Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 2/1 kur. 55-61
  • Uangalizi Wenye Upendo wa Kundi la Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uangalizi Wenye Upendo wa Kundi la Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “KUNDI”​—NI NINI?
  • KUWEKA KWA KITHEOKRASI KATIKA KUNDI
  • VYEO VITANO VIKUBWA VYA UANGAUZI
  • SEHEMU NYINGINE ZA UANGAUZI
  • Waangalizi Wanaochunga Kundi
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Kushirikiana Kabisa na Waliowekwa wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Kundi la Kikristo na Utendaji Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Usitawi wa Muundo wa Tengenezo
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 2/1 kur. 55-61

Uangalizi Wenye Upendo wa Kundi la Mungu

“Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha.”​—1 Tim. 5:17.

1. Ni maulizo gani juu ya tengenezo la mashahidi wa Kikristo wa Yehova inawezekana yamekumbukwa na watu fulani wanaposoma Mnara wa Mlinzi?

KAMA msomaji wa gazeti hili, bila shaka unajua jambo fulani juu ya tengenezo la kisasa la mashahidi wa Kikristo wa Yehova. Huenda ikawa hata unafahamiana kabisa na tengenezo lenyewe na kazi zake mbalimbali. Labda wewe unatumikia katika cheo fulani katika hilo au chini ya uongozi wake. Kwa upande mwingine, huenda ikawa kwamba unayojua juu ya tengenezo lenyewe ni machache, hata hivyo unafurahia kusoma gazeti hili. Kwa tumaini, unalisoma kwa kawaida kwa sababu unajua kwamba habari linayotoa inakamatana na jambo fulani ambalo katika hilo unaweza kuweka matumaini yako, yaani, ufalme wa Mungu. Lakini, huenda ukakumbuka maulizo fulani unaposoma gazeti hili, inawezekana yanayofanana na haya: Je! mashahidi wa Yehova wanafanikiwaje katika kazi zao za kuhubiri na uchapishaji za ulimwengu wote? Je! ni watu wa namna gani wanaotumiwa kuongoza kazi? Ni mazoezi ya namna gani wanayopokea wale wanaopewa vyeo vya uangalizi kukamatana na kazi ya mashahidi wa Yehova?

2. Toa mifano fulani ya uangalizi na namna unavyotia ndani mambo mengi,

2 Uangalizi​—tunadhani, ni neno lijulikanalo sana na wengi wetu, lakini maana yake ni nini? Mama anamtazama mtoto wake akicheza; mwalimu anayasikiliza kwa makini majibu ambayo wanafunzi wake wanatoa kwa maulizo yake; kiongozi wa tarabu, kwa roho na uchangamfu, anaongoza kikundi kikubwa kuimba wimbo unaojulikana sana. Hali hizi zote zina jambo moja la kawaida: uangalizi au usimamizi, uangalizi unaotolewa na mzazi, mwalimu, kiongozi. Uangalizi unaonyeshwa kwetu katika sehemu zote za maisha, tangu tunapolelewa kama watoto wadogo na kuendelea. Uangalizi ni sehemu ya maisha. Kwa kweli, mtu anaweza kuepuka uangalizi mwingi wa kibinadamu kwa kujitenga kabisa tu na ulimwengu, na hilo si shauri la kupendeza.

3, 4. (a) Taja faida fulani za uangalizi. (b) Ni uangalizi wa namna gani wenye matokeo zaidi na unaoshukuriwa?

3 Uangalizi, ukizoewa inavyofaa, utatuletea faida nyingi. Kwa mfano, kupitia kwa mazoezi yenye upendo na yanayolingana na Maandiko ya uangalizi wa wazazi, tunakuwa watu wenye nguvu na waliokomaa, kwa kimwili, katika akili, kwa adili na kwa kiroho. Kupitia kwa uangalizi wenye hekima wa mwalimu, tunakuwa watu wenye ujuzi, wenye akili. Katika muziki wa tarabu ustadi wa kikundi chote cha watu wenye ujuzi unapatanishwa sawasawa kwa njia ya uangalizi wenye hekima na matokeo ni furaha​—furaha kwa kila mmoja wa wale wanaoshiriki katika kuzidisha furaha ya kusikiliza ya wengine.

4 Uangalizi wenye upendo unaoongozwa vizuri, na kusimamiwa kwa uaminifu unayafikiria maoni ya moyoni ya wanaoangaliwa. Hii nayo inaweza kufanya utii, kushirikiana, na kukubalika kwa uangalizi kuwe furaha ya kweli. Ikiwa uangalizi wenyewe ni wenye upendo na wa uaminifu, mengi yanaweza kutimizwa.

5. Eleza linalotukia ambapo uangalizi wa wazazi haupo.

5 Ni jambo la kushukuriwa kwamba wazazi wana sehemu kubwa ya kushika katika kuleta hali ya heshima kwa wote wawili na furaha katika jamaa zao. Uangalizi wa namna hiyo usipotolewa, magumu yanatokea. Katika makala moja yenye kichwa “Wazazi Ambao si Wenye Upendo Walaumiwa kwa Sababu ya Kizazi Kikaidi,” Detroit Free Press la Jumamosi, Mei 16, 1970, lilisema yafuatayo: “‘Wazazi wanaoona ni vigumu zaidi kuwapenda watoto wao kuliko kuwapa fedha, wanaowalea bila kupenda na hata kuwaadhibu bila kupenda, wameshiriki katika kuleta kizazi cha wakaidi wa vyuo vikuu,’ alisema daktari wa akili wa Harvard University siku ya Ijumaa. Dr. A. M. Nicholi alisema, ‘Matakwa ya wakati juu ya baba wenye kufanikiwa sana​—au hata juu ya baba wengi wasiofanikiwa sana wenye kazi mbili​—yanakuwa na matokeo ya nyumba zisizo na washiriki wenye kupatana. Zaidi ya hayo, saa anazotumia mama nyumbani na ubora wa kukamatana kwa mama na mtoto vinaendelea kupungua.’”

6. Tunaweza kwenda wapi ili kupata mambo yanayofaa na yenye msaada juu ya uangalizi wenye upendo? Sababu gani?

6 Je! ungesema kwamba kuna magumu ya kushindwa katika sehemu ya kukamatana kwa kibinadamu? Kwa wazi yako. Tunaweza kwenda wapi, basi, kupata mambo ya kufaa juu ya uangalizi wenye upendo na utii wa hiari, ili tuwe watu wa maana, wenye furaha, wenye kuleta sifa kwa ushirika wetu na Mungu wetu? Tunafaidika sana kwa upande huu tunapochunguza umbo na kazi ya kundi la Kikristo leo, kwa sababu ya ukamilifu wake kwa mfano wake wa karne ya kwanza unaoelezwa kwa ajili yetu katika Maandiko.​—Matendo 15:2, 22, 23; 16:4, 5.

“KUNDI”​—NI NINI?

7. (a) Maana ya “kundi la Kikristo” ni nini? (b) Ni faida gani zitakazoletwa na Yesu Kristo na “kundi” hili hivi karibuni? Namna gani?

7 Sasa, tunaposema “kundi la Kikristo,” maana yake ni nini? Kwa maoni ya Maandiko na mafundisho, kundi la Kikristo kwa wazi lina wanafunzi 144,000 wanaosemwa kama “mwili” wa Kristo, ambao Kristo Yesu ndiye Kichwa chake. Wanafunzi wenyewe wamechaguliwa na Mungu kufanya pamoja na Masihi Yesu tengenezo la kimbinguni lenye ufalme wa Kimasihi wa Mungu. (Kol. 1:18, 24, NW; 2 The. 2:13) Karibuni Yesu Kristo na “kundi” hili, waliotukuzwa mbinguni, watatoa faida za ajabu kwa wanadamu wote. Faida hizi zitatiririka kupitia kwa taratibu mpya ya mambo ambamo upendo, furaha na amani vitakaa, sio chuki, uvunjaji wa sheria na huzuni. Wakati huo utakuwa wakati wa kufurahi kweli kweli, ambapo hata wafu watafufuliwa na dunia yote ifanywe kuwa paradiso chini ya serikali ya Kifalme ya kimbinguni ya Mungu, ambayo itatoa uangalizi wenye upendo kwa wanadamu wote.​—Dan. 7:14, 18; Yohana 5:28, 29; Ufu. 21:1-5.

8. (a) Eleza namna neno “kundi” linavyotumiwa katika mazungumzo haya. (b) Je! tuna mfano gani wa Maandiko kwa matumizi haya? Eleza.

8 Lakini kwa ajili ya mazungumzo yetu hapa, neno “kundi” linatumiwa likiwa na maana ya makusanyiko ya mahali pale pale ya watu wa Kikristo walio sehemu mbalimbali za dunia yote po pote ambapo watu wanajikusanya pamoja kwa kawaida kujifunza juu ya mapenzi ya Yehova kwao. Mfano wa Maandiko kwa kuyaita makusanyiko hayo ya sehemu wanayoishi watu “makundi” unaonyeshwa waziwazi katika Matendo 8:1, 1 Wakorintho 11:16 na Warumi 16:3, 4 (NW). Na, kulingana na 1973 Yearbook of Jehovah’s Witnesses, kuna makundi kama hayo 28,407 katika nchi 208 ulimwenguni mwote.

9. (a) Ni jambo gani lilisemwa mbeleni juu ya kundi la Kikristo na ukuzi wake? (b) Je! tunaona uhakika wake leo? Eleza.

9 Je! kundi la Kikristo ni wonyesho wa nini leo? Kwa wazi ni wonyesho wa upendo na hekima ya Mungu. Hakuna anayeyajua na kuyatunza matakwa yetu zaidi ya afanyavyo Yeye. (Zab. 145:14-16) Alijua na akaeleza mbeleni kwamba ibada ya kweli ingeyavuta maelfu ya watu wenye mioyo minyofu na kwamba ingetakiwa wafundishwe, waelimishwe, na kusaidiwa mpaka waweze kufanya wanafunzi zaidi kama wao wenyewe. (Isa. 54:13; 60:22; Mt. 28:19, 20) Kwa kweli, wahudumu 434,906 waliobatizwa juzijuzi wa mashahidi wa Kikristo wa Yehova wameongezwa katika kazi inayopanuka ya hawa Wakristo waliojiweka wakf katika muda wa miaka mitatu tu iliyopita.

KUWEKA KWA KITHEOKRASI KATIKA KUNDI

10. (a) Tafadhali eleza uongozi wa kundi la Kikristo. (b) Je! ni kitu gani kinalolifanya kundi liwe la kitheokrasi katika umbo?

10 Lakini ni nani anayeongoza kundi hili linalopanuka kwa kasi, huenda ukauliza? Je! ni mtu mwenye akili sana, mwanadamu fulani ambaye ni kiongozi mwenye ufundi mwingi? Hapana, kwa maana kundi la Kikristo linaongozwa kitheokrasi, maana yake ikiwa ni kwamba linaukubali uongozi wa Yehova Mungu tu kama unavyoendeshwa kupitia kwa Mwanawe ambaye ni Mfalme aliyetawazwa, Yesu Kristo. (Isa. 33:22; Ebr. 12:2; Ufu. 19:16) Hili ndilo jambo linalofanya kundi liwe la kitheokrasi katika umbo, kushikilia utawala wa Kimungu. Ikiwa tengenezo fulani ni la kitheokrasi kabisa, ni lazima liongozwe kabisa na Mungu na nguvu anazoongoza. Ni jambo la maana, basi, kila mmoja akubali kwamba Yesu Kristo ndiye Kichwa cha kundi la Kikristo, na vile vile aonyeshe heshima inayostahili kwa wale waliomo duniani ambao wamewekwa kitheokrasi katika vyeo vya uangalizi.​—Flp. 2:9-11; 1 Kor. 11:3; Matendo 14:23.

11. (a) Eleza kukamatana kwa baraza inayoongoza na kundi la “mtumwa mwaminifu mwenye akili.” (b) Inawezaje kusemwa kwamba kila mmoja anayewekwa kwa uangalizi amewekwa na roho takatifu?

11 Watu fulani katika kundi la Yehova la Kikristo wana madaraka makubwa ya Uangalizi. (Luka 12:48) Kwa mfano, washiriki wengine wa baraza inayoongoza vile vile ni washiriki wa baraza ya viongozi ya Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania. Tena, baraza inayoongoza inafanywa na washiriki wa kundi la “mtumwa mwaminifu mwenye akili” anayetajwa katika Mathayo 24:45-47, na inawakilisha kundi hilo. Kama baraza inayoongoza inawaweka wazee na watumishi wa huduma wanaoshika vyeo katika kundi la Kikristo. Wao nao wanafanya kazi ya maana katika migawo yao mbalimbali, yote wakifanya kwa utukufu wa Yehova. Kwa kuwa kila mtu anayewekwa na baraza inayoongoza anatumikia katika cheo fulani cha uangalizi, kila mmoja anayewekwa ni lazima atimize sifa fulani kama zinavyoonyeshwa na Yehova Mungu katika Neno lake Biblia. Kila anayewekwa basi anaweza kusemwa amewekwa na roho takatifu ya Mungu, wala si na mwanadamu ye yote. Hii vile vile inaonyesha waziwazi kwamba kundi ni la kitheokrasi.​—Mt. 23:8-12; Matendo 13:2-5; 2 Pet. 1:20, 21.

12. Eleza walio na wajibu wa kuendeleza kazi katika makundi ya mahali pale pale wanapoishi.

12 Walio na madaraka zaidi ya kuendeleza kazi katika eneo la mahali pale pale wanapoishi ni hawa wenye kuwekwa wa pekee katika kundi. Wanawekwa na roho takatifu kulichunga kundi la Mungu na kuweka mfano unaofaa. (Matendo 20:28; 1 Tim. 4:12; 1 Pet. 5:2) Kadiri ionekanavyo wao ni watu wa kawaida, zaidi, wanaowekwa kama wazee au waangalizi. Wao ni “wazee,” kama inavyoonyeshwa katika 1 Timotheo 5:17. Wanatumikia pamoja kama “baraza ya wazee.” (1 Tim. 4:14, maelezo ya chini, NW) Hutawafahamu watu hawa kutokana na vazi lo lote lisilo la kawaida, au kutokana na majina yo yote ya kidini. Huenda hata ukafanya kazi karibu karibu na mmoja wa wanaume hawa kazini pako katika banki, duka la vyakula, au katika mjengo fulani. Lakini, ingawa huenda wakawamo katika kazi ya kimwili ya kawaida, iliyo ya maana ili kuyatunza madaraka yao ya jamaa, wao zaidi ni wahudumu wa Mungu na waangalizi waliowekwa katika kundi.

13. (a) Je! mtu anastahilije kuwa mwangalizi? (b) Kazi kubwa za waangalizi ni zipi? (c) Je! wanapata mazoezi ya pekee kwa kazi yao?

13 Je! kustahili kama mwangalizi ni jambo la ukubwa? Hapana, kanuni ni moja ambayo ni ya kiroho. Sifa za Maandiko kwa waangalizi zimewekwa katika 1 Timotheo 3:1-7 na Tito 1:5-9. Kila mwangalizi anayewekwa na baraza inayoongoza ya “mtumwa mwaminifu mwenye akili” ni lazima atimize sifa hizi. Basi, je! kazi zao za maana ni zipi? Kazi zao ni ‘kulichunga kundi la Mungu,’ kuona kwamba wote katika kundi wanasaidiwa kutimiza wajibu wao wa kujiweka wakf katika njia inayokubalika na Yehova Mungu, na kwamba wote wanaoishi katika eneo lililogawiwa kundi wanapewa nafasi ya kupokea ushuhuda wote kwa kawaida juu ya Ufalme. Ili kuwawezesha zaidi wanaume hawa kufanya hivyo, na ili waweze kufundisha kwa matokeo mema zaidi, ambalo ni mojawapo la madaraka yao makubwa, mazoezi ya pekee yanatolewa katika Shule ya Huduma ya Ufalme ya Watch Tower Society, inayoendeshwa katika afisi ya tawi ya Sosaiti kwa kusudi hilo.

VYEO VITANO VIKUBWA VYA UANGAUZI

14. Ni jambo gani zaidi linalomwezesha mwangalizi-msimamizi ye yote kufanikiwa katika kazi yake?

14 Kila kundi lina mwangalizi-msimamizi. Je! ni jambo gani linalomwezesha mwangalizi-msimamizi kufanikiwa katika kazi yake? Ni kumwiga Yesu katika kuonyesha upendo kwa “kondoo” na ukarimu kwa wageni wanaoshirikiana na kundi. (Mt. 11:28-30) Chini ya uangalizi wa Kristo Mfalme, kila mwangalizi-msimamizi ni lazima awe kwa njia ya kiroho kama mahali pa kujificha kujikinga na upepo na mahali pa kujificha kujikinga na dhoruba, kama vijito vya maji katika nyika, kama kivuli cha jabali zito katika nchi yenye uchovu.​—Isa. 32:1, 2.

15. (a) Habari gani ilisemwa juu ya mwangalizi-msimamizi fulani? (b) Sababu gani wanaume wa namna hii ni ‘watu wa kuheshimiwa kwetu’?

15 Angalia, tafadhali, aliyosema mwangalizi wa mzunguko mmoja anayesafiri wa mashahidi wa Yehova juu ya mwangalizi-msimamizi fulani katika mzunguko wake: “Ndugu A. alikuwa kama baba, lakini baba ambaye hakuwaendekeza watoto wake, ambaye aliwafundisha kwa ushupavu, akiwasaidia kufanya yaliyo haki. . . . Hakuwa mtu wa kuchukuliwa na fikira, lakini alionyesha upendo mwingi kwa watoto wake pamoja na kuwatia moyo na kuwaonya.” Kwa wazi, wanaume wa namna hiyo ni ‘watu wa kuheshimiwa kwetu.’ (Flp. 2:29) Watu hawa wanawasadia wote katika kundi kukua kufikia kukomaa kwa kiroho na kukuza shukrani ya moyoni kwa kweli. Ujuzi wao na uwezo wa namna mbalimbali, bidii yao kwa huduma na utumishi wao kwa ajili ya kundi chini ya ukichwa wa Kristo kwa kweli vinawaonyesha waziwazi kama “vipawa katika wanadamu.”​—Rum. 12:4-8; Efe. 4:8, NW.

16. Je! mwangalizi wa shambani anatimizaje kazi yake kama mmojawapo wa “wazee” katika kundi?

16 Ili kutoa uangalizi wenye upendo unaotakiwa, kuna wazee wengine wanaoshirikiana na mwangalizi-msimamizi. Kazi za mmoja wa hawa, mwangalizi wa shambani, kwa mfano, ni nyingi, lakini zaidi inampasa apatanishe kazi ya kuhubiri ya Ufalme ya kila kikundi cha wahudumu katika makundi ili kwamba ushuhuda wote utolewe katika eneo. Mwangalizi wa shambani vile vile anaweka maandishi yaliyo sawa ya huduma ya shambani ya kundi. Halafu, mara moja kwa mwezi, ripoti yote ya kuhubiri ya kundi inapangwa na kutumwa kwa afisi ya tawi ya Sosaiti. Mwishowe ripoti zote za tawi zinatumwa kwenye makao makuu ya Sosaiti Brooklyn, New York, na zinawekwa pamoja na kuchapwa katika Yearbook of Jehovah’s Witnesses. Ripoti hii ya kila mwaka vile vile ina mambo ya kupendeza kutoka katika kundi la ulimwengu wote la wahubiri wa Ufalme.

17. Kazi ya mwangalizi wa mafunzo ya Biblia ni ya maana kadiri gani?

17 Mwingine wa “wazee” katika kundi ni mwangalizi wa mafunzo ya Biblia. Yeye anapendezwa kutia moyo na kuendeleza ibada safi katika eneo zaidi kwa kupitia kwa marejeo kwa wanaopendezwa na kutayarisha mafunzo ya bure ya Biblia ya nyumbani. Mashahidi wa Yehova kwa furaha wanafanya marejeo kwa watu wanaopendezwa na kuongoza mafunzo hayo ya nyumbani ya Biblia. (Gal. 6:6) Mwangalizi wa mafunzo ya Biblia anatoa uangalizi unaotakiwa katika sehemu hii ya elimu ya Biblia kwa kuwasaidia watu mbalimbali katika kundi kuanzisha mafunzo mapya na kuyaongoza kwa njia ya kufaidi. Na wanaopendezwa hivi karibuni wanapoanza kuhudhuria mikutano ya kundi, anageuza fikira zaidi kuwaelekea ili kusaidia katika ukuzi wao wa kiroho. Kupitia kwa uangalizi wake wenye upendo na uwezo mzuri wa kufundisha, watu zaidi katika eneo lililogawiwa kundi wanapata ujuzi wa kweli wa Neno la Yehova na kusudi, jambo hili likiwa la maana ili wapate wokovu.​—Matendo 4:12.

18. Sababu gani funzo la Mnara wa Mlinzi ndio mkutano wa maana zaidi wa kundi kwa mashahidi wa Yehova kila juma?

18 Kila juma msaada mkubwa wa funzo la Biblia unaochapwa na mashahidi wa Yehova, gazeti la Mnara wa Mlinzi, unasomwa na kundi lote pamoja. Hii inafanywa kwa njia ya mazungumzo ya maulizo na majibu. Kwa ajili ya mkutano huu kundi lote kwa kawaida linakutana mahali pamoja. Kupitia kwa safu za Mnara wa Mlinzi mwangaza zaidi unakuja juu ya Neno la Mungu kwa kadiri Yehova anavyolijulisha. Kwa sababu ya taratibu ya maana ya mazungumzo haya, funzo la Mnara wa Mlinzi ndio mkutano wa maana kupita yote kwa mashahidi wa Kikristo wa Yehova wote na watu wanaopendezwa. Kwa hiyo, kiongozi wa funzo la Mnara wa Mlinzi, anayesimamia mkutano huu, ana daraka la maana. Funzo hili linawawezesha wote kuungana katika mawazo mamoja.​—1 Kor. 1:10.

19. Mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi anafanya nini kwa faida ya kundi? Eleza faida za shule hii.

19 Mhudumu mwingine aliyeagizwa anayetoa uangalizi wenye upendo kwa njia ya kuwafundisha wengine katika kundi moja kwa moja ni mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Anasimamia Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, mkutano ambao unafanywa katika Jumba la Ufalme jioni moja kila juma. Hii ni shule ya mazoezi inayoendelea bila kukoma kwa wanaume, wanawake na watoto. Wanafunzi wanatoa hotuba fupi za Biblia kwa kikundi juu ya habari zilizogawiwa. Vitabu mbalimbali na vikaratasi vya speech counsel vilivyotengenezwa kwa kusudi hilo vinatumiwa, na mwangalizi wa shule, ambaye ni mshauri anayestahili, anatoa mashauri yenye msaada kwa maendeleo na vile vile ya kulisaidia kundi kupata faida zote kutokana na habari nzuri inayozungumzwa. Nyuma ya muda fulani katika mazoezi haya Biblia inasomwa yote, na mafundisho mbalimbali ya Biblia na habari zinazungumzwa zote. Wote wanaotaka kwa kweli kumtumikia Yehova wanakaribishwa wajiandikishe katika shule hii. Je! wewe umekwisha fanya hivyo?

SEHEMU NYINGINE ZA UANGAUZI

20. (a) Eleza namna kiongozi wa funzo la kitabu la kundi ana pendeleo zuri katika kundi. (b) Sababu gani ni jambo la lazima kwamba awe mwalimu mwema? (c) Ni faida gani zinazowajia waliopendezwa hivi karibuni na vile vile wahudumu wa Ufalme kupitia kwa mpango wa funzo la kitabu la kundi?

20 Kiongozi wa funzo la kitabu la kundi yuna pendeleo la ajabu kukamatana na kufundisha katika kundi. Kwa sababu anafanya kazi karibu karibu na kikundi kidogo cha wahudumu wenzake, ili kuijenga imani yao na kuwasaidia kukamilisha ‘ustadi wa kufundisha’ ili nao vile vile wawasaidie wengine, yeye mwenyewe anapaswa kuwa mwalimu mwema. (1 Tim. 4:15, 16; Tito 2:6, 7) Kwa kusudi hili, mwanzoni mwa juma, kwa kawaida, mashahidi wa Yehova na watu wanaojifunza Biblia nao wanaenda kwenye Jumba la Ufalme au kwenye nyumba iliyo karibu zaidi iliyoshauriwa na kundi kwa funzo la saa moja la kikundi chini ya uongozi wa kiongozi wa funzo la kitabu la kundi, wakitumia Biblia na kitabu kilichotolewa na Watch Tower Society. Hapo unaweza kufahamiana na majirani zako wa karibu zaidi ambao vile vile wanapendezwa kumtumikia Yehova na kuishi katika taratibu yake mpya yenye haki. (2 Pet. 3:13) Kadiri ndogo ya kikundi inawezesha na kutia moyo kuzungumza bila kusita na kujizoeza kutangaza imani yako mbele ya wengine. Wakati ule ule, ujuzi wako unanolewa na maelezo ya wengine wanaohudhuria.​—Mit. 27:17.

21. Je! ni kwa njia gani vitabu na eneo la kuhubiri vinavyotolewa kwa mashahidi wa Yehova?

21 Inawezekana umeona kwamba mashahidi wa Yehova wanatumia mahubiri yaliyochapwa ya Biblia wanapofundisha. Bila shaka, vile vile, umeona kwamba Mashahidi wanatoa gazeti ili hili Mnara wa Mlinzi, pamoja na Awake!, katika huduma yao ya waziwazi ya nyumba kwa nyumba. Vitabu hivi vinatolewa kwao kupitia kwa makundi yao. Kwa kweli, kama wahudumu wa Kikristo wanatoa kwa watu wote magazeti au vitabu, mchafuko ungetokea ikiwa nyumba zingetembelewa kwa mtindo wa kurukaruka. Ili kuzuia jambo hili, kila kundi linagawiwa eneo fulani na Watch Tower Society. (Gal. 2:9) Kwa kupanga mgawo wa sehemu ndogo-ndogo za eneo hilo kwa mhudumu mmoja mmoja, mwangalizi wa shambani anahakikisha nyumba zote zilizo katika mipaka ya kundi zimemalizwa kwa utaratibu.​—1 Kor. 14:33.

22. Mashahidi wa Yehova wanalipaje gharama za maana katika kundi?

22 Ingawa mishahara hailipwi kwa waangalizi na watumishi wa huduma waliowekwa kwa kazi za pekee katika kundi, kutunza Jumba la Ufalme, na vitu kama hivyo, kunachukua gharama fulani, zote ambazo zinalipwa kwa michango ya kujitolea. Hakuna visahani vya sadaka katika makundi ya mashahidi wa Kikristo wa Yehova, hakuna bahasha, sehemu za kumi au orodha za wanaochanga. (Mt. 6:1-4) Kila mmoja yu huru kuchanga atakavyo.​—2 Kor. 9:7.

23. Eleza namna uangalizi wenye upendo unatolewa kupitia kwa kundi lote la Kikristo ulimwenguni kote.

23 Kanuni ya uangalizi wenye upendo inaonekana wazi, si juu ya msingi wa mahali pamoja, lakini vile vile katika usimamizi wa tengenezo la ulimwengu wote la mashahidi wa Kikristo wa Yehova. Usimamizi huu unaendeshwa kutoka katika makao makuu ya ulimwengu wote katika Brooklyn, New York, yanayofanya kazi kupitia kwa matawi 95 ya Watch Tower Society ulimwenguni kote kwa sasa. Matawi haya yanatembelewa kila mwaka na rais wa Watch Tower Bible and Tract Society au na wajumbe waliowekwa kwa njia ya pekee wanaojulikana kama waangalizi wa eneo la dunia (zone overseers). Vivyo hivyo, makundi yanatembelewa karibu mara mbili kila mwaka na wazee, wahudumu wenye kusafiri wanaoitwa waangalizi wa mizunguko, ambao kila mmojawao ana wajibu wa kutoa msaada wenye upendo kwa karibu makundi 22. Makundi yote katika kila mzunguko yanakusanyika pamoja mara mbili kwa mwaka, wakati ambao wanatembelewa na kutiwa moyo na mhudumu mwingine mwenye ujuzi, anayeitwa mwangalizi wa wilaya. Kwa kawaida anatumikia kuanzia mizunguko 20 kufikia 22. Waangalizi wa mizunguko na wilaya wanaripoti utendaji wao moja kwa moja kwa afisi ya tawi. Kwa kweli kanuni hii ya usaidizi na uangalizi wenye upendo imesaidia sana katika ukuzi wa mashahidi wa Kikristo wa Yehova miaka iliyopita.

24. (a) Uangalizi huu wenye upendo unaonyesha nini, na chini ya uongozi wa nani? (b) Ni sababu gani za lazima za kushirikiana na waliowekwa wa Mungu?

24 Je! haya yote yanaonyesha nini? Yanaonyesha wazi kwamba Yehova ana kusudi la ajabu katika kutoa kweli kwa kila mtu leo kwa njia ya utaratibu, na kazi hii yote inafanywa chini ya uongozi wa Yesu Kristo kama Mchungaji Mkuu na Mwangalizi, ambaye chini yake wanaume waliowekwa wanatumikia katika kutimiza mapenzi ya Mungu. (Efe. 1:9, 10; 1 Pet. 5:4) Zaidi ya hayo, mwisho wa taratibu hii ya kale ukiwa unakaribia karibu sana, hivi karibuni hakutakuwako na mwingine ye yote aliyepo sasa wa kusimamia mambo ya dunia isipokuwa hawa waliowekwa kwa njia ya pekee na Mfalme, Yesu Kristo. (Zab. 37:37, 38; 45:16) Kwa kweli, basi, kuna sababu za lazima kujifunza kushirikiana na wanaume kama hao leo, na hiyo ndiyo habari ya makala yetu ifuatayo, ambayo tunakazia fikira zenu.

[Picha katika ukurasa wa 58]

Waangalizi wanaonyesha kupendezwa kwenye upendo kwa ndugu zao za Kikristo, wakiwasaidia katika kundi . . .

. . . na vile vile katika kuhubiri habari njema

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki