AspctStyle/stock.adobe.com
Yesu Atakomesha Vita
Yesu alipokuwa duniani, alionyesha anawapenda watu sana, kufikia hatua ya kudhabihu uhai wake kwa ajili yao. (Mathayo 20:28; Yohana 15:13) Hivi karibuni ataonyesha tena kwamba anawapenda watu kwa kutumia mamlaka yake akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu ‘kukomesha vita katika dunia yote.’—Zaburi 46:9.
Ona jinsi Biblia inavyofafanua kile ambacho Yesu atafanya:
“Atamwokoa maskini anayelilia msaada, pia mtu wa hali ya chini na yeyote ambaye hana msaidizi. Atamhurumia mtu wa hali ya chini na maskini, naye ataokoa uhai wa maskini. Atawaokoa kutoka katika ukandamizaji na ukatili.”—Zaburi 72:12-14.
Tunaweza kuonyeshaje uthamini kwa ajili ya mambo yote ambayo Yesu amefanya na atakayotufanyia? Njia moja ni kujifunza zaidi kuhusu “habari njema ya Ufalme wa Mungu,” ujumbe ambao Yesu alihubiri. (Luka 4:43) Soma makala yenye kichwa “Ufalme wa Mungu Ni Nini?”