Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w25 Novemba uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
  • Habari Zinazolingana
  • Kupambana na Hayawani Wawili Wakali Sana
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Kitabu cha Ufunuo Kinamaanisha Nini kwa Maadui wa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • N’nini Kinachozuia Amani ya Ulimwengu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Kufisha Babuloni Mkubwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2025
w25 Novemba uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Ni “wazo” gani ambalo Yehova atatia katika mioyo ya mataifa hivi karibuni?

Kuhusu kuanza kwa dhiki kuu, Ufunuo 17:​16, 17 inasema hivi: “Zile pembe kumi ulizoona, na yule mnyama wa mwituni, hao watamchukia yule kahaba na kumfanya kuwa ukiwa na uchi, nao watakula nyama yake na kumteketeza kabisa kwa moto. Kwa maana Mungu alitia hilo ndani ya mioyo yao ili kutekeleza wazo lake, ndiyo, kutekeleza lile wazo lao moja kwa kumpa yule mnyama wa mwituni ufalme wao.” Zamani, machapisho yetu yalisema kwamba “wazo” ambalo Yehova ataliweka katika mioyo ya mataifa ni la kuharibu dini za uwongo.

Hata hivyo, marekebisho yanahitajika. “Wazo” ambalo Yehova ataliweka katika mioyo ya mataifa ni kwamba wampe “yule mnyama wa mwituni ufalme wao.” Ili kuelewa jinsi jambo hilo litakavyotimizwa, fikiria maswali yafuatayo.

Ni nani wahusika wakuu katika unabii huu? “Yule kahaba” ambaye anaitwa pia “Babiloni Mkubwa”; anafananishwa na milki ya ulimwenguni pote ya dini za uwongo. “Mnyama wa mwituni mwenye rangi nyekundu” ni ishara ya shirika la amani lililoanzishwa mwaka wa 1919 na likaitwa Ushirika wa Mataifa na sasa linaitwa Umoja wa Mataifa. (Ufu. 17:​3-5) “Zile pembe kumi” zinafananisha serikali zote zinazomuunga mkono yule mnyama wa mwituni.

Kuna uhusiano gani kati ya kahaba na yule mnyama wa mwituni mwenye rangi nyekundu? Kahaba amekuwa ‘akiketi juu ya’ mnyama wa mwituni, akimbariki na kujaribu kumshawishi, na hata kumtawala.

Ni nini kitakachompata kahaba? Yule mnyama wa mwituni, pamoja na zile pembe kumi zinazomuunga mkono, “watamchukia yule kahaba.” Wakionyesha chuki yao, watapora mali yake na kufunua uovu wake. Nao watatekeleza hukumu ya Yehova kwa kahaba huyo, yaani, kwa kumharibu kabisa. (Ufu. 17:1; 18:8) Huo utakuwa mwisho wa mashirika ya dini za uwongo. Hata hivyo, kabla ya hilo kutukia, Yehova atasababisha mataifa yafanye jambo ambalo halijawahi kutokea katika historia ya utawala wa wanadamu.

Yehova atasababisha mataifa yafanye nini? Atatia ndani ya mioyo ya zile pembe kumi “wazo lake,” yaani, “[wampe] yule mnyama wa mwituni [mwenye rangi nyekundu] nguvu na mamlaka yao”—Umoja wa Mataifa. (Ufu. 17:13) Fikiria hilo linamaanisha nini. Je, serikali za wanadamu zitaamua tu zenyewe kumpa mnyama wa mwituni nguvu na mamlaka yao? Hapana! Unabii unaonyesha kwamba Mungu mwenyewe ndiye atakayewaongoza wafanye hivyo. (Met. 21:1; linganisha Isaya 44:28.) Je, jambo hilo litafanyika hatua kwa hatua? Hapana! Inaelekea kwamba badiliko hilo litatukia ghafla. Kisha, mnyama huyo wa mwituni aliyepewa nguvu zaidi atatekeleza hukumu ya Yehova dhidi ya mashirika ya dini za uwongo kwa kuyaharibu kabisa.

Hivyo basi, tunaweza kutarajia nini? Hatupaswi kutarajia kuona taarifa za habari zikisema kwamba hatua kwa hatua serikali zinaanza kuliunga mkono zaidi na zaidi shirika la Umoja wa Mataifa. Jambo tunaloweza kutarajia ni hili: Kwa ghafla sana, Yehova atafanya mataifa yote yampe mnyama huyo wa mwituni nguvu zao. Jambo hilo litakapotukia, tutajua kwamba dhiki kuu inakaribia kuanza. Kwa sasa, acheni “tukae macho na kutunza akili zetu” kwa sababu mabadiliko ya ghafla yatatukia hivi karibuni!—1 The. 5:6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki