‘Ni Haya Yesu Akiitwa Mungu’
● Akiandika katika “The Expository Times”, Mwalimu wa dini Vincent Taylor anaarifu: “Injili zinaonyesha wazi kwamba ujuzi wa Yesu ulikuwa mchache, kwamba Yeye aliuliza maulizo kusudi apate ufahamu tu . . . kwamba Yeye alimpinga mtawala tajiri aliyemwita Yeye ‘Bwana Mwema’ kwa kumwuliza, ‘Kwa nini kuniita mwema? hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu.’ [Marko 10:18] Maulizo haya yamesababisha haya mara kwa mara na yataendelea kufanya hivyo ikiwa bila ya mageuzi Yesu ataitwa Mungu.” Lakini haitokezi ugumu wo wote mtu akilikataa fundisho la utatu na kuyaamini ambayo Yesu mwenyewe aliyasema, yaani, kwamba Mungu, Baba, ni mkuu kuliko Yesu Kristo.—Yohana 14:28.