwana wangu,” akamukaribisha tena mu familia. Baba yake alisema hivi: “Alikuwa amepotea na amepatikana.” (Lu. 15:​11-32) Mbele Yesu akuye ku dunia, ni wazi kama aliona namna Baba yake alionyesha huruma watenda-zambi wengi wenye walitubu. Kwa kweli, ile habari yenye Yesu alizungumuzia inagusa moyo sana na inaonyesha namna Baba yetu Yehova ni mwenye rehema! w24.08 11 fu. 11-12

Siku ya Ine, 29 Mwezi wa 1

Mukuwe na akili ya muzuri.—1 Pe. 4:7.

Mukristo mwenye iko na akili ya muzuri anafanya yake yote juu ya kukamata maamuzi ya muzuri yenye inapatana na namna ya kufikiri ya Yehova. Mukristo wa vile anajua kama uhusiano wake pamoya na Yehova njo wa maana zaidi mu maisha. Iko mwenye usawaziko na anakubali kama hajue mambo yote. Anaonyesha kama anamutegemea Mungu kwa kusali kwake kwa ukawaida na kwa unyenyekevu. Tunajua kama tunapaswa kuendelea kusali kwa Yehova hata kama tuko na uwezo mbalimbali. Kwa hiyo, tunasali kwa Yehova juu ya kumuomba muongozo na tunatumainia kama yeye njo anajua mambo yenye itatuletea faida; ni muzuri tufanye vile zaidi sana wakati tunatafuta kukamata maamuzi ya maana. Tuko wenye shukrani sana juu Yehova alituumba na uwezo wa kuonyesha sifa zake. (Mwa. 1:26) Ni kweli kama hatuwezi kumuiga Yehova kwa ukamili.—Isa. 55:9. w25.03 11 fu. 13; 13 fu. 17-18

Siku ya Tano, 30 Mwezi wa 1

[Upendo] unatumaini mambo yote, unavumilia mambo yote.—1 Ko. 13:7.

Tunapaswa kuepuka kushakia nia ya wengine. Kama mutu hatuonyeshe shukrani juu ya mambo yenye tulimufanyia, tunaweza kujiuliza: ‘Huyu mutu hana shukrani ao alisahau tu kuonyesha shukrani?’ Pengine kuko sababu zingine zenye zilifanya asionyeshe shukrani vile tuliwazia. Watu fulani ni wenye shukrani, lakini hawajue namna ya kuionyesha. Wanaweza kusikia haya kupokea musaada, zaidi sana kama zamani ni wao njo walikuwa nasaidia wengine. Hata ikuwe nini njo ilifanya wasionyeshe shukrani, upendo wa Kikristo utatusaidia tusiwawazie mubaya na tuendelee kuwa na furaha ya kutoa. (Efe. 4:2) Ukuwe na uvumilivu. Mufalme mwenye hekima Sulemani aliandika hivi kuhusu ukarimu: “Tupa mukate wako juu ya maji, kwa maana kisha siku nyingi utaupata tena.” (Muh. 11:1) Sawa vile hii maneno inaonyesha watu fulani wanaweza kutuonyesha shukrani kisha wakati murefu ni kusema, “kisha siku nyingi.” w24.09 30 fu. 18-19

Siku ya Posho, 31 Mwezi wa 1

Wale wenye wanazoea kufanya zambi, uwakaripie mbele ya watazamaji wote, ili ikuwe onyo kwa wengine. —1 Ti. 5:20.

Wakati fulani wanatutangazia mu kutaniko kama mutu fulani amekaripiwa. Mu hali ya vile, tunaendelea kupitisha wakati pamoya na ule mutu juu tunajua kama alitubu na ameacha tabia yake ya mubaya. Anaendelea kuwa Mukristo mwenzetu na iko na lazima ya kutiwa moyo na waamini wenzake. (Ebr. 10:​24, 25) Lakini, mambo iko tofauti wakati mutu anaondolewa mu kutaniko. ‘Tunaacha kushirikiana’ na ule mutu, ‘hata hatukule chakula pamoja na mutu wa namna hiyo.’ (1 Ko. 5:11) Je, ile inaonyesha kama tutafanya sawa vile hatumujue kabisa? Hapana. Kwa kweli, hatutapitisha wakati pamoya naye. Lakini Wakristo wanaweza kutumia zamiri yao yenye kuzoezwa na Biblia ili kuamua ikiwa wanaweza kualika ku mikutano mutu mwenye ameondolewa mu kutaniko, pengine mutu wa familia ao rafiki yao wa zamani. w24.08 30 fu. 13-14

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine