Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 5/15 kur. 237-240
  • Ukamatano wa Ubatizo wa Maji na Wokovu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ukamatano wa Ubatizo wa Maji na Wokovu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KIONGOZI WETU WA KIMASIHI
  • Ubatizo—Takwa la Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Maji Yachukua Ulimwengu
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Jinsi Ubatizo Unavyoweza Kutuokoa Sisi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Maana ya Ubatizo Wako
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 5/15 kur. 237-240

Ukamatano wa Ubatizo wa Maji na Wokovu

1. (a) 1 Petro 3:20, 21 anaunganisha namna gani kuchukuliwa kwa nafsi nane za kibinadamu katika Gharika na ubatizo wa Kikristo? (b) Ubatizo unatofautianaje na maji?

UKAMATANO wa ubatizo wa maji na wokovu unaelezwa na mtume Petro katika barua yake ya kwanza, sura ya tatu. Akiisha kusimulia juu ya kufufuliwa kwa Yesu katika roho na kuhubiri kwake kwa roho zilizo kifungoni, Petro anaendelea kusema hivi: “Uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingojea katika siku za Nuhu, wakati safina ilipokuwa ikiundwa, ambayo ndani yake watu wachache, yaani, nafsi nane, walichukuliwa salama katika maji. Lile linalolingana na hili pia linaokoa ninyi sasa, yaani, ubatizo, (si kuondolewa kwa uchafu wa mwili, bali ombi lifanywalo kwa Mungu kwa dhamiri njema,) kupitia kwa ufufuo wa Yesu Kristo.” (1 Pet. 3:20, 21, NW; RS; AT; Mo) Si maji yanayookoa. Ubatizo huo siyo maji ya ubatizo. Ubatizo ni kupita katika maji kwa kuzamishwa humo. Ubatizo ni tendo, si maji.

2. (a) Waebrania 11:7 inaonyeshaje jambo lililotokeza wokovu wa Nuhu katika gharika? (b) Ijapokuwa kutembea kwa Nuhu na Mungu mbele ya gharika, ni hatua gani ya uamuzi ambayo ilimpasa achukue ili aokolewe?

2 Nuhu hakuokolewa na maji ya Gharika. Namna alivyookoka, Waebrania 11:7 inatuambia hivi: “Kwa imani Nuhu akiisha kuonywa na Mungu katika habari za mambo yasiyoonekana bado, kwa jinsi alivyomcha Mungu, aliunda safina, apate kuokoa nyumba yake. Na hivyo akauhukumu makosa ulimwengu, akawa mrithi wa haki ipatikanayo kwa imani.” Hata wakati Gharika ilipokuwa haijafika “Nuhu alikuwa mtu wa haki, mkamilifu katika vizazi vyake; Nuhu alikwenda pamoja na Mungu.” (Mwa. 6:9) Lakini ulifika wakati ilipompasa Nuhu afanye uamuzi mkubwa. Hii ilikuwa wakati Mungu alipomwonya juu ya mambo ambayo yangekuja katika kizazi chake na akamwamuru ajenge safina kubwa mno. Kufanya hivi kulitaka imani na utii upande wa Nuhu. Sasa ulizo lilikuwa hivi, Je! Nuhu angefanya mapenzi ya Mungu? Yeye aliamua kufanya jambo hili lililokuwa kubwa kuliko yote katika maisha yake. Basi akajitoa mwenyewe, akajiweka mwenyewe wakf kwa kufanya mapenzi ya Mungu. Jambo hili liliongoza kwenye wokovu wake na nyumba yake. Waliokolewa katika safina hiyo.​—Linganisha Waebrania 10:7-9.

3. (a) Basi safina hiyo ya wokovu ilikuwa mfano wa nini kwa habari ya Nuhu na jamaa yake? (b) Kwa utii wao kwa sababu ya imani, ni mali gani ya ndani ambayo nafsi hizo nane zilijipatia?

3 Hivyo safina hiyo ikawa mfano wa kujiweka kwa Nuhu wakf afanye mapenzi ya Mungu na kufanya kwake mapenzi hayo ya kimungu kwa imani na utii. Safina hii, uliokuwa wonyesho thabiti, unaogusika na unaofaa wa kujiweka wakf ili kufanya mapenzi ya Mungu, ndiyo iliyookoa Nuhu na nafsi nyingine saba za kibinadamu. Maji ya Gharika hayakuokoa; yalileta kifo kwa wale waliokuwa nje ya safina. Ndani ya safina, Nuhu na nyumba yake walipita katika maji na wakaokolewa. Kwa kujiweka mwenyewe wakf afanye mapenzi ya Mungu kwa habari ya safina kisha kuijenga Nuhu alipata dhamiri njema kwa Mungu. Nyumba yake ilifanya vivyo hivyo pamoja na yeye. Ile haki ambayo walikuwa nayo mpaka wakati wa kujenga safina, hiyo peke yake, isingaliwaokoa katika Gharika. Nyumba ambayo ndani yake Nuhu na jamaa yake waliishi mpaka kuingia katika safina iliharibika.

4. Kama ilivyoonyeshwa katika habari ya Wayahudi chini ya agano la Torati ya Musa, kwa sababu gani dhamiri njema ni kitu cha kuomba kwa Mungu?

4 Jambo linalolingana na hili ndilo linalotukia kwa wale wanaokuwa wanafunzi waliobatizwa wa Yesu Kristo. Dhamiri njema kwa Mungu si jambo fulani tunalozaliwa nalo au tunalojifanyia wenyewe kwa masharti yetu wenyewe kwa kazi za kujitafutia haki wenyewe. Wayahudi walijaribu kupata dhamiri njema kwa Yehova Mungu kwa kujitahidi kupata ukamilifu katika kufanya kazi zilizoamriwa katika agano la Torati la Musa na taifa lao, lakini walishindwa. Ndiyo sababu, kila mwaka, kila Siku ya Upatanisho (Tishri 10), iliwapasa watolewe dhabihu za upatanisho na kuhani mkuu wa Israeli, ili kurudisha dhamiri yao njema kwa Mungu. Hivyo dhamiri njema ndilo jambo ambalo inatupasa tuombe kwa Yehova Mungu.

5. (a) Tunafanyaje ombi kwa Mungu kwa dhamiri njema, na kuipata? (b) Mpaka wakati huo, tulikuwa tukifanya mapenzi ya nani?

5 Ndiyo sababu Petro, wakati wa kusema yaliyomo katika ubatizo, anasema hivi: “Si kuondolewa kwa uchafu wa mwili, bali ombi lifanywalo kwa Mungu kwa dhamiri njema.” (1 Pet. 3:21, NW) Basi, tunafanya ombi namna gani kwa hiyo dhamiri njema? Tunafanya hivi kwa kufanya kama Nuhu, kujiweka wenyewe wakf, mbele ya kupita katika maji. Kama Nuhu sisi tunajiweka wakf wenyewe kwa Yehova Mungu tufanye mapenzi yake na tangu wakati huo kuendelea kuyafanya. Na kwa kuwa hii inashughulika na kushirikiana na agano jipya la Yehova ambalo Yesu Kristo ndiye Mpatanishi, inatupasa tufanye kama vile watu wa Israeli katika Mlima Sinai walivyofanya mbele ya kuingizwa katika agano la Torati la Musa, wakijiweka wenyewe wakf kwa Mungu kwa maneno haya: “Yote ambayo Yehova amesema sisi tuna nia ya kuyafanya.” (Kut. 19:8; 24:7, 8, NW) Mpaka wakati huo sisi ‘tulitenda mapenzi ya Mataifa’ na tukaishi “katika tamaa za wanadamu”; lakini sasa tunajiweka wenyewe wakf ili tuishi “kwa mapenzi ya Mungu.” (1 Pet. 4:1-3, 19) Hii inatokeza kupata kwetu dhamiri njema, kwa maana tunapojua kwamba tunafanya mapenzi ya Mungu tunajifurahisha dhamiri njema.

6. Kwa kuwa sasa tunaweza kufanya mapenzi ya Mungu kwa kutokamilika, jambo gani ambalo tunahitaji litumiwe kwa ajili yetu ili kutunza dhamiri njema?

6 Bila shaka, tunaweza kufanya mapenzi ya Mungu katika njia isiyokamilika, na kwa sababu hiyo tunahitaji damu ya upatanisho ya Yesu Kristo itumiwe na Mungu kwa ajili yetu, kutusafisha sisi na doa la dhambi na kutokamilika. Kama Waebrania 9:14 inavyouliza: “Basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa [roho ya] milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai?”

7. (a) Basi, kujiweka kwetu wakf kwa Mungu kupitia kwa Kristo kunaonyesha nini kweli, kulingana na 1 Petro 3:21? (b) Ili kutunza dhamiri hii njema, ni lazima tutafute msaada gani wenye kuendelea?

7 Hivyo kujiweka wenyewe wakf kufanya mapenzi ya Mungu kwa kweli ni “ombi lifanywalo kwa Mungu kwa dhamiri njema.” Dhamiri njema inatokea, si kutokana na kufanya kazi zetu wenyewe za kujitafutia haki yetu wenyewe, ambayo ni “matendo mafu,” bali kutokana na kazi za Mungu zilizoagizwa, mapenzi ya Mungu. Hili ndilo tunajiweka wenyewe wakf kwake Yeye tufanye. Ili kutunza dhamiri hii njema tangu wakati tulipoipokea, ni lazima sikuzote tutafute msaada wa faida za damu iliyomwagwa ya Yesu Kristo kama dhabihu ya upatanisho ya Siku ya Upatanisho ya mfano iliyo kuu. Kama Waebrania 9:22, NW inavyotukumbusha, “isipokuwa damu inamwagwa msamaha hautukii.” Kwa sababu hii sisi, ambao tunasamehewa kupitia kwa Kristo, ‘hatujioni tena kuwa na dhambi.’​—Ebr. 10:1, 2.

8. (a) Kwa sababu ya kutubu kwetu na kuongoka na kujiweka wenyewe wakf, Mungu anatumia nini kwa ajili yetu, na kwa matokeo gani kwetu? (b) Basi ubatizo wetu wa maji unaweza kusemwa kuwa unafananisha nini? (c) Ni maandiko gani yanayoonyesha kama ni ubatizo wa maji peke yake ndio unaotuokoa sisi?

8 Ndivyo kujiweka wenyewe wakf kwa Mungu kunavyokuwa “ombi lifanywalo kwa Mungu kwa dhamiri njema.” Sababu gani hivyo? Kwa sababu ya kuwa kwetu katika hali isiyokamilika, yenye dhambi, hatukubaliki kwa Mungu. Hivyo, kwa sababu tunatubu dhambi na kugeuka au kuongoka na kujiweka wenyewe wakf kwa Mungu kupitia kwa Kristo, Yehova anatumia damu yenye kusafisha ya dhabihu ya Kristo ya upatanisho kwetu, kwa njia hiyo kutuondolea laana ya dhambi na kutupa dhamiri njema kwake Yeye. Kwa hiyo inaweza kusemwa kwamba kubatizwa kwetu katika maji, kupita kwetu kwa utii katika maji ya ubatizo, kunafananisha kujiweka kwetu wakf kwa Yehova Mungu kupitia kwa Yesu Kristo. Kukubali kwa utii kwa Nuhu kufanya mapenzi ya Mungu kwa kujenga kulimwokoa yeye na nyumba yake, na kujiweka kwetu wakf kwa Mungu tufanye mapenzi yake halafu kwa uaminifu kuyatimiza ‘kunatuokoa sisi sasa.’ Kwa habari hii sisi tunaita juu ya jina la Yehova ili tuokoke. (Ebr. 13:15) Tunamwamini Bwana Yesu ili tuokoke. (Matendo 4:12) Tunafanya ungamo la wazi au tangazo la wazi kwa vinywa vyetu kwamba ‘Yesu ni Bwana’ na tunaamini katika mioyo yetu kwamba “Mungu alimfufua katika wafu,” ili tuokolewe.

9. Ni jambo gani ambalo mtu ambaye amechukua hatua hizo za hakika hawezi kulisema mwishowe juu ya “ombi [lake] lifanywalo kwa Mungu kwa dhamiri njema”?

9 Kwa sababu hiyo hakuna mtu anayechukua hatua hizo za hakika kama toba, kuongoka na kujiweka wakf aliye na sababu ya kusema mwishowe kwamba “ombi [lake] lifanywalo kwa Mungu kwa dhamiri njema” halikujibiwa hata kidogo na Mungu hakumpa dhamiri njema hata kidogo na hivyo kujiweka kwake wakf hakukuwa kwa maana na sasa si kwa lazima kwake.

10. (a) Ili tupate kuokolewa, inatupasa tujitoe wenyewe kwa kitu gani? (b) Kwa sababu gani ni “kupitia kwa ufufuo wa Yesu Kristo” kwamba vile vile ubatizo huo unatuokoa sisi sasa?

10 Kwa hiyo sasa tunaweza kufahamu kwamba ikiwa tunataka tuokolewe inatupasa tujitoe wenyewe kwa ubatizo wa maji, kwa kufuata mfano wa Yesu Kristo na kwa kutii amri yake. (Mt. 28:19, 20) Hakuna liwezalo kusemwa waziwazi zaidi kuliko ilivyosemwa katika 1 Petro 3:21, NW, yaani: “Lile linalolingana na hili pia linaokoa ninyi sasa, yaani, ubatizo, . . . kupitia kwa ufufuo wa Yesu Kristo.” Inatupasa tuamini kwa mioyo yetu kwamba Mungu alimfufua yeye kutoka kwa wafu. Yesu Kristo aliyefufuka ndiye wa lazima kwa wokovu wetu, kwa maana Mwana wa Mungu aliyefufuka peke yake ndiye angeweza kutenda kama Kuhani Mkuu wa Mungu katika kutoa kwa Mungu mbinguni bei ya damu yake yenye uhai iliyomwagwa kwa ajili yetu tupate msamaha wa dhambi na kutokeza dhamiri njema. Yeye ni wa lazima katika Mungu kutupa sisi dhamiri njema katika kujibu ombi letu.​—1 Pet. 3:22.

KIONGOZI WETU WA KIMASIHI

11. Kufua mavazi yao katika damu ya Mwana-Kondoo kunatokeza nini kwa “mkutano mkubwa,” na wana sababu gani nzuri kumshangilia Mwana-Kondoo huyu wa Mungu?

11 Hata “mkutano mkubwa” ambao leo unakusanywa kutoka kwa mataifa yote, kabila, jamaa na lugha wanafua mavazi yao na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo Yesu Kristo na kwa njia hiyo kupata dhamiri njema kwa Mungu. Wana sababu nzuri kusimama mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na kupunga matawi ya mitende na kulia kwa sauti: “Wokovu una Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo.” (Ufu. 7:9-14) Ndivyo wanavyomshangilia Wakili Mkuu wa Yehova wa utawala wa kimungu. Huyu ndiye wanayemfuata kama Mchungaji na Kiongozi wao.

12. Wakili Mkuu wa Utawala wa Kimungu anapaswa afuatwe na nani duniani, na kufanya kwao hivi kutakuwa na maana gani kwao?

12 Wote wanaokuwa wanafunzi waliojiweka wakf na kubatizwa wa Wakili Mkuu wa utawala wa kimungu yawapasa wamfuate yeye. Ili wafanye hivi, ni lazima wamtazame “sana Wakili Mkuu na Mkamilishaji wa imani yetu, Yesu.” (Ebr. 12:1, 2, NW) Kufanya kwetu hivi kwa upendo kutakuwa na maana ya wokovu wetu wa milele kwa sifa ya milele ya Mtawala wa wa Kimungu mkuu, Yehova Mungu.

​—Kutoka The Watchtower, Nov. 15, 1972.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki