Jangwa Lageuzwa Kuwa Paradiso
Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi
1. Ili dunia iwe paradiso, ingekuwa lazima hali gani zimalizike?
HAKUNA sehemu yo yote ya dunia leo iliyo paradiso, iliyo huru na uchafu wote na hatari. Hewa na maji vinachafuliwa kwa kadiri ya kuogofya. Maeneo makubwa ya nchi yanageuzwa kuwa machukizo. Mashindano makali, uadui na chuki vinatisha furaha ya mwanadamu na afya. Ajali, ugonjwa na kifo vinashiriki katika kuleta taabu na huzuni ambayo imeipata jamaa ya kibinadamu kwa muda mrefu.
2. Biblia inatoa uhakika gani juu ya kuletwa kwa paradiso?
2 Je! kuna wakati mambo yatakapokuwa vingine? Ndiyo, Biblia Takatifu inatupa uhakika wenye kuburudisha moyo kwamba dunia hii itakuwa paradiso iliyo huru na ugonjwa wote, huzuni, maumivu na kifo. (Luka 23:43; Ufu. 21:3-5) Yeye aliyeahidi paradiso, Yehova Mungu, anao uwezo na hekima vile vile ya kuileta. Katika fadhili zake zenye upendo vile vile ametoa maandishi ya matendo yake yaliyopita kwa utimizo wa ahadi zake. Maandishi haya katika Biblia yanatupa uhakika kabisa kwamba hakuna litakalolizuia kusudi la Yehova lisitimie.
3. Je! kuletwa kwa paradiso ni jambo jipya kwa Yehova Mungu?
3 Kuletwa kwa paradiso si jambo jipya kwa Yehova Mungu. Yeye aliwaweka wanadamu wa kwanza, Adamu na Hawa, katika paradiso katika sehemu ya dunia iliyoitwa “Edeni.” Karne nyingi nyumaye alihakikisha kwamba nchi ya Yuda, iliyokuwa imekuwa jangwa lenye ukiwa nyuma ya ushindi wa Kibabeli, imegeuzwa kuwa ‘bustani ya Edeni,’ paradiso. Na katika karne hii Yehova Mungu amewabarijd watu wake waliojitoa na paradiso ya kiroho.
NCHI YA YUDA YAGEUZWA
4, 5. Kwa sababu gani kugeuzwa kwa nchi iliyoachwa ukiwa ya Yuda kuwa paradiso hakukuwa kazi nyepesi?
4 Karne zaidi ya 25 zimepita tangu nchi ya Yuda iwe ukiwa, bila ya mwanadamu wala mnyama wa kufugwa. Kugeuzwa kwa nchi hiyo kuwa paradiso hakukuwa jambo jepesi. Mataifa ya karibu hayakutaka kuona jambo hili likifanywa. Hata hivyo, Yehova Mungu alimwambia nabii wake Ezekieli:
5 “Itabirie milima ya Israeli, useme, Enyi milima ya Israeli, lisikieni neno la [Yehova]. Bwana [Yehova] asema hivi; Kwa sababu adui amesema juu yenu, Aha! na, Mahali pa juu pa zamani pamekuwa petu tupamiliki; basi tabiri useme, Bwana [Yehova] asema hivi; Kwa sababu, naam, kwa sababu wamewafanya ninyi kuwa ukiwa, na kuwameza pande zote, mpate kuwa milki kwa mabaki ya mataifa, nanyi mmeambwa kwa midomo yao waongeao, na kwa masingizio ya watu; kwa sababu hiyo, enyi milima ya Israeli, lisikieni neno la Bwana [Yehova]; Bwana [Yehova] aiambia hivi hiyo milima na vilima, mifereji ya maji na mabonde, mahali palipoharibika na kuwa ukiwa, na miji iliyoachwa na watu, ambayo imekuwa mateka, na kuzomewa na mabaki ya mataifa, walio karibu pande zote; basi Bwana [Yehova] asema hivi; Hakika kwa moto wa wivu wangu nimenena juu ya mabaki ya mataifa, na juu ya Edomu yote, waliojiandikia nchi yangu kuwa milki yao, kwa furaha ya mioyo yao yote, kwa jeuri ya [nafsi] zao, ili waitupe nje kuwa mawindo.”—Eze. 36:1-5.
6, 7. Ijapokuwa makusudi ya mataifa ya karibu, ni nini kingetukia bila shaka kwa nchi iliyoachwa ukiwa ya Yuda, na kwa sababu gani?
6 Mataifa adui yaliyo karibu ya nchi ya Yuda yalikuwa na kusudi lao wenyewe la kichoyo juu ya eneo lilioachwa utupu. Lakini Yehova alikuwa na kusudi jingine, nalo kusudi lake lingetimizwa. Mataifa yenye choyo yaliyo karibu yasingeipata nchi. Jitihada zao zenye pupa zingepatwa na mabaya. Hakuna Waedomu wo wote ama mataifa mengine ambao wangeruhusiwa kuifanya miji iliyoachwa ya Yuda kuwa mawindo wala kuitumia nchi kama mahali pa malisho. Mwishowe Yehova angehakikisha kwamba nchi, “nchi ya Israeli,” ingegeuzwa kutoka kwa hali ya ukiwa isitawi kama paradiso yenye Waisraeli waliorudishwa na wanyama wao wa kufugwa. Yehova alimwambia Ezekieli:
7 “Katika kutabiri habari za nchi ya Israeli, uiambie milima na vilima, mifereji ya maji na mabonde, Bwana [Yehova] asema hivi; Tazama, nimenena katika wivu wangu na hasira yangu, kwa sababu mmechukua aibu ya mataifa; basi Bwana [Yehova] asema hivi; Nimeinua mkono wangu, kusema, Hakika, mataifa walio karibu nanyi pande zote, wao watachukua aibu yao. Lakini ninyi, enyi milima ya Israeli, mtachipuza matawi yenu na kuwapa watu wangu Israeli matunda yenu; maana wa karibu kuja. Maana, tazama, mimi nasimama upande wenu, nami nitawaelekea, nanyi mtalimwa na kupandwa mbegu; nami nitaongeza watu juu yenu, nyumba yote ya Israeli, naam, yote pia, nayo miji itakaliwa na watu, na mahali palipoharibika patajengwa. Nami nitaongeza juu yenu mwanadamu na mnyama, nao watazidi na kuzaa; nami nitawakalisha watu ndani yenu, kwa kadiri ya hali yenu ya kwanza, nami nitawatendea mema kuliko mema ya mianzo yenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi [Yehova]. Naam, nitaleta watu watembee juu yenu, naam, watu wangu Israeli; nao watakumiliki, nawe utakuwa urithi wao, wala hutawafisha watoto wao tena tangu leo.”—Eze. 36:6-12.
8, 9. Kwa sababu gani katika wakati wa Ezekieli utimizo wa ahadi ya Yehova juu ya kurudishwa kwa nchi ya Yuda ulikuwa jambo la kutafutwa?
8 ‘Nyuma huko katika siku za nabii Ezekieli utimizo wa kiapo cha Yehova ulikuwa ungali jambo la kutafutwa na kuchunguzwa, makumi ya miaka ya uhamisho wa Kibabeli yakiwa yanabaki. Ni kama vile Yehova alivyotangaza kupitia kwa Ezekieli:
9 “Kwa ajili ya jambo hili nitaulizwa na nyumba ya Israeli, ili niwatendee; nami nitawaongeza kwa watu kama kundi la kondoo. Kama kundi lililo tayari kutolewa sadaka, kama kundi la Yerusalemu katika sikukuu zake zilizoamriwa; ndivyo itakavyojazwa watu, miji ile iliyokuwa maganjo; nao watajua ya kuwa mimi ndimi [Yehova].”—Eze. 36:37, 38.
10. Ahadi ya kurudishwa kwa nchi ya Yuda ilianza kutimizwa lini, na kwa hiyo mataifa mengine yalipaswa kukubali nini?
10 Huko kujazwa kwa miji ya Yuda iliyoachwa ukiwa na watu kulipaswa kutafutwe kutoka kwa Yehova na Wayahudi hao waliohamishwa waliotubu na waliotamani utimizo wa ahadi zenye rehema za Yehova. Wengi wa Wayahudi hao waliohamishwa waliokoka nao wakairudia nchi yao wakazione ahadi za Yehova zikitimizwa. Katika mwaka wa 537 B.C.E., mshindi wa Babeli, Koreshi, alitoa tangazo lililowaruhusu wahamishwa wa Kiyahudi wairudie nchi yao na kulijenga hekalu upya katika Yerusalemu. (Ezra 3:1, 2, 12) Waisraeli wakiwa wameirudia miji yao na kuanza kazi ya kujenga upya na kupanda, yalipaswa mataifa yakubali kwamba Yehova alikuwa ametimiza mageuzi ya ajabu. Ni kama vile Yehova alivyokuwa ametangaza kupitia kwa Ezekieli: “[Watu] watasema, Nchi hii, iliyokuwa ukiwa, imekuwa kama bustani ya [Edeni]; nayo miji iliyokuwa mahame, na ukiwa, na magofu, sasa ina maboma, inakaliwa na watu.” (Eze. 36:33-36) Waedomu, hata hivyo, wakawa watu waliohamishwa mwishowe na, nyuma ya uharibifu wa pili wa Yerusalemu katika mwaka wa 70 C.E., wakakoma kuwako kama taifa.
PARADISO YA KIROHO YAFANYIZWA
11. Mabaki watiwa mafuta wa mashahidl wa Yehova wa Kikristo waliingia lini katika hali ya utumwa, na kwa sababu gani?
11 Katika nyakati za kisasa mabaki yaliyotiwa mafuta ya Israeli wa kiroho, mashahidi wa Yehova wa Kikristo, wameona mambo yanayolingana na yale ya Waisraeli wa asili katika karne za saba na sita B.C.E. Mnamo Vita ya Kwanza ya Ulimwengu walipatwa na mateso ya kidini na uonezi nao wakaingia katika hali ya kutekwa nyara. Yehova Mungu aliruhusu hili litokee kwa sababu ya kosa kwa upande wa mabaki ya Israeli wa kiroho. Lakini halikuwa kusudi lake makao yao ya kiroho yakae ukiwa, Kristendomu akiichukua nafasi yote ya kidini mnamo kipindi cha nyuma ya vita.
12. Kristendomu alipatwaje na aibu katika mwaka wa 1919 C.E.?
12 Kama vile Edomu na mataifa mengine yaliyokuwa karibu ya Israeli wakati wa kale, Kristendomu aliaibika sana katika mwaka wa 1919 C.E. Hii ni kwa kuwa mambo ya aibu aliyokuwa ametabiri na kutumainia yawapate mabaki yaliyoteswa ya Waisraeli wa kiroho yalikosa kutukia. Katika mwaka huo makao haya ya kiroho yalianza kufufuka yakiwa na Waisraeli wa kiroho.
13. Tofautisha maendeleo kati ya mashahidi wa Yehova wa Kikristo na linalotukia katika Kristendomu.
13 Ijapokuwa ushirika wa makanisa na orodha ya wanachuo wa dini vimepungua sana katika miaka ya karibuni, mashahidi wa Yehova wa Kikristo tangu mwaka wa 1919 na kuendelea wamefurahia maongezeko ya ajabu hata leo. “Milima” ya makao yao ya kiroho imekuwa hai ikiwa na waabudu wengi waliojitoa wa Yehova Mungu. Ulipofika mwaka wa 1935 “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Mchungaji Mwema walianza kushirikiana na mabaki yaliyotiwa mafuta ya Waisraeli wa kiroho na kwa njia hiyo wakawa wenye kutenda juu ya “milima ya Israeli” ya mfano. Hata mateso ya ulimwenguni pote mnamo Vita ya Pili ya Ulimwengu hayakuiondolea “milima ya Israeli” ya mfano idadi yake wala kuipunguza. Ingawa huko nyuma katika mwaka wa 1928 ni watu 44,080 tu waliokuwa wakizitangaza “habari njema” za ufalme wa Mungu, katika mwaka wa 1972 hesabu ya watangazaji hao ilifikia kilele cha watu 1,658,990 katika makundi 28,407 katika nchi 208.
14. Katika nyakati za kisasa, miji ya Israeli wa kale na maboma yake inaweza kulinganishwa na nini?
14 Tangu mwaka wa 1919 C.E. na kuendelea makundi ya mabaki yaliyorudishwa ya Waisraeli wa kiroho yalikuwa kama miji ya Israeli wa kale. Yakawa ‘na maboma’ zaidi kwa usimamizi bora juu yao wa utendaji katika kuutimiza unabii wa Yesu kuzihubiri habari njema za ufalme wa Mungu uliosimamishwa. (Mt. 24:14) Yakawa yenye maboma imara zaidi katika mwaka wa 1938 wakati ambapo utawala wa kitheokrasi uliowekwa katikati, pahali pa utawala wa makundi ya mahali pamoja, wa usimamizi ulitumiwa kwa makundi yote duniani kote.
15. Ni ‘kujazana kwa watu’ gani kunakotokea kati ya mashahidi wa Yehova wa Kikristo?
15 Kwa kweli Yehova Mungu ameyajaza makao ya kiroho ya mashahidi wake wa Kikristo na “watu kama kundi la kondoo.” (Eze. 36:11, 37, 38) Kama vile kabila kumi na mbili za Israeli zilivyokuwa zinamiminikia Yerusalemu na hekalu lake wakati wa zile “sikukuu” tatu (Kupitwa, Pentekoste na Sikukuu ya Vibanda), ndivyo mashahidi wa Yehova wa Kikristo walivyofurahia kumiminika pamoja, si kwenye Majumba ya Ufalme ya mahali pao tu, bali, katika njia ya kustaajabisha, kwenye makusanyiko yao ya kawaida ya mzunguko, wilaya, ya kitaifa na ya mataifa yote.
16, 17. Mikazo ya leo haikuwafanyia nini Waisraeli wa kiroho katika makao yao ya kiroho?
16 Mikazo katika kizazi hiki cha machafuko ya utawala na jeuri haikuwafanya Waisraeli wa kiroho waliorudishwa watoweke katika makao yao mapya walimokaa, kana kwamba, wamemezwa na adui zenye kuleta vita ama na njaa katika nchi yao. Maono yao yamekuwa kama yale yanayosimuliwa katika Ezekieli 36:13-15, ambapo Yehova anaendelea kusema na nchi ya Israeli:
17 “Bwana [Yehova] asema hivi; Kwa kuwa watu hukuambia, wewe nchi u mwenye kula watu, nawe umekuwa mwenye kufisha watu wa taifa lako; basi hutakula watu tena, wala hutafisha watu wa taifa lako tena, asema Bwana [Yehova]; wala sitakusikizisha tena aibu yao wasioamini, wala hutachukua matukano ya watu tena; wala hutalikwaza taifa lako tena, asema Bwana [Yehova].”
18, 19. (a) Ni kwa njia gani na lini nchi ya Kanaani ilikuwa imewameza wakaaji wake? (b) Lililotukia kwa Israeli wa kale katika mwaka wa 537 B.C.E. na nyuma ya hapo linalinganaje na hali ya mabaki waliotiwa mafuta tangu mwaka wa 1919 C.E. na kuendelea?
18 Nchi ya Kanaani ilikuwa na sifa mbaya juu ya uharibifu wa watu wake kana kwamba wakimezwa na nchi hiyo. (Hes. 13:32) Yehova alipowaleta Waisraeli kwenye nchi ya Kanaani katika mwaka wa 1473 B.C.E. nao wakaangamiza mataifa saba, ilikuwa kana kwamba nchi ndiyo iliyowala, ikawameza wakaaji hao.
19 Katika mwaka wa 607 B.C.E. mfalme wa Babeli aliishinda nchi ya Yuda naye akahamisha wengi wa Wayahudi wenye kuokoka, nayo nchi ikaachwa ukiwa bila ya mwanadamu wala mnyama wa kufugwa. Ilionekana tena kana kwamba nchi ilikuwa imewameza wakaaji wake na ikaliondolea taifa la Ufalme wa Yuda watoto wake. Mapema, katika mwaka wa 740 B.C.E., ilikuwa imeliondolea taifa la Ufalme wa Israeli watoto wake. Lakini kwa baraka ya pekee na ulinzi wa Yehova nchi iliyoachwa ukiwa wakati fulani isingepatwa na jambo kama hili tena kwa habari ya mabaki ya Waisraeli waaminifu yaliyokuwa yamerudishwa kutoka uhamishoni katika Babeli katika mwaka wa 537 B.C.E. na kuendelea. Ndivyo ambavyo imekuwa na kwa makao ya kiroho yalikorudishwa mabaki katika mwaka uliofuata vita wa 1919 C.E. Wangali wako, wakiwa hai, wenye mazao, wenye kuongezeka. Paradiso ya kiroho inayofurahiwa na watu wa Mungu itaendelea kuwapo.
JINA LA MUNGU LATIWA NDANI
20, 21. Kwa sababu gani Yehova aliwarudisha mabaki wa mfano katika mwaka wa 537 B.C.E. na mabaki waliofananishwa katika mwaka wa 1919 C.E.?
20 Kwa sababu gani Yehova Mungu aliyaleta mambo haya makubwa? Haikuwa kwa sababu ya ustahili kwa upande wa mabaki ya mfano katika mwaka wa 537 B.C.E. na kuendelea wala kwa upande wa mabaki yaliyofananishwa katika mwaka wa 1919 C.E. na kuendelea. Jina takatifu la Mungu lilitiwa ndani. Twasoma:
21 “Tena, neno la [Yehova] likanijia, kusema, Mwanadamu, nyumba ya Israeli walipokaa katika nchi yao wenyewe, waliitia uchafu kwa njia yao na kwa matendo yao. Njia yao mbele zangu ilikuwa kama uchafu wa mwanamke wakati wa kutengwa kwake. Kwa hiyo nalimwaga hasira yangu juu yao, kwa ajili ya damu waliyoimwaga juu ya nchi, na kwa sababu wameitia uchafu kwa vinyago vyao. Nikawatawanya katika mataifa, wakatapanyika katika nchi nyingi; kwa kidiri ya njia yao, na kwa kadiri ya matendo yao, naliwahukumu. Nao walipoyafikilia mataifa yale waliyoyaendea, walilitia unajisi jina langu takatifu; kwa kuwa watu waliwanena, wakisema, Watu hawa ni watu wa [Yehova], nao wametoka katika nchi yake. Lakini naliwahurumia kwa ajili ya jina langu takatifu, ambalo nyumba ya Israeli walikuwa wamelitia unajisi katika mataifa waliyoyaendea.”—Eze. 36:16-21.
22. Kwa sababu gani kuhamishwa kwa Israeli wa kale katika Babeli na utumwa wa mabaki waliotiwa mafuta katika Babeli Mkuu kulileta suto kwa jina la Mungu?
22 Kwa kuwa Waisraeli walikuwa wameondoka katika nchi ya Yehova kama wahamishwa, ilionekana kwamba Yehova, waliyejidai kuwa Mungu wao, hakuweza kuwalinda na adui zao. Hii ilileta suto juu ya jina lake takatifu. Iliyafanya Mataifa yasiyo ya Kiyahudi yalitaje jina lake kwa njia mbaya. Vivyo hivyo, mabaki yaliyotiwa mafuta ya Waisraeli wa kiroho yalipoletwa katika utumwa wa Babeli Mkuu na hawara zake za kisiasa na za kijeshi mnamo Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, hii ilifanya ionekane kana kwamba wao kama washiriki wa Ushirika wa Wanafunzi wa Biblia wa Mataifa Yote hawakuwa Wakristo wa kweli. Ilionekana kana kwamba Mungu wa kweli hakuwa upande wao na hakuwa akiwalinda. Hii ilililetea suto jina la Mungu ambaye walikuwa wamejiweka wakf kwake. Kwa hiyo, ilikuwa lazima Yehova ajiheshimu mwenyewe kwa kuwa na huruma juu ya jina lake mwenyewe. Hilo lilikuwa jina takatifu nalo halikustahili kunajisiwa na walimwengu. Kwa maana alikuwa na mabaki yaliyojitoa ambao walikamatana na jina lake, basi lo lote alilolifanya kwa ajili ya huruma kwa jina lake lingepaswa liwe lenye huruma kwa mabaki hayo.
23. Yehova amelitakasaje jina lake kati ya mataifa?
23 Kile ambacho Yehova Mungu amefanya katika kuwarudisha watu wake katika nyakati za kisasa kimeyatimiza maneno ya unabii wa Ezekieli. (Eze. 36:22-24) Yehova amelitakasa jina lake kweli kweli kati ya mataifa kwa kutokeza watu walio wakf wanaoliona jina lake kama takatifu. (Eze. 36:38) Wao wanashughulikia kuliletea jina hilo utukufu na si kulisuta kwa njia yo yote kwa sababu ya mwenendo mbaya kwa upande wao. Wao wanachagua kumtii Mungu kama Mtawala kuliko wanadamu wakati sheria ya Mungu inapopingana na sheria zilizotengenezwa na wanadamu wasiomjali Mungu.—Matendo 5:29.
24. Kusafisha kwa Yehova kwa mabaki waliotiwa mafuta na kuwapa kwake “moyo wa nyama” na “roho mpya” kumemaanisha nini kwao?
24 Yehova ameyasafisha mabaki yake yaliyorudishwa uchafu wa kidini kwa njia zake zenye kusafisha, kama kuwamiminia maji safi. Wakiwa safi bila ya “vinyago,” wao wanakataa kuwaabudu wakuu wa kisiasa, wa kijeshi ama wa kidini ama kufanya ishara na mambo ya ibada ya sanamu, michoro ama mifano. Yehova amewaondolea ugumu wo wote wa moyo naye akawapa “moyo wa nyama,” moyo unaosukumwa na upendo na upendano kufanya mapenzi yake. “Roho mpya” ambayo Yehova ameitia ndani yao ni roho takatifu yake. Hii imefanya watokeze tunda la roho—“upendo, furaha, amani, uvumilivu, fadhili, wema, imani, upole, kujiweza.”—Eze. 36:25-28; Gal. 5:22, 23, NW.
25, 26. Ni nini kimeondoa maoni mabaya waliyoyapata mataifa juu ya Yehova kwa sababu ya kuwaadhibu watu wake?
25 Kusudi aondoe maoni yo yote mabaya ambayo mataifa yalipata juu yake kwa sababu ya kuwaadhibu watu wake, Yehova amewabariki sana tangu mwaka wa 1919. Imekuwa kama vile Yeye alivyoahidi kupitia kwa Ezekieli:
26 “Nami nitawaokoeni na uchafu wenu wote; nitaiita ngano, na kuiongeza, wala sitaweka njaa juu yenu tena. Nami nitazidisha matunda ya miti, na mazao ya mashamba, msipate tena kutukanwa na mataifa kwa sababu ya njaa. Ndipo mtazikumbuka njia zenu mbaya, na matendo yenu yasiyokuwa mema, nanyi mtajichukia nafsi zenu kwa macho yenu, kwa sababu ya maovu yenu na machukizo yenu. Ijulikane kwenu ya kuwa silitendi neno hili kwa ajili yenu, asema Bwana [Yehova]; tahayarikeni, na kufadhaika, kwa sababu ya njia zenu, Enyi nyumba ya Israeli.”—Eze. 36:29-32.
27. Washiriki wa mabaki waliotiwa mafuta wanauonaje wakati wao uliopita kama watumwa wa Babeli Mkuu, na hii ina matokeo gani mazuri kwao?
27 Kwa sababu ya wema huo wa kimungu kwao, washiriki wa mabaki yaliyotiwa mafuta wanajisikia kujichukia kabisa wanapotazama nyuma kwa ambavyo walivyokuwa wakati uliopita. Inawafanya watahayarike, inawafanya wajione wenye haya, wanapofikiri tu juu yake. Nia hii inawaondolea maelekeo yo yote ya kujitia tena katika mambo machafu ya kiroho na ya ufisadi, kwa makusudi. Kwa sababu ya matokeo ambayo fadhili zisizostahili za Yehova zimewaletea katika makao yao yaliyorudishwa, yeye anawaokoa na uchafu wao wote. Wanafahamu sana ya kwamba haikuwa kwa ajili ya wema wo wote wao wa siku zilizopita, si kwa ajili yao, kwamba, kwa usemi wa mfano, yeye akaiita ngano yenye kuuendeleza uzima ichipuke kutoka udongoni na kuzaa kwa wingi sana hivyo, ili kwamba mataifa ya kilimwengu yasiwasute kwa sababu ya kuwa na njaa ya chakula cha kiroho. Wanashukuru kwamba Mungu ameacha ijulikane kwao kwamba amewafanyia haya yote kwa ajili ya jina lake takatifu. Kwa hiyo kwa unyenyekevu wote wanalitakasa jina lake.
28. Kwa sababu gani twaweza kuwa na hakika kwamba dunia hii itakuwa paradiso?
28 Haya yote yanaonyesha kwamba ahadi za Yehova zinazoshirikishwa na jina lake takatifu zitatimizwa. Kwa kuwa ni kusudi lake kuigeuza dunia hii iwe paradiso, twaweza kuhakikisha kwamba hili litatukia. “Habari njema” kwa leo ni kwamba unabii wa Biblia unaelekeza kwenye kizazi hiki kama kile kitakachouona mwisho wa mwanadamu kuiharibu dunia. Kwa hiyo sasa ndio wakati wa watu wenye mioyo minyofu kusimama upande wa ibada ya kweli katika ushirika na mashahidi wa Yehova wa Kikristo, ambao sasa wanazifurahia baraka za paradiso ya kiroho.—Kutoka Kitabu “The Nations Shall Know that I Arn Jehovah”—How?