Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Tanzanian sign language publications (2020-2026)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Jumatano, Aprili 15

Mpendane.—Yoh. 15:12.

Watu wa Yehova wanapenda kusaidiana. (2 Kor. 8:4) Hata hivyo, nyakati nyingine tunahitaji ujasiri ili kufanya hivyo. Kwa mfano, vita vinapotokea, wazee wa kutaniko wanatambua kwamba ndugu na dada zao wanahitaji kutiwa moyo, kutegemezwa, na labda kupewa Biblia na machapisho yetu au mahitaji ya kimwili. Kwa sababu wanawapenda kondoo, wazee wanahatarisha uhai wao ili kuwaandalia ndugu na dada mahitaji yao. Katika hali kama hizo, ni muhimu tudumishe umoja. Unga mkono mwongozo unaotoka kwenye ofisi yenu ya tawi. (Ebr. 13:17) Wazee wanapaswa kupitia kwa ukawaida mipango ya kutaniko lao ya kujitayarisha kwa ajili ya majanga, pamoja na miongozo ya tengenezo kuhusu mambo ya kufanya majanga yanapotokea. (1 Kor. 14: 33, 40) Uwe jasiri lakini mwenye tahadhari. (Met. 22:3) Fikiri kabla ya kutenda. Usihatarishe uhai wako isivyo lazima. Mtegemee Yehova. Anaweza kukusaidia ili uwapatie ndugu zako msaada kwa njia iliyo salama. w24.07 27:8, 11

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026

Alhamisi, Aprili 16

Katika taabu yangu nilimwita Yehova, . . . na kilio changu cha kumwomba msaada kilifika masikioni mwake.—Zab. 18:6.

Mfalme Daudi alimjua Yehova na alimtegemea. Maadui wake, kutia ndani Mfalme Sauli, walipojaribu kumuua, Daudi alisali kwa Yehova ili kupata msaada. Baada ya Mungu kujibu sala yake na kumwokoa, Daudi alisema hivi: “Yehova yuko hai!” (Zab. 18:46) Daudi alipotumia maneno hayo, hakuwa akikubali tu kwamba Mungu yuko. Kitabu kimoja cha marejeo kinasema kwamba Daudi alikuwa akionyesha uhakika wake katika Yehova “akiwa mungu aliye hai ambaye sikuzote hutenda kwa niaba ya watu wake.” Naam, Daudi alijua kutokana na mambo aliyojionea maishani kwamba Mungu wake alikuwa hai, na uhakika huo ulichochea upya azimio lake la kumtumikia na kumsifu Yehova. (Zab. 18:​28, 29, 49) Kuwa na uhakika kwamba Yehova ndiye Mungu aliye hai kunaweza kutusaidia kumtumikia kwa bidii. Tutakuwa na nguvu za kuvumilia majaribu na kichocheo cha kuendelea kufanya kazi kwa bidii katika utumishi wake. Pia, tutaazimia kuendelea kuwa karibu na Yehova. w24.06 25:3-4

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026

Ijumaa, Aprili 17

Msiruhusu mtu yeyote awapotoshe kwa njia yoyote.—2 The. 2:3.

Tunaweza kujifunza nini kutokana na maneno ya Paulo kwa Wathesalonike? Tunaposikia jambo fulani ambalo halipatani na kile ambacho tumejifunza katika Biblia, au uvumi fulani wenye kusisimua, tunahitaji kutumia utambuzi. Katika Muungano wa Sovieti, pindi moja maadui wetu walisambaza barua ambayo ilionekana imetoka makao makuu ya ulimwenguni pote. Barua hiyo iliwatia moyo baadhi ya akina ndugu wajitenge, na kuunda tengenezo linalojitegemea. Barua hiyo ilionekana kuwa ya kweli. Lakini ndugu waaminifu hawakudanganywa. Walitambua kwamba ujumbe wa barua hiyo haukupatana na mambo ambayo walikuwa wamefundishwa. Leo, maadui wa ile kweli wanatumia Intaneti na mitandao ya kijamii ili kutuvuruga na kutugawanya. Badala ya ‘kutikiswa upesi kutoka kwenye kufikiri kwetu,’ tunaweza kujilinda kwa kuchunguza kwa makini ikiwa mambo tunayosikia au kusoma yanapatana na kweli ambazo tayari tumejifunza.—2 The. 2:2; 1 Yoh. 4:1. w24.07 28:14-15

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki