Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 8/15 kur. 369-374
  • Mungu Awapenda Sana Wanyenyekevu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Awapenda Sana Wanyenyekevu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JAMBO GANI LILILO LA MAANA ZAIDI SASA?
  • JE! WEWE UNAIONA HAJA YA KIROHO?
  • LO! NAMNA MIPANGO YA YEHOVA ILIVYO YENYE KUFIKIA WATU WOTE!
  • MPANGO ULIO KAMA JAMAA
  • UKWELI WA JITIHADA
  • ITIKIA KATIKA IMANI
  • Katika Kundi, Itikia Huruma za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • “Naye Atawakaribia”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Mungu—Yeye Ni Nani?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Ujumbe Ambao Ni Lazima Tuutangaze
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 8/15 kur. 369-374

Mungu Awapenda Sana Wanyenyekevu

“[Yehova] ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.”​—Yak. 5:11.

1. Ibada ya Yehova Mungu ni yenye kuenea kwa kadiri gani, na hii inakamatana namna gani na Yakobo 5:11?

TANGAZO hili lenye kuvutia, “[Yehova] ni mwingi wa rehema, mwenye huruma,” linampendekeza Yehova kwetu, bila kujali sisi tukoje. Bila shaka tunataka tutendewe kwa huruma na kwa rehema na zaidi na Yeye ambaye tunamkubali na ambaye tunamwabudu kama Mungu Aliye Juu Zaidi. Watu wengi katika dunia yote kwa hakika wanamwabudu Yehova Mungu na wanapokea faraja nyingi na kutumainishwa katika kupokea kwao rehema na huruma za Yehova. Watu hawa wanaobarikiwa hivyo ni watu wa namna mbalimbali; kwa kweli, ni wa namna mbalimbali kama wasomaji wa gazeti hili. Wakati unapolifikiria shauri hili sasa linalotolewa kwako katika lugha yako mwenyewe na kulifanya lipatikane kwako mahali pako mwenyewe, utajua kwa hakika kwamba watu wengine, walio tofauti na wewe, wanaoishi mahali pengine wakiwa na desturi na namna mbalimbali za maisha, nao vile vile wanayafikiria maneno haya ya Yakobo mwandikaji wa Biblia. Yakobo alikuwa mwanafunzi wa Kristo Yesu na kwa hiyo, alikuwa Mkristo na mwabudu na shahidi wa Yehova, Mungu na Baba ya Yesu Kristo.

2. Ni katika vipindi gani vya historia ambapo sifa za upendo za Yehova zimeonyeshwa? Kwa nani?

2 Katika historia yote, sifa zenye upendo za Yehova zimeonekana kwa wale wanaomwabudu, zamani na vile vile sasa. Kwa kweli, katika kueleza kwake juu ya huruma na rehema za Yehova, Yakobo alielekeza kwa manabii wa Mungu wa nyakati za kale. Alitaja uhakika wa kwamba walitumia uvumilivu na wakavumilia mateso wakati walipokuwa wakisema katika jina la Yehova kama manabii na mashahidi wake. Katika sura ya 5, mstari wa 11, Yakobo anasema hivi: “Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa [Yehova] ya kwamba [Yehova] ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.” Hiyo ni kweli; mwisho wa Ayubu ulikuwa kweli ushuhuda wa kuonyesha rehema ya Yehova na upendo wa uaminifu kwa mtumishi wake mwaminifu Ayubu, aliyeendelea kuwa mkamilifu kwa Yehova. Inafaa kwamba, si mwandikaji wa Biblia Yakobo tu, bali sisi katika wakati huu tuyakubali mambo ya hakika ya historia ya kidini na kujua namna Yehova anavyoshughulika na wanadamu wenye ukamilifu na kutumia rehema na huruma zake kwa ajili yao. Matokeo mazuri haya yanaonwa sasa katika wale wa wanadamu wanaoona ubora wa shughuli zenye rehema za Yehova na kuziitikia.

3. Watu wanatofautiana katika njia gani?

3 Siku hizi zenye taabu ambazo katika hizo tunaishi zina mambo mengi ambayo ni yenye ukali na yasiyo ya rehema. Hali Zinazowazunguka wanadamu zinafanyiza namna zote za mapingamizi ya kipekee. Hii ni kwa sababu watu ni wa namna zote za maisha, wa “aina zote.” Hali hii ya namna mbalimbali ya maisha na hali za watu ni kubwa kweli kweli. Watu wengine wana elimu nyingi, wengine kidogo, na wengine wanayo ndogo sana. Wengine ni wenye asili moja ya kitaifa, wengine ni wenye asili nyingine na, kwa kweli, kuna mataifa mengi na hata lugha nyingi zaidi ambazo watu wanatumia. Hali ya vyeo inatofautiana na mtu huyu na mtu huyu kama ulivyo uwezo wa kimwili na wa akilini. Ijapokuwa wote wanao urithi wa kutokukamilika na kwa hiyo hawana tumaini la kweli la uzima pasipo mipango ambayo Yehova Mungu amefanya, kadiri ya kuasi kwa kila mtu matakwa ya haki ya Mungu inatofautiana na mtu huyu na mtu huyu. Inaonekana kwamba hakuna mwisho wa namna mbalimbali za maisha na hali za wanadamu.

4. Tofauti katika watu inakuwa na matokeo gani kwa habari ya Neno la Mungu?

4 Matokeo ni ya kwamba watu wanapokutana na Neno la Mungu wanaitikia katika njia za namna mbalimbali. Kwa watu wengine hakuna kuitikia ili watoe shukrani za upendo kwa mipango ya Muumba, kwa sababu wana kiburi mno, ni wenye kinaya mno au ni wenye kutakabari mno. Halafu, kwa upande mwingine, kuna watu wanaojiona kuwa wanyenyekevu sana hata wanajiona wenyewe kuwa hawastahili kupokea huruma na rehema za Yehova. Kwa wazi wewe ungali mtu wa namna tofauti​—wala wewe si mtu mwenye kinaya mno wala si mwenye kuvunjika moyo mno usiweze kufikia na kupokea ambacho Yehova anatoa kwako kama mtu mmoja. Ndiyo, unaweza kuona kwamba kweli unapendezwa na sifa zenye rehema na upendo za Yehova Mungu.

JAMBO GANI LILILO LA MAANA ZAIDI SASA?

5. Jambo gani linaonyeshwa hapa kuwa la maana zaidi kuliko namna ya maisha ya mtu?

5 Kwa kadiri unavyojifunza juu ya Neno ambalo Mungu mwenye rehema ametoa, Biblia Takatifu, ndivyo unavyofahamu zaidi ya kwamba, toka mwanzo mpaka mwisho, linafundisha kwamba wewe unatiwa au huenda ukatiwa katika baraka za Mungu. Ni jambo la maana sana kujua kwamba si namna ya maisha yako, bali, maoni yako sasa na itikio lako sasa la yale ambayo yametolewa na Yehova na kwa yeye yamefanywa yapatikane kwa namna zote za watu, kutia na wanyenyekevu, ndilo jambo la maana.

6. Ni nafasi gani iliyo kubwa ambayo imewapasa watu wote wafaidike nayo?

6 Kuonyesha kwamba Yehova kwa upendo anawezesha watu wa namna zote wapatane naye kupitia kwa Kristo Yesu inaonyeshwa mara nyingi. Kwa mfano, 1 Timotheo 2:3-6, NW inasema hivi: “Jambo hili ni jema na lenye kukubalika machoni pa Mwokozi wetu, Mungu, ambaye mapenzi yake ni kwamba aina zote za watu zipate kuokolewa na kupata maarifa sahihi ya kweli. Kwa maana kuna Mungu mmoja, na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, mwanadamu Kristo Yesu, ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi unaolingana kwa ajili ya wote​—hili ndilo linalopaswa kushuhudiwa kwa nyakati zake zenyewe.” Kutokana na hili, ni “aina” gani za watu zinazonyimwa nafasi ya kuokolewa na kupata kujua maarifa sahihi ya kweli? Hakuna! Hivyo watu wote wamepaswa wafaidike na toleo la kimungu. Kusiwe mtu wa kujifikiria mwenyewe kuwa juu kwamba asifaidike na mpango wa Mungu, na, wakati uo huo, kusiwe mtu wa kujiona mwenyewe kuwa mnyenyekevu mno hata ajione kutofaa kupokea na kujifunza kweli na hatimaye “ukombozi unaolingana kwa ajili ya wote” utumiwe kwa ajili yake ili aokolewe na urithi huu wa kutokukamilika, dhambi na mauti. Hili vile vile ni jambo la maana sana.

JE! WEWE UNAIONA HAJA YA KIROHO?

7. Ni maoni gani yanayofaa juu ya haja zetu za kiroho?

7 Huyu Kristo Yesu, “ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi unaolingana kwa ajili ya wote,” alipohudumia duniani mbele ya kufa kwake katika dhabihu alitangaza hivi: “Wenye furaha ni wale wanaoona haja yao ya kiroho, kwa kuwa ufalme wa mbingu ni wao.” (Mt. 5:3, NW) Wale wanaoona haja yao ya kiroho, au “walio maskini wa roho” (Union Version; The Kingdom Interlinear Translation), hawaonyeshwi hapa kuwa wanakataliwa kwa sababu ya kuwa maskini katika roho bali, pahali pake, wanatamkwa kama wakiwa wenye furaha, wenye kupendwa sana na Mungu? Kwa sababu gani? Kwa sababu wao wanaiona haja waliyo nayo na wanaikubali mipango ya kutosheleza haja yao ya kiroho. Si wenye kujipa moyo mno kwa kadiri ya kutakabari. Kama hii ingekuwa hivyo, wangekuwa wakijidanganya wenyewe katika kufikiri ya kwamba hawana haja ya mipango ya Yehova. Hapana, bali wakiwa wanyenyekevu katika roho na wakikumbuka ya kwamba wao, kama wengine wa wanadamu, wanayo haja inayoweza kutoshelezwa na mipango ya Yehova peke yake, wanakuwa na maoni yanayofaa katika shauri hili. Hawazuiwi na wazo fulani lenye makosa walilo nalo kwa sababu ya namna fulani ya maisha yao. Hili ni jambo ambalo ni zuri sana kwetu kulifikiria, bila kujali sisi tu nani na mahali tunapoishi duniani.

LO! NAMNA MIPANGO YA YEHOVA ILIVYO YENYE KUFIKIA WATU WOTE!

8. Mipango ya Yehova ni yenye kufikia wote kwa kadiri gani?

8 Neno la Mungu na makusudi ya Yehova kama yalivyoandikwa humo si kwa ajili ya kabila au taifa au jamaa fulani tu. Ukweli wenyewe ni kwamba watu wa mataifa yote wanakubalika kwa Mungu na wanapendwa na yeye, naye anawaruzuku wote kwa ukarimu. Maneno ya unabii juu ya hili yanapatikana katika Ufunuo sura ya 7: “Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za Mwana-Kondoo, wamevikwa mavazi meupe, wana matawi ya mitende mikononi mwao; wakilia kwa sauti kuu wakisema, Wokovu una Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo.” “Hawataona njaa tena, wala hawataona kiu tena, wala jua halitawapiga, wala hari iliyo yote. Kwa maana huyo Mwana-Kondoo, aliye katikati ya kiti cha enzi, atawachunga, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji yenye uhai, na Mungu atayafuta machozi yote katika macho yao.”​—Mist. 9,10, 16, 17.

9. Ili kupokea uhakikisho wa uangalifu wa Yehova kama unavyosemwa katika Ufunuo 7:16, 17, inatupasa tutimize takwa gani?

9 Tena hapa unaweza kuona namna mipango ya Yehova ilivyo yenye kuwafikia watu wote, ikikufikia wewe si kitu wewe ni mtoka ‘taifa au kabila au jamaa au lugha’ gani. Si kitu ikiwa wewe unaona njaa ile ile au ya mfano au kiu ya kuondolewa hali za ulimwengu za ukatili na zisizo za huruma, unapata katika unabii huu ahadi na tumaini la kutokuwa na njaa na kiu ya kutaka kuondolewa joto la hasira yake ikiwa kwa unyenyekevu unamhesabia Yehova wokovu. Je! wewe unafanya hivi, kumhesabia Mungu wokovu? Ikiwa sivyo, ni sababu gani? Je! kweli ni sababu ya kutosha kutokufanya hivyo? Ikiwa wewe waona njaa na kiu ya haki, bila shaka unaweza kushibishwa, kama ilivyosemwa tena na Yesu katika Mathayo 5:6: “Heri wenye njaa na kiu ya haki; maana hao watashibishwa.”

MPANGO ULIO KAMA JAMAA

10. Ni mambo gani yenye kuvutia yanayopatikana katika jamaa?

10 Mpango wa jamaa ndiyo mojawapo la mambo yanayotofautiana hapa na pale kulingana na desturi na taratibu za watu mbalimbali. Kwa kawaida, katika jamaa nzuri kuna ujamaa unaofaa na wenye kupendeza kati ya washiriki mbalimbali. Hivi ndivyo ilivyo zaidi kwa habari ya jamaa ambayo wote ni waabudu wa Yehova Mungu, na wote wanatumia matakwa na uongozi wake katika maisha yao ya jamaa. Uhakika mwingine juu ya jamaa zote ni wa kwamba ni zenye watu wa namna mbalimbali; huenda vikawako vitoto vichanga, watoto, watu wazima, watu wenye makamu na ambao ni wazee sana katika jamaa moja. Ijapokuwa katika njia mbalimbali kila mtu yu tofauti na wengine, wote wana mahali pao katika mpango wa jamaa na hakuna sababu kwa ye yote ajione kuwa mdogo mno machoni pa Mungu au wanadamu.

11. (a) Ni mpango gani ulio kama jamaa, na katika njia gani? (b) Ni maendeleo gani yanayowezekana katika “jamaa” ya Kikristo?

11 Wale wa “mkutano mkubwa” wa sura ya saba ya Ufunuo wanaletwa katika mpango ulio sawa na ule wa jamaa. Je! kuna sababu yo yote kwa wale waliomo katika mpango huu wa Kikristo ulio kama jamaa kuwa na maoni ya udogo kwa sababu ya uzee, vizuizi, kutokuwa na elimu, haya au kutokuwa na uwezo unaolingana na wengine katika jamaa? Hapana, hakuna sababu ya kujiona mdogo mno, ijapokuwa huenda mtu anajaribu kushinda udhaifu wake. Basi, ikiwa namna ya maisha yako imetokeza vizuizi vyako sasa, bila kujali ni vizuizi gani, imekupasa ukumbuke ya kwamba ukiwa mwaminifu sasa kwa Yehova Mungu utaweza kufanya mageuzi na kuwa mtu wa “aina” inayofaa kujidai kwako Mkristo. Njia moja ambayo katika hiyo Maandiko yanaonyesha geuzi hili inapatikana katika Waefeso 4:23, 24: “Mfanywe wapya katika roho ya nia zenu; mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.” (Tazama vile vile Warumi 12:2.) Je! hilo si jambo lenye kutia moyo na vile vile lenye kuvutia kwa mtu anayetaka aongeze ubora wa “aina” yake?

UKWELI WA JITIHADA

12. Ni jitihada gani iliyo ya lazima upande wetu?

12 Unyofu wa moyo wa mtu katika kuwa na tamaa nzuri unaonyeshwa, kwa sehemu, kwa jitihada anayofanya, akiitumia akili na moyo wake na kujaribu kuutimiza mradi huu. Ijapokuwa ni jitihada ya upande wake mwenyewe, haifanywi kwa nguvu yake mwenyewe, si kwa kutojali mpango ambao Yehova kupitia kwa Kristo Yesu anafanya ili kutosheleza haja ya kiroho anayoona. Angalia namna hili linavyosemwa katika 1 Timotheo 4:10: “Kwa maana twajitaabisha na kujitahidi kwa kusudi hili, kwa sababu tunamtumaini Mungu aliye hai, aliye Mwokozi wa watu wote, hasa wa waaminio.” Basi “aina zote za watu” zahitaji zifanye bidii na kujitahidi zenyewe. Na kwa baraka ya Yehova unaweza kufanya hivyo kwa kufaulu? Sasa, je! hilo si jambo lenye kutia moyo?

13. (a) Juu yako mwenyewe, ni jambo gani ambalo labda utafikiria kwa faida? (b) Kwa habari ya roho ya Mungu, ni mambo gani ya hakika yaliyo yenye msaada hapa?

13 Je! umepata kufikiria uhakika wa kwamba wewe kama mtu bi nafsi unazo sifa asizokuwa nazo mtu mwingine? Kwa kweli umepata kufikiria. Kuna mambo uwezayo kufanya katika njia na kwa kadiri ambayo hapana mtu mwingine awezaye kuyafanya sawasawa kama unavyoyafanya. Huna lazima ya kutahayarika kwa sababu ya mambo ambayo mtu mwingine anafanya au aweza kufanya. Pahali pake, itamfaa kila mtu azifikirie sifa zake mwenyewe, na kuzitumia hizi kwa kumsifu Yehova katika ibada yake. Kila mtu anazo karama za asili na hizi zaweza kusitawishwa kwa matumizi bora. Tena, ziko karama ambazo Wakristo wanapokea kupitia kwa utendaji wa roho ya Yehova Mungu, lakini hata katika hili si kila mtu aliye na karama ile ile. Bali, kama 1 Wakorintho 12:4-6 isemavyo: “Basi pana tofauti za karama; bali [kuna roho ile ile]. Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule. Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.” Mtu mnyenyekevu anaweza kuzisitawisha karama zake za asili na hata akajipatia nyingine mpya na aweza vile vile kupokea msaada na baraka za roho takatifu ya Yehova juu ya moyo na akili na jitihada zake, vyote hivi katika kumwabudu kwake na kumtumikia kwa furaha ‘Mungu yule yule azitendaye kazi zote katika watu wote.’

14. Kwa sababu ya sifa za watu wengine, ni maoni gani yenye usawa ambayo imempasa kila mtu awe nayo?

14 Mara nyingine inaweza kuwa msaada sana ikiwa mtu anawatazama wengine wanavyofanya. Labda atatazama huku na huku na kuwaona watu wengine walio na uwezo wa kufanya. Kwa kweli, katika kufanya hivyo huenda akajiona hawezi lakini haimpasi ajione hivyo. Bali, mtu anaweza kujifunza kwa kuzitazama sifa nzuri za mwingine, na kwa kadiri awezavyo labda anaweza kuchukua mfano wa sifa hizi na labda hata kuomba na kukubali msaada kutoka kwa mtu ambaye ni mwenye uwezo katika njia fulani. Walakini, haimpasi kwa hakika mmoja ajaribu kuwa mtu huyo mwingine, bali imempasa awe alivyo mwenyewe tu, na kuwa sehemu yo yote ya mwili wa tengenezo la Kikristo ambayo amegawiwa na Mungu.

15. Eleza mfano unaofaa wa mwili wa kibinadamu, kama unavyopatikana katika 1 Wakorintho, sura ya 12.

15 Kwa kweli, ikitumia mwili wa kibinadamu kama mfano wa tengenezo la kundi la Wakristo, Biblia inaonyesha kwamba sehemu za mwili zinazoonekana kuwa nyonge bado zinahitajiwa sana sana, kwa njia hiyo kutoa mfano wa wale ambao huenda wakaonekana kuwa wanyenyekevu katika kundi la Kikristo. “Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi? Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni mmoja. Na jicho haliwezi kuuambia mkono, Sina haja na wewe; wala tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, Sina haja na ninyi. Bali zaidi sana vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa vinyonge zaidi vyahitajiwa zaidi. Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana. Kwa maana viungo vyetu vilivyo na uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha mwili, na kukipa heshima zaidi kile kiungo kilichopungukiwa; ili kusiwe na faraka katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe. Na kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia nacho, na kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.”​—1 Kor. 12:19-26.

ITIKIA KATIKA IMANI

16. Ni kufikiria gani kwa imani ambako ni kwa lazima?

16 Akiisha kuweka katika akili zake uhakika wa kwamba Mungu awapenda sana wanyenyekevu, na kusadikishwa katika moyo wake kwamba yeye anaweza kutiwa katika mipango ya upendo ya Yehova, mtu mnyenyekevu anaweza, kwa faida, kukubali kwamba yeye, vile vile na wengine, yampasa awe na imani. Basi mwacheni anayejiona kuwa ana haja ya kiroho ajiulize mwenyewe hivi: Je! kweli mimi nina imani katika Yehova Mungu na katika Mwana wake? Je! ninaisadiki ahadi ya Mungu kunisaidia mimi? Maelezo ya Yesu juu ya hili yanaonyesha kwamba kusadiki huko kungeonyeshwa kwa kuendelea kumwomba Yehova roho yake, kama inavyosemwa: “Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa; kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa. Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamwombao?”​—Mt. 7:7, 8, 11.

17. Kwa habari ya roho ya Mungu, ni tofauti gani ya utendaji inayopaswa ifahamiwe?

17 Ulizo jingine: Je! wewe unafahamu kwamba roho ya Mungu inafanya matendo mbalimbali, ikifanyiza uwezo wa namna mbalimbali ambao washiriki wa kundi wanao, na katika njia hii kutoa mahitaji yote ya kundi? Hivyo ndivyo ilivyo, kwa sababu 1 Wakorintho 12:11, NW inatupasha habari kwamba “matendo yote haya roho moja ile ile huyafanya, ikimgawia kila mmoja mmoja kama ipendavyo.” Je! hii ingeweza kuelekea kuwa na maana ya kwamba mtu mnyenyekevu anategemea uwezo wake mwenyewe? Hata kidogo. “Mtu akisema, na aseme kama mausia ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina.”​—1 Pet. 4:11.

18. Mtu anawezaje kufaidika na nguvu ambayo Mungu anatoa? Toa mifano.

18 Ili matokeo mazuri ya nguvu ambazo Mungu anatoa yapatikane, ni lazima mtu awe tayari kupokea mafundisho na mazoezi na katika njia hii anaweza hata kuwa mwenye manufaa zaidi kwa Mungu kuliko yule anayeona hana haja na mafundisho, mazoezi au shauri. Mfano wenye kufaa wa hili wakati wetu unapatikana katika wahudumu wale ambao kwa kujitolea wanatumikia katika makao makuu na afisi za tawi za Sosaiti, zinazotengenezwa kwa kusudi la kusaidia kazi ya injili ya mashahidi wa Yehova katika sehemu mbalimbali za ulimwengu. Makao na afisi za tawi zinajaa sana wahudumu ambao wanafanyizwa kuwa jamaa ya Betheli. Wahudumu hao huenda kwanza wakawa hawana ujuzi kabisa katika kazi yenyewe ya maana ambayo wanaombwa waifanye. Kazi hii ni kutia na kushughulika na mambo mengi yanayohitajiwa ili kuchapa Biblia na mahubiri na vitabu vya kusaidia kujifunza Biblia vinavyogawanywa na mashahidi wa Yehova shambani mwote. Kwanza wengi hao wanaojitolea kufanya utumishi wa Betheli wanajiona kwamba huenda wasiweze kuzifanya hata kidogo kazi wanazogawiwa. Walakini, ni wanyenyekevu na wenye kutaka kufundishwa, wanapata mazoezi mazuri tangu mwanzo, wanajifunza mambo ya msingi, na wanajifunza kufanya mambo katika njia inayofaa. Kwa sababu hiyo, wanajifurahisha matokeo ya kweli na kuendelea kupata utimizo wa sehemu ya maana sana ya kazi ya tengenezo la kitheokrasi la Yehova.

19. Mnyenyekevu anawezaje kufanya maendeleo katika kundi?

19 Vile vile katika makundi ya mashahidi wa Yehova: wapya au walio na haya wamepaswa wakubali msaada unaopatikana, na kujaribu sana kushirikiana na tengenezo la kundi. Katika kufanya hivyo watajifunza njia bora na za msingi za kufanyia kazi ya kutoa ushuhuda, nao wenyewe watashiriki sana ndani yake. Lo! maendeleo mazuri namna gani ambayo wanyenyekevu wanafanya katika njia hiyo!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki