Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mrt makala 109
  • Yesu Atakomesha Uhalifu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Atakomesha Uhalifu
  • Habari Zaidi
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Atakomesha Umaskini
    Habari Zaidi
  • Yesu Atakomesha Vita
    Habari Zaidi
  • Unaweza Kumwamini Nani?—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zaidi
  • Wewe Unataka Uhalifu Umalizwe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Habari Zaidi
mrt makala 109
Mhalifu akimfuata mwanamke aliye peke yake. Mwanamke huyo anamwona na kupiga simu kuomba msaada.

alfa27/stock.adobe.com

Yesu Atakomesha Uhalifu

Kwa kuwa Yesu aliteseka na kukabili ukosefu wa haki anaelewa vizuri hali hiyo. Alishtakiwa kwa uwongo, akapigwa ingawa hakuwa amekosea, akafikishwa mahakamani kwa tuhuma za uwongo, akahukumiwa kimakosa, na akauawa kikatili. Licha ya kwamba hakuwa na hatia, alikubali bila ubinafsi kudhabihu “uhai wake uwe fidia badala ya wengi.” (Mathayo 20:28; Yohana 15:13) Sasa, akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu, hivi karibuni atahakikisha haki inatendeka duniani kote, na kukomesha uhalifu kabisa.​—Isaya 42:3.

Biblia inafafanua jinsi ulimwengu utakavyokuwa baada ya Yesu kuchukua hatua:

  •  “Watu waovu hawatakuwepo tena; utapaangalia mahali walipokuwa, nao hawatakuwepo. Lakini wapole wataimiliki dunia, nao watafurahia kwelikweli wingi wa amani.”​—Zaburi 37:10, 11.

Tunaweza kuonyeshaje shukrani kwa mambo yote ambayo Yesu ametufanyia na ambayo atatufanyia wakati ujao? Njia moja ni kujifunza zaidi kuhusu “habari njema ya Ufalme wa Mungu,” ujumbe ambao Yesu alihubiri. (Luka 4:43) Soma makala yenye kichwa “Ufalme wa Mungu Ni Nini?”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki