Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 10/15 kur. 459-460
  • Je! Wewe Unataka Nini Kutoka kwa Serikali?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unataka Nini Kutoka kwa Serikali?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Habari Zinazolingana
  • Mahitaji Wanayotazamia Watu Kutimiziwa na Serikali
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Kuwa Raia wa Serikali ya Mungu
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Afya Na Furaha—Waweza Kuzipataje?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Namna Mahitaji Yetu Yatakavyojazwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 10/15 kur. 459-460

Je! Wewe Unataka Nini Kutoka kwa Serikali?

TUNAPOSOMA matangazo ya wanasiasa na watawala tunaona kwamba wana ujuzi wa mambo mengi ambayo ni ya lazima kwa wanadamu kuwa wenye furaha. Wanasiasa wanajua la kuahidi ili kupigiwa kura na watu. Uhakika huu unaonyesha kwamba viongozi wa ulimwengu kwa jumla hawakutupilia mbali au kusahau wajibu wao kama viongozi wa watu. Lakini watu wengi wangekubali kwamba matakwa haya hayakutolewa mara nyingi. Je! huku ni kutazamia mengi mno kutoka kwa serikali?

Kwa kweli, kutaka kwa wanaume na wanawake kuwa wenye furaha hakuna haja ya maneno mengi. Ni mambo machache ya kawaida ambayo ni ya lazima. Kwa mfano, watu hawatazamii serikali kuwapa mahitaji yote ya maisha. Wala hawataki serikali inayowawekea kanuni ya kila tendo la maisha yao. Wanataka uhuru kufanya kazi wanayoweza kufurahia, wakiwa na uhakika wa kwamba sikuzote watafanya kazi ili kuruzuku jamaa zao. Wanatamani kuwa na wakati wa kufurahia matunda ya kazi yao, kuishi na jamaa zao kwa amani, bila woga wa shambulio, unyang’anyi au masumbufu. Wangeshukuru kuwa na mazingira safi, yasiyotiwa uchafu, sehemu zisizo na fujo kwa tafrija, ambapo uzuri wa uumbaji wa asili na wanyama wa pori unaweza kufurahiwa.

Ili wanaume na wanawake wawe wenye furaha kweli kweli, lazima vile vile wawe huru. Lazima wawe na uhuru wa kuwaza, uhuru wa ibada, uhuru wa kusema wanachoamini, kukusanyika pamoja na kutenda kama waonavyo inafaa, mradi tu hawaingilii uhuru na haki za wengine.

Je! wewe usingekuwa mwenye furaha kuishi mahali penye uhuru kama huo na salama? Ni serikali nzuri peke yake, pamoja na ushirikiano wa watu wake, ndiyo inayoweza kuhakikisha kuleta vitu hivi. Kama ungeweza kuwa ukipeleka habari bila malipo, kusafiri na kushiriki pamoja na watu wa mataifa mengine mkiwa na urafiki wa kweli, kama usingekuwa na mashaka au kuogopa walikuwa wakikupangia vita, namna hilo lingekuwa jambo la kufariji!

Hapo pana ugumu. Hata kama serikali za kitaifa zingeleta salama na amani ndani ya mipaka yake, hili halingehakikisha amani kati ya mataifa. Ingetakiwa serikali ya ulimwengu kufanya hivyo.

Kuna jambo jingine la lazima kwa furaha, na hilo ni afya ya watu. Nyakati za karibuni, serikali zimefanya mengi katika kupambana na ugumu huu. Kwa kweli, furaha haikamiliki isipokuwa mtu awe mwenye afya njema, na isipokuwa anaowapenda wawe wenye afya vile vile. Na hakuna ye yote anayefurahia afya inayozidi kupendeza, amani na uhuru ambaye anataka kuachana na hali hiyo kwa kufa. Kwa hiyo ili kuwa na furaha ya kweli, isiyotiwa huzuni, ingekuwa lazima woga wa kufa uondolewe. Lakini ni serikali gani inayoweza kufanya hivyo? Ni serikali gani inayoweza kutoa matakwa ya hakika na ya kutosheleza maisha na wakati ule ule itosheleze matakwa ya moyoni na ya kiroho ya raia zake? Au, kuna uwezekano huo?

Je! serikali yo yote inaweza kuyaleta yote, au hata mengi ya mambo haya ya kupendeza na ya lazima kwa watu wake? Je! serikali yo yote inaweza kukazia upendo huo na ushirikiano kati ya watu wake ili kwamba hali zenye kupendeza ziletwe? Au tuna sababu ya kuamini kwamba mwendo wa kuelekea lengo hili unafanywa? Je! maandishi ya utawala wa kibinadamu wa kisasa yanaonyesha nini?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki