alfa27/stock.adobe.com
Yesu Atakomesha Uhalifu
Kwa kuwa Yesu aliteseka na kukabili ukosefu wa haki anaelewa vizuri hali hiyo. Alishtakiwa kwa uwongo, akapigwa ingawa hakuwa amekosea, akafikishwa mahakamani kwa tuhuma za uwongo, akahukumiwa kimakosa, na akauawa kikatili. Licha ya kwamba hakuwa na hatia, alikubali bila ubinafsi kudhabihu “uhai wake uwe fidia badala ya wengi.” (Mathayo 20:28; Yohana 15:13) Sasa, akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu, hivi karibuni atahakikisha haki inatendeka duniani kote, na kukomesha uhalifu kabisa.—Isaya 42:3.
Biblia inafafanua jinsi ulimwengu utakavyokuwa baada ya Yesu kuchukua hatua:
“Watu waovu hawatakuwepo tena; utapaangalia mahali walipokuwa, nao hawatakuwepo. Lakini wapole wataimiliki dunia, nao watafurahia kwelikweli wingi wa amani.”—Zaburi 37:10, 11.
Tunaweza kuonyeshaje shukrani kwa mambo yote ambayo Yesu ametufanyia na ambayo atatufanyia wakati ujao? Njia moja ni kujifunza zaidi kuhusu “habari njema ya Ufalme wa Mungu,” ujumbe ambao Yesu alihubiri. (Luka 4:43) Soma makala yenye kichwa “Ufalme wa Mungu Ni Nini?”