Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 12/15 uku. 575
  • Kweli ya Biblia Inawafikia Watu Kwa Njia MbaliMbali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kweli ya Biblia Inawafikia Watu Kwa Njia MbaliMbali
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Habari Zinazolingana
  • “Umtazame Mtu Mnyofu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • “Kutoka Kinywani mwa Watoto Wachanga”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Furaha ya Kutimiziwa Mahitaji ya Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Mwenendo Mwema Unavuta
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 12/15 uku. 575

Kweli ya Biblia Inawafikia Watu Kwa Njia MbaliMbali

YEHOVA Mungu anapendezwa kabisa na hali njema ya milele ya wanadamu. Maandiko Matakatifu yanatupa sisi matumaini ya kwamba ni mapenzi ya Mungu kwamba “watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli.” (1 Tim. 2:4) Na leo watu kwa kweli wanafikiwa na habari ya Biblia, nyakati nyingine katika njia za ajabu sana.

● Shahidi kutoka Canada anasimulia: “Nilikuwa nikifanya kazi katika duka la kahawa jioni moja. Kati ya wale wanaofanya kazi usiku alikuwa kijana wa kike ambaye sikuwa nimeona mbeleni. Kama ilivyokuwa tabia yake, mmoja wa wafanya kazi alianza kufanya mzaha wa mambo ya ufisadi. Niligeuka na kuondoka kwa kuchukizwa. Bila ya mimi kujua, kijana mpya wa kike aliwauliza wengine wa vijana wa kike, ‘Kuna nini kwa yule?’ Walimwambia kwamba nilikuwa mmoja wa mashahidi wa Yehova. Ingawa kijana huyu wa kike aliishi katika mtaa wangu, sikumwona tena mpaka wakati fulani nyumaye tulipokutana katika duka dogo la vyakula.”

Matokeo yalikuwa nini? Kwa sababu ya kuona kushikamana kwa Shahidi na kanuni njema, kijana huyo wa kike alikubali kuwa na funzo la Biblia la nyumbani na nyuma ya mwaka mmoja akawa Shahidi aliyebatizwa.

● Katika Italia, mmoja wa mashahidi wa Yehova ambaye siku mbalimbali za juma anasaidia mumewe katika kazi ya duka la matumizi ya umeme yu macho kuwafahamisha wengine habari ya Biblia. Siku moja mtu alikuja kununua taa ya mezani. Nyuma ya kuonyeshwa taa mbalimbali, aliuliza kama angeweza kuona kama taa zenyewe ni nzuri kwa kitu fulani cha kusoma. Kwa haraka Shahidi alimpa msaada wa kujifunza Biblia “Mambo Mawili Yasiyobadilika Asiyoweza Mungu Kusema Uongo,” akafungua penye sura “Kuachiliwa kwa Uovu na Mungu Karibu Kumalizika.” Mtu huyo alianza kusoma Shahidi akimshughulikia mnunuzi mwingine.

Dakika nyingi zikapita. Nyuma ya kusoma kurasa chache katika sura hiyo, huyo mtu aliuliza maulizo fulani juu ya mambo yenye kupendeza aliyokuwa amesoma na kuomba nakala ya kitabu hicho. Alipokipokea, alielekea mlangoni. “Lakini hukutaka kununua taa?” Shahidi akamkumbusha. Taa haikumpendeza tena, lakini alikubali mara moja kuwa na funzo la nyumbani la Biblia.

● Mume na mke katika Tahiti walipata vitabu kadiri fulani kutoka kwa mashahidi wa Yehova walipowatembelea nyumbani mwao. Lakini mume na mke hawakuwa na kupendezwa ko kote katika kusoma vitabu hivyo. Nyumaye walinunua nyumba mpya katika eneo jingine. Huko Mashahidi wawili waliwatembelea, wakafukuzwa na mume yule. Nyuma ya kisa hiki mke alimwuliza mumewe kuondoa vitabu katika banda la motokaa, akitupa vile visivyotakiwa tena. Alipokuwa akichunguza vitabu mbalimbali, alikiona “Mambo Mawili Yasiyobadilika Asiyoweza Mungu Kusema Uongo.” Akikumbuka ziara ya karibuni ya Mashahidi, akajiambia mwenyewe, “Hiki ni kimojawapo cha vitabu vyao.”

Alipokuwa karibu kukitupa alikifunua na kutazama aya moja. Ilivuta fikira zake. Kwa hiyo akakaa chini na papo hapo akakisoma kitabu toka jalada mpaka jalada, akikimaliza usiku huo nyumaye.

Siku iliyofuata akasoma katika gazeti kwamba mashahidi wa Yehova walikuwa na kusanyiko. Alihudhuria kusanyiko hili pamoja na mkewe. Kwa kuvutwa na aliyosikia, alipata vitabu zaidi. Majuma matatu nyumaye funzo la Biblia lilianzwa naye na mkewe. Karibuni akaanza kushiriki na wengine mambo mema aliyokuwa akijifunza kutoka katika Neno la Mungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki