Mwezi wa 4
Siku ya Tatu, 1 Mwezi wa 4
Haya ndiyo mapenzi ya Baba yangu, kwamba kila mutu mwenye anakubali Mwana na kumuamini akuwe na uzima wa milele.—Yoh. 6:40.
Juu mwili na damu ya Yesu ituletee faida tunapaswa kuonyesha imani katika bei ya ukombozi. (Efe. 1:7) Wale wenye Yesu aliita “kondoo wengine” hawapaswe kula mukate na kunywa divai wakati wa Ukumbusho, tukio yenye tunafanya kila mwaka. (Yoh. 10:16) Wanakula mwili na damu ya Yesu mu njia ya mufano. Wanafanya vile kwa kuonyesha imani katika zabihu ya ukombozi ya Yesu na baraka zote zenye tutapata kupitia ile zabihu. (Yoh. 6:53) Lakini, wenye wanakula mukate na divai wanaonyesha kama wako katika agano jipya na wako na tumaini ya kutawala pamoya na Yesu mbinguni katika Ufalme. Kwa hiyo, ikuwe tuko watiwa-mafuta ao kondoo wengine, ni jambo ya maana sana tuonyeshe imani ili tupate uzima wa milele. w24.12 12-13 fu. 14, 16
Usomaji wa Biblia kwa ajili ya Ukumbusho: (Mambo yenye ilitokea muchana: Nisani 12) Matayo 26:1-5, 14-16; Luka 22:1-6
TAREHE YA UKUMBUSHO
Kisha Jua Kushuka
Siku ya Ine, 2 Mwezi wa 4
Musiogope, kundi ndogo, kwa maana Baba yenu amekubali kuwapatia ninyi Ufalme.—Lu. 12:32.
Wakati ya Chakula cha Mangaribi cha Bwana, Yesu alipatia mitume wake mukate wenye hauna chachu na kuwaambia kama ule mukate unafananisha mwili wake. Kisha akawapatia divai na kusema kama inafananisha “damu ya agano.” (Mk. 14:22-25; Lu. 22:20; 1 Ko. 11:24) Agano jipya ilifanywa tu na “nyumba ya Israeli [ya kiroho]” wenye watakuwa “katika Ufalme wa Mungu.” (Ebr. 8:6, 10; 9:15) Wakati wa Chakula cha Mangaribi cha Bwana, Yesu alikuwa nazungumuzia “kundi ndogo.” Mitume wenye walikuwa na Yesu mu ile nyumba wakati alianzisha Chakula cha Mangaribi cha Bwana, njo walikuwa wa kwanza mu ile kundi ndogo. Wao njo watatawala mbinguni pamoya na Yesu. w24.12 11 fu. 9-10
Usomaji wa Biblia kwa ajili ya Ukumbusho: (Mambo yenye ilitokea muchana: Nisani 13) Matayo 26:17-19; Marko 14:12-16; Luka 22:7-13 (Mambo yenye ilitokea kisha jua kushuka: Nisani 14) Yohana 13:1-5; 14:1-3
Siku ya Tano, 3 Mwezi wa 4
Mungu alipenda ulimwengu sana na hivyo akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee, ili kila mutu mwenye anamuamini asiharibiwe lakini apate uzima wa milele.—Yoh. 3:16.
Yesu alisalitiwa, alikamatwa, alitukanwa, alishitakiwa mambo ya uongo, alihukumiwa, na hata alipigwa. Maaskari walimupeleka fasi kwenye alipaswa kuuawa na wakamupigilia misumari ku muti. Wakati alikuwa navumilia kwa uaminifu ile maumivu yote, kuko mwenye alikuwa naumia hata zaidi, Yehova Mungu. Yehova alijizuia juu asitumie nguvu yake yenye haina mipaka ili kuokoa Mwana wake. Juu ya nini? Sababu ni moya tu, upendo. Zabihu ya Yesu njo jambo kubwa yenye inaonyesha kama Yehova anakupenda sana. Alijiima sana juu yako, alikuwa tayari kuvumilia maumivu ya nguvu sana yenye hauwezi hata kuwazia, juu ya kukukomboa kutoka mu zambi na kifo. (1 Yo. 4:9, 10) Kwa kweli, anapenda kusaidia kila umoya wetu kupiganisha zambi, na ku mwisho kupata ushindi! w24.08 6 fu. 13-14
Usomaji wa Biblia kwa ajili ya Ukumbusho: (Mambo yenye ilitokea muchana: Nisani 14) Yohana 19:1-42
Siku ya Posho, 4 Mwezi wa 4
Kristo aliteseka kwa ajili yenu.—1 Pe. 2:21.
Tunaweza kuelewa muzuri zaidi namna Yehova anatupenda sana kama tunafikiria mambo yenye ilimuomba afanye juu atutolee ile zabihu. Shetani anasema kama hakuna mutumishi wa Yehova mwenye atabakia muaminifu wakati iko mu hali ya nguvu. Juu ya kuonyesha kama Shetani anasema uongo, Yehova aliruhusu Yesu ateseke mbele ya kufa. (Yob. 2:1-5) Yehova alijionea namna wakubwa wa dini walimucheka Yesu, aliona namna maaskari walimupiga, na namna walimupigilia misumari kwenye muti. Kisha Yehova alijionea namna mutoto wake mupendwa alikufa kisha kuteseka sana. (Mt. 27:28-31, 39) Yehova alikuwa na uwezo wa kusimamisha ile magumu kwa wakati wowote. (Mt. 27:42, 43) Lakini kama angefanya vile, bei ya ukombozi haingelipwa na hatungekuwa na tumaini ya kukombolewa. Kwa hiyo Yehova aliruhusu Mwana wake avumilie ile mateso yote mupaka wakati alikata roho. w25.01 22 fu. 7
Usomaji wa Biblia kwa ajili ya Ukumbusho: (Mambo yenye ilitokea muchana: Nisani 15) Matayo 27:62-66 (Mambo yenye ilitokea kisha jua kushuka: Nisani 16) Yohana 20:1
Siku ya Yenga, 5 Mwezi wa 4
Walimuona kwa muda wa siku makumi ine (40).—Mdo. 1:3.
Ni siku ya 16 ya Nisani mwaka wa 33 kisha kuzaliwa kwa Yesu. Mitume wa Yesu wako na huzuni na wanaogopa sana. Bawili kati yao banatoka Yerusalemu na kuenda Emau. Mwanaume moya mwenye habajue anabakaribia na kuanza kutembea pamoya nabo. Mitume wanamuelezea namna balishavunjika moyo juu ya mambo yenye ilimufikia Yesu. Ule mwanaume anaanza kubafasiria juu ya mambo yenye habawezi kusahau mu maisha yabo. “Akianza na Musa na Manabii wote,” akabafasiria juu ya nini Masiya alipaswa kuteseka na kufa. Wakati banafika Emau, ule mwanaume mwenye habajue, anaonyesha yeye ni nani, ni Yesu mwenye amefufuliwa! (Lu. 24:13-35) Yesu alitokea banafunzi yake mara mingi mu siku 40 za mwisho zenye alipitisha ku dunia. Mu ile kipindi, Yesu alitia moyo banafunzi yake benye balikuwa na huzuni na woga bakuwe bahubiri na balimu ba habari njema ya Ufalme benye bidii. w24.10 12 fu. 1-3
Usomaji wa Biblia kwa ajili ya Ukumbusho: (Mambo yenye ilitokea muchana: Nisani 16) Yohana 20:2-18
Siku ya Kwanza, 6 Mwezi wa 4
Mujijenge ninyi wenyewe juu ya imani yenu takatifu zaidi.—Yud. 20.
Bila kufanya jambo yoyote, mutoto anaweza kukomaa na kufikia kuwa mutu muzima kisha wakati. Lakini hakuna mutu mwenye anaweza kukomaa kiroho bila kufanya jambo yoyote. Kwa mufano, ndugu na dada katika Korinto walikubali habari njema, wakabatizwa, wakapokea roho takatifu, na kufaidika na mafundisho ya mutume Paulo. (Mdo. 18:8-11) Lakini, miaka fulani kisha kubatizwa, wengi wao walikuwa wangali watoto kiroho. (1 Ko. 3:2) Ili tukomae kiroho, tunapaswa kwanza kuwa na nia ya kukomaa. Wale wenye “kupenda kukosa uzoefu,” wenye wanafurahia kubakia watoto kiroho, hawatafanya maendeleo. (Mez. 1:22) Hatupendi kuwa sawa watu wazima wenye wazazi wao wangali nakamatia maamuzi. Lakini, tunapenda kukamata mambo na mikono mbili na kuhangaikia siye wenyewe hali yetu ya kiroho. Kama ungali najikaza ili ufikie kukomaa kiroho, umuombe Yehova akupatie “hamu na pia nguvu za kutenda.”—Flp. 2:13. w24.04 4 fu. 9-10
Siku ya Pili, 7 Mwezi wa 4
Yehova . . . hataki mutu yeyote aharibiwe.—2 Pe. 3:9.
Yehova anatuambia mawazo yake kuhusu kuhukumu watu. (Eze. 33:11) Yehova haiko haraka kuharibu watu milele. Ni mwenye rehema nyingi sana, na wakati wote wenye inawezekana, anaonyesha ile sifa. Tunajua nini kuhusu watu wenye hawatafufuliwa? Biblia inazungumuzia tu mifano kidogo ya watu wenye hawatafufuliwa. Yesu alionyesha kama Yuda Iskariote hatafufuliwa. (Mk. 14:21) Yuda Iskariote alijua kama jambo yenye alitaka kufanya ilimupinga Yehova Mungu na Mwana wake, lakini aliifanya tu. (Mk. 3:29) Vilevile, Yesu alisema kama viongozi fulani wa dini wenye walimupinga hawangekuwa na tumaini ya ufufuo. (Mt. 23:33) Na mutume Paulo alionya kama waasi-imani wenye hawatubu hawangefufuliwa.—Ebr. 6:4-8; 10:29. w24.05 4 fu. 10-11
Siku ya Tatu, 8 Mwezi wa 4
Yehova analinda waaminifu.—Zb. 31:23.
Wakati tunabakia karibu na Yehova, Shetani hawezi kutufanyia jambo yoyote yenye inaweza kutuumiza milele. (1 Yo. 3:8) Mu dunia mupya, Yehova ataendelea kulinda kiroho marafiki wake waaminifu lakini pia atawalinda ili wasikufe tena. (Ufu. 21:4) Ni pendeleo kubwa kuwa mugeni mu hema ya Yehova, ni kusema kuwa na uhusiano wa pekee na wa milele pamoya naye. (Eze. 37:27) Tunapaswa kufanya nini ili tuendelee kuwa wageni mu hema yake? Kama mutu fulani anakualika kwake, utapenda kujua mambo yenye anatazamia ufanye. Vilevile, tunapenda kujua mambo yenye Yehova anaomba wageni wake wafanye. Upendo wetu kwa Yehova unatuchochea tufanye yetu yote “ili kumupendeza kwa ukamili.” (Kol. 1:10) Hatupaswe kusahau hata siku moya yeye ni nani, na tunapaswa kumuheshimia sikuzote. Kufanya vile kutatusaidia tuepuke tabia zenye zinaweza kumukasirisha. Sikuzote tunapenda ‘kutembea kwa kiasi’ pamoya na Mungu wetu.—Mik. 6:8. w24.06 4 fu. 8-9
Siku ya Ine, 9 Mwezi wa 4
Alitetea wakosaji.—Isa. 53:12.
Yehova alimuomba Abrahamu, atoe mwana wake Isaka kuwa zabihu. Bila shaka ile ilipaswa kuumiza sana Abrahamu. Hata vile, alimutii Yehova. Lakini ku dakika ya mwisho, Yehova alimuzuia asiue mwana wake. Mufano wa Abrahamu, unafundisha batu yote benye imani hii kweli ya maana sana: Yehova anapenda sana wanadamu mupaka angekuwa tayari kutoa Mwana wake mupendwa kuwa zabihu. (Mwa. 22:1-18) Kisha miaka mingi, Yehova alipatia Waisraeli Sheria. Mu ile Sheria aliwaomba watoe zabihu za mingi ili kufunika zambi zao. (Law. 4:27-29; 17:11) Zile zabihu zilionyesha kama kungekuwa zabihu kubwa zaidi yenye ingekomboa kabisa wanadamu kutoka katika zambi. Kupitia roho yake, Mungu aliongoza manabii wake kutabiri kama ule uzao, ni kusema Mwana wa pekee wa Mungu, alipaswa kuteseka na kuuawa juu ya kukomboa wanadamu, ni kusema kukukomboa na weye kutoka katika zambi na kifo! —Isa. 53:1-12. w24.08 4 fu. 7-8
Siku ya Tano, 10 Mwezi wa 4
Ninapenda sana sheria yako! Ninafikiri sana juu yake muchana wote.—Zb. 119:97.
Wakati unasoma Biblia uhakikishe kama uko natumikisha mambo yenye uko nasoma. Wakati unasoma jambo fulani mu Neno ya Mungu, ujiulize hivi: ‘Naweza kutumikisha namna gani hii habari leo ao mu siku zenye ziko nakuya?’ Kwa mufano, tuseme mu usomaji wako wa Biblia, muko 1 Watesalonike 5:17, 18. Kisha kusoma ile mistari mbili, unaweza kuacha kwanza kusoma na kufikiria ikiwa unakuwaka na zoea ya kusali na ikiwa unakuwaka nasali kwa moyo wote kabisa. Pia, unaweza kufikiria mambo yenye ungependa kumushukuru Yehova. Pengine unaweza kuamua kumushukuru Yehova juu ya mambo tatu fulani. Hata kama unatumia dakika kidogo tu juu ya kufikiria mambo yenye uko nasoma, ile itakusaidia ukuwe musikiaji na mutendaji wa Neno ya Mungu. Fikiria faida yenye utapata kama unafanya vile kila siku wakati unasoma Biblia! Utafikia kuwa mutumishi muzuri wa Yehova. w24.09 4-5 fu. 9-10
Siku ya Posho, 11 Mwezi wa 4
Mufanye angalisho, ili musipoteze mambo yenye tumefanya kazi ili kuyatokeza, lakini ili mupate zawabu kamili.—2 Yo. 8.
Yehova alituumba mu njia ya ajabu. Ni kweli tunakuwaka na furaha wakati tunapewa, lakini tunakuwaka na furaha zaidi wakati tunapatia wengine. Tunajisikiaka muzuri wakati tunasaidia ndugu zetu. Na tunafurahi wakati wanatuonyesha shukrani. Lakini ikuwe wanaonyesha shukrani ao hapana, tutakuwa na furaha juu tunajua kama tulifanya jambo ya muzuri. Usisahau kama hata kama unapatia wengine nini, “Yehova anaweza kukupatia nyingi zaidi.” (2 Ny. 25:9) Hata tupatie wengine nini Yehova atatupatia vitu mingi zaidi kupita vyenye tunapatia wengine! Na hakuna furaha yenye inapita furaha ya kubarikiwa na Yehova mwenyewe. Basi tuazimie kuiga Baba yetu wa mbinguni mwenye ukarimu. w24.09 30-31 fu. 20-21
Siku ya Yenga, 12 Mwezi wa 4
Ninakusifu, Ee Yehova Mungu wangu, kwa moyo wangu wote, na nitatukuza jina lako milele.—Zb. 86:12.
Yehova iko na rehema na huruma. (Zb. 103:13; Isa. 49:15) Anajitia pa nafasi yetu; wakati tunaumia yeye pia anaumia. (Zek. 2:8) Anafanya ikuwe mwepesi kwetu kumukaribia na kuwa marafiki wake. (Zb. 25:14; Mdo. 17:27) Ni munyenyekevu; “anainama ili aangalie mbingu na dunia, anainua mutu wa hali ya chini kutoka katika mavumbi.” (Zb. 113:6, 7) Juu ya ile mambo yote, tunapenda kabisa kumupatia Mungu wetu Mukubwa utukufu. Tunamupatia Yehova utukufu juu tunapenda wengine wamujue. Watu wengi hawajue kweli juu ya Yehova. Juu ya nini? Juu Shetani amepofusha akili zao kwa kueneza habari za bongo juu ya Yehova. (2 Ko. 4:4) Shetani amefanya watu waamini kama Yehova analipishaka kisasi, haangaikie watu, na ni yeye njo ameleta mateso mingi mu dunia. Lakini siye tunajua kweli juu ya Mungu wetu! Tuko na nafasi ya kuelezea watu ile kweli, na kwa kufanya vile tunamutukuza Yehova.—Isa. 43:10. w25.01 3 fu. 6-7
Siku ya Kwanza, 13 Mwezi wa 4
Shetani . . . anapotosha dunia yote yenye kuikaliwa na watu.—Ufu. 12:9.
Hata kama Yesu, Mwana wa Mungu alikuwa mukamilifu na alifanya miujiza ya ajabu, Shetani alitumia watu fulani ili kueneza habari mingi za uongo kumuhusu. Kwa mufano, viongozi wa dini waliambia watu kama mamlaka ya Yesu ya kufukuza pepo wachafu ilitoka kwa “mutawala wa pepo wachafu.” (Mk. 3:22) Wakati Yesu alikuwa nasambishwa, viongozi wa dini walimushitaki kama alimutukana Mungu na walichochea watu waombe auawe. (Mt. 27:20) Kisha, wakati wanafunzi wa Yesu walikuwa nahubiri habari njema, wapinzani wao ‘walichochea mubaya watu’ ili wawatese. (Mdo. 14:2, 19) Kuhusu andiko ya Matendo 14:2, Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 12, 1998, ulisema hivi: “Zaidi ya kukataa ule ujumbe, Wayahudi wapinzani walianzisha kampanye ya kuchochea Watu wa Mataifa ili wao pia wasiwasikilize Wakristo.” Leo Shetani angali “anapotosha dunia yote yenye kuikaliwa na watu.” w24.04 11 fu. 15-16
Siku ya Pili, 14 Mwezi wa 4
Je, Muamuzi wa dunia yote hatatenda jambo lenye kuwa sawa?—Mwa. 18:25.
Kupata uzima wa milele haitegemee ni mu kipindi gani mutu anakufa. Yehova ni muamuzi mukamilifu, maamuzi yake ni yenye haki na yenye kuwa sawa. (Zb. 33:4, 5) Tunaweza kuwa hakika kama “Muamuzi wa dunia yote” atafanya mambo yenye kuwa sawa. Inapatana pia na akili kusema kama kupata uzima wa milele ao hapana haitegemee fasi kwenye mutu anaishi. Mamilioni ya watu wanaishi mu maeneo kwenye hawapate nafasi ya kujifunza juu ya Ufalme, hatuwezi kuwazia kama Yehova atahukumu tu wale watu wote kuwa “mbuzi.” (Mt. 25:46) Muamuzi mwenye haki wa dunia yote anahangaikia sana wale watu kupita namna tunawahangaikia. Hatujue namna Yehova ataongoza matukio wakati wa taabu kubwa. Pengine watu fulani kati yao, watapata nafasi ya kujifunza juu ya Yehova, kumuamini na kuwa upande wake wakati atajitakasa mbele ya mataifa yote.—Eze. 38:16. w24.05 12 fu. 14-15
Siku ya Tatu, 15 Mwezi wa 4
Mupendane.—Yoh. 15:12.
Watu wa Yehova wanapenda kusaidiana. (2 Ko. 8:4) Lakini, wakati fulani inaomba kuwa hodari ili kufanya vile. Kwa mufano, wakati vita inatokea wazee wanatambua kama ndugu na dada zao wako na lazima ya kutiwa moyo, kutegemezwa, na pengine wako na lazima ya musaada wa kiroho ao wa kimwili. Juu wanapenda kondoo wa Mungu, wazee wanajitia katika hatari ili kutolea ndugu zao musaada wenye wako nao lazima. Mu hali ya vile, ni jambo ya maana kuendelea kuwa na umoja. Fuata muongozo wa tawi ya inchi yenu. (Ebr. 13:17) Wazee wanapaswa kuchunguza kwa ukawaida mipango mbalimbali ya kujitayarisha kwa ajili ya misiba, na pia muongozo wenye tengenezo inatoa kuhusu namna ya kutenda wakati musiba unatokea. (1Ko. 14:33, 40) Ukuwe hodari lakini muangalifu. (Mez. 22:3) Ufikiri mbele ya kutenda. Usijitie mu hatari bila sababu. Umutegemee Yehova. Anaweza kukusaidia juu utolee ndugu zako musaada mu njia yenye kuwa salama. w24.07 4 fu. 8; 5 fu. 11
Siku ya Ine, 16 Mwezi wa 4
Katika taabu yangu nilimuitia Yehova, . . . na kilio changu cha kumuomba musaada kikafika katika masikio yake.—Zb. 18:6.
Mufalme Daudi alimujua Yehova na alimutegemea. Wakati alikuwa nakimbia maadui wake, kutia ndani Mufalme Sauli, Daudi aliomba Yehova amusaidie. Kisha Mungu kujibia sala yake na kumuokoa, Daudi alisema hivi: “Yehova ni mwenye kuishi.” (Zb. 18:46) Wakati Daudi alisema ile maneno hakukuwa tu anamaanisha kuwa anajua kama Mungu iko. Kitabu fulani kinasema kama Daudi alikuwa naonyesha kuwa iko hakika kama Yehova “ni Mungu mwenye kuishi mwenye anatenda kwa ajili ya watu wake sikuzote.” Kwa kweli Daudi alijionea mu maisha yake namna Yehova ni Mungu mwenye kuishi, na kujua vile kulifanya aazimie kabisa kumutumikia na kumusifu. (Zb. 18:28, 29, 49) Kuwa hakika kama Yehova ni Mungu mwenye kuishi kunaweza kutusaidia tuendelee kumutumikia kwa bidii. Tutakuwa na nguvu ya kuvumilia magumu na tutachochewa kuendelea kumutumikia Mungu kwa nguvu yetu yote. Pia tutaazimia kuendelea kubakia karibu na Yehova. w24.06 20-21 fu. 3-4
Siku ya Tano, 17 Mwezi wa 4
Musiache mutu yeyote awadanganye ninyi kwa njia yoyote.—2 Te. 2:3.
Maneno ya mutume Paulo kwa Watesalonike inaweza kutufundisha nini? Wakati tunasikia habari fulani yenye haipatane na mambo yenye tumejifunza mu Biblia ao wakati tunasikia habari za ajabu-ajabu, tunapaswa kuwa na utambuzi. Wakati wa utawala wa Wasovieti, maadui wetu walipatia ndugu barua yenye ilisemekana kuwa inatoka ku makao makubwa. Ile barua ilitia moyo ndugu fulani wajitenge na tengenezo na wafanyize kikundi yao. Ile barua ilionekana kuwa ya kweli. Lakini ndugu waaminifu hawakudanganywa. Walitambua kama ujumbe wenye ulikuwa mu ile barua haukupatana na mambo yenye walikuwa wamefundishwa. Leo, wakati fulani maadui wetu wanatumia teknolojia ya sasa ili kujaribu kutuvuruga na kutugawanya. Kama ile hali inatokea, “akili [yetu] isivurugwe haraka,” tujilinde kwa kujiuliza ikiwa mambo yenye tunasikia inapatana na kweli zenye tunajua tayari.—2 Te. 2:2; 1 Yo. 4:1. w24.07 12 fu. 14-15
Siku ya Posho, 18 Mwezi wa 4
Kama mutu yeyote anafanya zambi, tuko na musaidizi.—1 Yo. 2:1.
Uamuzi wa maana zaidi wenye mutu anaweza kukamata ni uamuzi wa kujitoa kwa Yehova na kuingia mu familia ya waabudu wake. Yehova anapenda batu yote bafanye vile. Juu ya nini? Anapenda bakuwe barafiki yake na baishi milele. (Kum. 30:19, 20; Gal. 6:7, 8) Lakini, Yehova hakaze mutu kumutumikia. Anaacha kila mutu aamue mambo yenye atafanya. Sasa mambo itakuwa namna gani kama Mukristo mwenye kubatizwa anavunja sheria ya Mungu na kufanya zambi nzito? Kama hatubu, anapaswa kuondolewa mu kutaniko. (1 Ko. 5:13) Hata vile, Yehova anatumainia kabisa kama ule mutenda-zambi atamurudilia. Na ile njo sababu kubwa yenye ilifanya Yehova atoe zabihu ya ukombozi, juu watenda-zambi wenye kutubu waweze kusamehewa. Yehova ni Mungu mwenye upendo sana, anaomba watenda-zambi watubu.—Zek. 1:3; Ro. 2:4; Yak. 4:8. w24.08 14 fu. 1-2
Siku ya Yenga, 19 Mwezi wa 4
Kama moyo wako unakuwa na hekima, basi moyo wangu mwenyewe utafurahi sana.—Mez. 23:15.
Wakati mutume Yohana aliandika barua yake ya tatu, watu fulani walikuwa naeneza mafundisho ya uongo na kuleta migawanyiko mu kutaniko. Lakini, wengine waliendelea “kutembea katika kweli.” Walimutii Yehova na ‘waliendelea kutembea kulingana na amri zake.’ (2 Yo. 4, 6) Wale Wakristo waaminifu walimufurahisha Yohana, lakini pia walimufurahisha Yehova. (Mez. 27:11) Tunajifunza nini? Uaminifu unaletaka furaha. (1 Yo. 5:3) Kwa mufano, kujua kama tuko namufurahisha Yehova, kunatuletea furaha. Yehova anafurahi wakati anaona tunashinda majaribu ya mu huu ulimwengu na tunakubali kweli. Malaika mbinguni wanafurahi pia. (Lu. 15:10) Siye pia tunafurahi wakati tunaona bengine banaendelea kuwa baaminifu. (2 Te. 1:4) Wakati huu ulimwengu utapita, tutakuwa na furaha juu tuliendelea kuwa baaminifu kwa Yehova hata wakati Shetani alikuwa natawala dunia. w24.11 12 fu. 17-18
Siku ya Kwanza, 20 Mwezi wa 4
Kila mumoja aendelee kutafuta, hapana faida yake mwenyewe, lakini faida ya ule mutu mwingine.—1 Ko. 10:24.
Unapaswa kuchunguza mutu kwa muda gani mbele ya kumuambia kama unamufurahia? Kama mwanzo-mwanzo tu unaambia mutu kama unamufurahia anaweza kuwaza kama unakamataka maamuzi bila kufikiri kwa uangalifu. (Mez. 29:20) Lakini kama unakamata tena wakati murefu sana mbele ya kumuambia, ule mutu anaweza kuona kama uko mutu wa kusita-sita, zaidi sana kama alitambua kuwa unapendezwa naye. (Muh. 11:4) Kumbuka kama mbele ya kuzungumuza na mutu haiko lazima ukuwe hakika kabisa kama mutaoana. Lakini unapaswa kuwa hakika kama uko tayari kwa ajili ya ndoa, na kama ule mutu anaweza kuwa bibi ao bwana muzuri kwako. Sasa utafanya nini kama unatambua kuwa mutu fulani anapendezwa na weye? Kama weye haupendezwe naye uonyeshe vile waziwazi kupitia matendo yako. Haiko muzuri kufanya mutu awaze kama inawezekana muanzishe uhusiano fulani, lakini weye hauwaze vile.—Efe. 4:25. w24.05 22-23 fu. 9-10
Siku ya Pili, 21 Mwezi wa 4
Nitakuja tena na nitawapokea ninyi katika nyumba yangu mwenyewe.—Yoh. 14:3.
Ni watiwa-mafuta wa kweli na waaminifu tu njo Yesu atakaribisha mu Ufalme wa mbinguni. Mutiwa-mafuta yeyote mwenye haendelee kuwa macho kiroho, hatakusanywa pamoya na “wenye kuchaguliwa.” (Mt. 24:31) Maneno ya Yesu inahusu watu wote wa Mungu, ikuwe wako na tumaini gani, wote wanapaswa kuona ile maneno kuwa onyo ya kuwasaidia waendelee kuwa macho na waaminifu. Juu tumefikia kumujua Yehova muzuri, tuko hakika kama kama maamuzi yake yote ni ya muzuri. Hatuhangaike ikiwa Yehova anachagua kutia mafuta mutu fulani mu siku zetu. Tunakumbuka maneno ya Yesu kuhusu wale wafanyakazi wenye walifika saa ya kumi na moya mu mufano wake wa shamba ya mizabibu. (Mt. 20:1-16) Wale wenye walialikwa kutumika mu shamba ya mizabibu nyuma walipokea mushahara uleule na wale wenye walianza kutumika mbele. Vilevile, watiwa-mafuta wote watapokea zawabu yao ya kuishi mbinguni kama wanabakia waaminifu, ikuwe walitiwa mafuta wakati gani. w24.09 24 fu. 15-17
Siku ya Tatu, 22 Mwezi wa 4
Kristo aliteseka kwa ajili yenu, akiwaachia ninyi mufano ili mufuate hatua zake kwa ukaribu.—1 Pe. 2:21.
Yesu alituachia mufano muzuri juu ya namna ya kutenda wakati banatutendea bila haki. Ona namna batu ya familia yake na batu bengine balimutendea bila haki. Batu ya familia yake benye habakumuamini balisema kama amepoteza akili, viongozi wa dini walisema kama alikuwa natumika pamoya na pepo wachafu, na maaskari Waroma walimuchekelea, walimutendea mubaya kimwili, na ku mwisho walimuua. (Mk. 3:21, 22; 14:55; 15:16-20, 35-37) Lakini, Yesu alivumilia ile matendo yote ya ukosefu wa haki bila kulipiza kisasi. Mufano wake unatufundisha nini? (1 Pe. 2:21-23) Yesu alituachia mufano muzuri wenye unatusaidia kujua namna ya kutenda wakati banatutendea bila haki. Alijua wakati wa kubakia kimya na wakati wa kusema. (Mt. 26:62-64) Haiko kila saa njo alijibia wakati bengine balisema mambo ya uongo juu yake. (Mt. 11:19) Na wakati aliamua kusema hakutukana ao kuogopesha benye balikuwa namutesa. w24.11 4-5 fu. 9-10
Siku ya Ine, 23 Mwezi wa 4
Kristo Yesu alikuja katika ulimwengu ili kuokoa watenda-zambi.—1 Ti. 1:15.
Wazia unapatia mutu mwenye unapenda zawadi ya muzuri na yenye itamusaidia. Utahuzunika sana kama ule mutu anaweka tu ile zawadi bila kuitumikisha. Lakini, utafurahi sana kama anaitumikisha muzuri na anakuonyesha shukrani. Ile mufano inapenda kutufundisha nini? Yehova ametoa Mwana wake kwa ajili yetu. Bila shaka anafurahi sana wakati tunaonyesha shukrani juu ya ile zawadi ya muzuri sana, na juu ya upendo wake wenye ulimuchochea atoe bei ya ukombozi! (Yoh. 3:16; Ro. 5:7, 8) Lakini, vile wakati iko napita, tunaweza kuona ile zawadi ya bei ya ukombozi kuwa jambo ya kawaida tu. Kama hatuendelee kuonyesha shukrani juu ya bei ya ukombozi, itakuwa sawa vile tunaweka tu fasi moya zawadi ya muzuri yenye Mungu alitupatia bila kuitumikisha. Juu ile isitufikie, tunapaswa mara kwa mara kufikiria mambo yenye Mungu na Kristo walifanya kwa ajili yetu. w25.01 26 fu. 1-2
Siku ya Tano, 24 Mwezi wa 4
Fikiri sana juu ya mambo hayo; zama katika mambo hayo, ili maendeleo yako yaonekane wazi kwa watu wote.—1 Ti. 4:15.
Ndugu mwenye iko najikaza juu akuwe muzee hapaswe kuwa muamini mupya. Hata kama haiombe ukuwe umebatizwa kwa miaka mingi, uko na lazima ya wakati juu ufikie kuwa Mukristo mwenye kukomala kiroho. Mbele ya kuwekwa kuwa muzee unapaswa kuonyesha sawa Yesu kama uko munyenyekevu, na kama uko tayari kumungojea Yehova akupatie mugao kwa wakati wenye kufaa. (Mt. 20:23; Flp. 2:5-8) Unaweza kuonyesha kama uko mushikamanifu kwa kushikamana na Yehova na kanuni zake na kwa kufuata muongozo wa tengenezo. Maandiko inaonyesha wazi kama mwangalizi anapaswa kuwa na uwezo wa kufundisha. Ni kusema ni lazima muzee akuwe musemaji muzuri sana? Hapana. Wazee wengi wenye uzoefu, hata kama hawako wasemaji wazuri sana, wanafundishaka muzuri mu mahubiri na mu ziara za uchungaji. w24.11 23-24 fu. 14-15
Siku ya Posho, 25 Mwezi wa 4
Ninapenda amri zako kuliko zahabu, hata zahabu safi.—Zb. 119:127.
Fanya utafiti wakati unapata mu Biblia andiko yenye hauelewe muzuri. Kisha utafakari juu ya mambo ya mupya yenye umepata, na ujiulize kama inakufundisha nini juu ya Yehova, juu ya Mwana wake, na namna inaonyesha kama wanakupenda. (Zb. 119:97, maelezo ya chini) Usivunjike moyo kama haupate jambo fulani ya mupya ao jambo fulani ya ajabu kila wakati unajifunza na kufanya utafiti. Uko sawa mutu mwenye iko natafuta zahabu. Mutu mwenye iko natafuta zahabu anapitishaka saa mingi ao hata masiku mingi mbele apate hata kalijiwe ka kidogo ka zahabu. Lakini anaendelea kutafuta juu kila kalijiwe ka zahabu kenye anapata ni ka maana sana. Kweli ya Biblia ni ya maana hata zaidi kupita zahabu! (Mez. 8:10) Kwa hiyo, ukuwe muvumilivu na uheshimie programu yako ya kusoma Biblia.—Zb. 1:2. w25.01 24-25 fu. 14-15
Siku ya Yenga, 26 Mwezi wa 4
Kama vile Yehova aliwasamehe ninyi kwa kupenda, ninyi pia munapaswa kufanya vilevile.—Kol. 3:13.
Yehova anapenda tukuwe tayari kusamehe wenye wanatuumiza. (Zb. 86:5; Lu.17:4; Efe. 4:32) Tunaweza kuumia sana juu ya mambo yenye mutu anasema ao kufanya, zaidi sana kama ule mutu ni rafiki wa karibu ao mutu wa familia. (Zb. 55:12-14) Wakati fulani, maumivu yetu inaweza kuwa sawa ya mutu mwenye anachomwa kisu ao anaingizwa kisu mu mwili. (Mez. 12:18) Tunaweza kujaribu kufanya sawa vile hakuna kitu. Lakini kufanya vile ni sawa vile kuacha kisu mu kilonda. Vilevile, hatuwezi kutazamia kama maumivu yetu itaisha ikiwa tunafanya tu sawa vile haiko. Wakati mutu anatukwaza, ku mwanzo tunaweza kukasirika. Biblia inaonyesha kama mutu anaweza kuwa na kasirani. Lakini inatuonya kama hatupaswe kuacha kasirani itutawale. (Zb. 4:4; Efe. 4:26) Juu ya nini? Juu mara mingi kasirani haikuwake na matokeo ya muzuri. (Yak. 1:20) Kumbuka kama unaweza kukasirika, lakini ni weye njo utaamua kama utabakia na kasirani ao hapana. w25.02 15 fu. 4-6
Siku ya Kwanza, 27 Mwezi wa 4
Hekima inalinda uzima wa mwenye kuwa nayo.—Muh. 7:12.
Yesu alitoa mufano wenye ulionyesha kama ni upumbavu kujiwekea makuta bila kuwa “tajiri kwa Mungu.” (Lu. 12:16-21) Hakuna mwenye anajua bya kesho. (Mez. 23:4, 5; Yak. 4:13-15) Zaidi ya ile juu tuko wafuasi wa Kristo, tuko na tatizo ingine. Yesu alisema kama tunapaswa kuwa tayari ‘kuachana’ na vitu vyetu vyote. (Lu. 14:33, maelezo ya chini.) Wakristo wa Yudea wa mu karne ya kwanza walikubali kwa furaha kupoteza vitu vyao. (Ebr. 10:34) Wakati wetu bandugu mingi bamekubali kupoteza vitu ao kazi juu walikatala kujiingiza mu mambo ya politike. (Ufu. 13:16, 17) Nini njo ilibasaidia kufanya vile? Balikuwa hakika kabisa kama Yehova atatimiza hii ahadi yake: “Sitakuacha hata kidogo, na sitakutupa hata kidogo.” (Ebr. 13:5) Tunafanya yenye tunaweza juu ya kutayarisha maisha yetu ya kesho, na kama mambo yenye haikutazamiwa inatokea tuko hakika kama Yehova atatutegemeza. w25.03 29 fu. 13-14
Siku ya Pili, 28 Mwezi wa 4
Kwa kuwa sasa tumeacha nyuma fundisho la musingi juu ya Kristo, tusonge mbele kuelekea ukomavu, bila kuweka tena musingi.—Ebr. 6:1.
Yehova anatutolea musaada ili tufikie kukomaa kiroho. Wachungaji na walimu katika kutaniko ya Kikristo wamezoezwa ili kusaidia Wakristo wakuwe ‘wenye kukomaa kabisa’ kiroho, “na kufikia kipimo cha ukomavu kamili cha Kristo.” (Efe. 4:11-13.) Yehova anatutolea pia roho yake takatifu ili itusaidie kuwa na “akili ya Kristo.” (1 Ko. 2:14-16) Zaidi ya ile, Mungu ametupatia vitabu ine vya Injili vyenye kuzungumuzia utumishi wake ku dunia. Vinatusaidia kujua namna ya Yesu ya kufikiri, kusema, na kutenda. Kama unaiga namna ya Yesu ya kufikiri na kutenda, unaweza kufikia muradi wako wa kuwa Mukristo mwenye kukomaa kiroho. Lakini ili tufikie kukomaa kiroho, tunapaswa pia kuacha “nyuma fundisho la musingi juu ya Kristo,” ni kusema mafundisho ya musingi ya Kikristo. w24.04 4-5 fu. 11-12
Siku ya Tatu, 29 Mwezi wa 4
Uwezo wa kufikiri utakulinda, na utambuzi utakuchunga.—Mez. 2:11.
Kila siku tunapaswa kukamata maamuzi. Maamuzi fulani ni ya mwepesi kukamata, sawa vile kuamua tutakula nini ao tutalala saa gani. Lakini kuko maamuzi yenye inakuwaka nguvu kukamata juu inaweza kuwa na matokeo juu ya afya yetu, juu ya wapendwa wetu, juu ya ibada yetu ao juu inaweza kutuletea ao kutukosesha furaha. Tunapenda kukamata maamuzi yenye itakuwa na matokeo ya muzuri juu yetu na juu ya familia yetu. Na zaidi ya yote, tunapenda kukamata maamuzi yenye itamufurahisha Yehova. (Ro. 12:1, 2) Jambo ya maana yenye unapaswa kufanya juu ukamate uamuzi muzuri ni kutafuta kujua habari zote. Juu ya nini ni jambo ya maana kufanya vile? Wazia mutu mwenye kuwa na ugonjwa wa nguvu anaenda kuona munganga. Unawaza munganga ataamua ni matunzo gani ule mugonjwa anapaswa kupata bila kuchunguza hali yake ao kumuuliza maulizo? Hapana. Na weye utakamata maamuzi ya muzuri kama unatafuta kwanza kujua habari zote zenye zinahusu hali yako. w25.01 14 fu. 1-3
Siku ya Ine, 30 Mwezi wa 4
Yehova . . . amesamehe zambi yako. Hautakufa.—2 Sa. 12:13.
Tunajua nini kuhusu rehema ya Yehova? Ameonyesha namna gani kama “hataki mutu yeyote aharibiwe”? (2 Pe. 3:9) Tuone namna alionyesha rehema watu fulani wenye walifanya makosa makubwa. Mufalme Daudi alifanya zambi nzito, alifanya uzinifu na aliua. Lakini, Daudi alitubu. Kwa hiyo, Yehova alimuonyesha rehema na akamusamehe. (2 Sa. 12:1-12) Mufalme Manase alifanya mambo mingi ya mubaya sana mu sehemu kubwa ya maisha yake. Hata vile, Yehova alimuonyesha rehema na akamusamehe juu alitubu. (2 Ny. 33:9-16) Ile mifano inaonyesha kama Yehova anaonyeshaka rehema wakati wowote wenye anaona kama kuko sababu ya kufanya vile. Yehova atafufua wale watu juu walitambua kama walifanya makosa makubwa na wakatubu. w24.05 4 fu. 12