MSEMO WA BIBLIA
Kutumia ‘Zawadi Yako ya Kiroho’
Sisi sote huthamini kitia moyo tunachofurahia tunapokuwa pamoja na ndugu na dada zetu Wakristo. Lakini kitia moyo hicho kinahusisha mengi zaidi ya kuwa tu pamoja. Biblia inaita uwezo wetu wa kuimarishana imani kuwa “zawadi ya kiroho.” (Rom. 1:11, 12) Tunawezaje kuitumia zawadi hiyo kikamili?
Toa zawadi kwa kusema maneno yaliyochaguliwa vizuri. Kwa mfano, tunaweza kutoa maelezo mikutanoni ambayo yanamkazia fikira Yehova, Neno lake, na watu wake, badala ya sisi wenyewe. Tunapozungumza na waabudu wenzetu, tunaweza kuchagua habari zinazojenga.
Watie moyo wengine kupitia maamuzi na matendo yako. Kwa mfano, baadhi ya ndugu na dada wameamua kubaki katika utumishi wa wakati wote licha ya changamoto wanazokabili kibinafsi. Wengine wanahudhuria mikutano ya katikati ya juma kwa ukawaida licha ya kuwa na ratiba ya kazi yenye shughuli nyingi au tatizo la kudumu la afya.
Je, unawatia moyo ndugu na dada zako kupitia mambo unayosema na kutenda? Je, unakuwa makini kukubali zawadi za kiroho kutoka kwa ndugu na dada zako?