Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 6/1 kur. 250-257
  • Kukusanywa kwa Mataifa Yote Kwenye Hekalu Moja kwa Ibada

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kukusanywa kwa Mataifa Yote Kwenye Hekalu Moja kwa Ibada
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUNDI LA MAKUHANI WADOGO WA KIROHO
  • NYUA ZA HEKALU ZASONGAMANA NA WAABUDU
  • Hekalu la Kweli Moja Mahali pa Kuabudu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Hekalu Kubwa la Kiroho la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Hekalu
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 6/1 kur. 250-257

Kukusanywa kwa Mataifa Yote Kwenye Hekalu Moja kwa Ibada

1. Yehova alimfanya Yesu awe kuhani wa kiroho namna gani, na ni mahali gani patakatifu palipotokea wakati huo?

SASA mahali patakatifu pakubwa pa kiroho pa hema ya Yehova Mungu palitokea. Namna gani? Kwa sababu sasa “Patakatifu” pa hekalu la kiroho la Mungu palipofananishwa palitokea. Hii ilikuwa kwa sababu Mungu alimimina roho yake takatifu juu ya Yesu akamfanya Yesu kama kuhani wa kiroho. Mungu alimzaa Yesu kwa roho yake ili amfanye Mwana wa Mungu wa kiroho, mwenye kuvikwa heshima ya ukuhani mkuu zaidi kuliko ule wa kuhani mkuu wa kidunia wa Kiyahudi wa jamaa ya Haruni.

2. Katika njia hiyo Yesu alikuja kuwa katika hali gani, na aliweza kuingia katika sehemu gani ya hekalu la kiroho la Yehova, afanye nini humo?

2 Kwa hiyo Paulo anaandika hivi: “Hapana mtu ajitwaliaye mwenyewe heshima hii, ila yeye aitwaye na Mungu, kama vile Haruni. Vivyo hivyo Kristo naye hakujitukuza nafsi yake kufanywa kuhani mkuu, lakini yeye aliyemwambia, Ndiwe mwanangu, mimi leo nimekuzaa kama asemavyo mahali pengine, Ndiwe kuhani milele kwa mfano wa Melkizedeki.” (Ebr. 5:4-6) Ndivyo Yesu alivyokuja kuwa katika hali ya kuzaliwa na roho, ingawa bado alikuwa katika mwili. Katika hali hii aliweza kupaingia “Patakatifu” pa mfano pa hekalu la kiroho la Yehova. Katika “Patakatifu” hapo aliweza kutoa uvumba wa sala, sifa na utumishi kwa Mungu kama uvumba.

3. (a) Vile vile ni chumba gani kingine cha hekalu la kiroho la Yehova kilitokea, na kikiwa na sehemu gani ndani yake? (b) Ndivyo hekalu la kiroho la Yehova lilivyoanza kutenda kazi tangu wakati gani na kuendelea?

3 Sasa, vile vile, Patakatifu Zaidi pa hekalu la kiroho la Mungu palitokea, yaani, eneo la mbingu anakokaa Yehova Mungu mwenyewe katika kiti cha enzi juu ya makerubi wa kimbinguni, kama juu ya kiti cha rehema au “funiko la kupatanisha.” Katika eneo hili la kimbinguni ambalo sasa limechukua mfano wa chumba cha Patakatifu Zaidi au chumba cha ndani ndani, Yehova anaketi katika kiti cha enzi juu ya funiko la kupatanisha la sanduku la agano jipya, akiwa tayari na mwenye nia ya kupatanishwa, kutulizwa, kulainishwa kwa toleo la dhambi, dhabihu kamilifu ya kibinadamu ya Kuhani Mkuu wake Yesu Kristo katika ukomo wa Siku ya Upatanisho kubwa iliyofananishwa. (Law. 16:1-34) Ndivyo sasa hekalu kuu la kiroho la mfano la Yehova Mungu lilivyokuwa limetokea, likiwa na Patakatifu Zaidi na Patakatifu pa mfano na ua ukiwa na madhabahu yake ya dhabihu. Tangu ubatizo wa Yesu katika Mto Yordani katika mwaka wa 29 C.E. hekalu la kweli la Yehova lilikuwa likitenda kazi, likiwa na baraka zitakazokuwa kwa wanadamu wote.

4. (a) Ni wakati gani Yehova alipompitisha Yesu Kristo katika “pazia” kuingia katika Patakatifu Zaidi pa kweli, na namna gani? (b) Siku ya Upatanisho iliyofananishwa ilimalizika wakati gani, na namna gani?

4 Sasa, jambo peke yake lililomtenga Yesu Kristo kama Kuhani Mkuu na Patakatifu Zaidi pa Yehova lilikuwa lile “pazia” la mfano, kile kizuizi cha mwili. “Nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu.” (1 Kor. 15:50) Kwa sababu hii Yesu Kristo alimaliza dhabihu yake kamilifu ya kibinadamu katika “madhabahu” ya Mungu kwa kufa kama kafara asiye na hatia katika Siku ya Kupitwa, Nisani 14, ya mwaka wa 33 C.E. Lakini siku ya tatu ya kufa kwa Yesu, yaani, Nisani 16, Mungu Mwenye Nguvu Zote alimpitisha Kuhani Mkuu wake Yesu Kristo katika “pazia” hilo la katikati, kwa kumfufua kutoka kwa wafu, si kama Kuhani Mkuu mwenye mwili na damu, bali kama Kuhani Mkuu katika roho, mwenye kushiriki “tabia ya Uungu” na kuvikwa kutokufa. (1 Pet. 3:18; 1 Kor. 15:42-54; 2 Pet. 1:4) Lile “pazia” la hekaluni, linalofananisha kizuizi cha kimwili, sasa lilipitwa na Yesu Kristo aliyefufuka, na hivyo katika siku ya 40 tangu kufufuka kwake aliweza kupaa kwenye mbingu yenyewe na kuonekana mbele za Mungu akiwa na bei bora ya damu yake yenye kupatanisha dhambi, kuitoa kwenye kiti cha enzi cha Mungu cha upatanisho kwa ajili ya wanadamu wote. Kwa toleo hilo ile Siku ya Upatanisho kubwa iliyofananishwa ikamalizika.

KUNDI LA MAKUHANI WADOGO WA KIROHO

5, 6. (a) Yesu Kristo alianza kujenga kundi lake juu yake mwenyewe kama Mwamba wakati gani? (b) Washiriki wa kundi waligeukaje kuwa makuhani wadogo wa kiroho, na 1 Petro 2:5, 9 anasemaje juu ya hili?

5 Kwa msaada wa yote yaliyotangulia, hakuna jambo ambalo lingeweza kuwa wazi zaidi kuliko kwamba hema iliyojengwa na Musa na mahekalu yaliyojengwa na Sulemani, Zerubabeli na Herode katika Yerusalemu hayakufananisha kundi la wanafunzi wa Kristo. Kundi hilo la Kikristo halikutokea mpaka siku ya 50 wakati Yesu alipokwisha kufufuka na alipokuwa amekwisha kupaa mbinguni na kuonekana katika “mbingu yenyewe” mbele za Mungu kwa ajili yao. Akisema kwa habari yake mwenyewe kama Mwamba wa mfano, Yesu alisema hivi kwa mitume wake kumi na wawili: “Juu ya mwamba huu nitajenga kundi langu, na milango ya Haʹdes haitalishinda.” (Mt. 16:18, NW) Yeye alianza kujenga kundi hili la kiroho katika sikukuu ya Pentekoste siku kumi tangu kupaa kwake mbinguni katika mwaka wa 33 C.E. Yeye aliipokea roho takatifu kutoka kwa Mungu na akaimiminia juu ya wanafunzi wake waliokuwa wakingojea duniani katika Yerusalemu. Katika njia hii wakazaliwa kwa roho na hii ikatokeza kugeuka kwao kuwa wana wa kiroho wa Mungu. Kwa roho ile ile walitiwa mafuta wawe makuhani wadogo chini ya Kuhani Mkuu wao Yesu Kristo. (Matendo 2:1-36) Mtume Petro anasema juu ya hili, akisema hivi:

6 “Ninyi wenyewe pia kama mawe yaliyo hai mnajengwa kuwa nyumba ya kiroho kwa kusudi la ukuhani mtakatifu, kutoa dhabihu za kiroho zenye kukubalika kwa Mungu kupitia kwa Yesu Kristo. Lakini ninyi ni ‘ukoo uliochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya pekee, mpate kutangaza pote sifa bora’ za yeye aliyewaita ninyi kutoka katika giza kuingia katika nuru yake ya ajabu.”​—1 Pet. 2:5, 9, NW.

7. Kama makuhani wadogo wa kiroho, wanaingizwa katika eneo gani lililofananishwa na vile vile katika chumba gani cha hekalu la kiroho, ili wafanye nini katika mahali hapo?

7 Hii “nyumba ya kiroho” imejengwa kwa “mawe yaliyo hai” ambao ni makuhani wadogo wa Yesu Kristo. Wanaambiwa hivi: “Kwa hiyo, ndugu watakatifu, wenye kuushiriki mwito wa mbinguni, mtafakarini sana Mtume na Kuhani Mkuu wa maungamo yetu, Yesu.” (Ebr. 3:1) Kama nyumba ya makuhani hao wadogo inawapasa “kutoa dhabihu za kiroho zenye kukubalika kwa Mungu kupitia kwa Yesu Kristo.” (1 Pet. 2:5, NW) Hii ina maana kwamba wameingizwa katika ua wa mfano mahali ilipo “madhabahu” ya mfano ya Mungu, ili watoe hapo “dhabihu za kiroho” zao, juu ya msingi wa “mapenzi” ya Mungu. Vile vile hii inamaanisha kwamba, katika hali yao ya kuzaliwa kwa roho kama wana wa kiroho wa Mungu, wameletwa katika chumba cha kwanza cha mfano au “Patakatifu” pa hekalu la kiroho la Mungu. Humo wanajifurahisha mwangaza wa kiroho kana kwamba kutoka kwa kinara cha taa cha dhahabu chenye matawi saba, na kula chakula cha kiroho kana kwamba kutoka katika meza ya dhahabu ya mkate wa wonyesho na kutoa sala, sifa na utumishi kwa Yehova Mungu kana kwamba kusimama penye madhabahu ya dhahabu ya uvumba iliyosimama mbele ya pazia la ndani.

8. (a) Hivyo, basi, Patakatifu pa hema au hekalu palifananisha nini? (b) Ua wa raakuhani ulifananisha nini?

8 Kutokana na maoni haya, Patakatifu pa hekalu palifananisha hali ya kuzaliwa kwa kiroho ya ukuhani wa kiroho wa Mungu hata wakati washiriki wa ukuhani huu wangali wako katika mwili wa kidunia, katika nyama. Ni ujamaa wa pekee wa kiroho kwa Mungu unaotengwa na walio nje kana kwamba kwa pazia hata hawa hawawezi kuufahamu. Ule ua wa kikuhani mahali ilipokuwa madhabahu ya shaba unafananisha hali yao ya pekee ya kibinadamu pamoja na Mungu. Yeye anawatazama, si kama wenye dhambi wasiokamilika, waliolaaniwa na wasiofaa kutumikia katika “madhabahu” yake, bali kama wanafunzi waliotubu, kuongoka, kubatizwa wa Yesu Kristo ambao anahesabu kuwa wenye haki, wasio na dhambi, kwa sababu ya imani yao katika Mungu na kupitia kwa damu ya upatanisho ya Kuhani Mkuu Yesu Kristo. (Rum. 5:1, 9; 8:1; 3:24-26) Hivyo ule ua wa hekalu wenye madhabahu ya shaba ulifananisha hali yenye haki ya makuhani wadogo wa kiroho wa Mungu kwa habari ya miili yao yenye nyama.

9. (a) Makuhani hawa wadogo wa kiroho wanaingiaje katika Patakatifu Zaidi palipofananishwa, na je! wakiwa na dhabihu yenye kupatanisha dhambi? (b) Watatumikiaje katika Patakatifu Zaidi?

9 Kwa kuwa “nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kutokuharibika,” makuhani hawa wadogo waliozaliwa kwa roho walio chini ya Kristo vile vile inawapasa wakipite kizuizi cha kimwili kama kinavyofananishwa na lile “pazia” la ndani la hekalu. Wanafanya hivi kwa kufanya ukuhani wao wa kiroho duniani mpaka mauti ya kibinadamu, na kufuata hilo, katika wakati wa Mungu, anawafufua kutoka kwa wafu pamoja na ufufuo wa Kristo, yaani, kama viumbe vya kiroho vya asili ya kimungu na kutajirishwa na kutokufa na kutokuharibika. Kama ilivyoandikwa: “Hupandwa [katika mauti] mwili wa asili; hufufuliwa mwili wa roho.” (1 Kor. 15:42-44; Rum. 6:4, 5) Katika njia hii wanaingizwa mbele za Mungu Aliye Juu Zaidi, lakini, bila shaka, si kama wakimtolea dhabihu zo zote za kupatanisha dhambi. Hilo limekwisha kufanywa na Kuhani Mkuu wa Yehova,’Yesu Kristo, katika Siku ya Upatanisho ya mfano. Lakini, wakiungana wakati huo pamoja na Kuhani Mkuu wao mbinguni, wataweza kutumikia kama “makuhani wa Mungu na wa Kristo, na watatawala kama wafalme pamoja naye kwa miaka elfu.”​—Ufu. 20:4, 6, NW.

10. Katika 1 Wakorintho 3:9, 16, 17, Paulo analinganisha kundi la Kikristo kwa “jengo” gani, lakini hii isifahamiwe kuwa na maana gani, na kwa sababu gani?

10 Wakati wangali wako duniani, wanalinganishwa na mambo fulani. Kwa mfano, katika 1 Wakorintho 3:9, wanaambiwa na mtume Paulo hivi: “Ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.” Tunauliza, “Ni jengo” gani? Jibu linapewa katika mistari ya kumi na sita na kumi na saba, NW: “Je! ninyi hamjui kwamba ninyi watu ni hekalu la Mungu, na kwamba roho ya Mungu inakaa ndani yenu? Ikiwa ye yote anaharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu yeye; kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, hekalu ndiyo ninyi watu.” Hii haisemi au kumaanisha kwamba wao walifananishwa na hema iliyojengwa na Musa na mahekalu katika Yerusalemu. Katika hekalu ambalo Paulo anasema juu yake katika kitabu cha Waebrania Mungu mwenyewe anakaa humo, yeye mwenyewe akiwamo humo. Lakini hekalu lile ambalo Paulo anasema kwamba ndilo kundi Mungu mwenyewe hakai humo kwa namna ya mwili. Roho ya Mungu tu ndiyo inayokaa katika hekalu hili la mfano. Mungu anakaa humo kwa njia ya roho yake tu, kwa sababu washiriki wa hekalu hilo wako katika mwili wenye nyama duniani.

11. Shauri la msingi linaonyeshaje tofauti kati ya kundi kama hekalu na hekalu la Yehova katika mbingu?

11 Hekalu la Mungu katika mbingu halikujengwa juu ya msingi wa mitume na manabii wa Kikristo. Lakini kundi la Kikristo kama hekalu limejengwa juu ya Wakristo, mitume na manabii. Katika Waefeso 2:20-22, NW mtume Paulo anaandika hivi: “Ninyi mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, hali Kristo Yesu mwenyewe ndiye jiwe la pembeni la msingi. Katika umoja na yeye jengo zima, kwa kuunganishwa pamoja katika upatano, linakua kuwa hekalu takatifu kwa Yehova. Katika umoja na yeye ninyi, pia, mnajengwa pamoja kuwa mahali pa Mungu pa kukaa kwa roho.”

12. (a) Kwa sababu ya kukaa nini ndani yake ndiyo maana kundi duniani linafananishwa na hekalu, na hata hivyo kiko wapi katika hekalu kuu la kiroho la Mungu? (b) Kama “hekalu” la Mungu wa kweli duniani, kundi halipaswi likubali nini ndani yake lenyewe?

12 Ni kwa sababu roho ya Mungu inakaa ndani ya kundi hili lililounganishwa kwa upatano la makuhani wadogo wa kiroho kwamba kundi hili linaitwa “hekalu” la Yehova Mungu. Yeye mwenyewe yuko juu katika Patakatifu Zaidi pa kimbinguni pa hekalu lake kuu la kiroho. Jamii hii ya hekalu ambao bado wako duniani wanajikuta wenyewe wamo katika chumba cha “Patakatifu” cha hekalu kuu la kiroho. Kwa sababu ya kufananishwa na hekalu duniani ambamo Yehova anakaa kwa roho yake, kundi hili lililozaliwa kwa roho halipaswi kukubali namna yo yote ya ibada ya sanamu au ibada ya miungu ya uongo ndani yake. “Pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu?” anauliza mtume Paulo, halafu anaongeza kueleza: “Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”​—2 Kor. 6:16.

NYUA ZA HEKALU ZASONGAMANA NA WAABUDU

13. Wakati kundi lililozaliwa kwa roho litakapoondoka duniani, ni hali gani, kama inavyofananishwa na chumba cha hekalu, itakayotoweka?

13 Kundi hili lililozaliwa kwa roho linalofananishwa na hekalu lazima lionwe kama takatifu. Katika wakati wake kundi hili litaondoka duniani. Kwa kuondoka kwao, hali ya kuzaliwa na roho ya makuhani wadogo wa kiroho (kama inavyofananishwa na chumba cha Patakatifu cha hekalu la Yerusalemu) itatoweka. Makuhani hawa wadogo wa kiroho watakuwa wamekipita kizuizi cha kimwili (kinachofananishwa na pazia la ndani la hekalu) kuingia katika Patakatifu Zaidi pa kimbinguni kwa njia ya kufa kwao katika mwili na kufufuliwa kwao katika roho.

14. Ufunuo 21:1, 2 unalifananishaje kundi la 144,000 makuhani wadogo katika Patakatifu Zaidi pa kimbinguni?

14 Lo! litakuwa pendeleo takatifu kama nini kwa makuhani wadogo 144,000 wa hekalu la kiroho la Yehova kujikuta wenyewe katika Patakatifu Zaidi pa hekalu, mbele zenyewe za Yehova Mungu! Sehemu hii haikufananishwa katika habari za makuhani wadogo waliotumikia hekaluni katika Yerusalemu, lakini kwa uzuri inafananishwa katika kitabu cha mwisho cha Biblia Takatifu. Humo kundi la 144,000 makuhani wadogo wanaotumikia chini ya Kuhani Mkuu Yesu Kristo linafananishwa na bibi-arusi wake katika siku ya arusi. Kwa usemi wenye kupendeza sana mtume wa Kikristo Yohana anasimulia juu ya huyu bibi-arusi mwenye watu wengi ndani yake, akisema: “Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena. Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.”​—Ufu. 21:1, 2.

15. Yerusalemu wa kale wa kidunia na Yerusalemu Mpya inalinganaje juu ya kuwa na jengo la hekalu?

15 Tunakumbuka kwamba Yerusalemu wa kale wa kidunia, mpaka kufika mwaka wa kuharibiwa kwake na majeshi ya Kirumi katika mwaka wa 70 C.E., ulikuwa na hekalu lenye kupendeza sana ndani yake. Lakini namna gani juu ya Yerusalemu Mpya wa kimbinguni, ambao mtume Yohana aliona katika njozi yapata miaka 26 wakati hekalu la Yerusalemu wa kale lilipokuwa limekwisha kuharibiwa katika mwaka wa 70 C.E.? Wakati Yohana anapoendelea kueleza kwake kuzuri juu ya Yerusalemu Mpya wa kimbinguni anatuambia, akisema: “Nami sikuona hekalu ndani yake; kwa maana [Yehova] Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo, ndio hekalu lake. Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-Kondoo. Na mataifa watatembea katika nuru yake.”​—Ufu. 21:22-24.

16. Ni nini juu ya mahali pa makuhani wadogo 144,000 kinachofanya jengo la hekalu katika Yerusalemu Mpya lisiwe la lazima, na Yehova mwenyewe ni hekalu lake namna gani?

16 Kwa sababu gani Yerusalemu Mpya wa kimbinguni uwe na hekalu ndani yake, jengo lililo tofauti ili makuhani wadogo 144,000 watumikie ndani yake na hivyo kutoa utumishi mtakatifu kwa Mungu kwa njia ya kuzunguka kupitia kwa jengo? Kwa sababu gani, hali wanapokuwa mbele zenyewe za Mungu ‘wanamwona uso wake’? (Ufu. 22:4) Yehova Mungu mwenyewe ndiye hekalu la Yerusalemu Mpya. Yerusalemu Mpya wa kimbinguni silo hekalu. Hapana, Yehova Mungu Mwenyezi ndiye hekalu. Yeye anajaa mahali, anaenea mahali, pa hekalu kwa mji wa kimbinguni. Kwa kuwa yeye yuko huko, si kwa njia ya roho, bali yeye mwenyewe akiwako huko, yeye hana lazima ya kuwa na jengo tofauti ambalo kwa hilo wakaaji wa Yerusalemu Mpya, makuhani wadogo 144,000 wangekuwa wakimwabudu na kumtumikia yeye kwa njia isiyo ya moja kwa moja. Hivyo wanamtolea yeye utumishi mtakatifu moja kwa moja chini ya ukuhani mkuu wa Mwana-Kondoo, Yesu Kristo.

17. Mwana-Kondoo vile vile pamoja na Yehova Mungu, ni hekalu la Yerusalemu Mpya namna gani?

17 Ndiyo sababu Mwana-Kondoo anashiriki pamoja na Yehova katika kuwa hekalu la Yerusalemu Mpya. Kama Ufunuo 21:22 usemavyo: “Na Mwana-Kondoo” vile vile. Yeye mwenyewe yuko katika Patakatifu Zaidi pa hekalu la kiroho la Yehova. Yeye amekwisha kutoa moja kwa moja kwa Mungu dhabihu yenye kupatanisha dhambi ya Siku ya Upatanisho iliyofananishwa. Kama Kuhani Mkuu mfano wa Melkizedeki, yeye ameketi mkono wa kuume wa Mungu.

18. Ni katika ‘eneo gani la hekalu la kiroho la Yehova ambamo watu watapata faida kutokana na Siku ya Upatanisho, na dhabihu za Siku ya Upatanisho zilitolewa kwa ajili ya nani ili kuonyesha hili?

18 Ingawa wakati huo haitakuwako tena hali ya kuzaliwa kwa roho ya makuhani wadogo 144,000 kama ilivyofananishwa na chumba cha Patakatifu cha hekalu, nyua za kidunia za hekalu kuu la kiroho la Yehova zitaendelea. Watu walio duniani watakaofaidika na Siku ya Upatanisho ya Yehova watafanya hivyo katika nyua hizo. Hii inapatana vizuri na uhakika wa kwamba toleo la dhambi la Siku ya Upatanisho lilitolewa si kwa ajili ya jamaa ya kikuhani tu bali kwa ajili ya wote wanaobaki wa watu waliomwabudu Yehova katika hekalu lake.

19. (a) Ni nani ambao nabii Zekaria alisema wangejiunga wenyewe kwa Yehova “katika siku hiyo” na kuomba kibali chake? (b) Kana kwamba mpango wa jambo hilo, ni ua gani wa ziada uliokuwamo katika hekalu la Herode Yerusalemu, na Sulemani wakati wa kufungua hekalu aliombea nani wasio wa Israeli?

19 Wakati nabii wa Mungu Zekaria alipokuwa akitoa unabii juu ya kujengwa upya kwa hekalu katika Yerusalemu katika karne ya sita mbele ya Wakati wetu wa Kawaida, aliongozwa na roho ya Mungu kusema: “Na mataifa mengi watajiunga wenyewe kwa Yehova katika siku hiyo, na watakuwa watu wangu; nami nitakaa katikati yako wewe.” “Ndiyo, watu wengi na mataifa yenye nguvu watakuja kumtafuta Yehova wa majeshi katika Yerusalemu, na kuomba kibali cha Yehova.” (Zek. 2:11; 8:22, American Standard Version) Kupatana na unabii huo wa kuja kwa wasio Waisraeli kumwabudu Yehova katika hekalu lake, hekalu lililojengwa na Mfalme Herode, lililokaa mahali pa hekalu lililojengwa katika wakati wa nabii Zekaria, ndani yake mlikuwamo, si ua wa makuhani na madhabahu yake, na tena ua wa Israeli na ua wa wanawake tu, bali vile vile ua wa Mataifa au watu wasio Waisraeli. Hata karne zilizotangulia hili, Mfalme Sulemani, wakati alipokuwa akifungua hekalu la kwanza katika Yerusalemu, aliwaombea wageni waliotoka nchi za mbali kuja kuabudu katika hekalu la Yehova.​—1 Fal. 8:41-43; 2 Nya. (Sik.) 6:32, 33.

20. Tangu wakati gani, zaidi, unabii huo wa Zekaria umekuwa ukitimizwa, na kwa sababu gani twauona ukitimizwa tangu wakati huo?

20 Ule unabii uliosemwa zamani na Zekaria umekwisha kuanza kutimizwa sasa katika wakati wetu, zaidi tangu mwaka wa 1935 C.E. Maana yake utimizo wakati wangali wako mabaki ya makuhani wadogo wa kiroho duniani, wanaotumikia katika chumba cha Patakatifu cha hekalu la kiroho la Yehova. Kwa sababu hiyo ule “mkutano mkubwa” wa wageni wanaokuja makundi makundi kutoka sehemu zote za dunia kwenye nyua za hekalu moja la kiroho la Yehova wanaonana na kushirikiana na makuhani hawa wadogo wa kiroho ambao bado wako duniani. Tarehe ya mwaka wa 1935 C.E. inaonyesha mwaka wakati huo “mkutano mkubwa” wa waabudu wa Yehova wasio makuhani ulipoanza kujulikana kuwa ukija kwenye hekalu, kwa sababu katika mwaka huo wenye kukumbukwa unabii wa Ufunuo 7:9-17 juu ya “mkutano mkubwa” au “kundi kubwa” ulielezwa kulingana na mambo ya hakika ya wakati huo. (Tazama The Watchtower toleo la Agosti 1 na 15, 1935.) Tunapotazama njozi ya Ufunuo iliyoonwa na mtume Yohana, ni kama tunaona “mkutano mkubwa” wa mataifa yote wa waabudu wakiadhimisha Sikukuu ya Vibanda ya mfano katika hekalu la Mungu.

21. Yohana anasimuliaje juu ya “mkutano mkubwa” huu katika Ufunuo 7:9-15?

21 Akituambia mambo ambayo anaona, Yohana anasema hivi: “Tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za Mwana-Kondoo, wamevikwa mavazi meupe, wana matawi ya mitende mikononi mwao; wakilia kwa sauti kuu wakisema, Wokovu una Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo. . . . Hao ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu, nao wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo. Kwa hiyo wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, nao wanamtumikia mchana na usiku katika hekalu lake, na yeye aketiye katika kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao.”​—Ufu. 7:9-15.

22. (a) Juu ya hekalu la kiroho la Mungu, ni wapi ambapo huo “mkutano mkubwa” unapomtumikia Yeye mchana na usiku? (b) Njozi ya Yohana inaonyeshaje kwamba hekalu la kiroho limeokoka “dhiki ile iliyo kuu,” na huko “mkutano mkubwa” unakubali faida gani?

22 Njozi hii nzuri inaonyesha “mkutano mkubwa” wa mataifa yote kama ukimtumikia Yehova katika hekalu lake, yaani, katika nyua za kidunia walizowekewa wale wasio Waisraeli wa kiroho, kana kwamba ilikuwa katika “ua wa Mataifa.” Ah, ndiyo, katika njozi ya mtume Yohana hekalu kuu la kiroho la Yehova Mungu limeokoka “dhiki ile iliyo kuu” ya siku hizi za mwisho, kwa maana huu “mkutano mkubwa” umeokoka “dhiki ile iliyo kuu” nao wanajikuta wenyewe wako katika hekalu la Yehova wakipunga matawi ya mitende kama tawi la mtende la mapokeo la sikukuu (lulaba) lililopungwa na watu wakati wa Sikukuu ya Vibanda. Kwa Yehova Mungu na kwa Mwana-Kondoo wake wa dhabihu, Yesu Kristo, ndiko wanakohesabia wokovu wao, na sasa wanatazamia uzima usio na mwisho wenye furaha na utumishi wa kimungu katika taratibu mpya ya mambo ya Mungu katika dunia ya paradiso. (Ufu. 7:16, 17) Kwa kushukuru wanakubali faida za toleo la dhambi lililotolewa Siku ya Upatanisho ya Yehova iliyo kuu.​—Law. 16:1-34.

23. (a) Kwa sababu gani “mkutano mkubwa” huo sio peke yake utakaosongamana katika nyua za kidunia za hekalu la kiroho wakati wa Ukuhani Mkuu wa Kristo wa miaka elfu? (b) Itawapasa hawa wajiunge katika kuadhimisha nini ili wapate uzima wa milele duniani?

23 Walakini, waokokaji hawa wa “dhiki ile iliyo kuu” ambayo kwa hiyo taratibu hii ya sasa ya mambo itakoma sio peke yao watakaosongamana katika nyua hizo za wokovu. Wakati wa Ukuhani Mkuu wa miaka elfu wa Mwana-Kondoo Yesu Kristo pamoja na makuhani wake wadogo wa kiroho 144,000 katika makao ya kimbinguni ya hekalu la kiroho la Yehova, “kutakuwa na ufufuo wa wafu, wenye haki na wasio haki pia.” (Matendo 24:15; Ufu. 20:4, 6, 11-14) Wote hawa inawapasa waje kwenye nyua za hekalu la kiroho la Yehova na kujiunga katika kumtumikia na vile vile kwa furaha kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda ya mfano iliyo kuu. Hakuna wokovu kwa uzima wa milele katika paradiso ya kidunia kwa njia nyingine yo yote. Mistari ya mwisho ya unabii wa Zekaria inaonekana kama ikionyesha hivyo. Watakaofufuliwa wote wanaotaka uzima wa milele duniani yawapasa waje kwenye hekalu la kiroho ili “kumwabudu Mfalme, [Yehova] wa majeshi,” na “kushika sikukuu ya Vibanda.” Lo! utakuwa wakati wenye furaha isiyoneneka kama nini kwa wale watakaofanya hivyo!​—Zek. 14:17, 18.

24. (a) Ni hekalu gani ambalo Yehova Mungu anakubali, na ni kwenye hekalu gani ambako inawapasa wote waje ili wapate uzima katika taratibu mpya? (b) Ni habari gani ambazo sasa ni pendeleo la wale waliokwisha kuwa katika nyua kuwapelekea wengine?

24 Vile vile, yenye baraka ni maoni ya sisi sote leo tulio katika nyua za hekalu la kiroho la Yehova sasa, kwamba wengine kati yetu wamo katika ua wa ndani wa makuhani ama hesabu kubwa zaidi ya sisi wamo katika nyua za waabudu wasio makuhani wa Mungu Aliye Juu Zaidi, Yehova wa majeshi. Hili ndilo hekalu peke yake ambalo Mungu wa wokovu anakubali. Ndilo hekalu moja peke yake ambalo kwa hilo inawapasa watu wa mataifa yote waje ili washiriki katika ibada iliyo safi na hivyo wapate wokovu wa milele katika taratibu mpya yenye haki ya Mungu. Hekalu hilo sasa liko wazi kwa kukusanywa kwa watafutaji wote wa Mungu mmoja aliye hai na wa kweli. Hizi ndizo habari kuu kweli kweli zinazoungana na matukio ya nyakati zetu za ajabu. Ni pendeleo la maana sana la sisi sote tunaotumikia katika nyua za hekalu la kiroho la Yehova kupeleka habari njema zenye kuokoa uhai kwa wengine wote, mbele ya kuja “dhiki ile iliyo kuu.”

​—Kutoka The Watchtower, Dec. 1, 1972.

[Maelezo ya Chini]

a Tazama The Mishnah, cha Herbert Danby (cha mwaka wa 1933), ukurasa wa 178, mafungu 5, 6 na 7.

Tazama The Temple, cha Dr. A. Edersheim, (cha mwaka wa 1874), kurasa za 238, 242.

Tazama Volume 10 ya Cyclopaedia ya M’Clintock na Strong, ukurasa wa 148, fungu la mwisho chini ya “21st of Tishri.”

[Sanduku/Mchoro katika ukurasa wa 255]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

HEKALU LILILOJENGWA UPYA NA HERODE (Ramani ya Msingi)

1. Patakatifu Zaidi

2. Patakatifu

3. Madhabahu ya Toleo la Kuteketezwa

4. Bahari ya Kusubu

5. Lango la Ndani la Hekalu

6. Kizuizi cha Mawe

7. Lango Zuri

8. Lango

9. Hekalu

10. Ua wa Makuhani

11. Ua wa Israeli

12. Ua wa Wanawake

13. Ua wa Nje

14. Ua wa Mataifa

15. Ukumbi wa Kifalme

16. Ukumbi

17. Ukumbi wa Sulemani

18. Ukumbi wa Kaskazini

19. Ukuta wa Mji

20. Katikati

21. Bonde la Kidroni

22. Mlima wa Mizeituni masharikini

MAANA YA UNABII

PATAKATIFU ZAIDI: Eneo lenyewe la mbingu anakoketi Yehova mwenyewe katika kiti cha enzi

PATAKATIFU: Hali ya kuzaliwa kwa roho ya Yesu Kristo na 144,000 Wakristo waliotiwa mafuta wakati wangali wako katika mwili

PAZIA: Pazia kama cha kutenga kati ya Patakatifu na Patakatifu Zaidi lilifananisha kizuizi cha kimwili kinachotenga ukuhani duniani usikaribie mbele za Mungu mbinguni

MADHABAHU: Mapenzi ya Mungu kama yanavyoonyeshwa na nia yake kukubali dhabihu kamilifu ya kibinadamu ya Yesu

UA WA MAKUHANI: Hali yenye haki ya Yesu Kristo na makuhani wadogo wa kiroho wa Mungu kwa habari ya miili yao yenye nyama

UA WA MATAIFA: Hali yenye haki ambayo inawapasa wanadamu wote wafikie ili wamwabudu Mungu kwa kukubalika

[Picha katika ukurasa wa 251]

Yesu alipotiwa mafuta kwa roho takatifu katika mwaka wa 29 C.E., hekalu kubwa la kiroho la Mungu lilitokea

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki