Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 2/1 kur. 51-55
  • Kristendomu—Mpinzani wa Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kristendomu—Mpinzani wa Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • IBADA YA MWASI WA MUNGU
  • KUJITIA KATIKA SIASA
  • HATIA YA DAMU
  • Hawakujifanyia Jina Maarufu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Watu Wanajenga Mnara Mkubwa
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Ushindi wa Kimungu—Maana Yake kwa Wanadamu Wanaotaabika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Jumuiya ya Wakristo Imesaliti Mungu na Biblia
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 2/1 kur. 51-55

Kristendomu​—Mpinzani wa Mungu

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1-3. (a) Sababu gani linaelekea kuwa jambo geni kwa wengi kusikia kwamba Kristendomu anapigana na Mungu? (b) Sababu gani si jambo geni hivyo wakati maonyo ya mitume Paulo na Petro yanafikiriwa?

JE! KRISTENDOMU, yaani, utawala wa mataifa yanayojiita ya Kikristo, anapigana kweli na Mungu? Inasikika kama fumbo​—matengenezo yale yale yaliyo na jina la Kristo na yanayodai kuwa katika agano na Mungu yanafundisha na kuwaongoza wafuasi wake kutokumtii Mungu!

2 Si jambo geni, hata hivyo, unapofikiria kwamba mtume wa Kikristo Paulo alisema juu ya watu fulani katika kundi la Kikristo siku zake ambao, alisema, walikuwa “mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo. Wala si ajabu,” Paulo aliendelea, “maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.”​—2 Kor. 11:13, 14.

3 Zaidi ya hayo, wote Paulo na mtume Petro walionya juu ya uasi mkubwa wa imani ya kweli ambao ungetokea nyuma ya kifo cha mitume. Kama matokeo, wengi wanaojiita Wakristo, walisema, wangefuata “mafundisho ya mashetani” na kwa unafiki waseme uongo. Wangekuwa wenye “mfano wa utauwa” lakini ‘wangekana nguvu zake.’ ‘Wangesema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao.’ ‘Wangeingiza kwa werevu uzushi wa kupoteza [wanafunzi wa Kikristo],’ wakimkana “hata Bwana aliyewanunua.”​—1 Tim. 4:1, 2; 2 Tim. 3:5; Matendo 20:30; 2 Pet. 2:1-3; 2 The. 2:3-12.

4, 5. Ni mambo gani kati ya yale ambayo Mungu alimfunulia Ezekieli kwa njozi, na sababu gani inatupasa tupendezwe nayo?

4 Vile vile, kwa kutazama lililotukia kwa Israeli, taifa ambalo lilikuwa katika agano na Mungu, tunaweza kuona mfano unaogusa moyo, ndiyo, mfano wa hali ya Kristendomu leo. Kati ya mambo ya “kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya [taratibu za mambo]” ni ambalo Mungu alimwezesha nabii wake Ezekieli aone.​—1 Kor. 10:11.

5 Ezekieli, ingawa kwa mwili alikuwa katika Babeli umbali wa maili 500, alihamishwa katika njozi, ili apelekwe katika ukaguzi wa hekalu la Yehova katika Yerusalemu. Kwanza, aliona “sanamu ile ya wivu” katika mahali pa ndani pa kuingilia. Halafu uliingia mfuatano wa viongozi sabini wa Israeli, katika vyumba vya siri, wakitoa uvumba kwa michoro ya wanyama wa kuchukiza na vitu vitambaavyo. Hili lilikuwa jambo la kuchukiza sana, lakini Yehova aliendelea kusema kwa Ezekieli, akisema: “Utaona tena machukizo makubwa mengine wanayoyatenda.”​—Eze. 8:13.

IBADA YA MWASI WA MUNGU

6, 7. Nani aliyekuwa mungu Tamuzi, ambaye wanawake wa Kiisraeli walikuwa wakimlilia?

6 Halafu, katika behewa la ndani, Ezekieli anatoa habari, “Tazama, wanawake wameketi wakimlilia Tamuzi.”​—Eze. 8:14.

7 Je! Tamuzi huyu alikuwa nani? Kulingana na Wababeli na Washamu, alikuwa mungu wa mimea. Katika kusini ya magharibi ya Asia, mimea inamea wakati wa mvua na mafuriko matulivu na kufa wakati wa ukavu. Kifo cha mimea kilionwa kama mfano wa kifo cha Tamuzi, na kifo chake ndicho kiliombolezewa kila mwaka wakati wa joto kali mno, na waabudu sanamu wa Tamuzi. Wakati wa mvua ulipofika Tamuzi alidhaniwa kurudi kutoka katika ulimwengu wa chini, kama alivyofananishwa na kukua tena kwa mimea.

8, 9. Ni kukamatana gani kunakofanywa na kitabu cha The Two Babylons kati ya Tamuzi na Nimrodi, na Nimrodi alifanya nini?

8 Je! Waisraeli wangevutwaje kuabudu sanamu? Sababu gani walifuata mazoea ya ibada kama hiyo? Tunapofikiria historia na habari juu ya ibada ya Tamuzi inakuwa wazi zaidi. Katika kitabu chake The Two Babylons Dr. Alexander Hislop anamshirikisha Tamuzi na Nimrodi, mwanzilishi wa mji wa Babeli, karibu miaka 180 nyuma ya gharika ya siku za Nuhu.

9 Nimrodi alikuwa kilembwe cha Nuhu. Kulingana na Mwanzo 10:1, 6, 8-12, NW, Nimrodi alikuja kujulikana kama “mwindaji hodari kwa kumpinga Yehova.”a Alikuwa kiongozi katika kujenga Mnara wa Babeli wa kidini ili kuzuia amri ya Mungu kwamba watu watawanyike na kuijaza dunia. Utii kwa amri hii ungalisimamisha ngome za ibada ya kweli duniani kote. (Mwa. 9:1) Lakini Nimrodi alionekana kama mtu hodari kwa wafuasi wake. Kulingana na mwandishi wa historia wa Kiyahudi Josephus: “[Nimrodi] polepole aliigeuza serikali kuwa utawala wa uonezi,​—bila kuona njia nyingine yo yote ya kuwaondoa watu katika kicho cha Mungu, isipokuwa kuwaingiza katika tegemeo imara la uwezo wake. Alisema vile vile angejilipiza kisasi na Mungu, akifikiria kuuzamisha ulimwengu tena; kwa sababu hiyo angejenga mnara mrefu mno maji yasiweze kuufikia! . . . Sasa umati ulikuwa tayari sana kufuata uamuzi wa Nimrodi, na kudhani ni woga kujitiisha chini ya Mungu; na wakajenga mnara.”​—Antiquities of the Jews, Book I, sura ya IV, mafu. 2, 3.

10. Sababu gani Wababeli walimlilia Nimrodi (Tamuzi)?

10 Mapokeo ya kidini yanaeleza kwamba Nimrodi aliuawa kwa sababu ya kumwasi Yehova, Mungu wa Nuhu. Wafuasi wa Nimrodi waliona kifo chake kibaya kama msiba au hasara, na wakamfanya mungu. Kila mwaka walikumbuka kifo chake tarehe ya kwanza au ya pili ya mwezi ulioitwa Tamuzi, wakati ambao wanawake waabudu sanamu waliililia sanamu yake. Hivyo sababu ya kilio hiki cha waabudu wa Kibabeli juu yake inajulikana. Vile vile, uhakika wa kwamba Nimrodi anajulikana na wanafunzi kama akishirikiana na Marduk (Merodaki), mungu mkuu wa Wababeli, unatuwezesha kuona sababu gani Wayahudi, wakiwa chini ya Babeli wakati huo, na katika hatari ya kuangamizwa na hii Mamlaka ya Ulimwengu ya siku hizo, ingewezekana washawishwe kufuata ibada ya Tamuzi.

11, 12. (a) Jaribio lilikuwaje la kuingiza msalaba wa kipagani katika ibada katika hekalu, na umeingizwaje katika dini za Kristendomu? (b) Sababu gani mazoea haya ni ya kuchukiza?

11 Tamuzi aliwakilishwa na herufi ya kwanza ya jina lake, ambalo ni msalaba wa zamani, tau. “Ishara ya msalaba” ilikuwa alama ya kidini ya Tamuzi. Kwa hiyo kulikuwako jaribio la kuingiza ibada ya msalaba wa kipagani katika hekalu la Yehova katika Yerusalemu.

12 Lakini hii inakamatanaje na Kristendomu? Je! ibada ya Tamuzi inaendelea humo, kwa kwa kumpinga Mungu? Kwanza, namna gani juu ya “ishara ya msalaba” katika Kristendomu? Msalaba, ambao juu yake dini za Kristendomu zinadai Kristo aliuawa (ingawa kwa kweli ulikuwa mti), unaonwa kama ishara iliyo kubwa kupita zote ya Ukristo. Hata unapigiwa magoti na kupigwa busu na wanadini fulani. Kati ya Wayahudi nyuma ya kurudishwa kwao kutoka Babeli, mti ambao juu yake mtu aliuawa ulionwa kama chukizo, kitu cha kuzikwa kisionekane. Anasema mkuu wa Kiyahudi, Moses Maimonides, wa karne ya kumi na mbili: “Mti ambao juu yake mtu ye yote ametundikwa unazikwa; ili kwamba jina baya lisibaki nao na watu wasije wakasema, ‘Huu ndio mti ambao juu yake fulani alitundikwa.’ “Lakini Kristendomu kwa kweli anaheshimu kitu kile kile ambacho, kulingana nao, kilikuwa chombo alipotesewa Yesu mpaka kufa.

KUJITIA KATIKA SIASA

13, 14. (a) Nimrodi alikuwa mwanzilishi wa vitu gani? (b) Maana ya neno “mwindaji” ilikuwa nini kama lilivyotumiwa na Wababeli kwa Nimrodi?

13 Lakini, kama Yehova alivyosema yangekuwa maono ya Ezekieli, sisi vile vile tutaona mambo ya kuchukiza hata zaidi kupita hayo kwa habari ya ibada ya Tamuzi au Merodaki katika Kristendomu. Biblia inasema juu ya Nimrodi kwamba “mwanzo wa ufalme wake ulikuwa Babeli na Ereku, na Akadi, na Kalne, katika nchi ya Shinari. Akatoka katika nchi ile akaenda mpaka Ashuru, akajenga Ninawi, na Rehoboth-iri, na Kala; na Reseni, kati ya Ninawi na Kala, nao ni mji mkubwa.” (Mwa. 10:10-12) Hivyo Nimrodi alikuwa ndiye mwanzilishi wa miji na taratibu za kisiasa za utawala, tofauti na mapenzi ya Yehova Mungu. Dini zote za uongo zilitoka Babeli nyuma ya gharika ya siku za Nuhu. Mwanzo 10:8, 9 panasema kwamba “alikuwa [Nimrodi] hodari kuwinda wanyama mbele za [ Yehova].”

14 Neno “kuwinda,” kulingana na desturi ya kale ya Wababeli na Waashuru, lilitumiwa si kwa kuwinda wanyama wa porini tu lakini vile vile kwa shughuli za kijeshi za kuvishambulia viumbe vya kibinadamu kama mawindo. Kwa hiyo Nimrodi alijifanya mwenyewe mmwagaji wa damu ya mwanadamu katika vita.

15. Twaonaje kukamatana kati ya Nimrodi na Kristendomu kwa habari ya msalaba na uwindaji wa Nimrodi?

15 Namna maelezo haya juu ya Nimrodi yanavyomfaa Kristendomu vile vile! Kama Nimrodi, yeye vile vile amesimamisha taratibu zake mwenyewe za kidini. Hizi kwa kawaida zinadhaniwa kupatana na Biblia Takatifu lakini, kwa kweli, zinapatana na mafundsho ya kidini ya Babeli ya kale. Mfalme Konstantino ndiye mtawala aliyeufanya Ukristo kuwa Dini ya Taifa ya Milki ya Kirumi. Kulingana na mwandishi wa historia ya kidini Askofu Eusebius wa Kaisaria, Konstantino alisema kwamba “wakati wa adhuhuri wakati jua lilipokuwa likianza kushuka aliona kwa macho yake mwenyewe zawadi ya ushindi ya msalaba wa mwangaza mbinguni, juu ya Jua, ikiwa na mwandiko [katika Kigiriki] KWA HUU SHINDA.” Hii, kwa kweli, ilielekea kutoa ruhusa “takatifu” kwa nia zake za kisiasa. Ishara hii, msalaba, ndipo ikatumiwa katika ngao za askari zake, jeshi la waabudu wa mungujua, ambao waliondoka kuua na kushinda.

16, 17. Ni kwa kadiri gani dini za Kristendomu zimefuata mfano wa Nimrodi kwa kuchanganya dini na siasa?

16 Kama Nimrodi, Kristendomu hakujiweka katika dini kwa njia safi; amejichangamanisha katika siasa za kilimwengu, akisimamisha, po pote alipoweza, mwungano wa Kanisa na Taifa, Kanisa likiwa linajaribu kuambia Taifa la kufanya. Amedai kwamba wafalme wake wa kisiasa wametawala “Kwa mapenzi ya Mungu.” Mwandishi wa historia H. G. Wells anaandika juu ya kuvikwa taji kwa Charlemagne kama mfalme wa “Milki Takatifu ya Kirumi” na Papa Leo: “Leo III (795-816), aliyemkaribisha Charlemagne kuwa Kaisari na kumvika taji bila kujijali mwenyewe.” (Pocket History of the World, chapa ya Machi, 1944, uku. 233)

17 Si kwamba tu Kristendomu amewatawaza na kuwaondoa watawala katika kiti cha enzi, lakini hata maaskofu wake, maaskofu wakuu na mapapa wametukuzwa kwa “viti vya enzi” vya kimwili na wangali wanasemwa “kutawala” majimbo yao. Linganisha mwendo huu na maneno ya mtume wa Kikristo katika 1 Wakorintho 4:8.

18. Tofautisha mfano wa Yesu na ule wa viongozi wa dini wa Kristendomu.

18 Wanasiasa wa ulimwengu huu wanapewa vyeo vikubwa na kufikiriwa sana katika taratibu za kanisa. Namna ilivyo tofauti na mfano wa Yesu Kristo, ambaye alikataa kufanywa mfalme duniani na wanadamu! Kwa gavana wa Kirumi Pontio Pilato, alisema: “Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wagenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa.” (Yohana 18:36) Tofauti na hili, Kristendomu anasisitiza kwamba ni wajibu wa washiriki wake wa kanisa kujitia katika siasa. Nyakati nyingine, na katika sehemu fulani, anajaribu kuwatangazia juu ya wagombea uchaguzi wa kisiasa watakaowapigia kura. Washiriki wa viongozi wake wa dini hata wametenda kama watawala wa kisiasa, kama rais, au kama waziri mkuu, na vivyo hivyo.

HATIA YA DAMU

19. Je! Kristendomu amefuata mfano wa Nimrodi kwa habari ya umwagaji wa damu?

19 Na namna gani juu ya umwagaji wa damu usiozuiwa uliofanywa na “Nimrodi, hodari wa kuwinda wanyama mbele za [Yehova]”? Aliyofanya Nimrodi yalikuwa mfano mdogo tu wa Kristendomu! Kwa kadiri kubwa zaidi, yeye vile vile ameingia kama “mwindaji” katika shughuli za kijeshi na silaha za kimwili. Vita vikatili zaidi vya historia yote ya kibinadamu vimepiganwa na washiriki wa Kristendomu, kati yao wenyewe na wanaoitwa makafiri na wapagani. Haya yote hayalingani na mfano wa Kristo. Ni ya Kibabeli na ya mfano wa Nimrodi.’

20. Ni jambo gani linafanana siku hizi kati ya kumlilia Tamuzi hapo kale na matendo ya wanadini katika Kristendomu?

20 Hasara ya maisha za kibinadamu katika vita hivi imeleta kilio kisichoelezeka kwa wanawake wa Kristendomu. Siku za ukumbusho zinafanywa kila mwaka ambapo walioletewa huzuni na vita wanaenda makaburini kupamba viwanja vya mashujaa wao waliouawa. Vifo vya wakuu hodari wa vita na mabwana wengine wenye vyeo vya juu vinaombolezewa na washiriki wapenda nchi, wenye roho ya kitaifa wa Kristendomu, hawa wakisifiwa katika makanisa ambamo maombi ya mazishi yanafanyiwa. Haya yote yanapatana na uhakika wenye sifa mbaya wa kwamba makanisa yametumiwa kama vikao vya kuandika askari wapya na vya kueneza habari (propaganda) nyakati za vita. Kukamatana huku kote kwa kazi hizi za kisiasa na za kijeshi na “nyumba ya Mungu” (kanisa) katika Kristendomu kunatukumbusha juu ya wale wanawake Waisraeli walioketi na kumlilia Tamuzi katika behewa la ndani la hekalu la Bwana Mungu Mwenye Enzi Yote katika siku za Ezekieli.

21, 22. Mwendo wa Kristendomu umetokezaje maadui wa Ukristo na kwa kweli kutoa mahali pa Ukomunisti na fundisho la mageuzi kuzaliana?

21 Je! tendo la Kristendomu limekweza jina la Yehova, Mungu wa Biblia? Hapana, pahali pake limeleta suto, na chuki na uadui kuelekea Ukristo kwa upande wa watu wa nchi zisizo za Kikristo. Uwakilishaji mbaya wa Kristendomu wa Mungu wa Biblia, pamoja na matendo yake yasiyo ya Kikristo, umetayarisha mahali pa Ukomunisti kuzaliana.

22 Tena, ni sawa katikati ya Kristendomu ambapo fundisho la mageuzi limewapata wafuasi fulani wake wenye nguvu sana. Sababu gani? Kwa sababu yeye ameifanya Biblia ionekane kujipinga yenyewe, yenye upuzi na makosa kwa sababu ya mafundisho yake mwenyewe ya upuzi, ya uongo na yasiyo ya akili nzuri kama Utatu, moto wa mateso, imani ya kwamba Mungu anawaandikia watu fulani hukumu ya milele na wengine uzima wa milele na mafundisho yake juu ya vita, kujitia kwake katika siasa na, lisilo dogo, kugeuka kwake kwenye upekuzi mbaya wa kutoa makosa katika Biblia. Wengi wa viongozi wake wakuu wa dini wamepita kadiri kwa kulitegemeza fundisho la mageuzi.

23. Nia ya Kristendomu ni nini kuwaelekea wale wanaotangaza habari njema za ufalme wa Mungu wa Kimasihi, na anasimama wapi, katika hukumu ya Mungu?

23 Matengenezo ya kidini ya Kristendomu, katika mataifa yake yote, yamepinga kutangazwa kwa habari njema za ufalme wa Mungu wa Kimasihi. Viongozi wa kidini wamefanya shauri pamoja la kuwasukuma watawala wa kisiasa waipige kazi marufuku na wamechochea mashahidi wa Yehova wakamatwe na kufanyiwa ghasia na makundi, watu ambao wanawaita wote wajifunze Biblia ili wafahamu inayofundisha kwa kweli. Kristendomu, anayejitia katika ibada ya Nimrodi, kwa kweli ni sehemu ya Babeli Mkuu, milki ya ulimwengu ya dini ya uongo, na kwa wote wanaokamatana naye, amri ya Mungu ni: “Tokeni kwake, . . . msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.”​—Ufu. 18:4.

24, 25. Matokeo yatakuwa nini kwa Kristendomu kwa sababu ya mwendo wake, na mtu ambaye ni mshiriki wa mojawapo la makanisa yake anapaswa kufanya nini?

24 Historia ndefu ya Kristendomu ya kupigana na Mungu inakaribia mwisho wake. Amemfanyia Mungu mzaha kwa kuchukua jina lake na la Mwanawe na kisha kuyaletea masingizio mabaya kupita yote. Lakini “Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.” (Gal. 6:7) Kristendomu atalipa pigano lake na Mungu kwa kutoweka kwake.

25 Je! wewe u mshiriki wa mojawapo la makanisa ya Kristendomu? Basi chunguza Maandiko wewe mwenyewe kwa msaada wa Wakristo wa kweli, na umwache Kristendomu mwenye hatia ya damu. Mgeukie Mungu wa kweli na ufalme wake wa Kimasihi kwa uzima.

​—Kutoka Kitabu “The Nations Shall Know That I Am Jehovah”​—How?

[Maelezo ya Chini]

a Tazama The New World Translation of the Holy Scriptures, chapa ya 1953, maelezo ya chini Juu ya Mwanzo 10:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki