Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 5/1 kur. 199-207
  • Utawala wa Kimungu— Juu ya Wanadamu Mwanzoni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Utawala wa Kimungu— Juu ya Wanadamu Mwanzoni
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MWENDO WA WALE WANAOUPINGA
  • WANADAMU WANALETWA CHINI YA UTAWALA WA MASHETANI
  • Utawala wa Kimungu—Je! Sisi Tunauunga Mkono au Tunaupinga?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Utawala wa Kimungu—Tumaini la Pekee la Wanadamu Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Suala Linalokuhusu Wewe
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
  • Kwa Nini Tunahitaji Ufalme wa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2020
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 5/1 kur. 199-207

Utawala wa Kimungu​— Juu ya Wanadamu Mwanzoni

“Yehova mwenyewe ameweka imara kiti chake cha enzi katika mbingu zenyewe; na juu ya kila kitu ufalme wake mwenyewe umetawala.”​—Zab. 103:19, NW.

1. “Mpango” ni nini, kulingana na maana yetu ambao katika huo sisi sote tulizaliwa, na tutaukadirije?

SISI SOTE tulizaliwa katika “mpango.” Kwa neno hilo je! tunamaanisha taratibu ya mambo iliyopo hapa katika dunia yetu? Sivyo! Tunamaanisha mpango ambao dunia yetu ni sehemu yake iliyo ndogo sana. Tunamaanisha mpango unaofika mpaka katika anga la juu. Unatia zaidi ya kundi la nyota nyingi ambazo jua letu ni mojawapo tu la majua hayo mengi. Unatia makundi yote ya nyota ambazo hakuna darubini kubwa kuliko zote zilizofanywa na wanadamu ambazo zimeweza kuzifanya zionekane na macho ya kibinadamu. Mpango huu ni mkubwa mno ajabu hata inakuwa lazima kuupima kwa vipimo vya mwendo vinavyoitwa na wataalamu wa nyota light years (mwendo wa nuru kwa mwaka mmoja). Bila kujali ukubwa wake, yampasa kila mtu akubali kwamba ni mpango wa ajabu sana. Ulikuwa umekwisha kuwapo wakati vijana wa leo wenye kupinga walipokuwa hawajakuwapo, au wakati wanadamu walipokuwa hawajaumbwa. Sisi sote tuliletwa katika mpango huu, si kwa mapenzi au kuchagua kwetu wenyewe. Basi, je! mpango huu ndio wa kupinga?

2. Kwa sababu gani isingewezekana mwanadamu awe mwenye daraka la kuongoza “mpango” huu, na akili yetu inaonyesha nini juu ya mwenye kuuongoza?

2 Ni nani anayeongoza mpango huu ulio mkubwa ajabu? Wakati sisi wanadamu hatujatokea ulikuwa umekwisha anza kutenda kwa utaratibu. Hauhitaji sisi tuuendeshe milele, kuufanya uendelee kuning’inia mle angani na kufanya kazi kwa upatano sana. Bila haja ya kusema, ni mkubwa mno kwetu, uko mbali mno kupita uwezo wetu kufika. Sisi hatuwezi kuuongoza kutoka hapa duniani kwa fataki, meli za angani au vyombo vinavyoongoza. Mpango huu si matokeo ya bahati tu bila ubuni. Ikiwa tungehesabu kulingana na sayansi, zingekuwako sababu zisizoweza kuhesabika kupinga jambo moja tu linaloelekea kuonyesha kwamba “mpango” huo wenye upatano, wenye utaratibu mkubwa sana, unaotenda kwa ukamilifu ulitokea kwa ajali, kwa bahati tu. Haukuweza kutoka pasipo kitu, kwa maana hakuna jambo lisilotokana na kitu. Wingi wa nguvu zote zenye uhodari kama vile zilivyo katika mpango huu haukuweza hata kidogo kutokana na nafasi iliyo wazi, kutokana na utupu. Kulingana na uwezo wetu wa kuwaza ambao tumejaliwa nao, ulitokana na chanzo kikuu chenye uwezo na nguvu zisizo na mwisho. Na “chanzo” hicho bila shaka ni chenye akili, chenye ujuzi zaidi kuliko kuwa na uwezo wa nguvu zote. Bila shaka ndicho kinachoongoza mpango huo.

3. (a) Inatupasa tukate shauri gani juu ya mwongozi wa “mpango” huu unaoonekana, na ni jina gani linalofaa kwake? (b) Ni jina gani la cheo kama linavyopewa katika Biblia Takatifu?

3 Hatutaki tutende kwa ujinga, sivyo? Yaani, wapumbavu, wasio na akili, wasiofikiri, ambayo maana yake vile vile, ni kutokuwa watu wa kisayansi? Hakuna jambo jinginelo kwa wanadamu wenye kufikiri, wenye akili kuliko kukubali kwamba Mwongozi mkuu wa “mpango” huu wa ajabu wenye uzuri, ubuni na uwezo ni Mtu mwenye akili, ijapokuwa haonekani kwa macho yetu haya yaliyo dhaifu. Je! ye yote ana jina bora la cheo la kumwita Mtu huyo kuliko “Mungu”? Hivyo ndivyo Kitabu ambacho ni Kikubwa Zaidi kuliko vitabu vyote duniani kinavyomwita Mtu huyo. Na kinafanya hivi katika sentensi yenyewe ya kwanza, kikisema: “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.” Katika lugha ya awali ambayo katika hiyo sehemu hii ya Kitabu iliandikwa neno letu la Kiswahili “Mungu” ni Elohimʹ. Kama The Holy Name Bible, inayokataa kabisa jina la cheo “Mungu,” inavyosema sentensi hii katika njia hii: “Katika mwanzo Elohim aliziumba mbingu na dunia.” (Mwa. 1:1) Muumba uyu huyu wa mbingu ndiye mwenye madaraka ya hicho Kitabu cha vitabu vyote, Biblia Takatifu, na tangu mwanzo mpaka mwisho Kitabu hiki chenye zaidi ya kurasa elfu moja kinamfunua Muumba huyu mwenye akili kuwa Mungu wa utendaji mkamilifu, wa hekima, haki, upendo na nguvu kamilifu. Yeye anaweza kabisa kuongoza “mpango” huu unaoonekana.

4, 5. (a) Kulingana na Biblia, dunia hii imetundikwa juu ya nini, na dunia yetu inalinganaje ukubwa na mpango mzima? (b) Ni maulizo gani ambayo Ayubu aliulizwa wanastahili wanasayansi waulizwe?

4 Dunia yetu imetundikwa katika anga pasipo kitu cha namna yenye kuonekana. Kama hicho Kitabu cha vitabu vyote kilivyosema katika masimulizi yake juu ya mzee Ayubu punde kuliko miaka elfu tatu mia tano iliyopita, katika sura ya ishirini na sita, mstari wa saba: “Yeye hutandaza kaskazi juu ya nafasi isiyo na kitu, na [kuitundika dunia] pasipo kitu.” Kulinganisha na jua, mwezi na nyota zisizohesabika, dunia yetu ni kama chembe ndogo tu ya mavumbi katikati ya mavumbi mengi. Kwa kuwa Mungu wa kuumba ndiye anayeongoza au kutawala mpango wote mkubwa, lazima awe tena mtawala wa dunia. Utawala wake, si ule wa viumbe vya kibinadamu duniani, ndio utawala wa kweli, wa awali, wa haki kwa dunia. Imempasa Muumba aongoze kuumba kwake mwenyewe. Mwanadamu hakuiumba dunia hii kama makao yake ya milele. Juu ya jambo hili la maana sana maulizo yale yale yastahili kuulizwa kwa wanasayansi wa kisasa na waalimu wa maendeleo yenye mageuzi kama yalivyoulizwa kwa mzee Ayubu na Mungu kwa habari ya kuumbwa kwa dunia. Kwa Ayubu alisema hivi:

5 “Basi jifunge viuno kama mwanamume, maana nitakuuliza neno, nawe niambie. Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya nchi? Haya! sema, kama ukiwa na ufahamu. Ni nani aliyeamrisha vipimo vyake, kama ukijua? Au ni nani aliyenyosha kamba juu yake? Misingi yake ilikazwa juu ya kitu gani? Au ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni, hapo nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha? . . . Je! umeiamuru asubuhi tangu siku zako zilipoanza? Umeyajulisha mapambazuko mahali pake? Yapate kuishika miisho ya nchi, waovu wakung’utwe wakawe mbali nayo?”​—Ayubu 38:3-13.

6. (a) Ni nani ambao Mungu anasema walishuhudia kuumbwa kwa dunia? (b) Kwa sababu gani sisi hatuna uwezo wa kuhukumu kutamka kwa Mungu kwa miaka 6,000 iliyopita juu ya kazi yake ya kuumba?

6 Katika kujibu maulizo hayo, sisi sote leo ingetupasa tuseme kwa unyenyekevu kwamba hatukuwako. Wale ambao Mungu anawaita hapa “nyota za asubuhi” na “wana wote wa Mungu” walishuhudia kuumbwa kwa dunia na wote walipendezwa na sehemu ndogo hii ya “mpango” unaoonekana. Vema, basi, je! sisi viumbe vidogo vya kibinadamu tunayo sababu yo yote ya kumlaumu Mungu kwa namna alivyoumba makao yetu ya kidunia? Wakati Mungu alipomaliza kuyatayarisha kuwa mahali pa kukaa wanadamu na kuwaweka juu yake, ndipo, kama mstari wa mwisho wa sura ya kwanza ya Biblia Takatifu usemavyo, “Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana.” (Mwa. 1:31) Kwa kuwa Muumba mwenyewe alitazama kuumba kwake kwa kidunia na akaona kuwa “chema sana,” sisi ambao tumetokea ikiisha kupita miaka 6,000 tu nani hata tuseme kwamba hakukuwa “chema sana” kwa maoni yetu ya kibinadamu? Sisi tu nani leo hata tuhukumu ambavyo hali ya dunia ilivyokuwa miaka 6,000 iliyopita wakati Mungu alipomwumba mwanamume na mwanamke wa kwanza katika ukamilifu wa kibinadamu na kuwaweka katika Paradiso ya Furaha? Hali yenye kuchafuka ya dunia leo sio msingi kwa hukumu ya kweli.

7. (a) Ni utawala wa namna gani ambao wanadamu walikuwa nao katika mwanzo wao, lakini wanadamu wamekuwa wakiitawala dunia kwa maoni gani sasa kwa maelfu ya miaka? (b) Ni juu ya ulizo gani juu ya utawala inatupasa sasa tuamue?

7 Sisi tupo hapa kwa ruhusa ya kibali cha Muumba. Sisi tu nani, basi, hata tufikiri kwamba sisi wanadamu tunayo haki ya kuongoza dunia hii kama tupendavyo bila kujali Muumba, Mungu? Hata hivyo ndivyo historia ya kibinadamu inavyoonyesha kwamba wanadamu wamekuwa wakiongoza dunia kwa maelfu ya miaka. Mwanzoni, wakati wa kuumbwa kwa wanadamu, wanadamu walijifurahisha utawala wa kimungu. Leo wanadamu wanapata taabu chini ya utawala wa kibinadamu unaomtupilia Mungu mbali na kupinga utawala wa kimungu. Watawala wa kibinadamu wasiokamilika wanatamani watu wote wautumainie utawala wa kibinadamu tu na kuupinga utawala wa kimungu kama vile wao, watawala wa kibinadamu, wanavyofanya. Kama isivyopata kuwa zamani, ulizo ambalo juu yake inatupasa tufanye uamuzi ni, Utawala wa kimungu​—Je! sisi tunauunga mkono au tunaupinga? Ikiwa tunauunga mkono, una maana gani kwetu sisi? Ikiwa tunaupinga, una maana gani kwetu sisi na kwa wale wanaotutegemea? Na tuone, kwa maana tunatamani kuchagua jambo litakalomaanisha furaha kwetu na kwa wanaotutegemea sisi.

MWENDO WA WALE WANAOUPINGA

8. (a) Wale waliopo duniani wanaoupinga utawala wa kimungu wanao nani upande wao? (b) Wanalazimishwa kukubali nini juu ya kama kulikuwako sikuzote uadui kwa utawala wa kimungu ama sivyo?

8 Wale ambao leo wanaupinga utawala wa kimungu, yaani, utawala wa Mungu wa dunia wanao watu wengi upande wao. Inaelekea wanao watu wengi zaidi kuliko wanavyojua. Inaelekea upande wao wanao wale ambao hawapendi kuwakubali kama wako upande wao na kushirikiana nao. Tunamaanisha nini? Kwa sababu wao ni watu wenye kusadiki tu mambo yanayoonekana katika filosofia yao, wanakataa kukubali kwamba kuna kitu cho chote ambacho ni cha kiroho, hata kukana kwamba kuna Mungu, ambaye ni Roho. Kwa vyo vyote hawamfikirii Mungu sana, wala kuwako kwa mtu mwingine ye yote wa kiroho mwenye akili. Kwa kweli hawana msingi wenye akili kwa kuwa na maoni haya ya moyoni; hata hivyo wanayafuata sana kwa kujipumbaza wenyewe wasione mambo ya hakika ya wazi. Walakini, itawapasa wakubali kwamba uadui huu kwa utawala wa kimungu ulikuwa una mwanzo. Kuna historia inayohakikisha kwamba ulikuwa na mwanzo wake miaka 6,000 iliyopita. Haukuanzia na mwanadamu, bali mwanadamu alijitia ndani yake.

9. (a) Kupinga utawala wa kimungu kulianzia na nani, na ni taabu ya nani kutoka kwake iliyoonyesha kuwako kwa mtu huyo? (h) Ayubu aliunga mkono utawala wa nani, na hivyo Shetani alitamani kujaribu nini juu ya Ayubu?

9 Basi, uadui kwa utawala wa kimungu ulianzia na nani? Haukuanzia na kiumbe kidogo sana, kama nyoka, bali na kiumbe kisicho cha kibinadamu, mmoja wa wale ambao Mungu alimwambia mzee Ayubu kama wakiwa “wana wote wa Mungu.” (Ayubu 38:7) Ayubu alipata taabu sana na mwanzishi huyu wa uadui kwa utawala wa kimungu. Ayubu alipashwa habari kwamba jina la huyu alikuwa Shetani. Katika usemi wa Ayubu jina Shetani lilikuwa sawa na kusema “Mpinzani.” Lakini “Mpinzani” wa nani? Wa Mungu, bila shaka! Ayubu alipendelea utawala wa kimungu. Shetani alionyesha kwamba upinzani wake ulikuwa juu ya Mungu kwa kujaribu kumharibu Ayubu kwa sababu ya kuunga mkono utawala wa Mungu. Shetani hakuwa mtu wa kuwazika tu kwa Ayubu kama asivyokuwa mtu wa kuwazika tu kwa Mungu mwenyewe. Wakati taabu ya Ayubu ilipomalizika, Mungu alimfunulia Ayubu nani aliyekuwa mwenye madaraka kwa mateso na majaribu yake. Alikuwa huyu Shetani. Shetani alikuwa amejitokeza wakati wa mkutano wa “wana wote wa Mungu” mbinguni. Huko alimwomba Mungu aondoe ulinzi wake juu ya Ayubu na kumwacha amjaribu Ayubu juu ya uaminifu wake kwa utawala wa kimungu.

10. Ni jambo gani ambalo Shetani alidai kwamba, akiruhusiwa, angeweza kumfanya Ayubu alifanye, na Yakobo 5:11 anaonyesha nini kama Ayubu alishindwa?

10 Shetani alidai kwamba, akiruhusiwa, yeye angeweza kumfanya Ayubu amtukane Mungu mbele za uso wake mwenyewe. Hii ilikuwa zamani katika karne ya kumi na saba mbele ya Wakati wetu wa Kawaida. Jaribu la uvumilivu na uaminifu wa Ayubu liliandikwa katika kitabu cha Ayubu ili sisi tusome. Je! Shetani aliweza kumlazimisha Ayubu kuingia katika kundi la wapinzani wa Mungu na la kupinga utawala wa kimungu? Zaidi ya karne kumi na sita zilizofuata mwanafunzi wa Kikristo Yakobo ndugu mzazi mmoja na Yesu Kristo aliandika juu ya hili na kusema: “Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa [Yehova] ya kwamba [Yehova] ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.”​—Yak. 5:11.

11. Habari inaonyeshaje kwamba Mungu alimshinda Shetani kwa vile Ayubu hakumkufuru Mungu mbele za uso wake?

11 Kwa habari ya Ayubu, Yehova Mungu alimshinda Shetani, kwa maana Shetani alionekana kuwa mwongo. Namna gani? Wakati Shetani alipoleta majaribu juu ya Ayubu, tunasoma, “katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi, wala hakumwazia Mungu kwa upumbavu.” Wakati hali ya Ayubu ilipoonekana kuwa mbaya sana na mke wake asimtumaini tena, alimwambia hivi: “Je! wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? umkufuru Mungu, ukafe.” Lakini Ayubu alimwambia hivi: “Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya?” Kwa sababu hiyo maandishi yanasema hivi: “Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.” Kwa kumaliza, wakati Mungu hajageuza hali ya Ayubu, aliwaambia washtaki watatu wanafiki wa Ayubu hivi: “Hasira zangu zinawaka juu yako, na juu ya hao rafiki zako wawili; kwa kuwa ninyi hamkunena yaliyo sawa katika habari zangu, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu.” (Ayubu 1:1-22; 2:9, 10; 42:7, 8) Kwa kweli, jambo hili lilionekana kuwa kemeo kwa Shetani, naye alionyeshwa wazi kama mchongezi au Ibilisi.

12. Ulikuwa muda gani mbele ya wakati wa Ayubu na mahali gani ambapo ulizo juu ya utawala wa kimungu lilipotokezwa, na kwa matokeo gani kwa siku ya saba au Sabato ya Mungu ya uumbaji?

12 Ndivyo mtu huyu wa historia, Ayubu wa nchi ya Usi, alivyoendelea kuwa mwaminifu kwa Yehova kama Mungu Mwenye Zote. Ayubu aliunga mkono utawala wa kimungu. Walakini, ilikuwa zaidi ya miaka 2,400 mbele ya jaribu la Ayubu kwamba Shetani Ibilisi akatokeza ulizo juu ya utawala wa kimungu. Hii ilikuwa mara Muumba, Yehova Mungu, alipokuwa amepanda Bustani ya Edeni mamia fulani ya maili kuelekea upande wa mashariki ya kaskazini ya mahali pa nchi ya Usi. Yehova alikuwa amemweka mwanamume na mwanamke wa kwanza katika hiyo Paradiso ya Furaha ili waishi na kutumikia chini ya utawala wa kimungu. Wakati huo ilikuwa kama mwanzo wa siku ya saba ya uumbaji wa Yehova, kama mwaka wa 4026 B.C.E., au karibu miaka 6,000 iliyopita. (Mwa. 1:28 mpaka 2:3) Je! siku hii ya saba ya uumbaji, hii Siku ya Sabato kuu kwa Yehova juu ya kuumba kwa kidunia, iliendelea kuwa tulivu, na viumbe vyote mbinguni na duniani vikinyenyekea kwa uaminifu utawala wa kimungu? Yale yanayotupata sisi wenyewe leo na vile vile historia ya kidunia kwa miaka 6,000 iliyopita yanajibu Hapana. Utulivu wa hii Siku ya Sabato kuu ya Yehova ulianza kuchafuliwa karibu tangu mwanzo wake wenyewe.

13. “Mwana wa Mungu” wa kimbinguni alijifanyia shawishi namna gani, na lilimvutia katika mwendo gani?

13 Wakati huo wenye maana sana mmoja wa hao “wana wote wa Mungu” mbinguni aliyekuwa ameshuhudia kuumba kwa Yehova kwa mwanamume na mwanamke katika Bustani ya Edeni aliacha tamaa ya kichoyo iingie katika moyo wake na kuiacha imvute na kumwongoa katika utawala wa kimungu. Yeye alianza kuona wivu juu ya utawala wa Mungu wa haki juu ya wanadamu hawa wawili ambao Mungu aliamuru wazae jamaa kubwa na kuijaza dunia yote, wakati uo huo kueneza Paradiso katika Edeni kwenye miisho yenyewe ya dunia. (Mwa. 1:26-28) Huyu “mwana wa Mungu” wa kimbinguni sasa akaja chini ya shawishi la kujifanyia mwenyewe na akatamani kuwa na utawala huo juu ya wanadamu wa kwanza wawili na jamaa yao ambayo wangejaza dunia kwayo. Yeye alisitawisha tamaa hii ya kichoyo mpaka ikachukua mimba ikazaa dhambi. Dhambi hiyo ikawa ndio mwanzo wake wa kumpinga Mtawala wa Kimungu aliye juu ya wote, Mungu Yehova Aliye Juu kuliko wote na Mwenye Nguvu Zote. Katika njia hii huyu “mwana wa Mungu” wa kimbinguni alijigeuza mwenyewe akawa Shetani au Mpinzani. Mungu hakuwa wa kulaumiwa hata kidogo kwa sababu ya hili kana kwamba akimshawishi ye yote mbinguni au duniani afanye ubaya, uovu.​—Yak. 1:13-15.

14. Katika Edeni Shetani alifanyaje tofauti na alivyofanya penye mkutano wa “wana wote wa Mungu” mbele za Yehova, na alimfanya Hawa amsikilize namna gani?

14 Hakuna kukusanyika kwa wana wa Mungu wa kimbinguni mbele za Yehova Mungu kunakosemwa kuwa kulitukia katika Bustani ya Edeni wakati huo. Wala Shetani hakufunua yaliyokuwa katika moyo wake na, kama katika habari ya Ayubu, kumwomba Mtawala Mkuu kupita wote Yehova aondoe ulinzi wake kwa Adamu na Hawa katika Bustani ya Edeni. Kwa kuwa wakati huo kulikuwa hakuna uovu katika makao yote ya kuwako, kulikuwa hakuna kitu ambacho juu yake wanadamu hawa wawili wa kwanza walipaswa walindwe. Basi haikuwa lazima kwa Shetani kumwomba Yehova amfungulie njia ya kuwafikia Adamu na Hawa na kuwajaribu na kuwafanya raia hawa wa kibinadamu wa kidunia wa utawala wa kimungu watende dhambi juu ya Mungu. Akiisha kuvutwa na shawishi lake mwenyewe, aliendelea kujifanya mwenyewe Mshawishi Mkuu kwa kuweka shawishi katika njia ya Adamu na Hawa. Bila kufunua kusudi lake la kichoyo kwa wana wengine wa kimbinguni wa Mungu, kwa kunyetea alijisingizia na kwa udanganyifu akamtumia nyoka katika Bustani ya Edeni kama mjumbe wake mwenye kuonekana kama hadhuru ili atege mtego. Mwanamke Hawa, ingawa kukamilika kwake kwa kibinadamu, hakujua kwamba kiumbe cha kiroho kisichoonekana, Shetani, alikuwa akimtumia nyoka ili ionekane kama ndiye anayesema ili amshawishi. Basi, mahali pa kukataa kusikiliza, yeye alisikiliza.

15. Shetani alijigeuzaje kuwa Ibilisi, na alimwongoza Hawa aende katika mwendo gani?

15 Kwa njia ya nyoka, mwana wa Mungu mhaini, Shetani, alianzia katika sheria ya Mungu juu ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, kana kwamba Mungu alikuwa akitumia vibaya utawala wake wa kimungu. Sasa Shetani akajigeuza mwenyewe kuwa Ibilisi, ambayo maana yake ni Mchongezi, kwa kumwita Mungu mwongo ambaye hakuweza kufikiliza adhabu kwa kuvunja sheria yake juu ya kula tunda lililokatazwa. Je! Hawa angekufa kama angepinga utawala wa kimungu na kutumia utawala wa kibinadamu? Hasha! akasema Shetani Ibilisi kupitia kwa nyoka. “Hakika hamtakufa, kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.” Hawa hakuweza kumwona Shetani Ibilisi kama sisi leo tusivyoweza kumwona kwa macho yetu ya asili. Sasa akiacha tamaa ya kichoyo ambayo imefanyika sasa hivi kwa kitu kilichokatazwa imvute na kumshawishi, yeye alizaa dhambi ya kibinadamu kwa kuutilia shaka utawala wa kimungu na kuvunja sheria ya kimungu. Shetani Ibilisi alijua kwamba jambo lifuatalo Hawa mkosaji angejaribu kumshawishi mume wake kichwa, Adamu, ale pamoja naye tunda lililokatazwa.​—Mwa. 3:1-6.

16. Adamu alipataje tunda lililokatazwa, na alifanya uamuzi juu ya ulizo gani la msingi, kwa matokeo juu ya nani?

16 Hawa alitaka mtu wa kujiunga naye katika kosa. Alitamani mume wake ajiunge naye. Mume hakuchuma tunda lo lote kutoka kwa mti uliokatazwa kwa shauri la mke wake, ila mke wake ndiye aliyetoa tunda kwake. Sauti yake ikawa yenye kuomba sana, ikimshawishi ashiriki pamoja naye katika kula tunda lililokatazwa. Kwa kudanganywa, yeye hakufikiri ingemwua kufanya hivyo. Uamuzi unaopasa jamaa nzima ya kibinadamu sasa ukawa wa Adamu kufanya. Ilimpasa afanye uamuzi, si kwa ajili yake mwenyewe tu, bali kwa ajili ya watoto wake wasiozaliwa bado waliokuwa viunoni mwake. Alikutana na ulizo kubwa, Utawala wa kimungu​—Je! mimi ninauunga mkono au naupinga? Mahali pa kuisikiliza sauti ya Baba yake wa kimbinguni ya kuonya juu ya matokeo yenye hatari ya kula tunda lililokatazwa, Adamu aliisikiliza sauti yenye kushawishi ya mke wake. Yeye hakuchagua kumwonyesha yule “nyoka” kuwa mwongo na Mungu kuwa wa kweli. Bali, yeye alichagua kumpendeza mke wake. Alikubali tunda lililokatazwa mkononi mwake.​—Mwa. 3:6, 12, 17.

WANADAMU WANALETWA CHINI YA UTAWALA WA MASHETANI

17, 18. (a) Adamu aliamua kwa ajili ya utawala wa nani, naye alijipanga upande wa nani? (b) Mtume Yohana anachanganuaje utawala wa nani ambao mzaliwa wa kwanza wa Adamu alikuwa chini yake?

17 Hapa upinzani wa utawala wa kimungu duniani ulianza. Adamu, kichwa cha kidunia cha jamaa ya kibinadamu, aliamua kwa ajili ya jambo jinginelo, ingawa inaelekea kuwa hakujua wakati huo. Kama Hawa mke wake, hakumwona Shetani Ibilisi kwa macho yake ya asili kama nguvu iliyokuwa ikimwongoza yule “nyoka” asemaye, bali, vile vile, Adamu alikuwa akiamua kwa ajili ya utawala wa Shetani katika kuupinga utawala wa kimungu. Adamu na Hawa sasa wakawa upande wa Shetani Ibilisi​—katika kuupinga utawala wa kimungu, utawala wa kitheokrasi. Ndiyo sababu Adamu na Hawa walifukuzwa kutoka katika Paradiso ya Furaha, wazae watoto wao nje katika ardhi ambayo Mungu alilaani. Mtoto wao wa kiume wa kwanza, Kaini, alionyesha alikuwa chini ya utawala wa nani wakati alipomwua Habili ndugu yake mtu mwenye kumwogopa Mungu. (Mwa. 3:17 mpaka 4:16) Katika kusema juu ya hili mtume Yohana anaandika hivi:

18 “Huu ndio ujumbe ambao mmesikia kutoka mwanzo, kwamba imetupasa tuwe na upendo kwa mmoja na mwenzake; si kama Kaini, aliyetokana na mwovu na akamwua ndugu yake. Na ni kwa ajili gani alimwua? Kwa sababu kazi zake mwenyewe zilikuwa za uovu, lakini zile za ndugu yake zilikuwa za haki.”​—1 Yohana 3:11, 12, NW.

19. Kama alivyokuwa Kaini, wanadamu leo wanaonyeshaje kwamba hawaunyenyekei utawala wa kimungu?

19 Yote haya yanaonyesha matokeo mazito yanayotokana na kuupinga utawala wa kimungu. Je! leo tunaona ndugu akimwua ndugu yake? Hakuna mtu ambaye anaweza kukana kwamba hatuoni mauaji hayo yakitukia kwa kadiri iliyo kubwa mno, zaidi wakati vinapotokea vita vya ulimwengu. Labda watu ambao ni wenye hekima ya ulimwengu huu wa sasa watasema kwamba Shetani Ibilisi hayumo katika shauri hili. Lakini tunayo habari kutoka kwenye vyanzo vyenye kutumainika zaidi kuliko kutoka kwa watu hawa wenye kufuata maoni yao wenyewe. Wenye kuchukia ndugu zao na wauaji wa ndugu zao leo wanatokana na mwovu yule yule sasa kama walivyokuwa katika siku za Kaini na Habili, lakini sasa wako zaidi kuliko walivyokuwa katika karne ya kwanza ya jamaa ya kibinadamu duniani. Ndiyo, na zaidi kuliko katika karne ya kwanza ya Ukristo, wakati mtume Yohana alipoandika maneno hayo yaliyotangulia juu ya upendo wa ndugu na kumchukia ndugu. Kwa hiyo, kuna ushuhuda wenye nguvu kwamba leo wanadamu hawako chini ya utawala wa kibinadamu tu bali, bila kujulikana kwao, vile vile wako chini ya utawala wa Kishetani. Kuongezeka kwa kukosa upendo wa ndugu kunaonyesha kwamba wanadamu hawanyenyekei utawala wa kimungu. “Mungu ni upendo,” ndivyo tunavyosoma katika 1 Yohana 4:8, 16.

20. Ni katika siku za nani kulitokea mtengano katika utawala wa Shetani juu ya wanadamu, na ni watu gani kufika kwake walioupendelea utawala wa kimungu?

20 Tangu siku ambayo Adamu na Hawa walipoanza kuupinga utawala wa kimungu mpaka sasa, kumekuwako mtengano mmoja tu wa muda katika utawala wa Kishetani juu ya wanadamu. Hii ilikuwa katika siku za mzee Nuhu, mtu wa kumi katika mstari wa kutoka kwa Adamu. Mbele ya Nuhu, shahidi mwaminifu Habili alikuwa ameunga mkono utawala wa Mungu ambaye aliabudu. Tena, nabii Henoko, mtu wa saba katika mstari wa kutoka kwa Adamu, aliunga mkono utawala wa kimungu. Kwa wazi ili Henoko asipate kuuawa na wapinzani wasiomwabudu Mungu, Yehova Mungu alimwondoa kwa mwujiza katika dunia wakati alipokuwa mwenye umri wa miaka 365 tu. (Mwa. 5:18-24; Ebr. 11:4, 5; Yuda 14, 15) Nuhu aliunga mkono utawala wa nani inaonekana wazi kutokana na habari iliyomo katika Mwanzo 6:9, inayosomwa hivi: “Hivi ndivyo vizazi vya Nuhu. Nuhu alikuwa mtu wa haki, mkamilifu katika vizazi vyake; Nuhu alikwenda pamoja na Mungu.”

21. (a) Ni kwa msaada wa unabii gani wa Yesu tutafanya vema kuangalia hali iliyokuwako katika siku za Nuhu? (b) Habari katika Mwanzo inaonyeshaje kwamba utawala wa kimungu haukukubaliwa katika siku za Nuhu zilizotangulia gharika?

21 Sisi leo tutafanya vema ikiwa tunaangalia hali ya ulimwengu iliyokuwa katika siku za Nuhu mpaka mwaka wake wa umri wa mia sita. Kwa sababu gani? Kwa sababu Yesu Kristo katika unabii wake juu ya hali za ulimwengu wakati wa “mwisho wa taratibu ya mambo” alisema maneno haya yenye maana: “Kama vile ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu. Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika . . . wasitambue, hata Gharika ikaja, ikawachukua wote, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.” (Mt. 24:3, 37-39) Zaidi ya kula, kunywa na kuoa na kuolewa mambo yaliyokuwa yakifanyika katika siku hizo mbele ya Gharika, kulikuwako hali iliyomtaka Muumba ailete Gharika hiyo yenye kuenea dunia yote. Ilikuwa ile iliyosimuliwa katika Mwanzo 6:11, 13, ambapo tunasoma hivi: “Dunia ikaharibika mbele za Mungu, dunia ikajaa dhuluma. Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia.” Kwa hakika, basi, utawala wa kimungu haukukubaliwa.

22, 23. (a) Katika siku zilizotangulia Gharika, utawala wa Shetani ulipataje mkazo zaidi kukamatana na ‘‘kuolewa” kwa wanawake? (b) Ilionekana wazi namna gani kwamba watoto wa Kinefili wa ndoa zenye mchanganyiko wa malaika na wanadamu hawakuwa wenye msaada wa adili kwa wanadamu?

22 Katika siku hizo mbele ya Gharika, utawala wa Kishetani juu ya jamaa ya kibinadamu ulipata mkazo zaidi. Namna gani? Basi, katika habari ya Yesu juu ya siku za Nuhu alisema juu ya “kuolewa” kwa wanawake. (Mt. 24:38) Kati ya wanawake hao walioolewa wakati huo walikuwako wanawake wengi waliochukuliwa na watu ambao Mwanzo 6:4 unawaita “wana wa Mungu.” Walikuwa ‘wana wa Mungu’ wa kimbinguni, kama Shetani Ibilisi wakati mmoja alivyokuwa, lakini walishawishwa washuke na kuanza kuishi duniani kwa sababu ya binti za wanadamu “wazuri,” waliopatikana kwa kuolewa.

23 Basi hawa “wana wa Mungu” wa kimbinguni walijivika miili kama wanadamu “Wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.” Labda, kila mtu akiwa na zaidi ya mke mmoja. Kati ya watoto wa ndoa hizo za mchanganyiko wa malaika na wanadamu walikuwako wale ambao Biblia inawaita Wanefili, ambayo maana yake “Wangushaji,” yaani, wale wanaoangusha mtu au kitu fulani kwa nguvu. “Waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa.” (Mwa. 6:1-4) Kwa wazi majitu hayo ya Kinefili au Waangushaji hawakuwa wenye msaada wo wote wa adili kwa jamaa safi ya kibinadamu, kwa maana kufuata hapo Biblia inaarifu kwamba dunia ilikuwa ikiharibika na ilikuwa ikiharibiwa kwa dhuluma. Hii inaonyesha kabisa kwamba hao “wana wa Mungu” wa kimalaika walikuwa wametenda dhambi katika kuoa “binti za wanadamu” kwa kutosheleza nyege.

24. (a) Je! ‘wana hao wa Mungu’ wenye kuoa walifanya dhambi, na walijipanga upande wa nani (b) Wakati wa Gharika, jambo gani liliwapata Wanefili, na ‘wana wa Mungu’ waliooa walilazimishwa kufanya nini?

24 Kwamba wana hao wa Mungu wa kimbinguni walifanya dhambi kwa kuacha sehemu yao ya kiroho isiyoonekana na makao yao wenyewe yanayofaa katika utumishi wa mbinguni wa Mungu inasemwa kwa uhakika katika Biblia. (1 Pet. 3:19, 20; 2 Pet. 2:4, 5; Yuda 6) Hii inawaweka kabisa katika kuupinga utawala wa kimungu mwote mbinguni na duniani. Hiyo inawaweka upande wa utawala wa Kishetani na chini yake. Watoto wao majitu, Wanefili, hawakuokolewa katika gharika ya dunia yote; hakuna hata mmoja wao aliyeingizwa katika safina kuu ambayo Nuhu na wana wake watatu walijenga. Wakiwa wanadamu kwa sababu ya mama zao za kibinadamu, walikufa maji katika Gharika, pamoja na jamaa zao za kidunia. Baba zao za kimalaika walivua miili ya kibinadamu na pasipo kutaka, kwa lazima, wakatoweka katika makao ya kiroho. Huko ndiko ilikowapasa wajiunge na Shetani Ibilisi kama mtawala wao.

25. Na kwa njia hiyo kukatizwa kwa utawala wa Shetani kulitokezwaje, na wanadamu walipata mwanzo mpya chini ya nini?

25 Gharika ya dunia yote ilikatiza utawala wa Kishetani juu ya jamaa ya kibinadamu. Nuhu na mke wake na watoto wao watatu na wakwe zao watatu, ndani ya safina wakati wa Gharika, wote waliunga mkono utawala wa kimungu. Waliokoka ule uharibifu mkubwa wa gharika ya dunia yote, lakini wote wale waliokuwa wakiupinga utawala wa kimungu walikufa maji katika gharika. Kwa hiyo, wakati Nuhu na waokokaji wenzake walipotoka katika safina kuja katika dunia iliyo safi, tena jamaa ya kibinadamu ikawa chini ya utawala wa kimungu. Kwa ushuhuda wa uhakika huo Yehova Mungu kama Mtawala wa Kimungu alimwambia Nuhu na jamaa yake wafanye jambo ambalo alikuwa amewaambia Adamu na Hawa katika Edeni wafanye, kujaza dunia na watoto wao, wakiwa chini ya sheria fulani za kimungu zilizosemwa. (Mwa. 6:13 mpaka 9:7) Ndivyo wanadamu walivyopata mwanzo wa pili chini ya utawala wa kimungu.

26. Kwa kupatana, kwa sababu gani isingefaa Mungu awe mwenye kujali kidogo juu ya hali za kidunia leo, na twajuaje kama atafanya jambo fulani juu ya hili kama katika siku za Nuhu?

26 Ikiwa kuharibika kwa dunia na kuijaza na dhuluma katika siku za Nuhu mbele ya gharika kulistahili kutajwa katika Biblia Takatifu, bila shaka kuharibika kukubwa zaidi kwa dunia na kuijaza na dhuluma yenye kuenea zaidi mahali pote katika karne hii ya ishirini vinafaa kutajwa. Je! Mungu Muumba anajali kidogo hali hii ya sasa ya ulimwengu ambayo ni mbaya zaidi kuliko alivyojali ile ya wakati wa Nuhu? Kwa kupatana sana imempasa awe mwenye kujali zaidi kuliko wakati huo na kwa hiyo kumlazimu kufanya jambo fulani juu ya hali hiyo kama Muumba wa mbingu na dunia. Yesu Kristo Mwana mwaminifu wa Mungu alitoa unabii kwamba Mungu angefanya hivyo.

[Picha katika ukurasa wa 206]

Watu waliokuwa mbele ya Gharika waliendelea kula, kunywa na kuoa na kuolewa, “wasitambue, hata Gharika ikaja” ikawaangamiza wale wote waliopuza utawala wa kimungu. “Ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu.”​—Luka 17:26, 27

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki