Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 1/1 kur. 8-14
  • Kumhimidi Yehova Katika Mashirika Yetu ya Kila Siku

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kumhimidi Yehova Katika Mashirika Yetu ya Kila Siku
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • PENYE KAZI YETU YA KIMWILI
  • SHULENI AU MASOMONI
  • PENYE MAKUSANYIKO PAMOJA NA NDUGU ZETU
  • TUNAPOKUWA PEKE YETU
  • Mahali pa Vijana Katika Jamii ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Tunawafurahia Vijana Wanaotembea Katika Njia ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Vijana Wakristo Iweni Imara Katika Imani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Jihadhari na Mashirika Mabaya Katika Siku Hizi za Mwisho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 1/1 kur. 8-14

Kumhimidi Yehova Katika Mashirika Yetu ya Kila Siku

“Mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.”​—1 Kor. 10:31.

1. (a) Kanuni ya Maandiko inayopatikana katika 1 Wakorintho 10:31 ina matumizi makubwa namna gani? (b) Ni sehemu gani ya maisha ya kila siku ambayo tutaangalia katika somo letu?

KUMHIMIDI Yehova maana yake ni kumsifu, kumtukuza. Kama watumishi wa Yehova waliojiweka wakf, mashahidi wake wametoa kabisa maisha zao ili wamhimidi Mungu wao, Yehova. Hivyo ni kwa kupendezwa kwa moyo kwamba tunaangalia maneno ya mtume Paulo: “Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.” (1 Kor. 10:31) Tunafahamu kwamba, wakati Paulo anapozungumza maoni ya Mkristo juu ya kula na kunywa katika mstari huu yeye anasema kanuni kubwa​—kufanya mambo yote kwa utukufu wa Mungu​—ambayo imepaswa iongoze kila jambo tunalofanya. Kama Wakristo wa kweli, sisi tunajua kwamba huduma yetu kwa wengine, kuhudhuria na kushiriki kwetu katika mikutano ya kundi, na funzo letu la kipekee na la jamaa zote hizi ni njia ambazo tunamhimidi na kumsifu Yehova. Lakini kwa karibu wote wa sisi, mambo haya ya kwanza katika maisha zetu yakiisha kufanywa, sehemu kubwa ya maisha yetu ya kila siku inabaki. Tunawezaje kumhimidi Yehova katika wakati huu na katika mashirika yanayoletwa na wakati huu?

2. Ni katika nyakati gani ingekuwa lazima kwa Wakristo kuwa katika ushirika na wasioamini, na imetupasa tujihadhari na nini?

2 Ni vizuri kwetu kuangalia katika jambo hili kwamba, ingawa Wakristo wa kweli hawatafuti ushirika wa watu wa kilimwengu, ni lazima mara nyingi kuandamana na watu hao. (Yohana 17:15, 16) Mara nyingi inawapasa akina baba kutumia sehemu kubwa zaidi ya saa zao za kila siku wakifanya kazi pamoja na washiriki wa kilimwengu ili wapatie jamaa zao riziki. Watoto wa masomo, ili wapate elimu, inawapasa watumie sehemu kubwa ya wakati wao wakiwa pamoja na wanashule wenzao wasiojali kumhimidi Yehova. Zaidi ya ushirika huo ambao ni wa lazima, Wakristo wa kweli wataepuka kuandamana au kufanya urafiki na wale wasioshiriki upendo wao kwa Yehova Mungu. Ni mwendo wa hekima na maisha kufanya hivyo.​—1 Kor. 15:33; Mit. 13:20.

3. Ni katika vipindi gani vingine kuliko wakati wa funzo la kipekee, mikutano na utumishi wa shambani imetupasa tuangalie kumhimdi Yehova?

3 Kwa kuwa Wakristo wengi sana inawapasa wakutane na mashirika ya kilimwengu kila siku ili watimize madaraka yao, tutazungumza namna tunavyoweza kumhimidi Yehova kwa maneno yetu na mawazo yetu katika mashirika yetu yote ya kila siku. Kwa kuongeza, hii ingetia vipindi vile wakati tunapoweza kukusanyika pamoja na ndugu zetu kwa viburudisho na hata nyakati zile wakati tunapojikuta tuko peke yetu. Ndiyo, tunawezaje kumhimidi Yehova katika mashirika yetu ya kila siku?

PENYE KAZI YETU YA KIMWILI

4. Ni katika njia gani nyingine zaidi ya mwenendo wetu mzuri tunaweza kumhimidi Yehova mahali tunapofanya kazi ya kimwili?

4 Ninyi vichwa vya jamaa vya Kikristo mnalo daraka zito kupatia jamaa zenu riziki, na mara nyingi kulitimiza kunawaingizeni katika kushirikiana na watu wa kilimwengu mahali penu pa kazi. Bila shaka, mwenendo wenu mzuri ni ushuhuda mwema kwa watu hao na unaleta utukufu kwa Yehova. Lakini ziko vile vile nafasi za kumhimidi Yehova kwa usemi wetu katika mashirika haya. Maongezi ya wafanya kazi wenzetu kwa kawaida yanakuwa juu ya hali za kilimwengu na matukio, sivyo? Kwa kadiri hali za ulimwengu zinapoongezeka kuwa zenye taabu na zenye kufadhaisha na kwa kadiri kusumbuka kwa watu kunavyoongzeka, ndivyo na nafasi zetu zinavyoongezeka kugeuza mawazo ya wafanya kazi wenzetu kwenye ufumbuzi ulioahidiwa wa Yehova kama unavyosemwa katika Biblia.​—Luka 21:25-33.

5. Tunaweza kufundishaje wafanya kazi wenzetu kwa matokeo juu ya Biblia? Tungetaka tuepuke nini?

5 Katika kutoa ushuhuda huo kwa wafanya kazi wenzetu tunataka tufuate shauri la Paulo kwa Timotheo mahali ambapo anasema hivi kwa sehemu: “Haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi; bali kuwa mwanana kwa watu wote, . . . akiwaonya kwa upole wao washindanao naye.” (2 Tim. 2:23-26) Ndiyo, kwa kutumia maulizo ya busara, kuwatia katika mazungumzo na kufikiri juu ya maoni ya Biblia kisha kutumia kuwaza kuzuri, tunaweza kuanza kuwafundisha juu ya Yehova. Katika yote haya na tuepuke ubishi na ‘maulizo yenye upumbavu.’ Tunataka tuzungumze pamoja nao na kufikiria pamoja nao katika njia ya wema na yenye upole, na katika njia hii tunaweza kuleta utukufu kwa Yehova.

SHULENI AU MASOMONI

6. Sababu gani wahubiri vijana wanazo nafasi bora kutoa ushuhuda wakati wako shuleni?

6 Hakuna wakati wo wote zamani ambapo vijana, wakiwa bado ni wanafunzi shuleni, wamepata kufahamu sana na kushughulika sana na magumu na mambo yasiyo ya haki ya watu wazima walio karibu nao. Hakuna wakati wo wote zamani ambapo vijana wamekuwa wakitafuta maana ya uzima kama wanavyotafuta leo. Hii ina maana kwamba sisi, tulio vijana wa Kikristo, tunazo nafasi za pekee kumhimidi Yehova katika mashirika yetu pamoja na wanashule wenzetu na waalimu. Mtunga Zaburi alitutia moyo sisi kufanya hivi, akisema: “Msifuni [Yehova] . . . vijana waume, na wanawali, wazee, na watoto; na walisifu jina la [Yehova], maana jina lake peke yake limetukuka; adhama yake i juu ya nchi na mbingu.”​—Zab. 148:7,12, 13.

7. Una faida gani katika kuzungumza na wanadarasa wenzako?

7 Mlitazame darasa lenu kama sehemu yenu ya pekee ya kumsifu Yehova humo. Ni sehemu iliyo na watu wenye umri sawasawa kama ninyi na walio na kupendezwa kule kule. Wala hakuna wakati ambapo utakosa kumkuta mtu. Wengi, kwa sababu ya ujana wao, watakuwa tayari kusikiliza, kutafuta kweli, kuweza kufikiri, bila chuki. Upatapo wanaopendezwa unaweza kuwarudia watu hao karibu wakati wo wote kwa maana sikuzote wako. Nao wanakujua wewe kama mwanadarasa mwenzao, si mgeni, na hivyo watazungumza pamoja na wewe pasipo kusita. Ndiyo, katika njia nyingi wanadarasa wenzako ndilo “shamba” zuri kuliko yote na lenye rutuba zaidi sana la watu ulio nao kumhimidi Yehova ndani yao.​—1 Kor. 3:6-9.

8. Nafasi moja ya kutoa ushuhuda kwa wanadarasa wenzako inakuwa wakati gani, na ungeutoa ujumbe kwa njia gani?

8 Katika maongezi ya vivi hivi pamoja na mmoja au wengi wa wanashule wenzetu, mara nyingi tunaweza kupeleka maongezi kwenye maoni ya Biblia juu ya magumu ya ulimwengu na njia ya kuyaondolea, kwenye unabii wa Biblia, au kwenye kufaa kwa shauri la Biblia juu ya magumu na mikazo inayowapata vijana leo. Tena hapa, ni jambo la maana sana kwamba tuseme nyakati zote katika njia ya unyofu wa moyo, ya utulivu, huku tukifikiria maoni yao. Imetupasa tutumie kufikiri kuzuri katika maongezi hayo, kufundisha kwa maulizo yenye kuamsha fikira, na kuwa wapole, si wenye kushikilia kauli yetu, katika njia yetu ya kusema.​—2 Tim. 4:2; 1 Pet. 3:15.

9. (a) Unawezaje kumsifu Yehova katika mazungumzo ya darasani, na unaweza kujitayarisha kwa kufaa kwa vipindi hivyo namna gani? (b) Mashahidi wengine vijana wamepata matokeo gani katika kutoa ushuhuda shuleni?

9 Mara nyingi mazungumzo ya darasani yanatoa nafasi bora kutoa ushuhuda. Masomo ya sayansi yanatufungulia njia ya kutoa sababu nzuri za kumwamini kwetu Yehova kama Muumba wa uhai na ushuhuda wa ukweli wa kisayansi wa Biblia. Hii inaweza kufanywa katika kuongea peke yetu pamoja na mwalimu wetu au wanadarasa wenzetu, au wakati darasa lote linapopewa nafasi ya kuzungumza. Kwa vipindi hivyo inafaa kujitayarisha kwa kujifunza kwa uangalifu vitabu hivi Did Man Get Here by Evolution or by Creation? na Is the Bible Really the Word of God? Tukifahamu vizuri mambo mazuri yenye akili katika vitabu hivi, tutakuwa tayari kutoa sifa na heshima kwa Yehova wakati tunapata nafasi. Vijana wengi wa Kikristo wameona inafaa kuwa na nakala ya vitabu hivi wakati wako shuleni, kwa vile mara nyingi mazungumzo ya habari hizi yanawafanya wanadarasa wengi kutaka kuchunguza zaidi jambo hili. Mhubiri kijana mmoja wa habari njema anatoa ripoti juu ya kitabu Evolution hivi: “Siku moja niliangusha vitabu tisa katika darasa moja. Kesho yake nikaangusha kimoja kwa kijana mwanamume aliyekuwa hajasema na Mashahidi zamani. Alishinda usiku wote akikisoma na mwisho akasema: ‘Nitachukua vitano vya hivyo!’ “Kijana mwenye umri wa miaka kumi na miwili anasema hivi: “Mwalimu wangu alisoma sehemu chache za kitabu na kesho yake akakipendekeza kwa darasa. Hivyo niliweza kuangusha nakala 34!” Ndiyo, wakati ambao karibu vijana wote wanapofundishwa kutilia shaka nguvu ya uumbaji ya Yehova na hata kuwako kwake, vijana wa Kikristo wanaweza kufanya vema kuonyesha kwamba wao ‘wanamkumbuka Muumba wao katika siku za ujana wao.’​—Mhu. 12:1.

10. (a) Ni mazungumzo gani ambayo kijana Mkristo angeweza kutumia katika masomo ya shule ili kutoa maoni ya Biblia? (b) Sababu gani shauri la Mhubiri 12:12, 13 linafaa?

10 Masomo ya historia yanaweza kutupatia nafasi ya kueleza juu ya ukweli wa Biblia kulingana na historia na hivyo kumpa Yehova sifa kama Mtungaji wa Biblia. Masomo ya usemi au ya lugha ya Kiingereza yanatoa vipindi vya kutoa hotuba kwa darasa zima. Kijana wa Kikristo anaweza kuchagua kuwako kwa Mungu, fundisho au ulizo la kidini, serikali kamilifu, au mojawapo za habari nyingine nyingi za Maandiko itakayomwezesha atoe kwa kufahamika maoni ya Biblia na mafundisho juu ya somo. Mara nyingi somo linatolewa kwa mazungumzo ya darasa lote wakati wa kumalizika kwa hotuba. Hii inatoa nafasi nzuri kwa ushuhuda zaidi na kwa kujua ni wanadarasa gani wanaopendezwa kwa kweli katika Biblia. Mwisho kupendezwa kwao kunaweza kusitawishwa katika mazungumzo ya faraghani. Katika njia hii tunaweza kusaidia wanafunzi wenzetu wafahamu hekima ya shauri la Yehova katika Mhubiri 12:12, 13: “Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili. Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.”

11. Ni sifa gani ambazo inampasa mtu atumie katika kutoa kweli kwa wanadarasa wenzake, na anaweza kuombea nini kama Wakristo wa kwanza walivyofanya?

11 Kutokuogopa na uhodari ndizo sifa ambazo tunataka sana ikiwa tutazitumia vizuri nafasi zetu zote kumsifu Yehova katika shule. Ndugu mmoja ambaye amejifurahisha huduma ya upainia ya wakati wote na utumishi wa Betheli kwa muda wa miaka tisa tangu amalize masomo ya juu anasema hivi: “Wakati ninapoikumbuka sasa miaka yangu ya shule, ninafahamu nafasi tele nilizokuwa nazo wakati huo kumsifu Yehova, na naweza kuwafikiria wanadarasa wengi ambao, inaelekea sana, wangaliitikia vizuri. Lakini sikutumia nafasi hizo mara nyingi kwa sababu sikuwa na uhodari nilio nao sasa wa kuzungumza juu ya Yehova na makusudi yake bila kizuizi. Kama ningeweza kurudi kwenye siku hizo na kuishi tena!” Je! wewe ni shahidi kijana wa Yehova ambaye bado anasoma shuleni? Sali kama Wakristo wa kwanza walivyosali: “Basi sasa, [Yehova], . . . ukawajalie watumwa wako kunena neno lako kwa ujasiri wote.” (Matendo 4:29) Omba kama Paulo alivyowaomba ndugu zake wa Efeso. Yeye aliomba kwamba wasali kwa ajili yake, “nipewe usemi wa kufumbua kinywa changu, ili niihubiri kwa ujasiri ile siri ya Injili; . . . nipate ujasiri katika hiyo kunena jinsi inipasavyo kunena.” (Efe. 6:19, 20) Heshima gani na utukufu gani ambao vijana wa Kikristo wanaweza kumletea Yehova kwa kuwa wasioogopa na hodari katika kumhimidi Yehova katika mashirika yao ya kila siku.

12. Jambo gani linalofanya vijana wetu kuwa tofauti na vijana wengine wa taratibu hii? Toa mfano.

12 Si usemi tu wa vijana wetu, bali mwenendo wao vile vile mzuri, unawafanya wawe tofauti na wale wa taratibu hii, hivyo kumsifu Yehova. (Flp. 2:14, 15) Lo! namna mama wa Kikristo alivyojivuna na kufurahi kupokea pongezi hili kutoka kwa mwalimu wa binti yake: “Si mara nyingi hii inatukia kwamba mwalimu anaweza kuandika pongezi kama hili, lakini binti yako ni mwenye mwenendo na adabu nzuri kuliko wote ambao nimeonana nao huku au mahali po pote. Hakika, yeye ni sifa kwako na ningefurahi ikiwa angeweza kuwa na mimi kwa miaka mingi zaidi.” Zaidi ya sifa kwa mama yake, je! hakuwa sifa kwa Yehova ambaye kanuni zake za haki ndizo zilizokuwa zikiongoza maisha yake? Ebu fikiri namna moyo wa Yehova ulivyopendezwa wakati binti huyo alipokuwa akimhimidi katika mashirika yake ya kila siku.

PENYE MAKUSANYIKO PAMOJA NA NDUGU ZETU

13. Ni katika wakati gani mwingine tunaweza kumhimidi Yehova katika mashirika yetu ya kila siku?

13 Ni jambo zuri kutafuta viburudisho na michezo katika ushirika wa ndugu zetu. Hili linatuhakikishia ushirika unaofaa na kuturuhusu kustarehe pasipo kujiona lazima ya kujihadhari, kujiona kunakofuatana sikuzote na mashirika ya kilimwengu.​— Zab. 133:1.

14. (a) Tunawezaje kufanya ushirika wetu kati ya Wakristo wenzetu kuwa wenye kufurahisha na vile vile kujenga kwa kiroho, na shauri la Paulo katika Waebrania 10:24, 25 lilielezaje hili? (b) Ni njia gani fulani zilizoshauriwa tunazoweza kwa hizo kufanya makusanyiko yetu kuwa yenye kufurahisha na yenye kujenga vile vile?

14 Ingawa huenda tukawa na wakati wa kufurahisha tukitazama kipindi cha televisheni kilichochaguliwa kwa uangalifu, kucheza wo wote wa michezo mingi, au kuamkia tu, tunaweza kukifanya kipindi hicho kuwa chenye kufurahisha na vile vile chenye kuleta zawadi kwa kiroho kwa kuongea juu ya mambo ya kiroho. Je! si wazi kwamba mtume Paulo vile vile alikuwa akifikiria vipindi hivyo wakati aliposema hivi: “Tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri; wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia”? (Ebr. 10:24, 25) Ikiwa sisi ndio tunaokaribisha wengine labda tutataka tufanye mpango ili sehemu ya jioni hiyo itumiwe katika “kuhimizana katika upendo na kazi nzuri.” Njia nyepesi ya kufanya hivi ambayo imeonekana kuwa yenye kufurahisha sana na yenye kujenga sana kwa ndugu wengi ni kumwomba kila mtu aliyepo asimulie namna alivyojifunza na kuikubali kweli. Si kitu tumemjua Yehova kwa muda gani, kusikia mambo haya yaliyoonwa na kuyasema kunafufua kushukuru kwetu ujamaa wetu na Yehova na kutuhakikishia imani yetu katika tengenezo lake. Au labda mwenye kukaribisha wengine kwake atataka achague sura zenye kuamsha fikira katika Biblia na kikundi kizima ndipo kinaweza kuisoma pamoja. Mstari wo wote usiofahamika kabisa na kila mtu aliyepo unaweza kuzungumzwa, na hii inaweza kuongoza kwenye mazungumzo yenye kupendeza ya Maandiko ambayo ni yenye kutia imani nguvu sana. Lo! namna jioni inayotumiwa katika njia hii pamoja na ndugu zetu inavyoweza kuwa yenye kupendeza! Namna tunavyojiona kuchangamka na wenye furaha tukiisha kuwa na kipindi hicho cha ushirika kwa sababu, hata wakati wa kuburudika, tumefanya “yote kwa utukufu wa Mungu.”​—1 Kor. 10:31.

TUNAPOKUWA PEKE YETU

15, 16. (a) Tunawezaje kumhimidi Yehova wakati tunapokuwa peke yetu, na katika kipindi hiki cha wakati tunaweza kuombea nini? (b) Je! ni lazima kusali kwa vipindi vilivyopangwa tu, na lilikuwa shauri gani la Paulo na Petro juu ya pendeleo la sala?

15 Katika maisha ya kila siku tunajikuta mara nyingi tuko peke yetu. Akina mama wa nyumbani huenda wakashinda karibu mchana wote wakiwa peke yao wakifanya kazi ya nyumbani. Huenda akina baba wakawa peke yao kazini au wakati wa kwenda na kutoka kazini. Mara nyingi watoto wanajikuta wenyewe wako peke yao kwenye mchezo au katika likizo lao. Labda utauliza hivi, Tunawezaje, tunapokuwa peke yetu, kumhimidi Yehova katika mashirika yetu ya kila siku?

16 Tunaweza kufanya hivi kwa kutafuta ushirika wa Yehova katika nyakati hizo. Wakristo wote katika umri wo wote wanaweza kuzungumza na Yehova wakati wo wote. Kuna furaha kuu katika kuongea na Mungu katika nyakati zisizotazamiwa na kufanyiwa mpango kama wakati ambapo ikitukia tunakuwa katika siku nzuri, pasipo na mawingu. Tunaweza kuzungumza na Yehova kwa moyo wetu wakati tunapotembea. Kumsifu na kumhimidi na kumshukuru Yehova sana kwa sababu ya kuwa hai, kwa kumjua yeye, na kwa kweli ambayo ametupa. Sitawisha mazoea ya ushirika huo wa sala pamoja na Yehova ili ujione kutamani kuzungumza na yeye wakati wo wote na zaidi wakati unapokuwa peke yako. Paulo aliwashauri ndugu zake wa Thesalonike ‘kuomba bila kukoma,’ na Petro alisema: “Mkeshe katika sala.” (1 The. 5:17; 1 Pet. 4:7) Usifanye sala zako za sifa kwa Yehova ziwe kawaida tu, kwa vipindi vile vile vilivyopangwa tu. Usiache hata kidogo maneno yako mwenyewe kwa Yehova yapoteze maana yao na ubora wa kutoka moyoni. Ndugu mmoja wa makamu alisema kwamba yeye anasali wakati anapoamka wakati wa usiku. Anasema: “Wakati huo ndipo ninapotoa sala zangu bora.” Ndiyo, kupitia kwa kusali bila kuacha tunaweza kumhimidi Yehova wakati tuko katika ushirika pamoja na yeye.

17. Sababu gani inafaa kwetu kuwafikiria watu wenye imani wanaosemwa katika Biblia tunapokuwa peke yetu?

17 Unapokuwa peke yako ni vizuri vile vile kuchagua mtu mwaminifu anayesimuliwa katika Biblia na kufikiria maisha yake na mambo ambayo alipatwa nayo. Waebrania 13:7 linasema: “Wakumbukeni wale . . . waliowaambia neno la Mungu; tena, kwa kuuchunguza sana mwisho wa mwenendo wao, iigeni imani yao.” Watu hao waaminifu wa kale wamemaliza maisha zao, na njia ya uaminifu ambayo wameenenda imeandikwa kwa karne nyingi sasa. Hivyo tunaweza kwa moyo wote kuchukua mfano wa imani yao bila kusita au kuwaza kama mwenendo wao utakuwa wa uaminifu au sivyo.

18. (a) Onyesha mfano namna tunavyoweza kufikiri na moyoni kushirikiana na ndugu zetu waaminifu ingawa tuko peke yetu na ingawa wametimiza mwendo wao katika maisha. (b) Sababu gani huu ni mmoja wa ushirika bora ambao tunaweza kuwa nao?

18 Kwa mfano, wakati tunapokuwa peke yetu na kufanya jambo fulani lisilotaka uangalifu wetu wa sikuzote, tunaweza kuchagua kufikiria uaminifu na uvumilivu wa mtume Paulo. Ebu fikiria majaribu aliyopata na kuyaona katika akili zako kama yakitukia. Pata maono ya kumwona akishinda usiku kifungoni bila kupata usingizi, akipigwa viboko 39 katika vipindi mbalimbali vitano. (2 Kor. 11:23-33) Mwone akipigwa kwa mawe na wakaaji wa Listra na kuachwa amelala chini nje ya mji kama mfu. Ona furaha ya wanafunzi wanaomkusanyikia wakati anapoamka na, ijapokuwa amepigwa vibaya sana na kusikia uchungu, anarudia mjini halafu, kesho yake, anaondoka pamoja na Barnaba ili kuendelea na safari yake ya umisionari. (Matendo 14:19, 20) Halafu, fikiria maneno yake kwamba “Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.” (1 Kor. 10:13) Katika njia hii, tunapokuwa peke yetu, tunaweza kuchagua washiriki walio bora, na kwa kufikiria mwendo wa maisha yao, tunatiwa nguvu na kuongozwa kumhimidi Yehova kama walivyofanya.

19, 20. (a) Wengine wameonaje faida kubwa katika kusikiliza na kujifunza nyimbo za Ufalme? (b) Tunajifurahisha ushirika wa nani wakati tunapoimba na kuzifikiria nyimbo hizi za Ufalme?

19 Wanapokuwa nyumbani peke yao akina mama na wake za Kikristo wameona ni jambo la faida kusikiliza nyimbo za Ufalme, au kukumbuka sauti zake ili waweze kuimba huku wakifanya kazi. Dada mmoja anasema hivi: “Mara nyingine ninapokuwa peke yangu nyumbani, ninajiona mwenye huzuni kidogo na mpweke. Lakini ndipo ninapoanza kupiga sahani za nyimbo za Ufalme nilizo nazo na inanichangamsha na kufanya siku yangu kuwa yenye furaha.” Sasa dada huyu amejua kuimba nyingi za nyimbo za Ufalme bila kutazama kitabu cha nyimbo. Wengine wamejifanyia mradi kujifunza maneno ya kila wimbo wa Ufalme ili waweze kuimba bila kutazama kitabu wakati wanaposikia sauti ya wimbo. Maneno ya nyimbo hizi ni yenye kujenga zaidi sana.

20 Kama mfano, ebu angalia wimbo namba 28 katika kitabu cha nyimbo “Kuimba na Kufuatana Wenyewe kwa Muziki katika Mioyo Yenu.” Kichwa cha wimbo huu ni “Mpe Yehova Sifa!” na fungu la pili linasema hivi: “Mweke mbele yako; Ukajifiche. Ili uangaze Nuru ya mbingu. Utembee naye, Na kumtafuta, Weka sikuzote Huduma kwanza.” Lo! namna maneno hayo machache yalivyo na maana! Tunapotua na kufikiria maneno, tunaona kwamba kila wimbo wa Ufalme umejaa sana maana na faida ya kiroho. Kwa kuimba kwetu nyimbo hizi kwa Yehova, tunajifurahisha ushirika pamoja na yeye na kumletea utukufu katika yote tuyafanyayo. Basi fuata onyo hili lililoongozwa na roho ya Mungu: “Endeleeni kufundisha na kuonyana kwa zaburi, sifa kwa Mungu, nyimbo za kiroho kwa uzuri, kuimba katika mioyo yenu kwa Yehova.”​—Kol. 3:16, NW.

21. Imetupasa tutafute kufanya nini katika mashirika yetu yote, na hii ingetimiza kanuni gani ya Maandiko?

21 Katika kuzungumza kwetu habari hii, tumeona lazima ya kumsifu Yehova katika matendo na mashirika yetu yote. Hata ingawa tutaona ni lazima kushirikiana na wale wasio na imani kutimiza madaraka yetu katika maisha, tunaweza kuvitumia vipindi hivyo kumpa Mungu wetu heshima. Mahali petu pa kazi, na tuutazame ushirika huo kama nafasi ya kufahamisha wafanya kazi wenzetu na Yehova na makusudi yake katika njia ya upole na yenye akili. Tukiwa shuleni, na tuitumie kwa faida nzuri nafasi yetu kutoa ushuhuda wa unyofu wa moyo kwa uhodari kwa wanadarasa wenzetu na waalimu. Tunapokusanyika pamoja kama ndugu, tunaweza kutiana nguvu katika imani, kuona ubora na bidii kwa maongezi yetu. Na tunapokuwa peke yetu, na tutafute ushirika wa Yehova kupitia kwa nyimbo na sala, na kupitia kwa ushirika wa watumishi waaminifu wa zamani wa Mungu katika mawazo yetu. Na tumhimidi Yehova katika maisha zetu zote na katika mashirika yetu yote ya kila siku, na hivyo kufanya “yote kwa utukufu wa Mungu.”​—1 Kor. 10:31.

[Picha katika ukurasa wa 9]

Huenda hali za ulimwengu zinazokuwa mbaya zaidi zikafungua nafasi mahali ambapo mtu anafanya kazi ya kimwili kuelekeza kwenye makusudi ya Mungu

[Picha katika ukurasa wa 10]

Vijana wa Kikristo wanazo nafasi bora shuleni, kama katika masomo ya sayansi, kusema juu ya kazi ya Yehova

[Picha katika ukurasa wa 12]

Kila siku tunapojifurahisha kazi ya Yehova, inafaa kuonyesha kushukuru kwetu kwake

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki