Maswali Kutoka kwa Wasomaji
● Je! mashahidi wa Yehova wanaonaje adhabu ya kifo?—U.S.A.
Mashahidi wa Kikristo wa Yehova wanashikilia ambayo Maandiko Matakatifu yanatoa kama maoni ya Mungu ya adhabu ya kifo. Wanajua kwamba Yehova Mungu, kama Muumba wa mwanadamu, ana haki yote kabisa ya kuweka sheria ambazo ni lazima zitiiwe ikiwa mtu ataendelea kufurahia maisha. Kwa hiyo, wakati Mungu anapoamua kwamba watu fulani wanastahili hukumu ya kifo kwa sababu ya kuendelea katika mazoea ya dhambi, anaweza kuchukua uhai wao kwa haki. Mifano miwili inayojulikana ya adhabu ya kifo kama hiyo iliyotolewa na Mungu ni uharibifu wa wanadamu wasiotii katika Gharika nyumaye uharibifu wa Sodoma na Gomora.—2 Pet. 2:5, 6.
Kama Mpaji wa Sheria, Mwamuzi na Mkuu Mwenye Enzi Yote, Yehova Mungu anaweza vile vile kuwapa wengine uwezo wa kufisha wavunjaji wa sheria. Nyuma ya gharika ya siku za Nuhu kwa mfano, aliwapa wanadamu uwezo wa kutoa adhabu ya kifo kwa uuaji wa kukusudia. Tunasoma: “Atakayemwaga damu ya mwanadamu damu yake huyo itamwagwa na mwanadamu maana kwa mfano wake Mungu alimfanya mwanadamu.” (Mwa. 9:6) Mamlaka (uwezo) ya kibinadamu, kwa kumfisha mwuaji, ingekuwa ikitenda kama “mtumishi wa Mungu, amlipizaye kisasi mtenda mabaya kwa ajili ya ghadhabu.”—Rum. 13:4.
Kwa kweli, wengine wanaweza kutia shaka kama mamlaka za kibinadamu zinaweza kwa haki kuwafisha watu mmoja mmoja kwa sababu ya matendo ambayo Neno la Mungu halionyeshi yanastahili kifo. Huo ni wajibu ambao serikali ni lazima zichukue mbele za Mungu. Lakini hakuna msingi wa Biblia wa kusema kwamba serikali zinalaaniwa kwa kuagiza hukumu ya kifo kwa wauaji. Maoni ya Mungu ni kwamba mtu anayetoa uhai wa mtu mwingine kwa kukusudia anapata hasara ya uhai wake mwenyewe. Leo, hata hivyo, serikali nyingi zinaachana na maoni ya Mungu ya adhabu ya kifo, hii bila shaka ikiwa ni sababu moja ya uhalifu ulioongezeka na uvunjaji wa sheria.