Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 3/15 uku. 143
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Kubali Mwongozo wa Mungu Aliye Hai
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Damu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 3/15 uku. 143

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Nyama inapokatwa ikitayarishwa kupikwa, au nyuma ya kuikatakata ikiisha kupikwa, majimaji mekundu huenda yakatiririka. Je! nyama kama hiyo inafaa kuliwa na Mkristo?​—U.S.A.

Mkristo anaweza kula nyama ya wanyama walioondolewa damu yao tu wakati wa kuchinjwa. Biblia inaamuru: “Mjiepushe . . . na damu, na nyama zilizosongolewa.”​—Matendo 15:29.

Kweli, hata nyama ya wanyama walioondolewa damu vizuri huenda ikaonekana nyekundu sana au huenda ikawa na majimaji mekundu juu yake. Hii ni kwa sababu kuondoa damu hakuondoi kila alama ya damu katika mnyama. Lakini sheria ya Mungu haitaki kwamba kila tone moja la damu liondolewe. Inataja tu kwamba mnyama anapaswa kuondolewa damu.

Ndipo, vile vile, kuna majimaji katika nyama ambayo yakichangamana na alama zilizobaki za damu yanakuwa mekundu. Majimaji hayo yaliyo katikati ya chembe yanafanana na yale ya damu. Lakini siyo damu na kwa hivyo hayatiwi katika katazo la damu. Hivyo kuwako kwa majimaji mekundu tu hakufanyi nyama isifae kwa chakula. Mradi tu mnyama ameondolewa damu vizuri, nyama yake inaweza kutumiwa kama chakula kulingana na Maandiko.

Huenda zikawako nyakati, hata hivyo, ambazo Mkristo ana sababu ya kuamini kwamba mnyama labda hakuondolewa damu kwa kufaa. Ikiwa hana njia ya kupata uhakika, anaweza kuchagua kutoila nyama na hivyo aepuke kusumbua dhamiri yake. Hii ni kupatana na kanuni inayotajwa katika Warumi 14:23: “Aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki