Maswali Kutoka kwa Wasomaji
● Maoni ya mashahidi wa Yehova ni nini juu ya kazi ya kuamua kesi za kortini?—U.S.A.
Mashahidi wa Yehova wanakubali kwamba jambo ambalo watu wanafanya juu ya kuamua kesi za kortini ni shauri la kipekee, linaloongozwa na ambavyo dhamiri inasema.
Kwa kadiri inavyowapasa, mashahidi wa Yehova kwa desturi hawajioni kwamba imewapasa waketi kama mahakimu wa watu wengine. Wakati alipotolewa nafasi ya kuamua kesi, Mfano wao Bwana Yesu Kristo aliikataa, akisema: “Ni nani aliyeniweka mimi kuwa mwamuzi au mgawanyi juu yenu?” (Luka 12:14) Mtume Paulo alitokeza maulizo yanayofanana na hili katika barua yake kwa Wakorintho: “Yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani [ya kundi la Kikristo]? Lakini hao walio nje Mungu atawahukumu.”—1 Kor. 5:12, 13.
Halafu, tena, watu wengi wanaotumikia kama waamuzi wa kesi hawataki waongozwe na sheria za Neno la Mungu katika kufikia uamuzi. Waamuzi wengine wametafuta habari kwa kupiga falaki (kuagua kwa nyota), wamefanya upendeleo na kuamua isivyo haki au wamekazwa na wengine katika kutoa uamuzi. Hivyo kuna hatari ya kuwa mshiriki wa kupotoa haki. Wakati uhai wa mshtakiwa unapotiwa ndani, hii ingeweza kumaanisha kujiletea hatia ya damu. Ndivyo inavyoweza kuonwa sababu gani kutumikia kama mwamuzi wa kesi za kortini kunavyoweza kuongoza kwenye kupingana kukubwa kwa dhamiri.
Matakwa ya halali ya kufanya kazi ya kuamua kesi na mipango ya kuachiliwa inatofautiana mahali na mahali. Katika United States, huenda hali katika tarafa moja ikawa tofauti sana na ile iliyomo katika tarafa nyingine. Mara nyingine kueleza maoni yako kwa karani wa korti au kwa hakimu huenda kukaondolesha jina lako katika orodha ya wale wanaotazamiwa kuwa waamuzi. Kwa kweli, maoni ya Korti katika West Virginia, Minnesota na Washington yametegemeza haki ya mtu kukataa kazi ya kuamua kesi kwa sababu za kidini. Na katika tarafa ya Colorado watu ambao kwa hati za vithibitisho wanaweza kuonyesha kwamba wao ni mashahidi wa Yehova wanaachiliwa wasifanye kazi ya kuamua kesi.
Walakini, maachilio hayaruhusiwi kila mahali. Ikiwa mtu hawezi kuachiliwa wakati anapotakiwa afanye kazi ya kuamua kesi hata akiisha kueleza mambo kwa hakimu, hata hivyo, anaweza kueleza maoni yake ya dhamiri juu ya kesi hiyo wakati anapoulizwa na wanasheria mbele ya kuanza hukumu. Ikiwa maoni yake ya dhamiri hayakubaliwi kama yenye kumwondoa katika kazi ya kuamua, Mkristo anaweza kuona kwamba inampasa akatae kutumikia ili asiihalifu dhamiri yake. Ikiwa hivyo imempasa ajitayarishe kupokea matokeo yo yote ambayo huenda yakatokea kwa sababu ya kuamua kwake.