Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w73 8/15 kur. 383-384
  • Wakati wa Kuwa Kama Mtoto

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakati wa Kuwa Kama Mtoto
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • WATOTO KATIKA UOVU
  • WATOTO KWA HABARI YA KUTUMAINI KAMA MTOTO
  • Kukazania Ukomavu wa Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Kukomaa kwa Kikristo Ni kwa Lazima Ili Kupata Uzima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Je, Wewe Ni Mkristo “Aliyekua Kabisa”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • ‘Acha Kuendelea Kwako Kuwe Dhahiri’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1973
w73 8/15 kur. 383-384

Wakati wa Kuwa Kama Mtoto

JE! NI nani anayetaka kuwa kama mtoto? Je! kuwa mtu mzima, aliyekomaa, si hali ya kupendeza sana? Kwa kweli ndivyo, hata kama vile mtume Paulo alivyoonyesha alipoandika: “Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto.”​—1 Kor. 13:11.

Kwa maana na kwa lazima ni kukomaa kwa kimwili, kwa akili na vile vile kwa maono, hata hivyo, kuna namna ya kukomaa ambayo ni ya maana hata zaidi. Na hiyo ni ipi? Kuwa mtu mzima kwa kiroho au kukomaa kwa kiroho. Namna hii ya kukomaa inamwezesha mtu kutofautisha ubaya na wema. Inamwezesha Mkristo kuendelea kuwa imara ingawa mafundisho yanayopingana, majaribu na mikazo. Kukomaa kwa kiroho kunamwezesha mtu ‘kukesha, kusimama imara katika Imani, kufanya kiume, kuwa hodari.’​—1 Kor. 16:13; Ebr. 5:14.

Kwa kuwa kukomaa kwa kiroho ni kwa maana sana kwa Wakristo, wanaambiwa: “Msiwe watoto katika akili zenu; . . . bali katika akili zenu mkawe watu wazima.” (1 Kor. 14:20) Ndiyo, Yesu Kristo “alitoa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti; na wengine kuwa wachungaji na waalimu; kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; hata na sisi sote [tutakapofikia]. . . kuwa mtu mkamilifu, . . . ili tusiwe tena watoto wachanga,” na goigoi na wenye kutumiwa vyepesi kwa sababu za kichoyo.​—Efe. 4:11-14.

Lakini pamoja na hayo yote Biblia vile vile inaonyesha kwamba kuna mambo fulani ambayo kwayo ni jambo la kupendeza sana kuwa kama mtoto, kama kitoto. Haya ni mambo gani na sababu gani ni jambo la maana kuwa kama mtoto kwayo?

WATOTO KATIKA UOVU

Maana moja ambayo kwayo Maandiko yanawapendekeza Wakristo kuwa kama watoto ni wakati mambo ya uovu yanaingia. Hivyo wakati mtume Paulo aliandika, “Msiwe watoto katika akili zenu,” mara moja aliongeza maneno, “lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga.”

Hakuna shaka juu yake, uovu ni jambo ambalo Wakristo hawataki kuwa na ujuzi wake, hawapaswi kutaka wo wote. Inapokuwa habari ya kuwa bingwa wa kuwadanganya wengine, au kutenda kama mnafiki, au kujipatia sifa kwa njia ya ufisadi au upotovu, basi inafaa sana kwamba Wakristo wawe kama watoto, safi, wasio na ujuzi.

Leo maelekeo katika ulimwengu wa kufurahisha ni ya “kukomaa” kwa upande wa uovu. Uhakika huu unatiliwa mkazo na taratibu ya Kiamerika ya kukuza sinema. Kwa wingi wanaelekea kusawazisha kukomaa na uchafu na mazoea ya ngono yanayokatazwa katika Neno la Mungu. Kwa hiyo, Wakristo wanaotaka kutii shauri la kuwa watoto wachanga katika uovu ingekuwa vizuri wajihadhari na sinema zinazoshauriwa kwa watazamaji “waliokomaa.”

Namna linavyofaa, basi, shauri la kuwa watoto kwa habari ya uovu! Je! mtu anawezaje kukaa katika hali ile safi? Msaada mmoja mkubwa ni kujihadhari na namna ya mashirika. “Msidanganyike; [mashirika] mabaya huharibu tabia njema.” (1 Kor. 15:33) Hiyo maana yake ni kujitenga na ushirika wa waasherati, wazinzi, wanaume au wanawake wenye kulalana wenyewe kwa wenyewe na wahanithi katika maisha yote, kadiri mtu awezavyo. Lakini vile vile ina maana ya kuwaondoa akilini mwa mtu kwa kutowafikiria watu wa namna hiyo, kwa kutosoma juu yao ili kusisimua mwili, kwa kutowatazama katika televisheni au katika kiwambo cha sinema. Moyo wa kibinadamu una hila na kwa wepesi unaweza kupata mwonjo wa mambo kama hayo na kujaribiwa kuvuka furaha ya kuwazika juu yake na kushiriki katika hayo kabisa. Lililo bora zaidi ni kuepuka majaribu yote ya namna hiyo kwa kuendelea kuwa watoto kwa habari ya uovu.​—Yer. 17:9; Flp. 4:8

WATOTO KWA HABARI YA KUTUMAINI KAMA MTOTO

Wakati mmoja Yesu alisali: “Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya umewaficha wenye hekima na akili; umewafunulia watoto wachanga.” Yesu alisali hivyo mara tu nyuma ya wale wainjilisti sabini aliokuwa ametuma na kurudi wenye furaha kwa sababu ya waliyoweza kufanya, kama vile kuweza kutoa pepo wachafu.​—Luka 10:17-21.

Wanafunzi wanyenyekevu wa Yesu walikuwa kama watoto wakilinganishwa na waandishi “wenye hekima na akili” na elimu ya juu sana, Mafarisayo na Masadukayo. Lakini Mungu aliwafunulia mambo ambayo wapinzani wa kidini wa Yesu wenye elimu ya juu sana hawakujua kwa sababu wanafunzi walikuwa kama watoto kwa maana nyingine bado.

Yesu alikazia fikira za wanafunzi wake juu ya jambo hili wakati mmoja walipokwisha kumwuliza: “Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni?” Kwa wazi aligundua kadiri fulani ya kiburi na tamaa ya kujitakia makuu kwa kumwuliza ulizo hili. Kwa hiyo, ili kuwafunza somo alimwita mtoto mchanga na “akamweka katikati yao, akasema: ‘Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni,’” licha ya kuwa wakubwa kupita wote humo! “Basi ye yote ajinyenyekezaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.” (Mt. 18:1-4) Ndiyo, kuliko kuonyesha kiburi kama viongozi wa kidini “wenye hekima na akili,” wanafunzi ni lazima waonyeshe unyenyekevu kama wa mtoto, kutumaini kama kwa mtoto katika Baba yao wa kimbinguni ambaye sasa alikuwa akiwafunulia kweli hizi kupitia kwa Mwanawe.

Kwa wazi, basi, kukomaa kwa kimwili na kwa maoni ya moyoni ni kwa maana na kunafaa; na zaidi hivyo ni kukomaa kwa kiroho. Lakini kukomaa kwa kiroho kunatutaka ‘tugeuke’ na kuwa kama watoto wachanga katika mambo haya: ‘katika uovu kugeuzwa watoto wachanga,’ kwa kuwa na imani kama ya mtoto na kutumaini na kujiweka huru na kiburi chenye tamaa ya kujitakia makuu.​—1 Kor. 14:20.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2026 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki