Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 3/15 kur. 140-143
  • Je! Unaelekea Kukwazwa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Unaelekea Kukwazwa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UNYENYEKEVU NA KUFIKIRI
  • JIHADHARI NA KUTAFUTA NJIA YA KUTOKEA KWA KUKOSA FURAHA
  • NIA INAYOFAA
  • Wewe Umekwazwa na Mambo Yaliyofanywa na Wengine?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • “Uvumilivu na uwe na Kazi yake Kamilifu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Wenye Uhakika katika Ulimwengu Unaozungukwa na Mashaka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Dumisha Imani Thabiti
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 3/15 kur. 140-143

Je! Unaelekea Kukwazwa?

YESU KRISTO alisema: “Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.” (Yohana 8:31, 32) Mbele ya mtu kuwa mwanafunzi wa kweli wa Yesu Kristo, kutia imani katika dhabihu ya ukombozi na kuwa mfuasi wa Kristo, ni mtumwa wa dhambi na kifo. Inampasa afanye geuzi.​—Yohana 8:34.

Mtume Paulo aliwaonya Wakristo katika Efeso, Asia Ndogo, ‘wavue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya.’ (Efe. 4:22) Ndiyo, utu wa kale ulikuwa na tamaa mbaya ambazo zilipaswa ziondolewe.

Kwa hiyo, mtu anapomjia Mungu kwa msaada wake Yeye, ni lazima awe na nia ya kugeuza akili yake. (Rum. 12:2) Anakuja kufahamu kwamba “jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu, mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao. Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa [roho yake].” Tunapaswa kutengeneza kufikiri kwetu kwa ufunuo huu mpya kwetu.​—1 Kor. 2:9, 10.

Ikiwa unayo maelekeo ya kukwazwa kwa sababu hushiki kabisa maelezo fulani ya Andiko au jambo linalokamatana na tengenezo au mtindo fulani unaokuja kupitia kwa kundi la “mtumwa mwaminifu mwenye akili,” kumbuka hali yako mbele za Mungu. Fikiri: Je! nimehakikisha hali yangu sawasawa? Je! nimeendelea kugeuza akili yangu? Je! nitaacha kufanya hivyo sasa?​—Mt. 24:45-47.

Vile vile, chunguza moyo wako. Jiulize mwenyewe: Je! kuna tamaa, maelekeo fulani, choyo fulani inayonizuia nisiyaone au kuyakubali maoni yenyewe? Je! ni kweli katika kila jambo ninayotafuta, au ninataka mambo fulani yawe kama mimi ninavyotaka?

UNYENYEKEVU NA KUFIKIRI

Unyenyekevu ni wa maana kwa Mkristo ili avumilie mpaka mwisho. Majaribu yanayokuja kutoka kwa mateso mara nyingi si magumu kama kupigana na utu wa kale pamoja na kiburi chake na mikazo yake ya kumpatanisha mtu na tamaa zake. Mtu anayefikiri anajua zaidi kupita kundi la Kikristo anapaswa kujiuliza mwenyewe: ‘Je! najua kabisa historia ya watu wa Mungu?’ Labda mambo unayoshauri au namna unavyotaka mambo yafanywe tayari yamekwisha jaribiwa miaka iliyopita na kuonekana ni makosa. Fikiri: ‘Je! nina hekima kuu zaidi kuliko wale ambao wamemtumikia Yehova Mungu kwa uaminifu kwa makumi ya miaka, ambao wametumia maisha zao katika uchunguzi, kujifunza na utumishi wa Mungu, wakiongoza kazi ya watu wake duniani kote? Je! Mungu kwa ghafula amenipa hekima kuu zaidi kuwapita hawa?’

Kwa habari hii, fikiria ambayo mtume Paulo aliandikia mwangalizi wa Kikristo Timotheo. Nyuma ya kuwaeleza watu fulani waliopinga kweli, Paulo alisema: “Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao.”​—2 Tim. 3:14.

Ikiwa unayo mashaka, unaweza kufuata shauri hili jema. Ulipojifunza Biblia kuja katika ujuzi wa kweli juu ya Yehova Mungu na Mwanawe Yesu Kristo, ulikuwa unajifunza. Wewe ulihakikisha mambo yenyewe kadiri ulivyoendelea mbele. Ulisadikishwa kuamini mambo uliyokuwa ukijifunza, lakini si kwa sababu ya ujanja au mkazo kwa upande wa aliyekuwa akikufundisha. Pahali pake, Maandiko yenyewe, pamoja na msaada wa roho ya Mungu, yalikusadikisha. Ulisadikishwa kabisa juu ya kweli. Wewe ulijua ulikuwa sawa katika kuikubali. Huenda ukawa uliendelea mbele na kuonyesha imani yote kwa wakf wote kwa Mungu, ukibatizwa “kwa jina la Baba, na Mwana, na [roho takatifu].” (Mt. 28:19) Kwa sababu hiyo, ulisema, ‘Ninakuja kufanya mapenzi yako, Ee Mungu.’ (Ebr. 10:7) Ulifanya hivyo kwa hiari, kutoka moyoni mwako. Sababu gani, sasa, utilie shaka kile ambacho wakati mmoja ulikikubali kabisa na kuamua? Sababu gani ukwazwe na labda kuondoka katika njia hii ya ujuzi unaoendelea kuongezeka, kwa sababu ya jambo moja au mawili usiyofahamu kabisa?

Vile vile, fikiri “ni akina nani ambao ulijifunza kwao” mambo haya. Je! walikuwa wakitaka fedha yako? Je! walikuwa pale kukudanganya, kukutumia kwa kujifaidi wenyewe? Au walikuwa wapumbavu na wasiweze kukufundisha mambo ya msingi ya Mungu? Je! kundi ambalo ulishirikiana nalo lilizoea kazi mbovu, kwa unafiki wakijifanya kuwa waalimu wa kweli? Pahali pake, je! hawakupendezwa zaidi katika hali yako ya kiroho kupita ye yote alivyokuwa amefanya mbeleni?

Timotheo alijua kwamba mama yake na bibi (nyanya), na nyumaye, mtume Paulo na Wakristo wengine, walikuwa wamemfundisha wakipendezwa na faida zake bora mioyoni mwao. Vile vile, mfano wao ulikuwa mwema. Lakini Paulo alijua ilimpasa kuyasema mambo haya kwa Timotheo kumtia nguvu kwa majaribu na, inawezekana, mashaka ambayo huenda yangemjia.

Kwa hivyo, ikiwa unaelekea kukwazwa, inakupasa ufikirie maneno haya ya Paulo na, zaidi, shauri lake kwa Wakristo Waebrania katika Yerusalemu. Aliwaonya: “Wakumbukeni wale waliokuwa wakiwaongoza, waliowaambia neno la Mungu; tena, kwa kuuchunguza sana mwisho wa mwenendo wao, iigeni imani yao.”​—Ebr. 13:7.

Ndiyo, shikamana na mwendo wa uaminifu. Je! unataka mwenendo wako uweje? Mzuri, bila shaka. Kwa uzima, bila shaka. Basi una kanuni katika maneno ya mtume: ‘Iga imani yao.’ Ndugu hawa wamebaki katika imani yao; wao ‘wamemngoja Yehova.’ (Zab. 130:5, 6) Wamevumilia katika majaribu na katika nyakati ambazo maelekeo yasiyo makamilifu ya kibinadamu yangalionyesha mwendo tofauti. “Bayana ya mambo yasiyoonekana” huenda nyakati nyingine ilikuwa vigumu kuiona. Lakini waliendelea kuwa na imani na wana furaha katika kumtumikia Yehova.​—Ebr. 11:1.

JIHADHARI NA KUTAFUTA NJIA YA KUTOKEA KWA KUKOSA FURAHA

Kwa habari ya jambo hili la furaha, kuna njia nyingine ambayo kwayo unaweza kujaribu hali yako. Uliza, ‘Je! mimi nina furaha; napata furaha ya kweli katika kumtumikia Yehova?’ Ikiwa umepoteza furaha yako, kuna hitilafu fulani, lakini si katika Yehova au watu wake. Ni wewe unayekosa jambo fulani. Umepoteza kadiri fulani ya hali yako ya kiroho. Ikiwa unarudi nyuma, bila kuwa na ushirika wenye furaha​—kwa moyo wote​—pamoja na ndugu zako, ikiwa unajitenga mwenyewe, ukifikiria yako mwenyewe, jihadhari! Ni ishara ya kukuonya. Mithali iliyoongozwa na roho ya Mungu inasema: “Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe; hushindana na kila shauri jema.”​—Mit. 18:1.

Ukiona kwamba umekwazwa au kusumbuliwa na jambo linalofundishwa katika tengenezo la Mungu, au marekebisho fulani yanayofanywa, kumbuka hili: Mungu ameweka ya kutosha katika Biblia kutoa msingi wote kwa imani. (2 Tim. 3:16, 17) Vile vile aliacha mengine ya matukio mbalimbali yasiandikwe katika Biblia, ili kwamba mtu ambaye moyo wake si wenye haki, anayetaka kutoa kosa, anayetaka kupata udhuru kwa kuiacha njia ya kweli, aupate.

Vivyo hivyo Yehova amepanga kabisa hali njema ya kiroho ya watu wake wote kupitia kwa kundi la Kikristo. Ukisikia maneno yenye mashaka au kuona matendo yenye mashaka, hata kosa au matendo yaliyokosewa, kwa upande wa mtu fulani katika kundi, usikwazwe na kupoteza kibali cha Yehova kwa sababu ya hilo. Kwa sababu kundi la Mungu, kwa kweli, limefanyizwa na wanadamu wasio wakamilifu, mtu asiyempenda Yehova kwa kweli na watu wake bila shaka anaweza kupata udhuru wa kuondoka. Mtume Yohana aliandika kwamba wengine walikuwa wamekengeuka. Alisema: “Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu. Maana kama wangalikuwa wa kwetu, wangalikaa pamoja nasi. Lakini walitoka ili wafunuliwe kwamba si wote walio wa kwetu.” (1 Yohana 2:19) Yehova alitaka namna ya waaminifu, wenye kupenda, wenye kufahamu, namna ya ambao wanavumilia. Wale walioondoka bila shaka waliona jambo la kulalamikia ambalo lilitetea matendo yao akilini mwao wenyewe na mioyo. Lakini “[Yehova] awajua walio wake.” Msingi ulio imara wa kundi lake hautashindwa. Alimwongoza mtunga Zaburi kwa roho yake kuandika: “Wana amani nyingi waipendao sheria yako, wala hawana la kuwakwaza.”​—2 Tim. 2:19; Zab. 119:165.

NIA INAYOFAA

Taabu, mashaka na sababu za kukwazwa vitatokea. Je! mtu atafanya nini, wakati huo? Mtume alionyesha roho wanayopaswa wote kuwa nayo aliposema: “Nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele; nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu. Basi sisi tulio wakamilifu natuwaze hayo; na hata mkiwaza mengine katika jambo lo lote, Mungu atawafunulia hilo nalo. Lakini, hapo tulipofika na tuenende katika lilo hilo.”​—Flp. 3:13-16.

Ikiwa unazo taabu, majaribu, au ukiona mambo usiyoweza kufahamu kabisa kwa kadiri unavyoifahamu kweli, sali kwa Mungu. Yakobo anasema: “Mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa. Ila na [aendelee kuomba] kwa imani, pasipo shaka yo yote.” (Yak. 1:5, 6) Mkaribie Mungu kwa uhuru katika nyakati za majaribu makali au hukumu nzito, kwa kuwa mtume Yohana anasema: “Katika hili pendo limekamilishwa kwetu, ili tuwe na ujasiri katika siku ya hukumu.” (1 Yohana 4:17) Kama tukikaribia “kiti cha neema” wakati wo wote wa lazima, tunaweza kwa matumaini kutazamia msaada. Mungu ndipo atafunua nia inayofaa kwetu.​—Ebr. 4:16.

Halafu, tenda kulingana na sala zako. Fikiria: Ni kwa kadiri gani nimefanya maendeleo katika utumishi wangu kwa Yehova? Nimeyafanya wapi? Haikuwa kupitia kwa funzo la Neno la Mungu, ushirika pamoja na watu wa Mungu, kutumia kanuni za Biblia katika maisha ya kila siku, kutoa maelezo katika mikutano na kutimiza migawo mingine? Je! haikuwa vile vile kwa kuingia katika utendaji wa kuhubiri? Je! haikuwa katika njia hizi kwamba ulisitawisha uhuru wako wa kusema katika imani na uwezo wako kutoa habari njema kwa wengine? Basi, Paulo anashauri, “na tuenende katika lilo hilo.”

Ukifanya mambo haya ukiwa katika hatari ya kukwazwa, Mungu atarudisha furaha yako katika kumtumikia, na utaweza kuonyesha alilosadiki mtume Paulo, ambaye aliandika: “Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.”​—Rum. 8:38, 39.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki