Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 5/15 uku. 240
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Habari Zinazolingana
  • Jihadhari na “Sauti ya Wageni”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Kondoo Wanaitikia Sauti ya Mchungaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Wayahudi Wasikia Sauti ya Mungu​—Je, Wataonyesha Imani?
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Ubora wa Sauti
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 5/15 uku. 240

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Sababu gani Matendo 9:7 linaonyesha kwamba washiriki wa Sauli waliokuwa safarini walisikia sauti, na hali Matendo 22:9, likiripoti juu ya kisa kile kile, linataja kwamba hawakuisikia?​—Argentina.

Nyuma ya ufufuo wake na kupaa kwake mbinguni, Yesu Kristo alimtokea Sauli wa Tarso (nyumaye mtume Paulo) na akasema naye kwa sauti ya kusikika. Lakini “wasafiri wenzi wa Saulo wakasimama kimya, kwa kuwa waliisikia sauti lakini hawakumwona ye yote.” (Matendo 9:7, An American Translation) Likimtaja Paulo kama akisema juu ya tukio ili hili, Matendo 22:9 linasema: “Wale wanaume waliokuwa nami wakaona mwangaza ule, lakini hawakuisikia sauti ya aliyekuwa akisema nami.”​—AT.

Uchunguzi wa maana ya neno la Kigiriki kwa “sikia” ni wenye msaada kwa kuazimia jambo hili linaloelekea kama tofauti. Linaweza kuwa na maana ya kusikia jambo fulani bali kuelewa linalosemwa. Wale waliokuwa wakisafiri na Paulo bila shaka walisikia sauti lakini, kwa sababu ilipunguzwa na haikusikiwa waziwazi, hawakuelewa habari aliyopashwa Paulo.​—Linganisha 1 Wakorintho 14:2, ambapo neno la Kigiriki kwa “sikia” limetafsiriwa “husikiliza.” (NW)

Tafsiri mbalimbali za Biblia vile vile zinaonyesha tofauti hii. New American Standard Bible inatafsiri maandiko yanayofanyiwa maneno kama ifuatavyo: “Wanaume waliosafiri naye wakasimama kimya, wakiisikia sauti, lakini wasimwone ye yote.” “Waliokuwa nami wakauona mwangaza, ndiyo, lakini hawakuelewa [maelezo ya pembeni: Au, kusikia (kwa ufahamu)] sauti ya Yeye aliyekuwa akisema nami.” Tafsiri ya Kijeremani ya Leander van Ess inasema: “Kwa kuwa kweli waliusikia uvumi, lakini wasimwone ye yote.” “Lakini sauti ya aliyekuwa akisema nami hawakuielewa.” Richard Francis Weymouth anatumia tafsiri zinazoonyesha kwamba wale watu waliisikia sauti lakini hawakusikia “maneno yake Yeye” aliyesema na Paulo. Vivyo hivyo, New World Translation inasema kwamba wale watu walisikia “mvumo wa sauti,” bali ‘hawakusikia [‘hawakusikia kwa kuelewa,’ maelezo ya pembeni] sauti ya aliyekuwa akisema’ na Paulo.​—Matendo 9:7; 22:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki