Sababu Gani Kumtumaini Mungu?
Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi
1. Yehova anawataka nani kama watumishi wake?
YEYE Aliye Mkuu Zaidi, Mwenye Enzi wa ulimwengu wote, Yehova Mungu, anawataka kama watumishi wake wale wanaomtumaini kabisa peke yao. Wo wote wanaodai kuwa watu wake lakini wakimkana yeye kwa nia, neno na tendo hawawezi kutazamia kupata ukubali wake na baraka. Neno la Mungu linasema: “Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake, na moyoni mwake amemwacha [Yehova].”—Yer. 17:5.
2. Kwa sababu gani imetupasa kuona ubora wa onyo la historia ya kale ya Biblia?
2 Bila shaka hatutaki kuwa kati ya waliolaaniwa. Kwa kuwa Yehova Mungu hageuki, cho chote kilichofanya watu wabarikiwe au walaaniwe wakati uliopita ndicho kitakacholeta matokeo yale yale leo. (Mal. 3:6) Kwa hiyo ni hekima kwa upande wetu kuona ubora wa maonyo ya wakati wa kale kama yanavyopatikana katika Biblia.
MFANO WA KALE
3. Eleza Ohola alikuwa nani, Oholiba na “mama” yao.
3 Onyo moja kama hilo linatolewa kama mfano katika Ezekieli sura ya 23. Mfano huo unatia ndani dada wawili walioshindwa kumtumaini Mungu na kutazama upande mwingine kwa baraka na ulinzi. Dada mkubwa alikuwa Ohola na aliye mchanga zaidi, Oholiba. Ohola anaonyeshwa kama akifananisha Samaria, mji mkuu wa mwisho wa ufalme wa kaskazini au wa makabila kumi wa Israeli, na Oholiba kama akifananisha Yerusalemu, mji mkuu wa ufalme wa kusini wa Yuda. Miji mikuu ikifananisha falme, dada wanafananisha falme mbili. Kwa hiyo “mama” yao ni tengenezo lile moja la kitaifa la Israeli ambalo baba yake ni Ibrahimu, Isaka, Yakobo na wana kumi wawili wa Yakobo.—Eze. 23:2, 4.
4. Ni maandishi ya namna gani Ohola na Oholiba waliyojifanyia katika “ujana”?
4 Tangu mwanzo maandishi ya dada hao wawili hayakuwa bora. “Nao walizini huko Misri; walizini wakati wa ujana wao.” (Eze. 23:3) Hii ikawaje? Wazao wa Yakobo, waliokaa Misri wakati mmoja, walishindwa kuuzuia mtego wa ibada ya sanamu iliyoendeshwa katika nchi hiyo. Kwa kadiri ionekanavyo walianza kufikiri kwamba jambo fulani lingepatikana kwa kuicha miungu ya Kimisri. Waliacha kumtumaini Yehova kama Chanzo cha baraka za kweli na ulinzi, na kwa hiyo wakawa wenye hatia ya kufanya umalaya wa kiroho.
5. Kwa sababu gani Ohola angeweza kusemwa kama dada “mkubwa”?
5 Ndiyo, wakati ambao dada mkubwa Ohola na dada aliye mchanga zaidi walipoanza kufanya umalaya katika Misri, ufalme wa kaskazini wa Israeli na ufalme wa kusini wa Yuda hazikuwako. Lakini makabila ya Israeli ambayo mwishowe yalifanyiza falme hizo yalikuwako. Makabila yaliyofanyiza ufalme wa kaskazini, au Ohola, yalitia ndani na yale yaliyotoka kwa wana wakubwa zaidi wawili wa Yakobo, Reubeni na Simeoni, na vile vile kutoka kwa mwana mzaliwa wa kwanza wa Yakobo na Raheli, yaani, Yusufu, ambaye wana wake wawili Efraimu na Manase wakawa makabila mawili mbali mbali. Kwa hiyo Ohola angeweza kwa haki kuitwa dada “mkubwa.”
6. (a) Ni lini na namna gani Ohola na Oholiba wakawa wa Yehova? (b) Kwa sababu gani Ohola na Oholiba wangeweza kusemwa kama ‘wakizaa wana na binti’?
6 “Wakawa wangu,” alisema Yehova nyuma ya kuyaeleza maono ya Kimisri ya wanawake hao wawili wa mfano. Hili lilitukia mwaka wa 1513 B.C.E., Yehova alipowakomboa Waisraeli na kuwaleta katika agano kwa njia yake katika Mlima Sinai. Wakiwa wameingia katika agano na Yehova, taifa ‘liliolewa’ naye kama mke kwa mume. Washiriki mmoja mmoja wa taifa wakawa watoto wa tengenezo wa Yehova na kwa hiyo Ohola na Oholiba wangeweza kusemwa kama wakianza ‘kuzaa wana na binti’ tangu wakati huo na kuendelea.—Eze. 23:4.
KUSHINDWA KWA OHOLA KUMTUMAINI YEHOVA
7. (a) Ni lini na namna gani Ohola na Oholiba walipotokeza? (b) Jina “Ohola” lina maana gani, na kwa sababu gani hili linafaa?
7 Lakini, haikuwa mpaka mwaka wa 997 B.C.E. kwamba Ohola na Oholiba wa mfano wakatokeza wazi. Katika mwaka huo makabila kumi ya Israeli yalikataa kuendelea kuitii nyumba yenye fahari ya Daudi na yakasimamisha ufalme wao wenyewe. Uasi huu haukufuta agano ambalo taifa lote lilikuwa limeingia ndani yake na Yehova katika Mlima Sinai. Falme zote mpya zilikuwa zingali katika agano hili na kwa hiyo zilikuwa zingali chini ya Yehova kama kwa Mume wa kiroho. (1 Fal. 11:29-39) Lakini ufalme wa makabila kumi, Ohola, ulikataa kujinyenyekeza kama mke kwa Yehova na ukawa unaabudu sanamu. Ohola (likimaanisha “Hema Yake”) alipiga hema yake mwenyewe ya kuendeshea ibada ya kidini. Alimsahau Yehova, kwa kuwa ufalme wa kaskazini uliingilia ibada ya ndama wa dhahabu na nyumaye ukaingiza ibada ya Baali. Ohola vile vile aliacha kumtumaini Yehova kama Mlinzi wake na akazoea siasa na mataifa ya kipagani, zaidi Ashuru.—2 Fal. 15:17-22; Eze. 23:5-8; Hos. 5:13; 12:1.
8. Eleza yaliyotukia kwa Ohola kwa utimizo wa Ezekieli 23:9, 10.
8 Kushindwa kwa Ohola kumtumaini Yehova na kuendelea kuwa mwaminifu kwake kulileta mabaya. Ezekieli 23:9, 10 anasema: “[Yehova alimtia] katika mikono ya wapenzi wake, katika mikono ya Waashuri, aliowapendelea. Na hawa wakaufunua uchi wake, wakatwaa wanawe na binti zake, wakamwua yeye kwa upanga; akawa jina la aibu kati ya wanawake; kwa maana walitoa hukumu juu yake.” Ndiyo, Yehova aliuachilia ufalme wa kaskazini kwa Waashuru wakatili ambao kwa tamaa walipenda kuulazimisha urafiki wa kilimwengu. Waashuru walitenda kama wafikilizaji wa hukumu ya kimungu, wakimtendea Ohola wa mfano alivyostahili kutendewa mke mzinzi. Wao ‘waliufunua uchi wake’ kwa kuinyang’anya nchi watoto wake wa Kiisraeli, wakiwahamisha mbali sana. Na kwa upanga wa vita walimwua yeye kama taifa la kisiasa, wakiuharibu mji mkuu wake wa kitaifa Samaria, mwaka wa 740 B.C.E. Ohola kweli akawa “jina la aibu kati ya wanawake,” yaani, kwa falme za kipagani za wakati huo. Walimdharau kama taifa lililokuwa limepata aibu na walitetema kwa ajali yake.
OHOLIBA HAFAIDIKI KUTOKANA NA MFANO WA OHOLA WA KUONYA
9. (a) Maana ya jina “Oholiba” inakaziaje fikira kwenye pendeleo la kipekee lililofurahiwa na ufalme wa Yuda? (b) Oholiba alionyeshaje kwamba hakuona ubora wa pendeleo hilo?
9 Oholiba, akifananisha ufalme Wa Yuda, alikuwa na sababu nzuri ya kutazama sana ajali ya jirani yake. Kulingana na maana ya jina lake (“Hema Yangu I katika Yeye”), Oholiba alipendelewa kwa kuwa na hema ya Yehova au hekalu katika mji mkuu wake Yerusalemu. Lakini alishindwa kuona ubora wa hili. Lakini aliudharau mfano wa kuonya wa Ohola na kuendesha umalaya wake wa kiroho kwa njia ya kupita kadiri hata zaidi,—Eze. 23:11-17.
10. Oholiba alizoeaje siasa siku za wafalme Wayahudi Ahazi na Hezekia?
10 Akimsahau Yehova na agano lake lililolingana na ndoa, Oholiba, ufalme wa kusini, vile vile alizoea siasa na Ashuru. Hii ilikuwa mbaya hivyo siku za mfalme wa Kiyahudi Ahazi. Tofauti na onyo la Yehova kupitia kwa nabii Isaya, Ahazi alimwita mshindi wa Kiashuru Tiglath-pileseri amsaidie kupambana na falme zilizoungana za Shamu na Israeli. (Isa. 7:1-20; 2 Fal. 16:5-10, 17, 18) Mfalme Hezekia, mrithi wa Ahazi, aliona namna kujipendekeza kwa Ohola kwa upendeleo wa Ashuru kulivyomalizika kwa njia ya msiba mwaka wa 740 B.C.E., Samaria na ufalme wake ulipoharibiwa. Hali yeye, ingawa alikombolewa kutoka kwa mfalme wa Kiashuru Senakeribu, Hezekia aliukaribisha urafiki wa Wababeli,—Isa. 37:36–39:7; 2 Fal. 19:35–20:18.
11. (a) Ni lini zaidi Oholiba ‘alipozidi kuharibika kwa kupendelea kwake’ kuliko dada yake Ohola? (b) Lini na namna gani Oholiba akaanza ‘kukumbuka siku za ujana wake’?
11 Ni zaidi karibu na mwisho wa karne ya saba B.C.E., walipotawala Yehoyakimu na Sedekia kama wafalme chini ya Babeli, kwamba Oholiba ‘akazidi kuharibika kwa kupendelea kwake’ kuliko dada yake Ohola kwa kujipendekeza kwa upendeleo wa kisiasa wa Mamlaka ya Ulimwengu ya Kibabeli. (Eze. 23:11-16) Urafiki huu wa mataifa yote uliendelea wakati wa utawala wa wafalme wote mpaka Oholiba alipochoshwa na utawala wa Babeli. Kwa hiyo ‘nafsi yake ikafarakana’ na Wababeli kwa kumwasi mfalme wa Babeli. (Eze. 23:17) Wakati huo Oholiba alianza ‘kukumbuka siku za ujana wake, alipofanya mambo ya kikahaba katika nchi ya Misri,’ yaani, alianza kutazama upande wa kusini kuelekea Misri kwa msaada wa kijeshi ili kuutegemeza uasi wake.—Eze. 23:19.
12. (a) Yehova alionaje juu ya umalaya wa Oholiba, na hii ilimaanisha nini kwake? (b) Kwa sababu gani waliokuwa wapenzi wa Oholiba wangeweza kusemwa kama “watu wenye haki”?
12 Mwendo wa Oholiba, kama ule wa dada yake, ilikuwa lazima uongoze kwenye mabaya. Yehova alichukizwa na ufalme wa Yuda. Hii ilimaanisha kwamba, kama kwa habari ya ufalme wa kaskazini, Yehova angemwacha Oholiba wa mfano mikononi mwa wapenzi wake wenye tamaa. (Eze. 23:18-23) Oholiba alikuwa mwovu sana hivyo kwamba Yehova angeweza kumsema aliyekuwa mpenzi wake, Wababeli, kama “watu wenye haki,” yaani, walielekea kuwa “watu wenye haki.” Vile vile walikuwa “watu wenye haki” katika maana ya kwamba wangefikiliza hukumu ya haki ya Yehova. (Eze. 23:43-49) Kupitia kwa nabii wake Ezekieli, Yehova alionyesha mapema ambalo wapenzi hawa wangemfanyia Oholiba:
13, 14. Ukitumia Ezekieli 23:24-27 kama msingi, eleza yaliyosemwa yangetukia kwa Oholiba.
13 “Watajipanga juu yako . . . pande zote; nami nitawapa uwezo wa kuhukumu, nao watakuhukumu sawasawa na hukumu zao. Nami nitaweka wivu wangu juu yako, nao watakutenda mambo kwa ghadhabu; watakuondolea pua yako na masikio yako; na mabaki yako wataanguka kwa upanga; watawatwaa wanao na binti zako; na mabaki yako watateketea motoni. Pia watakuvua nguo zako, na kukuondolea vyombo vyako vya uzuri. Hivyo ndivyo nitakavyoukomesha uasherati wako, na uzinzi wako, ulioletwa toka nchi ya Misri; usije ukawainulia macho yako, na kukumbuka Misri tena.”—Eze. 23:24-27.
14 Kwa hiyo, Yehova Mungu angewaruhusu wapenzi wa Oholiba watumie maamuzi yake ya hukumu kulingana na njia yao wenyewe ya kikatili. Wangeuharibu uso mzuri wa Oholiba au sura ya kitaifa. Mfalme wake aliyetiwa mafuta na maafisa wengine wakuu, ambao walikuwa kama “pumzi ya mianzi ya pua [yake],” wangeondoshwa. (Omb. 4:20) Makuhani wake, waamuzi na wenye ujuzi wa vitabu, ambao walikuwa kama masikio ya kusikiza na kuusawazisha usimamizi wa taifa, vile vile wangeondoshwa kwa nguvu. Kilichosalia kwa Oholiba mzinzi kingepatwa na upanga wa kufisha wa Wababeli washindi. Wale ambao wangeokoka kati ya wana zake na binti wangechukuliwa mateka. Masalio yake, mali ya kimwili isiyoweza kuchukuliwa, ‘ingeteketea motoni.’ Hivyo Oholiba angevuliwa mavazi yake na vyombo vya uzuri ambavyo kwavyo alizoea utongozi wake kama taifa.
15. (a) Kwa sababu gani Oholiba hangeweza kuokoka mabaya kwa kuwaasi Wababeli? (b) Ni kikombe gani kilichojaa ambacho Oholiba angelazimishwa kunywa, na kwa kadiri gani?
15 Pengine Oholiba alifikiri kwamba angeokoka mabaya haya kwa kusikitikia ushirika na Babeli na kugeuka kwa kuchukizwa. Wababeli, hata hivyo, hawangesahau mapatano yake nao. Na kugeuka kwake kutoka kwa Wababeli na kuja kuwachukia hakukumwondolea mabaya aliyomfanyia Yehova Mungu. Oholiba hakuwa akitubu kwa sababu ya uzinzi wake wa kiroho. Alikuwa yungali na nia ya kuvunja agano lake na Yehova na kwa njia ya uzinzi ajitie katika mapatano na mataifa ya kipagani, kama vile Misri, ili kuhakikisha salama yake. Kwa hiyo Yehova angeufunua uchi wake kwa kuyafunua maandishi yake kama malaya asiye na haya. Kama dada yake Ohola, angelazimishwa kunywa kikombe kilichojaa cha uharibifu wa kitaifa na uhamisho kutoka nchi yake. Oholiba angelazimishwa kulipa kabisa malipo ya kimungu kwa kukosa kwake uaminifu kwa Mungu, kana kwamba akipaswa kutafuna na kusaga “vigae” vya kikombe chake ili kunywa kila tone la unyevu lililokuwamo. Kwa mataifa yenye nia ya ukorofi karibu naye, Oholiba angekuwa chombo cha ‘kudhihakiwa na kudharauliwa.’ Mambo haya yote yalimpata mwaka wa 607 B.C.E. wakati ambao Yerusalemu uliharibiwa kwa utimizo wa hukumu ya Yehova.—Eze. 23:28-35.
KUSHINDWA KWA KRISTENDOMU
16. Kwa sababu gani imempasa Kristendomu kukumbuka yaliyotukia kwa Ohola na Oholiba?
16 Kwa wazi Ohola na Oholiba, falme za Kiisraeli za kaskazini na kusini, walilipa malipo ya ajabu kwa kushindwa kumtumaini Mungu na kukosa kuwa waaminifu kwa ujamaa wao wa agano naye. Hii imepaswa iwe kama mfano wa kuonya kwa Kristendomu na wafuasi wake wote. Kwa sababu gani? Kwa sababu, kama Ohola na Oholiba, Kristendomu anadai kuwa katika ujamaa wa agano na Mungu. Lakini je! Kristendomu kweli anamtumaini Mungu? Je! pahali pake hakujiunga na taratibu za kisiasa za ulimwengu huu na je! yeye hatumaini uwezo wa kijeshi kwa ulinzi? Bila shaka! Kwa hiyo Kristendomu ana hatia ya umalaya wa kiroho. Neno la Mungu linatangaza: “Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu.” (Yak. 4:4) Kunayo maandishi ya ajabu ya hatia ya Kristendomu. Ni maandishi yanayolingana na maandishi mabaya ya Ohola na Oholiba, ambao juu yao mashtaka yafuatayo yalifanywa:
17. Ni dhambi gani mbaya zilizotia ndani umwagaji wa damu zilizofanywa na Ohola na Oholiba?
17 “Wamezini, na damu imo mikononi mwao, nao wamezini na vinyago vyao; tena wana wao walionizalia wamewapitisha katika moto ili waliwe nao. Tena wamenitenda haya; wamepatia unajisi mahali pangu patakatifu, siku ile ile, nao wamezitangua sabato zangu. Kwa maana walipokuwa wamekwisha kuvichinjia vinyago vyao watoto wao, ndipo walipoingia patakatifu pangu, siku ile ile, wapatie unajisi, na tazama, wamefanya hivyo kati ya nyumba yangu.”—Eze. 23:37-39.
18. Kristendomu amepakaje mikono yake madoa ya damu?
18 Uzinzi wa kiroho ambao kwa huo Kristendomu akajifanya mwenye hatia hauwezi kukanwa. Urafiki wake na wanasiasa usiokoma, majeshi na wafanya biashara wanaopata faida kubwa ni aibu ya waziwazi. Madhehebu ya kidini ya Kristendomu yamefanya uzinzi wa kiroho vile vile na “vinyago.” Pahali pa kuwaelekeza wanadamu kwenye ufalme wa Mungu kama tumaini la pekee kwa wakazi wa dunia, Kristendomu leo anaabudu Umoja wa Mataifa kama tumaini la mwanadamu kwa amani lililo bora na la pekee. Kristendomu amewatoa wana wake na binti zake kama dhabihu kwa mungu wa vita. Mikono yake ina madoa ya damu. Yeye amemwaga damu katika vita vya kidini, katika vita kati ya Wakatoliki na Waprotestanti, katika hukumu za wazushi wa dini na katika vita viwili vya kutisha vya ulimwengu katika karne hii, wakati ambao Wakatoliki walipigana na Wakatoliki na Waprotestanti wakapigana na Waprotestanti. Ingawa ni wenye mikono yenye damu, wafuasi wa Kristendomu wanaingia katika wanapopaita mahali patakatifu pa Mungu wakati wa inayoitwa “siku ya sabato.”
19, 20. Je! Ohola na Oholiba walitendaje kama malaya wastadi?
19 Maelezo ya kutenda kwa Ohola na Oholiba kama malaya wastadi vile vile yanamfaa Kristendomu. Maelezo haya yanasema;
20 “Mmewatuma watu kuwaita watokao mbali; ambao mjumbe alitumwa kwao, na tazama, wakaja; nawe ulijiosha kwa ajili yao, ulitia rangi macho yako, na kujipamba vyombo vya uzuri; ukaketi juu ya kitanda cha enzi, na meza imetandikwa tayari mbele yake, ambayo juu yake uliweka uvumba wangu na mafuta yangu. Na sauti za wingi wa watu wenye hali ya raha zilikuwa pamoja naye; na pamoja na watu wasio na adabu, waliletwa walevi . . . [na] wakawatia [wanawake] vikuku mikononi, na taji nzuri juu ya vichwa vyao.”—Eze. 23:40-42.
21. Kristendomu ametendaje kama malaya mstadi?
21 Kama malaya mstadi, Kristendomu amejaribu kujifanya mwenye kuvutia kadiri iwezekanavyo kwa ulimwengu, kwa kweli, hata kwa watu wapotovu zaidi, kama “walevi toka jangwani.” Madhehebu yake yameifanya dini nyepesi kwa walimwengu kama hao. Wanaweza kuungana naye kama washiriki wa makanisa wakati ule ule wakiendelea kuwa sehemu ya ulimwengu wenye choyo, unaoabudu sanamu na wenye madoa ya damu. Kama malipo kwa mapendeleo yo yote ya kidini yanayowaletea furaha ya kimwili, wanamtukuza Kristendomu. Kana kwamba ilikuwa, ili kuipamba mikono yake iliyogeuzwa myekundu na damu wanaweka vikuku mikononi mwake, na kuweka taji juu ya vichwa vya madhehebu yake, wakiwapa viongozi wa dini usimamizi wa kidini juu yao.
22. Ni nani au ni nini kitakachokuwa chombo cha kuleta uharibifu wa Kristendomu?
22 Maandishi ya Kristendomu yakiwa kama yale ya Ohola na Oholiba wa kale, yeye hawezi kuokoka mabaya. Kama vile waliokuwa wapenzi wa Ohola na Oholiba walivyowaharibu, vivyo hivyo Kristendomu ataharibiwa mikononi mwa waliokuwa wapenzi wake. Yehova Mungu atahakikisha hili limetukia. Hii inahakikishwa katika kitabu cha mwisho cha Biblia, ambamo milki ya ulimwengu ya dini ya uongo, “BABELI MKUU,” inaonyeshwa kama malaya. (Ufu. 17:3-6) Kwa habari ya ambalo waliokuwa wapenzi wa kisiasa watamfanyia “BABELI MKUU,” Ufunuo 17:16 panasema: “Hao watamchukia yule kahaba, nao watamfanya kuwa mkiwa na uchi, watamla nyama yake, watamteketeza kabisa kwa moto.”
23. Ni lazima mtu achukue tendo gani yasije yakampata mabaya pamoja na “BABELI MKUU”?
23 Ikiwa unataka kuokoka usipatwe na yatakayompata “BABELI MKUU,” mtumaini Yehova Mungu na kumtolea yeye ibada ya pekee. Huwezi kufanya hivi kwa kubaki katika lo lote la matengenezo ya kidini ya Kristendomu, ambayo yanafanyiza sehemu iliyo kubwa ya “BABELI MKUU.” Neno la Mungu linaamuru: “Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.” (Ufu. 18:4) Nyuma ya kujitenga na yeye, shiriki na wale ambao kwa kweli wanamtumaini Mungu na uendelee kuwa mwaminifu kwake.
—Kutoka Kitabu “The Nations Shall Know that I Am Jehovah”—How?