Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 11/15 kur. 525-527
  • “Iweni Waigaji wa Mungu”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Iweni Waigaji wa Mungu”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUWA WENYE UPENDO NA KUSAMEHE
  • KICHUKIE ANACHOKICHUKIA MUNGU
  • WAIGAJI KATIKA UVUMILIVU
  • “Iweni Waigaji wa Mungu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Ni kwa Njia Gani Tunavyoweza Kuwa “Waigaji wa Mungu”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • “Iweni Waigaji wa Mungu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Mwige Yule Anayeahidi Uzima wa Milele
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 11/15 kur. 525-527

“Iweni Waigaji wa Mungu”

WATU wengine wanasema mambo yenye kukashifu juu ya maelekeo ya kibinadamu ya kuiga. Lakini kuiga kwaweza kuwa msaada kweli kweli. Kwa kuiga unaonyesha kwamba unaheshimu sana kinachofanywa na mwingine hata kutaka kufanya kile kile.

Watoto wanawaiga wakubwa wao bila ya kufundishwa kufanya hivyo. Hii inaweka daraka zito juu ya wazazi wao. Je! wazazi wanasema uongo, kupunja, kuiba, kutumia usemi wenye matusi, mchafu au mpotovu? Bila shaka na watoto wao watafanya yale yale. Je! wazazi ni wenye maisha ya uaminifu na safi, wakizishikilia sana kanuni za Biblia? Basi inaelekea sana kwamba watoto wao watakua wakifanya yale yale.

Kwa habari ya kuiga imesemekana hivi: ‘Mara nyingi anayeiga maovu anapita mfano uliowekwa, hali anayeiga mema mara nyingi hupungukiwa.’ Kwa mfano: ugumu wa kujaribu kuuiga mfano mwema u wazi zaidi kwa Wakristo wote wanaopenda kulitii onyo la mtume Paulo: “Iweni waigaji wangu mimi, hata kama vile mimi ninavyomwiga Kristo.”​—1 Kor. 11:1, NW.

Kwa maana mara nyingi tunapungukiwa katika kuiga mfano mwema, je! isingekuwa hekima kujaribu kuuiga mfano ulio bora kabisa, ulio mkubwa zaidi kupita yote, ulio wa hekima zaidi, wa haki zaidi, wenye upendo zaidi na usio wa kichoyo? Yeye anayeutoa mfano huo bila shaka anajulikana wazi na wasomaji wengi wa gazeti hili, yaani, Muumba, Yehova Mungu. Hata hivyo nyakati nyingine maulizo yanatokea. Je! hilo lawezekanaje? Je! hicho si kiburi tu hata kufikiria kumwiga Mungu? Je! lisingekuwa jambo lenye kuvunja moyo hata kujaribu?

Hapana, hata kidogo. Biblia Takatifu yenyewe inatusihi hivi: “Iweni waigaji wa Mungu, kama watoto wapendwa.” Kwa kweli, Yehova Mungu anaamuru: “Lazima mwe watakatifu, kwa maana mimi ni mtakatifu.”​—Efe. 5:1; 1 Pet. 1:16, NW.

KUWA WENYE UPENDO NA KUSAMEHE

Lakini je! amri hizi za kimungu zawezaje kutimizwa, kwa kuwa sote tu wasiokamilika? Hatuwezi kumwiga Mungu katika kuwa kwake mwenye nguvu zote, wala sisi si huru na dhambi, kama yeye alivyo. Lakini tunaweza kuwa na lengo la kumwiga yeye katika sifa zake za adili. Kwa mfano, twaweza kujaribu kumwiga Mungu kwa kuwa wenye upendo, kwa kuwa na upendo wa kanuni unaoitwa katika Kigiriki agápe. Kuwa mwenye upendo maana yake ni kutokuwa na choyo, kupendezwa na hali njema ya wengine. Tuwe tajiri ama maskini, wazee ama vijana, wenye nguvu ama dhaifu, twaweza kujitahidi tusiwe wachoyo. Mungu alituwekea mfano wa ajabu katika hili, kwa maana yeye aliitoa hazina aliyoipenda zaidi kupita zote kusudi awakomboe wanadamu, kama vile tusomavyo: “Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”​—Yohana 3:16; linganisha Matendo 14:17.

Twaweza kumwiga Yehova Mungu kwa habari ya kutokuwa kwake mchoyo kwa kuitii amri ya Maandiko: “Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema.” (Gal. 6:10) Biblia inasimulia namna upendo wa kimungu unavyoonyeshwa: “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo . . . hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya.” Kwa kadiri tuzoeavyo namna hii ya upendo, ndivyo tutakavyokuwa tukimwiga Yehova Mungu.​—1 Kor. 13:4-7; 1 Yohana 4:8.

Kuwa wenye nia ya kusamehe ni sehemu ya upendo, na katika hili vile vile ni lazima tumwige Mungu. Lazima? Ndiyo, kwa maana tusipomwiga yeye katika hili Yeye hatatusamehe. Yesu Kristo aliirudia-rudia kanuni hii kwa kutia mkazo. Alisema kwamba asiyesamehe wengine, naye Mungu hatamsamehe yeye. (Mt. 6:12-15) Wakati mwingine Yesu alitoa mfano mrefu juu ya jambo hili, uliomalizia na onyo lake: “Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.” (Mt. 18:35) Ni kwa habari ii hii ya kusameheana mtu na mwenzake kwamba mtume Paulo anatusihi tuwe waigaji wa Mungu: “Iweni wenye fadhili kwa mtu na mwenzake, wenye huruma sana, mkisameheana mtu na mwenzake kwa kupenda kama vile Mungu naye kupitia kwa Kristo alivyowasamehe ninyi kwa kupenda. Kwa hiyo, iweni waigaji wa Mungu, kama watoto wapendwa, na mwendelee kutembea katika upendo.”​—Efe. 4:32; 5:1, NW

KICHUKIE ANACHOKICHUKIA MUNGU

Njia nyingine ambayo kwayo sisi watu wasiokamilika walio dhaifu na wanaoweza kufa twaweza kumwiga Mungu ni kwa kukichukia anachokichukia yeye. Je! hata na Mungu anachukia? Ndiyo, yeye anachukia uovu na watenda mabaya wa kukusudia, hata na wanafiki wa kidini. Je! Yesu hakumwiga Babaye katika hili na je! hakuwachukia wanafiki wa kidini? Bila shaka alifanya hivyo, akirudia-rudia kusema: “Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki!”​—Mt. 23:13-33; Yohana 5:19.

Kwamba Yehova Mungu mwenyewe anauchukia uovu kweli kweli na wale wazoeao mabaya inaonekana katika Mithali 6:16-19: “Kuna vitu sita anavyovichukia [Yehova]; naam, viko saba vilivyo chukizo kwake. Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, na mikono imwagayo damu isiyo na hatia; moyo uwazao mawazo mabaya; miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu; shahidi wa uongo . . . naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.”

Kama tukivichukia vitu hivi, tutakuwa tukifanya nini? Kwa upande mmoja, tutakuwa waangalifu tusije tukavizoea vitu hivyo wenyewe, na, kwa upande mwingine, tutaepuka kuwa rafiki za wale wazoeao mambo hayo maovu. “Kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi?” Kwa kweli, twaweza kumwiga Mungu kwa kuwa waaminifu kwa kanuni zake zenye haki na kwa njia hiyo ‘tuwe watakatifu kama yeye alivyo mtakatifu.’​—2 Kor. 6:14; 1 Pet. 1:16.

WAIGAJI KATIKA UVUMILIVU

Kwa kutaja njia nyingine moja tu ambayo katika hiyo sisi wanadamu twaweza kumwiga Mungu, kunayo sifa ya uvumilivu, nguvu za kushikilia kazi zetu, kuziondoa nadhiri zetu na kutimiza ahadi zetu. Je! Mungu Mwenye Nguvu Zote na mwenye hekima yote Yehova, anaweza kuvumilia mambo kweli kweli? Jambo fulani likituudhi tuweze kulizuia, lakini tuchukuliane nalo kwa sababu fulani nzuri, hapo yaweza kusemwa tunalivumilia jambo hilo lenye kuudhi, sivyo? Ndivyo na Yehova Mungu. Uovu wote, udhalimu wote, taabu yote na zaidi mateso yote ya watumishi wake waaminifu yanamtia uchungu yeye. Yeye angeweza kuyazuia haya mara moja kwa kuwaondoa waovu wote, lakini kufanya hivyo kungewanyima wengine nafasi ya wokovu. Kwa hiyo twasoma: “[Yehova] hakawii kuitimiza ahadi yake,” kama vile ahadi yake ya kuumaliza uovu na kurudisha hali za paradiso katika dunia hii. “Bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.”​—2 Pet. 3:9.

Vile vile, kwa kuwa Yehova Mungu ni mwenye huruma, ameombwa msaada wa kuvumilia. Kwa hiyo twasoma kwamba Israeli, watu wake, walipopatwa na taabu, yeye naye alitaabika: “Katika mateso yao yote yeye aliteswa.” (Isa. 63:9) Yeye amevumilia vile vile kwa maana amevumilia karibu miaka elfu sita jina lake likisutwa, tangu wakati ambapo Shetani Ibilisi alipomwita Mungu mwongo katika bustani ya Edeni kufikia wakati huu ambapo wengi wanaeneza fundisho la kwamba “Mungu amefariki.”​—Mwa. 3:1-5.

Imetupasa tumwige Mungu kwa habari hii. Imetupasa tuonyeshe huruma kwa kuchukuliana kwa uvumilivu na masumbuo na mambo yenye kuudhi yaliyosababishwa na makosa ya wengine. Hatutaona uchungu kwa sababu waovu wanasitawi, wala haitupasi tuzifanyie serikali jeuri kwa sababu ya zinayoyaruhusu, bali, imetupasa kuzoea uvumilivu. Usipoweza kuyasawazisha mambo kulingana na kanuni za Biblia, basi mwige Yehova kwa kuonyesha wazi sifa hii ya kimungu ya uvumilivu. Kumbuka, Mungu ameahidi: “Bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo.”​—Zab. 37:1-11.

Kwamba yawezekana kwa kweli kwa wanadamu wasiokamilika kumwiga Mungu katika mambo haya na mengine inaonyeshwa kila siku na mashahidi wa Kikristo wa Yehova zaidi ya milioni moja na nusu. Wao wanampenda Mungu sana na mwanadamu mwenzao hivyo kwamba wanatoa wakati wote wawezao kutoa bila choyo kwa kuzihubiri habari njema za ufalme wa Mungu na katika kufanya wanafunzi. Wao wanamwiga Mungu kwa kuwa wenye kusamehe, kutolipiza kisasi kwa wale wawatesao. Na wanaiiga chuki ya Mungu ya yaliyo mabaya kwa kuzoea haki. Wanaonyesha uvumilivu kwa kuuendeleza utendaji wao ulioamriwa na Mungu, mwaka kwa mwaka, bila ya kujali mateso, kwa uvumilivu wakimngojea Yehova Mungu ayatengeneze mambo.

Sababu gani usionane na mashahidi wa Yehova upesi uwezavyo? Wakaribishe mara nyingine wakufikiapo mlangoni pako, au upange wakutembelee. Watafute katika kitabu cha simu. Wao watakuonyesha namna wewe vile vile unavyoweza kuwa mwigaji wa Mungu, kwa utukufu wa Mungu na kwa wokovu na baraka yako mwenyewe ya milele.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki