Je! Unaitumainia Sayansi kwa Ulimwengu Bora?
Makala Hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi
1. Je! ni maelekeo ya kawaida ya watu kuitumainia sayansi kwa ulimwengu bora?
JE! WATU wanaitumainia sayansi iuokoe ulimwengu kutokana na uharibifu na kuufanya mahali ambapo watu watapendezwa kuishi? Maoni huenda yakawa tofauti, wengine wakisema Ndiyo, wengine, Hapana. Lakini tunayosikia na kusoma katika matangazo ya biashara na ya radio na vile vile ya magazeti kwa kawaida yanaelekeza kwa ambayo mwanadamu anafanya au anayoweza kufanya kama ‘tumaini la pekee.’ Au mwisho kwa jumla unafikiwa kwamba ‘ikiwa kuna njia ya kufikia amani ya ulimwengu na furaha, ufahamu wa mwanadamu ni lazima uitoe.’ Mungu, kwa sababu hiyo, anasahauliwa.
2-6. Ni ushuhuda gani kwamba mwanadamu anasifiwa kwa ulimwengu bora unaonyeshwa katika gazeti la Boston, na katika Science News?
2 Mfano wa kuwaza kama huko ni makala katika Boston Herald Traveler juu ya habari “Je! Mwanadamu Anaweza Kuendesha Ulimwengu Wake?” Ilikazia fikira kwenye makosa makubwa sana ya mwanadamu, lakini ikamalizia: “[Mwanadamu] ataendelea kujikwaza, akimwagwa damu na kumwaga damu, . . . mpaka atakapojua namna ya kumaliza vita vyake au atakapoharibu kabisa sayari yake.”
3 Katika magazeti ya kisayansi, sayansi inasifiwa kama yenye karibu uwezo unaopita wa kibinadamu. Juzijuzi Science News, chini ya kichwa “Maarifa ya Uzazi: Uwongo au uhakika?” ilisema, katika mafungu yake ya kwanza:
4 “Taratibu ya maisha imevunjwa na maarifa ya uzazi yanakaribia. . . . ”
5 “Chini ya ufito wa ajabu wa elimu ya uhai na asili yake (biology) mwanadamu sasa polepole anakuwa tofauti sana na alivyokuwa. . . .”
Kwa kutoridhika kuwahesabia wanaume wanaopaswa matendo yaliyotiwa chumvi, makala inamalizia, ikiwapa cheo kizuri na madaraka makubwa kwa siku za usoni za wanadamu:
6 “Wataalamu Wapya wa elimu ya uhai na asili yake, tofauti na mfano wao wa uongo wa kisayansi, wanapendezwa sana na uwezo walio nao ili kuonyesha namna hali ya wakati ujao wa wanadamu itakavyokuwa na wanatamani kuona kwamba kazi yao bora haidharauliwi.”
7. Kikundi katika Kristendomu, kutia ndani na viongozi wa dini wa kisasa, kimefanya nini, na sababu gani tendo lao ni la upumbavu?
7 Je! ni jambo la busara kuhesabia sayansi na maendeleo yake ya mambo ya kimwili uwezo wa kuwaokoa wanadamu? Au ni jambo la akili kutumainia elimu ya kilimwengu na sayansi ya kisiasa, ambavyo vimesababisha sana hali iliyopo ya taabu? Lakini hivyo ndivyo kikundi cha maana, chenye kuongoza katika Kristendomu, kutia na viongozi wa kisasa wa kidini, kimefanya. Wameacha kumwabudu Mungu wa Biblia Takatifu, Yehova, na kuanza kuabudu mwingine wa chagua lao wenyewe. Hata wanakana kuwako kwake. Pahali pa kumtumainia kama chanzo cha hekima, wanawatolea wanasayansi wa kisasa na watu wenye busara heshima kuu, wakitia imani zaidi katika wanadamu vivi hivi kuliko wanavyoitia katika Yehova.
MAONI YA MUNGU
8-10. Yehova alimfunuliaje Ezekieli nia yake ilivyokuwa kuwaelekea Wayahudi waabudu jua?
8 Nia ya Mungu Mwenyezi ni nini, Muumba wa mwanadamu, aliyempa uwezo wa kuwaza na kutoa vitu vinavyotakiwa kwa hali yake njema? Yeye anaonaje juu ya kugeuka mwanadamu kuelekea sayansi kama mwokozi?
9 Yehova Mungu amefanya jambo fulani liandikwe katika Neno lake Biblia linaloonyesha anavyoona, na atakayofanya juu yake. Hili linapatikana katika ripoti ya nabii Ezekieli juu ya yaliyokuwa yakiendelea pale pale kati ya watu walioitwa wa Mungu katika Yerusalemu karibu miaka mitano tu mbele ya uharibifu wake katika mwaka wa 607 B.C.E. Akisimulia aliyoona katika njozi, Ezekieli aliandika:
10 “Akanileta mpaka ua wa ndani wa nyumba ya [Yehova], na tazama, mlangoni pa hekalu la [Yehova], kati ya ukumbi na madhabahu, walikuwako watu kama ishirini na watano, wamelipa kisogo hekalu la [Yehova], na nyuso zao zimeelekea upande wa mashariki, nao wanaliabudu jua, kwa kuuelekea upande wa mashariki. Basi, akaniambia, Umeyaona haya, Ee mwanadamu? Je! ni jambo dogo sana kwa nyumba ya Yuda, wayafanye machukizo wanayoyafanya hapa? kwa maana wameijaza nchi hii udhalimu, tena wamerejea nyuma ili kunikasirisha; na, tazama, wanaliweka tawi puani [mwangu]. Kwa sababu hiyo mimi nami nitatenda kwa ghadhabu; jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma, na wajapolia masikioni mwangu kwa sauti kuu, sitawasikiliza.”—Eze. 8;15-18.
11, 12. Wanaume fulani wa Kiisraeii walikuwa wakimpa Yehova kisogo namna gani, na kwa kuvunja amri ipi?
11 Hapo wanaume hawa wa Kiisraeli walipokuwa, palikuwa ni behewa la ndani la hekalu palipowekwa wakf kwa Yehova. Walikuwa karibu na ukumbi wa hekalu lenyewe, katika nafasi iliyo katikati ya ukumbi na madhabahu ya kutolea dhabihu iliyo katikati ya behewa ya ndani. Lakini, jambo la kushangaza, hawakuwa wakimwabudu Yehova mahali hapo, wala hawakuwa wakiinamia madhabahu yake ya kutolea dhabihu iliyokuwa upande wao wa mashariki. Ingaliwapasa kutazama magharibi, kuelekea hekalu. Sababu gani?
12 Basi, hapo katika chumba cha hekalu cha ndani kabisa, Patakatifu Zaidi Sana, palikuwa na Sanduku la Agano lililokuwa takatifu. Juu yake palikuwa na nuru ya mwujiza Shekina iliyofananisha kuwako kwa Yehova. Lakini kuliko kutazama makao haya ya mfano ya Mungu wale wanaume ishirini na watano walikupa Kuwapo kwa Kimungu kisogo na kutazama mashariki. Wakimtupilia mbali Mungu waliyedai kuwakilisha, walikuwa wameinama wakiabudu jua katika anga! Hii ilikuwa kuvunja amri ya Mungu moja kwa moja iliyo katika Kumbukumbu la Torati 4:15-19.
13. Wayahudi hao 25 waabudu jua waliongezaje matukano kwa Yehova?
13 Kwa kutoridhika na kutokutii huku kwa wazi, wale wanaume waliongeza jeuri, kwa kuwa, “tazama,” Yehova alisema, “wanaliweka tawi puani [mwangu].” (Eze. 8:17) Tawi hili lilitumiwa katika ibada ya sanamu na huenda ikawa lilikuwa limekatwa kwa njia fulani kuwakilisha uume au kiungo cha uzazi cha mwanamume. Kwa vyo vyote ni lazima liwe lilikuwa jambo la kukasirisha sana au la matusi kulishikilia puani mwa Yehova, kana kwamba angalifurahia kulinusa. Ibada hiyo ya sanamu ya namna ya jua kwa upande wa hao wanaume ishirini na watano ilifuatana na tendo lao la kujaza “nchi hii udhalimu.”
WATUKANAJI WA KISASA WA MUNGU
14, 15. Kristendomu vile vile amempaje Yehova kisogo?
14 Je! Kristendomu, kwa kweli, kwa uhakika, amefanya mambo mabaya sawasawa na yaliyofanywa na hao wanaume wa Kiyahudi? Je! kuna usawa wa kisasa? Ndiyo.
15 Sayansi ya kisasa imetendewa kama “ng’ombe mtakatifu,” ambaye ni lazima achukuliwe kwa heshima na ambaye ni lazima achukuliwe kuwa mbele ya Biblia na Mungu. Busara ya wanasayansi inayodhaniwa kuwa “yenye maendeleo,” pamoja na mafundisho yake yote, imetendewa kama namna ya kisasa ya hekima iliyoifanya Biblia kuwa “kuukuu.” Kwa kweli ufundi wao unaweza kuchunguza sheria za Mungu kwa kadiri ndogo tu na unaweza kufanya kazi katika mipaka tu ya sheria hizo. Lakini njia mbalimbali za kupasha habari karibu kila mara zinasifu ufundi wenyewe pahali pa Mungu aliyewezesha iwe hivyo. Zinasema kana kwamba mwanadamu ni mkuu, ‘akivumbua siri za maumbile’ na kuwa bwana wa ulimwengu wote.
16. (a) Je! mwenendo huu wa ibada kuelekea viumbe ni jambo jipya? (b) Sababu gani mwenendo huu ni wa hatari sana leo?
16 Je! mwenendo huu ni jambo jipya, kukazia huku kwa fikira zote kuelekea kiumbe cha kibinadamu, kutoa huku kwa sifa yote kwa mwanadamu ambaye Mungu aliumba? Hapana, maelekeo ya wanadamu kufanya hivyo yalielezwa karne nyingi zilizopita na mmoja wa mitume, aliyeandika: “Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika; wakaubadili utukufu wa Mungu asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo.” Tofauti na uzito mkubwa wa jambo lenyewe, lakini, ni kwamba sasa wakati umefika kwa ulizo kufikia upeo na kumalizwa milele.—Rum. 1:22, 23.
17. Kutua mwezini kwa majuzi kunaonyeshaje ambukizo la wanasayansi na ibada ya jua?
17 Ambukizo la Kristendomu na ibada ya miungu ya uongo, kutia ndani na kuabudu kwa sayansi ya kisasa, linajionyesha lenyewe wazi kwa ujanja sana. Kwa mfano, Julai 20, 1969, wakati ambao mwanaanga wa kibinadamu aliukanyaga mwezi mara ya kwanza, ni nani aliyetukuzwa kwa sababu hiyo, kulingana na namna kundi la kisayansi linalopaswa katika mpango huo lilivyoviita vitu vilivyotumiwa? Bila shaka si Yehova, Muumba wa mwezi. Ni mungujua wa uongo aliyetukuzwa. Namna gani hivyo? Kwa kuwa chombo cha anga kilichoundwa na mwanadamu na kutumiwa wakati huo (kama kinavyotumiwa kwa kutua juu ya mwezi nyuma ya hapo) kilipewa jina la “Apollo.” Kati ya vyanzo vyote vya majina vilivyoko, asili ya miungu ya Kigiriki ilichaguliwa. Phoebus Apollo alikuwa mungujua wa Wagiriki wa kale na alikuwa ndugu pacha wa Artemi (au, Diana), mungu-mwezi wa kike.
18. Sababu gani ulikuwa upumbavu kuvipa vyombo hivi vya anga majina ya kipagani, na Kristendomu amezidi kuonyesha kwamba anaabudu “jua” la kisayansi namna gani?
18 Sababu gani watu wenye busara watumie sheria za Muumba kutimiza tendo la ajabu na kisha kutangaza na kulipa fahari jina la mungu-jua wa kale, ambaye kwa kweli si mungu hata kidogo? Ni wazi kwamba fahari ya wanadamu inawekwa mbele ya Mungu. Zaidi ya hayo, ukubali wa kawaida wa Kristendomu wa fundisho lisilohakikishwa la mageuzi ni mmojawapo wa uhakika unaomweleza wazi kama mwabudu “jua” la wanasayansi.
19, 20. Onyesha matokeo juu ya Kristendomu ya kuabudu “jua” la kisayansi.
19 Je! maelekeo haya ya sayansi kuelekea upagani, ambamo sayansi inatumainiwa kama “jua,” chanzo kikubwa cha kuwaelimisha wanadamu, yamewaleta wanadamu karibu zaidi na ulimwengu bora? Huko nyuma katika siku za Ezekieli mwendo kama huo ulileta jeuri katika nchi ya Israeli. Leo haujakuwa bora. Viongozi wa dini wa Kristendomu ama wamekuwa hawataki ama wamekuwa hawawezi kusimamisha matumizi ya sayansi ya kisasa ya kuvumbua na kutumia silaha za vita za kikatili zaidi, yaliyofikia upeo wa kuendeleza makombora yenye nguvu sana. Pigano la Vita ya Kwanza ya Ulimwengu na ya Pili lilitegemea sana utendaji wa wanasayansi. Jeuri iliyojaza dunia haikuletwa na vita hivyo viwili tu vilivyopiganwa zaidi na Kristendomu. Elimu ya kilimwengu ya kisasa inayoabudiwa imewaondolea watu wenye kwenda kanisani kicho cha kweli cha Mungu, na jeuri inatendwa sehemu nyingi, hata wakati wa amani. Kipindi cha wakati tangu 1914 C.E. kimeitwa rasmi “Kizazi cha Jeuri.”
20 Ufundi wa sayansi ya kisasa umetumiwa katika uchumi na biashara. Matokeo yake yamekuwa ni uchafu unaoongezeka unaoharibu mazingira ya asili ya wanadamu. Inahofiwa kwamba dunia hii karibuni itakuwa mahali pasipofaa kwa kuwako kwa wanadamu. Na namna gani juu ya mazingira ya kiadili ya wanadamu?
21. Kristendomu, kwa sababu hiyo, ‘amewekaje tawi la matusi puani mwa Yehova’?
21 Adili mpya imechaguliwa inayoona hata uasherati, uzinzi na kulalana kwa mwanamume na mwenzake na mwanamke na mwenzake kama mambo ya kujifurahisha na inayaruhusu kihalali. Viongozi wa dini wa Kristendomu wanajizuia wasitangaze ambayo Biblia inasema juu ya mambo haya. Kwa kweli, viongozi wengi wa dini wakubwa wamejitokeza hadharani kwa kupendelea sheria ambazo zinawaweka huru wafisadi na adhabu kwa kutenda mambo machafu kama hayo. Magonjwa ya kisonono na kaswende yanaendelea kuongezeka kwa sababu hiyo, kwa kweli, yamewashika watu wengi! Ikiwa hii inawachukiza watu wengi wanaomcha Mungu leo, je! ni lazima iwe namna gani kwa Mungu mwenyewe? Ni jambo la kuchukiza sawasawa na wakati ambao wale waabudu 25 katika hekalu la Yehova katika Yerusalemu walipokuwa kwa matusi ‘wakiliweka tawi’ puani Mwake.
JE! MUNGU ATAFANYA NINI JUU YAKE?
22, 23. Yehova alichukua hatua gani kama matokeo ya ibada ya sanamu ya jua ya Wayahudi?
22 Mbali na kumwonyesha Ezekieli machukizo yaliyokuwa yakiendelea katika hekalu la Yehova katika Yerusalemu, je! Yeye alichukua hatua yo yote kama matokeo? Ndiyo. Kama alivyosema: “Mimi nami nitatenda kwa ghadhabu; jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma, na wajapolia masikioni mwangu kwa sauti kuu, sitawasikiliza.”—Eze. 8:18.
23 Jambo hili kwa kweli lilitokea? Ndiyo. Wakati ambao, karibu miaka mitatu na nusu tu nyumaye, Nebukadreza aliuzingira Yerusalemu, watu walikuwa katika msiba mkubwa. Ilikuwako njaa kubwa. Akina mama hata waliwala watoto wao wenyewe. Maradhi yaliwaua maelfu. Ugomvi kati ya Wayahudi waliozingirwa uliongezea taabu. Askari wa Nebukadreza walipouingia mji, wachanga kwa wazee waliuawa barabarani. Wakuu walinyongwa. Watumwa walikokotwa utumwani Babeli. Hata ingawa Mungu alikwisha weka jina lake katika mji na hekalu, hakutenda ili kuwaokoa, hasira yake ilikuwa nyingi sana kwa sababu ya ibada ya sanamu yenye kuchukiza ya Wayahudi na mazoea yao machafu. (Omb. 2:21; 4:9, 10; 5:12) Je! tufikiri Mungu atatenda tofauti leo?
24. Kristendomu ameletaje suto kubwa zaidi juu ya jina la Mungu kuliko wale Wayahudi waabudu jua katika siku za Ezekieli?
24 Kristendomu amedai kuwa na jina la Mungu na la Kristo na kuwaongoza watu katika njia zao. Lakini, tofauti yake, Kristendomu ameleta suto lililo kubwa zaidi juu ya Yehova Mungu na Mwanawe na juu ya ibada Yake. Amekuwa chombo katika mkono wa adui wa Mungu Shetani Ibilisi cha kuwaondoa wengi iwezekanavyo kutoka kwa Mungu wa kweli.
25, 26. Biblia inaonyesha ni nini kitakachompata Kristendomu na wale aliogeuza katika ibada ya “jua” la kutengenezwa na mwanadamu la sayansi?
25 Kama matokeo, Kristendomu mwasi, kafiri, pamoja na taratibu zake za kidini, ataona hasira ya Yehova bila huruma na bila kusikiwa kwa vilio vyao. Biblia inaeleza kuanguka kwa milki ya ulimwengu ya dini ya uongo, Babeli Mkuu wa mfano, ambaye Kristendomu ndiye sehemu yake yenye nguvu. Likimfafanua kama kahaba mkuu, Neno la Mungu la unabii linasema: “Mapigo yake yatakuja katika siku moja, mauti, na huzuni, na njaa, naye atateketezwa kabisa kwa moto. Kwa maana [Yehova] Mungu aliyemhukumu ni mwenye nguvu.”—Ufu. 18:2, 8.
26 Ndipo kugeuza kwake kwa viongozi wa ulimwengu katika ibada ya “jua” ya sayansi ya kibinadamu pamoja na fundisho lake la mageuzi kutakapozaa matunda yake yote. Biblia inafunua kwamba taratibu za kisiasa na za biashara zitashindwa na kuangamizwa katika mikono ya Yesu Kristo katika pigano la Har–Magedoni, ambalo linakuja mara tu nyuma ya uharibifu wa dini za uongo.—Ufu. 16:14-16; 19:17-21.
27. Ni nani atakayefaidika kutokana na tendo kali la Mungu juu ya “waabudu jua” wa kisasa?
27 Tendo la Mungu, ingawa kali, litakua kwa faida ya wale wasioheshimu na kutukuza jua, kwa upumbavu na kwa njia ya ibada, liwe ni tufe la kawaida lililo angani, au liwe ni “jua” la kibinadamu la inayoitwa sayansi. Wao ni watu wenye heshima kwa Muumba wa ulimwengu wote. Wanamtumainia kwa uzima na faraja za taratibu bora, na hawatakata tumaini.—Isa. 45:22.
28. Watu ambao wameweka tumaini lao katika “jua” la sayansi ya kibinadamu wanapaswa kufanya nini?
28 Hata wale walioitumainia sayansi, wakifahamu kwamba wamekuwa wakiabudu sanamu, wanaweza kupata msamaha, wakimgeukia Mungu. Kwa kuwa “[Yehova] ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.” Wanaweza kujifunza juu ya mipango yake kupitia kwa funzo la Biblia na wanaweza kutazamia baraka alizokusudia kwa wanadamu mwanzoni—dunia safi kwa kweli, yenye haki. Halafu wataona ukweli ambao juu yake mtunga Zaburi aliimba kale: “[Yehova], Mungu, ni jua na ngao, [Yehova] atatoa neema na utukufu. Hatawanyima kitu chema hao waendao kwa ukamilifu.”—Yak. 5:11; Zab. 84:11.
—Kutoka Kitabu “The Nations Shall Know that I Am Jehovah”—How?