Maswali Kutoka kwa Wasomaji
● Je! ni lazima samaki aondolewe damu mbele ya kuliwa?—U.S.A.
Biblia haitaji juu ya kuondoa damu ya samaki. Tunasoma juu ya wanyama wa nchi kavu na ndege peke yao: “Mtu ye yote . . . ambaye amemshika mnyama, au ndege ambaye huliwa, katika kuwinda kwake; atamwaga damu yake, na kuifunika mchanga.”—Law. 17:13.
Samaki waliofaa kuliwa kulingana na masharti ya sheria ya Musa hawakuwa na damu nyingi ya kutosha kumwagwa na kufunikwa mchanga. Inaonekana kwamba ni kwa sababu hii ndiyo Torati haikutoa maelezo yo yote juu ya kuondoa damu ya samaki.
Kwa vile hakuna maelezo ya Maandiko yanayosema kufinya au kuloweka nyama ili kuondoa damu, hakuna mtu aliye chini ya sharti la kushughulika mno ili aondoe damu katika samaki. Bila shaka, damu ya kila namna ya kiumbe inafananisha uhai wake na kwa hiyo ni takatifu. Basi, ikiwa, wakati wa kumpasua samaki, mtu anaona damu nyingi, imempasa aiondoe.