Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
Tanzanian sign language publications (2020-2026)
Toka
Ingia
Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Leo

Alhamisi, Aprili 16

Katika taabu yangu nilimwita Yehova, . . . na kilio changu cha kumwomba msaada kilifika masikioni mwake.—Zab. 18:6.

Mfalme Daudi alimjua Yehova na alimtegemea. Maadui wake, kutia ndani Mfalme Sauli, walipojaribu kumuua, Daudi alisali kwa Yehova ili kupata msaada. Baada ya Mungu kujibu sala yake na kumwokoa, Daudi alisema hivi: “Yehova yuko hai!” (Zab. 18:46) Daudi alipotumia maneno hayo, hakuwa akikubali tu kwamba Mungu yuko. Kitabu kimoja cha marejeo kinasema kwamba Daudi alikuwa akionyesha uhakika wake katika Yehova “akiwa mungu aliye hai ambaye sikuzote hutenda kwa niaba ya watu wake.” Naam, Daudi alijua kutokana na mambo aliyojionea maishani kwamba Mungu wake alikuwa hai, na uhakika huo ulichochea upya azimio lake la kumtumikia na kumsifu Yehova. (Zab. 18:​28, 29, 49) Kuwa na uhakika kwamba Yehova ndiye Mungu aliye hai kunaweza kutusaidia kumtumikia kwa bidii. Tutakuwa na nguvu za kuvumilia majaribu na kichocheo cha kuendelea kufanya kazi kwa bidii katika utumishi wake. Pia, tutaazimia kuendelea kuwa karibu na Yehova. w24.06 25:3-4

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026

Ijumaa, Aprili 17

Msiruhusu mtu yeyote awapotoshe kwa njia yoyote.—2 The. 2:3.

Tunaweza kujifunza nini kutokana na maneno ya Paulo kwa Wathesalonike? Tunaposikia jambo fulani ambalo halipatani na kile ambacho tumejifunza katika Biblia, au uvumi fulani wenye kusisimua, tunahitaji kutumia utambuzi. Katika Muungano wa Sovieti, pindi moja maadui wetu walisambaza barua ambayo ilionekana imetoka makao makuu ya ulimwenguni pote. Barua hiyo iliwatia moyo baadhi ya akina ndugu wajitenge, na kuunda tengenezo linalojitegemea. Barua hiyo ilionekana kuwa ya kweli. Lakini ndugu waaminifu hawakudanganywa. Walitambua kwamba ujumbe wa barua hiyo haukupatana na mambo ambayo walikuwa wamefundishwa. Leo, maadui wa ile kweli wanatumia Intaneti na mitandao ya kijamii ili kutuvuruga na kutugawanya. Badala ya ‘kutikiswa upesi kutoka kwenye kufikiri kwetu,’ tunaweza kujilinda kwa kuchunguza kwa makini ikiwa mambo tunayosikia au kusoma yanapatana na kweli ambazo tayari tumejifunza.—2 The. 2:2; 1 Yoh. 4:1. w24.07 28:14-15

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026

Jumamosi, Aprili 18

Yeyote akitenda dhambi, tuna msaidizi.—1 Yoh. 2:1.

Uamuzi muhimu zaidi ambao mtu anaweza kufanya ni kujiweka wakfu kwa Yehova na kuwa sehemu ya familia ya waabudu Wake. Yehova anataka kila mtu afanye hivyo. Kwa nini? Anataka wafurahie urafiki pamoja naye na waishi milele. (Kum. 30:​19, 20; Gal. 6:​7, 8) Hata hivyo, Yehova hamlazimishi mtu yeyote amtumikie. Anamruhusu kila mtu aamue kile atakachofanya. Namna gani ikiwa Mkristo aliyebatizwa anavunja sheria ya Mungu, na kutenda dhambi nzito? Ikiwa hatatubu, ni lazima aondolewe kutanikoni. (1 Kor. 5:13) Lakini hata ikiwa mtu huyo anaondolewa kutanikoni, bado Yehova anataka sana mtu huyo atubu na kumrudia Yeye. Kwa kweli, hiyo ndiyo sababu muhimu iliyofanya aandae fidia—ili mtenda dhambi anayetubu aweze kupata msamaha. Mungu wetu mwenye upendo anawahimiza wale waliotenda dhambi nzito watubu.—Zek. 1:3; Rom. 2:4; Yak. 4:8. w24.08 33:1-2

Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2026
Karibu
Hiki ni kifaa cha utafiti katika machapisho ya Mashahidi wa Yehova ya lugha mbalimbali.
Ikiwa ungependa kupakua machapisho, tafadhali tumia anwani jw.org.
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki