Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 11/1 kur. 486-489
  • Je! Umoja wa Mataifa Yote Waweza Kuwapo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Umoja wa Mataifa Yote Waweza Kuwapo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAHALI AMBAPO UMOJA WA KWELI UNAPATIKANA LEO
  • NAMNA AMBAVYO MUNGU ATALETA UMOJA
  • “MFALME MMOJA” ANAYELETA UMOJA
  • Familia ya Yehova Hufurahia Muungano Wenye Thamani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Umoja Katika Ibada Chini ya Mfalme-Mchungaji Wetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Dumisheni Muungano Katika Siku Hizi za Mwisho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Umoja Unatambulisha Ibada ya Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 11/1 kur. 486-489

Je! Umoja wa Mataifa Yote Waweza Kuwapo?

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1-3. (a) Je! kukosa mambo ya kimwili au ujuzi wa kazi ndiko kunakozuia umoja wa mataifa yote? (b) Ugumu wenyewe uko wapi?

UMOJA kati ya mataifa ni wa kutamanika sana leo. Majilio ya silaha za atomiki yanaufanya wa kutamanika zaidi. Kwa kweli, wanasayansi na wakuu wa serikali wanasihi jitihada zenye nguvu zaidi kuelekea umoja wakiogopa kwamba kama sivyo utamaduni kama tuujuavyo utatoweka duniani.

2 Je! ugumu huu upo kwa maana ulimwengu haujaendelea vya kutosha kuweza kuyaangalia matakwa yake katika njia ya ufundi ama ya uchumi? Sivyo. Ujuzi wa kisasa wa kisayansi na wa ufundi unaweza kutunza ukuzaji na ugawaji wa chakula cha kulisha kila mtu. Nyumba, mavazi na mahitaji mengine yote yanaweza kutolewa, zaidi ikiwa jitihada zote na vifaa vinavyotumiwa sasa katika vita na shughuli za kijeshi vingetumiwa kwa njia zenye msaada.

3 Basi, ni ugumu gani ulioufanya umoja wa ulimwengu kuwa fumbo, sikuzote ukizungumzwa lakini bila ya kupatikana? Je! si watu​—mwenendo wao kwa mtu na mwenzake? Kuna uadui kati ya mataifa. Lakini kwa uzito zaidi, kutoka huko kuja kwenye ujirani, twaona chuki kati ya mataifa, na, mara nyingi sana, chuki ya wazi kwa mtu mwingine. Watu wanachokozana. Kufuata kwa vijana yao wenyewe kwa kujitenga na wazazi na mambo mengine hata kunazitenganisha jamaa.

4, 5. Ufumbuzi wa ugumu wa umoja wa ulimwengu waweza kupatikana wapi?

4 Kwa hiyo, amani ya ulimwengu na umoja hauwezi kuwapo mpaka pawe na mageuzi katika mwenendo wa watu. Hata yawe ni maafikiano ya namna gani au sheria zitakazofanywa na mataifa, umoja wenye kuendelea hautakuwapo mpaka watu wenyewe wamekuja kupendana wao kwa wao, kila mmoja akifanya yampendezayo mwenzake zaidi. Jambo la maana sana ni elimu, kutia akilini na mioyoni mwa watu sababu ya kweli ya umoja.

5 Wanadamu wameshindwa kuitoa sababu hii, ijapokuwa wamefanya ahadi na mipango ya kisiasa. Hata hivyo, umoja wa mataifa yote utaletwa. Hili litafanywa na aliye wa pekee anayeweza kuifikia mioyo ya watu na kugeuza nia na utu. Huyu ndiye Muumba. Lakini yeye hageuzi nia kwa kutumia nguvu. Bali, anao mpango wa kuelimisha unaowasukuma watu kufanya mageuzi, kwa maana yeye anajua wanayoyahitaji. Yeye ndiye anayeusimamia mpango.

MAHALI AMBAPO UMOJA WA KWELI UNAPATIKANA LEO

6-8. (a) Tunaweza kuelekeza wapi kwa mfano unaohakikisha umoja wa mataifa yote unawezekana? (b) Mashahidi wa Yehova wanaupata umoja wao kutoka kwa chanzo gani na kwa nguvu gani?

6 Je! hii inasikika kama jambo la kukisia tu? Kama wewe ungeuona umoja huo ukizoewa kati ya hesabu kubwa ya watu, je! ungeamini kwamba wao ndio wenye ufumbuzi? Kikundi hiki kipo. Ndicho jamii ya mataifa yote inayojulikana kama mashahidi wa Yehova.

7 Je! watu hawa wanao umoja kweli kweli kati yao wenyewe katika sehemu zote za maisha na utendaji? Kwamba wanao ni wazi kwa watu wote ambao wameyaona makusanyiko yao makubwa yakifanywa, au ambao wamehudhuria mikutano yao katika Majumba ya Ufalme ya mahali pao. Je! wao wanautoa wapi? Kutokana na kujifunza na kulifuata Neno la Mungu Biblia. Si kwa sababu ya “wema” wao wenyewe, kwa maana wana utu mbalimbali nao walikuwa kama watu wengine wo wote mbele ya kuja kwenye ujuzi wa kweli ya Mungu na makusudi.​—Kol. 3:5-8.

8 Kusudi la Mungu ni kuwa na umoja wote kati ya watu juu ya dunia hii. Yeye amewakusanya pamoja waliolisikiliza Neno lake, naye amewapa roho yake, roho ya kweli, umoja na uhuru. (Yohana 16:13; Efe. 4:2, 3; 2 Kor. 3:17) Zamani za kale alifanya hivyo kwa muda mfupi kwa ajili ya taifa moja la watu, kama mfano wa anachofanya sasa na atakachokitimiliza kabisa.

NAMNA AMBAVYO MUNGU ATALETA UMOJA

9. Hali ilikuwa nini kati ya kabila kumi na mbili za Israeli tangu wakati wa Rehoboamu mpaka uhamisho wa Yuda katika Babeli?

9 Mfano huu wa kuungamanisha ulifanywa na Yehova alipoyaungamanisha mataifa mawili yaliyokuwa adui wakali kwa karne nne. Hapo mwanzoni haya yalikuwa taifa moja, wazao wa wana kumi na wawili wa mtu mmoja, lakini yalikuwa yamekuja kuchukiana na kupigana. Mithali ya Biblia ilikuwa kweli kwa habari yao: “Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuliko mji wa nguvu; na mashindano ni kama mapingo ya ngome.” (Mit. 18:19) Kumi ya makabila hayo yalikuwa yameasi na yakajitenga wakati wa utawala wa Mfalme Rehoboamu, mwana wa Sulemani, yakaunda ufalme wa kaskazini, ulioitwa nyakati nyingine, kulingana na kabila lililoongoza, “Efraimu” (mmojawapo wa wana wa Yusufu, mwanawe Yakobo). Ufalme wa kusini wenye kabila mbili uliitwa “Yuda.” Tangu kutekwa nyara kwa Efraimu na Waashuri na uhamisho wa Yuda mpaka Babeli, kabila zote kumi na mbili zilitawanyika sana. Ilielekea kuwa, si kwa maana ya kiroho tu, lakini vile vile kwa maana ya kijiografia, umoja usingeweza kupatikana kwao.

10-13. Kwa habari ya hali ya Waisraeli ya kugawanyika, Yehova alimfanyizisha Ezekieli ishara gani mbele ya Wayahudi katika Babeli?

10 Lakini hakuna lisilowezekana kwa Mungu. (Mt. 19:26) Walipokuwa wangali katika uhamisho huko Babeli, Yehova alimwinua nabii wake Ezekieli. Ili awasaidie na kuweka mfano wa unabii wa umoja katika wakati wetu, Mungu alimwambia Ezekieli hivi:

11 “Na wewe mwanadamu, twaa kijiti kimoja; ukaandike juu yake, Kwa Yuda, na kwa wana wa Israeli wenzake; kisha, twaa kijiti cha pili; ukaandike juu yake, Kwa Yusufu, kijiti cha Efraimu, na kwa nyumba yote ya Israeli wenzake; ukaviunge pamoja kwa ajili yako hiki na hiki viwe kijiti kimoja, viwe kimoja katika mkono wako.”​—Eze. 37:15-17.

12 Mfano huu wa umoja uliofanywa na Ezekieli, awe alishika vijiti viwili pamoja mkononi mwake ama viwe viliunganishwa kwa mwujiza, bila shaka ungewafanya Wayahudi watende mara moja. Akifikiria hili Yehova alisema:

13 “Wana wa watu wangu watakapokuambia, wakisema, Je! hutatuonyesha maana ya mambo hayo utendayo? waambie, Bwana [Yehova] asema hivi; Tazama, nitakitwaa kijiti cha Yusufu, kilicho mkononi mwa Efraimu, na kabila za Israeli wenzake, nami nitawaweka pamoja nacho, yaani, pamoja na kijiti cha Yuda, na kuvifanya kuwa kijiti kimoja; navyo vitakuwa kimoja mkononi mwangu. Navyo vijiti, ambavyo uliandika juu yake, vitakuwa mkononi mwako mbele ya macho yao.”​—Eze. 37:18-20.

“MFALME MMOJA” ANAYELETA UMOJA

14-18. (a) Yehova alikusudia nini kwa ishara aliyomfanya Ezekieli aifanye? (b) Je! Mungu aliwafanyia Israeli yaliyofananishwa na ishara ya Ezekieli?

14 Je! Yehova alikuwa na kusudi gani? Jambo fulani ambalo lingekuwa mwujiza kweli kweli, likiwaleta pamoja kama taifa moja, pamoja na faida kubwa aliyokusudia kwa ajili yao. Vile vile Mungu aliweka msingi wa uhakikisho wa umoja wa milele katika wakati wetu, wakati wa kutimilizwa kabisa kwa kusudi lake. Yeye alieleza:

15 “Nitawatwaa wana wa Israeli toka kati ya mataifa walikokwenda, nami nitawakusanya pande zote, na kuwaleta katika nchi yao wenyewe; nami nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi hiyo, juu ya milima ya Israeli; na mfalme mmoja atakuwa mfalme wao wote; wala hawatakuwa tena mataifa mawili, wala hawatagawanyikana kuwa falme mbili tena, hata milele.”​—Eze. 37:21, 22.

16 Umoja wa ajabu usingekuwa amani ya kuvumiliana tu kwa watu hawa waliogawanyika kwa kidini na kisiasa mmoja na mwenzake. Ingekuwa ya kweli, kutoka moyoni, kwa maana Yehova anaendelea:

17 “Wala hawatajitia uchafu tena kwa vinyago vyao, wala kwa vitu vyao vichukizavyo, wala kwa makosa yao mojawapo; lakini nitawaokoa, na kuwatoa katika makao yao yote, ambayo wamefanya dhambi ndani yake, nami nitawatakasa; basi watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.”​—Eze. 37:23.

18 Mungu aliurudisha umoja huko wakati alipowarudisha watu hawa waliotekwa nyara Yerusalemu kusudi wakairudishe ibada ya kweli. Walikuja kutoka kwa mataifa yote, watu wa kutoka katika kabila zote. Hata karne nyingi nyumaye, Yesu alipozaliwa, twawaona mawakili wa kabila kumi na mbili katika Palestina. (Matendo 26:7) Lakini umoja ulio kweli kweli, ulio wa milele chini ya “mfalme mmoja” ulikuwa unakuja bado.

19. Utimizo mkubwa zaidi wa ishara iliyotolewa kupitia kwa Ezekieli ulianza lini?

19 Lakini je! wakati ungekuja lini wakati ambapo umoja wa mataifa yote ungepatikana? Ulianza kwa njia ndogo nyuma ya Yesu kutiwa mafuta na roho takatifu ili awe mfalme. (Matendo 10:38) Yeye alisali kwa Mungu kwa ajili ya wale ambao wangekuwa ndugu zake za kiroho waliotoka katika kabila kumi na mbili za Israeli, na zaidi ya hayo, waliotoka kwa mataifa yasiyo ya Kiyahudi: “Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao. Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu.”​—Yohana 17:20, 21.

20. (a) Kwa sababu gani umoja sasa ni jambo la lazima kwa watu wote? (b) Mtunga Zaburi anaonyeshaje muhimu wa umoja chini ya “mfalme mmoja” wa Mungu?

20 Sasa tumo katika wakati ambapo umoja ni wa lazima, na si kwa ‘Israeli wa kiroho’ peke yake. (Gal. 6:16) Ulimwengu huu, ili uokoke, ni lazima uwe na umoja ulio kweli kweli, lakini hauwezi. Wala madhehebu zilizogawanyika za dini za Kristendomu, wala siasa wala sayansi haina ufumbuzi. Lakini, wafuasi wa Kristo wanao, si kutokana na hekima yao wenyewe, bali kutoka kwa Neno la Mungu. Mashahidi wa Yehova wamekuwa wakihubiri kuwako kwa yule “mfalme mmoja” katika mamlaka ya Ufalme kwa karibu miaka 60 sasa. Wametangaza uhitaji wa watu wote kuja chini ya utumishi na kibali cha yule “mfalme mmoja” aliyewekwa na Mungu, kama vile alivyoandika mtunga Zaburi: “Na sasa, enyi wafalme, fanyeni akili, enyi waamuzi wa dunia, mwadibiwe. Mtumikieni [Yehova] kwa kicho . . . [Mbusuni Mwana], asije akafanya hasira nanyi mkapotea njiani.”​—Zab. 2:10-12.

21. Mbali na Israeli wa kiroho, ni watu gani wanaotoa ushuhuda sasa si kwamba tu umoja wa mataifa yote unawezekana, lakini kwamba vile vile utakuja bila shaka?

21 Watu wote wanayo nafasi ya kuja katika umoja chini ya “mfalme mmoja” ikiwa ndivyo wanavyotamani. Tangu mwaka wa 1935 C.E. “mkutano mkubwa” wa watu wameshinda vizuizi na migawanyiko ya kitaifa, kikabila na ya kilugha. Hawa wanatumainia kuuokoka uharibifu wa ulimwengu uliogawanyika. Hawa, wakiwa na umoja ulio wa lazima kwa taifa la kibinadamu lililoungana katika mataifa yote, wanaweka mfano na ushuhuda kwamba taifa hilo la kibinadamu linaweza kuwako. Ndiyo. Inawezekana sana. Ni hakika, kwa maana Mungu amekusudia iwe hivyo.

22, 23. Kupitia kwa ‘mtumishi wa Yehova Daudi’ ni faida gani zinazoletwa kwa wale wanaokuja chini yake kama Mchungaji, kama zinavyosimuliwa katika Ezekieli 37:24, 25?

22 Hata sasa hivi kunayo ‘paradiso’ ya kiroho, “bustani ya Edeni” kati ya wale wanaomtumikia Yehova Mungu, ijapokuwa paradiso iliyo ya kweli pamoja na afya yote na dunia iliyorembeshwa ingali inakuja. Yesu Kristo ndiye “mchungaji mwema” anayewaleta wote pamoja kama “kundi moja.” (Yohana 10:11, 16) Yeye anatawala kama Daudi Mkuu, mrithi wa agano la Ufalme la milele. Yehova alionyesha sababu amani hiyo ipo, katika maneno yake ya unabii kwa Ezekieli:

23 “Na mtumishi wangu, Daudi, atakuwa mfalme juu yao, nao wote watakuwa na mchungaji mmoja; nao wataenenda katika hukumu zangu, na kuzishika amri zangu, na kuzitenda. Nao watakaa katika nchi niliyompa Yakobo, mtumishi wangu, walimokaa baba zenu, nao watakaa humo, wao na watoto wao, na watoto wa watoto wao, milele; na Daudi, mtumishi wangu, atakuwa mkuu wao milele.”​—Eze. 37:24, 25.

24-26. (a) Kwa sababu gani wale wanaokuja chini ya Mfalme na Mchungaji Yesu Kristo wanahakikishiwa amani? (b) Mungu amewafanyia nini wale wanaomtii ‘mtumishi wake Daudi’? (c) Wale walio watiifu wanajitahidi kutimiza nini sasa?

24 Yehova amemtoa kama “agano” au uhakika mzito wenye ahadi Mfalme Yesu Kristo, ambaye alionyesha kupendezwa kwa kweli na wanadamu alipokuwa duniani, hata akautoa uhai wake dhabihu. (Isa. 42:6) Hii inawahakikishia amani wale wanaomtii yeye. Umoja pamoja na Muumba unaoletwa na utawala wa Mfalme huyu unaelezwa na Mungu.

25 “Tena nitafanya agano la amani pamoja nao; litakuwa agano la milele pamoja nao; nami nitawaweka na kuwazidisha, na patakatifu pangu nitapaweka katikati yao milele. Tena maskani yangu itakuwa pamoja nao; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Na mataifa watajua ya kuwa mimi ndimi [Yehova], mimi niwatakasaye Israeli, patakatifu pangu patakapokuwa katikati yao milele.”​—Eze. 37:26-28.

26 Ibada safi ya Kikristo ya Yehova, patakatifu pake, i kati ya wale wanaoshikamana na Neno lake lililoandikwa, Biblia. Hema yake ya ulinzi wa kimungu na ujamaa i juu yao. Wao wanajitahidi kugeuza utu wao kwa kuyasitawisha matunda ya roho yake, upendo, furaha, amani, uvumilivu, fadhili, wema, imani, upole na kujiweza. (Gal. 5:22, 23) Hii inawaletea umoja. Inawezekana kwa watu wote leo kuungana nao na kutazamia uzima wa milele katika umoja na Mungu na wanadamu wenzao.

​—Kutoka Kitabu “The Nations Shall Know that I Am Jehovah”​—How?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki