panitan/stock.adobe.com
Yesu Atakomesha Umaskini
Yesu alipokuwa duniani, alionyesha kwamba anawapenda sana watu, hasa maskini na wenye matatizo. (Mathayo 9:36) Hata alidhabihu uhai wake ili kuwanufaisha wengine. (Mathayo 20:28; Yohana 15:13) Hivi karibuni, Yesu atathibitisha tena kwamba anawapenda watu kwa kutumia mamlaka na nguvu zake akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu ili kukomesha umaskini duniani pote.
Biblia inatumia maneno yenye kupendeza kufafanua mambo ambayo Yesu atafanya:
“Awalinde watu wa hali ya chini miongoni mwa mataifa, na awaokoe watoto wa mtu maskini.”—Zaburi 72:4.
Tunaweza kuonyeshaje shukrani kwa mambo yote ambayo Yesu ametufanyia na ambayo atatufanyia wakati ujao? Njia moja ni kujifunza zaidi kuhusu “habari njema ya Ufalme wa Mungu,” ujumbe ambao Yesu alihubiri. (Luka 4:43) Soma makala yenye kichwa “Ufalme wa Mungu Ni Nini?”